Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, August 18, 2015

RADHI YA WAZAZI-31


‘Sasa kilichotokea, baada ya mtundu kufungwa, wateja wote wa kampuni ya Mtundu, wakahamia kwa huyu  mtaalamu,kwahiyo mtaalamu akawa juu sana kibiashara kipindi hicho, na ukumbuke  kipindi cha nyuma kulikuwa hakuna ushindani mkubwa wa kibiashara kwenye nyanja hii ya mitandao na komputa, kwahiyo alikuwa na wateja wengi sana...’ akaendelea kuongea mpelelezi.

‘Hilo lipo wazi endelea....’akasema mkuu wake akiangalia saa yake.

‘Utandawazi na mambo haya ya mawasiliano yakaingiliwa na wawekezaji wengi njanja hii ikawa inakuwa kwa kasi,....makampuni mengi yakajielekeza huko,   kukaanza ushindani wa kibiashara, soko likawa na bidhaa nyingi kuliko wanunuzi,...’ akasema

‘Na kama ujuavyo, bidhaa zikiwa nyingi kuliko wateja, soko linapungua, bei zinalazimishwa bei kushuka, bila kujali gharama za uendeshaji,...na hali kama hii, ikaanza kuyumbusha makampuni mengi...bidhaa wanazo, utaalamu wanao, lakini wateja hakuna, hilo likaanza kumyumbusha hata mtaalamu ,mwenyewe na biashara yake..

‘Ndio ni kipindi hicho na ilikuwa ni tatizo la dunia nzima....au?’ akauliza mkuu

‘Ndio lilikuwa janga la wengi, ...na kwa huyu jamaa aliyezoea kujiona yupo juu, ana wateja wengi, alibweteka kwa kipindi hicho, ulipofika upinzani, akaanza kushuka ki biashara mambo yakaanza kumuendea mrama, ikafika mahali sasa hana wateja,...hana biashara, na kuanza kuandamwa na madeni,...mwanzoni kama walivyo, waajiri wengi, ..., akaanza kupunguza wafanyakazi...

‘Wengi hukimbilia kuunguza wafanyakazi kama njia ya kupunguza gharama, hivi hakuna njia nyingine mbadala...’ akawa kama anauliza huyu mkuu

‘Ni kifo cha mfa maji tu, kutapa tapa, zipo njia nyingine lakini hiyo hupewa kipaumbele.....’akasema

‘Haya endelea.....’akasema mkuu

‘Huku na huku ndipo akamkumbuka rafiki yake aliyekuwa huko jela...’

‘Ndio ulisema aliwahi kuonekena huko, ...lakini hilo la kumuendea rafiki yake mlijumuisha tu, sizani kama mliongea na huyo rafiki yake akakubali kuwa aliendewa kwa ajili hiyo, kutoa ushauri, je huo ushahidi una mshiko ...?’akasema

‘Tulifanya upelelezi huo kwa huyo rafiki yake, lakini huyo rafiki yake hakukubali, yeye alisema alitembelewa tu,..na huwa anatembelewa na wengi, lakini hawakuongelea maswala kama hayo...’akasema

‘Ikawaje sasa, maana huwezi kuniambia mtalaamu anayumba kibiashara, wakati sasa anaonekana kuwa miongoni mwa watu wanaofanya vizuri, ..... sijauona huko kuyumba kwake....hebu angalia sasa anavyofanya, anawasaidia vijana,kafungua makampuni mengi sana, ushahidi gani wa kuweza kuonekana kuwa alikuwa hivyo, na sasa yupo hivi..’akasema mkuu wake

‘Kwa mabadiliko hayo ya ghafla, ndipo sisi kama watu wa usalama tuliweza kumtilia mashaka, kwani kipindi cha miaka minne huko nyuma, alikuwa na hali mbaya kibiashara na ghafla akainuka,na ghafla akawa na....’ mkuu akataka kumkatiza, lakini akasita

‘Wateja hawakuongezeka kihivyo, kuonyesha kuwa biashara imeongezeka, lakini akaanza kuinuka, tukashangaa anapanua hata makampuni...akaanza hata kujenga mahusiano makubwa wa serikali,  na watu mbali mbali, akawa anapata zabuni serikalini...na utaona hata alianza kujiingiza kwenye mambo ya kisiasa akitumia mitandao yake....’akasema

‘Mhh,yawezekana alibuni mbinu zaidi za kitaalamu, na hizi zabuni si hab ukipata zabuni moja, ni pesa nyingi, kama una akili ya kibiashara unaweza kupanua biashara zako, lakini ni pale ukiwa na watendaji wazuri, wenye uzoefu, sasa huyu jamaa kama mnavyomuona ana akili sana ya kibiashara, kwahiyo hio sio sababu ya msingi au....’akasema mkuu

‘Mkuu tulifanya uchunguzi wa kina kwa hilo...utaoa kwenye ushahidi ....’akasema mpelelezi

‘Sawa naona muda unakwenda mbio...’akasema mkuu akiangalia saa yake na mwendesha mashitaka akawa anachukua kumbukumbu zake , na muda mwingi alimuachia mkuu huyo aulize maswali, kwa vile alishaongea na mpelelezi.

‘Sasa kukaanza hili wimbi,....ujambazi wa aina yake ukajitokeza, wizi wa benki kwa aina yake, ufisadi wa hali ya juu, watu wanaiba hadi benki kuu, watu wana weka pesa nchi za nje kwa wingi, hizi pesa zinapatikana wapi, wakati hali ya nchi ndio kama unavyoiona....

‘Na ukichunguza sana hawa watu wanaoweka pesa nje ni watu wa kisiasa, sio wafanyabiashara, wafanyabiashara inajulikana kwako haina shaka, lakini hawa watu wa kisiasa, inatia shaka,...tukahisi kuna jambo, tukahisi kuna mtu yupo nyuma ya haya na lazima awe na utaalamu wa hali ya juu,....’akasema

‘Sawa hilo tuliliongelea waati ninakua hii kazi, ....’akasema

‘Ndio mkuu, na unakumbuka kulikuwa na swala la siri za serikali, zikawa zinavuja, zinavujaje na kuwafikia watu wasiofaa..na zikifika kwa hawa watu wanazitumia kama biashara....unalifahamu hilo,...tuliliongelea pia....’akasema

‘Kwanini zivuje,..ni kwasababu siri hizo ziligeuka kuwa ni kuwa ni biashara, swali likawa hizi siri zimewezaje kutoka na kuwafikia hawa watu,....hili ni swali lilituumiza sana vichwa....’akaambiwa

‘Ndio maana nikataka ulichunguze, lakini....lakini haya mauaji, na huku kuvunjika kwa amani, watu wanalalamika sana, sikujua kuna mahusiano na hili...kwahiyo sasa tunahitajia ushahidi wa hali ya juu, sio huu tu, mimi haujanitosheleza,..’akasema

‘Ushahidi upo mkuu, nitakuja kukuelezea, hasa tukianza kuangalia ushahidi huo hatua kwa hatua,kama utahitaji mkuu.....’akasema

‘Je na huu ufisaidi wanaukuza hata kuleta sintofahamu kwa wananchi,.....haya ni mambo ya wanasiasa,...’akasema akiangalia saa yake mara kwa mara

‘Mimi sizani kama yana uhusiano na hii kesi, mimi naona kwa masilahi ya taifa, tusijiingize sana hawa watu wa ...na mambo ya kisiasa, unajua tukianza kuwalenga wanasiasa tunaweza kuanzisha uhasama usio na tija, vinginevyo, unionyeshe mahusiano yake na hii kesi ...ninasema hivyo nikiwa na maana ,nina kikao na wakuu, na hili ninaweza kuulizwa, ...’akasema

‘Mkuu, utakuja kuona mahusiano yake ,....usiwe na shaka mkuu...’akaambiwa

‘Ni muda...ok,..na , na wizi wa benki ok, huo ni ujambazi tu,..na unasema kuna kuweka pesa nje , kwenye benki za nje, hawa ni wafayabiashara na kwa utashi wao huwezi kuwazuia au sio, lakini inapokuja kwa wanasiasa inaleta walakini, sasa kama wanasiasa wameguka kuwa wafanyabiashara, hii inaleta shida, hili nitaliongelea na wakuu, ili tuone jinsi gani ya kufanya,......sasa niambie hilo nalo linahusianaje na hii kesi,...’akatulia

Wakati mpelelezi anafungua makabrasha yake mkuu akamgeukia muendesha mashitaka aliyekuwa akiandika andika mambo yake...

‘Eti muendesha mashitaka,....unajua mimi sijaelewa kitu, unaweza kuoanisha haya mambo na hii kesi yenyewe, maana huu ni uwanja wako, kama mumeshaongea, ni vyema ukanifafanulia hata wewe,... bado mnanichanganya....mimi naona tusichanganye mambo, najua kunaweza kuwa na maingiliano....au mnasemaje?’ akasema na kuuliza

‘Ni sawa mkuu, lakini kesi ya haya mauaji ina chanzo chake, na chanzo chake ndio hiki anachokuelezea mpelelezi...., haya mambo yanayotokea, vurugu, migomo,kuchomwa majengo, wizi sio bahati mbaya....ni mipango iliyosukwa,ni mambo yamepangwa na wajanja ili ionekane kihivyo inavyoelezewa na hata ku-uwawa kwa huyu mtu, sio bahati mbaya, mkuu...’akasema

‘Ukiangalia mfuatano wa haya matukio, utaona ni mpangilio fulani,...na ilitakiwa ionekane kihivyo, kuwa ni mambo ya kidini hayo, chuki za kidini hizo, au ni mambo ya kikabila, au ni mambo ya kisiasa tu,.... lakini ndani kwa ndani kuna ajenda ya siri....’akaambiwa

‘Ajenda ya siri! ni ajenda gani hiyo,....ya siri,...?’ akauliza mkuu akiangalia saa yake, na mara simu yake ikalia, akaiangalia akaikata .., akasema;

‘Kabla hujanijibu swali langu la hoja hiyo ya ajenda ya siri, kuna kitu nataka kufahamu kwako mpelelezi, ...kuna kijana mmoja, sio kijana sana...ni rafiki mkubwa wa kijana wangu....na wanafanya kazi pamoja..., nilikuambia pia ujaribu kuangalia nyendo zake, je katika kesi yako anahusika...maana nimesikia kuwa na yeye tumemshikilia, kwa vipi?’

‘Huyo ni mmoja wa vijana wetu tuliowatumia,hata bila wao wenyewe kujijua,...na tumemshikilia kwa madhumuni maalumu,  ...’akaambiwa

‘Kuwatumia!....kwa vipi...mbona hukuwahi kuniambia hilo kabla..’ akauliza kwa mshangao

‘Unajua huyu jamaa, ni rafiki mkubwa wa kijana wangu, na sikupenda, ...walifikia hata kugombea msichana..lakini nilimuambia kijana wangu aachane na hilo....wapo wengi...lakini nikamtilia mashaka ndio maana nikataka umchunguze, ...’akasema

‘Tulifanya hivyo mkuu, lakini kama nilivyokuambia yeye alikuwa kama chambo....’akatulia

‘Kwa vipi,...maana mwanzoni ulisema ana uhusiano na huyu mshitakiwa mkuu, ni mlezi wake,....lakini akaja kumkana, au sio, sasa je alikuwa akishirikiana na huyu mlezi wake kwa siri kwanini amkane, ....au ilikuwaje mpaka na yeye tukamshikilia, sipendi hii hali itaonekana imefanyika hivyo kwa vile alikuwa na uhasama na kijana wangu....’akasema huku akiangalia saa

‘Naona muda unakwenda, tuahirishe kikao mpaka baadaye, nina kikao na wakubwa au...?’ akauliza mkuu akiangalia saa yake.

NB: Naishia hapa kwa leo


WAZO LA LEO: Kwanini vurugu, kwanini migomo, kwanini uhasama wa kidini au wa ukabila, haya na mengine yawezekana ikawa ni mipango ya hali ya juu yenye malengo madhubuti, ya kurejesha ukoloni mambo leo, hayo ni maono yangu, na mwenye akili ayatizame kwa  uwoni wake, kwanini hayo yatokee sana sehemu zenye maliasili, madini na utajiri wa asili....
Ni mimi: emu-three

1 comment :

Faith S Hilary said...

Soon narudi maeneo haya wangu. Acha nianze moja. Nimekumiss saaaaaana