Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, April 2, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-104



‘Sasa ni ajenda ya mwisho, ajenda ya kusikia kauli na maamuzi ya wanandoa ambao ndio waliotuweka hapa…

Kwa namna nyingine tunaweza kuiita ajenda hii kuwa ni ajenda ya hukumu au hitimisho ya kile tuliyochokuwa tumeitiwa,.....na hapa mimi sitaingilia sana, maana wanandoa waliosababisha hiki kikao wapo hapa, na walishapata muda wa kukaa pamoja na kulijadili tatizo lao hili kwa mapana yake.....’akasema mwenyekiti.

‘Japokuwa kwa nilivyolisikia…’hapo akageuka kumuangalia mume wa familia, ambaye alikuwa kainamisha kichwa chini, halafu akageuka kuniangalia mimi.

‘Sitaki niongee mimi,..japokuwa naona …kama bado kuna sintofahamu kwa wanandoa hawa wawili..wengine kama docta na mwenzake wameshamalizana..

Sasa kwa vile tupo kwenye kikao cha wengi, na penye wengi hapaharibiki neno, natumai tutalimaliza hili swala kwa amani na upendo, ikishindikana mimi mwenyekiti nipo, itanibidi nitumie rungu langu la uenyekiti...’ hapo akatabasamu akimuangalia mke wake.

‘Sio shida…kulimaliza hili tatizo,sio shida kabisa.lakini kwanini tulazimishane, ..hapana, hili ni swala la wawili , waliopendana wenyewe, na kama ni kulimaliza tatizo lao walimalize kwa amani…au sio...

Tuendelee na sehemu ya kwanza ya hitimisho la kisa hiki...........

**********

 ‘Kama mnakumbuka kikao kilichopita ilibidi tuendeshe jambo hili la kifamilia kama kesi ili tuone haki inatendeka, kwa vile mlalamikiwa hakukubali wala kukiri kosa lake, kwahiyo tukaona ni vyema tukaliangalia hili jambo kwa undani zaidi…

Ilibidi tuliendesha kama kesi…kwa kutoa ushahidi, na maelezo yenye ushahid ndani yake,.. hadi pale ukweli mnzima ulipobainika,..ukweli huo ulikuja kufichua mambo mengine kabisa..lakini chanzo, ..ni familia husika,…sasa sijui ni kwa bahati mbaya, au ilikusudiwa, yote hayo tuliyaona wenyewe.

Hayo mambo yaliyotokea, ambayo kwa ushahid, yalipangwa, nisinelipenda kuyarajea hayo mambo, kila mtu kayasikia na kujionea..sasa leo kiko chetu kinaendelea,.

‘Sasa basi mimi kama mwenyekiti, inabidi nilisimamie hili kwa hekima zote ili mwisho wa siku tukimalize hiki kikao kwa kushikana mikono ..’ hapo akamuangalia mume wa familia ambaye bado alikuwa kainamisha kichwa chini.

‘Mimi bado natoa angalizo, kuwa hii ni familia yenye maadili yake, kama kuna mtu anaona kuwa hataweza kuishi nasi, kwa kufuata sheria zetu za kifamilia, basi awe huru kuondoka, hata kama ni mtoto wangu wa kumzaa,...ni vyema tukafynza kutii amri na sheria kuanzia kwenye familia, na hili liwe wazi kwa kila mtu,...

Hata hivyo, taratibu za familia ndogo, yaani za mke na mume zitaendelea kutumika,..hatuwezi kuziingilia, labda wao wenyewe wasema kuwa basi, hizo sheria kwa vile zimeleta mgongano, hatutazifuata tena, na kwa minajil hiyo kwa vile waliusajili huo mkataba, itabidi wafuate taratibu zao.

Haya yote tunawaachia wao,..leo ukumbi ni wao, wawili, sisi kama familia kuu hatustahili kuwaingilia,..hitimisho hili ni lao, kama kuna kusameheana, ni heri sana kwetu, kama kuna kuwajibishana, hewala....

Naombeni muda wenu kidogo, nataka kuteta na mawakili…kabla hatujaendelea…na mawakili wakasogea pale alipokuwa mwenyekiti wakawa wanaongea, ilitakiwa iwe maongezi kidogo, lakini ikachukua muda..naona wakili wa mume wa familia alikuwa akipinga jambo..

Lakini baadae wakakubaliana, na mwenyekiti akasema;

‘Unajua kama nilivyosema hapa kila kitu kimekamilika, pamoja na hayo yaliyoamuliwa huko mahakamani,lakini sis bado tuna maamuzi yetu, au sio, ndio maana pamoja na hukumu, bado sisi tuliambiwa turejee tukae kama familia kulimaliza hili tatizo letu…

‘Sasa basi wazee walisema, yaliyopita ni ndwele tugange yajayo, au sio jamani…’akasema mwenyekiti na wajumba wakasema

‘Sawa…’suti hafifu lakini.

‘Hayo yaliyotokea yawe ni fundisho kwetu, na tuape kuwa hatutarudia tena,tusameheane na kukiri kuwa tulikosea, na hatutareeja ujinga huo tena, kwani tumeshafinywa, mtu mzima ukifinywa, huona aibu,… eti jamani…leo iwe siku ya kusameheana na iwe hitimisho na ukurasa mpya uanze..’akasema mwenyekiti huku akimwangalia mume wa familia.

‘Hebu mwangalia mume wa familia alivyochongeka, ....ni taabu tupu, kwanini tufanye haya, tukijua kuwa ni makosa, tunamkomoa nani, ...baba, sasa ni wakati wako wa kurudisha mwili wako, ukae utulie ujipange vyema, muishi vyema wewe na mkeo wako na familia yenu kwa ujumla,...au sio, lakini sasa…’akasema na kutulia

‘Uamuzi wote upo mikononi mwa mke wako….’hapo akamgeukia mke wa familia.

Na mume wa familia akainua kichwa kidogo, hakusema neno

‘Kama ulivyoona hata mahakamani walikunyoshea kidole wewe, na kukupa onyo, na ulitakiwa ufungwe, lakini wakili wetu akafanya juhudi za ziada, akirejea maadili na tabia za familia kuu, matendo yetu mema ya kifamilia yakachukuliwa kukulinda wewe, ina maana kuachiwa kwako kunatokana na kumbukumbu za matendo yetu mema, maadili yetu mema yamukusaidia, sasa mimi kama mwenyekiti nikiwa hai sitakubali uadilifu wetu uporomoke tena, ...nawaomba kama wanafamilia  tuitunze hiyo kumbukumbu,...’akasema mwenyekiti.

‘Nimeona niongee haya kabla ya mke wa familia, sijui yeye ana maamuzi gani, hatujui,…ila nina imani kuwa baada ya kipindi hicho kifupi alichoweza kukaa, na kipindi hicho kifupi ambacho mume wake alishikiliwa…yeye atakuwa ameweza kukaa na kutathimini, kama ulivyoomba yeye, na …’akatulia kidogo.

‘Natumai hutatuangisha kwa hilo..

‘Baada ya mume wako kutoka huko aliposhikiliwa, uliomba wewe na yeye make pamoja, myajadili maswala yenu..natumai mlifanya hivyo au sio, ...na kwahiyo wewe kama mdhulumiwa, unayo haki yako ya upendeleo…, na hatutapenda wanafamilia wengine waingilie kati hayo maamuzi yenu

Na maamuzi yenu yasije kuwadhulumu watu wengine, ...kama kuna mtu atadhulumiwa kwa maamuzi yao..basi kila mmoja anayo haki ya kusema,na kikao hiki ndicho halali cha kuyasikiliza hayo malalamiko ya mtu anayeona kadhulumiwa…msiogope kusema jamani, sisi hapa tupo tutaangalia haki iko wapi.

‘Mke wa familia, tunakuomba uondoe jaziba, najua umeumia sana, lakini yote ni maisha, kwenye wema, na wabaya wapo, na halikadhalika kwenye wabaya na wema hawakosekani, na mitihani hii inakuwa ngazi ya kutuvusha daraja fulani,…kwa wenye hekima watalielewa hilo, au sio…

 Uliona pale mahakamani walisema nini…hawakutaka kuamua moja kwa moja japokuwa haki ilikuwa yako..mkataba wenu ulishahukumu..lakini bado wakasema tuwe na muda wa kutafakari, tuwe na muda wa kukaa kikao cha kifamilia,…sasa wewe, unayo haki, ya kuamua upendavyo..kwa vile wewe ndiye uliyedhulumiwa, na mkaaba wenu unakulinda kwa hilo..

‘Tunatarajia wewe utatoa maamuzi yako yenye hekima na busara,…haki ni yako, una haki ya kutumia mkataba wenu, au kutumia kauli yako mwenyewe, sisi kama wazazi tumeliongelea hilo, tukaona kwanini misisameheane mkayasahau yaliyopita na kuganga yajayo...’akasema mwenyekiti.

‘Nakumbuka kikao kilichopita tulimpa nafasi mlalamikiwa ajitetee, na kuelezea hisia zake, leo hatuna nafasi naye tena, leo ni siku ya mke wa familia kuongea yake na pia kutoa maamuzi yake, kwani imeonekana kweli kuwa mume wa familia ana makosa na mke wa familia ulitendewa isivyo haki, kwahiyo kwa upendeleo wewe mke wa familia una pewa  nafasi mbili, ya kwanza ni kumsamehe mume wako....

‘Upo tayari kumsamehe mume wako…?’ akasema mwenyekiti kama ananiuliza, na mimi sikujibu kitu nikawa kimia tu, maana hakuna aliyejua nina nini moyoni mwangu,…

‘Usinijibu kwa sasa utajibu muda wako ukifika…’akasema mwenyekiti

‘Ila napenda niseme hivi….kusameheana ni wajibu wa kila mwanadamu, ni daraka kubwa ya ucha mungu…ukikosa na kukosewa hatuna budi kusameheana, ni vyema tujifunze hilo...’akatulia

‘Lakini yote ni maamuzi yako wewe mke wa familia,…kama utakubaliana nalo, basi sisi kama wanafamilia, tutawashikanisha mikono, na tutamaliza haya mambo kwa amani na salama hilo ndilo kama wazee wenu tunalihitajia na kulitarajia kutoka kwako wewe mke wa familia, ila sio kwamba tunakulazimisha ufanye hivyo maana una nafasi nyingine ya pili...’akasema mwenyekiti.

‘Nafasi yako ya pili, ambayo mimi kama mwenyekiti, sitaipendekeza sana, japokuwa nyie mlikubaliana kwenye makataba wenu iwe hivyo, ...kuwa atakayekiuka mambo fulani,…mambo mabaya yenye kuleta kashfa… ambayo wenzenu waliamua kuyatumia kisiasa, na hata kidini hayakubaliki,..na kwene famila kuu  tumeyaanisha kama matendo yenye kuleta kashifa

‘Mhh…basi moja kwa moja ndoa inakuwa haipo…swali likaja je ni nani mwenye kuvunja ndoa…ni yoyote mke au mume…haya ni maswali manzito sana, na mume wa familia kasimamia hapo kuwa yeye ndiye ana haki yakuvunja ndoa…

Sasa mkataba wenu ulikuwa na maana gani,…mlikubaliana mbele ya wakili waliotambulikana, au sio na mola wenu ni shahidi…au sio…kwahiyo yakitendeka ya kuvunja ndoa, ndooa hapo inakuwaje…

‘Lakini hapo hapo tunaweza kurejea nafsi ya kwanza ya kusameheana,…kama mkoswaji, aliyekosewa, akaamua kusamehe..basi,…mambo yataendelea, na ndivyo tunavyotegemea hapa kwenye kikao hiki.

‘Tukumbuke jambo moja, sisi wanadamu wote ni wakosaji…hakuna mkamilifu, utamlaumu mwenzako kwa kosa hili kumbe na wewe una makosa mengne makubwa zaidi ya hayo unayomlaumu mwenzako au sio..kuna makosa mengi, sisi kama wanadamu tunayafanya kwa siri, sijui,…mimi sijui…mke wangu ananiamini sana kuwa sifanyi hivyo..hahaha....’akatulia mwenyekiti na kumwangalia mke wa familia.

‘Unapoteza muda bwana…’mke wa mwenyekiti akasema;

‘Sawa sawa, msaidizi wangu lakini ni wajibu wangu kuyaongea haya kama mzazi….maana hitimishi hili lisije kuwa ni mgogogo mwingine baadae…

Haya basi,..mimi naona nisipoteze muda, mke wa familia uwanja ni wako, ...’mwenyekiti akamwangalia mke wa familia.

************

Hapo mimi kama mke wa familia, kwanza nikasimama,…nikainamisha kichwa kidogo kutoa heshima kwa mwenyekiti..halafu nikageuka kumuangalia mume wangu..huku nikitafakari maneno ya mwenyekiti kuwa nina nafasi mbili, ya kwanza ni kusamehe, lakini ya pili ni kutumia mkataba wetu.

Kusamehe..yaha, yawezekana, moyoni sina kinyongi tena…lakini mkataba ulikuwa na maana gani…nifanyeje sasa…nikamuomba mola wangu anipe kauli yenye hekima na kulimaliza tatizo hili kabisa…

‘Naomba niongee nikiwa nimekaaa, ...mwenyekiti naomba kibali chako....’nikasema na mwenyekiti akatabasamu na kusema;

‘Nyie vijana bwana, mbona mnachoka mapema, haya wewe kaa tu, hata ukitaka lala, maana sote sasa hivi masikio na macho yetu ni kwako wewe….. sema yale yaliyo moyoni mwako, uwanja ni wako....’akasema mwenyekiti.

‘Nilitaka nisimame, lakini kama wenzangu walivyofanya kwa leo, nitaongea nikiwa hapa hapa, mtanisamehe kidogo, nipo kwenye wakati mgumu sana, namuomba mola wangu aniongoze tu..…’nikasema

‘Kwanza nimshukuru mwenyekiti kwa kunipa nafasi hii, ambayo, imekuwa kama vile mtu yupo kwenye chumba cha mtihani baada ya maandalizi ya muda mrefu. Ni kweli nimekuwa nikijianda kwa siku kadhaa nyuma hasa baada ya kikao kilichopita, ..ulikuwa ni wakati mgumu sana kwangu. Kama mke na kama mama wa watoto wawili….

‘Ni wakati mgumu maana kuna mambo mengi yalikuwa yakiendelea kichwani mwangu,..nikiwa sijui ya kesho yangu itakuwaje,

Je niamua nini, je hayo maamuzi yatakuwaje..

‘Haaah, …na leo ndio natakiwa kusema kile nilichokuwa nimejiandaa nacho, kiukweli hadi tunafika hapa bado mimi sijaweza kuwa na maamuzi ambayo ninaweza kusema ni sahihi kwangu…ndio ukweli wenyewe, utasemaje sasa, wakati …huna msaidizi..

Nilimuomba mungu wangu sana, na …akilini nikawa nawaza, ni kwanini najisumbua akili yangu wakati maamuzi tayari yalishajionyesha,…nilipoliwaza hilo, nikapumua, ni kweli mola ni wetu sote na kila kwenye shida, kila kwenye shinikizo la mawazo, mtegemee yeye, atakuongoza tu…

‘Nasema hilo kiukweli…maana maamuzi sio lazima mtu ayaongee, vitendo vitasadikisha hilo…ila kama alivyosema mwenyekiti, tunaomba sote mungu atupe hekima ili jambo hili liishe kwa amani na upendo, na mimi namuomba iwe hivyo....’nikageuka kumwangalia mume wa familia.

‘Pamoja na yote hayo, mume wa familia alipotoka rumande, huko alipokuwa ameshikiwa na polisi yeye na wenzake, maana imempita muda kidogo…, nilijaribu kukaa naye ili nione jinsi gani tutasaidiana kulitatua hili,...

‘Hili jambo, ni jambo gumu sana kuliamua peke yako, unaweza ukalitatua kwa jaziba, kwa hasira, mwisho wake ukaja kutulia ukaja kujijutia, na ni rahisi kuliongea kwa maneno ya haraka, lakini madhara yake ni makubwa, maana hili tatizo halinigusi mimi tu, linagusa kizazi changu ....ndio maana nimekuwa nikiliwazia sana.

‘Tulipoweka makubaliano, yetu, kila mmoja aliyapokea makubaliano yale ambayo yakaja kuwa mkataba wetu wa familia, …tuliyaweka kwa furaha tu.., na mimi sikutarajia kuwa mwenzangu angelikuja  kuyafanya hayo aliyoyafanya,sikuamini..ndio maana wengine waliniona mimi kama mjinga….yanaonekana wazi machafu, lakini mimi nikawa nimeyafumbia macho…sikuamini…hamjui tu siku tunawekeana hayo makubaliano yetu ilikuwaje,

‘Kiukweli kwangu ilichukua muda sana kulikubali kichwani, inafikia hatua unaona kama unaishi na watu wawili tofauti, na kwa ujumla nimekwazika sana sana..sio siri, sijui nitakuja kumuamini nani katika dunia hii..

‘Wazazi wangu lazima niwaamini, nazungumzia, mume….’nikatulia

‘Kiukweli sikujua kuwa unaweza ukaishi na mtu, mkachangiana naye kila kitu, ukampa moyo wako wote, kumbe mwenzako hayupo nawe kabisa, kumbe mwenzako anaye anayempenda kwa dhati…, wewe upo kwa ajili ya kutumika tu...ni dhuluma ya hali ya juu…’nikatulia huku nikionyesha uso wa huzuni.

‘Nimejaribu kuongea na mwenzangu ili nione vipi tutasaidiana kwa hili, kama binadamu, sikutaka kuwe na unyonge, kuwa kwa vile mimi nina hali hii au ile, ...kwahiyo nilimtaka ajitoe, aseme anataka nini, atoe ukweli wake ulio moyoni mwake...lakini haikuwa kazi rahisi...’nikainama kama nasoma kwenye karatasi.

‘Haikuwa kazi rahisi ndio maana nasema kwanini niumize kichwa wakati …ukweli upo wazi…’ nikatulia.

‘Kwa ujumla kama mlivyoona, nia na malengo ya mwenzangu na mwenzake, ilikuwa ni kupata maisha mazuri..hiy ndio ilikuwa ndoto yao…wenyewe wamelibainisha hilo, kwa kauli yam dada, japokuwa mume wa familia, kwa nafasi yake hakutaka kuliweka hilo bayana…kiukweli hawakuoa au kuolewa kwa mapenzi ya dhati ...’nikatulia

‘Kwahiyo wakatumia hadaa, wakajipatia mume na mke, ambao wana kile walichokitaka…, lakini nafsini mwao bado kulikuwa na mapenzi ya mwenza wao, kama walivyoita wao, mpenzi wa asili. …unakuwa kama umelala na gogo au sio..

‘Nimeshasikia wengi wakisema waume au wake, wanaweza wakawa hivyo katika mapito ya maisha,..moyoni wanaoa tu , lakini wanakuwa na wapenzi wao wa asili, lakini siku zinavyokwenda, wanakuja kuyasahau hayo ya zamani, ya mapenzi yao ya asili…na wangi wamefanikiwa hivyo na maisha yamesonga mbele…, hilo lawezekana au sio…nikajiuliza kwanini sisi hilo lisifanikiwe...unaona eeh..’nikatulia

Sasa nilitarajia kwa mwenzangu kuwa huenda itakuwa hivyo,…ndio maana baada ya yeye kutoka huko rumande,  nilipoongea naye akasema anahitaji nafasi ya pili,

‘Unahitajia nafasi ya pili kwa vipi…?’ nikamuuliza

‘Nahitajia kujirekebisha, …nimekosa basi, sasa unipe muda mwingine..’akasema

‘Kwani uliyofanya ulikosea,..au..?’ nikamuuliza

‘ndivyo ilivyoonekana, au sio..basi kwa vile ndio hivyo, nimeshajifunza, na mimi nipo tayari kuishi kama mume mwema. ..’ akaniambia hivyo.

‘Una uhakika na hilo…?’ nikamuuliza, kiukweli bado nilikuwa sina uhakika na hilo, japokuwa wazazi wangu wamenithibitishia hivyo, kuwa kwa mwanaume ikishatokea hivyo, basi hujifunza na hataweza kurudia makosa tena, ..mmh, ukishaumwa na nyoka kila ukiguswa na unyasi utashituka, huo ndio ukweli halisi kutoka moyoni...’nikageuka kumwangalia mume wa familia.

‘Mimi tukizidi kuongea nikamtolea mfano wa mpenzi wake wa asili ambaye kakiri makosa na kawa tayari kuchukua maamuazi magumu,...namsifu sana huyo mdada, ni mdada wa pekee sana…yeye  amekomaa kiutu uzima, hongera zake na namuombea mola afanikiwa katika maisha yake..

 Mimi nikamuuliza mwenzangu,

‘Unaona mwenzako alivyofanya, kaithibitishia dunia kuwa yeye yupoje, na ya kuwa yeye yupo tayari kusamehe kila kitu, kwa ajili yako, je wewe una msimamo gani,…?’ nikamuuliza

‘Msimamo gani…si nimeshakuambia, haya yote yamefanyika kwa chuki tu, mimi bado nasema hivi ndoa yangu haitavunjika kwa lolote lile…’akasema

‘Sasa ndoa huvunjwa kwa kosa gani..?’ nikamuuliza

‘Kosa hata liweje, mwenye mamlaka ya kuvunja ndoa ni mwanaume…’akasema

 Unajua huyu mtu hadi hapo hakuwa amenielewa…nini lengo langu la maswali hayo yote,nilimuuliza maswali hayo kimtego kuona moyoni mwake yupoje..

Sawa anakiri kuwa kakosea, lakini kwanini aliyafanya hayo makosa, kajibu vipi…

‘Mim niliyafanya hayo kama mume wa familia, nikiwa na lengo jema la familia yangu…niliwajibika kama mume wa familia, kiukweli majibu haya yalinivunja nguvu...’

Mke wa familia akatulia halafu akawaangalia wajumbe na kuendelea kusema;

‘Hebu angalieni hilo jibu katikati ya mstari kwa hekima..kweli mtu baada ya kukosea,angelitoa kauli hiyo, kuwa aliyafanya hayo japokuwa ni makosa, lakini aliyafanya hayo kama mume wa familia, ..

Haaah.....nikaona bado kumbe mwenzangu anaona kuwa alichofanya ni sahihi,na kwahiyo hali hiyo huenda inaweza ikatokea tena....’kama mume wa familia..si ndio hivyo maana yake…au nimuulize tena hapa mbele yenu asema ni kwanini aliyafanya hayo makosa..’nikasema

‘Hapana..huo sio muda wake tena, huu ni muda wako wa kutoa maamuzi..’akasema mwenyekiti.

Najua na siwezi kumuuliza hayo maswali mbele yenu tena,maana majibu yake yameshapigiwa mstari…..mwenye akili anaweza kuyatathimini, hata kwa akili ndogo tu…

Kiukweli mkiishi sana, ndani ya ndoa, mnajenga udugu, ni zaidi ya udugu, mnakuwa kitu kimoja, na swala la kuachana ni gumu sana, hata kama itakuwa ni kwa jaziba…sio rahisi kuchukua hatua hiyo…

Na mimi nimeliwazia sana hilo…unajua unapokosewa nijuavyo mimi, yule mkosaji ndiye anatakiwa kufanya juhudi za kulimalizia hilo tatizo,…ni hekima au sio…sasa nyie kama wajumbe mngelipenda kuniuliza swali kama hilo moyoni, je mume wangu tokea muda huo aliwahi kuifanya hiyo juhudi…

‘Huyu hapa muulizeni.’nikasema na hapo mume wa familia akataka kuongea lakini mimi sikumpatia nafasi, nikaendelea kuongea…

Tutaendelea na sehemu hii ...kidogo tu, ili siku isiidhe bure, tutakuja kwenye hitimisho la isa chetu mola akipenda.

WAZO LA LEO: Maamuzi ya hekimakwenye matatizo, huhitajia muda, huhitajia msaada wa yule aliyetuumba, sio kwa akili tu ya kibinadamu. Wengi wetu hukimbilia kutoa maamuzi yao, kwa jaziba,…au kuwa ‘usomi’ walio nao…lakini baadae wanakuja kukiri kuwa walifanya makosa.

 Subira ni muhimu sana kwenye matatizo,…


Ni mimi: emu-three

No comments :