‘Nimekuelewa sana dada yangu, nakushukuru kwa ushauri
wako,...lakini. eeh…’nikasita maana niliona kama gari linaingia getini, halafu
nikasema
‘Hayo ya mume wangu,..najua mnampenda na kumthamini sana, lakini
nawaombeni hayo mniachie mimi mwenyewe…’nikasema na sasa geti likawa
linafunguliwa, lilikuwa gari la mume wangu.
‘Oh wamerudi na kunikuta tena hapa, mimi naondoka…’akasema
‘Kwanini haraka hivyo…hatujamalizana …’nikasema
Na kabla hajajibu mume wangu akateremka kwenye gari, na wakili
wake,…na walipoteremka, badala ya kuelekea ndani, wakawa wanakuja pale
tulipokuwa tumekaa, na ikabidi tukatizie mazungumzo yetu.
Tuendelee na kisa chetu.....
‘Aheri bado mpo..nahisi hili litatufurahisha sote,…maana shemeji
yangu upo, na…na mke wangu ..unajua leo kutwa nzima tumekuwa tukilihangaikia
hili,…kutafuta haki, ..na haki haiji hivi hivi wakati mwingine au sio..’akasema
mume wangu na kumuangalia wakili wake ambaye alitikisa kichwa kukubaliana na
yeye.
‘Sasa hivi tumetokea polisi, kumuona Yule mpelelezi
anyeshughulikia hii kesi yako ..mke wangu mambo sasa yanakwenda vizuri
tu..imebakia maswala machache,..si unajua tena nchi yeu ilivyo…’akasema na
kumuangalia wakili wake.
‘Kwanini…maana haya yapo mikononi mwao, na tulikubaliana kuwa
hakuna haja ya kuwafuatilia, tuwaachie wao wafanye kazi yao…’nikasema
‘Ndio hivyo mke wangu, lakini ni wajibu wangu, eeh, na wakili hapa
kulifuatilia hilo, kuhakikisha kuwa, mke wangu upo na amani, haiwezekani watu
wakushuku tu, haiwezekani mtu auwawe tu, na sisi tubakie kimia, ni kwanini
…eeh, Yule alikuwa ni rafiki yangu mkubwa..hapana mimi sitakubali kukaa kimia
mpaka haki ipatikane…’akasema
‘Ok, kwahiyo…?’ nikauliza, na sasa wakili ndiye akaanza kuongea.
‘Kifupi ni kuwa polisi wanasema bado wanalifanyia kazi, lakini kwa
kuhusu wewe kama mshukiwa muhimu, halipo tena,…’akasema
‘Kabisa…kazi nzuri ya wakili wetu…’akasema mume wangu.
‘Lakini hata hivyo kabrasha la kesi halijafungwa, si unajua tena
mambo ya kisheria, kuna taratibu zinatakiwa kufutwa, ..na hilo ndilo tulikuwa
tunalifuatilia, ili kuhakikisha kuwa gabrasha hilo limefungwa..na wewe utakuwa
huru kabisa…’akasema
‘Lakini mimi nina wakili wangu analifanyia kazi hilo…’nikasema
‘Haina shida, yeye afanye kivyake na sisi kivyetu,..lengo letu ni
moja, na mwisho wa siku tutakaa pamoja…na kuona kila mmoja kafikia wapi, muhimu
ni kuhakikisha kuwa kesi hii haipo tena, ..lakini wkati huo huo, haki
imetendeka, na muuaji kapatikana…maana aliyefariki ni jamaa yetu..’akasema
wakili.
‘Sawa nashukuru …’nikasema
‘Sasa tatizo mke wangu, kila kitu ni gharama au sio..na unajua
hali niliyo nayo, nakwama kabisa, nilikuwa naomba…tukaongee ndani, unipitishie
hundi yangu..’akasema
‘Hundi ya malipo gani…?’ nikauliza
‘Ya wakili, na kufuatilia..na mambo mengine ya kikazi..ni pesa
nyingi kidogo, na sitaweza kupitisha hundi hiyo kwa sahihi yangu tu..’akasema
‘Naomba hilo tutaliongea baadae..’nikasema
‘Ni muhimu na haraka kuna mambo mengine nayafuatilia,…’akasema
‘Mume wangu tulishaliongea hilo, mimi siwezi kuweka sahihi yangu
…kwa kazi yoyote ya ushirika, hasa za makampuni, mpaja swala langu litatuliwe,
hilo lipo wazi, kwahiyo kama ni hundi ya namna hayo, samahani sana…’nikasema
‘Mke wangu hili ni la muhimu sana, tunataka tumalizane na kesi
yako,..na haki ya marehemu ipatikane,..ina maana wewe huna uchungu na hilo..na
hata kama huna uchungu na hilo,na je wewe hutaki uwe huru…?’ akauliza
‘Nitaongea na wakili wangu…’nikasema sasa nikisimama kutaka kupiga
simu kwa wakili wangu.
‘Wakili wao wa nini sasa haya ni yetu, hayamuhusu…’akasema
‘Wakili wangu ndiye anasimamia kesi ya mkataba..kila jambo kama ni
muhimu yeye ndiye anatakiwa atoe maamuzi ya kisheria, siwezi kulikwepa
hilo…’nikasema na wakili wangu akawa hewani.
‘Vipi umefanya kama nilivyokuambia…?’ akatangulia kuniuliza
‘Kabisa…lakini kuna tatizo hapa, mume wangu kaleta hundi ya
ushirika anasema anataka niweke sahihi yangu..nishauri…’nikasema na kumsikiliza
kwa makini halafu nilipomaliza kuongea naye, nikasema;
‘Kama nilivyosema kila kitu kinachohusu mkataba wangu wa zamani
kitapitia kwa wakili wangu,kwahiyo kama ni ya haraka usubiria anakuja…’nikasema
na hapo mume wangu akamgeuikia mwenzake na kusema
‘Twende zetu…’akamshika mkono na wakaanza kuondoka.
‘Vipi tena…?’ nikauliza lakini hawakunijibu kitu haoo, wakaingia
kwenye gari na kuondoka zao.
*********
Yule mama akawa kimia,
nahisi alijifunza jambo hapo, akasimama sasa akitaka kuondoka.
‘Mimi naondoka maana kijana wangu ana mambo mengi ya kufuatilia…’akasema
‘Umeona mwenyewe mambo yalivyo..’nikasema
‘Lakini yatakwisha tu, ila nahisi mume wako ana jambo…ila anaogopa
kukuambia, hebu nikuulize ni nini kikubwa kwenye huo mkataba wenu ..ambacho unahisi
kakivunja,…?’ akaniuliza
‘Siwezi kusema lolote kwa hivi sasa, ..’nikasema na hapo akakaa
tena kwenye kiti na kwa sauti ya chini akaniliza
‘Nilikuuliza kitu, je mume wako akiamua kukuambia ukweli,
utamsamehe?’ akauliza sasa akiangalia saa yake ya mkononi.
‘Hapo mimi sijui, ..kiukweli kachelewa sana kuwa mkweli na zaidi
anazidi kuharibu, na kwahiyo kama ataamua kufany ahivyo, najua kabisa itakuwa
ni kutokana na kushawishiwa, au kwa vile kaona kakwama…’nikasema
‘Nimekuelewa sana dada, ila
nauliza hivyo maana ndoa ni mashikamano ya mume na mke, na kila mmoja anawajibika
kuitii ndoa yake, lakini ni lazima mfike sehemu myamalize au sio…’akasema.
‘Ni kweli yataisha tu, lakini kuisha kwake ni baada y akuupata huo
mkataba wa zamani, tukae tuona unaemaje, na yeye akiri makosa yake, ..mengine
yatafuta baada ya hapo…
‘Nakuelewa sana mdogo wangu,...unajua kuna makosa madogo madogo
tunayoyafanya sisi wanandoa hasa wa kike, tunaona ni sahihi au ni madogo tu,
kwa namna yetu, kumbe kwa wenzetu ni tatizo kwao, na wao kwa uwezo wao wanaweza
kufanya jambo, na matokea yake kuna leta matatizo, na ushukuru wewe una uwezo
wako…’akasimama sasa akitaka kuondoka
‘Nafahamu hilo,najua hata mimi nina makosa yangu, lakini sio ya
kuvunja mkataba ..maana ni mambo ya kuelezana, kama nilikosea,
angeniambia,..usitetee hilo…sawa tulikuwa tunahangaika na majukumu ya kazi, na
mambo mengine yakawa kama hayana msingi, lakini je hayo ndio yafanye mtu
aka…hapana…’nikasema. ‘Ndio awali nikakuambia kuwa sisi wanawake tuna dhima ya
kuwalea wanaume wakati mwingine kama watoto wetu,…sina nia mbaya hapa…’akatulia
kama anawaza jambo.
‘Mfano nikuulize hivi ukiwa unamlisha mtoto wako vyema, akanisha
vyema anaweza kwenda kuomba chakula kwa jirani…?’ akaniuliza
‘Una maana gani…?’ nikamuuliza
‘Nijibu tu…’akasema
‘Hawezi…’nikasema
‘Basi ndio hivyo, wakati mwingine tunaweza kuwanyima watoto wetu,
eeh, unanielewa hapo, chakula,..haki yake, ikafikia akazidiwa, sasa akienda
kuom,ba chakula kwa jirani, utamlaumu nani…hahaha…’akasema na kucheka.
‘Sijawahi kufanya hivyo…labda …hapana, unajua hayo ni maswala ya
kuambiana, kwani mimi si mke wake, kwanini aogope kuniambia…ana njaa…’nikasema
‘Haahaha..tuyaache hayo..ila yakitokea haya ndio tunapata
fundisho, mimi nitashukuru sana mkilimaliza hili kwa amani, na sitafurahi kama
mtaishia kubaya, haya juhudi yetu itakuwa haina maana…’akasema
'Msimamo wangu upo wazi, …sifanyi kwa nia mbaya, lakini ikifikia
huko, nitafanyaje, je kama ndio imeanza hivyo, huko mbele itakuwaje, sasa hivi
kaanza kuandikisha watoto wa nje, je mama wa hao watoto ana dhamira gani,…ni
lazima niwe makini hapo…’nikasema
‘Ninachoweza kusema kwa msameheane, wewe ulivyo,....hutapoteza
kitu hapo au sio, bado una nafasi ya kuendelea na ..na kampuni yako,…nasema
hivyo sio kwavile na mtetea shemeji yangu, hapana…’akasema
‘Mhh…unajishuku dada…’nikasema
‘Pamoja na hayo, mimi namfahamu sehemu nyingina ya tabia yake…kila
mtu ana hulka lakini kuna hulka hujificha,..yeye ni mwanaume mwema sana, akimpta
mtu wa kumjua alivyo, ana huruma sana kwa watu, japokuwa katokea kizazi cha
tabia hizo zisizopendeza watu, na mengine ni shida tu..watu hawajapenda wawe
hivyo.....’akasema.
‘Nimekuelewa….ngoja tuone ..’nikasema
‘Sasa mimi naondoka tuonane lini sasa…nafahamu kuna maswala hayo
ya mawakili, wanafanya kazi zao, naona wanakipizana huku na kule,.. hata hivyo
ni lazima maisha yaendelee, naopmba tuje tukae tuongee tuone maisha
yanakwendaje, …haya yanayotokea sasa yasitufanye kusimamisha mambo mengine, naomba
nije tusaidiane mawazo ya maendeleo…’akasema
‘Sawa kwa hilo tu, hamna shida kabisa, tupo pamoja…’nikasema
‘Na kwa hili je…?’ akauliza sasa akinyosha mkono wa kuagana.
‘Hahaha, dada hujanielewa mpaka hapo…niakuambie kitu, baada
ya wiki mimi nitawapatia jibu langu,…kuhusu hili…kwa hivi sasa niacheni
nipambane na mume wangu.....’nikasema na kikunja uso wangu kuashiria dhamira ya
kweli.
‘Mhh, baada ya wiki sio sawa, basi ngoja waupitie huko mkataba
waone wafanyeje, hayo ni mambo ya kisheria, au sio…?’ akauliza
‘Huo mkataba wa kugushi, ..au?’ nikasema kama nauliza
‘Mhh..mimi sijui sasa…naona kwa hili litaleta utata…na hapo ndio
tunazidi kuchelewa,…namuonea huruma sana kijana wangu…kwani na yeye anachelewa
kuondoka, lakini hawezi kuondoka kabla hili tatizo halijaisha, ya mungu mengi...’akasema.
‘Ninachoweza kukuambia dada, huo mkataba kwangu ni batili, na kama
mtaendelea kuutumia basi msije kunilaumu, itabidi mimi niende mbele ya sheria,
ili haki itendeke…sasa kwa ushauri wangu wa haraka, msubirie baada
ya wiki, au hata kabla ya hapo, kama mume wangu atakuwa tayari kutimiza
masharti yangu, nitawaambia, ni nini cha kufanya..’nikasema
‘Sawa nimekuelewa, nashukuru sana,..’sasa akataka kuondoka na
ghafla akasimama.
‘Mungu wangu sijui kama mliongea na kijana wangu..kuna jambo
limezuka…’akasema sasa akarudi kukaa..
‘Samahani kidogo, ni muhimu kwa kweli…’akasema
‘Jambo gani tena…?’ nikauliza
‘Unajua huku kuzaa ovyo ovyo nje ..mitihani yake ndio hiyo,,..juzi,..kuna
msaidizi wa kijana wangu. Msaidizi katika mambo hayo ya mirathi,… Unajua
marehemu kila kitu alikiacha kwenye maandishi, utafikiri alijua atakufa…ndio
hivyo, usomi nao unasaidia, au sio…si ndio hivyo hata nyie mnakuwa na mikataba
ya ndoa nk..kusoma huko…’akasema
‘Mhh..kuna tatizi gani ..?’ nikauliza
‘Huyo msaidizi wake sasa..ni mtoto wa marehemu mwingine, alizaa na
mwanamke mwingine..na katika maelezo yake kwenye hayo maandishi
aliyoacha,..alitaka huyo kijana atambulikane na awe msaidizi wa kijana wangu,
kila kitu kwenye maandishi tena ya kisheria..unaona hapo..’akasema.
‘Sasa huyu msaidizi wake,…ni tatizo, yeye ni mtoto kama baba,
unanielewa hapo…’akaniangalia
‘Bado sijakuelewa…’nikasema
‘Ni hivi huyo kijana kamlanda baba yake sio kimatendo tu, bali pia
na yeye aliamua kusomea sheria..na ni wakili pia…’akasema
‘Mhh..kwahiyo…’nikasema
‘Na hata tabia za kazi ni kama alivyo baba yake, utafikiri
alimfunza hiyo tabia, si unamuelewa marehemu alivyokuwa, basi mtoto ndio zaidi,
na kiumri hajapitana sana na kijana wangu…’akasema
‘Sawa kwani kuna tatizo gani hapo, sioni tatizo maana sina jambo
na yeye, hayo ni yenu ya kifamilia au sio, au unataka kusema nini hapo…’nikasema
‘Mengi yaliyopitishwa kwenye kikao cha kifamilia yeye alikuwa
mpingaji sana, yeye alitaka kila kitu alichosema marehemu kitekelezwe hasa
kikiwa kwenye maandishi, mkataba…, unajua nilimuambia kijana wangu mapema awe
tayari kwa hili, kwahiyo mambo mengine asiyaweke wazi…’akasema
‘Kwanini sasa na ni haki ya kila mtu au sio, haikuwa na haja y
akuficha jambo…’nikasema
‘Wewe ni mungu tu alituongoza, maana huo mkataba wa kuelezea kuwa
kuna ..hizo kwenye makampuni yenu, haukuwahi kwenye hicho kikao, kijana wangu
alikuja kupewa baadae na kwahiyo hilo halikuzungumzwa siku hiyo..siku hiyo
ilikuwa ni madeni, na watoto hao wa nje waliposikia madeni ni mengi kuliko mali
za kurithi, wakaondoka mmoja mmoja, maana kijana wangu aliwaambia kila mtu
akubali kushika sehemu yake ya deni,…nani akubali hapo, hata huyo msaidizi wake
akaondoka akidai ana kesi anafuatilia...’akasema
‘Kwahiyo…unataka kusema kuwa huo mkataba wa kugushi bado haujafika
kwa warithi, kama huyo ..na wengineo ..ni vizuri, lakini mimi siutambui…’nikasema
‘Sasa huo mkataba halali upo wapi mdogo wangu…’akawa kama anauliza
‘Utapatikana tu dada….mume wangu atakuwa anafahamu upo
wapi…’nikasema
‘Tatizo ni muda..mana sijui kajuaje …huyo mtoto, katupigia simu
akidao kuwa tumemficha ukweli…sasa ni hivi kutokana na muda, kama kijana wangu
akiondoka, kurudi ulaya kabla hatujamalizana na hilo, mtakuja kupambana na huyo
mtoto, ni mkorofi kweli kweli, nina uhakika …hamtaelewana naye, ndio maana
tunataka mambo haya yaishe haraka, iwezekanavyo, wewe kaa na mume wako
myamalize haya mambo kwa haraka jamani, …’akasema
‘Kuisha haraka ni mume wangu…nimeshakuambia hilo, yeye ndiye
anachelewesha haya mambo, kama nyie mnaweza kumshauri fanyeni hivyo, alete
mkataba wa zamani, umenielewa hapo dada…’nikasema
‘Nilivyosikia, huu mkataba uliopo sasa nakala zipo kila mahali
panahusika, sasa sio rahisi mtu kukubaliana na kauli yako, sijui unanielewa
hapo…’akasema
‘Usijali, hilo litafanyiwa kazi..hamna shida …’nikasema
‘Mimi sitaki kubishana kwa hilo, ila ninachotaka kukisema hapa ni
hivi…unajua huyo kijana ni mtata kwa sheria,…anapenda sana kesi, nina uhakika
atawasumbua sana kwa hilo, na kama siku ile huo mkataba ungelifika mikono
mwake, sijui uingekuwaje...’akatulia
‘Dada…’nikataka kusema na yeye akanikatisha, akisema;
‘Sisi kuwa kusaidia hilo, tumesema hatujui, hatuna uhakika,
tutalifuatilia tukiupata basi tutamjulisha, lakini hakukubali, kasema huo
mkataba tunaufahamu tumemficha…...ndio maana tunataka tulimalize hili haraka…’akasema
‘Kwahiyo mlitaka mimi nifanye nini..?’ nikauliza
‘Sisi lengo letu ni kuhakikisha kuwa huo mkataba unafanyiwa kazi,
na kuondolewa kabisa,..mimi kwa ushauri wangu, kubali tu huo mkataba uliopo
halafu tunaongea na wakili sisi kama familia tunajitoa, nyie sasa mtajua
mnafanyaje na mume wako,..ni ushauri wangu huo…’akasema.
‘Msiwe na shaka na mimi, mimi simuogopi yoyote, ilimradi nipo
kwenye haki yangu, wanachotaka kupata sio haki yao, au sio.....kama kweli huyo
wakili na anaifahamu sheria, tutaangalia ukweli upo wapi na haki itatendeka,
lakini kama ndio hawo wenye tamaa..basi tutapambana hadi mahakamani, hilo usijali
kabisa…’nikasema.
‘Lakini muda sasa, na gharama…kijana wangu anaondoka hivyo,
lifikirie hilo kwa makini..’akasema.
‘Sawa nimekuelewa...’nikasema na mara simu yangu ikalia, nilipoangalia
nikaona ni namba ngeni kwenye simu yangu,, ...sikutaka kuongea na mtu
nisiyemfahamu kwa muda huo...tukaagana na mgeni wangu huo, huku simu inaendelea
kulia, baada ikakatika, ..baadae kidogo ikaita tena…, nikapokea na kuuliza
‘Nani mwenzangu...?’ nikauliza
‘Mimi ni mtoto wa marehemu Makabrasha....’akasema
‘Yupo huyo..na unasemaje?’ nikuliza
‘Nimesikia tetesi kuwa kuna mkataba unaoonyesha kuwa marehem
alikuwa na hisa kwenye kampuni zako, ni kweli si kweli…?’ akauliza
‘Mimi sijui hilo, ni nani kakuambia..?’ nikauliza
‘Wewe si mmoja wa wakurugenzi, kwanini hujui, na ni haki yetu kaam
warithi kulifahamu, je ni kweli au si kweli…?’ akauliza
‘Nimeshakuambia mimi sijui…je ndio taratibu za mirathi zipo hivyo,
wewe kuuliza hivyo tu kwenye simu,..unajua sheria wewe..?’ nikauliza
‘Naifahamu sana, mimi ni wakili, nimekuuliza hivyo, kwasababu kuna
hali inayoendelea kwa kiongozi wetu wa familia, analifahamu hilo na alilificha,
sasa natafuta ukweli, ili sheria ichukue mkondo wake…’akasema
‘Kwa kifupi, fuata sheria, ongea na kiongozi wenu, na ikibidi
ongeeni na wakili wetu, unanielewa,…’nikasema
‘Nasema hivi kama marehemu alikuwa na hisa kwenye kampuni zako,
inatakiwa utuambie, utupe memorandum, na vielelezo vyote vinavyostahiki, ili
tuweze kuorodhesha kwenye madai yetu, ndio maana nikakuuliza ili kuupata huo
ukweli..’akasema
‘Na mimi ndio nimekupatia hilo jibu…’nikasema
‘Sawa mimi nitafuatilia kuupata huo ukweli, na kama kuna njama
zozote za kuuficha ukweli, basi, sitasita kwenda mbele ya sheria…’akasema
‘Na samahani nikuulize tu, ni nani kakuambia mambo hayo?’
nikamuuliza
‘Nimesikia tetesi, hata kwenye kikao walisema kuna mikataba
mingine haijapatikana, wanaifuatilia…., niliwaambia mimi ni wakili wanipe mimi
nifanye ufuatiliaji wakachelea kunipatia, sema siku ile nilikuwa na kesi
nyingine ya haraka siweza kusubiria.., lakini sasa nipo na nafasi, nataka
kuuona huo mkataba...’akasema
‘Unasema ulisikia tetesi,..na unadai wewe ni wakili, unajua mambo
hayo ya kisheria yanafuatiliwaje au sio..au wewe tetesi tu kwako ni sababu, je ukisikia
tetesi kuwa wewe sio mtoto halali wa marehemu utasemaje…?’ nikamuuliza.
‘Unasema nini?’ akauliza kwa hamaki
‘Kuna tetesi kuwa wewe sio mtoto halali wa marehemu, wewe ni mtoto
wa kusingiziwa, je unazikubali hizo tetesi?’ nikamuuliza.
‘Sikiliza mimi nakuuliza mambo ya muhimu wewe unaleta mzaha,
sikiliza mimi nafahamu sana sheria, kama ni kweli, huo mkataba una haki zetu,
nakuhakikishia mimi nitafika hadi mahakamani…sasa kwa vile umejibu ki-huni,
nakupatia wiki moja tu, hilo liwe wazi, na ...hizo tetesi zako, hawo
waliokuambia waambie, hawana akili kwanini hawakusema hivyo wakati marehemu
yupo hai...’akasema.
‘Nilikuwa nataka kukuonyesha kuwa tetesi sio ukweli wa
mambo, kama ulisikia tetesi kuwa kuna mkataba kama huo wa halali wa hivyo
unavyosema, ilibidi ufuatilie kwanza sehemu husika..na ni vyema ukamuona wakili
wenu, kwani si mna wakili anayefuatilia mambo yenu ya kifamilia..’nikamwambia.
‘Mimi mwenyewe ni wakili, ndiye nimeteuliwa katima mambo ya
kisheria, lakini siku ile walinificha hilo jambo, sasa nimeanza kulifuatilia
mpaka nione mwisho wake...’akasema
‘Sawa, kama unaona ni haki yako fuatilia, ...ila ni vyema ukawa
na uhakika na hicho unachokidai,..sawa muheshimiwa..’nikamwambia.
‘Sawa …ila nitegemee kukuona, siku yoyote naweza kuja kuongea na
wewe kaika kulifuatilia hilo, nataka nionane na wewe uso kwa uso,….jiandae kwa
hilo….’akasema na kukata simu.
NB: Tuhitimishe? sehemu hii ilihitajia marekebisho mengi..lkn
hatukupata muda,....
WAZO LEO:Kunapotokea
mzazi mmoja kufariki hasa wa kiume, kuna watu wanajitokeza kudai, mali wakisema
na wao wana haki ya urithi, watu hawa wakati wa uhai wa merehemu, walikuwa
hawaonekani, na zaidi inawezekana kabisa marehemu alikuwa akiumwa kwa muda
mrefu, lakini hawakuwahi kufika, angalau hata kusaidia kidogo, hata angalau
kutoa pole, mpaka mzazi huyo nafariki.
Watu kama hao huja kujitokeza baadae wakati wa mirathi. Je huo
urithi, umetokea wapi, ukumbuke hiyo mali ilitafutwa na watu, na ni hawo hao
waliohangaika na marehemu, wenye uchungu naye…, wewe unakuja baadaye unadai,
mali, hiyo mali kwako itakuwa sio halali ...ni vyema tukajua kuwa, kila
penya faida kuna gharama zake pia.
Ni mimi: emu-three
No comments :
Post a Comment