Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, October 24, 2014

DUNIA YANGU-52



‘Yah, nipe….’akasema , na alipoishika simu yake mkononi, akaanza kutafuta namba anayoihitajia na kuanza kupiga kuwasiliana na watu wake, lakini kila aliyempigia simu hakuweza kumpata, akajikuta akiguna.
‘Mhhh..hapa sasa kuna tatizo.’ Akasema akiendelea kumpigia mwingine na mwingine maka akawamaliza watu wake muhimu.
‘Mhh, vipi tena hawapatikani?’ akauliza Yule binti, mdada

Tuendelee na kisa chetu….

*************
‘Hawa watu hawapatikani kabisa, au kuna baya limewakumba….mmh, sijui nimpigie nani kwasasa, wengi wa hawa watu wetu siwaamini sana, ok, …., ngoja nimpigie mkuu wangu wakazi, sijui kama karudi kutoka mapumziko ya muda….’akasema na kuanza kuitafuta namba yake….

Alipoipata akapiga, simu kwanza iliita, lakini ikakatwa….., akajaribu tena, ikawa sasa haipatikani, akajaribu tena na tena lakini haikupatikana kabisa, akatulia kuwaza, akataka kusimama,lakini akasita, akasema;

‘Ni nani alinileta hapa hospitalini?’ akauliza.

‘Mimi sijui, mimi nimekuja, niliposikia umelazwa hapa, sikuuliza hilo swali, muhimu ni kukuona wewe…’akasema

‘Ni nani alikuambia kuwa nimelazwa hapa?’ akauliza.

‘Ni baba alikuja kunitembelea kuona maendeleo yangu ndio akakutana na taarifa hizo za mabomu, kuna siku alikuja kwako akakukosa, akapanga aje jana, ni jana vile...ndio akapata taarifa kuwa yamekukuta hayo….akanipa taarifa na mimi nikamwambia ni lazima nije nikuone….’akasema.

‘Oh, nashukuruni sana kwa moyo wenu huo wa upendo, sasa huyu docta yupo wapi?’ akauliza.

‘Alitoka muda ule ule kabla hujazindukana, na alisema kama kuna dharura nimpigie simu, au nimuite…’akasema.

‘Basi tafadhali naomba ukaniitie….’akasema na Yule binti akasimama na kuondoka, Inspecta hakuchukua muda, alismama na kuanza kuvaa nguo zake, alipohakikisha kuwa kila kitu kipo sawa, akasogea dirishani, madirisha ya hapo kwenye hiyo hospitali ni ya viyooo, unaweza kulifungua lote, akafungua na kuangalia nje, akaona hakuna mtu, akarukia nje.

*********
Inspecta Moto, alitembea kwa haraka hadi sehemu wanaposimamisha mabajaji, akaingiza mkono mfukoni, akaona pesa zake bado zipo, akamuambia mwenye bajaji...

‘Unaweza kunipeleka Msasani, makabaurini, ….’akasema.

‘Msasani makaburini, mhh, ni makaburi ya eneo gani, mmh….ni yale ya karibu na baharini?’ akauliza akionyesha wasiwasi.

‘Yah, huko huko…’akasema Moto.

‘Mhh, kule tunaogopa hata kwenda, maana siku za karibuni kumebadilika kweli, kumekuwa ni uwanja wa mabomu, lakini twende tu, nitakuacha sehemu karibu na eneo hilo mimi sitafika huko ndani maana hakuruhusiwi watu kufika kwa hivi sasa….’akasema.

‘Hamna shida , wewe twende utaniacha sehemu unayooona wewe ni salama kwako…’akasema na wakaondoka, huku dereva akiuliza maswali ambayo Moto hakutaka kuyajibu, alikuwa na mambo mengi kichwani;

‘Kwanini wewe unakwenda huko, wakati kuna tishio, mbona umefungwa mkononi, ulipata ajali nini, naona kama uliungua, unakuwa kama hao waliookolewa kwenye huo moto, nasikia waliungu sana, nasikia mpaka sasa wengine hawajiweza hata kuongea….’akawa anauliza na kuongea, lakini Inspecta alikuwa kimiya, akilini akawa anajiuliza imekuwaje taarifa kama hizo zizagae haraka mitaani.

Walipofika karibu na bara bara inayoingia kuelekea makaburini,yule dereva akasimamisha gari, na kusema;.

‘Mimi nitaishia hapa bosi wangu, huko ndani sifiki,… unaona kule, wapo wenyewe, wanacheza na vitu vya moto, wameshazungushia uzio wa hatari, kwahiyo safari yetu imeishia hapa…’akasema.

Inspecta akamlipa huyo jamaa pesa yake, na Yule jama bado akawa anamchunguza sana Inspecta kwa makini, lakini Inspecta hakumjali, yeye akaanza kutembea kulekea huko ndani. Na akachukua simu yake akapiga namba.

Inspecta hakugeuka nyuma, alitembea kuelekea  eneo la makaburini hadi kwenye ule uzio wa hatari,…akageuka kuangalia wapi walipo askari, bila kujali akauruka ule uzio , na alipofanya hatua chache mbele akatokea askari akiwa na silaha yake mkononi na vifaa vyote vya kinga mwilini, ni mmoja wa maaskari wanaolinda hapo, Inspecta Moto akamuonyesha kitambulisho, na mara akatokea askari mwingine akiwa kavalia kiraia tu, akasema;

‘Mkuu vipi unaendeelaje, maana mimi nilikuwa mapumziko, nilipofika nikakutana na hili jukumu, nasikia ulikuwa katika hali mbaya sana, mbona umerudi huku tena mkuu, wewe kapumzike tu mkuu, sisi tutahakikisha mamb hapa yapo shwari…’akasema askari mmoja anayemfahamu.

‘Hebu niambia mumegundua nini hadi muda huu?’ akauliza.

‘Hakuna zaidi mpaka sasa, jengo kama unavyoliona hapo, limeungua lote, hakuna kilichoweza kuokolewa, wasiwasi wetu ni kuwa huenda bado kuna mabaki ya mabomu chini ya ardhi, ndio maana tunaendelea kulinda hapa…’akasema.

‘Kuna watu nawatafuta,…..’akatulia, halafu akawataja majina.

‘Mhh, mkuu hao jamaa hali zao ni mbaya, walikuwa kama wewe, nashangaa wewe umeweza kuja hapa, kwa taarifa nilizo nazo, wengine bado hawajazindukana, nasikia mabomu hayo yana sumu, au madawa ya kulevya,ni mabomu ya aina yake ambayo hayajajulikana yametengenezewa wpi, au yametengenezwa na mchanganyiko gani…..’akasema.

‘Ok, kwahiyo kwa jinsi unavyojua wewe,…mmh’ akatulia kwanza akiangalia kwa mbele, kuna watu walikuwa wakipite eneo la baharini karibu na lile boti, ambalo bado lilikuwa hapo;

‘Kwani wakati tukio hili linatokea wewe ulikuwepo?’ akaulizwa.

‘Hapana mimi nilikuwa mapumziko, nimekuja baadaye wakati kumeshaanza kutulia, kwahiyo jinsi ilivyotokea mimi sikuona…na hakuna cha zaidi tulichoambiwa zaidi ya kuendeleza na ulinzi hapa….’akasema.

‘Yah, naona hutaweza kunisaidia kitu, maana kulikuwa na watu ndani ya hili jengo, nilitaka kujua kuwa waliweza kuokolewa au ndio wameteketea humo ndani wote, na kule karibu na bot kuna nani wapo huko….?’ Akauliza.

‘Nijuavyo mimi, jengo hili ni kama halishi watu, yupo jamaa mmoja anafika mara chache na kuondoka, wanahisi huenda ndiye mumiliki, lakini tukio likitokea hakuwepo, na uanuliza kule kwenye boti, wapo watu wa usalama, hakuna shida mkuu…’akasema.

‘Wewe umepata wapi hizo taarifa na ulikuwa mapumzikoni?’ akauliza.

‘Mkuu, ukikabidhiwa lindo ni lazima upate taarifa zote, vipi mkuu, naona ajali imekupoteza kumbukumbu nini..pole sana mkuu…ila….’akatulia kidogo.

‘Nilipofika ili kutimiza wajibu wangu, nikajaribu kupiga ndogo ndogo, huwezi jua, nikawa nawahiji baadhi ya majirani, watu wanaoishi eneo hili, nimejaribu kuwahoji baadhi tu, wakasema hivyo, kuwa ni kama jengo lililohamwa,…’akatulia.

‘Wanasema kuna jamaa mmoja anaonekanaonekana,  huyo jamaa wanasema huenda hata yeye sio mwenye jengo, ili kaamua kuishi hapo kwa kubahatisha, ili awe anawahi kwenye shughuli zake, na hata wakati moto unatokea, sizani kama alikuwemo humo ndani, kama unavyoona jengo halijulikani tena, kama kulikuwa na nyumba…’akasema.

‘Kwahiyo ulipowahoji hao watu walisema hata hiyo jana, hakukuwepo na watu waliingia humo kabla ya tukio?’ akauliza.

‘Yah, wamesema hapakuwepo na watu humo ndani,…wanasema kwa vile ni sehemu haishi mtu, hakuna aliyekuwa na shauku ya kuangalia, na bomu la kaburini lilipotokea, watu wakakimbia, kwahiyo hakuna anayejua kilichotokea, kama kulikuwa na watu au la…’akasema.

‘Ahh, ok…’akasema Inspecta alipoona anapoteza muda, lakini huyo askari kanzu akaendelea kusema;

‘Nimesikia kuwa nyie wakati mnaingia mlitupiwa nje na upepo,…inanishangaza ni upepo gani huo mkuu, …?’ akauliza.

‘Nani kakuambia ni upepo…hata mimi sijui,ndio tunachunguza hivyo…’akasema Inspecta

‘Kwa ujumla mimi nilichopata kwa watu ndio hivyo, hakuna maelezo kuwa kulikuwa na watu humo ndani, na hata wachunguzi wetu, walijaribu kuchunguza, kwa taarifa nilizopewa, hawakuona dalili za maiti, au mabaki ya watu kuwemo humo ndani mkuu…’akasema

‘Ok, basi ngoja nipitie mara moja nione kama kuna dalili yoyote ya kitu ninachokihitajia, maana hizi taarifa kwasasa zinaanza kuchakachukuliwa, tutaona mwisho wake itakuwaje, ….’akasema huku akitembea kuelekea sehemu ya gofu la jengo,…

‘Mkuu hakuna kitu kabisa, nimepita kila sehemu , sijaona kitu cha kusaidia, ila wewe nenda kaangalie, na kama unahitajia msaada nije tusaidiene huenda tukapata chochote, ila sizani….’akasema na Moto hakumjibu akaelekea eneo hilo, na Yule askari mwenzake simu yake ikapigwa, akawa anasikiliza na kumuacha Inspecta Moto akielekea kwenye tukio akiwa peke yake.

Alijaribu kuangalia upande ule ambao anafahamu kulikuwa na chumba cha pili, lakini hakuona dalili na kitu kama miili, kulikuwa na mabaki mabaki ya takataka, lakini hakuna mlunduikano wa kuashiria mwili wa mtu au kitu kama hicho, au mabaki ya mifupa…akajaribu kuchunguza zaidi, hakuna kitu.

‘Ina maana hao watu walitoka,..haiwezekani,..niliwaona kwa macho yangu, watu  wakiwa wamelala sakafuni, sizani kama walikuwa na uwezo wa kutoka kwa haraka vile bila kuonekana…’akasema akizidi kuchunguza zaidi.

Na wakati anaendeela kuchunguza huku na kule, akaona sehemu yenye matofali yaliyojipanga kinamna, na kutengeeza kama boksi, akavutiwa na sehemu hiyo, akaisogelea, akainua yale matofali, na kwa chini ya hayo matofali, akaona kitu…simu….

Akainama kuikota, kwa uangalifu, akasita, akachukua leso yake, akainama kuchunguza vyema, akaigeuza akihakikisha haigusi kwa mkono wake bila kinga, ilikuwa sio simu ni ‘flash’ za kuwekea kumbukumbu za komputa, ni zile flash kubwa kama simu…

Akawa na uhakika kuwa sio kitu cha hatari, akiwa na leso yake vyema mkononi akaikota ile `flash’  na akasimama na kugeuka huku na kule akaona mfuko mdogo mweusi wa plastiki, akaiweka ile flash ndani ya huo mfuko, na kuiweka ndani ya mfuko wake wa suruwali…

‘Ni ajabu kabisa, haikuguswa kabisa na moto, inaonekana ilidondoka baadaye, au kuna mtu alikuwa nayo mfukoni ikadondoka, na ilikuwa sehemu ambayo haikuweza kuguswa na moto.

Akakagua kila mahali na aliporizika, akaanza kuondoka, na wakati anatoka eneo hilo, Yule asksri mwenzake akaja kwa haraka na kumuuliza;

‘Kuna kitu chochote umekiona…?’ akauliza

‘Kama kitu gani?’ aakuliza Moto

‘Chochote cha kuweza kusaidia,…maana macho ya wawili sio sawa nay a mmoja…’akasema

‘Sijaona kitu ….’akasema Moto

‘Ok, hata mimi sijaona chochote, wanasema tujaribu kuangalia kila kona, kama kuna kitu chochote kinachoweza kusaidia, iwe simu, au chombo chochote cha komputa, hawa watu ni wataalamu sana….’akasema

‘Nani kakupa maagizo hayo?’ akauliza

‘Msaidizi wa Mkuu…..’akasema

‘Ok, hamna shida, ndio kazi yetu kufanya hivyo, …’akasema na mara simu ya Inspecta Moto ikawa inaita, akaipokea bila kuangalia mpigaji , akasema kwa haraka..

‘Nani mwenzangu…?’ akauliza

‘Ina maana huna namba yangu..?’ sauti ya msaidizi wa mkuu wake ikasika hewani

‘Hii namba ni ngeni,… mkuu, sikuwa nimeihifadhi kwenye simu yangu…’akasema

‘Ni hivi, mkuu hali yake ni mbaya, wakati wanakuja kutoka nyumbani,  kama unavyojua kuwa alikuwa mapumziko mafupi ya kumuuguza mzazi wake..sasa wakati anarudi kuwahi kuja kuwa ansi kwenye uwanja wa mapambano, wakiwa njiani akapatwa na ajali, na hali yake ni mbaya yupo chumba maalumu cha wagonjwa mahututi, ….’akasema.

‘Oh, hiyo ajali imetokea lini..ina maana ni siku hiyo ya tukio?’ akauliza.

‘Ni jambo la ajabu sana, ndio, ni siku hiyo hiyo yalipokuwa yakitokea mabomu, ni kama hawa watu walijiandaa kuhakikisha wanavunja nguvu zote….inavyoonekana hata hiyo ajali imepangwa, japokuwa hatujathibitisha, mpaka mkuu atakapoweza kuongea, sasa hivi hajiwezi kwahiyo hatuwezi kujua lolote …..’akasema.

‘Kupangwa kwa vipi?’ akauliza Moto.

‘Wewe huoni hilo, hayo mabomu yalipangwaje, yalipangwa kinamna, mnataka kukimbili ahuku, huku linalipuka , mnakuwa mumechanganyikiwa, hamjui muende wapi,…hata hiyo ajali  ilitokea muda huo huo, huoni kuwa kulikuwa na njama za kumuua,..’akatulia kidogo na Inspecta Moto akwa kimiya,

‘Anyway, uchunguzi unaendelea, cha muhimu ni nyie mpone haraka muingie kazini, maana hawa watu wanajiona wameshinda, hawajashinda bado, ni lazima tuhakikishe wote wamepatikana vipi wewe mbona nasikia umetoroka hospitalini…?’akauliza.

‘Umesema mkuu wetu kalazwa wapi?’ akauliza swali kabla ya kujibu swali la mkuu wake.

‘Hospitali ya Docta Chize, mara nyingi huwa anatibiwa huko..’akaambiwa.

‘Docta Chize, kwani huyu docta yupo?’ akauliza.

‘Yah, ..yupo kwani alienda wapi?’ akaambiwa,  na kuulizwa, na simu ya Inspecta moto ikakata mawasiliano, akaangalia, akaona ni mtandao umekata.

‘Hii ni ajabu kabisa, simu yangu haina tatizo la mtandao, ni kitu gani hiki, …..’akasema na kuzima simu yake halafu akaiwasha tena..na alipoiwasha akaona ujumbe unaingia kwenye simu yake, akausoma, ulikuwa na maneno machache tu

‘BADO WEWE….’


WAZO LA LEO: Utawala bora ni pamoja na kuwa karibu na wale unaowatawala, ukahisi uwepo wao, na shida zao. Hutaweza kuwajua na kujua shida zao, kama utakuwa mbali na watu wako, ukajiwekea mazingiza ya juu kuliko ya wale unawatala, huo utakuwa ni ubinafsi. Ni sawa huenda ni lazima mtawala awe na hali tofauti na watawaliwa, lakini utajuaje shida zao, kama hujapatwa na hiyo shida, je mwenye shibe kweli anaweza kumtambua mwenye njaa..najiuliza tu. 

Ni mimi: emu-three

No comments :