Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, August 25, 2017

DUWA LA KUKU....41


‘Kwanini ulikimbia kwani hiyo video ilionyesha nini…?’ akaulizwa na hapo akatulia kama anawaza jambo, akaniangalia mimi, na alipoona namuangalia akageuza uso kuangalia kwingine, halafu akasema;

 'Hiyo video, ilionyesha karibu kila kitu, ….’akasema na kutulia

Tuendelee na kisa chetu

***************

‘Kila kitu , ...hya tuambie vitu gani hivyo, mbona unakuwa kama unaogopa kuviongea hivyo vitu, ukumbuke kuwa haya tunayafanya kwasababu yako, sasa usitupotezee muda hapa…’akasema mke 

'Unajua hapa natafakari mengi...sawa nitaongea tu, usiwe na shaka...'akasema

'Kwenye hiyo video, ilipoanza, ilikuwa inaonyesha kijana wangu, kakaa kashika shavu, kainamisha kichwa chini, baadae akainua kichwa, usoni kukaonekana machozi..kuashiria kuwa alikuwa analia..ndivyo ilivyoanza hivyo...baadae ikaonyesha anaongea, ...alikuwa anaongea mengi tu, lakini mimi nitaelezea yale yanayohusu hili tatizo.

'Ndugu walengwa, sikupenda kulifanya hili,...maana najua madhara yake, nawaheshimu sana wazazi wangu na kuwapenda sana, na najua baada ya kuuona huu ukweli, mtahakikisha kuwa video hii mumeiharibu, nisinelipenda hili likaenda zaidi ya nyie niliowalenga...'akalisema hivyo kwenye hiyo video.

'Mimi sina ubaya na mama, maana pamoja na ya kuwa awali nilihisi yeye ndiye mbaya kwa baba, lakini baada ya uchunguzi huu, nikagundua kuwa kumbe baba ndiye yupo nyumba ya haya mabaya yote kwa ushahidi wa haya mtakayoyaona...nampenda sana baba yangu, niliomba kila siku abadilike, niliomba kila siku ..ampende mama, niliomba kila siku hali yetu iwe kama zamani, lakini kila siku ilikuwa afadhali ya jana...

Basi hapo akaonyesha picha za wazazi wake, wakati wa ndoa, jinsi walivyokuwa wakipenda, na baadae akaonyesha kitu kama mpasuko...na kuweka ngurumo kwa radi, halafu akaanza kuongea...

‘Siku za baadaye hali ikaanza kubadilika, baba akawa kama hamjali mama, kukawa na mabishani hata kwa kitu kidogo, baadae nikahisi labda ni kutokana na hali za kiuchumi, maana kuna muda hali ilikuwa mbaya, maisha yalikuwa magumu, nikasikia mara kwa mara baba akisema ipo siku nitakuwa tajiri kama baba yako na wewe na wazazi wako mtakuja kuniheshimu.

Kijana alielezea mengi kwa jinsi alivyoona yeye....'hapo akatulia kuongea na mama Ntilie  akamuuliza

‘Sema ukweli wako, ni nani chanzo cha mabadiliko ya ndoa yenu, ni kitu gani kiliwafanya nyie wawili msielewane…?’ akaulizwa.

‘Ukiuliza hivyo utanifanya nijitetee nafsi yangu, mimi niliona kama mke wangu hanijali, kila nichomuambia hanisikilizi, anajiamulia anavyotaka yeye, vikao, shughuli, ..yaani hakuna kushirikishwa...na hilo likanifanya nihisi ni kwa vile mimi sikuwa na mali kama wazazi wake, kwahiyo uinabidi nitafute mali niwe kama wazazi wake …ndivyo nilivyoona hivyo…’akasema.

‘Ni kweli kuwa mke wako alifanya hivyo, kwa vile wewe hukuwa na mali kama wazazi wake..?’ akaulizwa.

‘Kwa muda huo nilifikiria hivyo, lakini baada ya haya yote niligundua kitu, kuwa ni udhaifu wangu tu, unajua tena sisi wanaume tulivyo,...ukiona huna kitu , mke ndiye mtendaji kuna hali ya...kujisikia vibaya fulani...kwahyo nikaona nitafuta namna ya kujionyesha kuwa mimi ni mwanaume...

Mara kwa mara kulikuwa na vikao vya watu fulani, unajua kwenye jami kuna makundi ya namna hivyo, wenye uwezo wanakutana kwenye mahoteli,..au vikao vya ..namna kwa namna, mimi ilifika sehemu siwezi kuhudhuria...sikuwa na kitu, na nikifika,..oh, labda michango , wenzangu wanatoa bila kusita, mimi, kwanza najiuliza..ni hali yangu ..lakini iliniuma sana..'akatulia

'Kwahiyo kwa hali hiyo, ikanivuta nifanye jambo...nikaanza kutafiti, wenzangu wamefanya nini..kwa bahati mbaya nikakutana na marafiki wa namna ambayo isingelinisaidia, na nikajikuta nimetekwa na mawazo yao zaidi, sikujali elimu yangu tena...'akatulia.

'Ni kwamba ilishafika mahali nahitajia mambo kwa haraka bila kufikiria mbele, na hao niliowauliza ndio wakanisimulia utajiri wa kupitia huko kwa shetani ….…’akasema.

Haya tuache hayo tuelezee kuhusu hiyo video...'akaambiwa

 ‘Kwenye hiyo video alielezea kuwa ile hali ya sisi wazazi kutokuelewana ilikuwa ikimkera sana , akawa anatafuta jinsi gani ya kuwasuluhisha wazazi wake, jinsi gani hata yeye anaweza kuleta utajiri, ili wazazi wake wawe na raha.. lakini hakuweza, hakujua, kwani hata elimu yake aliyopata japokuwa alifaulu vyema, lakini alikuw ahajapata kazi, kazi zimekuwa ni adimu...

'Kuna muda akavutika na biashara haramu....'hapo akatulia

''Biashara gani...?' akaulizwa

'Hakusema, ila alisema hivyo, kuwa alitaka atafuta njia ya kupata utajiri, huenda ukawafanya wazazi wake wakajirudi na kuwa kitu kimoja...hapo akawa anaonyesha jinsi wazazi wake wanavyogombana, kumbe tukigombana , alikuwa akatuchukua kwenye video yake.

Alielezea mengi tu, na hata kuwatupia lawama babu na bibi kwa jinsi walivywatenga watoto wao, anasema kwamba kama babu na bibi wangeliwachukua watoto wao walivyo, wakawawezesha kuliko kuwatenga , eti kwa vile bint yao hakukubaliana na wao, huenda mengine yasingelitokea...

Sasa ndio akaja sehamu ya pili, sehemu hii akawa anaonyesha, mabadiliko ya baba...

Akaelezea alivyoanza kuona mambo ya ajabu

‘Kiukweli nimevumilia sana, na sijui hata nianzie wapi..ila ninachoweza kuwa na uhakika nacho ni kuwa mambo yalianza kuwa mabaya pale baba aliporudi kutoka safari ya mikoani…ninaweza kushuhudia hilo, maana mimi nipo karibu sana na baba yangu.

'Siku hiyo aliporudi , usiku wake nilimuona akichimba shimbo upande wa mbele wa nyumba, na nikajua labda kuna kitu kichafu anakifukia, lakini kilichonishangaza, ni ile hali ya baba alikuwa hajavaa nguo, na ilikuwa ni usiku sana, na kuna matukio kama hayo yaliendelea kutokea. hapo akaonyesha kwa mbali picha ya mimi nikifanya jambo..nikiwa sina nguo..

Akaendelea...

'Mara nikaanza kuhisi kama kuna watu wanakuja usiku lakini siwaoni, na wakati mwingine nahisi kama kukabwa, hali hii ilikuja hata kutokea kwa mabinti wa kazi waliokuja hapo nyumbani, na kuna siku nilijaribu kumuuliza baba lakini hakutaka kuliongelea hilo nikahisi kuna kitu ananificha, aliniambia ni mambo ya kawaida ya watu wazima nisiwe na wasiwasi nayo…

Mimi napenda kudadisi, nikavutika sana nikawa nachunguza kinachoendelea usiku, na kawaida yangu nimejenga tabia hii ya kuhifadhi kumbukumbu nyingi kwenye video…basi nikaona hili la baba nitalichukua kwenye kumbukumbu zangu, ili baadae nije kumuonyesha..

Uchunguzi huu ulinifanya nigundue mambo ya kutisha zaidi...maana usiku nilioweza kuamuka, na kufuatilia, niliweza kumuona baba akifanya mambo ya ajabu ajabu...na cha ajabu kuna usiku mwingine nilikuwa siwezi hata kualala, maana nikilala najikuta naota ndoto mbaya, au nahisi watu wanakuja kunisumbua, japokuwa hata nikijitahidi kuna muda nazidiwa nguvu najiukuta nimelala…hali hii ikwa inanipa mashaka, nikaogopa hata kulala humo ndani.

Hata hivyo niliweza kuchukua baadhi ya video, zikimuonyesha baba akiamuka usiku, na kilichonita mashaka ni jinsi baba alivyokuwa akitembea...anakuwa kaam sio yeye...ndio maana hata niliposikua habari kuwa baba ana ugonjwa wa kuota kwamatendo nikakubaliana na hilo.

Lakini baada ya kuchunuza sana nikagundua sivyo hivyo wanavyosema kutokana na matukio haya nitakayoyaonyesha hapa ...hapo akaanza kuonyesha baba yake anavyotoka usiku...na kuna muda kama anaongozwa na mtu , mtu aiyeonakena...

 Ikawa inaonyesha video mbali mbali, nyingine baba yake akitioka usiku na kutembea kama roboti akielekea chumba cha msichana wa ndani, baadae anatoka, ..na vitendo kama hivyo vilikuwa vingi, lakini ambayo ilionyesha mambo ya ajabu

Baadae nikasikia kuwa mama katengeneza video ya kuchukua matukio humo ndani, nikachunguza mpaka nikaigundua ilipo, nikawa naifuatilia hiyo, na siku mama alipoipeleka kwa huyo mtu wake, mimi nikaifuatilia na kuiba, ...baada ya kukamlisha kazi aliyopewa,..huyo mtu namfahamu sana.

Na nilipoona hiyo video ndio nikaamini kuwa baba hakuwa na matatizo kama alivyosema docta kuwa baba anaota ndoto kwa vitendo, maana  ….ndani ya video hiyo walioekana watu waliojificha kwenye kitu kama giza, na huyo mtaalamu akakuza, na kuwaonyesha watu wa ajabu,..wachawi waliokuwa wakimuongoza baba, na mambo ya ya ucafu waliyokuwa wakifanya...

Video hiyo ikaonyesha kila kitu...inatisha , hata mie ambaye sikuwa na ufahamu wa hayo, niliogopa, na kiukweli nilijuata kwanini niliuangana na hao watu..sitaki hata kuelezea zaidi ya hayo niliyoyaona kwenye hiyo video, kwani baada ya kuiona nilihsii vibaya sana,…’akasema

‘Ina maana ni kweli hizo taswira za hao wachawi ziliweza kuonekana kwenye hiyo video…?’ akaulizwa.

‘Unajua kijana alichukua hiyo video akatoa nakala kama nne, hivi, moja akaniletea mimi, nyingine kwa mama yake nyingine kwa babu yake, nyingine sijui alataka kumpa nani, na ujumbe kuwa anakwenda na hatagemei kurudi, kurudi kwake labda apone, lakini kaba hajafanya hivyo, anataka wanafamilia wajua kinachoendelea ndani ya hiyo nyumba. Na alichogundua kuwa nyumba hiyo ilishatekwa na wachawi, na aliyesababisha hayo ni baba yake, na video hiyo ndio ushahidi...kiukweli ilionyesha kila kitu, hakuna ubishi...'akasema


Jamani dunia hii , usiku wengine wamelala, wengine wanafanya mambo ya ajabu kabisa,..nilipoona video ile, nikahisi kichwa kinauma,  nililia, nikalia…maana kweli kila kitu kilionena kiu-wazi, jinsi gani hao wanga walivyokuwa wakiingia na kufanya mambo, yao, ilikuwa kama unaangalia video ya kuigiza, kumbe ni matukio ya kweli, na mimi ni muhusika…sijui huyo jamaa aliwezaje kuzifichua hizo taswira za kichawi…’akasema.

‘Unasema ulilia sana, kwanini sasa ulilia, wakati ulipenda wewe mwenyewe..?’ akaulizwa.

‘Nyie hamjui jinsi gani nilivyokuwa nampenda huyo mtoto wangu, .jinsi gani nampenda mke wangu, hamjui ndani ya nafsi yangu kulivyo..lakini ningeliwezaje kulionyesha hilo, wakati akili imeshaona kuwa ili upendwe, ili uonekane ni bab bora ni mpaka uwe na mali...

Kiukweli kijana wangu ambaye nilishibana naye sana alikuwa huru kunielezea matatizo yake na mimi yake niliyoyaona anastahiki kuelezewa nilikuwa namuelezea, yeye alikuwa karibu na mimi kuliko, alivyokuwa kwa mama yake, muulizeni hata mama yake hapa analijua hilo…’akasema.

‘Sasa kwanini ulimfanyia hayo uliyomfanyia..mbona sisi hapo hatukuelewi...?’ akaulizwa.

‘Kama umenielewa vyema maelezo yangu tokea awali, mimi sikudhamiria kuyafanya hayo mabaya kwa nia ya kuiumiza familia yangu.., lengo langu ilikuwa kutafuta hali nzuri ya maisha, kwa masilahi ya familia yangu …na ujue shetani alivyo na nguvu nilijua hayo mambo ni ya muda mfupi tu, nitapata nitafikia kileleni kama hao ninaowaona, na maisha yataendelea, sikujua kuwa mambo hayo ni ya muda tu..yana mitihani yake…’akasema.

‘Sasa ikawaje…?’ akaulizwa.

‘Nilitoka kumtafuta, mtoto wangu, kwa marafiki zake, na sijui ilikuwaje siku kwa maana kwa, kila rafiki yake niliyemuendea, nikifika kwake anasemaa ametoka sasa hivi, ni kama alitaka kuwapitia marafiki zake kama anawaaga vile..mpaka usiku sikuweza kumpata , na nilipochoka ndio nikakumbuka kuhusu hizo video nyingine alizowatumia hao watu…

‘Ulijuaje kuwa kawatumia hao watu wengine na ni akina nani..?’ akaulizwa.

‘Kwenye hiyo video aliyonitumia mimi aliandika nakala kwa…mama, babu..na mtu mwingine hakumtaja…

‘Sasa ulikuwa una uhakika gani kuwa kweli kaituma kwa hao watu na kwa njia gani?’ akaulizwa

‘Hapo sikujua, nikaanza kumtafuta mke wangu, nijue wapi alipo, nikajua kama kamtumia mke wangu itakuwa humo humo ndani, nikatafuta sikuipata, nikamtafuta mtu wa karibu na baba mkwe ajaribu kuona kama kutakuwa na mzigo wowote uliotumwa huko, sikuweza kupata taarifa yoyote…kwani baba mkwe hakuwepo nyumbani.

‘Hayupo nyumbani, nakuomba uhakikishe kama kuna mzigo utafika hapo unaupokea na mimi nitakulipa pesa nyingi, si unanifahamu nilivyo,…sawa..’nikamwambia huyo mlinzi wa hapo nyumbani kwa baba mkwe, mlinzi huyu niliahi kumfanyia jambo kubwa, kiasi kwamba aliahidi kuwa hataniangusha.

‘Hamna shida bro…’akaniambia, kwahiyo hapo nikawa sina shida napo sawa, lakini ni swala la kubahatisha tu.

Mtu anayeweza kukusaidia ni yule bint…’nilipokumbuka hilo ndio nikaanza kumtafuta huyo binti, nilijua wapi naweza kumpata, nikaenda nyumbani hapo anapofanyia kazi, na nilipokutana naye hakutaka hata kuongea name.

‘Umekuja kufanya nini hapa, unataka kunigombanisha na mke wako au sio, kama ulivyofanya huko nyumbani mapaka nikafukuzwa kazi…hayo uliyonifanyia hayatoshi, nakuheshimu sana baba, nakuomba uondoke…’akasema

‘Nimekufanyia nini, kwanini unasema hivyo, unajua nimekuja hapa kufanya nini,..…?’ nikamuuliza sasa kwa hasira na sauti hiyo ikamfanya anywee na kutulia.

‘Unafikiri mimi sijui mlichonifanyia na huyo mchawi wako, nayajua yote, na najua kilichokuleta hapa ni hicho, mnanitakia nini nyie watu, tumewakosea nini,…’akasema kwa sauti ya huzuni.

‘Sijui unaongea nini, wenyewe hawapo humu…?’nikajifanya sijui kitu, ni kama vile nimekuja kukutana na wenye nyumba.

‘Wewe na huyo mchawi mpo kitu kimoja japokuwa unajifanya wewe hujui kinachoendelea, na unajua fika muda kam huu wenyewe wanakuwa kazini, …’akasema akiendelea na shughuli za usafi.

‘Sikiliza nikuambie kitu,…yule mzee mbaya wako amefariki, huna taarifa hiyo…’nikasema na yeye akashtuka kidogo, halafu akasema, kama kuuliza

‘Mzee gani…?’ akaniuliza, sasa akiwa kasimama na kuniangalia, uso wake ulijaa hamasa au wasiwasi fulani.

‘Yule mbaya wako wa kijini kwenu aliyetaka kukuoa…’nikamwambia

‘Nimesikia hivyo, na kifo chake nasikia ni kibaya kweli, alikuwa kipiga kelele kama anaumia,anaomba msamaha…mmmh, mpaka nikakufuru na kusema,..kumbe na yeye anakufaga, au ndio huko kuigiza kwake, maana kuna kipindi walisema hivyo, kesho yake tunaambiwa yupo hai…siwezi kuamini mpaka afikishwe kaburini, yule mzee alikuwa tishio…lakini ndio hivyo hakuna atakaye ishi milele…’akasema

‘Ndio keshafariki, usiwe na mashaka naye tena….’nikasema

‘Ndio umekuja kutoa taarifa au…?’ akauliza.

‘Hapana, najua watu wameshafahamu,..ila huu mguu ni wa kwako…nimekuja kwako unisaidie jambo moja..’nikasema na hapo akageuka kuendelea na shughuli zake, akasema

‘Nilijua tu…unajifanya umekuja kwa wenyeji hapa….haya niambie ni jambo gani, mimi sina uhusiano na huyo mtu, zaidi ya kuwa alitaka kunioa,nikamkatalia…kama ni mambo yenu ya kichawi, mimi sijui, na wala sijahusika kupambana na huyo mtu….’akasema

‘Sawa,…nisikilize kwanza,…mbona unakuwa na maneno mengi,… wewe unajua huko anapotokea, ni nani anaweza kunisaidia…unajua wewe unafahamu fika jinsi gani alivyopaharibu pale ndani kwangu, na nilishaongea naye akasema atayaondoa mambo yake, sasa ndio huyo ameshafariki,  ninataka nyumba yangu iwe safi, ni nani anaweza kunisaidia..?’ akaniuliza

‘Ni yule yule adui yake, yeye alikuwa ni mwalimu wake, nenda ukaonane naye, huyo ataweza kukusaidia…’akasema

‘Oh..mbona hata yeye kafariki pia….’nikasema na hapo huyo binti akadondosha ufagio aliokuwa kaushika kumbe alikuwa hajapata hiyo taarifa ya kifo cha huyo mzee mwingine.

‘Hapana ..ina maana hata yeye kafariki, unajua wale watu, nasikia kipindi cha nyuma walikuwa marafiki, mwalimu na mwanafunzi wake,..ghafla wakaja kukosana, wakaanza kupigana vita ..niliposikia huyo marehemu kaja hapa Dar, nikajua na huyo mwenzake atakuja tu, maana wanawindana kweli..oh, sasa, mimi sijui nikusaidieje…’akasema

‘Sasa baada ya hao ni nani mwingine anayeweza kunisaidia,maana haya mambo yamekuwa makubwa kwangu…’nikamuuliza

‘Mimi sijui..huko kijijini kwenyewe nimekuja kupaelewa baada ya matatizo yaliyotokea huko kwako…zaidi ya hayo mimi sitaki hata kurudi tena huko kijijini…, lakin kama hao watu wawili wamekufa, nahisi kijiji sasa kitakuwa na amani…’akasema

‘Mhh…sasa nitafanyaje…’nikabakia kushika kichwa

‘Sasa umekuja kwangu ukijua mimi nitakusaidia, hahaha, sikiliza baba,..mambo kama hayo ulitakiwa uende kuwauliza wazee wa huko huko, kijijini…na kuna watu wlifika hapa karibu, niliwaona, wnatokea huko kijijini, wao ni watu wa dini, hao wanaweza kukusaidia, kuliko njio hiyo ya kutafuta waganga wa kienyeji…’akasema

‘Nitawapataje hao watu…?’ nikamuuliza.

‘Niliwaona tu mara moja, sijui wapo wapi…jaribu kuulizia watuu…na jingine ni hilo la kwenda kuwaona wazee wa huko kijijini…’, aliniambia,

‘Lakini kuna mtu kasema wewe unaweza kunisaidia….’nikasema

‘Mimi nitakusaidia kwa vipi sasa, na kwanini asema hivyo, anahusika na hao watu nini,, anatokea huko kijijini au,..?….mimi kwa udadisi wangu niliwahi kuwauliza wazee, waliniambia matatizo mengine kama hayo yako, ambayo yanaingiliana na dhuluma,…wewe si umefanya mabaya, kwa watu , si ndio hivyo, kinachotakiwa ni kuwaendea hao uliowakosea uwaombe msamaha, hakuna njia nyingine…’akaniambia

‘Oh, basi mimi naanza kwako wewe…kukuomba msamaha….’nikasema

‘Kwani mimi umenikosea nin…si unakumbuka nilikulilia hali kukupigia magoti wakati nafukuzwa pale nyumbani kwenu.., ukasema wewe hujui lolote, ukanisaidi kuitoa ile mimba, huku ukidai sio ya kwako…uliniambia kabisa wewe, huna makosa mimi nakusingizia tu…’akasema

‘Kiukweli mimi hata sijui kitu,..ila nahisi kuwa nimekukosea sana, nakuomba unisamehe…’nikasema huku nikienda kumpigia magoti, yeye akabakia kushangaa tu.

‘Wewe mbamba, mna nini leo, …mimi sijui kitu…kama ulinikosea ni haki yangu kufahamu ulichonifanyia, niambie ulinifanyia nini, la sivyo sitaweza kukusamehe..nikuulize tena je ni wewe ulinipa hiyo mimba..?’ akaniuliza

‘Sina uhakika na hilo,…sio mimi…mi-mi-sijui…ndio maana nakuomba unisamehe, maana yaliyokuwa yakifanyika mimi sina uhakika nayo, si unajua ilivyo kuwa…’nikasema

‘Kama huna uhakika nayo, basi huna kosa, nenda kwa hao uliowakosea, hasa kijana wako, mimi niache niendelee na kazi za watu, usije kunifukuzisha kazi..…’akasema akiendelea na shughuli zake.

‘Kijana wangu nitampata wapi sasa…?’ nikamuuliza

‘Alikuja hapa akaniomba nimsamehe..na anaonekana kachanganyikiwa kabisa, nikamuuliza kosa langu akasema hana uhakika, kama ulivyosema wewe, akanipigia magoti huku analia, anataka nimsamehe, anadai kuwa kaambiwa ili apone awaombe msamaha wale wote aliowakosea, kwahiyo kaja kwangu,.., nikamwambia mimi sijui kosa langu kwake…akawa analia, hajijui,…mmh, nikamuonea sana huruma…’akasema

‘Oh, jamani kijana wangu, sijui nitawezaje kumsaidia, sasa wewe utanisaidiaje mimi…?’ nikamuuliza

‘Unajua nyie watu wawili mna nini sijui, hayo unayoniambia sasa hivi kijana wako kaniambia hivyo hivyo…na nilipomuuliza ana matatizo gani akasema…, lakini nikamuambia mimi siwezi kujua matatizo yake, wewe bab yake ndiye unaweza kuyafahamu…ndio akasema, wewe yaonekana hutaki kumsaidia kwa hiyo atakachokifanya anakijua yeye mwenyewe, ….’akatulia kama vile kasikia sauti

******************

‘Kuna nini..?’ nikamuuliza.

‘Bosi atakuwa kafika, nimesikia mngurumo wa gari lake…naomba tafadhali uondoke humu ndani haraka, isije kulete picha mbaya, yaliyopita bado yapo kichwani mwa watu, na mim sitaki kuzalilika tena…’akasema.

‘Usiwe na wasiwasi nitaongea na huyo bosi wako, mimi sina matatizo na hii familia, wananifahamu vyema…usijali kwa hilo…..’nikasema na haikupita muda, akaingia mama mwenye hiyo nyumba, aliponiona akaonyesha uso wa kushangaa, nikasalimiana naye na kumuambia nilikuja kuangalia kama mke wangu yupo hapa

‘Mke wako!!!….hapana, hayupo hapa, japokuwa ndio nafika…’ akasema huku akimuangalia mfanyakazi wake kwa mashaka, halafu akasema.

‘Nilihisi yupo hapa napiga simu yake haipatikani…’nikadanganya hivyo.

‘Mhh….mke wako aje hapa wewe usijue,… mke wako si yupo polisi…’akasema huku akimtupia tena jicho huyo mfanyakazi wake , ambaye kwa muda huo alikuwa akipanga panga vitu kwenye kabati.

‘Polisi…!!!? Kufanya nini huko…?’ nikamuuliza na yeye akashikwa na butwa, akiniangalia kwa mshangao.

‘Ok…yupo huko, kuhusu maswala ya huyo marehemu, kuna mambo anahojiwa, sasa shemeji, nikuulize tu, kwanini wewe hukufika siku ile hospitalini, wenzako wote walikuja, kasoro wewe, hata hivyo tumemalizana, na keshazikwa..mmh, ndio hivyo tena…yaani we yasikie tu…karibu shemeji mboana upo wima wima…’akasema

‘Kwanini azikiwe hapa, si anatakiwa kupelekwa huko kijijini kwao au..?’ akaulizwa

‘Yaani inatisha..japokuwa mwili uliwekwa kwenye majokofu, lakini umeoza, na kuanza kujaa mafunza..inatisha huwezi hata kuangalia…kwa hali iliyopo, wakaona ni bora tu kuzika hapa hapa kwenye makaburi ya city…’akasema

‘Mungu wangu…’nikasema

‘Sasa vipi kuhusu kijana wako, maana mke wako anasema kijana alikuwa akimitafuta kwenye simu, na alipotaka kumpigia tena akawa hapatikani, kwenye simu alikuwa akiongea huku kama analia, alivyosema mama yake, inaonekana hayupo vizuri, ….’akasema

‘Analia, analia nini, mbona ….’akataka kusema jambo halafu akakatisha.

‘Zaidi alisema ana mzigo muhimu sana kwa mama yake, alikuwa akitaka kumpatia mkono kwa mkono kwani anasafiri, kwani anasafiri kwenda wapi..?’ akauliza

‘Sijui kama anasafiri, lakini vijana wana shughuli zao nyingi, kama anasafiri ataniambia,…hata hivyo, hata mimi namtafuta, nilijua mke wangu yupo hapa , maana simu ya kijana nilipompigia alikuwa hayupo hewani..’nikasema

‘Mhh..huyo kijana mu8angalie sana, nahisi ana matataizo makubwa, …’akasema

‘Kwanini unasema hivyo…kwani unamuonaje wewe?’ nikauliza

‘Mke wako anadai kijana wake siku hizi hayupo sawa, na yeye anahisi huenda ni kunatokana na nyie wenyewe wazazi, ..’akasema

‘Kasema hivyo mke wangu, mmhh, siamini, kwanini asema hivyo…!?’nikaguna nikihisi huenda wameongea mengi kuhusu familia yake, kitu ambacho siki-kipendelea.

‘Ni katika kuongea tu, lakini mke wako hakutaka kusema zaidi, sasa kwa ushauri wangu mtafuteni kijana wenu mkae naye pamoja, muone mtamsaidiaje, hilo linaweza kuwa suluhisho, …kwani shemeji kuna tatizi gani, maana yule ni rafikiyangu lakini sio kila kitu anakiongea, hasa kuhusu mambo ya familia yake, namuona hana raha siku hizi…?’akaniuliza

‘Hamna kitu shemeji ni mambo ya kawaida tu,…sawa shemeji,nashukuru, kama takuwa hewani nitampigia simu, na kama ukimuona, basi mwambie namtafuta, au huenda sasa yupo nyumbani..nikasema na kuanza kuondoka, na wakati nipo nje….simu yangu ikaita…, alikuwa mke wangu.


‘Halloh..’nikasema

‘Sikiliza wewe mwanaume, kama kuna kitu kitatokea kwa mtoto wangu, nitakachokufanyia hutaamini, utakwenda kuozea jela..nakuhakikishia kwa hilo…’akasema

‘Kwanini unasema hivyo, kwani kuna nini kimetokea, na wewe upo wapi..?’ nikamuuliza

‘Nipo polisi, ndio naondoka huku, nikitoka hapa napitia kwa baba, nataka tuje naye huko nyumbani…’akasema, hapo nikahis labda ameshauona huo mkanda...na ukiona ilivyo, utahisi mimi ni mchawi...

‘Kuhusu nini…ni kuhusu huyo marehemu kwanini nyie muende polisi..?’ nikamuuliza

‘Kuna jingine ndilo limenichelewesha, askari wa kitengo cha madawa ya kulevya, alitaka kuongea na mimi , anadai kuwa kijana wetu  anatumia madawa ya kulevya, na wana wasiwasi kuwa anafanya biashara hiyo,…’akasema

‘Kwa ushahidi gani,…?’ akauliza.

‘Wanasema kuna kipindi ghafla hali yake ilikuwa nzuri, maisha ya juu sana, hana shughuli ya maana inayojulikana pesa alipatia wapi…na ameshaonekana akiwa kalewa hayo madawa….’akasema

‘Sio kweli, sasa umelimalizaje hilo, ngoja nitaongea na mume wa rafiki yako, tuone atavyoweza kutusaidia au unasemaje mke wangu….?’ Nikauliza na kusema

‘Usitake kusema hujui, hayo umeyasababisha wewe...'akasema hapo moyo ukanilipuka pwaah

'Kwanini unasema hivyo mke wangu, una ushaidi...'nikataka kusema hivyo bahato yeye akanikatiza kwa kusema

'Kwenye simu nilimuuliza ana matatizo gani akasema nikuulize wewe, na kuna huo mzigo anataka kunipatia, una kila kitu..nikamuuliza kitu gani, akakata simu, huku analia,…sasa nataka nikifika nyumbani unieleze ni nini kinachoendelea, na hata baba anataka kuja kuongea na wewe, na anaonekana kakasirika sana, mimi nimechoka..…’akasema na kukata simu.

‘Mungu wangu….’nikasema hivyo huku nakimbia..nakimbia kuuwahi huo mzigo kabla haujafika mikononi mwa mke wangu…na wakati nakimbia simu yangu ikaita tena nilipoangalia, nikaona ni namba ya yule mlinzi wa kule kwa baba mkwe

‘Halloh..’ nikaita na mara simu ikazima, kuangalia imejizima, nikaiwasha, kumbe chaji imekwisha, hapo hapo nikatafuta bajaji, sasa safari ikawa huko kwa baba mkwe, nikakutane na huyo mlinzi, huenda ndio huo mzigo...yaani hiyo video haifai kabisa waione wakwe zangu, najua wakiiona itakuwa ni ushahid wa kile wakilichokuwa wakikisema, na sizani kama kutakuwa na mjadala hapo...

Bajaji ilienda kwa kasi, kama nilivyomuomba huyo muendeshaji, na nikakaribia hapo kwa baba mkwe, sikutaka nionekane kwa mbali nikamuona huyo mlinzi kasimama mlangoni, na gari la baba mkwe linaingia…na nilimuona yule mlinzi kashika kitu...ni bahasha…nikajua ni huo mzigo wa video...

‘Hapa nikumuwahi tu…’nikasema na kushuka kwenye bajaji mbio mbio kuelekea nyumbani kwa baba mkwe...

‘Pesa yangu mzee….’mwenye najaji akaniuliza, na mimi sikuwa na muda wa kumsikiliza mbio mbio kuelekea kumuwahi huyo mlinzi, nyuma yangu bajaji inakuja kwa kazi

'Mzee pesa yangu...

WAZO LA LEO: Tusione kuwa kuongea, kutumia ulimi, kuandika mambo ya kiuzushi, ni jambo la kawaida tu, haya mambo ambayo yanaumiza wengine, yanasababisha madhara kwa jamii, ni dhuluma, na madhambi yake ni makubwa, maana hujui ukumbwa wa hayo madhara kwa wengine, hujui kiasi gani mtu mwingine anaumia na huo uzushi…, na je kuumia huko kunaishia wapi…na je hayo uliyoongea, au kuandika yana ukweli, yanasaidia jamii, tujiulize kwanza kabla ya kuandika, au kuzua,..

Hala hala jamani...tuweni makini sana na ulimi, tuweni makini sana  kalamu..tusione ni jambo rahisi tu,..Uzushi waweza kusababisha vita, na vita havina macho, watu wanauwana, na wamakufa watu wasio na hatia, watoto wadogo, wazee, akina mama,… je huoni kuwa wewe ulizua, ukachonganisha ndio wewe uliyewaua, …kwanini twajifanya wacha mungu , lakini matendo yetu ni ya kumcha shetani….


Tumuombe mwenyezimungu azisafishe nyoyo zetu, tupendane, tusaidiane,…ili dunia iwe ya amani na upendo.

Ni mimi: emu-three

No comments :