Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, June 26, 2018

YOTE HAYO NI KWA MAPENZI YA MUNGU-14


‘Mungu wangu’…nilijikuta na mimi nimesema hivyo

Kiukweli matukio ya siku hiyo, yalikuw ni mtihani kwangu, maana pamoja na nia nzuri niliyokuwa nayo kwa hii familia, lakini baada ya hayo matukio, …niliwaza mara mbili tatu…maana jiulize litokee jambo baya kwa mtoto, mim nitajielezaje, hasa jamaa akielezea kuwa mimi niliambiwa hayo mambo na mimi nikapuuzia,

Mama ataulizwa je, ni kweli, akisema ni kweli nimekwiisha

Kiukweli pale nilianza kujilaumu mimi mwenyewe..nikiona huenda nimefanya kosa,..mimi ndiye  nimesababisha kifo cha huyo mtoto, maana mtoto nilivyomuangalia, hana dalili ya uhai,..sasa imegeukia kwa mama, naye kwa hali kama hiyo kama ile hali ya kupooza mwili itamrejea, siji itakuwaje

 Wakati sasa mimi nahangaika na huyo mama, awali nilimuona jamaa akihangaiak na simu yake, ni kama anaandika ujumbe kwenye simu, kwa muda huo alijifanya kama hana wasiwasi, mimi kwa hasira nikasema;.

‘Hebu fanya jambo wewe mtu mbona umesimama tu..huu sio muda wa kucheza na simu unakuwa kama mtoto bwana, simu zipo kila siku …., hangaika na mtoto ili mimi nimuhudumie huyu mama,…au … unajua kufanya huduma ya kwanza,..au basi hata  ita usafiri, tuwawahishe hawa watu hospitalini…’nikasema

‘Niwapigie hospitali gani, utaweza kuita gari la wagonjwa hapa nyumbani, mimi hapa nilipo sina hata senti moja..najaribu kuomba chochote kwa jamaa yangu hapa,…unasema nacheza na simu, ..hahaha, hivi unafikiri mimi sina uchungu na hii familia, hapa natafuta pesa, bile pesa hapa, tutaumbuka…’jamaa akasema
‘Kwahiyo sasa umenielewa, kuwa hawa watu ni wa hospitalini..?’ nikawa kama nauliza

‘Hospitalini,..wakipigwa sindani hawa ndio basi tena..na huyo mtoto..hapana, …ngoja kwanza…’jamaa akasema, na kuanza kupiga namba kwenye simu, kiukweli sikumuelewa kwa muda huo.

‘Unawapigia watu wa usafiri, au…tuwahi hospitalini..?’ nikauliza

‘Huyu jamaa namdai pesa yangu, ni tapeli mkubwa,, we acha tu….sasa oh…unajua wewe haumini nilichokuambia, tatizo hata mtaalamu hapatikani kwenye simu sio kawaida yake, ..na haya yote wewe ndiye sababu…’akasema sasa akifuta jasho usoni.

‘Huu sio muda wake, muda huu ni wewe uwajibike kwanza, usilete visingizio vya kupoteza muda, na lolote likitokea baya, unafahamu sehemu yako..’nikasema

‘Ni lazima nikuambie ukweli …maana mimi nitafanya nini sasa..huyo mtoto..mwili wote umeshakuwa wa baridi..damu haifanyi kazi, hii ina maana gani ….nilikuambia lakini, hana hata semu moja ina joto, na mapigo ya moyo, siyasikii kabisa, hii ina maana gani…’akawa kamsogelea mtoto akamshika mwilini, kuanzia miguuni hadi shingoni, halafu akaweka kiganya cha mkono usoni. Hapo akahema kwa nguvu.

‘Mama yangu…’akasema hivyo…hapo sikuona dalili ya kuigiza, hapo niliona uso wa wasiwasi kabisa, jamaa alikuwa kachanganyikiwa.

Mimi kwa upande wangu nilikuwa nikijaribu kumuhudumia mama mjane, ili aweze kurejesha fahamu zake, lakini ilikuwa kazi isiyo na mafanikio, hata baada ya kutumia kila mbinu ninayoifahamu mimi, maana nilishajifunza hayo yote kupitia huduma za msalaba mwekundu nilipoona nimeshindwa…huku najifuta jasho..

Kwa haraka nikachukua simu yangu pale mezani nikampigia jamaa yangu;

‘Halooh, sasa hali ni mbaya zaidi, fanya haraka, upo wapi kwani, sasa fanya hivi, wapigie watu wa huduma ya kwanza, ndio kazini kwenu, mimi sina jinsi,…ni hatari, ni …ukifika utajionea mwenyewe…’nikasema na kumsikiliza

‘Anahitajika dakitari, na gari la wagonjwa, pia chakula,…ndio, hali zao ni mbaya sana, hawajala, na zaidi…ndio ndio..jitahidi sana ndugu yangu, hili sio jambo la kuongelea kwenye simu, haraka..,..’nikasema kwa sauti ndogo ndogo, hata jamaa yangu hakunielewa nimeongea nini, ..ila pale niliposema;

‘Mje na kila kitu …nahisi kuna uhalafu, kuna hujuma ndani yake, ni..sina…ila nahisi hivyo, uje ,, ufanye kazi yako…u…’hapo nikasema kwa nguvu na jamaa akasikia, na kunitupia jicho….huku akiendelea kulalamika.

 ‘Sasa unaona, haya yote umeyataka wewe…unaona wewe mtu…sijui umetoka wapi wewe hukutaka kunielewi, wewe umeweka njaa yako mbele…huyu mtoto tumeshampoteza, hii hali sio ya kawaida, kama ubaridi umeshaenea mwili mnima,..ndio basi tena,..mungu wangu na isiwe hivyo, nitafanyaje mimi,….. sasa na shemeji naye ndio hivyo, hilo ni janga jingine tena..’akasema akimuangalia shemeji yake…

‘Hata sijui..’nikasema hivyo, huku nikimpigia jamaa yangu mwingine simu, kujua ni nin kinachoendelea kwenye kusitisha zoezi la mnada, lakini akawa hapatikani. Jamaa sasa akamuacha mtoto na kusimama, akawa ananiangalia mimi na kusema;

‘Sikiliza nikuambie sasa, …hali ya shemeji haikutakiwa kabisa apoteze fahamu, maana ikirudia ile hali ndio basi tena,… hata sijui itakuwaje…huyu mtu hakutakiwa tena kupoteza fahamu kwa mshtuko,..unajua ilivyokuwa tena hayo ni maagizo ya docta , bingwa wa magonjwa hayo, …unajua, huyo awali alikuwa kafanya nini,..ka-kaparalize,…si unaelewa matatizo hayo yalivyo…?’ akawa kama ananiuliza na mimi nikabakia kimia tu

‘Na hayo,unasikia, ni wewe umeyasababisha, hapo huwezi kukwepa lawama,  haya umeyataka wewe mwenyewe kwa ukaidi wako, sijui wewe ni mtu wa wapi...’akasema sasa akihangaika na mtoto, na mimi sasa nikamrudia shemeji yake…hapo nikasema;

‘Nimeyataka mimi au wewe na huyo mtaalamu, wako…, ngoja polisi wafike hapa , utasema yote , nataka waje ili hili tatizo limalizike kabisa,…..’nikasema, na niliposema hivyo, kwanza akanitupia jicho, halafu akasema.

‘Polisi…!!! Hahaha, polisi watafanya nini kuhusu hili tatizo, haya ni maswala ua kifamilia, hata wakija nikiwaelezea, watasema kama tulishasema ni maswala ya kifamilia, basi yaishe kifamilia, maana ni maswala ya kimila..sasa haya umewaita polis waje kufanya nini…?’ akauliza

‘Kumbe unalijua hilo, kuwa sio swala la kipolisi ..lakini hata iweje lazima uwajibike,..najua kabisa unafahamu ni nini kinachoendelea hapa..ndio maana unasema hivyo, sasa ngoja tukuone ukipambana na hao watu..’nikasema

‘Tatizo wewe unafikiri naogopa saana, hapana, kwani ni mara ya kwanza kukutana nao…ukweli ni ukweli hata wakija, hata wakinifanya nini..mimi nitafanya nini, kama sina uwezo na jambo sina, …waje tu…’akasema kama kujipa moyo.

‘Wewe unalifikiri natania, nataka kwanza uje kunielewe kuwa mimi ni nani…’nikasema

‘Haijalishi…’jamaa akasema hivyo

‘Haijalishi sio…, ngoja hao jamaa waje ndio utaniamini kuwa mimi nipo hapa kwa madhumuni gani, hatuwezi kuendelea kuendekeza haya mambo, haki ya wajane na mayatima zinadhulumiwa na watu kama nyie, mnaojifanya wajanja…’nikasema

 Jamaa akawa anahangaika na mtoto, huku anasema;

‘Oh…haya bwana…ngoja nijaribu tena, ila…mimi sijui huenda nazidi kuharibu zaidi, maana mimi nafuata tu maagizo…’akasema hivyo, na wakati huo alikuwa kashikilia kile kichpa chenye unga unga ndani yake,.

Akatoa unga unga.. akawa anachezesha mkononi halafu akamweka mtoto puani….lakini mtoto akawa kimia…alipoona hivyo, sasa nikamuona jasho likianza kumtoka…akwa anampapasa mtoto kuanzia miguuni, hadi usoni…, uso wa jamaa sasa ukawa umeashiria mashaka na wasiwasi, akafanya tena, alafu akasema;

‘Mungu wangu..ina maana ni kweli…na hapa nimefanya kinyume na maagizo sikutakiwa kufanya tena hivyo,…oh, sijui itakuwaje mungu wangu..’akasema sasa akihaha.

‘Ina maana gani kusema ina maana ni ?…hahaha, sasa omba kusitokea tatizo, likitokea taizo huyo mtoto akapoteza uhai, ujue wewe utahesabika kuwa ni muuaji,..hilo sasa ni kosa la mauaji, umeua..mlifanya mkijua mnafanya mzaha..’nikasema.

‘Sikiliza mimi nafuata alivyosema mtaalamu, yeye alisema hivyo, mimi sijui zaidi mbona unanipakazia mambo ambayo mimi hayanihusu…’akasema

‘Hayo utayesema mahakamani ukiwa umesimamishwa kwa kosa la kuua..’nikaema

‘Sikiliza, ngoja nimpigie huyo mtaalamu  mwenyewe, maana hili sasa ni tatizo…, haiwezekani…uuuh…’akawa sasa kaonyesha kuchanganyikiwa kiukweli, nashukuru mama mjane  alikuwa bado hajazindukana, japokuwa na kuendelea kuwa hivyo ni tatizo pia

Mimi pale nikawa najitahidi tena kumpatia huduma ya kwanza yule mama ili azindukane lakini ikawa …hazindukani, ila nilihisi dalili ya joto, kuashiria bado uhai upo, nikahisi mapigo ma damu kwa mbali sana, hapo nikapata matuamini,..ghafla nasikia jamaa akisema

‘Shemeji, shemeji…..mtoto ame—ame---ku-ku…fa…’akawa anaongea huku kashika kichwa..
**************

‘Wewe mtu vipi wewe...nani kasema mtoto kafa…’kwa haraka nikamuacha shemeji, na kumsogelea jamaa, nikamsukuma pembeni.

Nilimsogelea mtoto,…sasa kwa tahadhari kama vile unashika kitu cha kuogofya, binadamu akili zetu ni dhoofu sana, hapo akili ilishahisi huyo mtoto hayupo tena duniani, kwahiyo …..taratibu nikamshika yule mtoto mwilini, mtoto alikuwa baridi…nikahisi mwili mnzima ukiniishia nguvu kabisa,..magoti sasa yanacheza cheza,…akilini nasema

‘Mimi ndiye nimeyasababisha haya…’ nikajikuta na mimi nimeduwaa..nimeshikwa na bumbuwazi, siamini hicho ninachokiona. Kwa jinsi inavyoonekana mtoto hana uhai,haiwezekani mwanadamu ukawa baridi hivyo.

‘Ina maana imekuwa ni kweli…haiwezekani…’nikasema sasa nikizama kwenye ibada, kumuomba muumba wa mbingu na ardhi, anikwepeshee na kikombe hicho,…kiukweli, hata mimi ule uwezo wa kuhimili jambo, uliniishia hapo nikiwazia mbali.

Na hapo hapo machozi yakaanza kunilenga lenga, maana hao watoto nilishawaweka kama ni watoto wangu, na hali niliyowakuta nayo, haikutakiwa ije itokee jambo kama holo, nilijikuta machozi yakianza kunilenga lenga. Lakini kwenye nafasi nyingine ikaniambia; ‘sio kweli, na wala usilie, huo ni uchuro..’

‘Mimi niliwaambia, mumeona sasa, ….’jamaa akawa anaongea huku sasa yeye analia..nilimuangalia moja kwa moja usoni, niliyaona machozi yake, sizani kama hiyo ni ya kuigiza,..jamaa kweli analia, kwahiyo ni kweli mtoto hatunaye duniani.

‘Haiwezekani…’nikasema sasa nikimkodolea macho yule mtoto.

‘Sasa mnaona..mimi niliwaambia nini.... wewe ndiye mbishi, wewe ndiye umemshawishi shemeji akafanya mambo kinyume na miiko aliyopewa, mimi hapo sijui tena la kufanya….’ Jamaa akasema sasa akigeuka  huku n akule, kawa kama kachanganyikiwa.

‘Sikiliza huyo mtoto hajafa…’mimi nikasema

‘Hajafa, hahaha, utafiki nacheka kumbe moyoni naumia...wewe..na uerevu wako, hujui mtu akifa anakuwaje..shika mapigo ya moyo, utaniambia…angalia alivyo, mimi ndio nimemfunika macho..huyo mtoto hatunaye tena...mungu wangu sijui mama yake...oops...’jamaa akasema

‘Una uhakika na unachokisema, unajua hatari yake…’mimi nikasema hivyo


‘Niliwaambia hatakiwi itokee zadi ya mara tatu, ni nani alinisikiliza eeh..mliniona mimi mjinga, au sio, mimi naendekeza mambo ya..ya….mimi siliniwaambia hivyo jamani… na miiko imenikataza kufanya lolote baada ya hapo..'akasema

'Mimi sijui ...'nikasema

'Ndug yangu hili ni janga, ...na...na..hebu ngoja kwanza, nimpigie simu huyu mtu, sijui atawezaje kutusaidia..maana mtoto keshapoa, aliniambia ikifikia hiyo hali haiwezi kusaidia kitu...’jamaa akasema huku akianza kupiga simu

'Sawa mpigie,...na umuambie kabisa, njama zenu zimeshagundulikana na ...yeye na wewe mtawajibika...'nikasema huku nikimtupia macho yule mtoto pale alipo,..nilihis mwili ukinisisimuka.

‘Jamaa hayupo hewani,..mungu wangu sasa tutafanya nini..’akasema sasa kijaribu kupiga simu tena na tena.

‘Hapokei,..simu haipatikani…’akasema sasa akiwa kashusha mikono ile ya kukata tamaa

‘Polisi wanakuja, watakuja kulimaliza hili tatizo, itabidi uongee kila kitu, na ufahamu wapi mtaalamu huyo alipo vinginevyo haya yote yatakuangukia wewe mwenyewe, hizi zote ni tamaa zenu, na usiposema yote, utaozea jela..’nikasema

‘Kwanini unasema hivyo, mimi sikuwaambia hayo, ..haya ni mambo ya kimila yanawahusu nini polisi,,… mimi nafuata alivyosema mtaalamu…’akasema sasa akijaribu kupiga simu tena, lakini hakuna kitu

‘Kwa usalama wako,  huyo mtoto hali yake ijirudie ili huyu mama akiinuka hapa amkute mtoto wake yupo salama, vinginevyo, wewe ndiye umemuua, unasikia, mimi ni shahidi wa haya yote, nimekuja kugundua kuwa nyie mna njama, sasa kazi kwako….’ Nikasema lakini kusema huko ni kwa kujipa moyo tu, kama kweli huyo mtoto keshakata roho, jamaa atafanya nini.

Mara simu yangu ikaita, kwa haraka nikaichukua na kuangalia ni nani mpigaji, …walikuwa vijana wangu, nikaanza kuongea nao .

‘Vi-vipi mumeshafika kituo cha polisi, …..sasa waambie waje hapa haraka,…na yeye mumempata, bado kwanini, sasa sikilizeni,..sikilizeni kwanza..hapa eeh….kuna tatizo kubwa sana hapa, nimemuambia huyo askari aje, yah..aje haraka..yule mpelelezi ndio, …msiimcheleweshe tena, ..ndio tatizo kubwa sana…’nikasema na kusikiliza

‘Ok…wewe unasema nini, ok, ok, nimekuelewa, sasa ….uje na huo ushahidi, ..fanya haraka…’nikasema .

*************

Wakati naongea na huyo jamaa yangu...huku kwa Dalali, pamoja alikuwa akihaha huku na kule lakini alipoona naongea kwa simu, na ...akasikia nikiaka polisi,...sasa akatulia na kuanza kusikiliza...na alipoona namtupia jicho, akaendelea kuhangaika na mttoto, mara asimame, mara afanye hiki na kile, ..alikuwa kiukweli keshachanganyikiwa,.hasa aliposikia nikitaja polisi,

Baadaye akasimama, akiwa kashika kiuno, naona alichoka ile hali ya kuinama akiwa anahangaika na huyo mtoto, akafuta jasho...alisimama vile kwa muda, na baadae kama kakakumbuka jambo, akauendea ule mkoba wake, akatoa chupa,...ilikuwa chupa ya mafuta.

Akarudi pale kwa mtoto, ...

'Mungu wangu nakuomba hii dawa, haya mafuta, yafanikishe,..mimi sijui zaidi ya uwezo wako, huenda nilikosea kutumia hizo dawa zaidi ya mara tatu, mimi sikujua, natarajia uwezo wako tu ..ewe mungu wangu...'jamaa akawa anasema hivyo, halafu, ...

Akamvua yule mtoto nguo zote...

'Inabidi tufanye hivi, ili mafuta haya yapite sehemu zote za mwili, huenda joto litarudi..lakini lisiwe joto la ugonjwa tena...'akasema, na mimi hapo sikusema kitu.

Akampaka huyo mtoto mafuta mwili mnzima, akimgeuza huku na kule, mtoto alikuwa ni kama ...naogopa hata kusema...alipomaliza kazi hiyo ya mafuta,  akachukua ule unga tena,  akafanya alichofanya, akampaka mtoto tena mwili mnzima ...halafu, akachukua na maji, akawa kama anayasomea hivi, akawa anamtupia mtoto , anayaweka kiganjani anamtupia mtoto yale maji....jamaa anahangaika mpaka jasho linamtoka

Akachukua ule unga unga, akamwekea mtoto kwenye matundu ya pua…baadae sana tumeshakata tamaa,…mtoto akapiga chafya

Mimi wakati huo, nahangaika na mama mjane, lakini tena kimoyo moyo naomba huyo mama usizindukane kwanza..hebu fikiria awali nilikuwa nafanya juhudi azindukane,..lakini kutokana na tukio la mtoto,  moyoni nikawa naombea asizindukane mpaka tujue hatima ya huyo mtoto

‘Ndio yeye kapiga chafya…?’ nikauliza sasa nikiwa nimesimama nikiwaangalia, nilimkuta jamaa naye kasimama, kaduwaa, ni kama haamini vile.

‘Khuuuuuh, hata siamini…’akasema huyu jamaa akimuangalia yule mtoto, yule mtoto sasa akawa anajinyosha, kam vile mtoto akitoka usingizini anayofanya, akafungua macho, …halafu akaanza kulia..akiita ;

‘Mama mama….’

Yaani pale nilipo, nilihisi kama…nimepata kitu gani,…nilihis kama naota, maana, kiukweli yule mtoto alikuwa kama keshakara roho, sikuamini..hapo hapo mimi kwa haraka nikamuendea mama mjane nikawa namfanyia huduma ya kwanza kwa haraka, sasa naombea azindukane haraka, ili mtoto amuone mama yake akiwa na hali nzuri, sio kama hivyo alivyolala

Nilifanya juhudi zote....lakini mama akawa hazindukani. Nilimuashiria huyu jamaa amzuie mtoto asije hapo kwa mama yake, isije ikaleta tatizo jingine tena kwa mtoto, jamaa akanielewa. Akawa sasa anambembeleza mtoto kiaina, ili atulie.

Nilijaribu tena na tena kutoa huduma kwa huyo mama, nikamuomba mungu, nikafanya kila kilichowezekana, lakini mama akawa ..hatikisiki, hakuna dalili ya mapigo ya moto,…mtihani mwingine!

****************

Jamaa alipoona shemeji yake hazindukana akasema;

‘Mungu wangu kama ....ni ule sroke, imatokea tena, ya kumvunja mwili huyo mama, hilo sasa ni janga, naye tuliambiwa, na madocta wake, isije kutokea tena, ikitokea tena,..si unalewa mwenyewe, hayo sasa ni mambo ya kisasa, wala sio ya mizumu..'jamaa akasema


'Kwahiyo..?' nikawa kama nauliza

'Kwani..umemfanya nini..wewe si umesema unajua huduma ya kwanza, au...?' jamaa akauliza

'Nimeshamfanyia lakini bado hazindukani....'nikasema

'Mhh..ndio yale yale..mimi sijui kama nitaweza tena..niliangaika naye mwaka mnzima, watu wakakimbia, nikahangaika mimi mwenyewe...usione wanadamu, wanakuona mwema ukiwa an kitu, subiria uumwe, subiria uishiwe...'akasema


'Usiongee sana, fanya unaloweza ...muda..polis wanakuja...'nikasema


'Wewe na polis wako bwana...'akasema sasa akiondoka kwa mtoto na kusogea pale tulipo, akasema

'Anatakiwa apate hewa, hapa hakuna ujanja, ..hatufanyi makusudi...mfunue hivi, ili hewa ipite, kwenye mapafu...'akasema huku akijaribu kuondoa nguo ili hewa ipite kifuani kwa huyo mama.

'Hizi ni dalili zile zile...sasa kama itatokea vile itakuwaje, maana sio kazi ndogo ...?' akauliza

‘Nikuulize wewe labda haya mumeyafanya kwa mama pia, ilikuwa kwa mtoto, sasa mumeelekeza silaha zenu kwa mama, kwasababu ni mbishi au sio..mumevizia akiwa keshadoofika kiimani, au sio…nawafahamu njama zenu nyie watu, ..’nikajikuta nasema hivyo, sikuwa na uhakika na hicho ninachokisema, kilinitoka tu.

‘Mtoto sasa hivi yupo safi..ooh, nashukuru sana mungu, … sijawahi, sijawahi kuogopa hivi..….ila sijui kama itachukua muda, sijui, kama itafanya kazi….maana hii ni mara ya ngapi sijui, na hii dawa sikuambiwa niitumie kwa mama yake ngoja tujaribu tu, …’akasema

‘Mimi hayo sijui hayo unayajua wewe…ngoja polisi afike utawaelezea wewe mwenyewe ni kwanini ipo hivyo, si unajua walivyo, na huo hapo ni ushahidi tosha, umeharibu ushahidi kwa mtoto, bado kwa mama sasa….na yule jamaa  mpelelezi, unamafahamu sana alivyo…’nikasema

‘Mpelelezi, ..hahaha, wa nini sasa, wewe jamaa bwana,..hivi hujanielewa, kwanini huniamini, mimi nafanya kujaribu tu, sina ujuzu wowote wa haya mambo…lakini tumuombe mungu nijaribu huenda ikasaidia,  lakini lolote baya likitokea tusije kulaumiana…’jamaa akasema

‘Aaah, mimi sijui lolote, ni wewe…kwa upande wangu nimeshalifikisha kwa wenyewe, wakija wao watajua..mtajuana wewe na wao..’nikasema jamaa sasa akafika kwa shemeji yake, kwanza akasita, akavuta nguo, na kuacha kifua wazi.

‘Mungu nisamehe tu…..geuka huko, usiangalia..’jamaa akasema

‘Aaah, wewe endelea tu, ..najua unajau ni nini unakifanya,…’nikasema

‘Mungu nisaidie…’jamaa akasema akawa anawewesa maneno haya hayaeleweki akawa anampaak shemeji yake hiyo dawa, kifuani, akaenda miguuni, akarudi kichwani, ….mama kimia, hakuna hata dalili ya kuzindukana.

Mara tukasikia mlango ukigongwa….mimi nikasema;

‘Polisi hao….’ Kauli yangu ilimfanya jamaa aka chini, ile ya mtu umekamaa mkao kama umechuchumaa, …na itokee jambo udondoke kwa nyuma, lakini uwahi kukaa, ndivyo jamaa ilivyomtokea…,

WAZO LA LEO: Matukio mengine hutokea ili kukuonyesha njia fulani, na ni wakati huo unatakiwa uwe na akili ya kutafakari kuhusu hili tukio au jambo hilo.., laweza kuwa ni baya, lenye mtihani ndani yake,..usikate tamaa, maana ubaya huo unaweza kuwa  ni ishara ya kukuonya, au kukusaidia kuepukana na jambo hilo au mengine yaliyopo mbele yako, kwahiyo uchukue tahadhari huku ukimuomba mola wako akuonyeshe njia sahihi…

Lakini pia laweza kuwa ni jambo jema, lenye heri na mafanikio kwako, hapo usilemae,..fanya jitahada ulifanikishe kwa malengo yaliyo mema, na wala usiingiwe na kiburi, ukajiona wewe umeweza kwa majaliwa yako.


 MSHUKURU MOLA WAKO KWA KILA JAMBO
Ni mimi: emu-three

No comments :