Nilimfikisha rafiki yangu nyumbani kwao, na akapokelewa na shoga
yake, na sikutaka kuongea nao zaidi nikaondoka, kwani ilikuwa ni usiku, na
nilikuwa na hasira kweli kweli...na wakati natoka hapo, mara, akakatiza mtu
mbele ya gari, nikafunga breki
'Wewe vipi...?' nikafoka
Na mara huyo mtu akasogea kwenye kiyoo cha gari, akaashiria
nishushe kiyoo, kwanza nilihofia, sikusha,..akasogea karibu kiasi cha suti
kusikika;
‘Usije ukatutosa tena bosi, kesho tunakuja kuchukua pesa
zetu....tutakuwa tumeshamaliza kazi...tunasubiria muda muafaka, kama umebadili
nia utuambie haraka, maana muda ukifika hakuna kurudi nyuma...na ukighairi bado
kuna gharama zetu ni lazima utulipe..’akasema
Mimi pale sikusema kitu!
Tuendelee na kisa chetu
**************
Wakati naendesha gari, kurudi nyumbani kwangu, nilianza kuwaza
hicho niichokusudia kifanyike, hapo hapo huruma ikaanza kunijia, nikikumbuka
jinsi gani nilivyohadithiwa na mmoja wa watu waliowahi kushuhudia ndugu yao
aliyewahi kufanyiwa hivyo, ni ukatili wa hali ya juu, alisema ndugu yao
alishindwa kuvumilia, haikupita muda ndugu yao huyo akajiua.
‘Ina maana mimi nimekuwa na roho mbaya kiasi hicho, japokuwa
rafiki yangu amenifanyia huo ubaya, lakini sio vyema, kumtendea hayo, huo
utakuwa ni ukatili wa hali ya juu, mbona nimechukua mambo kihasira zaidi, ina
maana ubaya nalipiza kwa ubaya wa kiasi hicho, ..kwanza huyo ni mama mtoto ,
analea, je hicho kitoto kitalelewa nani...’nikajiuliza
‘Ndio labda, nitamchukua mimi, na kumlea kama mtoto
wangu,....lakini kila nitakapomuona huyo mtoto nitakumbuka huo ukatili...mmh,
hapana...lazima nifikiriz zaidi hili...’nikawa nawaza kichwani huku naelekea
kwangu na muda unazidi kwenda.
Kabla sijafika nyumbani ndio nikakumbuka mazungumzo yangu na
rafiki yangu huyo tukiwa ndani ya gari;
'Vipi khali ya mtoto, mbona amekuwa mzungu, umemfanya nini
mtoto...?' nikamuuliza nilipotupia jicho kwa mtoto, na haraka akamfunika
'Ni fasheni tu, na kuogopa vijicho cya watu...'akasema
'Siku hizi umekuwa mshirikina..?' nikauliza
'Sio wa kikwetu, huo ni wa kitaalamu, ...sitaki watu wamfahamu
mtoto wangu alivyo, najua fitina ni nyingi sana, ambazo hazina
ukweli...'akasema
'Zina ukweli, ila unauogopa huo ukweli, au sio, kwa vile umevuka
mpaka..'nikasema
'Sawa...nitasema nini tena..ila kwa vile nimerudi tutamalizana na
wote wanye kutaka ukweli, na sina shaka juu ya hilo...'akasema
'Haya, ila jiandae pia kuachana na huyo mtoto..'nikasema
'Kwanini...?' akauliza
'Unajua ni kwanini, ahadi ni deni, nilishawahi kukuambia kabla,
kuwa dhamira yangu ni ile ile..'nikasema
'Sijakuelewa...'akasema
'Utaelewa tu muda ukifika, sizani kama wewe ni jasiri kiasi hicho,
wapo mjasiri lakini walishindwa, ogopa sana macho ya watu, ogopa sana watu
wakikunyoshea vidole kwa kashafa ya udalilishwaji..'nikasema
‘Huyu mtoto ndiye jicho langu, sitakubali kuachana naye hata siku
moja, na hao watakaotaka kufanya hilo, wajiandae pia, maana mimi sio yule wa
jana...’alisema kwa kujiamini
'Hahaha, ina maana unajiamini kiasi hicho,..hata baada ya hayo
madhambi, badala ya kutubu, ..'nikasema
'Sawa nilitenda madhambi, lakini kwa misingi ya kukubaliana,
sikujipeleka mwenyewe, sikulazimisha, na huenda yaliyotokea yalikuwa sio lengo
langu, ..lakini ufanyeje na imeshatokea, muhimu ni huyu kiumbe asiye na hatia,
nitampigania hadi tone la mwisho..'akasema
‘Hivi hata kama baba yake akimtaka, akaishi naye, kwani labda
utakwua kwenye hali mbaya, utamkatalia?’ nikamuuliza.
‘Kwa misingi ipi, kwani mimi nimekufa, au sina uwezi wa kumlea..na
hali mbaya gani hiyo ya kunifanya nishindwe kumlea mtoto wangu...hapana hilo
halipo..’akasema.
‘Baba yake ana haki na mtoto wake pia au sio...’nikasema.
‘Hata mimi nina haki na mtoto wangu, hilo sikubaliani nalo hata
siku moja, kwasabbu mimi mwenyewe nina uwezo wa kumlea, kwanini huyo anayejiita
baba aje kumdai mtoto wangu, kwani tuliahidiana hivyo, sikuahidiana na mtu kuwa
tuzae halafu mtoto awe wetu sote, hali halipo...’akasema.
‘Lakini wakija na hoja kuwa wanamtaka huyo mtoto, wamlee,
ikizingatiwa kuwa huyo baba mtoto ana mke wake, na mke wake yupo tayari kuishi
na huyo mtoto, utakataa?’ nikamuuliza.
‘Kwanini lakini...sijasema siwezi kumlea mtoto wangu,...aah, hebu
kwanza maana nina mengi ya kufikiria, nimesharudi nahitajia muda wa kutafakari
mengi kabla sijaanza kupambana na uhalisia, najua hata wewe unanihitajia sana
...lakini naomba muda kidogo...'akasema
'Muda utaupata tu...na huenda ukiwa umelala kitandani,
hujiwezi,...'nikasema
'Mhh...maneno yako yananitisha sana...'akasema
'Dada yangu, bosi wangu...mimi sina cha kuongea kwa leo,
sikujiandaa kwa hilo,.ila kwa hilo la mtoto na huyo anayejiita baba yake, kauli
yangu ipo wazi, kuwa huyu mtoto sitaachana naye kamwe,labda mimi niwe
maiti...’akasema.
‘Hujaniambia kwa kauli yako ni nani baba wa huyo mtoto ni
nani,...?' nikamuuliza
'Kifupi hana baba...'akasema
'Au unaogopa kwa vile ni mume wangu kama inavyojulikana na wengi,
maana nimeshayafahamu yoye hayo, na wapi mlipokuwa mkikitania?’ nikamuuliza
‘Waache watu waseme wapendavyo, lakini anayefahamu ukweli wa yote
ni mimi mwenyewe, na ukweli huo hautabadilika kwa maneno ya watu..kwa vile hata
mimi nina ushahidi wa kitaaamu, nina kila namna ya kujilinda..'akasema
'Ushahidi gani zaidi ya DNA, au umegushi hata hiyo, hata ukigushi
tutapima tena na tena..'nikasema
'Kwanini tufanye hivyo, nikitaka nini sasa....?' akauliza
'Mume wangu anamuhitajia mtoto wake, ..hapo alipo hana amani, na
ikizingatiwa ni mtoto wa kiume, anamuota na kuchanganyikiwa kwa ajili hiyo,
hujui jinsi ani mume wangu aliposikia una mtoto wake wa kiume
alivyofurahia...'nikasema
'Huyo shemeji, akiwa hivyo basi hana akili...'akasema
'Kwanini...?' nikauliza
'Wewe hujui jinsi gani niivyotaabika na huyo mume wako, hujui tu,
vinginevyo angeliishia kutembea na changudoa, lakini nilimsitiri, na kumlinda
ili aendelee kuitunza ndoa yake, lakini hayo hutanielewa kwa sasa nitakuja
kukusimulia yote, nipe muda nipumzish kichwa, na kukusanya ushahidi
wote..’akasema
‘Hahaha, yaani unajisifia kuwa uliweza kuhangaika naye, kuzini na
mume wa mtu huoni ni kosa kubwa, au ulimsitirije...?' nikauliza
'Nitakuja kukuelezea...'akasema
'Vyovyote iwavyo, zinaa, na kutembea na mume wa mtu ni dhambi
kweli si kweli..?' nikauliza
'Uliyajua hayo sio..sasa hivi unayajua hayo, umesahau eeh...kuwa
wewe ndiye uliyenishauri nikazini, nitembee na hata mume wa mtu...'akasema kwa
hasira.
'Hahaha...kwahiyo ukataka kunikomoa, au sio...na hata wakati
nakushauri hivyo mlishakuwa na mahusioano wewe ulitaka upate mwanya tu wa
kuyafanikisha hayo, mimi sikujua lengo lako ni nini,..na ushahidi
upo...'nikasema
'Mhh..kichwa kimechoka jamani..'akasema
'Utapumzika tu..japo sijui., sasa kwa kumbukumbu maana huenda huko
tunapokwenda tunaweza tusipate muda wa kuongea hivi tena, hebu niambie huo
mkataba wa bandia mlioutengeneza, na Marehemu, lengo lenu ilikuwa ni nini,
kulinda haki za mtoto, au kutaka mali, angalia mwenzko alikuwa na tamaa hiyo
sasa yupo wapi..?’ nikamuuliza
‘Mimi sijui lolote kuhusu huo mkataba, hayo ni ya kwao, mimi nina
maisha yangu ya kujitegemea mimi mwenyewe sijawa kilema,..ni wao tu
walinilazimsha kuweka sahihi, na wakati kaam ule sikuwa na jinsi,na sijakaa na
kuliwazia hio...'akasema
'Sasa unavyosema kuwa una kila namna ya kujilinda una maana
gani..?' nikauliza
'Mimi nazungumza maswala ya kitaalamu, kuhusu mtoto wangu,...kuwa
hana baba,kama wanavyodai watu, na nitalithibistiha hilo hata mbele ya
mahakama, huyu ni mtoto wangu mwenyewe....’akasema
‘Kwa vipi,...huwezi kuzaa mwenyewe, hukupandikizwa mbegu, wewe
ulizini na waume za watu, ndio ukazaa, na huyo mwanaume ni mume wangu, hata
kama ulizini na wengine, lakini aliyewezesha wewe kupata mimba ni mume wangu,
kwei si kweli...?’ nikamuuiza.
‘Kuzini ni kitu kingine, wangapi wanazini na hawapati
mimba,...sitaki kuyaongelea hayo zaidi maana hutanielewa, maana kwa hivi sasa
huwezi hata kukumbuka kuwa wewe ndiye uliyekuwa mshauri wangu mkuu, mimi sikuwa
na wazo hilo kabla, sikuwa na tabia ya kutembea na waume za watu
kabla,..'akasema
'Hahaha, hiyo ni kauli ya kujitetea, wakati mlikuwa mkikutana kwa
rafiki yako, ndio ilikuwa makao makuu yenu, mkisingizia mnaongea mambo ya kikazi,
au umesahau,...'nikasema
'Haina ukweli kabisa hiyo,..mimi nilianza kutembea na waume za
watu baada ya wewe kunishauri, nafahamu hutanielewa, na sina njia nyingine ya
kukuelewesha, kwasasa,...sina zaidi, naomba tusiongee, tutakuja kuyaongea siku
nyingine....’akasema
‘Hamna shida...lakini kiukwei, sitakuja kukuelewa kamwe, mimi
siwezi nikawa mjinga kiasi hicho, eti nikushauri ukazini na mume wangu halafu,
halafu kitendo hicho hujafanya mara moja, ungelisingizia kuwa ni bahati mbaye,
mlikuwa mumelewa, kumbe kila siku ndio ilikuwa kazi yenu...’nikasema.
‘Wewe hujui tu, ...usilolijua ni sawa na usiku wa giza,
...’akasema.
‘Ndio siwezi kukuelewa, hakuna sababu ya msingi ya kuzini na mume
wa mtu, tena mume wa rafiki yako, rafiki yako unayemtambua kama dada yako,
anayekuamini..mpaka sasa akili yangu inashindwa kuamini kama kweli wewe
ulifanya hivyo,huna sababu ya kusamehewa, ..’nikasema na kumwangalia,
alikuwa kakunja uso na kushika kichwa kuonyesha kukerwa na hayo ninayoongea.
‘Naomba tuyaache hayo mazungumzo dada maana hayana
ukweli..yananitesa sana moyo wangu, na kwa vile, nimesharudi ngoja nipate muda,
nitakuambia ukweli ulivyokuwa,..lakini kwa sasa naomba uniache, sina cha
kuongea zaidi...’akasema
‘Haya mimi naisubiri hiyo siku kwa hamu, maana umeshaniahidi mara
nyingi kuwa utaniambia, sasa umerudi, sasa utausema hata ukiwa hao
kitandani,...nataka kusikia huo utumbo wako, wa kujiidhinishia madhambi yenu,
mimi nilichotaka ni kauli yako tu, kuwa kweli ulizini na mume wangu, ungeisema
hapa, ningeshamalizana na wewe,...'unasikia
'Sawa nimesikia, na siwezi kusema uwongo..'akasema
'Ilimradi umekubali kuwa ulizini na mume wangu, hiyo inatosha...
inatosha kabisa...asante sana.’nikasema
'Sijakubaliana na hilo..lakini subiria...'akasema na mimi nikaka
kimiya,kwani hata mimi niikuwa na mawazo yangu kichwani, na hasira nilizokuwa
nazo zilikuwa kubwa sana, kwahiyo tukawa tupo kimiya hadi tunafika.
*******
‘Je ni haki kumufanyia huyo mama wa mtoto hayo ninayotaka
kuyafanya, akili yangu hakukubaliana na huo uamuzi, niliingiwa na
wasiwasi, nikawa na mawazo mengine kuwa niwazuie wasiendelee na hilo zoezi,
kwani kama walivyosema, vitendo watakavyomfanyia vinaweza kumuua, na hata kama
hatakufa hapo, lakini anaweza kuja kujiua mwenyewe
Nikaamua kuwapigia simu ili wasitishe hilo zoezi, lakini simu zao
zikawa hazipatikani, nikaamua kumpigia simu huyo rafiki yangu, ambaye alipokea
simu yangu halafu aliposikia sauti yangu, akakata simu.
Muda ukawa unakwenda na na sikujua kabisa nifanye nini, maana muda
huo ni usiku, na nisingeliweza kurudi kule kwa rafiki yangu, mara simu ikalia,
nilipoangalia mpigaji nikaona ni baba yangu;
‘Baba mbona simu usiku-usiku..?’ nikauliza baada ya kusalimia
‘Je kikao cha kesho kipo , kama ulivyotaka?’ akaniuliza
‘Ndio baba nimeamua iwe hivyo, ..’nikasema, maana nilipanga kuwa ,
tuwe na kikao cha pamoja, kikiwahusisha wazazi wangu. Niitaka kikao hicho kiwe
cha hitimisho ya hayo yote, ili hukumu itolewe na kila aliyehusika awajibike.
‘Basi itakuwa vizuri, na uwe na ushaidi wote, kwani sisi
hatutaweza kuvumilia hayo yanayotokea kwenye familia yako, nilishakuambia kuwa
mimi sitaki kashifa, sasa hicho kinachoendelea hapo kwenu kinaniharibia jina
langu...unalifahamu hilo, na mpinzani wangu wa kisiasa anazidi kuwa juu
yangu,..nikikosa kuchaguliwa safari hii, sitawasamehe..je una kila kitu?’akaniuliza
‘Kwanini unasema hivyo baba, kwani kuna nini kimetokea huko kwako…kwasabau
hayo yote hayana ukweli, zaidi ya kashfa za kupandikiziwa?’ nikamuuliza
‘Jana Askari walifika hapa kwangu na kunihoji, ...wanahisi kuna
uwezekano mkubwa kuwa mume wako kahusika kwenye mauaji ya Makabrasha, na wanayo
ushahid wa kutosha, na kwanini waje kwangu badala ya kumkabili mume wako,
unaona jinsi wanavyopanga mambo..’akasema
‘Na hapo najiuliza kwanini waje kwako, ungewauliza na kuwaambia
utalichukulia kisheria zaidi ili waogope..?’ nikauliza
‘Kwasababu wanatumiwa na mpinzani wangu, sio kwa kuwatuma lakini
mpinzani wangu anapandikiza fitina na askari kadi yao ni kuhakika ukweli,..na
zaidi wameniuliza mahusiano ya kampuni
zangu za zako, na kwanini kulionekana mikataba miwili..’akasema
‘Mikataba gani baba, hayo yanakuhusu vipi..?’ nikauliza
‘Yananihusu kwa vile nina hisa kwenye kampuni zenu, na kuna
mikataba kama hiyo ya kuuza hisa kwa watu wengine mimi nina maoni gani kama
mmoja wa wenye hisa..ni aswali ya mitego…’akasema
‘Kwahiyo umewarizisha kwa majibu..?’ nikauliza
‘Kuwarizisha kisiasa sio tatizo kwangu, tatizo ni huo mtego wa
mpinzani wangu alikuwa na malengo gani,..na muhimu kwetu ni kuhakiksha tupo
safi, familia ipo na mashirikiano manzuri, na isitokee kashafa nyingine tena…umenielewa..’akasema
Baba aliposema hivyo nikakumbuka hilo nililopanga litokee kwa
rafiki yangu, linaweza kuleta kashfa mbaya kwenye familia na inaweza ikawa ni
chanzo cha waandidhi kudadisi…oh, sasa nimefanya nini, nilitamani nikate simu,
nianende kufuatilia hilo.
‘Swali jingine ambalo linawatia shaka, ni kwanini mume wako
akamchuku amakabrasha kama wakili wake na ilihali tunatambua tabia ya huyo
wakili, na kwanini kuna mikataba miwili ya familia yenu, je huo mkataba mpya ulitayarishwa lini na
kwanini mkampa hiyo kazi Makabrasha, wakati mnamfahamu tabia yake?’ akauliza
‘Baba hilo ni moja ya jambo tutakaloliongea kesho, kuna mengi
yamefanyika, nakubali hilo, na nimeamua kesho niyaweka yote wazi,, ili
kijulikane kimoja, mume wangu hajambo, na anaweza kujieleza, na lolote linaweza
kutokea, sijaamua ni nini cha kufanya baada ya hapo, ukizingatia kuwa mume
wangu hajawa na afya ya kutosha, inabidi nitimize wajibu wangu kama mke
wake..’nikasema
‘Hujaamua la kufanya hadi sasa, wakati unaishi na mtu anayeweza
ku-kuua, kwa ajili ya mali zako, wewe hulioni hilo, kama wamefikia hatua ya
kubadili mikataba ya halali...na katika harakati zao, inaonekana walishindwana,
wakauana. Huoni kuwa mkono ukionja damu, inakuwa kama muonja asali, hajali tena
kufanya maasi,....hilo sisi hatutalikubali, kama wazazi tutachukua hatua
...’akasema.
‘Baba nafahamu, mnavyojisikia ...lakini...’nikataka kujitetea
lakini baba hakukubai kunipa nafasi , akasema;
‘Sitaki kusikia jambo jingine la kupinga maamuzi yangu, kama
unanikubali mimi kuwa ni baba yako, kama unamkubali mama yako, basi itabidi
ukubaliane na sisi, ....wewe huoni, wameamua kumuua,mtu wao wanayemuamini, na
kumtambua kama sehemu ya famiia yao, kwa ajili ya kuficha ukweli, unafikiri
watakuwa na huruma na wewe, binti yangu nilishakuambia huyo mume hakufai, mbona
unatuweka roho juu...’akasema
‘Baba nilishawaambia mambo yangu nitajua jinsi gani ya kuyatatua,
mwenyewe...niachieni,kwanza, nifanye nijuavyo mimi, ...msikimbilie kuchukua
maamuzi yenu kwanza,kesho nimewaomba ili muweze kusikia maamuzi yangu, ambayo
yatakuwa ni maamuzi yenye muafaka wa kudumu, nimesema sijafikia uamuazi bado,
lakini mpaka kesho nitakuwa nimeshaamua ni nini cha kufanya, kwani kuna mambo
ambayo nilikuwa nayamalizia...’nikasema.
‘Ulikuwa unamsubiria mpelelezi wako, ambaye
keshakusaliti,...usimwamini huyo binti, kesharubuniwa, na kwasababu ya mali
..kwasababu ya tamaa, na kwa vile ana mahusiano na mume wako hatajali lolote
itakao tokea kwako....anakufahamu udhaifu wako, anafahamu siri za kwako za nje
na ndani, kwahiyo hatasita kukufanyia lolote baya....’akasema.
‘Baba huyo nimeshamweka sawa, hana lolote kwangu,
nimeshamfahamu,...’nikasema
‘Sisi kama wazazi, tumeshafikia uamuzi, sisi kama wazazi,
kesho tutatoa maamuzi yetu,kwa masilahi ya familia kuu, hili siwezi kulivumilia
tena, na tuijaribu kuongea na mume wako, tuone lipi jema kwa hayo yote, asing’ang’anie
ndoa tu wakati haiwezi, hivi karibu nikiongea naye ananijibu kama sio yule mkwe
ninayemfahamu tena, kwanini kabadilika hivyo, wameshajua kuwa wamekuweka
mkononi mwao, ....’akasema.
‘Baba kwanini mnaongea na huyo mtu wakati yupo kwenye
matibabu,...hamuoni kuwa mtakiuka makubaiano yangu na yeye.....’nikasema.
‘Mume wako alishapona, na hayo yaliyotokea baada ya yeye kupona,
ni moja ya mbinu zao, sisi hilo tulishaiona, na tumeshaongea na dakitari wake,
na ingawaje dakitari wake anamtetea, lakini tuna uhakika kuwa mume wako
anafanya hivyo makusudi, ili kufanikisha maengo yake na sio malengo yake, yeye
anatumiwana mpinzani wangu bila hata ya yeye kulifahamu hilo...’akasema
‘Baba naombeni mniachie nifanye jinsi nionavyo
mimi,...nisingelipenda nyie muingilie kati kwenye maamuzi, kwani mimi sijashindwa
bado..’nikasema nikiangalia saa yangu
‘Ushindwe mara ngapi, kama umekubali, mume wako awe na nyumba
ndogo, umekubai mume wako, azae nje, hujashindwa hapo. Hilo lilikuwa ni jukumu
lako kubwa sana kuhakikisha kuwa mume wako anakuwa na utulivu wa ndani,
....hukuweza kulifanya hilo, na huo unaonyesha udhaifu, niambie kuhusu watoto
wa mume wako ....au unafikiri sisi hatufahamu hilo?’ akaniuliza
‘Watoto!! Watoto….?? watoto gani wa mume wangu,?!’ nikauliza kwa
mshangao
‘Unaniuliza, wakati sasa hivi umesema kuwa mambo yako utayaongoza
mwenyewe, ..hufahamu kuwa mume wako ana watoto nje..huoni athari zake, wewe
unalichukulia kawaida tu, hiyo ndio adabu tuliyokufundisha, huoni hiyo ni aibu
kwenye familia yetu,…’akasema
‘Baba mimi nimesikia tetesi za mtoto lakini sio watoto..’nikasema
‘Mhh,. Halafu unajifanya kuwa unaweza kujimudu mwenyewe, hivi
unatuweka wapi sisi,..hebu angalia maisha ya mbele, hao watoto, watakuja
kujitokeza na madai yasiyoeleweka, watakuja kugombana na wenzao, ...maana kwa
hivi sasa hamuwatambui, mpaka mmoja wenu afariki,..ndivyo ilivyo, ni heri
wangejitokeza muda huu, mkiwa hai, ili mjue ni nini cha kufanya, haya
tulikukanya, tunaifahamu sana hiyo familia...’akasema
‘Baba hili nimeligundua, lakini nijuavyo mimi , mtoto wa nje ni mmoja
tu, huyo wa pili sio kweli’ nikasema.
‘Huyo wa pili sio kweli, ni yupi wa kweli na yupi sio wa kweli?’
akaniuliza na mimi hapo sikuwa na uhakika wa kumuelezea nikasema.
‘Baba yupo mtoto namfahamu,...japokuwa mume wangu hajanikubalia,
na hata huyo mzazi mwenzake hajakubali lakini ushahidi wake kwa hivi sasa upo
wazi, hawezi kuliping ahilo tena...’nikasema
‘Mimi nina ushahidi, ana watoto wawili,...unamkumbuka yule mfanyakazi
wenu wa ndani aliyeondoka hapo bila kuaga,ulifuatilia ukajua ni kwanini
aliondoka bila kuaga,...hujui kuwa aliondoka kwa shinikizo la mume wako…?’
akauliza
‘Mhh…mbona sina habari hizo..’nikasema
‘Ndio sasa tunakuambia..mume wako anaweza hata kutembea na mdogo
wako kama mtaishi naye hapo nyumbani,…, ilikuwa siri yao wawili, huyo binti
aliondoka akiwa mja mzito, na mume wako anafahamu, akawa anamtumia pesa
za matumizi huko huko kwa siri, alijifungua, mtoto wa kiume, wanafanana na mume
wako kama mapacha...’akasema
‘Mhh, hilo kwangu ni jipya, sikuwahi kulisikia, nitamuuliza mume
wangu na ikibidi nitamtafuta huyo binti ii niweze kuhakikisha ...na kesho hayo
yote yatajulikana, na ingekuwa vyema huyo msichana awepo kwenye hicho kikao,
..nyie mlipata wapi hiyo taarifa?’ nikamuuliza
‘Sio kwamba tumesikia, huyo msichana yupo hapa kwangu, alikuja
kulalamika, kwasababu tangu mume wako aanze kuumwa hajatumiwa pesa za matumizi,
na ilikuwa bahati tu kumpata, na sisi ikabidi tumchukue aje hapa kwetu, alikuwa
mbioni kuja hapo kwako, tumelifanya hilo ili kuepusha kashifa zaidi…, sasa hili
halina siri tena, unafikiri wewe utachukua hatua gani, ili hii hali isifike kwa
hawa wadaku...’akasema
‘Oh,..baba naona unipe muda niweze kulfikiria hilo,,imekuwa ni
mshtuko kwangu,…kiukweli siwezi kuvumilia tena....’nikasema nikiwa nimeingiwa
na wasiwasi, kumbe namuhukumu mtu mmoja, na huyo je atahukumiwa na nani, na je
ni hawo wawii peke yao....
‘Huna haja ya kuumiza kichwa, nashukuru kusikia kuwa umeshaupata
huo mkataba wenu wa hiari, kati yako na mume wako,...nimeupenda, na ni vyema
sasa ukachukua hatua kama mivyokubaliana, na kama utashindwa kuchukua hatua,
ujue wewe huwezi kujiendesha wewe mwenyewe...huo ndio mtihani wako, sisi
tumeshachukua maamuzi yetu,....’akasema
‘Baba naomba nipumzike, maana akili yangu haipo sawa...’nikasema
‘Haya usiku mwema,..lakini uwe makini, usije ukachukulia hasira,
ukatenda mambo kama mtu asiyesoma, ujue kuna sheria,..ujue ni kitu gani unachotakiwa
ukifanye kama msomi, unasikia, usije
ukatenda mambo kama watu wengine, ...ukiharibu , sisi hatutakubali...’akasema
‘Sawa baba....’nikasema
Nikachukua simu yangu na kumpigia rafiki yangu, akawa hapatikani,
nikajaribu kuwapigia hawo watu niliowapa hiyo kazi, na wao wakawa
hawapatikani...sikukubali, nikatoka nje, na kuingia kwenye gari, sikuwa na muda
wa kuongea na mlinzi, nikalitoa gari, na wakati nataka kutoka mlinzi akaja
kunisalimia
‘Bosi unatoka?’ akaniuliza
‘Ndio kuna kazi nafuatilia, je mambo yapo sawa?’ nikamuuliza
‘Yapo sawa...’akasema lakini nilimuona kama alitoka kulala..
Wakati nimeshafika barabarani, nikahisi kuna mtu nyuma yangu,
ndani ya gari, na kabla sijaweka gari sawa, sauti ikasema;
‘Fuata maelekezo yetu, la sivyo, tutakufanya kitu kibaya..’sauti
nzito ya kiume ikasema na nikahisi kitu kikali kikigusa ngozi yangu, nikahisi
kuwa ni kisu....
NB; Kulikoni...
WAZO LA LEO:Ushauri
wa wazazi ni muhimu sana, tunaposhauriwa na wazazi wetu tujaribu kuwasikiliza,
hata kama tunajiona tuna uwezo zaidi yao wa kihali na mali, tujue kuwa wao
wameona mengi zaidi yako, na wamepitia maisha ambayo wewe hujawahi kuyapitia,
hekima zao zinaona mbali zaidi, tuwasikilize, tukae pamoja nao, tuone je mawazo
yao na mawazo yetu yanaweza kufikia muafaka wenye manufaa, tusichukulie ubabe
kwa vie tunazo, tumesoma sana, nk.
Hata hivyo, na wazazi nao wanahitajika kuwasikiliza watoto wao,
wasikie mawazo yao, kwani huenda kwa elimu yao mpya, na upeo wao wa
kuchanganyika na watu wanaweza wakaja na njia mbadala,...hii ni kwa nia njema,
kwani maafa yakitokea ni athari za pande zote.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment