Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, August 20, 2015

RADHI YA WAZAZI-32


Ushahidi ulianza kuonyeshwa hatua kwa hatua....na ikafikia sehemu ya ufafanuzi

‘Kwahiyo kilichoweza kumfichua huyu mtu ni pale alipoonekana  gerezani akimtemtembelea huyu Mtundu....

‘Ndio,....hilo lilitufanya turejee kesi ya huyu Mtundu, tukajua kuwa huko kwenda kwake magerezani, kulikuwa na jambo,.. .tukawa tunalichunguza hilo...

‘Je mliweza kuthibitisha hilo, maana katika maelezo yako ya awali ulisema hawa watu wawili, yaani mtaalamu na mtundu,  walikuja kukosana na sababu kubwa ni tabia za mtundu ambayo ilikuwa sio sahihi kwa mtaalamu. Mtaalamu hakupenda mambo yanayokwenda kinyume na elimu yake, sasa ikawaje na yeye akaelekea hukohuko,...?’ akaulizwa.

‘Mkuu, hakuna kitu kibaya kama njaa,...mtu ulizoea raha, biashara inaingiza pesa nyingi, ...halafu unashuka hadi kufikia hatua ya kukosa hata mishahara ya mwezi,ukumbuke huyu mtu alikuwa na wafanyakazi, wanahitajia mishahara yao, anatakiwa kulipa kodi nk.....ikafika hawezi kuyamudu hayo yote tena, unafikiri angelifanya nini

‘Kugundua utaalamu zaidi, kugundua biashara nyingine, huoni alivyoanzisha miradi mingine japokuwa hakuwa anaisimamia yeye, lakini yeye ndiye chanzo...’akasema mkuu.

‘Kutokana na pesa gani, alipatia wapi hiyo mitaji,...hakuna ushahidi kuwa alikopa mahali....’akasema mpelelezi.

‘Ina maana ndio ....

‘Baada ya yeye kuonekana gerezani, tulianza kufuatilia kazi zake, watu anaoshirikiana naye..., tukaanza kuunganisha moja baada ya jingine...ndio tukagundua kuwa yale yale ya mtundu ndio anayoyafanya huyu jamaa....ila ni kitaalamu zaidi...’akasema mpelelezi

Tuendelee na kisa chetu....

**********

‘Jana nilikuuliza kuhusu huyu kijana , rafiki wa mtoto wangu, ...’akaanza mkuu,

‘Ndio mkuu...kijana yule anatokea Afrika Mashariki,...historia yake ilikuwa wazi ilionekana hadi kwenye vyombo vya habari,....kilichowashangaza wengi  ni yeye kumkana huyo mlezi wake baadaye....’akasema

‘Kwanini sasa amkane wakati huyo mlezi ndiye aliyefanya juhudu zote hadi akapata wadhamini,....na hao wadhamini kuja kumsomesha huku Ulaya...?’ akauliza

‘Hilo pia ni moja ya jambo lililotufanya liweze kutusaidia kwenye uchunguzi wetu,....na kiukweli kijana alifanya hivyo, sio ni kutokana na tabia mbaya za mlezi wake, ....bali kulikuwa na sababu nyingine ambayo haikuwa wazi sana....’akasema

‘Huyu, kijana alikuwa na mahusiano na binti wa yule mama mtemi,na kipindi hicho huyo mama mtemi alikuwa na uhasama na mshitakiwa mkuu....uhasama wao haukuwa wazi kwani unahusishwa na mambo ya mlungula,..katika upelelezi wangi ikabidi nimvae huyu mama, ....huyo mama akaja kuniambia kuwa huyu mshitakiwa mkuu, alijaribu kumfanyia visa vya mlungula alipomuajiri nyumbani kwake....’akasema

‘Huyu mama aliweza kuyasema hayo! Kuwa alifanyiwa visa vya mlungula, na je aliweza kusema ni kitu gani alichomuhusisha nacho ili kumdai pesa za mlungula...?’ akauliza

‘Huyu mama hakutaka kusema undani wa hilo,...ila sisi kama wapelelezi tulichunguza, tukagundua hilo,..unajua huyu mama kwa kumbukumbu alipokuwa mmoja wa wahalifu,alikuwa na machafu mengi, ndio akafikiwa kufungwa...’akasema

‘Hilo linajulikana,...sawa...tusiende mbali sana kupoteza muda....’akasema mkuu

‘Huyu mama katika athari za kufungwa alipoteza kizazi,...alipoolewa na huyo mume wake, ...wakataka kupata mtoto, na mwanzoni huyu mama hakumuambia mumewe kuwa hana kizazi, ikabidi wahangaike sana, na mume alipogundua hilo, kuwa mkewe hana kizazi, hakutaka waachane, wakapanga kupata mtoto kwa njia nyingine yoyote ...’akasema

‘Walitumia mbinu , lakini hizo mbinu hazikuwa wazi,sio halali ..... wakapata huyo binti walie naye,....’akasema

‘Hazikuwa wazi kwa vipi?’ akauliza

‘Hakuna sehemu yoyote inayooyesha kuwa walifuata taratibu sahihi kisheria, ...ina maana walifanya hayo kwa kificha na isivyo halali,...’akasema

‘Ndio wakampata huyo binti, ni kiukweli wanampenda sana huyo binti yao, na..hawataki kabisa huyo binti afahamu kuwa kupatikana kwake sio kwa njia halali...na hawataki kabisa yeye ajua kuwa huyo baba yake sio baba wa kumzaa.....’akasema

‘Lakini ...’akataka kusema kitu mkuu

‘Wamejitahidi kulificha hilo, na binti anaamini kabisa hao ni wazazi wake halali, hadi huyu mshitakiwa alipoweza kugundua nyaraka zinazoonyesha tukio hilo, na kama anavyofahamika huyu mshitakiwa akipata kisababu kidogo hukitumia kuingiza pesa,..yeye alipolipata hilo, akaanza kulifanyia kazi, akaweza kwenda hadi kwa dakitari aliyefanikisha hilo tendo, akapata ushahidi wake,.....’ akasema mpelelezi.

***********

‘Sasa tukirejea kwa  huyu kijana, ...kijana kampenda binti wa huyu mama, na wakawa marafiki ,na mama mkwe ni adui wa mshitakiwa, je itakuwaje kwa huyu kijana kupata huyu binti ikiwa yeye ana mahusian na adui wa mama mkwe.

Kijana ikabidi aukane ulezi wa huyu baba yake, kuwa hamtambui, kuwa huyo baba alimtumia tu kama daraja ,lakini jana uhusiano kabisa na huyo baba.

Mama akaona ndio mwanya wa kumfundisha adabu huyu mshitakiwa...akampa kijana mashartim kama kweli hana mahusiano na huyo baba mlezi..’akasema

‘Masharti gani....?’ akauliza

‘Kama kweli huyu mshitakiwa sio mlezi wake kama alivyodai, basi atafute kila mbinu,...za kufanya huyo mlezi wake, afungwe....’akasema

‘Kwanini....?’ akauliza kijana

‘Ina maana hujui, kuwa huyu mtu ni mhalfu...’akaambiwa

‘Kama ni mhalifu mimi nipo tayari kutoa ushahidi ili afungwe...’akasema kijana

‘Ina maana hujui kuwa anauza madawa yasiyofaa, kuwa anajishughulisha na biashara ya mlungula...’akaambiwa na kijana japokuwa alikuwa anafahamu hayo,hakujua kuwa huyo mama anayafahamu kijana ikabidi akiri kuwa alifahamu lakini hakutaka kuingilia mambo yasiyomuhusu.

‘Kwasababu hanihusu mimi sikutaka kumuingilia mambo yake...’akasema

‘Sasa kama sio mlezi wako, kama huna uchungu naye, kama unataka kujitakasa kuwa wewe ni msafi , unaweza kuishi na binti yangu nataka utimize masharti yangu....’akaambiwa

‘Kijana akakubali....kutoa ushahidi ikiwemo kuwa mlezi huyo alikuwa akiuza madawa yasiyo halali, na pia anajishughulisha na biashara la mlungula,...

‘Hiyo haitoshi...ili umuoe binti yangu, nataka huyo mtu ashitakiwa...wewe mwenyewe uutafute ushahidi halisi, huyu mtu akamatwe kwani hafai katika jamii....’akaambiwa na mama mkwe.

‘Kwahiyo kijana akawa akitafuta kila mbinu kumnasa huyu mlezi wake, na kwa vile alikuwa akifanyia kazi kampuni ya mtaalamu, ....siku moja akamuona baba mlezi akifika maeneo hayo, kuona hivyo akahisi kuna jambo akatoa taarifa kwa mama mkwe....kuwa mlezi wake kaonekana akikutana mara kwa mara na mtaalamu

‘Kuna kitu gani wanajadili, amekuja kuomba kazi...?’ akauliza mama mkwe

‘Sizani kama nikuomba kazi, na sina uhakika wana jambo gani na huyoo bosi...’kijana akasema

‘Una hisi bosi wako ana jambo analofanya lisilo halali ?’ akauliza

‘Huwa kuna mambo yake anayofanya hataki watu wayafahamu, sasa nilimpomuona huyu mtu hapo, nahisi kuna jambo, nahisi bosi ana mambo ya siyo halali,...’akasema kijana

‘Huwezi kufahamu ni kazi gani kwa kuchunguza kwenye komputa zake...? akaulizwa

‘Nimechunguzwa nimeshindwa kujua..lakini nina uhakika kama huyu mtu kaja kwa 
mtaalamu kuna jambo linafanyika...’akasema.

‘Ngoja nitalifanyia kazi mwenyewe.....’akasema mama mkwe.

‘Sisi tulishalinasa hilo mapema,...hata wakati kijana anamuambia mama mkwe wake,

Mama mkwe akamuendea mtaalamu akiwa na lengo lake kichwani...ujue hawa watu hawa wahaivani, yaani mtaalamu na huyo mama, mama alipofika kwa huyu jamaa, jamaa akatambua kuna jambo...

‘Nikusaidie nini mama yangu.....’akamwambia kwa unyenyekevu, na huyo mama hakupoteza muda akamwambia anachokihisi..

‘Wewe mama nakuheshimu sana, kwanini unanishutumua kwa mambo hayo machafu.....’akang’aka mtaalamu

‘Sikushutumu ila kweli unashirikiana na wahalafu, mimi siwezi kuja kukuambia kitu kama hicho kama sina ushahidi,....sasa kama unataka nije kulifikisha kwa mbele za sheria, nikatalie...’akasema huyu mama, mtaalamu ikabidi ampooze huyo mama ...’akasema

‘Kwa vipi....?’ akauliza

‘Huyu mama anapenda sana pesa....mtaalamu analifahamu hilo, akamuahidi pesa nyingi pindi mipango yale ikifanikiwa, hakuambiwa ni mipango gani,.....

‘Huyu mama hakutaka aonekane kwa watu, kwahiyo alikwena kwa huyo jamaa mara moja, na mambo mengine yaliyofuata hakuwa anafika yeye kwa mtaalamu......akijua kuwa mtaalamu ni mjanja, na anajulikana na wakubwa,...na pia hakutaka kuonekana bado yupo na tabia ile ile ya kudai pesa kwa njia ya milungula, ....’akatulia

‘Sasa alifanyaje.....?’ akaulizwa

‘Akawa anamtumia kijana wetu...’akasema

‘Kijana yupi?’ mkuu akauliza kwa sauti kama ya kushituka

‘Rafiki wa kijana wako...yaani huyu mtoto aliyemkana mlezi wake...’akasema

‘Kwa vipi, nakumbuka ulisema kijana huyu pia mlikuwa mkimtumia kwa upelelezi, bila ya yeye kufahamu....?’ akaulizwa

‘Ndio..tulikuwa tukimtumia, ....lakini sio moja kwa moja, kuwa anasaidiana na polisi,...kulikuwa na watu wetu wakimfuatilia, na kupata taarifa kutoka kwake,....’akasema

‘Ehe, ikawaje...?’ akaulizwa

‘Na kijana keshapenda ....kwahiyo akawa tayari kufanya kila kitu atakachotuma na mama mkwe wake...akawa anatoa taarifa za bosi wake kwa huyu mama, na huyu mama akawa anadai pesa kwa mtaalamu, ..japo hakutaka ionekana ni  njia ile ile ya mlungula....’akasema

‘Mhh, huyu mama hajaacha tabia yake....’akasema mkuu

‘Mtaalamu akaona sasa kazungukwa pesa aliyokuwa akiipata kwa njia zisizo halali imeshaingiwa na mdudu, kuna mtu keshafahamu mipango yake, inabidi afanye mbinu za kuhakikisha kuwa huyo mama hafahamu dili zake, au amnyamazishe kwa lolote lile...akaona amtumie huyu huyu mshitakiwa.

‘Kitu kilichomshangaza ni kwa jinsi gani mambo yake yamegundulikana, na taarifa zake kufika kwa huyu mama, akawahisi watu wawili, kijana wa huyu mshitakiwa, na mshitakiwa mwenyewe, ndio akamuhamisha huyo kijana kwenye kitengo kingine, hakutaka kumfukuza kwani angelifanya hivyo angeonakena ana jamabo,...jamaa ni mjanja sana....

Hata hivyo huyu mama  naye hakuwa mjinga, akawa anafuatilia kujua ni dili gani ambayo huyu mtaalamu anaifanya akishirikiana na marehemu akaja kuigundua, na akampigia simu moja kwa moja mtaalamu na kumwambia mtaalamu kuwa keshagundua kuwa kuna dili ambayo yeye mtaalamu anashirikiana na mshitakiwa...’akamwambia

‘Dili gani wewe mama, unajua mimi nitakushitaki kwa kuniharibia jina langu...’akamwambia.

‘Nitaliharibu keli jina lako, natumai unanitambua nilivyo.....’akasema huyo mama na kukata simu

‘Mtaalamu anamfahamu huyu mama kuwa anaweza kufanya hivyo, ikabidi afanya mipango ya kuongea naye, na kumuahidi kuwa atajitahidi ampatie chochote, japokuwa huyu mtaalamu hakukubali kuwa anashirikiani kwa lolote na mshitakiwa, ila akasema;

‘Mama kama huyu jamaa ana dilii ni lazima nitaigundua, na nikigundua nitahakikisha unapata chochote,....mimi siwezi kufanya mambo kama hayo nina kazi  zangu za maana, naaminika na serikali...’akasema

‘Usinifanye mimi mjinga....najua,...na ole wako, ..unidanganye nitafuatilia hatua kwa hatua....’akasema huyo mama, na mtaalamu akafahamu huyo mama anaweza kufanya kweli, ikabidi akili ianze kufanya kazi.

Kama nilivyosema huyu mama japokuwa litoa vitisho hivyo, lakini hakuwa na malengo ya kumshitakia mtaalamu, mtaalamu sio adui yake japokuwa hawaelewani sana , adui yake ni huyu mshitakiwa, lakini kwa vile ana tamaa ya pesa, akaona ni sehemu nzuri ya kupata pesa huku na huku, ..kutoka kwa mtaalamu na kutoka kwa mshitakiwa.....’akasema mpelelezi.

‘Ukumbuke kuwa pamoja na kuwa huyu jamaa ana makampuni, na ni mkurugenzi, lakini makamuni mengi hayapo kwa jina lake, yeye ni kama muwekezaji wa hisa tu....na kama mpiga debe wa kuwezesha ajira kwa vijana....lakini kuna hiki kipato kingi alichokuwa akikipata kwa njia isiyo halali, kutoka kwa watu mbali mbali kwa njia ya mlungula, lakini sio kwa kupitia yeye, bali kwa kupitia kwa mawakala mbali mbali,...’akasema mpelelezi.

‘Ina maana kwa kazi hiyo alikuwa akipata pesa nyingi.....mimi sioni ni pesa nyingi kiasi cha kumfanya aitegemee.....’akauliza

‘Mkuu, huyu mtu alishawaweka wakubwa wengi, matajiri wengi, mikononi, anajua shughuli zao zisizo halali,...na ili zisijulikane ...inabidi watu hao wadaiwe pesa nyingi....sio kwa moja kwa moja, .. hao watu ilibidi watoe pesa nyingi kuziba mambo yao,...inategemea ni mtu gani, na anashughuli gani...wengine wana shughuli kubwa, ...na malipo yake yatakuwa makubwa zaidi.....’akasema mpelelezi.

‘Huyu mtu alishaweza kuingiza mambo yake kwenye mitandao ya kibenki, ....anajau jinsi gani ya kuwaibia watu, kwa kupitia kwenye akaunti zao...akiwatumia mawakala wake,....’akasema

‘Kwa vipi...?’ akauliza

‘Wewe unapokea taarifa kwa mtu kuwa yeye ana shughuli, anamtaji, anataka kuwekeza na wewe,.... umpatia habari hizi na hizi,ili akutimie pesa...wewe usiyejua unampatia,..hizo hizo taarifa wanazitumia, wanakuibia kwenye akauntii zako za benki...huu ni mfani mdogo tu,...lakini kwa wakubwa, anatuma ujumbe kuwa nimegundua kuwa una shughuli hizi na hizi zinakuingizia mabilioni ya pesa...ili usifikishwe kwa sheria, toa asilimia kumi....

‘Kirahisi tu hivyo...?’ akauliza

‘Wanatumia mawakala wao, wanakwenda moja kwa moja kuonana na hawa wakuu, wakiwa na vielelezo, mkuu, huyu anaona sasa nitaumbuka, anakubali, anatoa pesa....’akasema

‘Haiwezekani, kirahisi hivyo....’akasema

‘Hujakutana na hawa watu, wanahakikisha wakimuendea huyo mtu wanakuwa na vielelezo vyote na ni sahihi kabisa....kama unafanya hivyo, utasemaje....wengine wanajaribu kupambana, lakini kila wakifanya hivyo, wanagundua ndio wanajiweka hatarini zaidi, inabidi watoa.....’akasema

‘Ok, lakini tunazunguka tu...hatujajenga hoja ya kwabana hawa watu, hatujajenga hoja ya washitakiwa hawa na hasa ukiunganisha na haya mauaji nataka kuwe na hoja ambayo itawashika hawa watu, maana kama wamefikia kuua, unafikiri itakuwaje, jamii itatuelewaje,....’akasema mkuu

‘Ndio tunaelekea huko mkuu, nakuhakikishia hili kundi tutalimaliza, na tatizo hili litakwisha kabisa hapa maeneo yetu...utaona mwenye mkuu, kwenye ushahidi wetu kila kitu kipo tayari, .....’akasema mpelelezi, na mkuu akawa kama anawaza jambo, akasema;

‘Una majina ya wakubwa waliowahi kupatikana na hizi shutuma.....na ...na hawa vijana mliwatumia vipi, watasimama mahakamani kutoa ushahidi ?... je ni huyu peke yake au ni nani mwingine anahusika....?’ akauliza  akionekana na mashaka fulani. Na mara simu ya muendesha mashitaka ikalia, anaipokea na akawa anasikiliza,

Alipomaliza kusikiliza simu akawageukia wenzake akasema;

‘Mimi naona mengi tutayaona huko mahakamani....mnaonaje, hii kesi ipo kamili, hakuna utata...nimeshajitosheleza na huu ushahidi, na kesho kesi inaanza,...kwahiyo mimi nawasikiliza nyie tu....’akasema muendesha

‘Haiwezekani kesho kesi ianze, na kama ni lazima ianze nataka uvute muda...usianze moja kwa moja, uahirishe kuwa bado hatujajitosheleza, kuna mambo bado sijarizika nayo, kwa masilahi ya taifa..’akasema mkuu.

Muendesha mashitaka akatabasamu.....

Kesi ikaanza kesho yake.....

*******

Bro mimi....nashindwa kabisa kuamini kuwa kijana wetu alitumiwa kuniangamiza mimi, na alisimama mahakami kutoa ushahdi dhidi yangu mimi,...hakuwa na huruma kabisa na mimi....

Hakujali kabisa kuwa mimi ni mzazi wake, ...hata kama sio baba yake wa kumzaa, lakini mimi ni jamaa yake, mimi ndiye niliyemtoa hatarini, mimi ndiye....hata hata....’ alisema profesa kwa uchungu, akimuangalia kaka yake ambaye alikuwa akimsikiliza kwa makini...

Kaka yake akatabasamu.....

NB: Haya kijana wetu anaanza kuonekana tuone anahusikanaje ni hili janga je ilikuwaje mpaka baba mlezi amuone huyo mtoto hafai na hataki hata kumsikia.


WAZO LA LEO: Kuwafanyia wenzako ubaya kwa vile tu hawakuhusu,...ya kuwa sio ndugu zako, sio wenzako, hata wao wakiingia matatani, hayakuhusu, ilimradi tu,wewe unaneemeka,  unapata masilahi yako, wewe ukijinadi kwa maneno ya kejeli...., ‘mjini hapa’...utambue kabisa hiyo sio neema, ...huo sio ujanja , hiyo ni dhuluma, hata kama utapata leo, utashiba, utajijenga, utakuwa kiongozi,  lakini ukumbuke hiyo ni dhuluma, na dhambi hiyo itakuandama maishani mwako hadi kaburini, na hapa duniani ipo siku utadhalilika tu...
Ni mimi: emu-three

No comments :