Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, June 7, 2018

YOTE NI KWA MAPENZI YA MUNGU-8




 Nilipokea ile simu, ilikuwa ni yule wakili ambaye alikuwa akiishughulikia hiyo kesi ya huyo mama mjane na watoto wake…nilikuwa nimeshampelekea barua pepe, ya kumuomba ajaribu kuifufua hiyo kesi tena, na pia ajitahidi kuweka pingamizi , ili mnada wa nyumba usifanyike kwanza, kwani imekuja kundulikana kuwa deni hilo laweza lisiwe la mdaiwa,…

Nilipomtumia, hakunijibu hapo hapo, …alisubiria sana, baadae ndio akanindikia kwa kifupi,

‘Tutaongea….’hivyo basi tu

Kwahiyo siku ikawa nasubiri majibu kutoka kwake,…wakati huo huo nilikuwa nawasiliana na watu mbali, ambao niliona wanaweza kunisaidia, sikuwa na wazo la kwenda polisi. Niende polis kwa madai gani, hili nikaliweka pembeni kwanza

Sasa ndio huyo wakili akanipigia…

‘Wewe unasema tuifufute tena hiyo kesi, na tuweke pingamizi la kupiga mnada hiyo nyumba, hii ni kutokana na barua pepe yako,….mhh, unajua vitu kama hivi ulitakiwa uandike barua halisi ije pale ofisini, ipokelewe kwa utaratibu maalumu, ..sawa, hata hivyo hamna shida…’akatulia na mimi nikawa kimia tu.

‘Sasa, …nikuulize tu, una kitu gani cha ziada cha kuthibitisha madai yako..?’ akaniuliza

‘Usijali kwa hilo…kitakuwepo cha ziada,…wewe nipe muda,  kwa masilahi ya familia hiyo…’nikasema

‘Sikiliza, mimi ni wakili mwenye heshima yangu, najua kitu gani kinafaa na kisichofaa kwenye kesi kama hizi,..kama nilivyokuambia, nilipokuatana na huyo mama, kiukweli niliumia sana, nikaamua kuichukua kama ilivyo, bila kujali mambo muhimu…’akatulia

‘Kiukweli sijawahi kuumbuliwa..kama kesi hii,…unajua huruma, au hasira zinaweza zikakufanya ukafanya jambo bila kufikiria,…hiyo kesi haina mshiko, kitu cha kuibeba, hakuna ushahidi hakuna nyaraka….unajua,..sasa nikuulize, wewe umepata ushahidi gani mpya labda …?’ akaniuliza

‘Kwanza naomba ufanya kama nilivyokuagiza…kwenye hiyo barua pepe, mengine yatafuata tu, nipo kwenye michakato ya kukusanya ushahidi, usiwe na wasiwasi na hilo…’nikasema huku moyoni nikijua kuna kazi ngumu sana ya kulifanikisha hilo.

‘Ndugu yangu, sio swala la wasiwasi hapa…ni utaratibu wa kisheria,..usijifanye hujui hayo….’akasema akiendelea kulalamika.

‘Si ndio hivyo,…nimekuelewa..au…’nikasema

‘Na kuhusu swala la pingamizi, la kupiga mnada, hilo…unajua kosa alilolifanya huyo mama, licha ya kumshauri sana, ..ni kule kukubali kuwa swala hilo watalimaliza kinyumbani,..ni kwa vile alikiri kabisa kuwa hana pesa, na hana njia nyingine za kuweza kulipa hilo deni,…je wewe una namna nyingine ya kumsaidia huyo mama, kwenye kulipa hilo deni….?’ akauliza

‘Mimi sina pesa, ila pesa ya malipo, ya wakili, kama wewe na gharama nyingine, itakuja kupatikana tu,… muhimu ni wewe uwajibike kwa upande wako,…kuwezesha kesi hiyo kusimama tena,…na…kama una wasiwasi na malipo yako, wewe andaa nyaraka za kuthibitisha gharama zako, halafu baada ya kazi, utalipwa au..’nikasema.

‘Tatizo sio malipo, kwani nilipoichukua hiyo kesi awali nimelipwa nini, unanifahamu nilivyo…’akasema

‘Sasa tatizo ni nini…?’ nikauliza

‘Kupotezeana muda kwa kitu ambacho tulishakifanyia kazi…unanielewa hapo…’akasema

‘Ndugu yangu, na wewe unanifahamu nilivyo, lini nilikuomba kazi kama hizi ikawa ni kukupotezea muda, nikumbushe…’nikasema

‘Na hapa kwenye pingamizi la mnada…mhh, unajua labda nishauri jambo, ..tunaweza kulifanikisha hili kwa njia nyingine,...kama mtakubaliana nami…’akasema

‘Nakusikiliza wewe muheshimiwa….’nikasema

‘Tunaweza kuchelewesha kinamna, huo mnada, …lakini kwa njia hiyo itahitajika  gharama, je mnaweza kuwa na pesa, kiasi fulani, kufidia gharama za watu,…hao wa mnada, nk..umenielewa hapo…benki….nitajaribu kuongea nao, tuone,…sijui unanielewa…’akasema

‘Sawa, vyovyote uonavyo muheshimiwa, mimi nakusikiliza wewe, na kama kuna madai ya pesa, gharama za kulipa, ningeliomba yafanyike kimaandishi, kuwe na nyaraka za uthibitisho wa huduma hiyo, na malipo yatakuja kufanyika,..sio sasa, kwasasa hakuna pesa ya kulipa, wewe kama wakili udhamini hiyo, …’nikasema

‘Oh…ndugu yangu, mimi ndiye nidhamini, na hiyo pesa itatoka wapi, ..ndio maana nakuambia, hapo umeingia kwenye sehemu ambayo hujui chimbuko lake, …na hizi mbinu za kuchelewesha mnada,..pesa inahitajika kwa haraka, ..na sio rahisi kupata nyaraka kwa ..utaratibu huo, wewe mwenyewe unajua kuwa hilo tutalifanya kinyume na utaratibu…’akasema

‘Ndugu muheshimiwa, hayo yote nakuachia wewe, fanya upande huo, na mimi nifanye upande wangu, wa kukusanya ushahidi…ili haki iweze kutendeka, kumbuka huyu ni mama mjane, na watoto wake, kumbuka yeye hajaomba hili litokee, kumbuka hata wewe una familia, kumbuka…ndani ya hili kuna dhuluma,……’nikasema na yeye kwa haraka akanikatisha.

 ‘Sikiliza…wewe hujui jinsi gani nilivyohangaika na hiyo kesi ya huyo mama, kwa gharama zangu mwenyewe,..sijui kama ameweza kukuambia hilo… lakini sio hoja, je nikuulize kwanza, je umeweza kuongea na huyo shemeji wa huyo mama, ambaye ndiye msimamizi wa mirathi, ya hiyo familia..?’ akauliza

‘Sijaongea naye bado …yeye hayupo…’nikasema.

‘Ndio maana….unajua …wewe unataka kufanya hivyo kwa kigezo cha huruma tu,..lakini kama ungeliwahi kuongea na huyo jamaa, akakuelezea vyema, ungejirizisha kabisa…nakushauri kitu kimoja, hebu kwanza ongea na huyo jamaa, ili tusipoteze muda,..’akasema.

‘Nitaongeaje naye wakati yeye hayupo, na hata kwenye simu hapatikani…’nikasema

‘Ok,..ngoja nione la kufanya…’akasema na kukata simu.

Nilipomaliza kuongea na hiyo simu mama huyo mjane akawa na hamu ya kusikia nilichoongea , akaniuliza;

‘Wanasemaje…?’ akauliza

‘Bado…ila tuwe na matumaini tu…’nikasema

‘Mbona hujawauliza,kama kweli kesho wanakuja au hawaji kupiga nyumba mnada..?’ akauliza

‘Labda nikuulize wewe kwanza, je upo tayari kwa mapambano,…ili kuinusuru nyumba yenu…?’ nikamuuliza, bila kujibu swali lake,…nahapo akabakia kimia hakusema neno. Nikamuelewa, na baadae nikamuuliza;

‘Unasema mlikwenda  mahakamani, ..mlienda kwa dhumuni gani hasa, ni nini ulikuwa msingi wa kesi yenu…?’ nikauliza

‘Msingi wa kesi yetu ilikuwa kuhakiki kama kweli hilo deni ni la kweli au la….ina maana mimi nililalamika kutokukubaliana na hilo deni…’akasema

‘Ok,…kwahiyo kesi ikafanyika dhidi ya benki au sio…?’ nikauliza

‘Ndio…nikaambiwa nipeleke vielelezo, vinavyoonyesha msingi wa madai yangu,…na sikuwa na vitu vingi, zaidi ni hiyo statement ya benk, na mkataba,…’akatulia

‘Ambayo ni ushahidi wa benk kuwa kweli mnadaiwa, …’nikasema

‘Hatukuwa na namna nyingine ya kujitetea, nikatoa maelezo yangu, nikaulizwa ushahidi wa maelezo yangu, au mashahidi..’akatulia

‘Ehe,…mashahid uliwaita akina nani..?’ nikauliza

‘Mashemeji zangu na yule mzee, lakini huyo mzee hakupatikana kutokana na dharura zake…’akasema

‘Na wao waliongea nini cha kukusaidia wewe, yaani hao shemeji zako…?’ nikauliza

‘Walichoongea ni maneno tu, kama ilivyokuwa mimi, na walipobanwa na maswali walijikuta wakishindwa kujitetea, …’akatulia

‘Na mahakama iliamua nini…?’ nikamuuliza

*****************

‘Hayo ya Mahakamani we achana nayo tu, maana tulitakiwa tutoe ushahidi, tukatoa, ..kiukweli ilionekana kama tunapoteza muda tu, japokuwa mahaka hawajsema hivyo, kuwa tunapoteza muda….’akatulia

‘Wao mliowalalamikia walisemaje…?’ nikauliza

‘Upande wao, walitoa vielelezo vyote, walisema hilo deni lipo kisheria, sio kwamba nasingiziwa,  wakaniuliza kama ulivyoniuliza wewe kuhusu sahihi ya mume wangu, kama ndio yenyewe, kama naifahamu….nikakubali kuwa ndio yenyewe, maana naifahamu…’akatulia

‘Ehe,…’nikasema hivyo

‘Na wakili wao akadai kuwa sisi tunafahamu kuwa deni hilo lipo, ndio maana tukaomba kuliendeleza, na kuna muda tulifanya marejesho kiasi,…kuthibitisha kuwa tunalifahamu hilo deni,…ikafikia muda hatulipi kabisa,…na wanashangaa wakisikia kuwa mimi nadai silitambui, wakati hata mimi niliweka sahihi yangu kuendeleza hilo deni….’Akatulia

‘Je wewe uliweka sahihi..nataka uwe na uhakika na hilo, je kweli uliweka sahihi…?’ nikamuuliza

‘Mimi sijui…sikumbuki kufanya kitu kaam hicho…’akasema

‘Wakati umeanza kurejewa na fahamu zako, na kuwa na hali ya kujitambua, je shemeji yako alikuwa akifika kwako kuomba jambo, mfano, akitaka kwenda benki, au kwenye jambo ambalo na wewe ni lazima uhusikane…?’ nikamuuliza

‘Ndio mara kwa mara alikuwa akifika kwangu,..kuna vitu vilihitajia mimi na yeye kushirikiana, asingeliweza kuvifanya bila mimi…’akasema

‘Kama vipi…?’ nikauliza

‘Kuna malipo yake ya kazini, alikuwa hajachukua kuna malipo…ambayo ilitakiwa sote tuweke sahihi zetu, …’akasema

‘Hayo unayakumbuka au sio, na uliweka sahihi, ..?’ nikauliza

‘Ndio..’akasema

‘Ok…kwenye hatua hiyo ya kuwa wewe uliweka sahihi, ukasema hujaweka,…ulijiteteaje huko mahakamani, au wakili wako alikusaidiaje nataka kusikia hapo kidogo…?’ nikauliza

 ‘Kwenye kipengele cha sahihi, wakili wangu, aliingilia kati kuwa wao wanajichanganya…kwanza wamesema kuwa, mimi nilisahau, nilikuwa na tabia ya kujisahau, kwahiyo niliweza kuweka sahihi na kusahau, ..kwahiyo hiyo ina maana kuwa, mimi nilikuwa sijapona vyema,..’akatulia.

‘Ehee…ikawaje sasa…’nikauliza , kwani muda huo nilikuwa nasoma, ujumbe wa maneno kutoka kwa watu wangu.

‘Wakili wangu aliendelea kusema, yawezekana kuna mtu alitumia mwanya huo wa kunifanya niweke sahihi, kam ni kweli niliweka, maana sahihi ni yangu, na mimi nimekiri kuwa sahihi ni yangu,..…, kukawa na malumbano hapo ya kisheria…mimi hata sikuyatilia maanani…’akatulia kidogo

‘Basi wewe uliweka sahihi, halafu ukasahau kuwa uliweka…’akasema wakili wo

Nilijaribu kupinga lakini haikusaidia kitu…wakili wangu akaingilia kati…unaelewa, eeh, basi…’akatikisa kichwa na mimi nikamuuliza;

‘Je una uhakika kuwa kweli hukuweka hiyo sahihi yako..hebu jaribu kukumbuka vyema..?’ nikamuuliza

‘Sikumbuki kwakweli…’akasema kama akijaribu kujikumbusha

‘Kwa hali kama hiyo wewe mwenyewe unahisije, eeh… kuwa kuna mtu alikufanya ukasaini..au kuna mtu kagushi sahihi yako…?’ nikauliza

‘Kwa hali kama hiyo,..kiukweli hata mimi ..najiuliza tu bila majibu, siwezi kusema kitu, na,. nitamuhisi nani sasa…nimeweza sana hilo,…’akatulia

‘Kama binadamu ni lazima kuna mtu unamuhisi hisi au sio..?’ nikauliza

‘Mhhh…mtu, ha-ha-pana,…nitamuhisi nani sasa…mtu wangu wa karibu, mwenye shughuli na benki ni shemeji , lakini siwezi kumshuku yeye,.., nitamshukuje yeye, maana ..yeye ndiye  kanisaidia sana, atawezaje kufanya kitu kama hicho …’akasema .

‘Kwahiyo yeye shemeji yako alithibitisha mahakamani kuwa, wewe uliweka sahihi kuendeleza hilo deni..?’ nikamuuliza

‘Ndio…na ndiye aliyesema huenda kwa vile wakati huo nilikuwa na tatizo la kusahau ndio maana sijakumbuka..’akasema

‘Mhh..ulikuwa ukisahau..?’ nikauliza

‘Ndio hapo nikaanza kumshuku shemeji yangu, kwanini ananishikiza kuwa kweli nilifanya hivyo, wakati mimi nahisi sio kweli….’akasema

‘Wakili wako alisemaje..?’ nikamuuliza

‘Kiukweli wakili wangu alipambana na hilo, kuwa kumbe walifahamu kuwa mimi bado ni mgonjwa ni kwanini walifanya niweke sahihi, …?’ wakaulizwa

‘Kuweka sahihi haikuwa tatizo kwake, alishafanya hivyo kwa vitu vingine, kabla ya hilo la sahihi ya deni, na hata docta akathibitisha kuwa kweli nilikuwa vyema kiakili, …’wakasema

‘Kwahiyo kam ulikuwa vyema kiakili, ni kwanini hilo waseme umeshau…?’ nikamuuliza

‘Ni kauli ya shemeji…hata wakili wangu aliuliza hivyo kwa shemeji, na mwisho wake akatamka maneno ambayo sikuyapenda…’akasema

‘Maneno gani…?’ nikauliza

‘Eti, mimi naogopa tu kusema ukweli, ila kweli niliweka sahihi, ..wakili wangu akambana kumuuliza, je, ulimwambia ni deni…akasema ndio, hapo ndio alinifanya niongee vibaya, hadi wakili wangu akanisihi nitulie.

‘Baadae wakamuita shahidi ..ambaye ni docta aliyethibitisha kuwa mimi kipindi hicho nilikuwa naendelea vizuri, kwani tarehe hizo niliwahi kufika hospitalini, nakuonekana naendelea vyema..basi, ikaonekana mimi nadanganya, ..najua kuhusu hilo deni, …iliniuma kweli kweli…hasa pale wakili wao aliposema;

‘Kwa ushahidi wa docta inaonyesha mgonjwa hakuwa na hali na mbaya ya kushindwa kuweka sahihi,… ndio maana hata akakumbuka sahihi yake, mgonjwa alijua kuhusu hilo deni, hapa anafanya kudanganya mahakama…hapo nikaangua kilio…’akasema.

Kulipita kipindi kidogo cha ukimia, ndio baadae nikauliza hivi;

‘Baada ya hapo, si mlirudi nyumbani…, mkaja kukaa na shemeji yako kuongea, jinsi gani ya kuendeleza hiyo kesi, au mlikasirikiana, na ndio mkaja kukata tamaa moja kwa moja…?’ nikauliza

‘Hakukasirika kivile,..yeye alikimbilia kinilaumu tu, … kwanini simuamini..wakati amekuwa akiwajibika kwa ajili yangu na watoto, na anafanya hivyo akijua hiyo ni familia yake,..kama alivyokuwa kaka yake….alisema mengi, ..mimi ndio nikamwambia;

‘Shemeji nisamehe kwa hilo, …pamoja na hayo, bado mimi nataka kwenda mbele zaidi, maana nina uhakika hilo deni sio sahihi kuna kitu kimechezwa hapo…’akasema hivyo na kukaa kimia, kama ananisubiria mimi niulize swali, na ndio nikauliza hivi;

‘Akasemaje…?’ nikamuuliza

‘Yeye alisema, nitafika muda nitashindwa maana ukweli imeshabainishwa, na cha muhimu ilikuwa tukae tujadili tuone jinsi gani ya kupambana na hili tatizo…je kweli tunaweza kulilipa hili deni, au… ila kama kuna namna nyingine yeye bado yupo tayari kusaidia, maana hata yeye, hakuwa analifahamu hilo deni, kipindi cha awali, akasema;

‘Hata mimi shemeji nashangaa sana, na huenda …yawezekana, lakini kwanini kaka akanificha, na wakati mimi ndiye nilikuwa mtu wake wa karibu, na wakati mwingine yeye ndiye ananituma hata benki…’akasema hivyo

‘Alikuwa anatumwa benk….kufanya nini….?’ Nikauliza

‘Sijui…wanajuana na kaka yake, yeye alitamka hivyo..’akasema

‘Hebu niambie kuhusu shemeji yako jinsi gani unavyomfahamu, kiuadilifu na jinsi watu wanavyomuongelea huko nje, na haa kuhusu yeye na marehemu…?’

‘Kiukweli shemeji yangu ni …mtu mwema sana, katika ndugu zake, yeye alikuwa kipenzi cha marehemu,..kila jambo, atamuita yeye, hata kutaka ushauri wakati mwingine, unajua mume wangu hakuwa mbinafsi,..alipenda kila jambo liwe wazi hata kwa ndugu zake, alipenda kutumia, ‘kuna leo na kesho….’akatulia

‘Baada ya maongezi hayo ikafuta nini..?’ nikauliuza

‘Yeye shemeji, akasema atazidi kufuatilia zaidi, hasa huko benki kuona kama wanaweza kutusaidia,, kwa vile sasa imeshathibitishwa kisheria kuwa kweli hilo deni lipo, iliyobakia ni kuomba huruma yao,….na kwa vile mdaiwa keshafariki basi huenda wanaweza kulifuta hilo deni.

‘Je ni kweli alifuatilia…?’ nikamuuliza

‘Ndio, kiukweli shemeji kwenye mambo hayo ya kufuatilia jambo, ni mwepesi sana, si unajua kazi yake ilivyo…..alihangaika sana…akaja kuambiwa, deni haliwezi kufutwa, maana ni kubwa sana, …kama hatuwezi kuendelea kulipa, kidogo kidogo, basi, hatua nyingine itafuta kwa mujibu wa mkataba …’akasema

‘Je wewe uliusoma huo mkataba vyema, unasemaje….?’ Nikauliza

‘Ni mkataba wa kawaida wa kukopeshana, mtu na benk..kama, ujuavyo benk wana taratibu zao, na umeelezea vyema kila jambo…na nyumba ikawekwa kama dhamana, na kama itatokea tatizo la mdaiwa kufariki,  nk..nyumba hiyo inaruhusiwa kupigwa mnada…kisheria…’akatulia

‘Hata hayo waliandika, kuwa ikitokea mtu kufariki, nyumba itapigwa mnada, …?’ nikauliza kwa mashaka

‘Ndio..ipo…niliona…’akasema kwa kusita sita

‘Na kwenye kumbukumbu zako, ..je deni hilo kipindi marehemu yupo lilikuwa linalipwa kwa usahihi wake..ilivyojionyesha kwenye statement..?’ nikauliza

‘Kuna madai kuwa hata marehemu wakati yupo hai , mkopaji (yeye marehemu) alishaanza kuvunja  mkataba, kwa kutokulipa kama ilivyokubaliwa,kuashiria kuwa mkopaji alifanya makusudi,…mmh kuna maelezo hap mengi tu,..ila kwa ushahdi walitoa barua ya kumuonya mkopaji…..na mambo mengine  ya kisheria, sitaki hata kuyakumbuka…..’akasema

‘Kwahiyo kumbe, mkopaji alikuwa anafahamu….!?’ Nikauliza kwa mshangao.

‘Kwa madai yao ndio…lakini mimi sikuwahi kumsikia mume wangu akilalamika kuhusu hilo deni lolote, ndio maana mpaka leo siwezi kuamini hilo…’akasema

‘Ikawaje sasa…?’ nikauliza

‘Shemeji alikanishauri jambo, kuwa …. Labda na mimi nijaribu bahati yangu, niende huko benki huenda watanionea huruma kwa vile mimi ni mjane na nina watoto…ikabid kweli nifanye hivyo, lakini hakuna la zaidi , wao walitaka nikiri kuwa nimeshindwa kulipa hilo deni ili taratibu zingine za kisheria zifuatwe, kitu ambacho sikutaka kukubaliana nao..’akasema

‘Kwanini, wakati mahakama imeshathibitisha hivyo kuwa dni hilo ni halali na mume wako ndiye alikopa hiyo pesa..?’ nikauliza

‘Nilijua ni mtego, na kwanini nikiri kuwa hilo deni ni sahihi, wakati, sio kweli…sikukubali hilo kabisa, …ndio nikirudi nyumbani, na shemeji alipokuja akaniuliza imekuwaje, nikamwambia nilivyoambiwa huko benk, ….mwishoni akaniambia, unaona hata mimi niliambiwa hivyo hivyo…’akasema

‘Kwahiyo ikawaje?’ nikamuuliza

‘Ukumbuke kesi ya kwanza, ilikuwa ni namna ya kujirizisha kuhusu hilo deni kama ni la kweli au sio la kweli, na ikathibitishwa kuwa hilo deni ni la kweli kisheria…sasa katika kuhangaika ndio nikakutana na huyo rafiki yangu, nilisoma naye, nikamuelezea wee, akasema ngoja akaongee na mume wake, mume wake ni askari polisi…’akatulia

‘Oh…’nikaguna hivyo.

‘Baadae akanipigia simu, yaani huyo rafiki yangu, akasema mume wake kashauri kuwa , kwa vile bado sijarizika na hukumu,…na imefikia hatua nashuku kuwa huenda kuna mbinu zilifanywa kupatikana kwa hilo deni, basi,..nikafungue kesi ya madai ili upelelezi,ufanyike….’akasema

‘Kwahiyo kumbe uliwahi hata kufika polisi,…ni…iih,  kwa nia ya kuomba upelelezi ufanyike, ili kujirizisha kama kweli hilo deni lilipatikana kihalali au sio, vizuri sana,… je ulipofika huko walikuhoji vipi, maana hapo ulifanya sahihi kabisa..?’ nikauliza

‘Walinihoji mambo mengi tu, na mengine ni kama walivyofanya huko mahakamani, nikawapatia nakala ya hukumu,…baadae wakaniuliza ni kwanini siamini kuwa deni hilo ni halali kwa marehemu..nikawaambia kila kitu, baadae ndio wakauliza, ni nani naweza kumshuku kufanya hujuma kama hiyo..’akasema.

‘Ukawajibuje…?’ nikauliza

‘Mimi niliwaambia nionavyo mimi, ..yaani niliwaelezea kama nilivyokuelezea, sikutaka kuficha kitu, na nikaongezea kuwa mtu wa karibu sana ambaye anaweza kujua zaidi  kwenye hilo deni, sio kumshuku, ila kufahamu na kuweza kusaidia zaidi ni shemeji, ila nikawapinga hiyo kauli yao ya ‘kushuku’,…’akasema

‘Ukamtaja shemeji yako,..wakati huo yeye hayupo au sio,….sasa Ikawaje..?’ nikauliza

‘Huyo mume wa rafiki yangu alinitafutia askari mpelelezi mnzuri tu, ambaye anaelewa sana mambo hayo,na haraka akaanza kazi yake,…na ,…tahamaki shemeji anakuja kukamatwa…’akasema

‘Kwa kosa gani …?’ nikamuuliza na mara simu yangu ikawa inaingia ujumbe, na haikupita muda, mtoto wa huyo mama naye akaanza kulia…

NB: Leo nipo kwenye wakati mgumu kidogo, ngoja niishie hapa kwa leo


WAZO LA LEO: Katika tuhuma,…wengi ni wepesi sana kuwanyoshea wenzao vidole kuwa wamekosea, kuwa ni wabaya, nk….lakini twashindwa kujituhumu wenyewe kuwa nasi twaweza kuwa na makosa kama hayo, na pengine zaidi ya hayo tunayowatuhumu wengine. Ni vyema, tukajirizisha kwanza kwenye tuhuma yoyote, kabla ya kuwanyoshea wengine vidole.

Ni mimi: emu-three

No comments :