Sikuweza kuvumilia tena niliona liwalo na liwe, nataka kumpata
mtoto wangu…
Tuendelee na kisa chetu..
**************
Kuna kitu kimoja tunajifunza kwenye kazi zetu, hata siku moja
usitake hasira ndio zikutawale ukashindwa kuhimili nafsi yako, ukijua kuwa adui
yako ana kila kitu. Ni muhimu sana kuwa makini, kwani adui wengine hawajali,
kutoa roho za wengine sio kitu kigumu.
Kwahiyo pamoja ya kuwa niliondoka mle ndani kwa hasira, bado
utaalamu wangu wa kiupelelezi niliulinda, nilitoka kwa tahadhari, na
kuhakikisha kuwa sitafanya makosa
yatakayo mgharimu mtoto wangu.
Ujue kwa muda ule nilikuwa kwenye ofisi niliyopewa, ofisi yangu
eti kama bosi mtarajiwa, kwahiyo nilipotoka pale nilikuwa kwenye ofisi za
ghorofa ya juu, sio kule chini sehemu ya kulala…na anilijua siku hiyo
sitakubali kwenda kule tena, mpaka nijua hatima ya mtoto wangu.
Nikatoka mle ndani ya ile ofisi nikawa natembea nikipita ofisi ya
kwanza, ofisi ya pili nikasikia sauti, kwanza nilihakikisha mbele au nyuma
hakuna mtu anayenifuata, nilijua huenda maeneo yote hayo yana video za kuchukua
matukio, sikujali kwa hilo
Nilijifanya kama nataka kuingia kwenye ile ofisi, huku nikitegea
siku kubahatisha tu, hao watu humo ndani wanaongea nini…
‘Nimeshakufanyia kila kitu unachokitaka, nimekutii, nimekusaidia
na sasa umefanikisha kile ulichokitaka,kwanini bado waendelea kunifanya kama
mtumwa wako, ...’sauti ya kike ikalalamika.
‘Ndio wewe ni mtmwa wangu ulielewe hilo, japokuwa nafahamu kuwa
nakuonea, lakini ni kwa vile wakati mwingine hutaki kunitiii amri yangu,
inabidi nifanye haya ninayoyafanya sasa hivi..’sauti ya kiume ikasema
‘Kiukweli nimechoka..’sauti ya kike
‘Sikiliza ninachotaka mimi kutoka
kwako ni utii, nikitaka hiki ukifanye, basi ukifanye mara moja, ndivyo
makubaliano yetu yalivyo,...hata hivyo nisamehe, leo akili yangu haijakaa sawa,...nisamehe
mtumwa wangu eeh,..’sauti ya kiume
‘Sitaweza kukusamehe kamwe..’sauti ya kike
‘Nisikiliza basi…mimi nakuhakikishia kuwa, hili likikamilika, wewe
na wengine wote mtakuwa huru, usiwe na wasiwasi na hilo…haya mambo nataka
yamalizike ili hata mimi nitulie, na kuanza kula raha za dunia,….habu nikuulize
kwa hivi sasa kuna kitu unanidai...’sauti ya kiume ikauliza.
‘Nipe hizo kumbukuzi zote za mapicha machafu uliyochukua kutoka
kwangu na kwa watu wengine, niziharibu, hapo ndipo nitaamini maneno yako, ili
watu wawe na amani na ndoa zao...’ sauti ya kike.
‘Hilo kamwe lisikutie wasiwasi, ndoa zenu zitakuwa na amani kama
nyie wenyewe mtajituliza na waume zenu, tatizo nyie mumekimbilia kuolewa kwa
kutaka mali, na sio upendo, kwahiyo hilo sio kosa langu..au nimekosea…’sauti ya
kiume
‘Sio kweli, sisi pamoja na hayo tulishaamua kutulia na waume zetu,
mengine uliyatengeneza wewe, ili yatokee na upate unachokitaka..’sauti ya kike
‘Hapana sio kweli, mimi nilijua tu hamutaweza kutulia, hamtaweza
kuwa mbali mbali, ipo siku mtakumbukana, na sikufany aharaka kwa hilo, taratibu
kama yule ndege tai…anavyovizia mizigo,..kwahiyo sio kosa langu, ila mimi
nawahakikishia kuwa kazi hii ilikuwa na mipaka na muda wake, ikikamiliza, haina
haja tena, hizo picha, video, nitaviharibu, mbele yako, wewe nipe mud unimalize
kazi hiyo iliyobakia,...’ikasema sauti ya kiume
‘Na malipo yangu je…?’ sauti ya kike
‘Malipo gani zaidi, ..bado kazi haijaisha unataka malipo, malipo
yako utapata usiwe na shaka…’sauti ya kiume
‘Kazi gani imebakia,..mikataba si imeshakamilika su sio, sasa hivi
unamiliki hisa, kuna mipesa kibai umeshalipwa na wahanga wako wa
milungula,..bado huajtosheka unataka nini wewe, kiukweli wewe ni shetani asiyeshiba madhambi..’sauti ya kike
‘Hahaha napenda sana hiyo lugha yako, kumbe unafahamu kuwa mimi ni
shetani, basi mambo bado…kuna mambo bado hayajakamilika..’sauti ya kiume
Mara nikahisi kuna suti nyuma yangu…haraka nikajifanya kutembea
hadi ofisi za mbele na nilipohakikisha hakuna mtu, nikarudi tena kusikiliza kwa
muda kama ule ulikuwa mchana watu wanapita, lakini siku ile sikuona watu
wakipita pita na hata wakitokea ni mtu anatoka kwenye ofisi fulani na kuelekea
chini au juu.
Niliporudi pale nikasikia
‘Mimi nayaelewa hayo yote, kuwa ni mabaya na hayana mwisho mwema, ndio maana njiandaa kuachana na tabia hiyo,
nikikamilisha hili, natulia, ....nitakuwa na haja gani tena, wakati nitakuwa
mkurugenzi mkuu wa makampuni kadhaaa, yenye mabilioni ya pesa, ....tatizo
anayenichelewesha ni huyo mtu wako wako, ngoja akija kesho kutwa, eeh…’akatulia
‘Kesho kutwa au kesho..?’ sauti ya kike ikauliza
‘Kesho nina mambo mengine ya kufuatilia, kuhakikisha hiyo mikataba
imefika sehemu husika, na kwenda kukutana na wafadhili wangu, kuwahakikishia
kuwa mambo yapo kama ilivyotakiwa iwe, kwahiyo ushindi ni lazima…’sauti ya
kiume
‘Sikiliza…mimi sihitaji kuingie kwenye siasa, nataka kuwekeza
kijijini, mimi sitaki kuishi mjini, nataka maisha yangu yawe huko kijijini,
hadi hivi sasa mume wngu anafahamu nipo huko…’sauti ya kike
‘Najua sana ni nini unakifanya huko, na hayo yote ulifanya kwa
kuogopa au sio…sasa hutakwua an hajaya kuogopa, usitishike na wanaume akitaka
kukuacha, muambie afanye hivyo, hataweza maana hai hapo atakuwa hana
kitu…’akasema
‘Tatizo wewe unajiaminisha sana, unafikiri wao ni wajinga wakae
kimia tu..’akasema
‘Ndio maana nilikuambia hivyo kuwa muda wa kuziharibu hizo picha
na video bado, hukunielewa, hivyo vitu havijamaliza kazi zake, zitamaliza kazi
zake pale tutakapohakikisha hao watu hawana kitu na hawana namna ya kufanya,..na
wafadhili wangu wameridhika, na kushika hatamu…na mimi huku niwe na mamlaka ya
vitega uchumi vyote..’sauti ya kiume.
Kukawa na ukimia fulani hivi…halafu sauti ikasema
‘Kuna nini, mbona umesimama kuongea, una mashaka gani na maneno
yako au umeona nini…?’ sauti ya kike ikauliza
‘Kule ofisi ya bosi wako, hakuna ishara,…unaona hapa, kuna alama
nyekundu kuashiria kuwa huko kuna tatizo,.. yaonekana kamera za kuonyesha
matukio za kule hazifanyi kazi, kuna nini..unajua huyo bosi wako simuamini, ni
hatari sana, yawezekana kafanya jambo…’sauti ya kiume ikasema
‘Huyo mnamsumbua bure, yeye ni mzazi, na sioni umuhimu wake kwa
hili… muachieni akasome, na mpeni mtoto wake, hana tatizo na nyie..yeye
kawakosea nini..unajua hadi hivi sasa mimi kama mimi sioni umuhimu wake….’sauti
ya kike ikasema.
‘Wewe utakuja kuona umuhimu wake….na unanishangaza sana,…haya
yaliyotokea hadi yeye kuweka sahihi hujaona umuhimu wake, wewe hujui kuwa huyo
ndiye kiongozi wao wa usalama, huyo tukimweka mikononi, hao watu hawana ulinzi,
hawana mtu wa kumtegemea…sikiliza kama haupo upande wangu niambie, nifanye vitu
vyangu…’sauti ya kiume ikasema
‘Kwani mimi nilikuwa upande wenu, mimi mumenilazimisha na sina la
kufanya, nitakutii, ili utimize mambo yako, lakini mkimaliza …hapo na mimi
nitakuwa huru, na kiujumla mimi sitaki kujishughulisha na jambo lolote hata
bosi wangu nilishamuambia hivyo…’sauti ya kike.
‘Wewe au mwingine, ukiishiwa pesa hukumbuko ulichosema, sikiliza
wewe uwe upande wetu, sehemu ambapo pesa
hazikauki, unasikia,..oh, unaona hapa, hii alama bado inaonekana, na sioni
chochote kule alipo huyo bosi wako, yule mlinzi kaenda wapo, nampigia simu
hapatikani..’sauti ya kiume
Kukawa na ukimia kidogo, halafu sauti ikasema tena.
‘Nahisi mitambo ya pale imeharibika, kama sio yeye kafanya jambo
basi kuna tatizo, ngoja niongee na mtu wangu…’sauti kasema na kukawa na ukimia
fulani baadae sauti ikasema
‘Na huyu mshenzi sijui kaenda wapi, simu yake haipokelewi, sasa
sikiliza hebu nenda wewe, kaangalie kinachoendelea unasikia, …’sauti ya kiume
ikamsema
‘Sawa nitaenda, ila usiwe na wasiwasi na huyo mdada, nilishamuweka
sawa, anajua madhara yake anampenda sana mtoto wake, hawezi kufanya jambo la
ajabu, hebu angalia tena labda ni mitambo yako tu hiyo..’sauti ya kike ikasema.
‘Nisikiliza amri yangu…unasikia wewe nenda,…’sauti ikasema
‘Sawa bosi,…’kabla hajaondoka suti ikasema
‘Kabla hujaondoka,ule mkataba niliokuambia uuchukua kwa mume wako
upo wapi, unajua kesho, ndio siku nataka
kwenda kuufanyia kazi,..unafikiri nimesahau eeh..’sauti ya kiume
‘Nilikuambia bado sijaupata, na nitaupate na mimi sipo naye,
unajua mimi nipo wapi, unaniuliza kitu ambacho hata wewe unakifahamu, mimi nipo
wapi, si nipo kijijini, au umesahau,..hata hivyo, mimi naona hayo ya mume wangu
achana nayo, hayafai, hayana umuhimu, wa nini kwanza..?’ akauliza
‘Ina umuhimu sana, tunamuhitaji sana huyo mtu, achilia mbali na
kazi yake lakini pia kisiasa, ana umuhimu wake,…ngoja nikimalizia hii kazi mimi
mwenyewe nitamfuatilia, utaona nilivyo, …yeye mwenyewe atasalami amri, kuna
video yake mbaya nikimuonyesha ni lazima atanitafuta…’akasema
‘Video yake!! Video gani hiyo..?’sauti ya kike ikauliza
‘Siwezi kukuonyesha wewe…ukiiona unaweza ukachanganyikiwa, na sitaki uende kuleta fujo,..wewe una umuhimu sana hapa,
tatizo lako ulimuamini sana, hakuna msafi hapa, mimi wote nawafahamu madhambi
yao, asikudanganye mtu, wewe tulia na mimi ule nchi,…’sauti ya kiume.
Niliona nikiendelea kukaa
pale ninaweza kushukiwa kwahiyo nikasogea hadi kwenye mlango, nikausukuma ule
mlango kwa taratibu,.. nikaona unafunguka…mimi kwenye begi langu nilikuwa na
kifaa, nikakitoa na kuchukua kitufe kidogo, kama kitenesi, nikakiweka hicho
kifaa,..ni kidogo, huwezi kudhania ni kitu muhimu sana, nilipohakikisha kuwa
mlango upo wazi, nikakitumbukiza kile kitenesi, kikawa kinaserereka kulekea ndani.
‘Umedondosha nini…na mbona mlango kama upo wazi,..’sauti ya kiume
ikauliza
‘Kumedondoka kitu, !! ni kidude cha kuwekea peni, mmh, na wewe una
msikio, umesikiaje na wewe upo unaangalia mitambo yako huko..?’ sauti ya kike
ikauliza
‘Kila kitu kinachofanyika kwenye maeneo yangu ninakiona hapa..,
ila huyu bosi wako kawa mjanja…kwa hivi sasa simuoni kabisa, .., haya wewe nenda
kamuangalie..hivi sasa ni mchana sitaki mimi kuonana naye,.., hiyo kazi ni
yako, na akifanya ujanja tu..mtoto wake kiukweli atampoteza, sitanii hili,
unanifahamu nilivyo.’sauti ikasema
‘Sawa bosi…ngoja niende..’sauti ya kike
Na mimi niliposikia hivyo, nikageuka na kuondoka, kwa haraka nikitaka
kurudi ofisini kwangu, lakini kabla sijageuka, nikahisi mtu yupo nyuma yangu…
‘Unafikiri unafanya nini hapa…’ilikuwa sauti nyuma yangu na kabla
sijamjibu kitu mara mlango ukafunguliwa akatokea mdada,…mmh, sijawahi kumuona
huyu mdada kabla, muonekano wake ni kama mzungu fulani hivi, aliponiona kwanza
alishtuka baadae akasema
‘Kwanini hujapiga hodi,…nilikuambia ukija upige hodi, sasa
sikiliza bosi hana muda wa kuongea na wewe, twende huko huko ofisini
kwako..’akasema huyo mdada.
Na jamaa yule aliyekuwa nyuma yangu akabakia kaduwaa, …tukawa
tunatembea kuelekea kule ofisini kwangu na huyo jamaa sasa akawa anataka kufungua
mlango kuingia kwenye hiyo ofisi aliyotoka huyo mdada, huyu mdada akasema;
‘Wewe, Bosi alikuwa akikuulizia muda mrefu, kakasirika sana,
ukienda kuonana naye sasa hivi utalikoroga, wewe katulie kituoni kwako kwa
muda, baadae ndio uende, kama atakuhitajia tena..’akasema mdada
‘Poa….kwani hukumuambia kuwa nilitoka kidogo..’jamaa akasema na
kuondoka kurudi huko alipotoka.
Na sisi tukarudi ofisini kwangu, na huyo mdada aliyejiweka kama mzungu
akasema;
‘Wewe vipi kwanini unataka kuharibu…?’ akaniuliza
‘Sina amani nataka kuonana na mtoto wangu..’nikasema
‘Sikiliza nimeshakuambia kila kitu kitakuwa sawa, wewe hakikisha
unafanya kila wanachokita wao, kwanini hunielewi, utaharibu na utakuja
kujijutia, …’kabla hajamaliza akaona kazi niliyoifanya kule juu..
‘Mungu wangu, huyu mtu akija kuona hiki kwanini uemvunja hiyo taa,…?’ akauliza,
‘Wewe muite fundi, aje arekebishe kwa haraka lakini asirudishe
hiyo video kamera, wewe huoni kuwa hiyo video kamera ilikuwa imefichwa kwenye
hiyo taa,, je waweza kumuita fundi akarekebisha hilo tatizo kwa haraka..?’
nikamuuliza huyo mdada
Huyo mdada kwa haraka akachukua simu na kumpigia fundi, haikupita
muda akaja fundi akapata maelekezo, na haikuchukua muda, kila kitu kikawa sawa.
‘Safi kabisa,…’nikasema
‘Sasa wewe rudi kwa jamaa yako endelea kuongea naye, nataka kupata
ushahidi zaidi..’nikasema
‘Kwa vipi, ok, bosi nimekuelewa, ila tafadhali usifaney tena
hivyo, fuata wanavyokuambia, mengine niachie mimi, …’akasema huyo mdada na
kuondoka.
Nilisubiria kidogo, baadae nikachukua simu yangu na kugeuza upande wa
nyuma nikatoa kitu fulani kweney begi langu, nikakiweka kwenye ile simu, baadae mitambo yangu ikaanza kufanya kazi….nikawa
sasa nasiiliza kile wanachokiongea kule kwa huyo jamaa,, mpaka muda huo
nilikuwa sijafahamu ni nani, huenda ni Makabrsha, lakini sikuwa na uhakika huo.
‘Umemkuta bosi wako, kafanya nini mbona bado mitambo haionyeshi
kitu..hivi yeye hajui haya yote ni kwa jili yao, yeye akiwa mmojawapo..’sauti
ikauliza
‘Yupo lakini hana amani, anamtaka mtoto wake…’akasema
‘Mtoto wake wa nini, hajui hayo ni kwa usalama wa mtoto wake, wewe
unafikiri kama hao wenzetu wangelimchukua huyo mtoto ingelikuwaje, wangempima
kwanza DNA, halafau ikawa ndio sababu ya kuharibu kila kitu…’akasema mwanaume
‘Ni kawaida kwa mzazi yote hasa mama wa mtoto, huwezi kumlaumu kwa
hilo, ila nimeongea naye, baadae atarudi kule chini kujiandaa kwa ajili ya kile
mlichomuagiza au sio..’sauti ya kike
‘Sawa hakuna shinda baadae nitakwenda mwenyewe kuona kuna tatizi
gani..lakini sitaki akiwemo humo ndani..’sauti ya kiume.
.
‘ Sawa bosi, jihangaishe tu, lakini hawo hawo unawasumbua, ..hasa
huyo docta, na wengineo, watakuja kuwa mashahidi siku ukiwa umesimama
kizimbani...’ikasema sauti ya kike.
‘Thubutu, labda kizimba cha kaburini, lakini nikiwa hai , hivi
hivi, hanipati mtu, wewe hunijui tu, kila kitu kina plan A na B, ..kwa hivi
sasa wameshasambaatika na hakuna wa kumfunga paka kengele,…’sauti ya kiume.
‘Sawa bosi…’sauti ya kike.
‘Sawa bosi, sawa bosi,..unajifanya mtiifu kumbe kigeu geu…nakuambia
ukweli baada ya haya, utakuja kuniona umuhimu wangu, …hata hao watu wa usalama sasa hivi
wananiheshimu, kuna tatizo kidogo, nasikia, huko kwa mdhamini wa mikataba, kuna
kitu kimetokea, ..lakini nitamaliza hilo tatizi ..’sauti ya kiume ikasema.
‘Haya wewe jidanganye tu, umesema kuwa docta naye umepata video ya
mapicha yake mabaya, ulimpataje madhambi yake, maana namuona ni mtu mtulivu
sana,...?’ sauti ya kike ikauliza.
‘Hawo unaowaona watulivu, ndio balaa, wana mambo yao ya chini kwa
chini, na wakati mwingine ni uwoga tu, nilimkamatisha kabinti kamoja karembo,
...huyo binti alifika kwake kama mgonjwa, na huyu bint anajua kazi badala ya matibabu,
ikageuka kuwa kitu kingine,..sitaki uone hayo, hayo ni kwa ajili ya kazi,
msamehe tu, hata ingelikuwa ni mimi nisingeliweza kuvumilia, hahaha…’akasema
‘Mjinga mkubwa wewe kumbe sio yeye, ni wewe ulimkamatisha kabinti,
sasa unatarajia nini, kuwa utanitishia mimi, kuwa mimi nikiona hiyo video na
mapicha hayo mabaya,tutaachana na mume wangu…, hahaha, hata kama nitamfuma
akiwa mbashara, mimi sitaumia saaana…, maana najua mimi nina madhambi zaidi
yake..’sauti ya kike.
‘Ni wewe, lakini sio yeye, docta ni muoga wa kufumaniwa, anajali
sana ndoa yake, ila kwa …huyo mdada, alishindwa, na pia, …ile ya yeye n mpenzi
wake wa zamani, pia ninayo, siwezi kukuonyesha,..japokwua sio mbaya kihivyo,
lakini inaonyesha hisia za kuwa hao watu bado wanapendana, mimi kwangu inatosha
akbisa kama ushahid..hao watote hawaniwezi ..kila mmoja nimeshamuwekea kinaso
chake, …na wafadhili wangu watafurahi sana…’ akasema na mara sauti ikasimama.
‘Kiukweli mimi sitishiki tena na huo uchafu wako, fanya utakayo,
lakini mimi nina imani ipo siku utaumbuka, na ...’akatulia kidogo, hapo
nikaingiwa na wasiwasi, nikifikiria huenda wamekishitukia hicho chombo
nilichokipenyeza mle ndani.
‘Mbona unasita kuongea, ongea tu..mimi nakusikiliza..’sauti ya
kiume
‘Ni wewe nakuona kama unaangalia angalia chini, umeona kitu gani....’sauti
ya kike.
‘Kuna kitu hakipo sawa, una uhakika yule mdada hajafanya kitu, ..?’
akauliza
‘Kama wewe huniamini, nenda ukaone mwenyewe..’sauti ya kike
ikasema
‘Siwezi kwenda kweli kwa hivi sasa, ila nitakwenda, ni lazima kuna
kitu kimefanyika, nitakwenda kuhakikisha, huyo mdada ni hatari....’sauti ya
kiume.
‘Sasa mimi naondoka…kuna zaidi la kufanya..?’sauti ya kike
‘Usiondoke kwanza, nataka wewe uhakikishe huyo mdada akiondoka
umemuweka sawa, unasikia, asije akaharibu,…nilitaka muende naye hadi uwanja wa
ndege, lakini wewe utabakia huku nyuma kuhakikisha mambo fulani fulani, na
mtoto tumemuhamisha, kwa usalama zaidi..’akasema
‘Ina maana huyo mdada hataondoka na mtoto wake..?’ akauliza
‘Hapana huyo mtoto atampata siku ile akiondoka, siku akirudi masomoni
baada ya kuhakikisha kila kitu kipo shwari, huyo ndiye ndoana yetu kwa hivi
sasa, na ni kwa manufaa yake, ili wenzetu wasije kumuona huyo mtoto maana mpaka
sasa hawajahi kumuona sura yake..’sauti ya kiume
‘Na zaidi ya hapo utanihitajia kwa lipi zaidi au ndio nitakuwa
nimemaliza kazi na wewe..?’ sauti ya kike ikauliza
‘Unahitajika kuwepo pia na huyo mwenzako akija, nataka huyo kidume
wako, akubali kila kitu, aweke sahihi kwenye mikataba yote ikishamalizika hiyo
kazi imekamlika, yeye hana kitu, atakwua chini yangu, na wewe utamfanya
utakavyo, maana …usione kuwa mimi ni mbaya, nafanya hivyo, kwa vile yeye
akibakiwa na hizo mali hana akili ya kuziendeleza, umeona anavyofanya , …tunahitajia
watu kama mimi na bosi wako, na wewe…umenielewa, yeye ndio ataendelea kuwa na
hisa, lakini mamlaka,hayawezi…unasikia…’akasema
‘Mimi sitaki kuonana na yeye, unajua mimi sijulikani kuwa nipo
hapa Dar, unalifahamu hilo, pili, sitaki kuwa karibu na yeye kwa hivi sasa,
uzalendo utanishinda, kanisaliti vya kutosha, nita…’hakumaliza
‘Najua najua hilo, pole sana….lakini usimlaumu sana, maana yote
hayo yamefanyika ili kuhakikisha hili zoezi zima limekamalika, sizani kama wewe
una haja ya kuwa na wivu, au sio…’sauti ya kiume na kukawa na ukimia fulani
baadae akasema
‘Unaona eeh…nimegundua kitu kwenye hii mitambo, kule chumbani kwa
mdada, ile kamera imevunjwa, na waya zimeharibiwa ni nani kafanya hiyo kazi,
nahisi unalifahamu hilo..’sauti ya kiume
‘Mimi sijui..na mbona niliona ni taa tu imeharibika..’sauti ya
kike
‘Mbona hujaniambi,..na ni nani alitengeneza..?’ akauliza
‘Ni yule yule fundi wetu, sasa vitu vidogo kama hivyo ni mpaka
nikuambie au umenileta hapa kwa kazi..?’akaambiwa
‘Basi kwa ujinga wake…huyo fundi sijui lakini…atakuwa kaharibu
zile waya za kamera…itabidi baadae niende kuifanya hiyo kazi mwenyewe…’sauti ya
kiume.
‘Sawa..mimi sikulijua hilo…’akasema
‘Acha ujanja wako wewe, nakufahamu sana, wewe ni mnafikii …usifikiri
mimi nakuaminii sana, hakuna kitu kama hicho,…sikiliza alichofanya huyo bosi
wako hakiwezi kuniathiri kamwe, mweneywe utaona, najua kuna kitu kakipandikiza
mahali, kama sio kwako basi kuna mbinu katumia, huko alipo anatusikiliza..’akasema
‘Mimi sijui hayo… na sizani kama kuna ukweli wa hilo, hawezi
kufany ahivyo akijua kuwa mtoto wake yupo hatarini…’akasema mdada
‘Ni kweli, mimi sitasita kufanya lolote kwa mtoto wake, akijifanya
mjanja,atakuja kujuta,…ngoja nione la kufanya..’sauti ikasema na mimi pale pale
nikaharibu mawasiliano na kile kitufe kwahiyo hataweza kukigundua wapi kilipo.
Hata akikigundua ataona kama kitenesi tu kisicho na uhai
Mimi pale nilipo, sikutaka kupoteza muda, kwa haraka nikachukua
vitu vyangu, na kujiandaa kurudi chini, ili nikajiandae kwa ajili ya kwenda
uwanja wa ndege, nilikuwa radhi sasa kufanya kama walivyotaka, kwa usalama wa
mtoto wangu, sikuona kama kuna lolote zaidi, ilimradi nimepata uhakika wa
usalama wa mtoto wangu.
Nilikaa kidogo pale chumbani, na
ulipofika muda ambao ndege inayotoka huko inafika, akaja mtu kunichukua
hadi uwanja wa ndege na kama walivyotaka ndivyo nilivyofanya…
Mzungumzaji hapo akatulia
akimuangalia mwenyekiti na mwenyekiti alikuwa kimia, kama akiwaza jambo, na
mdada akaendelea kuongea;
‘ Na yaliyokuja kuendelea hadi siku ile ya tukio ni kama
nilivyowaambia awali..zaidi ni mambo ambayo sitakiwa kuyaongea hapa…maana hayo
ni ya kazi za polisi, ila kama mwenyekiti ataruhusu hilo, kwa kibali cha
polisi, kwanini tusiweke wazi, mnasemaje wajumbe
Mwenyekiti akatikisa kichwa kukataa.
*********
Mwenyekiti akachukua simu na kupiga namba akawa anaongea kidogo na
huyo aliyempigia halafu akasema;
‘Je mume wa familia hayo yaliyoongelewa hadi hapo na huyu askari
kanzu wenu au rafiki wa mke wako ni kweli,..unakubaliana nayo..?’ akauliza
mwenyekiti na mume wa familia akabakia kimia
‘Natumai sasa kama wewe ni muungwana, na …mimi nakushangaa sana,
hivi hadi hapo hujioni kuwa una makosa,…au wajumbe mnasemaje,..nilijua huyu
mtu, utaungama nasisi kama familia, akiri kosa, na tuwe kitu kimoja ili
kupambana na huyo adui yetu, eti jamani…’akasema mwenyekiti.
Mume wa familia akawa kimia tu, na wakili wake naye akawa kama
anafungua makabrasha yake, hakusema neno.
‘Mume wa familia, tunaongea na wewe hapo sio sehemu ya wakili
wako, maana ukweli sasa upo wazi, na
muongeji aliyepita ni mtu wako wa karibu, na zaidi ya hayo ni mtaalamu wa
upelelezi, unasemaje mume wa familia...?’ akauliza mwenyekiti, na mume wangu
akatulia kimiya kama sio yeye aliyeulizwa na baadae wakili wake akawa
anamuongelesha jambo, lakini mume wa familia akawa anatikisa kichwa kukataa.
Baadaye sana mume wa familia akasema;
‘Tatizo sio mimi kukubali hayo yaliyoongewa, au kukiri kosa, wangapi hadi hapo wana makosa,
ni mimi tu mwenye makosa, hapana,… tatizo hapo ni huyo muongeaji, mengi
kayaongea kutilia chumvi ili nionekane mimi ni mbaya, haya..si mumeshaona mimi
ni mbaya, nina makosa, na wengine je, …mnataka mimi niseme nini hapo…’akasema
‘Tunataka wewe uthibitishe kwa kauli yako je hayo yaliyosemwa ni
kweli au sio kweli, ili tuendelee..?’ akaulizwa
‘Kaongea mengi, kamuongea marehemu, kawaongelea watu wengi, na
wengi ni kama mimi, kila mmoja ana makosa yake, hata yeye muongeaji ana makosa
yake mengi , na mkumbue hayo aliyoyaongea nikipindi mimi nilikuwa mgonjwa, sasa mimi nitawezaje
kukiri kosa wakati sikuwa na ufahamu…’akasema
‘Unajua hueleweki, ina maana muda wote alichokuwa akiongea
muongeaji hakuwa na sisi, swali nakuuliza tena, haijalishi yaw engine je hayo
yanayokuhus wewe ni y akweli au sio ya kweli, maana hapa kikao kipo kwa ajili
ya familia yenu,…je ni kweli au si kweli labda nikuulize hivyo..?’ akaulizwa
‘Niwaambie ukweli wangu kutoka oyoni au sio, kwanza ..huyu mtu muongeaji
kwanza mimi simuamini, ndio ni mtaalamu wa kupanga hoja, lakini hakuwahi kutoa
ushahidi au shahidi wa yoet hayo aliyoyaongea, ni nani shahidi wa kumuunga
mkono hayo, ndio mimi au sio…ndio mnataka mimi niwe shahidi wake,..lakini mjue
jambo moja kuwa huyu mtu ni mnafiki mkubwa, msaliti, na hayo
aliyoyasema…’akasema
‘Kwahiyo hayo aliyoongea sio ya kweli..?’ akaulizwa
‘Ndio mengi sio ya ukweli, yapo ya ukweli hayaana ubishi, lakini
mengine kaongezea uwongo wake, na kafanya hivyo, kwa vile keshajua kuwa rafiki
yake kamshitukia, na akaona njia ya kujikosha na kutunga huo uwongo,, ...na kwa
uwongo wake huo, nitahakikisha, kuwa unawajibika,..’ akasema huku akiwa
kamwangalia mwenyekiti, na baadaye akamgeukia rafiki yangu na kusema;
‘Wewe, unafikiri kwa kuongea hivyo, umesalimika, unajidanganya,
hata siku moja tajiri hamuangalii masikini mara mbili, ukikosea ujue huna maana
kwake, umechezea shilingi kwenye shimo la choo, umenisaliti na mimi…, na
kwahiyo wewe huna maana kwao, na huna maana kwangu......kabisa huna maana
kabisa...’akasema
Wajumbe walimuangalia kwa macho ya kushangaa na alipoona hivyo,
haraka akisimama, na wakili wake akawa
anamuangalia kwa alama ya kuuliza machoni, yeye hakujali hilo, akaanza kutembea
kuelekea mlangoni, na watu wakabakia kimia tu, baadae kabla hajafika mlangoni
mwenyekiti ndio akasema;
‘Mjumbe unajua unachokifanya ni kukidharau kikao, unakwenda wapi,
wakati kikao hakijaisha, unanidharau
hata mimi mwenyekiti...’akasema mwenyekiti,
‘Siwezi kuendelea kukaa hapa kuzalilika, kila mmoja aliyesimama
ananisimanga mimi tu, wengine wana mabaya yao, hamtaki waambiwe, mnajua na mimi
ninafahamu kiasi gani kuhusu mabaya ya wengine,
kiukweli mimi siwezi kuvumilia tena, uwongo wenu umevuka mipaka najua kwa hivi
sasa sina langu au sio, na mumejitahidi kuni dhalilisha, kunivua nguo sina
thamani tena hapa..na ushahid upo wapi,
eehe, niambieni...’akasema na kabla hajamaliza sauti ikatokea kutoka kwa mmoja
wa wajumbe, ilikuwa sauti ndogo iliyochoka…’, ikisema;
‘Mimi ni shahidi wa hayo yaliyosemwa, ndugu mjumbe kabla
hujaondoka, ningelipedna mimi kuyathibitisha hayo, aliyoongea mjumbe aliyepita...’
sauti hiyo ikasema na wakati huo wajumbe wengi walikuwa wakimuangalia mume wa
familia, akitaak kutoka nje, na aliposikia
sauti hiyo akasimama
Na wajumbe wote wakageuka kumuangalia huyo muongeaji mpya, ni
nani, na hata mwenyekiti akafanya hivyo.
NB: Ni nani huyu tena, anataka kusema nini
WAZO LA LEO:
Ni kawaida kwa binadamu, kulalamika, pale anapotendewa ubaya, lakini binadamu
huyo huyo, akimtendea mwenzake anaona ni jambo la kawaida tu,...ni bahati
mbaya, ni ibilisi, nk , sio vizuri tukijenga tabia hiyo, kwani sote ni
binadamu hakuna mwenye moyo wa sugu, usiohisi maumivu, ndio maana wahenga
wakasema mkuki ni kwa nguruwe,...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment