Kiukweli kipindi hicho
nilikuwa na furaha sana, furaha ya kuwa naolewa kwenda kuishi mjini na mtu
mwenye uwezo, kwa muda fulani sikufikiria sana mapenzi yangu na mwenzangu,
akili hiyo ilinitoka kidogo.
Lakini kabla ya hapo, nilikuwa nimekutana na mdada mmoja, ilikuwa
ni bahati, tu,…nataka kulielezea hili najua wengi wanajiuliza ni kwa vipi
nikawa nafanya kazi hiyo hatari ya upelelezi.
Nahisi ilikuwa imepangwa
iwe hivyo…, unajua mwenyezimungu humkadiria kila mtu na namna yake ya kutokea,
riziki imepangwa hivyo, japokuwa ni muhimu kutafuta sababu, lakini iwe na
uhalali fulani, ..siku moja alitokea kibaka, akamkwapua dada mmoja mgeni,
sijawahi kumuona huyo mdada kabla,..ulikuwa mkubwa mnzuri, na kiukweli nihisi
utakuwa na vitu vya thamani kama sio pesa.
Pamoja na maisha ya umasikini pale kijijini, mimi niliwachukia
sana wezi,…basi yule kibaka alipomkwapua huyo mdada, akaanza kukimbia,
akanipita mimi, nikaingiwa na hamasa, kwanini nisifanye jambo, kwanini watu
hawaangaiki kumkimbiza yule mwizi, hapana lazima na mimi nifanye jambo
Nikaanza kumkimbiza, sasa watu wakawa wanaangalia kwa hamasa, mimi
kama mwanake nitafanya nini…na huyo kibaka ni mwanaume, na mwanaume kweli, anavyooneka, ana nguvu,…kiukweli
kama angejizatiti, nisingeliweza kupambana naye kwa uonekano wa hivi hivi,
lakini nilijiamini.
Kwa kukimbia mimi sio mchezo,…, yule kibaka alipoona aliyekuwa
akimkimbiza nyuma yake ni mwanamke, mdada tu,…akasimama
‘We mdada unataka kuumia…’akaniambia nilimpomkaribia
‘Nipe huo mkoba wa watu, na wewe uwe salama, usitutie aibu hapa
kijijini ..’nikasema
‘Hahaha, kwanza mkoba sio wako , pili wewe ni mwanamke tu, huwezi kunifanya chochote na
tatizo lako, hujui unayepambana naye, unajileta hadi huku,..kwenye mikono ya
fisi utajuta kufanya…’akasema, sasa akiniangalia kwa macho mengine ya kutaka
kufanya baya kwangu.
Nikawa nimeshamkaribia, hakuelewa kabisa malengo yangu, yeye akawa
sasa kazarau, kasimama, ananiangalia mimi nitafanya nini kwanza, … hakuamini,
maana nilichomoka kwa kasi na kuudaka ule mkoba mkononi mwake, na kuanza
kukimbia, kuelekea mbele, na hata alipojaribu kunifuata hakuweza kunipata.
Baadae mbele nikageuza na kurudi kule kituoni na kumkuta huyo
mdada aliyeibiwa mkoba bado kashikwa na bumbuwazi, nahisi kulikuwa na vitu vya
thamani sana, nikamkabidhi mkoba wake, hakuamini, alisema
‘Oh, umewezaje wewe au…’aliishia hivyo, nikajua labda kahisi kuwa
mimi ni miongoni mwa huyo mtu.
‘Uwe makini sana maeneo haya, …kuna vibaka..’nikasema
Na mara kwa mbali nikamuona yule jamaa akija,hakuogopa kurudi tena
hakujali, nahisi maeneo ya pale wanamuogopa sana, sasa …alipofika pale akataka
kunivamia mimi, kabla hata hajaniwahi mimi, akajikuta akipambana na huyo mdada,
ilikuwa dakika mbili hivi, ..yule kibaka akawa kalala kwenye vumbi, mdomo
unatoa damu, ilibaki historia.
Mimi pale nilipo nikawa na hamasa ya ajabu, alifanyaje, aliwezaje
kumviringa na kumbamiza mwanaume yule …hadi jamaa akasalimu amri, nikawa
najaribu kufanya kama yeye,..wakati huo watu wamejaa sasa..
‘Mwizi mwizi..sasa hata wale waliokuwa na hasira na huyo mtu
wakawa wanatoa hasira zake, yule mwizi alipigwa na alikuja kuokolewa na mgambo
wa kijiji..
Kiukweli tendo lile likawa mwanzo wa kunibadili, pale pale
nilimuambia huyo mdada, wakati akiwa ananishukuru kwa kuweza kumuokolea huo
mkoba , mimi nilisema tu
‘Napenda sana niwe kama wewe..’nilitamka hivyo tu, na huyo mdada
akasema
‘Ombi lako limefika kwenyewe,..’akasema
Ni kweli kumbe huyo mdada alikuwa na ziara yake maalumu na katika
harakati zake za kikazi akawa anatamfuta mdada jasiri anayeweza kumsaidia
kwenye kazi zake na ndio ikawa mwanzo wangu wa kuanza kujuana na huyo mdada.
‘Ngoja nimalize hii kazi, lakini nitamtuma mtu aje kukupa mafunzo
maalumu, tutawasiliana..ila nataka iwe siri, unajua kutunza siri wewe..?’
akaniuliza
‘Sana…’nikasema.
Basi huyo mwalimi kweli akaja, nikawa napata mafunzo maalumu, kwa
siri..na ndani ya mafunzo hayo, kitu muhimu nilichojengewa ni usiri, asijue
yoyote hata mpenzi wangu,..kuna namna walinijenga, nikakubaliana na hilo,.
Kiukweli hutaamini, nilitii, nikafanya hivyo, nikawa nimejiandikisha
pale kijijini kwa mafunzo ye ushonaji, lakini humo humo, nakutana na huyo
mwalimu wangu, napata mafunzo, asubuhi sana ni mazoezi, na jioni, akanijenga kiakili
, ujasiri wa mwili ..na hayo yalifanyika kabla sijafika huku mjini.
Hivyo ndivyo nilivyoweza kuwa mdada mwingine, …mengine sio muhimu
kuyaelezea hapa, au sio.. turejee sasa nirejee kwenye msingi wa maelezo yangu..
Aliporudi huyo mshauri alituambiaje,…..
‘Nawabariki mkaolewe lakini ndoa zenu ziwe na lengo moja la ndoa
tu ya makaratasi, mnanielewa…lakini ndani yake tuwe na mikakati mingine
mnasikia, nataka kuwafundisha jinsi gani ya kutengeneza maisha ya
baadae..mnielewe, sina nia mbaya kabisa,nia ni kuhakikisha na nyie mnakuwa
watu, au sio…….. ‘akasema
‘Baso mimi sijakuelewa…’nikasema
‘Muhimu kwanza hilo lifanikiwe..la ndoa, mkipata ile hati ya ndoa,
mengine niachieni mimi,…baada ya hapo, baada ya ndoa, nitakuwa na vikao vya
mara kwa mara,..kwa mmoja au kwa wote wawili, nitawapatia mikakati muhimu, ila
cha kwanza mpate hizo hati za ndoa, ni muhimu sana kwangu……’akasema
Basi ndoa zikafanyika…kwa sherehe na gharama ilikuwa juu yake,
kiukweli ilitoa fora, sio kwamba tulifanya siku moja, hapana, kila mtu ilitokea
kwa jinsi ilivyopangwa, ila sisi tulishazipanga siku hiyo,
Nipo ndani ya mume wangu naambiwa kuna mgeni, kutoka na kutana na
mzee mzima, akaniambia …nina haraka, ila nataka kitu kimoja, fanya ufanyavyo,
upate hati za biashara za mumeo..
‘Nini..?’ nikauliza , maana nilishasahau
‘Umesahau eeh, fanya hivyo…’akandoka.
Sikuweza kufanya hivyo, baadae ndio akapanga tukaja kukutana kikao
akiwemo mwenzangu, kila mmoja alishajisahau, ndio akatukumbushia ile ajenda
yetu
Alituelezea mikakati mingi sana, ukumbuke kipindi hicho mimi
nilishaanza kujengekea kivingine, nilikubali tu pale …, lakini akili yangu
ilikuwa na mtizamo mwingine wa maisha..mwalimu wangu alikuwa kajaribu kila
awezavyo kunifanya binti wa kisasa, mwenye elimu nyingine, na nilishaanza
kusoma masomo ya jioni, ndani yake kuna hayo masomo.
Pamoja na hayo moyo wangu hakuwa huru , haukuwa huru kwa vile bado
nilikuwa nampenda sana mpenzi wangu wa asili, kile kitendo cha kuishi na
mwanaume mwingine ambaye moyoni hayupo, ilikuwa kazi..kwa kipindi cha wiki moja
hivi lakini nashukuru sana docta aijitahidi naye akanibadili kifikira ..yeye
alikuja kugundua kuwa mimi sipo sawa, nakuwa nipo kam sipo,..aliligundua hilo
mapema sana.
Mtu wetu hakuchoka na siku moja akatuita tena, akasema;
‘Sikilizeni kwa hivi sasa sahauni yaliyopita mnasikia, muwe na
akili za kuona mbele, ili muonekane na hili lindi la umasikini, fanyeni
ninavyotaka ..tafuteni hizo nyaraka haraka kabla sijaondoka..alisema anataka
kusafiri.
Basi mimi nikajitahidi nikapata baadhi ya nyaraka ili tu kuona
anachotaka kukifanya, na mwenzangu halikadhalika,..
‘Hizi sio muhimu sana…nitakuja kuwaambia ninazotaka..’akasema na
hapo nikaona huyu mtu hana maana, kila ukimleta hiki anasema hicho sio chenyewe,
tafuta hiki, nikaona ni ujanja ujanja wake, nikaja kumuambia kuwa mimi siwezi
tena kufanya hivyo
Kuna jambo kubwa alipenda kutushauri, tujizuie kupata watoto,ili watoto wasije kuwa
ni kikwazo, na ikiwezekana tukutane sisi wawili kisiri tupate mimba, na hizo
mimba tuwabambikie waume zetu hiyo ni moja ya mikakati yake aliyokuja
kutushauri baada ya ndoa, ambayo haikuweza kufaulu.
‘Na muhimu zaidi mpate watoto wa kiume, mkiwapata hao, mimi
nitakuwa mwalimu wao..’akasema na sikuelewa ana maana gani
Mipango yake mingi
aliyokuwa akituelekeza haikuweza kufaulu kwa vile kama mlivyoona, mwenzangu
alianza kupata watoto na mke wake, na hilo lilimuuzi sana mshauri wetu, lakini
hakukata taamaa akawa bado anatuelekeza mengine ya kufanya.. .na alisema, huyu
kaharibu, lakini hata hivyo, kapata majike, hayo hayawezi kutuzuia kwenye
mikakati yetu, muhimu nyie wawili mpate madume, na hayo madume myajenge yaje
kuwa warithi wenu.
‘Ndoto ya madume ilimgusa sana mwenzangu, sijui aliambiwa nini na
huyo mtu, na hayo yakiendelea, wao hawakujua kuwa mimi nimeshajengwa upande wa
pili, nikiwa nao, nakuwa kama wao, nikitoka kwao nakuwa mwingine, na nikiwa na
mume wangu nakuwa mke wa nyumbani, hayo niliyaweza..
‘Jingine kubwa ilikuwa, kutafiti undani wa familia tulizoolewa,
tujue jinsi gani walivyopata utajiri wao..familia za wazazi wao,..alisisitizia
sana kwa mwenzangu mimi hakuwa na mambo mengi kwangu, hayo nilikuja kugundua ni
kwanini baadae.
Asikudanganye mtu, ukishaolewa au kuoa, akili yako yote inakuwa
kwenye ndoa yako, ndoa inanoga,asikuambie mtu, hasa kama umeingia kwenye sehemu
unayopata kila kitu, ndoto, na mipango tuliyopanga ikawa kama inayeyuka, na
kila tukikutana kila mmoja anakuwa na dharura zake utaona tu, hata huyo mshauri
tukawa tunampiga chenga, na hilo zoezi likawa kama limekufa, na kila mmoja
akawa na malengo na ndoa yake.
Ni kweli moyoni bado kila mmoja alikuwa akimkumbuka mwenzake,
lakini ki hali halisi, ni nani angekubali kuachia hali aliyo nayo, akarudi
kwenye umasikini, hakuna, tulipokutana tena, akiwemo mshauri wetu,
tukalibainisha hilo wazi kuwa ile mipango ya awali isitishwe, kwani
haiwezekani. Ndani ya ndoa kuna vikwazo vingi, kwahiyo hayo tuliyoyapanga
yasiwepo tena, kila mmoja kesharizika na ndoa yake.
Kauli hizo zikamkatisha tamaa mshauri wetu akatuona sisi ni
wasaliti, akatuona sisi hatuna maana, na akaapa kuzisambaratisha ndoa zetu, na
kusema hazitadumu, maana tumeolewa au kuoa, kwa ajili ya mali tu, na sio kwa
ajili ya upendo.
‘Nyie mtaona, sizani kama ndoa zenu zitadumu, nawafahamu sana nyie
mlivyo, kunguru hafugiki...mnafikiri mimi siwajui eeh, nitawachunguza juu
chini, na ipo siku mtanikumbuka…’ikawa kiapo chake.dhidi yetu
Ndoa ya mwenzangu ilianza kuonyesha nyufa…, baada ya kuzaa watoto wale
wawili, na katika makubaliano yetu ya awali ilitakiwa mtu asizae, kwani ukizaa
watoto watakuwa vikwazo, mwenzangu yeye akazihirisha wazi kuwa yeye hayupo tena
kwenye makubaliano hayo, akavunja miiko, mimi sio kwamba sikutaka kuza nasema
ni mungu mwenyewe alinipa huo mtihani, sikuweza kushika mimba mapema.
Kiukweli mimi sikuwa hivyo sana, yaani kujali hayo ya huyo
mshauri, kama nilivyosema nimeshajengwa kinamna, kitu ambacho sikuweza
kukiacha,..ni mapenzi yangu ya moyoni, sijui kwanini, japokuw akiuwazi
nilishaona kuwa mwenzangu hayupo nami tena, lakini sio mimi, moyoni muda mwingi
nilikuwa namuwaza yeye,..hata hivyo kutokana na mafunzo yangu nikaona hakuna
jinsi… nijipange kivyangu.
Baada ya mwenzangu kupata watoto wawili, nikaona mambo yanageuka,
na mara mwenzangu akaja kunikumbushia ile mipango yetu, nikashangaa, na
kumuuliza iweje sasa, na wakati yeye ana familia yake tana ana watoto wawili
tayari, akasema, hana raha kwenye ndoa yake,..
Aliniambia hivyo,..hana-raha-tena-kwenye-ndoa- yake…yeye anaishi
tu kwa vile ni sehemu yenye utajiri, lakini ndoa yake anaiona kama jela. Ohoo
nikakumbuka ule usemi usemao, utasema hakifai, au hakitoshi kwa vile unacho,
wakati ulipokuwa huna, ulikitamani.....sasa ndio yakawa kwa mwenzangu…sasa hana
raha tena kwenye ndoa yake…
‘Sasa unataka tufanye nini?’ nikamuuliza
‘Tumtafute Makabrasha atusaidie,..’akasema
‘Hahahah, hapana, sikiliza achana kabisa na huyo mtu, huyo mtu sio
mtu mwema, atakuangamiza, na kukuacha ukiumia, nimegundua kuwa huyo mtu ana
malengo yake binafsi,...’nikamwambia,na kweli mwanzoni akanisikiliza.
Kumbe mwenzangu alishaingia kwenye mambo mengine ya ndani zaidi.,
akawa hawezi kuvumilia, akaanza kutembea na mfanyakazi wao wa ndani kwake, na
sikuamini, mfanyakazi wake wa ndani ni mtoto mdogo sana kwake, ni lile umbile
kubwa tu ndilo lilimponza, ..hayo alinificha kabisa, sikuyafahamu hadi huyo
binti alipofika huko kijijini na mimba.
Huyo binti alipofika hakuonekana nilisikia tu yupo, nikajitahidi hadi nikaonana naye, kwasababu
anatoka sehemu ambayo mtu wangu wa moyoni yupo nilitaka kufahamu ukweli
nikamuuliza kulikoni, akasema ana mimba
, mimba ya nani, awali hakukubali nilipotumia ujanja wangu akaja kuniambia
ukweli, sikuamini, ikabidi niwasiliane na mwenzangu, mwenzangu akanikatalia, kata kata…lakini
ukweli ukaja kufahamika binti alipojifungua, maana sura haijifichi.
Nikakutana na Makabrasha, na yeye akajifanya hajui, lolote, kumbe
mwenzetu alishapata upenyo wa kuingiza mambo yake..hapo hapo kwenye hilo
tatizo,.., akawa kapata nafasi ya kupata taarifa zetu za ndani, na aliyewezesha
awali kulifanikisha hilo, yaani kupata taarifa za ndani, alikuwa ni huyo binti …
Huwezi kumlaumu, maana marehemu alikuwa ni mjanja sana, jinsi gani
alivyoweza kuingia ndani ya kuwekeza vitu, ni,..kwa vile binti wa watu hakuwa
mjanja wa kuligundua hilo, kwahiyo ikawa ni rahisi kwa mtaalamu kupandikiza
vitu vyake,..na baadae binti alipopata mimba, na yaliyotendeka humo ndani akaja
kuyapata kama ushahid wake wa kumnasa bwana mzee.
Kwangu mimi ikawa ngumu, na alipoona mimi ni mgumu na mjanja
kwake, ndio akatafuta njia nyingine,kwasababu hadi hapo alishaniona kama tishio
kwake, kwani najua njama zake, na pili sitoi ushirikiano anaoutaka yeye..
Na jingine huyu Makabrasha
alinifahamu toka siku nyingi, kuwa mimi sio mtu rahis sana wa kuingilika, kama
alivyokuwa mume wa famila, na alinifahamu kuwa mimi ni mpinzani wake, kwahiyo
akaona aniweke kwenye makucha yake kwanza, alichofanya ni kufuatilia nyendo
zangu, kila ninalolifanya yupo nyuma yangu, na alinipatia kwenye kazi
nilizokuwa nikipewa. Hakujua kuwa mimi nipo kazini.
Kuna kazi nyingine ilibidi ujifanye wewe ni changudoa, na inabidi
wakati mwingine ujitolee kufanya hata yale yasiyowezekana kufanya ili kuupata
ukweli, yeye akachukua kumbukumbu za matukio hayo, kama kinga yake, ujue kazi
hiyo nilikuwa naifanya hata mume wangu hajui, hadi leo mume wangu hafahamu kuwa
mimi nilikuwa siadii wa kujitegemea.
Kiukweli nilijitahidi sana kujificha, na ndicho bosi wangu
alikipendea hicho, na siri ya hayo yote ni kuwa sikuwahi kumuambia mtu naifanya
hiyo kazi zaidi ya bosi wangu..na kwa mume wangu yeye alijua nafanya kazi za kawaida
za biashara za hapa za pale za mikononi, mali kauli, na hivyo, kumbe mwenzake
nilikuwa na kazi za ushushu. Na alichoweza kukipata kwangu, huyu mtu ilikuwa
sio kwa madhambi yangu, yeye hakulijua hilo, ila niliogopa je mume wangu
akipata ushahidi huo itakuwaje..
Ukumbuke kuwa mimi na mpenzi wangu wa zamani pendo letu lilikuwa
kama linaanza kufifia hivi, lakini sio moyoni, na mimi niliona tukiendelea kuwa
karibu naye sana, hata yale ya siri yatakuja kujulikana, kwahiyo siku mume wa familia akikwazika huko
kwa mke wake, hana pa kwenda anakuja kwangu, tulikuwa tunakutana sehemu ambayo
tuna uhakika hatutaonekana na hata tukionekana nisitambulikane.
Kama nilivyosema awali mimi nilishakuwa mtu mwingine, kuwa naweza
kujibadili, naweza kujiweka kinamna ambayo mtu huwezi kunigundua, na nikifika
kwa mtu wangu najirudisha kwa hali yangu..ni utundu tu kidogo wa kucheza na
mavazi, ..na vipodosi , hata kuvaa ngozi za bandia, ..ni vitu vya kawaida ,
wala sio uchawi.
Lakini pamoja na hayo, mimi kwa vile nilishajitambua na nilishaona
haya yanayoendelea hayana mwisho mnzuri, nilianza kutumie hekima ya kumweka
mwenzangu katika njia sahihi, kuwa yeye ni mume wa mtu na mimi ni mke wa mtu,
inabidi hilo tuliheshimu sana, vinginevyo tutakosa kote,…hilo likawa sasa
linamkwaza mwenzangu.
Mimi nikawa najitahidi kulinda ndoa yangu yeye akitoka hapo hawezi
kuvumilia tena, anatoka kwenda huko anapokwenda, kulewa na kufanya mambo ya
aibu,.. nilikuwa naumia sana, maana wakati mwingine nayaona, ila sikutaka sana
kumfuatilia kwenye mswala yake, kwasababu nilijua nitaumia,…kuna wakati
mwingine unamuonea huruma, unafikia kumweka sawa, na hapo ..ndipo Makabrasha
akapata ule ushahidi alioutaka yeye..
Ina maana aliweka vifaa vya kuchukua kila tendo tunalolifanya, nia
na lengo lake ni kufanikisha kile alichokitaka...akilini na mafunzo yangu
yalikuwa bado machanga ya kugundua vitu kama hivyo, japokuwa nilikuwa nafahamu
vitu hivyo vipo, lakini sikuwa na….sikutilia maanani kuwa anaweza kutifanyia
hivyo, kabisa…
Makabrasha, alipoona pia kuwa hayo aliyakusanya kama ushahidi wa
kuninasa mimi hayampi mwanya wa kuyafanya yale anayoyataka yeye kuyafanya,
akaamua kuingia ndani zaidi, alimshawishi mume wa familia ajitahidi kuwa name,
alivyomshauri ili tupate mtoto wa kiume,..kumbe nia yake tendo halihis
lionekane na liwe ushahid.
Alikuja kuweka seehmu ya sisi kukutana, hatukuelewa lengo hilo,
kumbe humo alishaweka mitambo yake na bila kujielewa tukaja kunaswa..unajau
tena huruma yangu iliniponza, nikafanya kile ambacho nilikipiga vita sana, ..na
makabrasha akapata kitu cha kuninasa…
Ndani ya familia ya walengwa huko akaja kugundua hiyo mikataba,
aliigundua katika mazungumzo yao, ..sasa jinsi ya kuipata ..ndio akatumia mbinu
hiyo ya video za matukio, akagundua wapi ilipo, na..ilikuwa kazi rahisi
kumshawishi mume wa familia kutoa ufunguo…
Akawa sasa kafanikiwa kwa
kiasi kikubwa,..na iliyobakiwa ikawa ni lugha za vitisho,akitaka kitu
usipompatia, basi anaonyesha hayo madhambi, kuwa atayafikisha kwa mume wangu au
kwa mke wa jamaa..
Hapo mume wa familia ikabidi afanye kila anachoambiwa, angelifanya nini sasa, kwangu mimi bado
..japokuwa alikuwa na ushahidi lakini sana sana alitaka huko kwa mume wa
familia,..baadae akafanikiwa kutimiza hatima yake ya kuingilia nyumba hiyo ya
mume na mke wa familia kama alivyotaka yeye, kama alivyoelezea mwenzangu.
Kuna mengi aliyoyafanya
keshayaeleza aliyetangulia japokuwa kuna mengi mimi nayafahamu zaidi ya
hayo…ila hadi hapo utaona kuwa ilifikia muda, mume wa familia akawa hana jinsi,
ikabidi akubaliane na kile anachoambiwa na marehemu.
*********
Nashukuru mungu kuwa hadi
marehemu anaondoka, hakuwahi kunitambua upande wa pili wa kazi zangu, na hilo
lilinisaidia sana,…nakumbuka siku moja alituita mimi na mwenzangu,..
‘Nduguzanguni, najua tulifikia mahali tukawa hatuelewani
tena,..tukaondoa udugu wetu, urafiki wetu, nilijua itafika mahali mtakwama
mtarudi tena kwangu, kwa hiari au kwa nguvu..sasa mumerudi kwangu, au sio..’akasema
‘Nawafahamu sana, kuwa huko mlipo hampo kwa mapenzi, na sasa
nimepata ushahid huo, kuwa ndoa ya mume wa familia na mkewe haipo kwenye
msimamo mwema, hiyo ni kuashiria kuwa siku yoyote ndoa hiyo inaweza kuwa
marehemu, ..’akasema
‘Kwahiyo kabla ya hiyo ndoa haijafikia ukingoni, basi ni bora kuwa
na mpango wa pamoja, kuhakikisha mali zote za familia zinakuwa mikononi mwa
mume wa familia, lakini kwa vile mume wa familia ana mauchafu yake yakibainika
atanyang’anywa kila kitu, sio vyema ikawa mikononi mwake, basi itafutwe namna
mali hiyo itakuwa salama zaidi, kwahiyo mipango iwe ni namna gani mali hiyo
itakuwa mikononi mwake
‘Mimi nayafanya haya kwa ajili yenu, ..mnasikia, nina uhakika
ikiwa hiyo mali ikiwa kwangu kwanza kama wakili wenu , lakini pia kwa kumiliki
hisa zaidi ya nusu, itakuwa ni salama zaidi.
Hapo kwenye hisa mume wa
familia akapinga, lakini akaja kuambiwa kama hili analiona gumu, basi alipe
madeni ya huyo marehemu yote, kama ana uwezo huo..hakuwa na pesa, alishakuwa
mtu wa madeni, alishafanyiwa mengi, ya kutoa pea ili apate picha au video,
akakamuliwa hadi tone la mwisho, sasa akawa mtu wa madeni, isingelikuwa mke
wangu angeliuza hata magari yakampuni..sasa akawa anakopeshwa na marehemu,
hakujua anayefanya hayo yote ni marehemu,..
‘Marehemu alip[opiga mahesabu ya madeni anayomdai jamaa ikawa ni
makubwa sana, jamaa hana uwezo wa kulipa,. Sasa afanyeje.., basi marehemu akasema
njia ni rahis ni yeye kuyageuza hayo madeni kuwa hisa..alipe kwa kumuuzia hisa…ilikuja
kuwa ngumu awali, lakini mwisho wa siku
mume wa familia akawa hana hoja,..ikabidi auze hisa kwa kulipa madeni ya
marehemu..’akasema.
Kila mume wa familia
akipinga jambo, anakuja kuonyeshwa uchafu wake, anadaiwa madeni, ..basi akawa mtumwa wa jamaa…na
ikafikia muda sasa kashindwa akaja kwangu kuniomba msamaha, na kuomba
ushauri…na alikuja kipindi ambacho hata mimi marehemu ananindama,..na
ningemshauri nini mimi…, nilimuambia ukweli hayo umeyataka yeye mwenyewe
iliyobakia kwasasa umuache huyo jamaa afanye atakavyo
‘Mimi siwezi nitamuua…’akasema
‘Wewe una ubavu wa kupambana na Makabrsha, hilo sahau, labda kama
unataka kujitakia matatizo..’nikamwambia, lakini jamaa siku hiyo alitoka na
ajenda ya kutafuta namna ya kumuua Makbrasha, na hata tulipokutana tena na tena
akawa na ajenda hiyo hiyo, kuwa atatii yote, ila siku ya mwisho wa kusaini huo
mkataba wa kukabidhi kila kitu hapo ndipo siku atafanya kile alichokidhamiria…
‘Mimi sipo, ..kama unataka kufanya mauaji, usinihusishe mimi
kabisa..’nikamwambia
‘Nimekuambiatu..’akasema na siku zikawa zinakwenda nikaona wao
sasa wapo sambamba, mikakati ya pamoja, ikawa inafanyika, hadi wakafikia
kukubaliana kuwa hayo yafanyika kwa masilahi ya pamoja,..ndio ikapangwa
mikakati ya kubadili huo mkataba wa familia, hayo yalifanyika bila ya mimi
kushirikishwa.
‘Unajua pamoja na yote hayo mimi niliendelea kujitolea kuhakikisha
familia ya mke na mume ipo salama, ilikuwa moja ya kazi angu kutoka kwa bosi
wangu, kwa siri ajabu, lakini sikuweza kulitatua hilo, unauma na kupulizia,
huku unafahamu mbaya ni nani.. nikawa sasa nafanya kazi mbili kwa waakti mmoja,
Kumlinda mpenzi wangu, na kuilinda familia na huyo shetani,
asizidi kuleta madhara, na ili hilo lifanikiwe ikanibidi na mimi sasa niwe
mtumwa wa huyo jamaa..
Nikaja kugundua kuwa sio marehemu tu, kumbe hata marehemu alikuwa
akitumiwa, na kwa jinsi alivyofanya, isingelikuwa rahis kumdhibiti, ndio
nikaongea na bosi wangu kuhusu hilo, lakini sikuwahi kumuambia kuhus mahusiaono
yangu na mume wa familia, hilo lilikuwa siri kubwa sana kwetu anayefahamu ni
marehemu na ili marehemu aendelee kulificha hilo,..ni mimi kuwa mtumwa wake
Katika kuhangaika nikajikuta mikononi mwa wapinzani wa mzee, sijui
walinijuaje ila bado walikuwa hawana uhakika..na sio kwamba walinijua kutokana
na kazi zangu ila wanasema wameona mimi nina kipaji cha kuwatumikia, umbo,
sura..ujanja, kuongea, ..unajua tena,, wanakiniomba waniajiri kwao..
Kiukweli mimi niliwakatalia, japokuwa walikuwa tayari kunilipa
mapesa mengi, ili niajiriwe na wao, ..walipoona kuwa mimi ni mgumu ndio
wakamtumia Makabrsha, makabrasha akaja kuniambia hao watu wananihitajia, na hao
watu ni hatari sana, wakikutaka uwafanyie kazi zao ukikataa, wanakuua, hawasiti
kumuua mtu.
‘Sasa mimi nifanye nini..?’ nikamuuliza
‘Cha kufanya nitaambia utakuwa na mimi, nakuandaa ili baadae uje
kuajiriwa na wao..’akasema
‘Mpaka lini..?’ nikamuuliza nikiwa na malengo yangu kichwani
‘Mpaka nitakaporizika mimi, maana nakuhitajia kwa kazi zangu,
zikiisha basi, itabidi uende huko..’akasema.
‘Hapo una ujanja tena..ikabidi kwanza niandike barua ya kuacha
kazi kwa bosi wangu, lakini sikuweza kumuambia dhumuni langu ni nini, ila
nilitaka hata nikiingia huko, niwe na mikakati ya kulimaliza hilo kundi kwa
namna yangu mwenyewe japokuwa najua hiyo ni hatari kubwa sana kwangu.
Nikamwambia Makabrsha nimekubali, lakini kwa masharti, kuwa
aachane kabisa na familia ya mke na mume, aachana na kazi yake hiyo mbaya..
‘Hahaha, unajua hilo haliwezekani..’akasema
‘Kwanini…?’ nikamuuliza
‘Nitakuja kukuambia pale unakaposaini mkataba wa ajira kwangu, na
mkataba wa kukubali kuwa umeachana na familia hiyo ya mpinzani wa bosi wangu..
‘Mpinzani wa bosi wako..?’ nikauliza kama mshangao
‘Ndiyo mambo ambayo utakuja kuyafahamu baadae..’akasema
Wakati huyu mdada anaendelea kuongea, kukasikika sauti, ya mtu
kama analia..mdada akatulia kuongea na akitulia sauti hiyo inapotea badae akaja
kugundua ni nani analia..
‘Sasa unalia, utalia sana, hapa ndio nimeanza, nilikuwambia leo
ndio siku ya hukumu, upende usipende, hukuniamini, hapo ndio nimeanza…’akasema
mzungumzaji
NB: Naishia hapa kwa muda,
WAZO LA LEO: Ukweli unauma lakin ukweli ndio njia
sahih ya kutatua magumu yote, tujifunze kuwa wakweli kwa watu wenye kuaminika, …
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment