‘Unasema
yaonakena kuwa amefariki, ina maana huna uhakika bado…?’ akauliza kwenye simu na kuendelea kusikiliza
Baba mtu aliuliza huku
akijaribu kuangalia pembeni ili kijana wake asisikie anachoongea…, baadae
akasikiliza kidogo, halafu alipomaliza kuongea na simu akamgeukia mtoto wake na
kusema;.
‘Oh….sasa
sijui itakuwaje…’akasema
‘Ni
nani amefariki..?’ kijana akauliza na baba yake aliposikia hivyo akajua kijana
wake kamsikia, hakutaka ayajue hayo kwanza, akasema;
Tuendelee na kisa chetu...
************************
Nilitulia kwanza nikiwa sina nguvu,...unajua kuishiwa na nguvu..nikajikuta nimesema tu...
‘Bado
hawana uhakika…, yule mtu ana roho kama ya paka, nasikia kuna kipindi ilitokea
hivyo, wakawa wameshajua kafariki, baada ya muda akazindukana..ngoja
tusubirie…’akasema akiangalia pembeni, na kijana wake akamsogelea na kuuliza;
‘Lakini
ni nani huyo..?’ akauliza kijana, na mara simu ikaita , ilikuwa simu ya kijana,
na kijana kwa haraka akataka kuisikiliza....na baba mtu akataka kumzuia kijana
asiipokee, lakini kijana alikuwa ameshaiweka hewani, akawa anasikiliza….
‘Ndio
unasema, kuwa…taarifa,… taarifa gani hiyo, sijasikia taarifa yoyote..kwani
imekuwaje, hakuna nilichosikia bado, sawa nasubiria…kwani…!’ kijana akasema, na
kukatiza, yaonekana mpigaji alishakata simu. Kijana akageuka kumuangalia baba
yake, baba yake alikuwa karibu akijaribu kusikiliza hayo maongezi.
‘Ni
nani huyo…?’ baba akauliza akimuangalia kijana wake,na kijana wake akawa
anageuka wasiangaliane na baba yake, akasema;
‘Ni
rafiki yangu tu…’akamdanganya baba yake, na baba yake akageuka akiwa anataka kuondoka, kijana akageuka na kumuona baba yake
keshafika mlangoni, akamuuliza;
‘Sasa
baba mbona unaondoka, unakwenda wapi..?’ akauliza kijana akitembea kutaka
kumzuia baba yake asiondoke , lakini baba yake alishafika mlangoni..
‘Lazima
niende huko hospitalini nikaonane na huyo mtu akifariki kabla hajamalizana na
sisi unajua itakuwaje,…yaani ni muhimu sana nionane naye vinginevyo, hatutaweza
..oh, ngoja niondoke mwanangu, sijui itakuwaje…’akasema baba mtu, akionyesha
kuchanganyikiwa.
‘Kwani
ni nani huyo… mbona sikuelewi…baba, niambie..mbona unaondoka…’kijana akasema na
baba yake akawa ameshatoka nje, na kwa haraka kijana akachukua simu na kupiga
namba na alipopokelewa, akasema;
‘Mzee
kaondoka sasa nifanye nini..?’ akauliza na alipojibiwa akasogea kwenye sofa
akakaa, na kuinamisha kichwa chini, alibakia pale kwa muda, baadae akasimama,
…akatembea huku na kule kwa muda bila kutuilia, baadaye akashikwa kichwa na
kujikuna kwa mara nyingi, alikuwa kama anawashwa, akawa anahangaika kwa muda,
baadaye huyo akatoka nje
Wakati
anatoka simu yake ikawa inaita, yeye hakutaka kuipokea, akawa anatembea kuelekea
kituo cha mabasi hadi sehemu wanapokaa vijana na kuongea na mmojawapo,
wakasogea pembeni akapewa kitu mkononi, akatoa pesa na baadaye akaondoka pale
na kuelekea sehemu nyingine…
****************
‘Umemaliza….’akaulizwa
na mkewe na hapo akashika kichwa, na baadae akasema;
‘Hayo
ndio maelezo ninayoweza kuwasimulia, kwani baada ya hapo ndio ikaja taarifa
kuwa yule mzee mtaalamu amefariki kiukweli, na taarifa hizo nilizipata nikiwa nimeshafika hospitalini, nikiwa nahangaika kuonana naye…
‘Ina
maana siku ile ulikuwa upo hospitalini muda, wakati tunakutafuta kwenye simu…?’
akauliza mkewe.
‘Ndio, sikutaka kupokea simu zenu maana ningeliwajibu kitu mshindwe kunielewa,…nilifika hapo hospitalini muda, nia kuonana na huyo mtu, ili nimuwahi aniambie cha kufanya, maana kijana
ataponaje, wakati alikuwa hajamaliza hayo mambo yake…’akasema.
‘Sasa
ikawaje….?’ Akaulizwa.
‘Yaani
pale nilikuwa kama sio mimi….nilitaka hata kwenda kuiona hiyo maiti yake,
nilikuwa siamini kuwa huyo mtu ni marehemu..., lakini hao wahusika wa hapo hospitalini walinikatalia kuiona hata hiyo maiti.. , basi nikahangaika pale,
baadae wazo likanijia, nimpigie simu huyu adui yake, lakini sikuwa na namba yake ya
simu, nikampigia kijana wangu simu;
‘Unaweza
kunipatia namba ya huyo mganga wako…?’ nikamuuliza huyo kijana hata bila ya kusema haloo.
‘Mganga
wangu, yupi….baba…sipo vizuri kwa sasa, nipigie baadae…’kijana akakata simu,
nikahamaki nikampigia tena na tena, baadae nikasikia,
‘Simu
unayopiga haipatikani…’hapo nikajua mambo yameharibika.
Nilibakia
pale hospitalini kwa muda, na baadae ndio nikapokea simu ya mke wangu akiniarifu kuwa taarifa kamili
zimekuja huyo mtu keshafariki, na wao, hawawezi kuondoka hapo, hospitalini …mimi sikutaka
hata kuuliza kwanini hawataki kuondoka hapo hospitalini, nilikata simu.
Kiukweli kuwa muda huo ungeliniona ungelinihurumia, kuna muda, ninalia, kuna muda ninaongea peke yangu , hata sijielewi,.....baadae nikaona watu wanafika, nikamuona mume wa rafiki wa mke wangu ambaye ni askari akifika, mimi nikaona niondoke tu...
‘Kwanini
sasa na ulitakiwa uwepo hapo na mkeo ili kujua kinachoendelea…?’ akauliza mama
Ntilie.
‘Hapo
kichwa hakikuwa changu, na sikuwa nafahamu kinachoendelea kati ya mke wangu na huyo marehemu kuwa walikuwa huko hospitalini kwa dhumuni gani, hilo sikuwa nalifahamu,..na muda huo akili yangu ilikuwa inawaza mengi, nawazia jinsi gani nitaweza kumsaidia
kijana, nawazia hatima ya yoe hayo, ina maana baada ya hilo, kijana atamwambia
mama yake, na babu yake, kwahiyo itakuwaje, ndoa itavunjika.
Nilitoka
hapo nikawa nimepanga sasa niende kwa rafiki yangu mmoja, rafiki yangu huyo ndiye yule aliniunganishia na huyo
marehemu, nikijua yeye anaweza kunisaidia kimawazo, nilipofika kwake, hakutaka hata kuniona, kisa nilipofanikiwa sikumjali, ni kweli kipindi
hicho, sikutaka hata kumsikiliza matatizo yake, ..
‘Sikiliza
kwanza, kipindi kile nilikuwa nimechanganyikiwa…’nikasema kumwambia, hakutaka hata kunikaribisha ndani, mimi nikaingia kama kulazimisha tu..
‘Unachanganyikiwa
ukiwa na hali nzuri, hiyo hali nzuri ungeipataje kama sio mimi kukushauri uende
kwa huyo jamaa, sasa naona umefirisika, au sio,.sasa unataka nini kwangu…?’
akaniuliza.
‘Nina
shida, umepata taarifa…’nikamwambia
‘Taarifa
gani…?’ akaniuliza akiniangalia kwa uso wa kutaka kujua.
‘Yule
mtaalamu kafariki…’nikasema na jamaa akashikwa na butwaa kwa muda,….halafu
akasema
‘Oh, kumbe ni kweli, usiku nililiona hilo...ooh, sasa eeh...mungu wangu, mambo yameharibika…’akasema.
‘Sasa
ndio hivyo nimekuja kwako, unipe ushauri…si unajua...’nikasema
'Najua...najua...oh..hapana, sijui kitu, ondoka, ondoka...'akasema hivyo, na baadae akakaa kimia,
hasemi kitu ni kama ana jambo limemgusa zaidi ya huo msiba..akashika kichwa,
akataka kutembea kuingia chumbani, lakini akagundua kuwa kunma mgeni,
akasimama.
‘Unasikia,
bora uende, maana mambo yameharibika….’akasema
‘Ni kweli yameharibika, kijana wangu nitamfanyaje...'nikasema
'Kijana wako....?' akaniuliza akiniangalia kwa mshangao.
'Ndio, alikuwa hajamalizana naye...ndio nimekuja kwako unipe ushauri, maana yeye ndiye aliyenifanyia mambo
mengi, sasa yanamuathiri kijana wangu, nifanyeje sasa…’jamaa akauliza.
‘Wewe
unafikiria kijana wako tu, hujui mimi nina majanga kiasi gani,..yeye ndio
alikuwa kiongozi wetu, tunakula kwa kupitia mgongo wake, sasa kandoka, kukiwa
na mambo mengi hayajakamilika, hata mimi familia yangu ipo hatarini, bora
uondoke tu…kila mtu afe kivyake, ...'akasema
'Sijakuelewa ina maana na wewe alikufanyia mambo hayo kama mimi...?' nikamuuliza
'Yaani we acha tu,...lakini mimi sio kama wewe...ila sikiliza, mungu wangu sijui utafanyaje, maana kama mlikuwa hamjamalizana, imekula
kwako, jiandae kuwa tahira, vinginevyo, wewe au mkeo, au mtoto wako akatolewe
kafara,…’akasema akinisukuma jamaa niondoke.
'Akatolewe kafara la nini na nani...?' nikauliza
'Inabidi ufunge safari...mmh, kamuulize yule binti...'akasema
'Binti gani huyo...?' nikamuuliza
'Yule mfanyakazi wako wa kwanza...atakusaidia..mimi sijui zaidi ya hapo, nina mambo yangu mengi kichwani, sijui. maana kila kitu alikuwa nacho yeye, mambo ya usiku, ...mmh, sasa hili balaa...vitu vyangu vitakuwa wapi...'akasema akishika kichwa.
‘Kwahiyo
ina maana gani hapo mbona sikuelewi, au,… wewe ndio miongoni mwa watu
mliokuwa mkishirikiana naye usiku…?' nikamuuliza
'Wewe ondoka bwana usinichanganye..ondoka ondoka....'akasema kwa ukali.
'Wewe ndiye ulinielekeza kwake, wewe ndiye unayemfahamu, na sasa yaonyesha wewe ndiye mlikuwa mkishirikiana naye,...'nikasema
'Sikiliza sasa hivi tupo hatarini,...jamaa kazidiwa na adui yake, na kama ni hivyo wote washirika wake wapo matatani,hapo ni mmoja baada ya mwingine, bila kufanya jambo, tumekwisha...'akasema
'Kufanya jambo gani sasa...?' nikamuuliza
'Mimi sijui...mpaka nihangaike, sijui...wewe ondoka tu, siwezi kukusaidia kwa hilo...'akasema
'Sasa tusaidiane ..maana kama ni hivyo...'nikasema
'Nimekuambia uondoke nyumbani kwangu, usiniongezee matatizo..,..au nikuitie mwizi,..hebu ondoka, jamaa akazidi kunisukuma
niondoke , alikuwa kachanganyikiwa kweli, na mimi nikaona hapo sitasaidiwa kitu
ikabidi niondoke
**************
‘Ina maana huyo mtaalamu alifariki kutokana na
mapigano ya mambo yao na adui yake…?’ akaulizwa baada ya kupita kitambo, kwani
alikuwa kama hajisikii vyema, ikabidi atulie kwanza.
‘Yawezekana,…kwani
huyo mama ambaye aliongozana na huyo adui wa mpinzani wa mtaalamu wangu,
alitumwa kwenda huko hospitalini na huyo mpinzani, sijui alitumwa nini,…maana
nilisikia, alipofika tu ndio huyo marehemu akapiga ukelele,…kwahiyo kuna namna
ilifanyika hapo…’akasema.
‘Namna
ipi hiyo….?’ Akaulizwa.
‘Huyo
adui yake alikuwa natafuta mwanya wa kumuingia huyo adui yake,…na akaona njia
ni kumtumia huyo mwanamke, ..ni kama vile yeye alijificha nyuma ya huyo
mwanamke, na huyo mwanamke alipoingia tu, yeye akarusha hilo kombora lake,..au
yeye, alibakia sehemu akiangalia huo mwenendo, au huyo mama alipewa kitu
akifanye akifika huko hospitalini…’akasema.
‘Wewe
ni nani alikuambia hayo…kuwa huenda ilifanyika hivyo?’ kaulizwa.
‘Nahisi
hivyo tu…, maana baada ya hapo sikuweza kuonana na yoyote kati yao, zaidi ya
huyo jamaa niliyekwenda kwake akanifukuza..na huyo jamaa akatoweka siku kadhaa
alirudi baada ya mazishi, sijui alikwenda wapi, na hata aliporudi na yeye akawa
anaumwa sana..’akasema.
‘Sasa
ikawaje..?’ akaulizwa.
‘Basi
mimi nikarudi nyumbani, nikidhamiria kuonana na kijana wangu , na kijana
hakurudi mpaka kesho yake, na aliporudi nikamwambia kuwa huyo mtu kafariki, na
kijana hakutaka kusema na mimi akawa kimia tu, ndio nikamwambia naomba namba ya
huyo mganga wake, akanipa…’akatulia.
‘Ukampigia
huyo mganga wake..?’ akaulizwa.
‘Ndio
nilimpigia,…na alipopatikana akasema anaumwa, hataweza kuongea na mimi kwenye
simu…hali yake sio nzuri…na nikamuomba anielekeze hapo anapoishi, akasema
nimuulize kijana wangu atanielekeza, na nikamuuliza kijana wangu akanielekeza.
Nikajipanaga
kwenda kuonana na huyo jamaa nikijua sasa yeye ndiyo wa kutusaidia, kijana akawa
haongei zaidi ya kile unachomuuliza, anakujibu kwa mkato tu, akawa hana raha,
kama mgonjwa.
Basi siku iliyofuata nikaamua kwenda kuonana
na huyo mtu, nilitoka mapema kabisa, nilipofika nikakuta watu wamejazana,
nikauliza kulikoni, nasikia kuna msiba,..msiba wa nani, nikaambiwa ni mzee
mmoja alifika hapo, ni mgeni, na nilipodadisi sana, nikagundua kuwa ni huyo
niliyemfuata..hapo sikukaa tena nikarudi nyumbani.
Baadae
kijana akaja, akiwa anatetemeka, hali yake ni mbaya, nikajaribu kumdadisi ndio
akanipa taarifa kuwa huyo mganga wake naye kafariki,…na sasa hajui
ataponaje,..basi ikabidi nimliwaze kuwa nitamtafutia mtu mwingine asijali,
lakini moyoni nilikuwa sijui ni nani wakutusaidie, nilishakata tamaa.
‘Sasa kijana wako ataponaje, au mlifanya
juhudi gani …?’ akaulizwa
‘Kiukweli
kuanzia hapo, na mimi nikaanza kujisikia vibaya, kichwa kinauma kupitiliza,
nikawa kama naanza kuchanganyikiwa, nahisi vitu vingi kichwani,…’akasema
‘Sawa
ikawaje..?’ akauliza
‘Sasa
ikawaje…hahaha..hapo nikajua sina changu, sina familia, sina ….basi nikaanza
kuongea peke yangu kama mtu aliyechanganyikiwa.
****************
Kesho
yake nipo nipo tu..mara kijana akaja, na kunikabidhi bahasha, na hakusema kitu
akaondoka,…nilipoifungua hiyo bahasha ndio nikakuta kanda ya video,..cd
‘Video
ya nini…?’ akaulizwa
‘Sikujua
ya nini, maana ilikuwa haijaandikwa kitu juu yake, ila mimi nikaamua kwenda
kuitizama ina ujumbe gani ndani yake,..akilini nilishaanza kuingiwa na mashaka,
ukumbuke mimi muda huo nipo nipo tu, ila hamasa ya kuiangalia hiyo
video, ilinijia tu…nikaenda kuiangalia..mamamama..ni aheri nisingeiangalia…
‘Ilikuwa
na nini…?’ akaulizwa
‘Kila
kitu kama alichosema kijana..kila kitu, na mwishoni ..ooh, hapo nikaitoa……nilichofanya hapo, ni kuitoa na
kuiharibu, nikahakikisha hakuna hata salio limebakia, nikatoka humo ndani na
kuanza kukimbia, …
‘Kukimbia…unakimbia
kuelekea wapi…?’ akaulizwa
'Kumtafuta mwanagu ,kumuwahi kabla....hapana sikuwa na akili hapo, karibu ngongwe na magari...
‘NB: Haya,
jamaa ndio hivyo, je haya yaliendaje…maana baada ya hapa, mke anaanza kuingilia
kati..ilikuwaje kuhusu huyu jamaa na je ni nini hatima ya kijana , je kwenye
hiyo video kulikuwa na nini hasa….tutaendelea seehmu ijayo
WAZO LA LEO: Chuki ni tabia ya shetani, na yeye kazi
yake kupandikiza chuki kwenye nafsi zetu ili tukosane, ili kusiwe na upendo
kati yetu, nia ni kufarakanisha ndoa, udugu, na mshikamano. Tunatakiwa
tulishinde hili, na kulishinda hili n kujenga upendo, kuhurumiana, kusameheana.
Ukijiona wewe unawachukia wenzako, kwasababu mbali mbali ujue unatawaliwa na
shetani. Mpende jirani yako, mpende hata adui yako, utaweza kumshinda shetani.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment