Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, June 8, 2018

YOTE NI KWA MAPENZI YA MUNGU-9



'Tahamaki shemeji anakuja kukamatwa...'alisema mama mjane

‘Kwa kosa gani …?’ nikamuuliza na mara simu yangu ikawa inaingia ujumbe, na haikupita muda, mtoto wa huyo mama naye akaanza kulia…

Tuendelee na kisa chetu

Baada ya kipindi cha kama mapumziko, hivi, mimi nasoma ujumbe kwenye simu, na mama mjane anahangaika na mtoto wake...baadae akawa kama huyupo tayari kuongea na mimi nikalazimisha tu kwa kusema;

'Unasema mlienda polisi....ulienda kusema nini huko...?' nikauliza na yeye akaanza kuelezea tena;

‘Rafiki yangu mume wake ni polisi, kumbe aliongea na mume wake kuhusu tatizo langu, na mume wake, ndio akashauri mimi nilipeleke hilo swala polisi ili kufanyike upelelezi, na kama kuna udanganyifu kwenye hilo deni, ukweli utabainika tu...kiukweli niliposikia hivyo nikaingiwa na matumaini mapya.

Ehe..ukasema shemeji akaja kukamatwa, ..ilikuwaje..?' nikauliza

‘Na kweli mimi nilifanya hivyo….upelelezi ukaanza na siku kama ya pili yake, polisi wakaja kumchukua shemeji, na bahati mbaya siku hiyo shemeji alikuwa hapa nyumbani…’akasema

‘Alikamatwa akiwa hapo kwako,..., au aliitwa kituo cha polisi..?’ nikauliza

‘Askari waliovalia kiraia, walifika hapa nyumbani, na kutoa vitambulisho vyao, wakijieleza kuwa wao ni nani, na wanamuhitajia, shemeji waende naye kituo cha polisi kwa mahojiano…shemeji akawauliza ana kosa gani, wakamuambia ni katika kuisaidia polisi kutokana na tuhuma za deni la marehemu…’akatulia

Shemeji akaniangalia mimi kwa macho ya kushangaa, maana , nilikuwa bado sijamuambia lolote kuwa nimeenda polisi, na siku hiyo ndio nilipanga nije kumuambia …

‘Shemeji ni nini kinachoendelea…?’ akaniuliza na polisi hawakumpa muda wa  huo, wakaingilia kati na kusema;

‘Hayo maswali na majibu yako utayapatia huko huko kituoni, usiwe na wasiwasi ..’wakasema.

Basi shemeji kwa shingo upande akaongozana nao…na mimi nikaona sio jambo nzuri kukaa kimia, nikampigia simu ndugu yake mmoja kumuelezea, ili kama kuna lolote, au  likitokea lolote wao waweza kusaidia.

‘Uliwapigia ndugu hao wa nini tena…?’ nikauliza

‘Niliona ndio jambo nzuri, …mimi nisingeliweza kwenda huko, maana mtoto , huyu mkubwa naye alikuwa akiumwa malaria…na hata kuja kwa shemeji hapo ilikuwa kunisaidia apate dawa…’akasema

‘Ikawaje…?’ nikamuuliza

‘Waliniuliza kakamatwa kwa kosa gani, nikawaambia ameitwa tu kutoa maelezo kuhusiana na deni linalodaiwa kuwa ni la marehemu.

‘Hivi shemeji, hayo si tulishayamaliza…?’ wakaniuliza na nikajieleza, lakini ilionekana mimi ndiye nimemchongea ndugu yao kuitwa huko polisi..’akatulia

‘Sasa aheri ingelikuwa ni kuhojiwa tu na kurudi,…hakuruhusiwa kuondoka huko kituoni siku hiyo, na ndio ikaleta uhasama,…’akasema

‘Kwanini sasa, …hakuruhusiwa…kuondoka siku hiyo…?’ nikauliza

‘Nasikia alileta ubishi, hakutaka kutoa ushirikiano,…’akatulia kama anaogopa kuongea zaidi au kuna jambo kaliona.


‘Ndugu zake walisemaje….?’ Nikauliza akaitikia kwa kichwa halafu akasema;

‘Wao waliendelea kunilaumu, kuwa chanzo cha haya yote ni mimi, najifanya sijui lolote kuhusu hilo deni, wakati nilihusika kwenye matumizi…na huenda kaka yao, yaani marehemu hakuniambia kwasababu ya tabia yangu mbaya..wakaongea sana, sikutaka kujibishana nao kabisa, ila…’akatulai kidogo

‘Nilishindwa kuvumilia walipoanza kuongea maneno mabaya… hata mimi sikupenda hiyo hali ya shemeji kuitwa, kituo cha polis kujieleza, nilipendelea wamuhoji tu akiwa nyumbani, lakini nisingeliweza kuingilia kazi zao..wao walisema ni taratibu za kawaida tu..’akatulia

‘Ehe…’nikasema hivyo tu

‘Mimi nikawaambia hizo ni taratibu za kawaida za kipolisi, kuona kama wanaweza kupata lolote, na mtu wa kumuuliza kuhusu hilo deni ni shemeji,..maana yeye ndiye anajua zaidi,.’akatulia

‘Wao, hawakunielewa, ndio wakaanza kuongea maneno mabaya ya kashfa, na hapo sikuweza kuvumilia, ikabidi na mimi nianza kuongea vibaya,..ikawa sasa ni kujibizana vibaya, ilifikia sehemu nikaongea hata yale ambayo sikupaswa kuongea…’akasema

‘Kama yapi…?’ nikamuuliza

‘Kuwa shemeji yangu alifanya vibaya, kama aligundua deni, asingeendelea kuliongeza, na kwanini alinificha muda wote huo, ni lazima alikuwa akitumia deni hilo kwa masilahi fulani….’akatulia kidogo

‘Na huenda kuna ukweli ndani yake au sio,..ikawaje sasa..?’ nikauliza nikiangalia saa

‘Kiukweli kauli hii ilifika kwa shemeji, na hata alipoachiwa, alionekana kunikasirikia, japokuwa alijitahidi kuficha hiyo hali, ..akaniambia,  baada ya yeye kujitolea kwake kwa ajili ya familia, hiyo fadhila kwake, na ya kuwa yeye hataacha kuwasaidia watoto kwa vile ni watoto wao..ila mimi naonekana nina roho mbaya, sina shukurani….’akatulia

‘Wewe ulisemaje..nikauliza

‘’Yaani siku hiyo ndio niliwaona jinsi gani walivyokuwa wakinichukia, maana hata dada zao walifika kwangu wakiwa na huyo shemeji, na kuanza kunibwatukia, wakiniambia mimi ni mwanga, mchawi, eti huenda mimi ndiye nimechangia kaka yao kufa..sikufurahia kauli hiyo, nikawafukuza ndani kwangu.

Wakaondoka kweli, akabakia shemeji…yeye akawa muungwana kujaribu kunisihi kuwa ninalolifanya sio sahihi, na kama nilipanga kwenda polisi ningelimfahamisha mapema ili ajiandai kuwasaidia polisi, lakini polisi, wao wanafikia kumshuku vibaya…na kuanza kumtesa.

‘Ni kweli walimtesa..?’ nikauliza

‘Mimi sijui…polisi walisema walimuhoji tu, na kutumia lugha ya vitisho kidogo…’akatulia
Basi baada ya siku hiyo, ikawa sasa ni vita...hadi wazee wakaingilia kati, kutusuluhisha, na huku polisi wakiendelea na uchunguzi wao, mara kwa mara walifika kukutana na shemeji, na hata ndugu zake wengine, ikawa kama ni kero kwao.

‘Basi siku moja wakaja tena, shemeji na mawifi,…naona walijiandaa kwa shari, walianza kuongea kwa busara kidogo, wale shemeji, lakini ilipofikia zamu ya mawifi, ndio wakaharibu,…ilifikia hatua kutaka kupigana.

‘Kwanini mpigane…?’ nikauliza

‘Kwa nini waniambie mimi ni mchawi, eti nimloge mume wangu ili iweje sasa, hebu fikiria hata wewe hilo linaingia akilini kweli, ..kiukweli mimi nilijitahidi kuvumilia, wakati wanaongea, ikafikia muda nikashindwa, na nilipoanza kuongea, niliongea kweli….’akasema

‘Lakini hayo yote yalikuwa kwenye harakati za polisi kufuatilia na kutafuta ukweli  au sio, na swala hilo la kutafuta ni nani alifanya hujuma, kama kweli ipo, au sio….lilikuwa bado halijafika mahakamani au sio,…kuacha ile ya mwanzo ya kutafuta ukweli wa deni kama ni halali au la?’ nikamuuliza

‘Ndio….ilikuwa hivyo…’akasema

‘Ehe …ikawaje sasa?’ nikamuulza

‘Baadaye tukasuluhishwa, yakaisha kwa siku hiyo, lakini chuki ndani ya mioyo ilikuwa haimithilikia, hasa kwa mawifi dhidi yangu, hata tukikutana njiani hawanisalimii, nikawasalimia, wanaweza wakaitikia au wakakaa kimia tu…’akatulia

‘Wazee wakaliona hilo, ikabidi tuitwe kikao, ..hutaamini, siku hiyo ya kikao, utafikiri sio wao tena, wanajifanya watu wema kwangu, wakasema kama ninaona wamenikosea, basi wanomba msamaha, kwani wamefanya hivyo kwa uchungu wa ndugu yao, ..wamefiwa na bado wanaandamwa na mambo ambayo hawayayajui,…’akatulia

‘Nikawaambia mimi sina tatizo, maana mimi ndiye muathirika wa hayo yote…kama ni huzuni, hata mimi ninayo, na kinachoniuma ni kuwa mume wangu anabambikiwa deni, mimi sikubaliani na hilo deni, ndio maana natafuta ukweli…

‘Kwahiyo wewe unaumia kwa vile hilo deni linagusa masilahi yako,..lakini wewe hujali masilahi ya ndugu yetu ..kwasababu kama deni lipo, yeye huko atakuwa na wakati mgumu, kwanini mimi sitaki deni lilipwe ili roho ya ndugu yao iwe salama….wakasema hivyo…’akatulia

‘Mhh, ikawaje..?’ nikauliza

‘Mimi sikuwa na kinyongo nao zaidi , ilimradi wamejiona wamekosa, basi nikawaambia yamekwisha,…tumalizane kwa amani, mara mmoja wapo akasema;

‘Ili tuone kama kweli umetusamahe, basi achana na mambo hayo ya polisi, maana yanaleta picha mbaya kwenye familia yetu inaonekana kama sisi tumefanya hayo makosa, wakati sisi hatujui hata chanzo cha hilo deni,..ni vyema tuachane na polisi, na,..hayo mambo tuyamalize kinyumbani, ndivyo kaka yetu alivyokuwa kifanya, hakutaka mambo ya kesi kesi, hasa za polisi…’akasema hivyo.

‘Ukawajibuje..?’ nikauliza, maana huyu mama akiongea jambo, usipomuuliza swali atakaa kimia tu.

‘Mimi  nikawaambia hata tukiliongelea nyumbani hilo deni atalipa nani, ni lazima tutafute ukweli wa hilo deni, kwani huenda kuna mtu mwingine anatuchezea akili mbali na familia yetu, wao hawalioni hilo…na watu wazuri wa kutusaidia ni polisi…, ‘akatulia

‘Sasa walipoona sikubaliani na hilo, wakatoka nje, wakateta, baadae wakarudi mmoja wapo akauliza;

‘Ina maana shemeji, umeamua iwe hivyo, ndio mwisho wako…?’ akauliza

‘Mimi naona tuwaache polisi wamalize kazi yao kwanza..’nikasema

‘Unajua ndugu yetu, mtu anayekusaidia ndiye wanamshuku vibaya, ina maana kweli wewe humuamini shemeji yako..?’ wakaniuliza

‘Mimi siwezi kuwaingilia polisi,..sizani kama wanamshuku, wanaweza kumshuku yoyote, mbona hata mimi wanafikia kunihoji..mbona hilo hamsemi…’nikasema

Kiukweli, siku hiyo, hatukuelewama…wakaondoka sasa wakitoa lugha za vitisho …’akatulia

‘Walisemaje..?’ niakuliza

‘Kwanza walianza kusema sina fadhila, sina shukurani, sijali jinsi ndugu yao alivyojitolea kwa ajili yangu, basi kama ni hivyo na wao watafanya hicho ninachokitaka….na watahakikisha,najuta, nitakiona cha mtema kuni…’akasema

‘Ni nani alikuwa akiongea hayo…?’

‘Ni hao ndugu zake shemeji hasa mawifi…walikuwa wakiongea tu, kila mmoja na lake, uzuri wake pale walikuwepo wazee, na mmojawapo ni mzee Mtupe, ndiye aliyewasihi sana, lakini mhh,…’akasema

‘Ikawaje…?’ nikauliza nilipoona katulia tu

‘Kiukweli kikao cha kusuluhishwa siku hiyo hakikuisha vyema, ikabid kiahirishwe hadi siku nyingine huku nikiambiwa nikae nifikiria …nikauliza nifikirie nini, nikaambiwa hilo swala la kupelekana polisi, sio jambo jema,  kwanini namsumbua huyo shemeji, wakati hana kosa…’
Mimi nikawaambia;

‘Lakini sio mimi niliyemsumbua shemeji, hata yeye analifahamu hilo, na…ni utaratibu tu wa polis katika kutafuta ukweli, hajaambiwa ana kosa…’nikawaambia hivyo, lakini hawakukubali, wao wakataka nifute hiyo kesi ya malalamiko, ya kudai kuwa deni sio halali, na wao watasaidia katika kuutafuta ukweli, …’akatulia

‘Ukakubali…?’ nikamuuliza

‘Sikukubali..unajua walishanifanya na mimi niwe mkali,..niliona kama wanataka kunikalia tu, na kama polisi walishaanza kazi yao mimi ningeliwezaje kuwasimamisha, mimi niliona ni bora wamalize uchunguzi, ili hata na mimi nijirizishe..kwa kuendelea kuwa na msimamo huo,  ikawa nimejenga uhasama na familia hiyo,…na ..sijui ni kwanini,..huenda ni bahati mbaya tu au la…’akatulia

‘Kwa vipi…?’ nikauliza

‘Baadaye,..ni hata wiki haikupita, mara mtoto wangu huyu mdogo akaanza kuumwa, kweli kweli..kila ikifika muda wa kwenda polisi kufuatilia, mtoto anazidiwa, maana mimi nilishaamua baada ya ushahidi huo wa polisi kukamilika tunakwenda moja kwa moja, mahakamani, ..’akasema

‘Kwani hao polisi walikuambia wamegundua nini…?’ nikauliza

‘Wao,…hadi muda huo, walikuwa wamegundua kuwa  kweli hilo deni lipo…japokuwa, ya-we-ze-ka-na sioo halali ya marehemu,…sasa kama sio halali , ni halali kwa nani, na ni nani kafanya hivyo, kwa vipi, ..ndicho walikuwa wakiendelea kutafuta,…kwa tarifa hiyo, ikazidi kuwachanganya hao wanandugu, kwa vile ndugu yao ndiye msimaizi, wakahisi vibaya..lakini mimi mpaka hapo sikuwa na shaka na shemeji yangu kabisa kuwa yeye anahusika…’akatulia kidogo.

 ‘Kwahiyo hadi hapo aliyekuwa akishukiwa ni shemeji yako au sio, kutokana na uchunguzi wao, au yeye alikuwa akiandamwa na polisi katika kuisaidia tu, na kilichomfanya awekwe ndani ni kutokana na ubishi wake, au sio…?’ nikasema kwa kuuliza

‘Ndio hivyo, wala yeye hakuwa mshukiwa, alitakiwa tu kutoa maelezo, na kutoa ushirikiano tu, na wakati mwingine walienda naye hadi benki, sijui huko waliongea nini, maana sikuambiwa…’akasema na kabla sijamuuliza swali jingine akasema

‘Kiukweli hata mimi sikutaka ifikie hapo…maana sasa anayesumbuliwa ni shemeji , mtu aliyenisaidia sana,..’akatulia

‘Hata hivyo mimi ningelifanya nini, maana wanangu ndio wanaumia, na sasa nyumba inauzwa, inapigwa mnada,..na yote haya ni baada ya mimi kusema tuyamalize kinyumbani,nina imani kama ningewaachia polisi waendelee, basi,…huenda wangeligudnua jambo…’akatulia

‘Ina maana uliwazuia…kuendelea na uchunguzi wao…?’ nikauliza

‘Mimi ndio nilishindwa kutoa ushirikiano, kila nikiitwa kituoni, katika mahojiano sifiki,…’akasema

‘Kwanini…?’ nikauliza

‘Watoto..hasa huyu mdogo, ndio alianza kuumwa kweli kweli…’akasema

‘Polisi walifikia wapi, au hukuwahi hata kuongea nao…?’ nikamuuliza

‘Unajua kichonipa nguvu kipindi kile ni pale polisi waliposema kuwa kuna uwezekano kabisa hilo sio halai ya marehemu…wao walikuwa sasa wanahojiana na benki…kuona kuna kitu gani kinachoendelea huko ndani kwao,…, ila kiukweli deni hilo lipo, halina ubishi,..na ndio wakanishauri nitafute wakili mnzuri wa kusimamia hiyo kesi, huku wako wakiendelea na uchunguzi , hata hivyo, sikuwa na pesa, na mtoto akawa na hali mbaya sana…’akasema na kutulia kidogo

‘Baada ya mtoto kuzidiwa, ndio mmoja wapo wa hao ndugu akaja kuniuliza;

‘Hivi wewe una ubinadamu kweli, hivi nyumba ina thamani gani zaidi ya mtoto wako…’akasema

‘Nikamwambia, ukisema hivyo ina maana nyie ndio mnamloga mtoto wangu ili nikubaliana na matakwa yenu…’nikamwambia ..haaa, akacharuka na yeye, eti nimemwambia familia yao ni wachawi, ikazuka kesi nyingine ya mimi kuishuku familia ya mume wangu uchawi,..yaani ilikuwa ni taabu, huku mtoto anaumwa, huku wanafamilia wananisakama....’akatulia

‘Baada ya hapo ikawaje..?’ nikamuuliza

‘Cha ajabu wao wanashinikiza kama denii lipo kwanini nisiache tu nyumba ipigwe mnada ili hilo deni lilipwe na pesa itakayobakia tujenge nyumba nyingine ,eti kwa kufanya hivyo, kwenda mahakamani namshitaki marehemu aliyekopa hilo deni, na zaidi pia nawafanya ndugu zake wateseka kwa kitu ambacho hakiwahusu, na marehemu huko alipo, anawajibika kwa hilo deni, …..’akasema

‘Hakiwahusu tena…?!’ kwa mshangao

‘Ndio kauli yao hiyo…’akasema

‘Unasema mtoto akaanza kuumwa, … hilo la kuumwa kwa mtoto wako linahusikanaje na hiyo kesi,  kwa mtizamo wako wewe, unahisi wao ndio wamefanya hivyo, kuwa mtoto wako aumwe ili ushindwe kuendelea na madai yako..?’ nikamuuliza

‘Unajua nikiongea haya utadhani mimi naamini haya mambo ya kishirikiana,…mimi siamini hayo kabisa, mimi namuamini sana mungu , nimelelewa hivyo na ….moyoni mwangu, siamini sana mambo ya kulogwa, japokuwa yapo, siwezi kukataa….’akatulia

‘OK…’nikasema

‘Lakini  hiki kilichotokea hapa, ..oh, labda uwe na moyow a jiwe, mimi ninaishi maisha yasiyo salama, vitisho, na mambo ya ajabu ajabu yanatokea kila siku, usiku hatulali, mara wanalia mapaka…sijui vitu gani vinacheza kwenye bati juu..ni shida kweli, na kuna mtu kaniambia, ukilogwa ukaondoha humu ndani, ndio basi tena…’akasema

‘Kwanini huyo unamuamini, na kwanini akasema hivyo..?’ nikamuuliza

‘Sikutaka nikuambie hiki, ila ni mume wangu ananitokea kwenye njozi, na moja ya jambo analonisihi ni kuwa vyovyote iwavyo, nisikimbie, nisitoke humu ndani….unajua hisia , nahisi kama kweli yupo ndio ananiambia hivyo, naogopa kumhini, kumkatalia mume wangu, la sivyo, ningelishaondoka humu ndani….’akasema

‘Polea sana…’nikajikute nimesema hivyo

‘Tatizo sasa, wao wanawalenga watoto wangu, hawa watoto wana makosa gani….’akasema kwa uchungu

‘Una uhakika na hilo, kuwa ni watu wanaowalenga watoto, swali linakuja ni nani,…kaam sio hao shemeji zako, au…?’ nikamuuliza

‘Huyu mtoto mdogo, hakuwa na tatizo hilo kabisa, sasa kila nikitaka kufuatilia hilo jambo..hiyo kesi, kwenda huko polisi, huyu mtoto anashikwa na homa kali mpaka anakuwa kama ana dege dege, anapoteza  fahamu….,hebu niambie mtu kama wewe utaamini nini hapo, na utashangaa siku hiyo ikipita nikaamua nisiende, mtoto anakuwa mnzima hebu niambie hapo ni kitu gani hicho…’akasema

‘Ni ajabu kabisa…’nikasema hivyo.

‘Ilipotokea zaidi ya mara tatu,…siku moja nikasema potelea mbali ngoja niende….weeh, nilipigiwa simu hata kabla sijaanza kuonegea na polisi, mtoto kapotea fahamu…nilirudi nyumbani mbio,…nafika namkuta kweli mtoto kapoteza fahamu…nilichanganyikiwa, tukakimbiza hospitalini, tunafika mtoto kazindukana , lakini hali yake ni dhaifu kweli….ningefanya nini hapo..’akasema

‘Ulihakikishaje…sio kwamba nakupinga kwa hilo, lakini jinsi gani ulihakikisha kuwa mtoto anaumwa kwa sababu hiyo…?’ nikamuuliza

‘Mtoto anaumwa jamani…akianza kuchemka homa namkimbiza hospitalini, akipimwa hana malaria hana tatizo, …anaishia kupewa panadol…..nikirudi na kusema niachane na huko kufuatilia mtoto ni mzima kabisa, utasemaje hapo, …..sasa ulitaka nihakikisheje jamani..’akasema

Pale kwa kweli nilikaa kimia, nikiwaza yangu….
‘Niambie wewe, kama ungelikuwa ndio mama ungelifanya nini..?’ akaniliza

‘Je ulijaribu njia nyingine kwa watu wa dini, au tiba mbadala..?’ nikamuuluza

‘Hahaha, usifikiri mimi sio mama mwenye uchungu na mwanangu, kote huko nilifika, lakini sio kwa watu wa ramli, hapana,..hutaamini nikienda huko, mtoto akifika mbele ya hao watu hana tatizo ni mzima kabisa,..hata ukimuambia mtu anaona kama unamdanganya…nilipewa dawa, nikapata …maombezi, duwa nk…lakini kila ikifika siku ya kufuatilia mambo ni yale yale…mtoto wangu anadizi kudhoofika, ’akasema


Ilipita muda kidogo nikiliwazia hili, je mama kama mama atawezaje kupata haki zake kwa hali kama hii, kama alivyosema kila akitaka kufanya jambo, mtoto wake anaumwa,na keshahaikisha hilo…kwa mapenzi ya mama kwa mtoto wake itakuwa vigumu sana, hapo itakuwa vigumu, sasa …nitamsaidiaje, nikaona ni lazima nifanye jambo, nikasema

‘Shemeji wewe si unamuamini mungu?’ nikamuuliza


‘Swali gani hilo, kama nisingelikuwa namuamini mungu kwa hali kama hii ungelinikuta nimeenda kwa waganga wabaya,nikapambana na hao watu… lakini mimi namuamini  sana mungu na kwa haya sijawahi kwenda kwa waganga wabaya..ila kwa waganga wa dawa, nimewahi, siwezi kukudanganya…na zaidi mimi namuomba mungu wangu..’akasema

‘Sasa kama unamuamini mungu huoni kuwa huo ni mtihani tu, unajaribiwa tu , ili tu usitete haki zako, mimi nakushaurii sasa  tuifufue hii kesi …mimi kuna watu nitawasiliana nao wataweza kwenda mahakamani, ….wataweka pingamizi …..tusipoteze muda, unaonaje kwa hili…..’nikasema

‘Hapana…’akasema

‘Kwanini…hii ni haki yako, au sio…’nikasema

‘Ni haki yangu ndio, lakini sitaki …..kwanza nitaanzia wapi wakati nimeshakubaliana na hawa wana ndugu tukasema basi yaishe, kama ni nyumba watauza , italipiwa deni na kiasi kilichobakia tutajengea kibanda nyumba nyingine ya kawaida inatosha hata kama ni kibanda cha vyumba viwili inatosha…’akasema

‘Wewe niamini mimi, hapa kuna ujanja umechezwa, kuna mtu anakuzunguka, ili aifisidi haki ya wanao,…nikubalie tuipiganie haki ya watoto, kwani ukiacha hivi hata mume wako huko alipo atakulaumu, ina maana juhudi zote alizofanya zinapotea bure na wewe upo hai….mimi kuna watu wangu watapigania hili hadi haki yako itapatikana, niamini,…na watoto wata..kuna mtu wa dini atakuja atalimaliza hili tatizo….’nikasema na yeye akabakia kimia

‘Sikiliza, ….’nikasema na mara mtoto akaanza kulia, yeye akamkimbilia na mimi sikujali, nikasema

‘Ngoja niwasiliane na watu wangu, nitakuambia….’nikasema nikapiga simu kwa watu wangu nikawaelezea kwa kifupi ni nini kinatakiwa kifanyike, …kazi iaanza mara moja!

‘Sasa sikiliza shemeji, usijali kuhusu mtoto, kila mtu kaumbiwa uhai wake,…sikiliza, usilie,kwani, hebu kwanza….’nikasema mtoto alikuwa kalegea, ni kama ana….taka kukata roho, hapo moyo wangu phaa

‘Unaona ndiyo haya siyataki, hawa wanajua kila ninachotaka kukifanya, unaona …’ akawa anamshika mshika mtoto wake ambaye kwa muda huo alikuwa na joto kali , keshapoteza fahamu

‘Tumpeleke hospitalini..’nikasema

‘Tunajisumbua tu bure… , dawa ni kuachana na hayo madai,…’akasema mama mtu

Nilimuchunguza  Yule mtoto, kweli joto lilikuwa juu kweli, ..na hapumui kabisa, ni kama kapoteza fahamu, mimi nikaonelea twende hospitali tu, hivyo hivyo,..

‘Twende..twende..hamna cha kujiandaa, mtoto yupo kwenye hali mbaya…’nikasema sasa nikimbeba, huyo mtoto nikitembea kuelekea mlangoni, lakini kabla sijainua mguu wa pili, mara mlango ukagongwa, sikujali huyo mgongaji, nikasema;

‘Twende…’nikasema nikgeuka kumuangalia mama mjane, ambaye alikuwa kama kachanganyikiwa, anashindwa afanye nini, na mara mlango ukafunguliwa, sote tukageukia sasa kuangalia  mlangoni,…

Kimia kidogo...baadae mama mjane akasema;

‘Aheri umefika shemeji…’

NB:  HAYA MAMBO YAMEANZA, KAMA NI WEWE UNGELIFANYA NINI

WAZO LA LEO: Mwenyezi mungu anaweza kutupima kwa mitihani mingi, ….magonjwa, kukosa kazi,  misiba na kila jambo lenye kutia wasiwasi, na mashaka. Haya yakitokea, kamwe tusikimbilie kumshirikisha Mungu, au kuwashuku wengine kwa mambo ya kishirikina,..wengine hufikia kwenda kupiga ramli na mambo kama hayo, tukifanya hayo tutakuwa tumekufuru! Muhimu ni kuvuta subira, na kufanya taratibu halali, huku tukimuomba yeye, kutubu makosa yetu na hatimaye tutaishinda mitihani hiyo,…

Tumuombe mwenyezimungu atunusuru ni mitihani yenye kuzishinda nafsi zetu.
Ni mimi: emu-three

No comments :