Muendesha
mashitaka alielezewa kuhusu kesi yote, japokuwa alishaongea na mpelelezi,
kabla,... na jinsi kesi yenyewe ilivyo, na ni mmoja aliyewahi kufika eneo la
tukio, siku kulipotokea hayo mauaji, kwahiyo alikuwa ana ufahamu kiasi wa hiyo
kesi, alichokuwa akihitajia zaidi ni ushahidi ...
Basi
wakaanza mazungumzo, sasa akiwemo muendesha mashitaka, ambaye alikuwa muulizaji
maswali hapa na pale...
‘Mara nyingi
kesi zenu zinakuwa na utata, ...kwasababu mnakuwa na mambo mengi ya kibinafsi, na
wakati mwingine mnakuwa hamkubaliani kwa baadhi ya mambo....’akasema muendesha
mashitaka
‘Ukisema mambo
yetu ya kibinafsi una maana gani..?’ akauliza mkuu
‘Inawezekana
kukawa na mshitakiwa lakini kwasababu za kibinafsi mkaanza kusema hiki usiseme
hiki usifanye, mambo kama hayo huwa yananipa wakati mgumu....’akasema
‘Sasa
unataka rufanye nini, wewe siunatakiwa kuwafuata maelekezo ya mteja wako,
ilimradi yanaendana na sheria...’akasema mkuu
‘Mimi
niwaambie ukweli kama kweli mnataka hili tatizo liishe, niachieni mimi na huyu
mpelelezi,msiingilie kitu hata kimoja...tutalimaliza hili tatizo kabisa....’akasema
muendesha mashitaka
‘Ni lazima
niingilie, nikiona ni jambo linalogusa taifa, linalogusa masilahi ya taifa, sio
mimi napanga haya...,wakati mwingine napata shinikizo toka juu,kwa masilahi ya
taifa...’akajitetea.
‘Ok,sasa
hebu niambieni,ni nini kusudio lenu,hapa...mpaka sasa tuna watuhumiwa wakubwa
wawili, tukiacha hawa washitakiwa wengine,...je hawa washitakiwa wakubwa wawili
wana tatizo, kuna kikwazo kwao, kuna masilahi ya taifa ...?’ akauliza
‘Mimi sioni
kama kuna tatizo hapa mkuu...,kwasababu ushahidi wote tunao, ....kama nilivyokuonyesha na sasa ni kibali
tu cha mkuu hapa...kwangu nimemaliza kazi....’akasema mpelelezi
‘Kwahiyo
kumbe mlishaongea na kuonyeshana kila kitu, sasa hiki kikao kina umuhimu
gani...?’ akauliza na wenzake wakamuangalia wakionyesha mshangao.
‘Ok, hebu
nifafanulieni, wapi mlipofikia...?’ akasema mkuu alipoona hiyoo hali.
‘Mkuu,
unakumbuka ulimwambia msaidizi wako mambo yakiwa tayari aendelee, na ndicho
tulichkifanya, sasa ukisema kama tumeshaongea hiki kikao kina maana gani.....ni
kama unatulaumu kuwa tumefanya mambo wakati wewe haupo au....’akasema mpelelezi
‘Ok,
nimeshawaelewa....ninachoshangaa ni kuona msaidizi wangu hayupo, sijui ana
dharura gani hajanipigia simu, sijaongea naye....lakini mnielewe, ilibidi
nifike kabla kesi haijaanza, kwani kuna mambo natakiwa kuyasikia, kuna
wawezekaji, kuna masilahi ya taifa,.....’akasema
‘Mimi naona
ushahidi upo kamili,..na kama ulivyoona yote ni mambo yapo wazi, sizani kama
yanagusa masilahi ya taifa,...ni kero kwa taifa...watu kama hawa wanastahiki
adhabu kali, ili iwe ni fundisho, na .....hawa wahamiaji,......’akasema mpelelezi,
akiendelea kutoa ushahidi alioukusanya...
*********
‘Umesema
mmoja wa washitakiwa ni huyu jamaa wa mitandao, huyu jamaa amekuwa akiisaidia
sana serikali, amekuwa akiwaajiri vijana,...nashangaa sana kusikia kuwa na yeye
ni jambazi....hebu niambieni ujambazi wake upoje..?’ akauliza mkuu akiwaangalia
wenzake
‘Kwa nje
ndivyo anavyoonekana, na ni kweli ana kampuni kweli inahusika na mambo ya
mitandao,na anauza vifaa mbali mbali vya komputa na mitandao..,ni kweli amekuwa
msitari wa mbele kusaidia vijana, hasa kwenye ajira...’akaelezea
‘Sasa
hamuoni kuwa huyu ni mtu muhimu kwa maendeleo ya taifa?’ akauliza
‘Lakini
kiundani anakiuka sheria za nchi, ni fisadi, na kama unavyona kwenye ushahidi, yeye
anashughulikana na mikakati ya wizi... katika uchunguzi wetu tumelibaini hilo
kwa asilimia kubwa.....’akasema
‘Ngoja
kwanza, ..unasema yeye ni fisadi,...pia ana mikakati ya wizi, lakini haionyeshi
moja kwa moja kuhusika na kesi ya mauaji ...tunachoangalia hapa ni hii kesi ya
mauaji, kwanza’ akasema akionyesha kumtetea mshitakiwa huyo.
‘Huyu
mshitakiwa anahusika,kama utakavyozidi kuona kwenye ushahidi wetu....’akasema
‘Una uhakika
na hilo....sio kwamba namtetea,...mmh, sasa hii ni hatari...nilimuamini sana
huyu mtu, na kwenye kikao huko kwa wakubwa ni mmoja ya watu, niliowapigia debe,
oh, sasa, ok, tuendelee...’akasema mkuu
‘Mkuu huyu
mtu ni mjanja sana, yeye anadai huwa yeye hujihusisha tu na mikakati ya uzalishaji,
au mikakati ya biashara,... kuacha utaalamu wa mitandao na mawasiliano, kwahiyo
ukifika kwake, anakuwa na vitengo viwili, utaalamu wa mitandao na komputa,...hili
lipo wazi....
‘Lakini ana
shughuli nyingine,...mikakati ya biashara, kama anavyoiita, sasa hapa kwenye
mikakati ya kibiashara kuna mambo mengine yaliyojificha ndani yake kutegemeana
na wewe uliyefika kwake...’akasema
‘Kutegemeana
.....! Sasa mumegunduaje kuwa anahusika na mikakati ya ujambazi, mara ufisadi
na tena kuhusika na haya mauaji....?’ akaulizwa sasa akikuna kuna kichwa.
‘Ilikuwa
kazi ya ndani kwa ndani,...mwanzoni tulipata shida sana, lakini tukaja kupata msaada kutoka kwa yule mpelelezi,... wa kujitegemea,...ilibidi
tumtumie huyu mtu’akasema
‘Na huyu
mpelelezi anahusikaje, na y eye ni mmoja wa washitakiwa....?’ akaulizwa
‘Hapana, ila
tulimtumia tu....yeye sio miongoni mwa washitakiwa, atakuja kuwa shahidi muhimu
mahakamani, ikibidi....’akasema
‘Ikibidi,....?
Ok endelea,...’akaambiwa
‘Kwa
kumtumia huyu mpelelezi,ndiye aliyetupa njia mbadala ya kuja kumnasa huyu
mtu,...huyu mpelelezi tulikuwa tunamshuku kwa makosa mbali mbali,...tulimuhusisha
sana na uharabifu wa amani, na harakati hizo, lakini alikuja kutuonyesha kuwa
yeye sio chochote, kuna mtu ambaye hatujamshuku, na ni hatari zaidi.....’akasema
‘Kwahiyo
mumefanyaje ili akakubali kuisaidia polisi, maana mara nyingi huyu mpelelezi wa mitaani, anakuwa hapendi
kushirikiana na polisi, anasema polisi ilimuasi, ilimsaliti,....?’ akaulizwa
‘Tuliamua
kumshirikisha kinamna, tulimuahidi kuwa leseni yake atarejeshewa, unajua tulishaisimamisha
leseni yake kutokana na yeye kuhusishwa kwenye mambo mengi ya kijambazi..., na
kwa vile alikuwa hana kazi kwa muda, njaa imembana, akakubali kushirikiana na
sisi, na jambo moja likafichua jingine....’akasema
‘Kwa vipi?’
akauliza
‘Tulimpa hiyo
kazi ,kama kumuajiri....kwa makubaliano ya kuja kumlipa,...ilibidi tufanye
hivyo,ili tupate undani wa hilo kundi,....na imetusaidia sana, na nina uhakika
mwisho wa siku tutalimaliza hilo kundi na huyu jamaa naye tutamdhibiti kabisa,
kwa vile kila sehemu sasa tuna watu wetu....’akasema
‘Kwahiyo
akaweza kuongea na huyu mtaalamu, au huyu mpelelezi aliwezaje kuwasaidia hadi
mkagundua kuwa huyu mtaalamu anahusika na ujambazi, ufisadi na hata haya mauaji...?’
akaulizwa
‘Ilibidi
tumuachie huyu mtu, afanya anavyojua yeye, na huku hajui kuwa kuna watu wetu
wapo nyuma yake wakimfuatilia, ...na
huyu mtu,hakufahamu kuwa tumemtegea, tulishagundua kuwa huyu mtu haaminiki,
....kwa tamaa zake anaweza kutuficha mambo...tukamtegea vyombo vya kunasia
matukio, kila anapokwenda tukawa tunapata anachokifanya...’akasema mpelelezi.
‘Huyu mtu
una maana mpelelezi, au sio, je hakuweza kuligundua hilo....?’ akauliza
‘Hakuweza,
siku hizi mkuu, kuna utaalamu wa kila namna, haina haja ya kuweka vifaa
vikubwa, haina haja ya wewe kuwekewa kitu kikubwa, na ndivyo tulivyofanya kwa
huyu jamaa, na pia tukaweka watu wetu kwenye mitandao ya simu....’akasema
‘Mitandao ya
simu...?’ akauliza
‘Ndio mkuu, simu siku hizi zimekuwa ni sehemu muhimu ya kupata mambo yanayoendelea,
na ni rahisi sana kufuatilia kila kitu,...hizi simu zenye mitandao.
Tunazokuwa
nazo majumbani,...zinafichua kila kitu kinachofanyika tukitaka kukufuatilia,
kama utakavyokuja kuona kwenye ushahidi wetu huu mkuu
‘Ok,...kazi
nzuri,ehe...kabla sijaona huo ushahidi zaidi....,hebu naambieni kuhusu huyu
mtaalamu, maana mimi nilikuwa namuamini sana,imekuwaje kujiingiza kwenye haya magenge....?’
akauliza
‘ Ni kweli
ni mtaalamu sana, alifaulu masomo yake ya komputa, na mitandao, katika ngazi ya
hali ya juu,na alipomaliza masomo yake
chuokikuu, alikuwa na malengo ya kupata kazi nzuri, kwenye makampuni
makubwa,lakini ikawa sio bahati yake....’akasema
‘Mhh, kama
vijana wetu...’akasema mkuu
‘Huyu mtu,
yaani mtaalamu, alihangaika sana kutafuta kazi, lakini kila alipopata, ikawa
halipwi kama anavyotaka yeye, na kunatokea muda, anakosana na waajiri wake,
anaachishwa kwa sababu hizi na zile....na sio kwamba ni mbaya wa kazi, kazi
anaweza sana,lakini unajua tena waajiri wengine, hawataki kumuona mtu
anajifanya anajua sana zaidi yao....’
‘Baadaye
huyu mtaalamu akakutana na jamaa mwingine, huyu jamaa ni mtundu wa mitaani,
yeye hajasoma sana,...aliishia vyuo vidogo vya ufundi, lakini ana kipaji cha ufundi, hasa kuhusu komputa
na mitandao...
‘Mkuu, kama
huyu mtundu angelisoma zaidi huenda angelikuwa mkali zaidi ya huyu mtaalamu,
lakini ubaya wake hapendi shule..au nikutokana na hali za wazazi wake hawakuwa
na pesa za kumsomesha zaidi...
‘Huyu
mtundu, ndiye aliyekuja kujenga sumu kwa huyu mtaalamu,...hutaamini, mtaalamu
na usomi wake, alikuja kugundua...lakini ni baadaye kuwa rafiki yake alikuwa na
maana kubwa kwake....’
‘Huyu mtundu
yupo wapi kwa hivi sasa....?’ akaulizwa
‘Huyu
alikuja kukamatwa na kushitakiwa, ndio ni yule aliyeshitakiwa kwa makosa mengi
likiwemo la mauji, yaliyotokana na biashara ya mlungula(blackmail),...kwa hivi sasa yupo anatumikia kifungo,...’akasema.
‘Yawezekana
historia ikajirudia,...’akasema muendesha mashitaka na mkuu akatikisa kichwa
kama kukubali.
‘Ni kweli
yawezekana,...unajua hawa marafiki walipokutana, kipindi hicho, huyu mtundu ndiye
aliyemshawishi mtaalamu kuwa haina haja ya kusumbuka na ajira, alimwambia
hivyo, kwani yeye alikuwa na uzoefu wa mitaani, kazi za hapa na pale za
kujiajiri alizijulia, na maisha kwake yalikuwa hivyo...
‘Unajua wewe
ni ajira tosha,utaalamu ulio nao, huhitajiki kusumbuka,...wewe unaweza
kujiajiri....’akashauriwa na mwenzake wakati wanaongea.
‘Kujiajiri,
ni kazi kubwa sana,sina mtaji, sina akiba yoyote, pesa niliyokuwa napata ni hand to mouth...,hilo ndilo tatizo ‘akasema
mtaalamu.
‘Huhitaji
mtaji mkubwa kwa sasa...kwanza ni kuanza kutengeneza kile kisichohitajia
pesa, na kama ni vifaa, atanunua
mteja...na kama ni vifaa vingine mimi ninavyo, tutasaidiana kidogo kidogo,
...wewe nitakuelekeza, usiwe na wasiwasi...’akaambiwa
Na kweli
akavutika na hilo wazo, japokuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa, ....yeye alisomea
kuajiriwa, na ndio lengo yakena lengo la wasomi wengi....’akasema.
‘Huyu
aliyejifunza kutokana na utundu wa mitaani, na kipaji alicho nacho, akaanza
kumuelekeza huyu mtaalamu wa kusomea, ...wakaelekezana na ndipo huyu mtaalamu,
akamfundisha mwenzae kuwa mkopo yawezekana na utawasaidia, a kweli baadaye wakapata
mkopo kama mtaji wa kuanzia, wakaanzisha kampuni yao.
‘Kiukweli
kwa mtaalamu, ambaye alizoea ikifika mwisho wa mwezi anapata chochote, Ilikuwa
mwanzo mgumu kwake, lakini baadaye
wakafanikiwa...walikuja kupata wateja kutoka kampuni mbali mbali, na kuweza
kujitangaza, na hatimaye kampuni yao ikajulikana ...
‘Ndio hii
kampuni iliyopo sasa....?’ akauliza mkuu
‘Hapana sio
hii iliyopo sasa...’akaambiwa
‘Kwahiyo
kumbe,...hiyo ya utapeli sio hii,...hebu endelea kunifahamisha....sijui
mwanasheria, unanielewa kwa kuuliza maswali yangu, ni ili upate ufafanuzi
zaidi....mnielewe hapo....’akasema akionekana mwingi wa mawazo.
‘Unajua hapa
walikutana watu wenye mitazamo miwili tofauti, japokuwa waliweza kufanikiwa,
lakini kulikuwa na migongano ya hapa na pale kwenye utendaji wao wa kazi,
mtundu akawa ana mambo yake ya chini kwa chini, na mtaalamu akawa haafikiani na
hayo mambo ya chini kwa chini...
‘Mambo gani
hayo ya chini kwa chini...?’ akaulizwa
‘Huyu wa
mitaani , alitaka mambo yasiyo na utaratibu ule unajulikana, kama kulipa kodi,
kuwalipa wateja kwa wakati, kazi za halali, na vitu kama hivyo...yeye
alipendelea mambo yaende kiujanja ujanja, hata kazi nyingine ziwe za ujanja
ujanja, ilimradi pesa ipatikane...hali kwa mtaalamu ilikuwa kinyume, yeye
alitaka kutumia elimu yake zaidi....’akasema.
‘Elimu
ilimsaidia eeh,....sasa ikawaje akajiingiza huko...?’ akauliza mkuu
‘Kwa hali
hiyo, wakaja kutofautiana kabisa, na walipokaa kwenye kikao chao maalumu,
wakaona iliyo bora ni kuachana kila mmoja akawa na kampuni yake binafsi.
Wakakubaliana
na kweli kila mmoja akawa na kampuni yake binafsi, ....’akasema
‘Sasa wakiwa
na majina tofauti, ila walijitahidi wateja kuwafahamu, na haikuwa vigumu sana
kwa kipindi hicho...’akaambiwa
‘Sasa huyu
mtundu, akawa huru, kufanya mambo anavyojua yeye, mwanzoni alifanikiwa
sana,.... alikuwa na biashara halali na biashara haramu...hii biashara haramu
ndiyo iliyomuinua sana,...’akasema mplelezi.
‘Kama
ukiangalia kesi ya huyu mtundu, utakuja
kugundua kuwa, alikuwa na mipango ya kuwasaidia majambazi, kubuni mikakati, ya
kimitandao, na kuwaibia watu hata pesa zao kwenye akiba zao,....kwa ama
kuwahadaa, na watu hutoa kumbukumbu za amana zao bila kujijua,..au kwa kutumia
mbine za ujanja za mlungula,au kitaalamu blackmail....tukaja
kumkamata na akafungwa kifungo cha miaka mingi tu...sasa hivi yupo jela,
anatumikia kifungo....’akasema
‘Ok, huyo
alikuwa mtundu, sio huyu mtaalamu, au sio....huyu mtaalamu akawaje kujihusisha
na mambo hayo na elimi yake, na kuaminika kote na .....hata mimi, bado,maana
kaajiri vijana wetu, analipa kodi....anasaidia mambo mengo ya kijamii...’akasema
mkuu akionekana kama kutoakuamini.
‘Mkuu, sio
vyote ving’aavyo ni dhahabu,...’akaambiwa
‘Sawa,
endelea...lakini niulize yeye katika mikakati yake alikuwa akiwashirikisha watu
wake, wafanyakazi wake....vijana aliowaajiri...?’ akauliza hilo swali
‘Mkuu....kiutendaji
aliweza...japokuwa huenda walikuwa hawajui, au wanajua, lakini wasingeliweza
kufichua siri za kampuni...’akasema
‘Mlichunguza
hilo kwa wafanyakazi kuwa wanahusika...na nani na nani anahusika...?’ akauliza
‘Kwanza
mkuu, ngoja tuendelee na huyu mhusika mwenyewe...umuone alivyoweza kujiingiza
huko, na ndipo utagundua mwenyewe kuwa wanahusika au hawahusiki.....’akasema
‘Ok, endelea
NB: Naona
niishie hapa kwa leo , msione tunakawia kuingia kwenye undani wa jina la kisa
chenyewe, lakini haya yanatolewa,...yanagusa jamii, yalitokea kwenye kisa
chenyewe, na diary yangu, inatumia mfumo wa visa kama njia ya kufichua uovu
kwenye jamii, kueleimisha nk....
WAZO LA LEO: Elimu yako itakuwa na umuhimu sana
kama itakusaidia katika maisha yako lakini katika misingi ya haki na
ukweli,...na itatumika kusaidia jamii, kwa kuleta maendeleo katika kiu-adilifu...
ukiwa kama kiongozi, uwe ni wa siasa, maofisini, nk...timiza wajibu wako, kama
taaluma yako inavyokutuma ... na sio kuitumia kiujanja ujanja kunufaisha tamaa
zako binafsi, huo ni ufisadi wa taaluma.
No comments :
Post a Comment