Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, March 14, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-94


Niliwasiliana na mdogo wa mume wa familia;

‘Vipi umepewa ujumbe wowote na kaka yako..?’ nikamuuliza, nikasikia kama mngurumo wa gari kuonyesha kuwa yupo kwenye gari

‘Kaka ameshanipa ufunguo tayari, na hapa ndio nipo njiani, kwenda kuuchukua huo mzigo, …  lakini kwanini mnafanya hivyo, hamuoni kuwa ni hatari, je shemeji akigundua…mimi naogopa sana haya mambo yenu…’akasema akionyesha kuwa na wasiwasi.

‘Usijali, ni mambo ya kawaida, hayo ni kwa ajili ya kaka yako, sasa hivi hali ilivyo ni lazima tufane jambo, vinginevyo, ..sasa, unasikia, fanya hivyo, ukiwa tayari niambie, unasikia, sikiliza kwanza….’nikamuelekeza jinsi ya kufanya.

‘Sawa nimekuelewa…’akasema

 Kilichokuwa kimefanyika ni namna ya kuhakikisha kuwa mke wa familia hayupo nyumbani, na acheleweshwe kinamna  ili kila jambo likamilike kwa wakati, kwani mke wa familia hakuwa anafahamu ni nini kinachoendelea. Kazi hiyo ilibakia mikononi mwa mume wake,…

 Je ilifanyikaje…nahisi nyote mtapenda kusikia sehemu hiyo,…ukumbuke haya yanafanyika muda ambao mke wa familia anatarajia kurudi nyumbani.

*********

Mume wa familia  aliigiza kuzidiwa…si nilishaambia huyu mtu kuna hali ilitakiwa aigize kuumwa zaidi ya anavyoumwa, hapa sasa uone ushahidi.

‘Docta najisikia vibaya sana..sizani kama nitapona…’mgonjwa huyo

‘Utapona tu usiwe na wasiwasi ni dawa hizo…unasikia, wewe lala na tulia..’docta akasema.

‘Hapana docta, oh… kwa hii hali naomba umuite tu mke wangu, nataka kuongea naye, nahisi kukata roho…aaah.’akasema huku akigugumia maumivu.

Kutokana na matatizo yake hayo, mara nyingi kila anachohitajia inabidi apewe ili asiwe na msongo wa mawazo, kwahiyo docta kwa haraka akachukua simu. Kiukweli hapa docta hakufanya kutokana na maagizo, hapa alifanya kazi yake.

‘Halloh, mimi ni docta hapa, tafadhali nakuomba ufike hospitalini haraka iwezekanavyo,…’docta akasema

‘Kuna nini, mgonjwa kazidiwa…?’ akauliza

‘Hali kidogo imebadilika, …anataka kuongea na wewe, ni muhimu uje, maana imekuwa ni kero,..’akasema docta

‘Kero kwa vipi docta..?’ akauliza

‘Anataka kuongea na wewe, unajua kutokana na hiyo hali na dawa anazotumia,anakuwa kama mtu anayeweweseka-weweseka ,..ni kawaida, hata hivyo, kila anachohitajia kwa hivi sasa,  inabidi tu tumpatie, ili asiwe na msongo wa mawazo…..’akasema docta.

‘Lakini yupo vipi…?’ akauliza mke wa huyo mgonjwa.

‘Anahis maumivu…na ni kawaida, lakini ni muhim uje…’akasema docta.

‘Sawa nakuja docta, …nipo njiani, nilikuwa naelekea nyumbani, nakuja sasa hivi…’akasema mke wa familia.

Wakati hayo yanaendelea huku nyumbani mdogo wa mume wa familia alikuwa anafanya kazi aliyoagizwa, ….

Zoezi likakamilika!

 Kitu kingine muelewe, huyu docta naye alishawekwa sawa na Makabrasha, kwahiyo naye kila anachoambiwa anakubali, ila kwa siki huyo docta alijua kabisa mgonjwa kazidiwa....Makabrsha alikuwa sio mchezo.

 Silaha ikaletwa  sasa kazi jinsi gani ya kuingiza humo kwenye jengo...ukumbuek jengo hilo linalindwa na mitambo ambayo ikihisi kitu kama silaha itapiga ukelele..kuashiria jambo..

Nilishamuelekeza mdogo mtu ni nini cha kufanya, anachotakiwa ni kuifunga ile silaha kwenye kamba ambayo niliining’iniza kutoka rosheni ya pili,…na taa za upande ule nilizima.

Kwahiyo mimi nilishajiandaa kwa hili, nilikuwa na kamba ndefu, inayofika chini, ujue lile jengo lina rosheni,lakini kwa ajili ya kuiingiza hiyo silaha ndani, nilitumia rosheni ya pili,…

Baada ya ile silaha kufungwa kwenye hiyo kamba, nikaivua hadi juu,…sasa jinsi ya kuifikisha kwenye chumba changu, nilitumia njia zangu nyingine, sio muhimu kuelezea hapa, cha muhimu ilikuwa kuhakikisha kuwa mitambo ya kutizama matukio na kengele ya hatari ilikuwa imezimwa, umeona hapo.

Nilifanya hilo, na kitu kingine muhimu, kuna huyu mtoto wa marehemu, mtoto wa kufikia, huyu ni Makabrasha wa pili, yeye pamoja na kazi yake ya uwakili, lakini pia alikuwa mtaalamu wa mitambo hiyo,…ndio yeye alikuwa akiisimamia, yeye anafahamu kila kitu cha baba yake.

 Siku hiyo nlifanya uchunguzi wangu nikagundua kuwa mtoto huyo wa Makabrasha hayupo kwenye jengo maana mara nyingi yeye hufika usiku. Na alikuwa na kikao chake sehemu nyingine…lakini atafika hapo, sijui muda gani. Huyu ndiye niliyekuwa namuogopa hata kuliko baba yake!

Nikaichukua ile silaha na kuificha chumbani kwangu, kwani haikutakiwa kuwa mbali na mimi ili nikiihitaji nisipate taabu, nilihakikisha kuwa hayo yote niliyafanya kwa ujanja wa hali ya juu, mitambo imezimwa, na hakuna mtu aliyeniona nikiyafany hayo yote..…si unajua tena mimi ni nani.

  Baada ya kukamilisha hayo, nikarudi kwenye hicho chumba, hicho chumba kinafungwa muda wote, hakuna anayeruhusiwa kuingia zaidi ya Makabrsha mwenyewe au mtoto wake,..au kama kuna tatizo ni fundi wao maalumu.

Nilipoona kila kitu kimezimwa, nikarudi haraka ofisini kwangu, nikijifanya sasa kuhangaika kwanin mitambo na umeme umezima,…pamoja na hayo sikujua jinsi gani ya kufuta matukio kwenye mtandao, maana ni lazima pale ilipoishia itanionyesha mimi nikiingia kwenye hicho chumba.

 Sasa nikiwa kwenye ofisi yangu, najifanya kuhangaika na simu kumpigia fundi, ili aje awashe umeme, nikijifanya sijui wapi umeme ulipozimwa,..basi akiwasha niende kule kwenye mitambo niwashe, haya yalitakwia yafanyike kabla mtoto wa Makabrsha hajafika…

Nipo nampigia fundi,….mara mlango wangu ukagongwa, nikajua ni Makabrasha mwenyewe, huyu ningejua jinsi gani ya kumdanganya,…nikasogea kufungua,..mbele yangu nikakutana na yule mtu ambaye, sikutaka kukutana naye siku hiyo….

Mungu wangu huyu kaja saa ngapi!...

************

‘Mbona sipati ishara ya mawasiliano kutoka hapa, ni nani kazima mitambo ya usalama wa jengo, na kwanini umeme umezimika, kuna tatizo gani.. ?’ akaniuliza akionyesha wasiwasi

‘Mitambo ya usalama wa jengo, ipo wapi hiyo...aah, mimi sijui mambo yenu na wala sijui kama imezimwa, na kwanini izimwe!?...’ nikamuuliza kwa mshangao.

‘Na..na.umeme ndio umezimika nahis kulikuwa na shoti…mimi sijui ndio maana nampigia fundi…’

Na yeye hapo akaniangalia kwa mashaka, halafu  akageuka..

‘Huyu mtu anakwenda huko kwenye mitambo..hapo nikajua nitaumbuka.

Basi kwa haraka na mimi nikaelekea huko, kwenye chumba cha mitambo hiyo…nilimfikia lakini hakugeuka na hakujua mimi nipo nyuma yake, namfuatilia kwa nyuma kiujanja….Naona, mawazo yake yalikuwa kwenye hilo jambo analilifuatilia.

Akafika na kufungua mlango, akaingia ndani, na mimi kwa haraka nikaingia, chumba kilikuwa giza, ila kwa mngurumo wa hiyo mitambo, …sijui kwanini iliendelea kunguruma wakati mimi nilishazima..na umeme umezima…na kulikuwa baridi sana....hakugeuka nyuma, akawasha sehemu ambayo mimi nilizima.

‘Unaona kuna mtu alizima hii mitambo,..atakuwa ni nani huyu…nani mwingine anayeweza kuingia humu…kama sio huyu mwanamke, na kwanini aizime..huyu mtu nina mashaka naye…’akawa anaongea peke yake.

 Halafu akaenda kwenye meza yenye komputa na sehemu ya kuangalia kinachoendelea kwenye jengo,,…akakaa, ni baada ya kuwasha, sasa akatoa laptop, hiyo ipo ndani ya meza, inafungiwa, akaiwasha na kuanza kukagua kitu, akawa anaangalia ni nani aliyekaribia hicho chumba,  ni wazi kuwa ningelionekana mimi, sikuwa nafahamu jinsi gani ya kufuta matukio ya nyuma yake.

‘Ssshiit….’akasema hivyo tu.

 Kiukweli jinsi alivyowasha ile lapotop, niliona, japokuwa kwa shida, niligundua herufu alizobonyeza kuwasha ile komputa, ikanasa kichwani….alipohakikisha alichokitaka akatoka kwenye kiti chake sasa…akageuka nyuma, kama kutaka kutoka nje…

Ukumbuke nipo hapo ndani na sio mbali sana na hapo alipokaa,..na kwa hali kama ile nisingeliweza kurudi nyuma na kukimbia, angelinigundua na hapo ingelileta picha mbaya, na tendo hilo lingelionekana kwenye mitambo, nikatulia tu

Alipogeuka, akaniona,,,…nilitakiwa niondoke kwa haraka, lakini ikawa sio rahisi,…alipogeuka tu, akaniona. Akashituka na kuniangalia akiwa kakunja uso, kuashiria hasira na mshangao!.

‘Oh, wewe mtu, unakuwa kama mzimu, yaani ulikuwa ukinifuatilia nyuma, huku nilishawaambia hatakiwi watu kuingia huku, niambie umefuata nini, na inaonyesha wewe ndiye uliyefika huku, ...?’akasema kwa hasira.

‘Baba yako alinituma kufanya usafi sehemu zote...kwani kuna wageni muhimu alitarajia kuwa watakuja kumtembelea...’nikasema lakini nilifahamu kabisa kuwa kama ni usafi, huwa eneo hilo sijawahi kufika kufanya usafi na, yeye akasema;

‘Hata kama ni usafi, toka lini ukaja kufanya usafi eneo hili, wakati mimi sipo, haiwezekani, na hata kama ulifanya usafi kwanini ukazima mtambo mkubwa, ?’ akaniuliza kwa mashaka.

‘Mtambo mkubwa!!! Ndio mtambo gani huo…?’ nikauliza na yeye akawa ananiangalia kwa mashaka. Hapo hakusema neno kwanza, mimi nikasema;

‘ Mimi niliona kuwa eneo hili ni chafu, ndio nikaja kulifanyia usafi, ...na sijui kama nilizima, ndio kuna wakati nadeki, nikaona nisije nikarushwa maji, nikaharibu vitu vyenu,…sijui lakini nilipozima nikaona kila kitu kimezima, tatizo nilisahau kuwasha tena, kwani kuna kitu kimeharibika..?’ nikauliza

‘Wewe mtu sikuamini..nilishamuambia mzee, lakin..haya…’akasema

‘Tatizo ...mimi mambo yenu hayo siyajui…naogopa sana umeme..’nikasema

‘Ni nani alikupa ufungua wa chumba hiki?’ akaniuliza

‘Unauliza jibu, ninapotaka kufanya usafi, nilishawahi kuja kwako kukuuliza ufunguo upo wapi, eeh…, mimi ninafahamu wapi funguo zote zilipo, kwanini unaniuliza maswali mengi, mbona siku nyingine hujawahi kuniuliza, maswali kama hayo kuna nini kwani, mbona mnanitisha…’nikasema sasa kwa hasira.

‘Wewe mwanamke mimi sio mjinga…’akasema sasa akinionyeshea kidole, hakunifahamu kuwa mimi siogopi vitisho….nilitulia nione anataka kufanya nini.

Akasimama, aliponikaribia, akataka kugeuka, na mimi nikasema

‘Nani kakuambia wewe ni mjinga, kama hayo niliyofanya ni ujinga, basi unamtusi baba yako aliyeniamrisha mimi nifanye usafi..na ni mara ngapi nafanya usafi, na kwanini huendi kumuuliza baba yako, kama una wasiwasi na mimi, mbona unaniwekea vikwazo visivyo na msingi..mzee wako ananiamini ndio maana kaniajiri niwe karibu naye.’nikamwambia.

‘Mzee hajakufahamu kuwa wewe ni nani, mimi nimeshakufahamu…wewe sio mtu mnzuri kabisa…’akasema
‘Sawa nitamuambia baba yako, amtafute mtu mwingine, ..si ndio hivyo unataka au sio…ngoja akija,..leo itakuwa mwisho wa kuniona humu ndani..’nikasema

‘Leo iwe ni mwisho wako kuingia kwenye hiki chumba, tatizo ni kuwa umezima mtambo mkubwa wa mawasiliano, na kwahiyo umetufanya tushindwe kuwasiliana na humu ndani, ni hatari..na najua hili utakuwa umelifanya kwa makusudi....’akaniambia.

‘Kwa makusidi !!! Mbona sikuelewi…ili iweje,…’nikasema

Niliona hiyo hali ikiendelea itazidi kuchelewesha mambo mengine, nikajaribu kuifanya kazi yangu nyingine, plan B,  taratibu nikatabasamu, na kusema

‘Samahani mrembo, unajua wewe ukikasirika, ndio unapendeza zaidi..’Nikasema na kujirembua, nilishafahamu udhaifu wao, mtoto kama baba, akategeka, na kunisogelea, huku akisema;

‘Tatizo lako wewe kwasababu ya tabia yako unahisi kila mtu ni kama wewe....’nikasema huku nikijerembua.

‘Mhh..hahaha eti mimi mrembo, toka lini mwanaume akawa mrembo…’akasema na mim nikawa nimeshafika karibu naye, na haraka akanyosha mikono kutaka kunikumbatia…sikuwa na muda huo…

Unajua wakati mwingine ukiwa katika kazi kama yangu inabidi utumie kila mbinu, lakini akili kichwani mwako. Na alipoliona lile jicho, mtoto kama baba, akasawajika, nikamuona mate yakimtoka, akasahahu alichokuwa akiniuliza mara akasema;

‘Kwanza nikulize  lile ombi langu vipi,..?’ akanisogelea baada ya kuzima kitu kwenye mitambi, sikujua ni kwanini, na akanisogelea kujaribu kunishika na mimi nikasogea pembeni na kusema;

‘Ombi lako lipi, eeh, hivi wewe vipi..!!!’nikasema sasa nikibadilika ghafla

‘Aaah, vipi tena…’akasema

‘Wewe mwanaume,..unajifanya upo sawa na baba yako au sio, nilishakuambia upuuzi kama huo, siutaki, msinione nipo humu ndani mkafikiria mimi ni Malaya, kwanza kuhusu huo upuuzi wako nitamuuliza baba yako...kama yupo tayari kuchangia na mtoto wake...haya,’nikasema na yeye akageuka kuondoka karibu yangu, huku akisema;

‘Hivi wewe baba unamuona mtu wa maana kwako, ombi langu kwako ni siri yangu mimi na wewe, eti ukamuulize baba, unataka nilaaniwe nini....wewe jivunge tu, ipo siku utaingia kwenye anga zangu, ..’akasema na mimi hapo nikacheka. Nikaona sasa nimeshabadili muelekeo…

‘Kumbe unajua hilo, hehehe..mtoto kama baba…yatawashinda…’nikasema

‘Wewe cheka tu, unafikiri mzee yule atakuwa na wewe milele, akikuchoka anakutupa chini, wangapi walikuwa naye sasa hawatakiwi tena,.. hata kumsogelea hawawezi, yeye anamtaka mtu akiwa na shida naye shida zikiisha basi, huyu mtu ni takataka.., ...wewe jidanganye kwake, ukifikiria umefika....’akasema.

‘Kama alivyomfanyia mama yako au sio,…?’ nikauliza hivyo, na hapo ikawa kama nimemshika sehemu mbaya, akasimama, akageuka, sura ilikuwa imebadilika, ..…

‘Tafadhali, usimtaje mama yangu hapa, unasikia tuongee mambo mengine lakini usimtaje mama yangu, tafadhali nakuomba…’akasema

‘Ukiendelea kunifuata fuata sitasita kumtaja mama yako, unasikia,…’nikasema na hapo akageuka hakuniangalia sasa,…nikaona bado, nikasema..

‘Unafikiri mimi sijui… hata hivyo  mimi sijawahi kukuambia kuwa nina haja na baba yako, ...baba yako ndiye kanilazimsiha kuja kwa ajili ya mambo yake, mimi nina mume wangu, nina maisha yangu mazuri tu, na mume wangu nampenda, kama isingelikuwa haya mambo yenu unafikiri ningelikuwa hapa, na ipo siku mtajuta kwa hayo mnayoyafanya....’nikamwambia.

‘Hayo unayafanyiwa ni yenu na baba, mimi siyajui, ...na vitisho vyako, kwangu havina nafasi, nafahamu ni nini ninachokifanya kwa nafasi gani, usinitishe kabisa, mimi ninafahamu sheria, na sijawahi kukulazimisha kwa lolote lile, na hata hivyo ombi langu lipo pale pale, usiponitimizia najua jinsi gani ya kukupata...’akaniambia

‘Hahaha utafanya nini...?’ nikamuuliza

‘Siri zako zote anazozitumia baba kwa ajili ya kukupata wewe ninazo mimi, zipo kwenye mtandao, yeye akizihitajia mpaka aingie kwenye mtandao, na mimi ndiye nimezihifadhi, sasa utanidanganay nini, nikiamua kuzitumia dhidi yako, siutaumbuka wewe...sasa uamue moja kuwa na mimi au na baba..’akasema.

‘Nakuambia hivi ni bora umenifahamisha hayo, nitamuambia baba yako kila kitu, na hizo mbinu zenu..kumbe ndio mlivyo eeeh,..na ni bora aniambie ukweli nipo hapa kuchangia mtu na mwanae..kanifanya mimi Malaya sio..keshaniita mimi ni mtumwa wake, sasa wewe wataka kunifanya mimi ni Malaya, mtaniambia....’nikamwambia.

‘Hivi wewe una akili kweli,...kila kitu utamwambia baba,..utamuambia baba, huyu baba ndio nani, eeh….ok, …tuyaache hayo, naomba yaishe, au sio, samahani basi, namba tafadhali usije kumuambia baba....’akasema

‘Sasa tuelewane, ili nisimwambia baba yako, unifundishe jinsi gani ya kutumia huo mtandao, jinsi ya kutengeneza picha na kuziweka kwenye huo mtandao..’nikamwambia.

‘Unataka nikifundishe ili uje uzifute, ..hilo umenoa..’akasema

‘Kwahiyo unataka nikamuambia baba yako au sio..’nikasema

‘Sikiliza kama unataka nikufundishe, kwanza na mimi unikubalia ombo langu, mimi nitakufundisha kila kitu unachotaka…tena tuanze leo, unasemaje…’akasema

‘Sawa…’nikasema

‘Lakini tumekubaliana, nitakufundisha lakini malipo yake ni ...maombi yangu..’akasema sasa akitabasamu, uso umeshasawajika.

‘Kwanza unifundishe, malipo si baada ya kazi…’nikasema

‘Hahaha wewe mjanja sana, sikiliza kama kweli unataka hilo, tukubaliane, mimi nipo tayari,...na safari hii sikubali, kama ulivyonidanganya siku ile… la sivyo, na mimi nitaweza kukufanyia kitu ambacho hutaweza kunisahau....’akasema

‘Kitu gani, hujui haya yote baba yako anayasikia..’nikasema

‘Hahaha, wewe hunijui eeh, mimi sio mjinga kihivyo,…nikuambie kitu,..ujue na mimi ni wakili kama baba…kila ninachokifanya najua jinsi gani ya kujilinda,…’akasema na mimi sikumjibu

Nikageuka kama kutaka kuondoka,..yeye akageuka, nahisi alitaka kukiwasha kile kitu alichokuwa kakizima….

**********

  Alipogeuka akazima kile kitu na kutembea hadi mezani kwake hakugeuka, alishajua kuwa nimeondoka…akawasha ile laptop, akawa anatizama matukio, akawa sasa anafuta baadhi ya mtukio, nahisi ni hapo tulipokuwa tunaongea naye, alipomaliza, akazima ile laptop, akairejesha sehemu yake...

 Mimi nilikuwa pale karibu na mlango, sijaondoka… na alipomaliza shughuli zake, sasa akawa anatoka, kutaka kutoka kabisa humo ndani, akaniona nipo nimesimama, nimeshikilia ufagio,..hapo hakushituka, akaniuliza..

‘Mimi nilijua umeshaondoka, sasa unasubiri nini,  kama huna kazi ya kufanya, nenda nyumba ukalale..’akasema.

‘Nishakuambia kwa maagizo ya baba yako, natakiwa kuhakikisha kila kitu kipo sawa, ninafahamu ulipoingia kuna vitu umevuruga, kazi yangu ni kuhakikisha kila kitu kipo katika mpangilio wake, ili wageni wakija kusiwe na jambo la aibu...’nikasema

‘Ishia kule, nenda kaendelee na kazi zako huko,hapa sio sehemu ya watu, hii ni sehemu ya mitambo, huku hakuna mgeni anaweza kuingia ...’akasema na kutaka kuondoka.

‘Polisi je..?’ nikauliza hivyo, akashtuka, na kugeuka kuniangalia.

‘Polisi!!’ akasema kwa mshangao.

‘Hahaha, kumbe unawaogopa eeh, sasa ujue kuwa hao watu watakuja, kama sio leo, ni kesho….’nikasema

‘Kwanini, kuna nini kibaya…?’ akauliza

‘Naondoka, kaam hutaki nifanye usafi humu, nitamuambia baba yako umenizuia…’nikasema

 Mimi nina akili za ajabu sana, ukinionyesha kitu, au nikaona unavyofanya, akili yangu hunasa haraka sana, nilishaona jisni anavyoweka neno lake la siri, nikalinasa bila ya hata ya yeye kujua.

Kwa muda ule nilijifanya mjinga kabisa nisiyefahamu kitu, hata baba yake anafahamu kuwa mambo ya mitambo, mitandao, komputa sijui kitu….kumbe !

Aliondoka hadi ofisini kwake, na huko nikamfuata nikitaka anifundishe…, nia ni kuhakikisha akili zao, zinajua mimi ni zezeta wa mitandao, na komputa, hakuogopa kunifundisha akijua kuwa mitambo ipo wazi, anaonekana kwa kila anachokifanya.

Alinifundisha kidogo jinsi ya kuwasha komputa, na kuzima, jinsi ya kufungua vitu kwenye komputa, ni vitu vya kawaida, baadae akasema niondoke kwani ana kazi zake anataka kufanya, kabla hajaondoka,…hata hivyo kwa jinsi ninavyomfahamu  alionekana kama hayupo sawa.

 Baadae akaondoka

Usiku wake, nilitaka niingie kwenye hiyo mitambo, kwani ndio siku peke yake ningeliweza kufanya jambo, nilichofanya ni kuchelewesha kununua mafuta ya genetaror, nilijua mara kwa mra umeme unakatika, na mimi ndiye niliyekuwa nahifadhi fedha za matumizi madogo madogo ya ofisi, na nilitakiwa kuhakikisha mafuta ya genetor yapo,

Nilijua ikifika saa tatu, mafuta yatakuwa yamekwisha, na siku hiyo umeme ulikuwa hakuna, huku nikiomba huyo mtoto wa huyo  jamaa akaondoke na asirudi, au anachelewa, nilishangaa kweli siku hiyo kwani mpaka saa tatu alikuwa hajafika,....mara genetaror likazima, kukawa kizaa, zaa, giza, nilijua kwa jinsi ili mitambo ilivyo ikifika nusu saa itakuwa imezima, hapo nikajichelewesha kufuatilia, hadi nusu saa ikapita, ndio nikajitokeza

‘Mbona generator limezima, hujanunua mafuta..’akaniuliza Makabrasha

‘Naona nimepitiwa mambo yamekuwa mengi, ...nimemtuma mlinzi akanunue...’nikasema

‘Huo ni uzembe, unafahamu umuhimu wa umeme kwenye hili jengo, huoni watu wabaya wanaweza kutumia mwanya huu kufanya lolote...na kwanini hata ile mitambo ya akiba inayohifadhi umeme, umezima pia..ile inaweza kuhifadhi umeme wa masaa 24..’akasema.

‘Mimi nilishakuambia mambo ya mitambo, komputa, mimi sijui…kama hamukunielekeza jinsi ya kuwasha na kuzima nitajuaje..’nikasema

Hapo akachukua simu, akaongea na mtu wake ..

Mimi hapo nikaachana naye na kukimbilia kwenye hicho chumba. Kama nilivyojua, sehemu ile ya kuangalia matukio ya jengo ilikuwa imeshazima, kwa haraka nikakimbilia kwenye ile sehemu ilipowekwa laptop, ufungua wake nilikuwa nao tayari,…nikaichukua na kuifungua, nikawasaha, nilijaribu mara moja ile namba ya siri, ikakubali…

Nikatafuta sehemu hiyo inapohifadhia matukio..ile laptop ndio yenye kila kitu, ndio Server, …kwahiyo kwa kutumia yenyewe niliweza kuongoza mitambo yote humo ndani,…muhimu kwangu ni kufuta historia ya matukio ya nyume, yale ambayo nahis sio muhimu kubakia nayo.

Ilichukua muda kidogo kupata kumbukumbu ninazozitaka, ....nilikuta kumbukumbu nyingi za watu mbali mbali, ambazo kama zingeliwekwa hewani, nafikiri watu wengi wangeliumbuka, sikutaka kuangalia zaidi, kwani mambo niliyoyaona humo yanatisha,mimi nikazifutilia mbali, na kuhakikisha hazipo kwenye sehemu ya mabaki ya vitu vilivyofutwa, nikaangalia sehemu inayoangalia matukio ya jengo hadi umeme ulipozimika, nikazifuta.

Hapo nikapumua, sehemu ya kwanza ya mpango wangu ikakamilika.

Tuendelee…

WAZO LA LEO: Binadamu sio mtu au jiwe, ukasema utalichunga lisifanye kile usichotaka, kama kiumbe huyu aliyeumbwa na mola wake, hamtii yule aliyemuumba sembuse mamlaka…!!!


Kiukweli..ni kawaida ya wanadamu kukengeuka,…sheria ziliweka kwa ajili yake kwa masilahi yake, labda na mali zake,lakini wavunjaji sheria ni hao hao wanadamu..Na kiukweli wapo wanatajirika kwa hali hiyo ya kuvunja sheria, na wengine wanakuwa masikini kwa sababu hiyo hiyo ya uvunjwaji wa sheria… KIONGOZI ndiye anayebeba dhamana ya hili. Kumbe basi, kiongozi ni mtu muhimu kwetu, basi tusifanye makosa kumchagua kiongozi asiyefaa,…!!!
Ni mimi: emu-three

No comments :