Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, August 27, 2013

WEMA HAUOZI-55


Mama aliendelea kusimulia kisa hiki, akielezea pale walipokwenda hospipitali kumuona mwanasheria wakiwa wameongozana na mwanadada, na wakiwa njiani , wote wlikuwa kimiya, kila mmoja akiwa katingwa na mawazo yake, na kila mmoja akimuomba mola wake, mwanasheria huyo apone, au wamkuta akiwa hai…..

Swali ni je, mwanasheria huyu alikuwa akitaka kuwaambia nini wanawake hawa wawili, ukumbuke kuwa mmoja ni aliyekuwa mchumba wake, na wa pili ni mke wa marehemu kaka yake na yeye alitakwia kumrithi huyo mama kutokana na mila  na desturi zao….

Sasa endelea na sehemu hii uone ni nini kilitokea,

*******
Mwanasheria alifunua macho taratibu, na kuangalia mbele, na pale macho yake yakakutana na mwanadada. Mwanadada alikuwa hakuziweka nywele zake vyema, ahapo akatulia na kumwangalia kwa muda, akapitisha ulimi mdomono kama anataka kuongea kitu, lakini hakuongea, na kama kakumbuka jambo, akageza mboni za mcahp na kumwangalia mwanamama, hapo napo akatulia kwa muda,… halafu akafumba macho., na michirizi miwili ya machozi ikaonekana kitoka machoni.

Ilipita muda kukiwa kimiya, na wakina mama hawa wawili, waliona huenda mgonjwa hawezi kuamuka tena kwa wakati huo, na wakawa wanangaliana kila mmoja akisita kuongea kila alichokuwa nacho moyoni, na ikafika muda mwanadada akitaka kuongea, na alipoanza kupanua mdomo akitaka kuongea, akasitishwa na sauti kutoka kwa huyo mgonjwa, ikisema;

‘Nashukuru mumefika, na sikutegemea kuwa leo ninaweza kuamuka na kufungua huu mdomo,na nashangaa leo najiona nina nguvu, na … lakini nafahamu huenda imetokea hivi ili niweze kuongea na nyie, maombi na dua yangu huenda imetimizwa, kwani wanasema kila mmoja anapokaribia kufa, mola humpa muda, ili aweze kujitetea kwa mara ya mwisho….’akatulia akawa kama anakohoa kidogo.

‘Nahisi hivyo, kuwa mola kanipa muda huu, ili niweze hata kutubu dhambi zangu, …ahaa…dhambi, kila mmoja ana dhambi zake nyingi tu, ….lakini la muhimu kwangu mimi juu yenu na ili niweze kutoa maagizo muhimu, ambayo nafikiri ni muhimu kwangu kufanya hivyo, …ninachoshukuru ni kuwa nyie mumefika kutii maagizo yangu….kwani naogopa hata kukutana na ndugu yangu tena, kwani kila mara ananitokea na kunilaumu…..’akatulia na mwanadada akasogea karibu, lakini mwanamama alisimama pale pale alipokuwa amesimama, mbali na kile kitanda alicholala huyo mgonjwa.

Yule mgonjwa alifunua macho yale pale alipohisi mtu yupo karibu naye, na akaayfunua kumwangalia huyo aliyekuja kukaa karibu yake, na macho yake yakakutana nay a mwanadada ambaye alikuwa kakaa karibu naye, huku akimwangalia kwa macho ya huzuni, yule mgonjwa akafumba macho yake huku akisema;

‘Nakuomba na wewe mwanamama usogea karibu maana sauti yangu inaweza ikawa ya shida kusikika, na nataka nyote msikie kile kitu nitakachowaambia….’akasema na hapo mwanamama akasogea na kuja kusimama karibu, hakukaa karibu na kile kitanda kama alivyofanya mwanadada, yeye alisimama pembeni huku akiwa kaweka mikono yake kifuani, kama anaomba ….au kuogopa….

‘Naomba mnisikilize kwa makini, huenda …..sijui, lakini dalili zote zipo, wanasema ukiwa katika hali kama hii, ya kukaribia kukataa roho, huwa unajiona, na dalili mojawapo ni kujiona unakuwa karibu na waliotangulia,…utajiona  unawaota, marehemu…., basi ujue safari imeshafika,…na mimi sioni kwanini isiwe hivyo, maana nateseka kwa maumivu….na kila mara najiona nipo na ndugu zangu waliotangulia….na hawaishi kunilamu…’akatulia.

‘Pindi tu, nilikuwa na marehemu, mume wako mwanamama, na amekuwa akinilaumu kuwa nimeshindwa kutimiza ahadi zangu, nilzomuahidi kuwa nitawatunza wewe na mtoto, kuwa sitawatelekeza na ya kuwa nitazilinda mali zenu……lakini anasema sikufanya hivyo, na nimekuwa nikishirikiana na watu wanaotaka kumdhulumu mke wake na mtoto wake…..nikashangaa sana…’akatulia.

‘Je ni kweli nimeyafanya hayo….sikusita kumwambia kuwa mbona namejitahidi kutetea mali yake kama alivyoagiza, na ….cha ajabu aliniambia kuwa mimi ni mnafiki, muoga, na uanasheria wangu hauna maana katika familia, na sistahili kuwa kiongozi wa familia….’akatulia.

‘Ndugu yangu huyo aliongea mengi, na kudiriki kusema kuwa nimeshindwa hata kutimiza lile agizo kuwa nimchukue shemeji awe mke wangu,….na huku wakati alipokuwa duniani, nilikuwa najifanya nampenda, sasa kaondoka, ninampa mgongo….shemeji nakiri kuwa kweli nilishawahi hata kumwambia kaka yangu huyo kuwa nakupenda, lakini nilisema yale kama ….na nisingeliweza kuwa na mawazo hayo kuwa kifa nikuchukue…..lakini ikatokea hivyo’akatulia.

‘Sasa nifanyeje…?’ akawa kama anauliza na kumwangalia mwanadada.

‘Kaka yangu aliniambia sina la kufanya maana nimechelewa…..nimeshindwa kutimiza ahad hadi maafa yametokea, kwahiyo sifai tena…..’akatulia.

‘Nikamwambia kama nimechelewa ni nani atakayeweza kuwalinda, familia yake, na mtoto na ni nani atakayeweza kuzirejesha mali za mkewe na mtoto?’ akakohoa kidogo

‘Aliniambia keshapatikana mtu wa namna hiyo, na kila kitu kitarajea kwa mkewe na mtoto, haki ya mtu haipotei bure, lakini sio kwa kupitia kwangu, mimi nimeshindwa huo mtihani, iliyobakai nirejee huko walipo nikasubiri hukumu…na ndio maana nataka kutubu dhambi hizo za kushindwa kutimiza aahdi ay ndugu yangu huyo….’akasema

‘Nikasema naomba muda mwingine ili niweze kuyafanya hayo, yeye akasema hana mamlaka na hilo, kwani hata yeye aliwahi kuomba hivyo, lakini hakuweza kupewa huo muda, mwenye mamlaka hayo ni yule yule aliyetupa roho, na ndiye anayefahamu ni lini mja wake atareja  kwake, yeye hajui na wala hana uwezo wa kunitetea….’akatulia.

‘Basi ndugu yangu huyo akaniambia `karibu kwenye makazi ya kudumu….lakini hakikisha umeongea na mke wangu na huyo ambaye ni mtetezi wa haki, na kuwathibitshia kuwa hayo wanayotenda ni halali , na mafanikio yapo mbele yao…hiyo ndio kauli ya marehemu kaka, na alisema nihakikishe nimewaambia hivyo…’akatulia.

‘Lakini akasisitiza, kuwa kama nitapata muda, wa kurejea basi nitimize hayo muhimu ambayo aliniagiza, lakini sio kwa kutetea mali kwani yupo tayari mtetezi, …na nisimuangushe kwa hayo mengine, lakini yeye hana uhakika kuwa mimi nitapata muda huo tena…’akatulia halafu akamwangalia mwanadada,

‘Kwasababu hiyo mimi inabidi nikushukuru sana mwanadada kwa juhudi zako, nashukuru kuwa wewe umeweza kufanya yale ambayo mimi nilishindwa, kwasababu ya kugubikwa na wimbi nzito la kifamilia,…sikujua kuwa nilikuwa kwenye mtego, kumbe wenzangu walikuwa wakinitumia kwa maslahi yao binafsi..’akatulia.

‘Sikujua kuwa hata mtalaamu ambaye nilimwamini sana, na nikawa ninamshauri na kumuelezea kila kitu, nikijua yeye ni ndugu na rafiki wa kweli, ….lakini kumbe alikuwa ni adui namba moja wa familia yetu…’akatulia.

‘Niligundua hayo, hata kabla hatujafunga safari ya kwenda huko msituni kwani katika moja ya mipango yake ya hivi karibuni, ilikuwa ni kuniua mimi baada ya kugundua kuwa nimeshamfahamu …..kwani kuwepo kwangu kungemfanya ashindwe kukamilisha mipango yake, ya kumiliki ardhi yote, ….na hayo alishafanikiwa kwa kiasi kikubwa, kwani ana hati zote za kumuliki eneo lote la kwetu na la kwao….’akatulia

‘Je alipaatje hizo hati, ….nilishindwa kujua, ….nilishindwa hata kumfahamu kuwa ni ndumila kuwili,…huwezi amini alivyokuwa akijibadilisha, kumbe yote tuliyoona kuwa alikuwa akifanya kiongozi wa kijiji, kumbe ni yeye aliyekuwa akifanya, kwa vile wanafanana na  mzee wetu huyo…na aliyafanya hayo kwa ujanja wa hali ya juu, lakini kila mkosaji hawezi kufuta nyayo zake zote, …..’akatulia.

‘Nilikuja kumgundua pale mzee wetu huyu yupo mahabusu, …na kukatokea matendo ambayo yalionyesha kuwa ni mzee wetu huyo ndiye aliyekuwa akiyatend, nikawa najiulizaa iweje, ina maana kweli mzee wetu huyo ana nguvu za giza kiasi hicho, aweza kutoka jela, na kwenda kuyafanya hayo na kureeja bila ya walinzi kufahamu…sikuamini…nikataka kuhakikisha hilo’akatulia kidogo.

‘Siku moja, nikafuatilia, na jamaa yetu huyo alipofanya hayo aliyotaka kuyafanya….ushaihid muhimu ni pikipiki, japokuwa alikuwa akibadili mara kwa mara kwa kukodi pikipiki tofauti. Na siku moja nikaingiwa na wasiwasi na pikipiki, iliyokuwa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi huyo mtalaamu, nikataka kujua huyo mtu ni nani…..pindi kidogo akatoka mtu, akiwa kashikilia mawani makubwa, alipotoka alichelewa kuyavaa,...

Hutaamini , na sijui kwanini nilifanya hivyo, nilichukua simu yangu ambayo kwa muda huo ilikuwa mkononi na kumpiga picha, kwa haraka…. akachukua pikipiki na kuondoka, na mimi nikamfuatilia kwa nyuma kwa pikipiki, nikamuona akielekea msituni….nilijaribu kumfuatilia lakini sikuweza kwenda zaidi..siku hiyo sikuweza kufahamu ni mtu gani huyo…’akatulia.

‘Ile picha nilipoiangalia vyema, nilimuona ni mzee wa kijiji, nikawa na wasiwasi na hapo hapo nikapiga simu kituo alichowekwa mzee wa kijiji, kuhakikisha kuwa kiongozi huyo yupo huko jela, na maaskari  wakaniambia yupo huko jela, nikawaomba niongee naye na wakawa wakanipa nikaongea naye….

‘Nimekuja kugundua haya, baada ya safari hiyo tuliyokwenda sote huko msituni kuwa kumbe ni huyu jamaa alikuwa akituchezea,… na ukurudi nyuma na kuanza kuunganisha haya matukio yalivyokuwa unaweza kugundua kuwa kumbe ndio yeye…..’akatulia kidogo.

‘Yeye ndiye aliyesimamia kuchomwa moto kwa nyumba ya mama mkunga, akiwa katika umbile la kiongozi wa kijiji, maana kweli siku hiyo kiongozi wa kijiji alikuwa hayupo, na hayo mimi nilifanya uchunguzi na kugundua kuwa kweli hakuwepo…ndio maana nikawa nyumba yake kumtetea…’akatulia.

‘Lakini ukimtetea yeye, ina maana unamweka ndugu yangu marehemu,….nd dnio maana nikawa mnzito kumtetea huyu mzee, maana jinsi ilivyo kaka yangu kama wanavyomuita jemedari angelikuwa kwenye hatia,…na ndivyo ilivyojulikana, ….na hapo nikawa na kigugumiz, na kujiuliza kama sio huyo kiongozi wa kijiji ni nani mwingine, …kwa haraka haraka kila mmoja alifahamu kuwa ni kaka yangu, na hata mimi mwenyewe nilifahamu hivyo….’akatulia.

‘Huyu jamaa yetu alikuwa mjanja sana, kwani alijionyesha kaika jamii, kuwa yeye haruhusiwi kuvua yale mangua yake ya kiganga, kuwa ni mwiko kuyavua hata mahakamani mlimuona akiingia nayo, na yale manyoya na …jinsi alivyo kuwa usingeliweza kuijua sura yake halisi…’akatulia.

‘Mimi nilipoanza kumuhisi vibaya, nilijikuta nikimchunguza kwa karibu, kwanza baada ya kumsikia kuwa katoweka, nikawa namtafuta yupo wapi…haikuwa kazi rahisi kumgundua wapi alipokwenda, kwani hali yake ya awali ay kuvaa mavazi yale ilikuwa ndio chumba chake cha siri, na akijitoa kwenye hali hiyo, huwezi kumgundua tena, na hapo huwa nasi na kuweza kugundu  ni nini kinachoendelea…’akatulia.

‘Siku alipotoka mahakamani kutoa ushahidi mimi nilimfuatilia, akijua kuwa hakuna anayemfahamu, alipotoka hapo, alikwenda moja kwa moja kwenye jengo bovu, ambapo, alibadili yale mavazi yake, na kuwa mtu wa kawaida, …alipoondoka mimi niliingia na kuyaona yale mavazi yake, yaklwa yamefichwa,…na hapo nikagundua kuwa huyu mtu anajigeuza kwa njia hiyo,…kumbe, …..

‘Lakini wakati anatoka pale alikuwa kavaa mawani makubwa, usingeliweza kumgundua kuwa ni yeye, ….na kwa vile nilikuwa nimepoteza muda, kuingia pale alipoficha mavazi yake, sikuweza kumfuatilia tena huko alipoelekea…lakini nikakumbuka tukio la nyuma la huyo mtu niliyemuona nyumbani kwa mtaalamu, na nikagundua kuwa ni yule yule….japokuwa sikuwa na uhakika kisura, maana nilimuona kwa mbali…’akatulia

‘Ila niligundua kitu,mwili wake, na viatu alivyokuwa kavaa…ambavyo, tulipofika huko msituni, ndivyo alivyokuwa kavivaa siku hiyo….alikuwa mjanja, kiasi kwamba, hakufanya makosa lakini kosa hio akalifanya, …’akatulia.

‘Pamoja na yote ndugu huyu ni mpenda wanawake sana, hasa wasichana vigoli….na mmoja wa wasichana aliokuwa akiwataka ni msichana wa mkuu wa kituo cha upelelezi, na hapo niliweza kupata fununu…niliwahi kuongea na huyo binti, kipindi cha nyuma, na japokuwa alikataa kunielezea, lakini kwa kupitia kwa rafiki yake wa kiume, niligundua kwua msichana huyo alikuwa na mwanaume anamzuzua…kwani rafiki yake huyo wa kiume, alikuwa kamuhisi na alikuwa kilalamika…

‘Jamaa yetu huyu, alitumia kipaji alichopewa vibaya, kwani kweli alikuwa na uwezo wa dawa, kweli alikuwa na uwezo wa kutengeneza mazingara ya kumfanya mtu awe na mfadhaiko ambao ndio hayo tunayoyaita mashetani, na kila binti aliyemtaka, alimbambikia mambo hayo, na huyo binti anajipeleka mwenyewe kwa huyo jamaa bila kufahamu ni kitu gani anakifanya….’akatulia.

‘Kwahiyo huyo binti atakwenda hadi anapotaka huyo jamaa na kujikuta kafanyiwa uzalilishaji, na ila hali ikimuisha,anakuwa hajitambui ilikuwaje…na ni nani kamfanyia hivyo, na hukimbilia kusema kafanyiwa hivyo ni jinni mahaba….’akatulia.

‘Niliposikia kuwa huyo binti ana mashetani na huwa yakimpanda anaweza kupotea, mimi nikaingiwa na hamasa ya kutaka kujua huwa anapotea kwenda wapi….na wakati nafanya hayo, sikuwa na mawazo ya kuwa jamaa yetu huyo ndye anafanya hilo,na sikuwa nimelifanya hili kutokana na kesi yetu,  …..hapana nilifanya hivyo kwa vile nilitaka kugundua haya mambo yapoje,…ilikuwa kama sehemu ya kupoteza muda na kugundua mambo yanayotokea hapa kijijini kwa njia yangu ya kipelelezi…..

‘Huyu binti keshapotea mara kadhaa, na mojawapo nilimgundua akieleekea huko msituni…nilimfuatilia siku hiyo, na sijui nilikuja kupatwa na kitu gani, kwani nilipofika eneo la msituni, nikajikuta nimedondoka na kupoteza fahamu, nilipozindukana ilikuwa imepita nusu saa, na sikuona haja ya kuendelea kufuatilia nilirudi nyumbani, nikijua kuwa nimeshindwa kuweza kumfuataili huyo binti.

‘Sasa ..ukiunganisha haya yote, ….kupotea kwa huyo binti,….kumuona huyo jamaa akijibadili, na kueleka msituni, nikaanza kuunganisha haya matukio, …..lakini bado sikuwa nafahamu kuwa huyu jamaa ndiye mtaalamu, …’akatulia.

‘Niligundua hilo siku ile alipokuja kutoa ushahidi..na nikayapiga yale mavazi yake picha, …na nikawa na hamu ya kuongea na wewe kukuelezea hicho nilichogundua, lakini wewe ukawa hutaki….na ilipotokea nafasi hiyo ya kwenda huko msituni, nikaona sasa nakwenda kuhitimisha uchunguzi wangu…’akatulia.

‘Kwahiyo kutokana na uchunguzi wangu, wote walioshikwa nyuma hawana makosa, kama wana makosa ni yale yakutumiwa kiujanja na huyo jamaa, bila ya wao kujua, ….nawaambia hili ili mkienda mahakamani muwe makini na huyu mtu…pamoja na ujanja wake, pia anafahamu sheria, …muwe makini kwa hilo, lakini pia muwe makini na watu ambao ni muhimu, anaweza kuwaua wote ili kupoteza ushahidi…hasa kiongozi wa kijiji, mlindeni sana….’akatulia na akawa anahema kwa shida.

Mwanadada akageuka kuangalia kile chombo cha kuonyesha mapigo ya moyo, na akaona kama kinaanza kuonyesha ishara mbaya, akamwambia mwanamama ;

‘Nenda kamuita docta haraka….’akasema lakini mwanasheria akasema;

‘Wamesema kuwa wameshaidhibiti ile hali mbaya,, na iliyobakia nikuuguza majereha….nashukuru kusikia hivyo, na najua kama dakitari kazi yao ndio hiyo kumpa matumaini mgonjwa hata kama wanafahamu kuwa hatapona… msihangaika, …kumuita docta.’akatulia.

‘Lakini hayo yote ni mapenzi ya mungu, ninachotaka kusema hapa, ni kuwa kwanza pendaneni, kama ndugu,…kama nitaondoka, basi majukumu ya kumtunza,….mtoto, majukumu ya kifamilia, nakuachia wewe, mwanadada, nafahamu kuwa wewe hujawa familia yangu kwani hatujafunga ndoa, lakini wewe unaweza kumsaidia zaidi kuliko ndugu yoyote,kwenye familia yangu, na familia yangu, wote waliobakia ni wakorofi ….’akatulia

‘Kwanini nasema hivyo, ni kutokana na yaliyotokea, siwaamini tena ndugu zangu,….sikujua kuwa kuna mambo kama hayo ndani ya familia yangu,kwangu familia ilikuwa kila kitu,…hata hivyo siwezi kuwalaumu kwa hali iliyopo , maana ndivyo maisha ya kijijini yalivyo, …na ndivyo alivyoweza kuwahadaa watu wengi hapa kijijini huyu jamaa yetu ….ambaye wengi walimuamini sana.

‘Huyu jamaa alichukua muda kuwasoma watu, na akajua udhaifu wao, na ndipo akatumia mbinu alizo nazo, kwanza kwa kuwajengea imani kuwa yeye ni mtaalamu aliyetumwa kukilinda hicho kijiji, na hilo aliweza kulihalilisha kirahisi kutokana na kipaji alichokuwa nacho, kuwatibia watu na kuwabashiria mambo mengi, na aliweza kufahamu mengi yaliyokuwa yakitokea ndani ya familia,….kumbe alikuwa kasambaza waya na vyombo vya kuansia sauti sehemu nyingi, tu, kama mlivyoona ile antenna kule porini….’akatulia

‘Kila mtu alikuwa akishangaaa iweje mnaongea ndani, kesho yake, jamaa huyu anakuja kukuambia ulichokuwa ukiongea wewe na mkeo….watu wakafahamu huyu sio mtu wa kawaida, kweli ni mtalaamu….’akatulia kidogo

‘Ninafahamu kabisa sasa hana ujanja, na ili asiweze lolote, hakikisheni yule jamaa tuliyekwenda naye msituni yupo….ili kama kuna hadaa za kimazingara, muweze kumshinda,…..yule jamaa anamfahamu vyema huyu ndugu yetu,….hilo ni kazi kwenu….’akatulia kwa muda kiasi kwamba wakimama hawa wawili wakaingiwa na shaka, na mara huyo mgonjwa akasema;

‘Sasa basi kwanza kabisa, nimekuita mwanadada, ili uhakikishe unafuatilia hati zote za nyumba, hati zote za duka, hati zote za shamba, ambalo ni mali ya mwanadada, uhakikishe zinaandikwa kwa jina lake….nimeshaongea na wakili wetu, ambaye ndiye alisaidiana na mimi kuweka hivyo vitu vyote kwa jina langu, ila hilo shamba sikuwa na ufahamu nalo..lakini kwa vile kila kitu kitawekwa wazi huko mahakamani, ni jukumu lako mwanadada kuhakikisha vyote hivyo vinakuwa mikononi mwa mmiliki halali…

‘Nakuambia hivyo maana kila nikipitiwa na usingizi ndugu yangu huyo hunijia huku akinilaumu kuwa kwanini sifanyi hivyo, kwanini sikuambii ufuatilai hayo, ya hati miliki,…na naona ni kweli unahitajika kuyafanya hayo kwa haraka iwezekanavyo, kwani yupo ndugu yangu mkorofi, haelewei sheria, na ni mtu anayependa shari, sasa mtasumbuana naye sana kama nitakufa…kabla mambo hayo hayajawekwa sawa….’akatulia

‘Kama nitapona...oh, mungu wangu sijui, ...ila kama nitapona, kitu ambacho sitegemei, basi tutasaidiana kwa hilo….na dhamira yangu ya kweli ni kama nilivyokuambia mwanadada,kuwa kitu cha kwanza ni kufunga ndoa mimi na wewe, na kuhusu mwanamama, wewe ndiye utakayekuwa na maamuzi na hilo…wewe utaamua, kama …..kama ...oh, kama...’akawa anashindwa kumalizia, na kugeuza kichwa kumwangalia mwanamama ambaye alikuwa mlangoni, akitaka kwenda kumuita docta.

Kukawa na ukimiya na mwanadada ambaye alikuwa kazama kwenye mawazo, akageuka kumwangalia mawanasheria huyu, akamuona kafumba macho, na hatikisiki, na alipoangalia kule kwenye mashine ya kuonyesha mapigo ya moyo,akaona ile misitari ikianza kunyooka,…

‘Muite docta haraka….’akasema mwanadada na mwanamama akatoka mbio akiita;

 `Doctaaa…..
Mwanadada, akabakia akiwa kashika kichwa kama mtu aliyechanganyikiwa, akiwa keshakata tamaa, ……
NB: Je ndio mwisho wa haya yote, tuwe pamoja kwenye hitimisho la kisa hiki.

WAZO LA LEO: Haki inapotolewa kwa ubaguzi, inapoteza thamani yake ya kuitwa haki, kwani haki ni haki kwa kila mtu anayestahili kuipata. Kila mwenye dhamana na hili awe makini katika kuigawa au kuisimamia haki, asijali, jinsia, dini au kabila,….ukianza kuangalia hayo katika kuitoa haki, hiyo itakuwa sio haki tena, na huo utakuwa mwanzo wa kuleta mfarakano na manung’uniko katika jamii, na lolote baya likitokea, ujue wewe ndio chanzo, na hukumu ya mungu hutaweza kuikwepa. 

Ni mimi: emu-three

No comments :