Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, November 30, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-55


Tukiendelea na kisa hiki, nakuomba urejee sehemu ya kwanza kabisa wakati tunaanza hiki kisa, ambapo utakuta muhusika ambaye ndiye aliyekuwa akituhadithia kisa hiki ni Maua, hatua ya hitimisha tutakutana na mhusika mwingine. Kabla ya kufika kwenye hitimisho, tutamalizia sehemu hii ambayo inaturejesha pale tulipoanzia. Kisa hiki kina hatua sita, na hatua ya saba ni hitimisho, hitimisho hili ndilo litaelezea nini hasa kilitokea, hadi kufikia hapa tulipo, kwasababu kila jambo lina chanzo chake, wengi wetuu tunapenda kuangalia juu, juu, bila kujali asili ya jambo. Mhusika mkuu ndiye atakuchukua jukumu la kuhitiisha kisa hiki, na hatujui hitimisho hili litakuwa an sehemu ngapi, tuwe pamoja,tuone

********
Vigelegele vilitanda hewani, ikimaanisha kuwa kuna shughuli , na shughuli yenyewe ni ya heri. Vigelegele hivyo vilimshitua Mua toka katika dimbwi la mawazo, na kujikuta akisema, `hivi hii ni kweli au naota, ina maana ndio naolewa tena,….oh, ndio hivyo tena nitafanyaje, yote ni mapenzi ya mungu, kama alipanga iwe hivyo, hakuna wa kumpinga, ndoto yangu ya kuwa na wajukuu na mume niliyempenda imeshayeyuka, sasa naolewa bora kuolewa, sijui, kama itabadili ile ladha ya upendo niliyokuwa nayo awali, sijui…mungu wangu nisaidie ….’akasema akajikuta akiinua mikono juu na kujifuta usoni,...

Mikono yake ilikuwa imejaa majii ya machozi, na kilichosambaa usoni ilikuwa maji ya machozi. Maua akasimama toka pale alipokuwa amekaa kwa muda, aliona ni vyema kujishughulisha na hili au lile, ….hali ile ya kubakia peke yake, alishaizoea, lakini kutokana na shughuli iliyopo mbele yake alihitajika kutokubakia peke yake, alitakiwa kuwa na mpambe wake, …lakini mpambe wake alikuwa kiguu na njia, hatulii, ana mambo mia kidogo. Kila mara alikuwa kipokea simu za wateja wake, na wakati mwingine, ailibidi aombe zarura kukimbili ajambo fulani, atachukua pikipiki ya haraka, na baada ya dakika kadhaa kesharudi, …

‘Maua hapa tumecheza bugu, huyu mpambe kweli mpambe, lakini usitie shaka, ilimradi tupo name, hakitaharibika kitu…’akasema shangazi yake aliporudi na kumkuta Maua yupo peke yake. ‘Shangazi usijali mimi hali kama hii nilishaizoea, …’akasema Maua kujikosha, lakini moyoni aliona ni bora kuwa na mtu kuliko kubaia mwenyewe, alishangaa kwanini alikuwa na waiswasi isivyo kawaida, na katika kumbukumbu zake,hakuwa na tabia hiyo, hali hiyo ilimkumba tu baada ya kuonana na huyu tajiri, tangu siku ile alipopata masaada wa gari na kuanza kuonana naye, moyoni akawani mtu wa wasiwasi .

Alipomkumbuka huyu Tajiri, mara akakumbuka tukio la jana , ni tukio ambalo liliacha gumzo mitaani, na Maua akalitafsiri kama moja ya vikwazo vya kufikia sehemu nyingine ya maisha, maisha ya ndoa ya pili. Kikwazo hiki kilimpa fundisho, ingawaje fundisho hili halikumwingia akilini, hasa ukizingatia kuwa yeye hana tabia ya kuamini mambo ya imani za giza. Alijikuta akimwanza Tajiri Papaa, hakuamini kutokana na maeno ya watu aliyosikia, kuwa tajiri huyu mkubwa angeliweza kujihusisha na mambo hayo ya kishirikina….hapana, kwake yeye alijua kuwa watu wanaojihusisha na mambo hayo ni watu masikini, watu wa hali ya chini, ….

Maua alipowaza haya, yalimfanya kuwafikiria matajiri wengi anaowafahamu ambao utajiri wao hauna tofauti na utajiri wa jamaa huyu. ‘Kama ni hivyo basi haina maana ya kuwa tajiri……’akajikuta akisema, akiwaza kuwa huenda asilimi kubwa ya matajiri ambao utajiri wao umetokea ghafla huenda wanajihusisha na mambo hayo, lakini hata hivyo, akili yake iilikuwa haikubali kusadiki hivyo, licha ya tukio la jana ambali liliganda kwenye vichwa vya kila mmojawapo kuwa tajiri Papaa utajiri wake umetokana na nguvu za giza….

Kitu cha ajabu baada ya kupata taarifa kuwa tajiri huyo kapata ajali mbaya sana , kwani alipotoka pale alikuwa kama mtu aliyepagawa, labda kutokana na kuona aibu, au kuzalilishwa, au vinginevyo, aliondoa gari lake kwa mwendo wa kasi sana, na karibu agonge watu, na alipoingia barabrani, aliendelea na mwendo huo wakasi huo wa kasi, bila kujali magari mengina na kujikuta akikosakosa kugongana na magari mengine.

‘Wewe muhuni, hujui kuendesha gari nini…,’ madereva wengine walisikika wakimtukana na wengine hata kusimamisha mgari yao pembeni na kutoka nje wakiwa na lengo la kumfuta kwa kumkimbiza kwa miguu, lakini kila aliyeliona hilo gari, kwanza alishangaa, kwani mwenye gari hilo ni mtu anayejulikana sana, na anajua kuendesha vyema, aleo imekuwaje, na wengine wakahisi huenda gari lake limechukuliwa na wezi, na huyo mwizi alikuwa akitafuta njia ya kukimbia nalo.

‘Siamini kuwa ndio yeye, lazima kuna jambo…’wengine waksema huku wakiingia ndani ya mgari yao na kondoka. Lile gari lilipofika kwene njia panda, ambapo lilitakiwa kupinda kushoto au kulia, kwani barabnra hiyo ilifika kikomo na kutengeneza matawi ya barabra mbili ya kwenda kushoto au kulia, gari hilo halikufanya hivyo, likafululiza moja kwa moja na kupanda tuta kubwa lililokuwa mbele yake. Tuta hilo lilikuwa kubwa sana, na ukilivuka hilo tuta unandokea kwenye shimo kubwa sana.Shimo hilo limetokana na uchimbaji wa kokoto, kwani eneo hilo mwanzoni lilikuwa likichimbwa kokote, baadaye likapigwa marufuku na serikali, hata hivyo kokoto zilikuwa hazipatikani tena, kwahiyo kukabakia gema kubwa sana.

Inasemekana mwazoni kulikuwa na barabara inayokatisha hapo kwenda moja kwa moja, lakini mvua na uchimbaji wa kokoto, zikaporomo hiyo barabara na ikawa haipitiki tena, na wachimbaji wa kokotoa wakaibomoa kabisa. Lile gari lilipofika eneo hilo halikugeuka kushoto au kulia, lilinyosha moja kwa moja, na kukutana na hilo tuta kubwa na mbwele yake likagonga mti wa umeme uliokuwa ambao ulikuwa pembeni kabisa la hilo shomi, na kama isingelikuwa huo mti wa umeme, gari hilo lingeserereka na kuzama kwenye hilo gema.

Kilichotokea ni hilo gari kugeuka juu chini, kichwa kikigeukia huko lilipotoka. Ule mti wa umeme uliinama lakini haukudondoka. Gari lile kwa ajili ya mwendo kasi lilipanda lile tuta kubwa na lilipogonga ule mti, likaguke juu chini, na haikuchukua muda likawaka moto. Watu walioshuhudia tukio hilo, walisema ilichukua muda mchache sana kwa gari hilo kuwaka moto, na bahati nzuri, haikuchukua muda mrefu, gari la kuzima moto likawa limefika, kwani magari hayo hayapo mbali na hapo tukio lilipotokea.Gari la zima moto lilipofika liliwahi kuuzima ule moto kabla haujawa mkubwa,...

Maaskari polisi na uaslama barabrani wakawa wmaeshafika na kuanza kufanya kazi yao.
‘Afande mbona hakuna mtu humu ndani…’askari mmojawapo akawauliza wenzake.

‘Haiwezekani , hebu angalia vizuri, …”akasema mwenzake, ambaye naye alijaribu kumsaidia mwenzake kutizama ndani ya mabaki ya lie gari,lakini hawakuona dalili ya mtu au kiwiliwili cha mtu, hata walipoongezeka kuwa watatu, hawakuweza kuona chochote. Hata mashine maalumu ya kulitanua lile gari, lilipoletwa na kutanua lile gari, ili kuona vyema kwa ndani halikusaidia kitu, kwani kulikuwa hakuna dalilia ya kuwepo mtu mle ndani.

‘Hakuna mtu humu ndani, ina maana basi huyo dereva aliwahi kuruka kabla ya kutokea hii ajali…’akasema askari mmojawapo. Na hapo ikabidi waanze kazi ya kuwahoji watu, walioshuhudia hiyo ajali kuwa walimuona huyo dereva akiruka baada ya kutokea hiyo ajali au kabla hilo gari haligonga huo mti wa umeme na huenda wamuwahi kuona wapi alipoelekea.

‘Hakuna mtu aliyeruka, mimi nililiona kabisa hili gari likija, nilikuwa nimesimama hapa kwenye tuta nikalaiona hili gari likija kwa mwendo kasi, na wakati ule nilijua litapinda kushoto au kulia, lakini cha ajbu kilanyosha moja kwa moja, utafikiri lilikuwa linakuja kunigonga mimi, karibu linigonge, nikaruka pembeni na kuliangalia linavyoparamia tuta na kugonga huo mti wa umeme, likageuka juu chini na kuwa kama lilivyo hivyo, na ghafla likawaka moto…’akasema shuhuda.

‘Kwa jinsi lilivyosema kuwa lilikuwa likienda kwa kuyumayumba, ilionekana basi kulikuwa hakuna dereva ndani, lilikuwa limewashwa na kuachwa kutembea lenyewe, ….maana kama unasema lilikuwa limenyosha barabara, linakwenda kwa mwendo kasi, na kuyumbayumba, na halikujali kupinda kushoto au kulia, huoni kuwa lilikuwa linakwenda bila dereva…?akauliza askari.

‘Alikuwepo dereva, ingawaje huwezi kuona kwa ndani kwasababu limewekewa `tinted’, lakini mimi nilikuwepo kule gari lilipotokea, nilikuwa nimefika pale kumshusha mtu mmoja aliyenikodisha kwenye pikipiki yangu kufika hapo kwenye shughuli ya harusi. Nilipomshusha pale, nikawa nimesubiri, kama nitapata mteja mwingine wa kuondoka naye, na mara kukatokea mzozo…nilikuwa kwa mbali kidogo, sehemu ambapo gari hilo lilikuwa limewekwa, na mara mweney gari hilo akaja huku kazingwa na watu, na watu wengine wakawa wamelizingira hilo gari, wakiwa na nia ya kumzua huyo jamaa asipate nafasi ya kuingia kwenye gari lake…’akawa anaonge Yule mwendesha pikipiki kwa hamsa, utafikiri anatangaza mpira.

‘Mimi nikalisogeza pikipiki langu pembeni maana, isije ikaacha mlengwa na kunitio hasara, likaliwasha kabisa kutaka kuondoka, maana pia naogoap vurugu, …mara huyo jamaa mwenye gari, akiwa kifua wazi, sijui kama alikuwa akipigana na mtu,au vipi, lakini ilionekana shari limasmbaratika, kifua wazi, ….mzee mzima anaonekana akiwa katahayari, na kwa mbele nilimuona mama shughuli,…mama mmoja mashuhuri sana, akiwa anongea kwa jaziba, nafikiri ndiye aliyekuwa akipambana na huyu jamaa. Na bahati nzuri huyo jamaa akaingia ndani ya gari lake, nilimuona kwa macho yangu dereva wa hilo gari akiingia ndani na kuondoaka kwa mwendo kasi, karibu agonge watu, na mimi nikaondoka na pikipiki langu nikawa namfuatia kwa nyuma…’akasema huyo jamaa mwenye pikipiki.

‘Kwanini sasa ulimfuta nyuma, wakati unasema unaogopa vurugu, na unamfahamu mtu mwenyewe aliyeingia ndani ya hilo gari, ulimuona kabisa kwa sura yake kuwa ndiye mwenye gari..?akauliza askari huku akiandika kweney kijitabu chake.

‘Ndio , nani asiyemfahamu huyo jamaa, ni mashuhuri sana, hata wewe mwenyewe unamfahamu, huyu ni Tajiri Papaa, na aliondoka pale kwenye tukio utafikiri kuwa sio yeye, utajiri wake wote siku ile ulionekan sio wa maana, maana watu walikuwa wakiimba, ‘kumbe papaa ni mchawi…’ akasema yule mwendesha pikipiki.

‘Kwahiyo aliondoka kwa mwendo kasi kutokana na mzozano huo, na ukahakikisha kuwa kaingia ndani ya gari, ukamfuatilia kwa nyuma, na kuhakikisha kwa macho yako kuwa hakuruka….?’akauliza yule askari kwa haraka haraka, huku akiwa kama haamini yale maneno.

‘Ndio nilihakikisha kabisa akiingia ndani ya gari, shati lilikuwa limekatika vifungo, alikuwa kifua wazi, akawa kama anataka kulifunga hilo shati, lakini baadaye aliacha na kuingia ndani ya gari, nilikuwa karibu naye kabisa, akaingia ndani ya gari na kuliwasha, nimeshuhudia kwa mcho yangu mwenyewe…akaondoka nami nikamfuat anyuma,….’akasema yule dereva wa pikipiki.

‘Ulimfuatili kwa karibu karibu au ulikuwa umbali fulani ..?’akauliza skari mwingine.

‘Nilimfuatilia kwa karibu sana, maana nilikuwa na hamu ya kujua wapi aneleekea baada ya lile tukio, na hata kama angeliruka vipi ningeliweza kumuona, barabara ipo wazi…na kwa mwendo ule kama alngeliruka, tungelimkuta akiwa kavunjika vunjika barabarani….’akasema na kuonyesha kwa mikono jinsi kulivyo wazi, kuwa mtu akitoka barabrani na kukimbilia kokote ungeliweza kumuona kwa uzuri …’

‘Sasa yupo wapi, au gari lilipogonga pale kwenye nguzo labda alirushwa na kudondokea chini ya hilo bonde….?akauliza askari mwingine huku akichungulia bondeni.

‘Huko kote nimeshakagua mkuu hakuna mtu au dalili ya mtu kudondokea huko, na angerushwa vipi na kama unavyyona gari limebonyea hivi kama chapatti, lakini hakuna mlango uliofunguka na viyoo vya mbele vimevunjika kama hivi, havijatawanyika, vilelala kama chapatti, unaona vilivyo….’aksema Yule askari akionyesha vile viyoo

`Kama angerushwa kwa mbele, viyoo vingeacha uwazi, lakini angali kulivyo, hakuna uwazi huku. Hili gari ni la thahamani sana, hata viyoo vyake sio vile vya kawaida, vipo kama plastic vile, haivivunjiki ovyo, unaona vilivyo, kwahiyo kama mtu angelirushwa na kutokea mbele ya viyoo hivi vingelivunjika na kuacha uwazi, hapa hakuna uwazi, angalia na huku kwenye viyoo vya pembenei halikadhalika, ….’akawa anaonyesha askari kwa mikono huku akikagua

‘Hakuna hata tone la damu ndani ya gari….’akasema askari mwingine aliyekuwa akikagua na kuandika maelezo yake kwenye kitabu chake.

‘Haya ni maajabu, ina maana huyu mtu aliyeyuka ghafla na kupotea hewani..?’ akasema askari mwingine.

‘Huyo mwanga, nilijua tu utajiri wake wote ule ni wa kimazingara, haiwezekani akaibuka kuwa tajiri kwa ghafla vile, familia ayo naijua vyema, haikuwa na utajiri wowote, yeye kaanza na biashara ndogo tu ya genge, mara duka, mara huyo maduka, kampuni, magari..haiwezekani, kuna kitu…sasa simnaona…kapambana na waliomzidi kete…’akasema jamaa mmoja, na wale askari walikuwa wakiendelea kuandika andika mambo yao, hawakuwa na la zaidi la kuwahoji hawo watu, kwani walishaanza kuingiza mambo ambayo hayaandikiki.
Wadadisi hawakuishia hapo waliamua kwenda hadi nyumbani kwa huyo tajiri, lakini walikuta mageti yamefungwa, na wafanyakazi walipoulizwa walisema bosi wao kasafiri, hawajui kasafiri kwenda wapi na hawajui kuwa atarudi lini.

‘Kasafiri toka lini…?’akauliza mdodosai mmoja. ‘Kaaga asubuhi kuwa anasafiri, na hajarudi…’ akasema mlinzi.

‘Kwenda wapi…hamjasikia kuwa kapata ajali..?akauliza tena huyo jamaa. ‘Hatujasikia kitu kama hicho, ….’akasema huyo mlinzi , ambaye hakutaka kuhojiwa zaidi.

*********

Maua alijihisi hali isiyo ya kawaida, ilikuwa kama mtu kaleta moto ndani chumba, kkawa na joto lisilo la kawaida, akajihisi hawezi kuvuta hewa, hewa ilikuwa nzito kupita kiasi. Akaona heri asimame na kulifungua dirisha lote na hata ikiwezekana afungue na milango, akajaribu kuinua kichwa pale alipokuwa kakiegeemza kwenye sofa, lakini hakikuweza hata kutikisika, akaanza kuingiwa na wasiwasi, …

Mbona hali hii ni ya jabu kwake, inakuwaje mwili mzima unalegea, unakuwakama umepooza. Akaona ni heri amuite shangazi yake, akajaribu kutoa sauti, lakini sauti haikutoka. akiwa katulia kimiya, akimsubiri mpambe wake ambaye alitoka aliahidi kuwa atarudi muda sio mfupi, na aliambiwa sivae hilo gauni la harusi mpaka arudi.

Maua hakupendezewa, tabia ya kuvaa nguo watu wengine wakiwa wanamchungulia, lakini kwa vile ni siku maalumu, akaona asalimu amri. Yeye kwa muda huo alikuwa varandani na gauni la harusi lilikuwa limehifadhiwa vyema chumbani mwake. Na akiwa kajimpumzisha alishangaa kuona mwili mzima ukimusiha nguvu, alishangaa kuhisi mwili mzima ukilegea kila kiungo kilikuwa kama sio chake hali ili ilimshitu sana, kwani ilimkumbusha siku ili ilipomtokea, na siku ilipotembelewa na Yule tajiri, Tajiri Papaa.

Na kitu kama hisia kikamteka ubongo wake, alikuwa akiona sura ya ajabu, ile sura alishaahi kuiona, ikiwa imevaa vitu vilivyoficha sura ya Yule mtu, na safari hii, licha ya kuwa sura imejificha, lakini ilionekna kuwa ina hasira, chuki na haikuwa ina lepe la huruma,….Maua akajau leo kuna baya litatokea, na akaanza kuogopa, akajaribu kufunua mdomo kuataka kupiga ukulele,lakini mdomo ulikuwa kama sio wake, hakuweza hata kufunua sehemu yam domo, mdomo ulikuwa mkavu kupita kiasi.

Akaanza kuomba, kwani kiichobakia na ambacho kiliwezekana ni hicho peke yake, kuwa ubongo na akili na kuwaza zilikuwepo,lakini mwili peke ndio haukuweza kufanya kitu, akoamba , akaomba… Mara nyuma ya ile sura kukatokea sura nyingine kubwa sana, sura hiyo ilifunika sehemu kubwa na ile sura ya mwanzo ilionekana ndogo, …na kama ilihisi kuwa kuna kitu nyuma yake, ile sura ikagaeuka nyuma, na kuanza kutetemeka, na baadaye ikadondoka chini na kuteyuka, na ile sura ya mwanzo ikazidi kuwa kubwa na kuwa kama inafunika sehemu yote ya upeo wa macho wa Maua.

Maua lihisi kuwa sura ile alishaiona kabla lakini hakuweza kuitambua vyema, na baadaye ile sura ikapotea na ile hali ikaisha, na Maua akaweza kufunua mdomo na kujikuta akiita `shangazi….’.

Akainuka pale haraka haraka na kukimbilia mlangoni, lakini alipofika pale mlangoni badala ya kufungua mlango akajikuta akijicheka na kusema kimoyomo kuwa ni zile zilikwua kumbukumbu za uwoga kwasababu ya tukio la jana, uwoga huo ulimwingia kwasababu, habari zilizozagaa kuwa licha ya gari la huyo jamaa kupata ajali mbaya na kuungua lakini huyo jamaa hakupatikana akiwa ndani ya hilo gari. Ina mama hakufa kama watu walivyozania na alitokaje ndani ya lile gari, alipaa hewani kama mwanga, na kama alipaa hewani na kuepuka hiyo ajali, basi anaweza kuja hapo kiajabu vile vile.

Alipowaza hivyo mwili ukaanza kumuisha nguvu tena, moyo ukaanza kumwenda mbio, na kushindwa kabisa kusogea pale mlangoni alipokuwa kasimama, …safari hii hakuipa muda ile hali akaomba kwa juhudi zake zote, na mara kukawa kimiya na hali ya chumba ikawa shwari, na hewa ikawa kama kawaida, Na muda huu aliomba shangazi yake aingie haraka, ….na alipoona hata mpambe wake harudi haraka kama alivyoahidi , akaamua kuingia chumbani ambalo gauni la harusi lilikuwa limewekwa …

‘Huyu mpambe naye vipi kaeleeka wapi muda wote huu, alitakiwa tuwe naye sambamba, lakini ana pilikapilika kila mara kaitwa huku na kule kwenye pilika pilika zake….’akajikuta akilalamika peke yake.

‘Ndio ana shughuli zake, lakini sio muda kama huu, alishajitolea kwa shughuli hii, basi alitakiwa kila kiti akiweke pembeni kwanza mpaka shughuli hii iishe….’akaendela kulalamika.

Alijipa nguvu, na baadaye ile hali ikaanza kumuishia na nguvu zikaanza kumrejea tena baada ya kupumzika kidogo, ndipo akaingia chumbani kwake na kulichukua gauni lake la harusi, lililokuwa pale kitandani….

Maua akajiuliza kichwani, mbona fahamu hii hikuwepo kabla, kwani siku ya kulionunua nilikuwepo, nikasema swa hilohilo, nakumbuka niliitikia tu kwasababu kila mmoja alikubaliana nalo, rangi yake ilikuwa inakwendana na rangi yangu, mampmbo ymekaa vyema….lakini akili yangu haikuwepo kabisa. Ndipo nikakumbuka kwanini siku ile nilisita kulikubali haraka hilo gauni…licha ya kuwa nilisema sawa, lakini moyo hakuwa razi nalo…nikakumbuka.

Niliinama pale kitandani na kuliinua lile gauni, sasa nimekumbuka vyema, nikajisema kimoyomoyo, `hivi hawa watu wana maana gani kunichaulia gauni kama hili, utafikii sikuwepo wakati wa kulichagua hilo gauni….’akasema Maua huku akitabasamu.

Gauni lile lilikuwa sawasawa na guani alilolivaa Maua kwenye harusi yake ya kwanza, kwa kila kitu, utafikiri ni lille lile gauni, limechukuliwa na kurudishwa dukani, lakini Maua alikumbuka gauni lake la harusi alishalipiga mnada, aliamua kufanya hivyo, pale alipoamua na kutoa kauli kwa Maneno kuwa yupo tayari kuolewa na ye ye, …kwani ndilo lililokuwa limebakia, baadhi ya vitu vingine alikuwa kavichoma moto siku walipofanya dua ya mwaka ya kumrehemu aliyekuwa mume wake, siku ile aliamua kuchoma kila kitu kilchokuwa kikimkumbusha siku zake za nyuma, isipokuwa hilo gauni, na akalipiga mnada baadaye …

Tupo pamoja ni mimi wenu: emu-three

Thursday, November 24, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-54



‘Umefuata nini nyumbani kwangu…?’ Maua aliuliza kwa hasira, huku akiwa anaogopa, maana kwa muda ule watu wengi walikuwa wametokatoka katika maandalizi ya hapa na pale, na yeye alikuwa kabakia na shangazi yake ambaye naye alimuaga muda mfupi kuwa anatoka kidogo kwenda kusikojulikana, kwani hakutaka kusema wapi anapokwenda, lakini Maua alihisi kuwa shangazi yake hatakuwa akelekea kwenye biashara zake, lazima atakuwa kaelekea kwa huyo mtu aliyekuwa akimsema….

‘Mpenzi Maua, nakupenda sana, yaani ungelijua ninavyokupenda ungenihurumia na kunipenda zaidi na zaidi, nakuhitaji sana katika maisha yangu,…tangu nisikie kuwa unaolewa na huyo jamaa ambaye hana mbele wala nyuma, moyo wangu umekuwa ukiniuma sana, kwasababu nilikutegemea wewe uwe mke wangu, …wengine waliotangulia niligundua hawanifai, sehemu hiyo ni ya kwako wewe, nikubali uje tufaidi utajiri nilio nao…’yule jamaa akawa anaongea na kusogea karibu na mlango, nia yake ilikuwa hata kupiga magoti, lakini aliogopa wapita njia kutokana na heshima yake,a kaweka mikono mbele kama mtu anayemuomba mungu wake.

Maua alianza kuingiwa na wasiwasi, …na huwa kila mra akikutana na huyu mtu moyo wake unajenga hofu, hasa pale alipowahi kumtamkia kuwa anamtaka kuwa mke wake na kumkatalia, lakini hapo akajitahid na kumwambia, ‘Hivi wewe mwanaume, una akili kweli, yaani umetoka huko kote kuja kuniambia maneno kama hayo, ….ina maana hakuna wanawake kama mimi…, eti unadai tufaidi utajiri ulio nao, utajiri utanisaidia nini kama hakuna upendo, mimi sikupendi ndio maana sitaki kuolewa na wewe…naomba tafadahli uondoek usije ukanijazia watu hapa….’akasema Maua kwa hasira.
‘Mapenzi gani kama mtakuwa mnaishi kwa shida, ..ni kujidanganya tu Maua, mapenzi ni yale yaliyopo ndani ya raha ya utajiri, kila ukitakacho kipo. Na hili nakuthibitishia kwako Maua kuwa nilishakujenegea nyumba yako mwenyewe, na hatii hii hapa,….’akatoka karatasi kumuonyesha Maua, lakini Maua hakutaka hata kuiangalia.

‘Shika uiangalia Maua, imeshaandikwa jina lako, yaani siku tukitoka kwenye kufunga ndoa tu ile nyumba ni ya kwako , ni kiasi cha kujaza haya makubaliano kuwa umekubali kuwa mke wangu, na nyumba inakuwa ni mali yako, sio nyumba tu hata gari, lipo kwa ajili yako, …gari la kwako mwenyewe, yote haya nimeyafanya kwa vile ninakupenda Maua, unataka nifanye nini ili ujue kuwa nakupenda isivyo mithilika…’yule mtu akaongea huku akisogelea karibu na lipokuwa kasimama Maua, na Maua naye alikuwa akijitahidi kuataka kuufunga mlango, lakini alihisi kama mwili unamuishia nguvu….

‘Tafadhali nakuomba usinisogelee , na …..nakuomba u…uondoke hapa karibu na hii nyumba, …’ Maua akawa anaongea kwa shida, na kushangaa kwanini anajisikia vile, akjipa moyo, na kujitutumua, huku akihsisi jasho likimtoka.

‘Hebu ondoka, naona sijisikii kuongea na wewe….kama una haja ya kushuhuida ndoa yangu ikifungwa, nenda kasimama pale uliposimamisha gari lako,kwani majibu yangu umeshayapata na ulishayapata siku nyingi, cha muhimu nenda kamtafute mwingine, wapo wengi wanaopenda utajiri, wazuri na warembo sana kuliko mimi mara mia, ….’akasema Maua kwa kujitutumua huku akimuomba mungu ampe ujasiri na kuondokana na mtihani huo na akakusanya nguvu kutaka kuufunga mlango, lakini huyo jamaa akauwahi na kuuzuia kwa mikono wake.

‘Sikiliza Maua, mbona unanifanyia hivyo, hivi kweli unamuelewa huyo jamaa unayetaka kuolewa naye,unauhakika kama siyo yeye aliyemfanya mume wako atokomee huko alikotokomea,ili akupate wewe, unauhakika kweli kuwa mume wako alikufa kwenye hiyo ajali, kama sio mbinu za huyo jamaa, yako kumfanya mume wako ndondocha , anateseka huko alipo, ili akupate wewe kirahisi….fungua macho na fikira zako, maana kama angelikuwa kafa kama wengine, ungehisi hivyo….nina uhakika kuwa moyo wako haujakubali kuwa mume wako hajafariki, niambie ukweli hapo ulipo unaamini kweli kuwa mume wako kafa…?’ akauliza yule mtu na kwamwangalia Maua kwa makini.

‘Usiniletee ushirikina wako , kwanza nasikia hata utajiri wako ni wa kishirikina, ndioa maana hukai muda mrefu na wanawake…nenda zako sitaki kusikia hayo maneno yako tena…’akasema Maua huku akiingiwa na uchungu kwa kauli ile na kujikuta machozi yakimtoka kwa wingi, hayo maneno aliyotamka huyo jamaa yakawa yakirejea ubongoni mwake kwa mfulullizo `unaamini kweli kuwa mume wako kafa…’ni kweli hajawahi kuamini hilo, na hata siku alipomtamkia Maneno kuwa yupo tayari kuolewa na yeye,alitamka tu,lakini hakuwa makini , alijiona kama msaliti…alimwangalia tena yule tajiri ambaye alikuwa bado kashikilia mlango na huku kamkodolea macho.

‘Hayo ni maneno ya watu wasiopenda maendeleo ya wengine, utajiri wangu nimeupata kwa jasho langu,na kwasababu wao ni wavivu hawataki kuhangaika, wakizania kuwa utajiri unakuja hivihivi, wanaishia kunionea wivu, wanabakia kusema maneno ya kashifa kama hayo. Maua utajiri huu nimeupata kwa shida sana na ni kikuhadithia hutaamini,…’yule jamaa akaachia ule mlango na kuegemea pembeni yake huku kageuka kuangalia gari lake.

‘Maua usione watu matajiri ukafikiri wameibuka tu ghafla, watu wanakuwa wametoka mbali, wampitia majaribu mengi, huwezi amini kuwa nimeanzia na genge, nikapanda nikashuka nikaingia kwenye duka, nikapanda nikashuka, kidogo kidogo, …nikawa nafanya bisahara za kutoka mikoani, kidogokidogo,hadi duka likapanuka, baadaye nikapata mkopo na kuanzisha kampuni ya biashara,…na sio kirahisi hivyo, ndio kama zipo njia nyingine, lakini ni miongoni mwa juhudi zangu…’akamgeukia Maua.
`Maua mengine yanasemwa sana,….lakini sifanyi kwa kumuibia mtu, nafanya kwa kutafuta , sio kwa jasho la mtu mwingine… sio jambo rahisi tu kama wanavyozania watu. Na nikuambie Maua mengina yamejitokeza nifanye pale tu nilipokuona, sijawahi kuingilia maisha ya mtu mwingine, ila imadiriki kuafanya hivyo kwa ajili ya kukutaka wewe…nimeshindwa,kuona unachukuliwa an mtu mwingine wakati nakupenda….hapana, …’akasema yule mtu na kugeukia pembeni.
‘Kwahiyo hapo una maana gani…?’akauliza Maua.

Maua sisi wanaume wengi tunahangaika kwa ajili ya warembo kama nyie….sikudanaganyi, silali kwa ajili yako, na nitajitahidi kuhakikisha kuwa unanikubali…hadi hatua ya mwisho… Ama kwa hawo wanawake nilio-oa awali na baadaye tukashindana nao, ni kwasababu hawana upendo wa zati, walikuja kwangu kwa ajili wanataka mali, nilipowapa majukumu wakashindwa…., hatukuwa tunakubaliana na mmbo mengi, na nikawatimua, nafikiri yote ni kwasababu nafasi hiyo ni ya kwako…wewe nimekuchunguza na kukugundua kuwa tunaweza tukaishi pamoja, kwanza mchapa kazi, una nidhamu, mzuri…oooh,…..’akasema huyo jamaa huku akiwa kaangalia juu, kama anajenga taswira fulani.

‘Mhh, wanaume bwana, una uhakika gani na hilo, ..kwasababu wote uliowaoa na kuwaacha wameolewa na wanaume wengine na wanaishi kwa raha mstarehe,…kweli walishindwa kwako kwa wengine waweze, sema ukweli baba una yako yasiyobebeka….’Maua akajikuta anaongea na alishangaa kwanini anashindwa kuchukua uamuazi wa kuufunga ule mlango na kuondoka, mwili ulikuwa kama umekufa ganzi…’Maua alianza kuogopa, hasa pale mawazo mabaya ambayo yanaongewa kuhus huyu mtu yalipomjia akilini.

*********
Tajiri Papaa, kama anavyojulikana, anamiliki kampuni kubwa ya kibiashara, ambayo huagiza vitu mbali mbalimbali toka nje na kuuza kwa jumla na rejareja, ana magari ya safari, mabasi kwa malori, ana taksii nyingi zilizosambaa hapa nchini, na miradi mingi sana, na hakuna asiyemfahamu kwa utajiri wake. Watu wamekuwa wakijiuliza wapi alipoupatia huo utajiri, na mwishowe wakahisi huenda kuna namna.

Wanawake wengi wamekuwa wakinaswa kwa utajiri wake huo na wengi wamejitahidi kuolewa na yeye, lakini kila aliyeolewa , hakumaliza mwaka, aliachika, na kila aliyeachika hajawahi kusema kwanini kaachika, na hakuna aliyeingiwa na wazo la kudadiisi zaidi,…na hata hivyo huyo jamaa sijui ni kwasababu ya utajiri wake, huwa hachukui muda anaoa mke mwingine haipiti muda anaacha na kuoa , na wengine wakahisi kuwa huenda nia yake sio kuoa, bali ni kuwachezea wanawake, na kuwaacha.

Siku Maua alipokutana na tajiri huyu ni kipindi ambacho alikuwa na majonzi makubwa ya kupoteza mume wake, akiwa njiani akitokea hospitalini, alikuta gari likisimama mguuni mwake, na mara akatokea jamaa mtanashati, kavalia nguo za kifahari, ana urembo wa kuvutia, akamsogelea Maua ..
‘Maua ngoja nikusogeze hadi nyumbani, najua labda hunifahamu, mimi ni Tajiri Papaa, na nakupa poel sana ya kupotelewa na mume wako, na huenda atapatikana tu, yote ni mapenzi ya mungu, na kama utahitaji msaada zaidi mimi nipo tayari kukusafirisha hadi huko Mwanza tukajaribu kuhakikisha,…’akasema huyo mti kwa moyo wa huruma.

Maua hakupenda kupata huo msaada, lakini aple alipokuwa alikuwa hajisikii vyema, na kama isingelikuwa masaada wa hilo gari asingeliweza kufika nyumbani. Alijuta kwanini alijiamini , kwani shangazi yake alimmwambia asiondoke apke yake kwenda hospitalini, lakini akasema hakuna wasiw asi, anakwenda kuchukua dawa mara moja atarejea nyumbani, lakini alipotoka hospitalini, akawa ahajsikii vyema, akajitahidi kufika kituoni, lakini usafiri ukawa wa shida, ndipo akaamua kuchukua mdogo mdogo, kama kujipa zoezi,….

Mwanzoni alitembea vizuri, lakini alipofika mbele kidogo akajihisi kizunguzungu, na moyo kumwenda mbio, akakaa kidogi kwenye mti weney kivuli, na baadaye akaanza kutembea, na alipoona kuwa hataweza, ndipo akaamua kuchukua taksi, au usafiri wowote utakaomfikisha nyumbani, inagwae alishatembea nusu ya safari, na wakati anasubiri, ndipo akatokea huyu jamaa.
Maua aliwahi kusikia sifa za huyu mtu, kwakweli anaonekana ni jamaa mkarimu,na utajiri wake ulikuwa umemvika, kwani hakujivunga kwa kuvaa vyema na hata gari lake lilikuwa ni la kifahari,

‘Maua usijal;I sana, najua hali uliyo nayo, lakini yote ni mapenzi ya mungu, cha muhimu ni kujikaza, ingawake ni kazi kubwa sana, lakini jitahidi sana,…Mhuja alikuwa mmoja wa watu niliowafahamu katika kazi zangu za biashara na nashukuru kuwa amewahi kunisadia sana, na niliposikia hilo tukio, nikasema nijaribu na mimi kutoa msaada wangu, na kama ulivyosikia mimi nilijitolea kuchangia usafairi wa ndege wa kumchukua Maneno, na nilikuwa tayari kwenda nay eye….’akasema huyo jamaa

‘Ahsante sana, nashukuru sana, nilisikia hivyo, lakini sikuwahi kukutana na wewe na kukupa ahsantezangu, mungu akubariki sana…’akasema Maua.

‘Usijali, mimi nipo pamoja na wewe na kama kuna lolote unahitaji, mimi nipo tayari kukusaidia bila matatizo, kwasababu leo kwako kesho kwangu, hayo yote hakuan anayeyaomba, na ukikwamba usikose kunipigia simu, na nitaitahidi kuwa karibu na wewe kuhakikisha kuwa hupati shida, kwasababu ya wema wa mume wako, na hata hivyo sioni kwanini wewe upate shida wakati tupo watu wenye nafasi ya kusaidia..’akasema yule mtu kwa maneno yaliyojaa huruma na Maua akamshukuru na kuteremka ndani ya lile gari la kifahari, kwani walikuwa wameshafika nyumbani kwake.

Na wakati wanaagana yule jamaa akamshika Maua mkono na kumsindikiza hadi mlangoni, na wakati anataka kuondoka, akatoa bulungutu la pesa na kumshikisha Maua mkononi huku akisema kuwa hiyo ni sehemu ndogo tu ya kuhakikisha kuwa Maua anaishi maisha bora sawa au zaidi ya alivyokuwepo mume wake. Maua alitaka kuzikataa zile pesa, akinyosha mkono kumrudishia yule mtu, lakini mara akatokea Shangazi na Maua akarudisha mkono wake ili kuzificha zile pesa zisionekane na shangazi yake na yule akaharakisha kuingie kwenye gari na kuondoka.

‘Maua yule ni nani, sio Tajiri Papaa….mungu wangu, usije ukadanganyika na utajiri wa huyu mtu, ndio ana utajiri sana, na anaonekana mrembo, lakini utajiri wake ni wa pesa chafu, na ujiulize kwanini tajiri kama yule hakai na mke, leo kaoa huyu , mara kaacha, kesho kaoa huyu , mara kaacha, kuna nini ndani ya amisha yake,….achana kabisa na mtu huyu….’akasema Shangazi yake.

‘Shangazi mbona sina mawazo hayo, yaani hii hali ya huzuni imeisha lini hadi niingie kwenye tamaa za naman hiyo, wala sikuwa na habari ya huyu mtu, alichofanya nikusaidia usafi baada ya kunikuta njiani, na akaniambia kuwa ndiye aliyesaidia katik usafiri wa Maneno kwenda Mwanza , kwahiyo nilifurahi kuwa nimemuona na kumshukuru….shangazi, mimi sitapenda mume mwingine zaidi ya Mhuja, na nitamsubiri hadi atakaporudi, najua bado yupo hai….’akasema Maua kipindi hicho hakukubali kabisa kuwa Mhuja keshapotea duniani.

Baadaye huyo jamaa hakuishi hapo, akawa kila akipata upenyo anakuja kwa Maua na kuongea kidogo na akiondoka huacha hela nyingi tu, na akaahidi kumfungulia Maua duka kubwa la biashara,, lakini kwa Maua ilikuwa ni kama mbuzii anapigiwa gita, hakuwa akimsikiliza, ila kiheshima, akawa anamkaribiosha na kuitikia yale yanayofaa kuitikiwa lakini muda mwingie, mawazo hayakuwepo hapo, na ilikuwa kama vile hakuna mtu anyeongea naye.

‘Maua nakuona kila siku nikija hapa unakuwa mbali, na inakuwa kama vile sipo, unaonaje tukisafiri nchi za nje, ili uondoe mawazo, twende kama Miami, au …Ufaransa, au ncho yoyote unayopenda, ili uondoe mawazo, unasemaje..?’akauliza huyo tajiri.

‘Hapana, nipo katika majonzi ambayo hata kama nitakwenda wapi, haitasaidia kitu, nashukuru sana kwa kuwa name katika wakati huu mgumu, na nisingependa kukuudhi kwa lolote, ila nakuomba usihangaike sana, na mimi, kwani sina chochote ninachokiona zaidi ya kumbukumbu za mume wangu, na sitaona kingine zaidi yake, nakuomba tafadhali usihangaike na mimi na kuwa na mawazo yoyote kuhus mimi…tafadahali na nitafurahi kama utaondoka tu, …’akasema Maua na siku hiyo alikataa kata kata kupokea chochote kutoka kwa huyo jamaa.

Baadaye huyo jamaa akaamua kupitia kwa shangazi mtu, kuomba kama inawezekana amuoe Maua, ilitarajiwa itakuwa hivyo, kwani shangazi alishahisi ujio wa huyo jamaa utaandamana na habari kama hiyo, shangazi hakumkatisha tamaa na alimwendea Maua kumpa hiyo taarifa…
‘Shangazi unasemaje…hivi mimi watu wananionaje….sitaki mwanaume yoyote hata awe tajiri wa kupindukia, mimi najua mume wangu atakuja…’akasema Maua na kuanza kulia.

‘Sio kwamba nimekubali hilo ombi, ila ni wajibu wangu kufikisha ujumbe, na kama nilivyokushauri awali , kuwa huyo jamaa akikuona uue kuna kuachika, sijui kwanini inakuwa hivyo, kwani wengi walioolewa na yeye na hata kuachika hakuna aliyetoa siri ya kwanini imekuwa hivyo….sisi kama wazazi tunakuombea upate mume , na tunakuomba ukubali ukweli kuwa Mhuja hayupo, ….’hayo yalikuwa maneno ya shangazi yake kipindi hicho.

Kulifuta mlolongo wa kutokuelewana kabisa kati ya Maua na huyo jamaa, kwani lifikia hatua akawa kama analazimisha na ndipo Maua akapiga marufuku kwa huyo jamaa kuja nyumbani kwake tena, lakini hakukata tamaa, mpaka Maneno akaingilia kati karibu hata ya kugombana na huyo jamaa. Na ukajengwa uadui kati ya Maneno na huyo jamaa, kwani Maneno hakuwa anapendeela ukaibu wa huyo jamaa na Maua, lakini kwa uda ule hakupenda kuingilia kwa karibu, na alipopata ile safari ya Arusha akaona ndio nafasi ya kucheza karata yake ya ushindi.

Leo jamaa huyu hapa mlangoni na kaja siku ambayo hakutaka kabisa kuonana naye na alishampiga marufuku kuja nyumbani kwake, lakini hakukoma,....

‘Wewe mwanaume, nilishakupiga marufuku usikanyage hapa kwangu, kwanini hunielewi, nakuomba tena kwa mara ya mwisho sitaki kukuona hapa nyumbani kwangu, na sasa hivi nitakuitiwa polisi maana unajifanya kiziwi….’akasema Maua.

‘Hahaha utaniitia polisi …Maua usifike huko, maana hakuna polisi anaweza kunikamata kwa kosa gani, kwa kosa la kuja kukuto9ngoza, au kukusaidia kukuzuia usiolewe na huyo hohe hahe, ili uje ukale utajiri wa bure….Maua nakupenda sana, …’akasema yule jamaa akijaribu kuufungua mlango.
‘Wewe mtu umefuata nini hapa nyumbani…?’ ilikuwa sauti ya shangazi na Maua akashukuru sana kuwa shangazi kaja ataokoa jahazi. Yule jamaa akasogea pembeni na kusalimia kwa adabu, kuonyesha kuwa ni mtu mweney heshima zake.

‘Nakuuliza umefuta nini hapa, maana nimefika kwako sijakukuta, nikaambiwa umetoka …nataka kujua kwanini hukomi kuifuta futa hii familia, tulishakukataa bado unang’ang’ania, na isitoshe unaleta mambo yako ya kishirikina ndani ya familia hii…unafikiri hatukujui….’akasema shangazi nan je watu wachache walishaanza kuja...

‘Mama tafadahli sikuwa na nia mbaya, nilikuwa kuonana na Maua mara moja, nakuomba unielewe, nilitaka tu kumkanya Maua kuwa kunikataa mimi ni kosa kubwa sana,….’akasema huyo jamaa.
‘Kwahiyo ndio umeamua kumwangiwa usiku haikutosha umeamua kuja hadi mchana na uchawi wako….sasa nakua dakika tano uwe umetoweka hapa nyumbani kwangu, la sivyo nitakuumbua….’akasema shangazi mtu.

‘Mama hayo yametoka wapi tena, mambo ya uchawi sijui, nini …nakuomba nipo chini ya miguu yako niombee kwa Maua aachane na huyo anayetaka kumuoa, aje tukaishi kw raha mstarehe…nilishamnunulia gari, nyumba….sasa hivyo vyote anaviacha kwa ajili ya huyo jamaa…mama hebu fikirieni hayo kwa makini kabla hamjafanya makosa….’akasema huyo jamaa.

‘Hivi wewe hiunielewi eeh, jamaa mnamuona huyu jamaa , utajiri wake wote ni wa kishirikina, kama mnabisha mimi nitawaonyesha….’akamsoegelea yule jamaa, na watu wengi walishakusanyika, ….kabla yule jamaa hajajua nini kitakachofuata shangazi akamshika shati la yule jamaa na kulivuta kwa nguvu, likafunguak vifungioa, na haraka kabla yule jamaa hajajua nini kinachoendelea, shangazi akakiona kile alichokitaka, akalivuta lile shati kwa nguvu na kushika kamba iliyokuwa imeonekana kuvaliwa shingoni mwa yule jamaa, akaivuta...

‘Wewe mama vipi mbona unakosa adabu, unataka kufanya nini….’yule jamaa akaanza kujitetea lakini alishachelewa, kamba ile ilivutwa kwa nguvu na kukatika, na shangazi akawa, keshaivuta na mwisho wa ile kamba lilioenekana bonge la hiriszi nyekundu….akaitupa mbali kabisa mahali waliposimama watu ili waione.

‘Mnaona hiyo…huo ndio uchawi wake wa kuwangia watu usiku…’akasema Shangazi.
Watu waliokuwepo hapo wengine walikimbia, wengine waliisogelea ile hirizi, na yule jamaa kwa aibu akaikimbilia kuiokota, mlakini watu wakaipiga teke na kwenda mbali zaidi…
Msimruhusu akaichukua, lazima tumkomeshe na uwanga wake…’watu wengine wakasema na mmojawapo akaichukua na kusema watu walete mafuta ya taa, na kweli utafikiri ilipangwa, mafuta ya taa yakapatikana haraka...

‘Jamani jamani mnataka kufanya nini….’yule jamaa akawa anahangaika kuitafuata ile hirizi yake, na alikuwa kama kachanganyikiwa, lakini hakuna aliyempa nafasi hiyo, watu walimzonga wakimzomea, `papa kumbe mwanga,papa kumbe mwanga…’na baadaye akaona aibu na kukimbilia kwenye gari lake ambapo watu walishalizunguka, na huku wanamuimbie `papa kumbe mwanga….’akapata nafasi ya kuingia kwenye gari lake huku ile hirizi yake ikitiwa mafuta tayari kwa kuiinguza, yeye haraka akaondoa gari kama mwehu, na aliondoka pale kwa mwendo kasi ajabu…..

Ile hirizi likuwa kila ikiwekwa moto haiwaki, watu wakawa wanahangaika nayo, mapaka wakatokea wazee ambao walijitambulisha kuwa wametokea kwa Maneno , wakaichukua ile hiriz na kuifungua , na baaadaye wakawasha moto , na kuungua, kulitokea harufu kali, na ikalipuka kama bomu. Na wakati hayo yakiendelea mara akaja mtu na kusema kuna ajali mbaya imetokea, gari la papa limepanda tuta la barabara na kugonga nguzo ya umeme, likalipuka…..

NB; Haya niambieni kuhusu tukio hili, je limetokea sababu ya nguvu ya giza, jamaa hatujui kuwa yupo hai au vipi, na ndoa hiyoooo, inanukia, je huko kwa akina Sweetie nako vipi, tuwepo katika mfululizo huu, na inabidi nipitie kuona kama tuhitimishe au kuna sehemu imebakia, na zaidi nategeema kutoka kwenu, nipeni maoni tuwe pamoja, kama hamtojali


Ni mimi: emu-three

Tuesday, November 22, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-53



Maneno alikuwa keshavaa na alikuwa akimsubiri msaidizi wake ambaye alitoka kidogo, na kumuacha peke yake ndani, akiwa peke yake alijikuta akiwaza mengi, alishangaa toka jana akili yake ilikuwa haitulii vyema, hakuwa akiamini kuwa kweli sasa anakwenda kukabidhiwa yule mtu aliyekuwa akimpenda kwa moyo wake wote, hakuamini kuwa baada ay muda ataitwa mume wa mtu, …lakini upande mwingine wa akili yake alijikuta akiwaza ndoto aliyoiota jana, …
***
Ilikuwa ni sehemu ya tambarare sana, na macho yake yaliweza kuona mbali sana, na ilionekana alikuwa akisubiri kitu ambacho kwa muda ule hakuweza kukigundua ni kitu gani, na muda ulikuwa ukienda na hicho kitu hakikutokea, mara ghafla akasikia sauti kama upepo ukivuma, na likaja vumbi ambalo lilizoa matakataka na kuingiwa machoni, akajipangusa haraka, kwani wakati anainua mikono kujipangusa aliona taswira ya kitu mbele yake, …na wakati huo huo vumbi lilikuwa limeshaingia machoni, kwahiyo hisia za haraka ni kuondoa hilo vumbi machoni.

Alipikicha machonja cha mkono wake, na kujaribu kuangalia mbele yake, akashangaa macho yake yakiwa yana ukungu, ukungu ambao ulimfanya asione vyema, akapikicha tena , lakini kila alivyozidi kupikicha, ndivyo alivyozidi kupunguza nguvu ya uoni wa macho yake, na cha ajabu mbele yake alihisi kuwa kuna mtu anakuja, lakini kwa vile macho yalikuwa hayaoni vyema, hakuweza kumgundua ni nani, ila ilionekana huyo mtu anamfahamu sana. Je ni nani huyu mtu…?

Tatizo likawa ni jinsi gani ataweza kuona, maana akipikicha macho kwa mkono anazidi kuharibu nuru ya kuona, na akiacha vumbi linamkereketa machoni, na vile vile alikuwa na hamasa ya kutaka kumuona huyo mtu anayemjia, kwani alihisi anakuja kumzuru, …na kama ni hivyo kwanini alisimama pale kumsubiri kwa muda mwingi hivyo…alihisi kuwa alikuwepo hapo kusubiri kitu, na kitu hicho kumbe ni mtu , na mtu huyo inaonekana ni mtu anayemfahamu, lakini amekuja kwa nia mbaya, kwa vipi , ilikuwa ni hisia ilivyomtuma…

Akainua mikono kujipikicha teana kwani vumbi lilikuwa linamkereketa sana machoni, na sasa akajipikicha kwa nguvu sana, ili kuondoa ule utando uliojivika machoni na kumfanya asione vyema, alifanya hivyo mara kadha, huku anaomba , tatizo hilo limtoke, maana limeshaanza kumpa wasiwasi, isije ikawa ndio mwanzo wa kumpa upofu. Alikumbuka kisa cha jamaa yake eliyepoteza macho yake hivyo hivyo ,…alimuhadithia kuwa tatizo lake lilienza kwa kuingiwa vumbi machoni, ilikuwa vumbi kidogo tu ,akajipikicha na kila akifanya hivyo ndivyo ilivyoharibu macho yake na sasa ni kipofu.

Alipokumbuka hicho kisa cha jamaa yake akaanza kuogopa , na aliogopa hata kuondoa vile viganja vya mikono machoni, licha ya kuwa alishamaliza kazi ya kuondoa vumbi lililokuwa likimuathiri, na nia yake sasa ni kumuona huyo jamaa aalyekuwa akimjia, na kama ni adui ajiandae kupambana naye. Na kipindi anapikicha macho, mawazo ya hiyo taswira ya mtu haikuwa na umuhimu sana zaidi ya macho yake kuona. Aliogopa kupoteza macho, kwani macho ni kipenzi cha mtu, ambaye alijaliwa kuwa nayo.

Sasa akaanza kuyafunua macho yake, alifnya hivyo kwa wasiwasi na kwa hiyo aliyafunua kwa utaratibu sana , na kila hatua ilikuwa ni kiwewe kwake, kwani badala ya kuona mbele, baadala ya kuona mwanga, badala ya kuona ule upeo aliokuwa akiuona toka mbali, na badala ya kuiona ile taswira, aliona giza, giza nene, ….hakuamini akili yake, hakuamini kuwa sasa haoni tena, ina maana kawa kipofu,hapana …hapana, haiwezekani….

‘Ina maana nimekuwa kipofu..haiwezekani, oooh, mungu wangu nimekosa nini,…mungu wangu nisaidie nisamahe makosa yangu, kama kuna kitu nimekosa naomba unisamehe, naomba unirudishie macho yangu tena, sitarudia tena…’Maneno lijikuta akilia kwa sauti, na mara akazindukana, kumbe ilikuwa ni ndoto.

Alipoamuka cha kwanza kabisa, ni kukimbilia kwenye kiyoo, kukagua macho yake kuhakikisha kuwa kweli yapo sawa, na alipoona yapo sawa, akarudi kitandani kutulia, akiwazia ile ndoto, huwa haamini mambo ya ndoto, au ushirikina,…ila ile ndoto ilimtisha, kwanini ilenge macho yake…hakuamini, akaeeleka bafuni na kunawa, akajaribu kupikicha macho yake kama alivyokuwa akifanya kwenye ile ndoto na alipoona hakuna athari yoyote akarudu kitandani kulala, na kabla hajashikwa na usingizi mlango ukagongwa.

‘Nani sahizi teana asubuhi hii…?’akauliza kwa sauti.

‘Mimi baba yako mkubwa, nimefika na ugeni mkubwa sana…’ilikuwa sauti ya baba yake mkubwa, baba ambaye ndiye alimlea, na taarifa zilizofika awali ni kuwa hataweza kuhudhuria hiyo harusi kutokana na muda uliopangwa, na alilalamiak kweli na hata kufikia kusema labda mwane hakutaka ahudhurie hiyo arusi yake kwasababu anajishirikisha na mambo ya matambiko. Lakini akaipa baraka kuwa ifanyike tu maana asingeliweza kuacha shughuli zake za shamba kuna mbegu alishazitayarisha mapaka azipande kwanza. Maneno akajiuliza sasa imtokeaje mpaka akaamua kuacha hizo mbegu na kuwahi kufika tena kwa muda muafaka…kwa kweli, ilikuwa ni mshangao kwa Maneno.

‘Mimi nashangaa bwana harusi mtarajiwa unalala mpaka sahizi, ulitakiwa muda huu unachukua mazoezi, unajiimarisha mwili maana unakwedna kuingia uwanjani, lazima uonyeshe kuwa kazi unaiweza, sio unaingia uwanjani, hata dakika kumi na tano hazijaisha umechoka…namna gani mwanangu, unataka uniangushe…’ilikuwa kauli ya baba yake ambaye kwa kuongea Maneno kasingiziwa, na pembeni yake alikuwa kaongozana na wazee wengine watatu , ambao Maneno anawafahamu kuwa na wazee wa huko kijijini.

‘Baba na wewe kwa utani wako …hujazeeka tu, …mzee mbona raha, sikutarajia kuwa mngelifika, maana taarifa ile ya kunikatisha tamaa ilinivunja nguvu kabisa, mama yeye mbona hajafika,au yupo njiani? Niasameheni sana kwa kushindwa kubadili tarehe ya harusi , sio kusudio langu, ….’Maneno akawa anaongea hili na lile huku akaipokea mizigi ya wale wazee.

‘Haya yote yamepangwa ili iwe hivyo, usijali sana, ni heri pia kwako, …..Ingelikuwa hivyo nije na mama yako, lakini kama nilivyosema kuna mbegu zilikuwa tayari, …kwahiyo tukajiapnda, nije mimi au yeye, nikaona hapana, lazima nije mwenyewe, niliwaza sana, nikasema hapana, ,mtoto nimelea mwenyewe, nikampeleka jando mwenyewe, nikamsomesha, …halafu anafikia kuoa, nikose, hapana, ..sitaeleweka vyema na mdogo wangu huko alipo, nikawakusanya wenzangu hawa tukasema lazima tuwahi , maana lazima tufanye vitu vyetu kabla hujaweka mwali ndani, lazima tuweke mazingira yawe safi, na kweli tukiwa njiani tukahisi jambo, kama tusingeliwahi, mwanangu sasa hivi ungelikwua ukilia upofu….’akasema yule mzee.

‘Ningelikuwa kipofu, baba mbona sielewi hilo, ina maana ile ilikuwa sio ndoto ni kweli…?’Maneno akauliza kwa mshangao.

‘Wewekijana bado mdogo sana, hii dunia ina mambo ya ajabu huwezi kuyaona, ila sisi wazee tulishayajua hayo mapema sana…kuna jinamizi linakuandama, na hili ni kwasababu ya hii ndoa, …hebu kwanza niletee maji kwenye beseni tuondoe huo utando ambao umekwisha wekwa machoni mwako, unajiona kuwa unaona, kumbe huoni, huo utando ukipenya machoni mwako, basi umeshakuwa kipofu, utakuwa uanona giza …..’akasema mzee mwingine waliyeandamana na baba yao na kumfanya Maneno abakie kuduwaa.

Maneno akaleta majisafi kwenye beseni na wale wazee wakalizinguka lile beseni wakiozungumza maneno ambayo Maneno hakuyaelewa vyema, na mara akasikia mlio, ilikuwa sauti ya upepo,kama ule ule upepo aliousikia kwenye ndoto, na mara nje kukawa kama kuna vumbi, linalotokana na huo upepo, alichofanya Maneno na kuficha macho yake kwa kuvaa miwani yake ya jua...

‘Haya njoo hapa unawe hayo macho yako, ondoa hiyo miwani, haisaidii kitu , kama ingelisaidia ungeliivaa wakati huo utando ulipokuingia mwanzoni. Mwenzako alishajiandaa kukuharibu macho yako, alijua akikuharibu hayo macho hutampata huyo binti. Amekuwa akikuwinda kila siku, ila imani yako ya dini imekusaidia sana…, lakini alishajua wapi pakukupatia, alijua kuwa wewe ukilala unajisahau sana na hilo ni kwa wengi, watu wakilala wanalala kama magogo, hawamkumbuki mungu, utalalaje masaa manne au sita, bila hata kujigeuza na kumshukuru, au kumuomba mungu wako…sasa wenzenu wanatumia mwanya huo…na, hapo alitupa bomu lake…bahati yako….tuliliona sisi wakati tupo njiani, tukalizuia….’akasema yule mzee aliyeongozana na baba mkubwa.

‘Haya mapya ,sasa huyo jamaa ni nani?’ akauliza Maneno.

‘Haina haja ya kumfahamu, maana tutakuingiza kwenye ushirikina, nia yetu ni kusawazisha haya majambo, ila ni kwamba kuna mtu alikuwa anataka kumuoa huyo binti kabla yako, na wewe ukamizidi kete, sasa yeye kaamua kwenda mbali zaidi, akasahau kuwa kuna mungu, na kila kilichpangwa na mungu hakipingiki, kama kweli mungu kakupangia wewe kuwa huyo binti ni wa kwako, hataweza, atajisumbua na mwsiho wa siku ataumbuka…yeye, kuna mengi zaidi ya hayo , ila kwa vile umeshaharibu, haisadii kitu, huyu atakuwa wakwako…mungu atakusaidia’akasema baba mkubwa.

‘Namshukuru mungu,na namuomba mungu afanye hivyo, ila ningeliepnda kujau angalau kidogo, ndio nimeharibu, lakini sio kwa hivyo, wote tunafanya haivyomsiszani kuwa nyie wazee walimuoa tu, hata ,,,lakini namuomba mungu anisaidie na ndoa yetu ifanikiwe, nawashukuru wazee wangu kwa kufika wakati muafaka..’akasema Maneno.

‘Mshukuru sana mungu wako na mshukuru sana dada yako anakupenda sana, alisisitiza sana na kuniomba nisikose, alifikia hata kulia, kunibembeleza nifike, ni juzi nikaoata ndoto kuwa kuna jinamizi linakuandama, na ndoto kwangu ni kiyoo, inanibashiria mengi, nikaoan niwaone hawa wazee, na wao wakakubali kuwa kuna jinamizi, nikasema aaah,lazima tufike huko na wazee wenzangu hawa, …najua kuwa mnazarau sana mambo ya asili, …na baya zaidi mnazarau mambo ya sili na kujifanya mnafuata mambo ya kisasa, …’akasema baba mkubwa.

‘Tatzi hawa wanajifanya wanafuta dini, lakini dini yenyewe hawaijui, hawaifuati itakiwavyo, huwezi ukasema wewe ni dakiatari wakati hata udakiatari huujui, dini inakuwa kama kiini macho tu, kudanganyana, isomeni vyema, na ifuateni vyema, sio nusu nusunu, mnachofuata ni mambo ya kuiga, na mwisho wa siku mnazurika bila kujua, …mungu hampo naye, mambo ya sili mumeyazarau, mnaishi usasa ambao hautibi bila kuacha majeraha, na majereha mengine hayatibiki pia….’akasema mzee mmojawapo.

‘Duuh, kweli , lakini ni bora kufanya hivyo kuliko kukimbilia mambo ya asili kwa ujumla, yapo mazuri, tutayafuata lakini mambo, yale yaaah,…’akasema Maneno.

‘Nakuelewa vyema kijana, sasa hebu fikiria huyo mwenzako angetaka kukufanya kitu kibaya ungeligfanayje maana jamaa huyo alitaka hata kukiharibu kiumbe kisicho na hatia, lakini hajafanikiwa, …binti yupo safi ,….hongera bwana mdogo, ingawaje umeharibu kabla…cha muhimu jaribuni kusoma mambo yote , ya wazungu nay a wazee wenu pia….’akasema baba mkubwa, lakini Maneno hakuelewa kabisa baba yake alikuwa na maana gani, `kuharibu’ mawazo yake yalikuwa jinsi gani wazee hawo walivyogundua hilo tatizo aliloliota …..

‘Mwambie huyu, na wenzake wanaojifanya wasomi, ndio someni, lakini someni pia na mambo yenu ya asili, yapo mengi yatawasaidia…hata wazungu sasa wanafanya utafiti wa dawa asili na kuzirutubisha, wamegundua kuwa kuna tiba safi kabisa…na pia sisi wazee wenu wapo waliobarikiwa kuwa na uoni wa mbali,..huo ni usomi wa hali juu, uoni huo wanao wazee wenu, lakinihatujakwenda shule, lakini tuanaweza kufanya mambo yetu tukaona hatari inayokuja tukajihami nayo, hebu jiulize, hilo bomu, lililotupwa na huyo mwenzako ulikuwa uanlijua, …mbona sisi tumelijua, tuakalizua kabla halijakuathiri wewe na mwenzako na mtarajiwa… huo ni usomi wa asili, ….sasa zarauni hayo, na sisi mababu zenu tunaondoka, mtabakia na usasa wenu….’akasema mzee mwingine na kumuacha Maneno hoi.

Maneno akaishia kutabasamu, maana wanavyomtaja mtarajiwa wake, wanazidi kumpa hamasa siku ifike, yeye hakuwa na mawazo zaidi lakini maneno haya ya mwisho yakamzindua na kuuliza…

‘Umesema mwenzangu na matarajiwa, inaonyesha kama mnataja watu wawili, yupi tena huyo mtarajiwa mwingine?’akauliza Maneno.

***********
Maua alijikuta kihema kwa wasiwasi, na kila alivyojaribu kukimbia alikuta hilo jitu linalimfuta lipo nyuma yake, lilikuwa jitu la ajabu limejifunika majani, na mara kwa mara aligeula ili kulitizama ni jituu gani, lakini hakuweza kuligundua sura yake, akazidi kukimbia, na akaanza kusukia maumivu, makali, maumivu hayo yalianza kama kichomi, na baadaye yakawa makali sehemu yote ya tumboni…

‘Ohhh, mtoto wangu….’akajikuta akisema

‘Na bado nitahakikisha kila kitu kinaondoka humo tumboni, na baadaye utakuja kunipigia magoti…’akasikia sauti kali ikisema, ni sauti ambayo alishawahi kuisikia, lakini hakuweza kuitambua mapema kuwa ni ya nani.

‘Huniwezi wewe, na ikuogopi….’akasema kwa kujipa moyo, huku anakimbia.

‘Tutaona mwisho wake…’ile sauti ikamjibu.

Aliendelea kukimbia , lakini sasa nguvu za kukimbia zilipungua sababu yay ale maumivu na lile jitu likwa limemkaribia na kumpita mbele yake likasimama na kusema `haya sasa hebu angalia akzi yangu, …’

‘Maua akajiuliza aangalie nini, ..!’

Kwasababu yay ale maumivu ya tumboni, Maua akaamua kuinama kutizama chini, mara akashituka na kurudisha macho kuliangalai lile jitu, na hakuona mtu tena, aliona mwanga mkali ukimmulika machoni, na alihsis kama alisikia kitu kama ukulele, lakini hakuweza kuwa na uhakika nao, mawazo yake yalikwua kuangalia kile kitu alichokiona mwanzaoni, na kuinama tena kujiangalia , lakini hakuweza kuinamisha kichwa, ilikuwa kama mtu aliyesimikwa hawezi kuinama.

Maua aliwaza akijiuliza kuwa hicho alichokiona mwanzaoni ni ndoto au ni kweli, na kama ni ndoto mbona sasa anashindwa kuinama na kujiangalia chini, na sasa hakusikia tena yale maumivu ya tumbo, bali alihisi njaa, akasema ngona niinuke nikatafute chakula, lakini mwili ulikuwa kama umekufa ganzi, akaanza kuwa na wasi wasi, ina maana mwili umekufa ganzi, ina maana kashikwa na kiharusi, haiwezekani, akajaribu tena na tena , lakini hakuweza…na mara ghafla aksikia kitu kama ukulele ambao ulimfanya ahisi vibaya masikioni, …akazindukana,kumbe ilikuwa ni ndoto.

‘Maua vipi , mbona nimesikia kama ulikuwa unapiga ukulele, na kuweweseka, ulikuwa ukimuota tena aliyekuwa mume wako nini, nakuomba sana ukubali kuwa huyo hayupo tena duniani, sasa mfikirie Maneno…?’ ilikuwa ni sauti ya shangazi yake, ambaye alikuwa kasimama mlangoni. Na Maua aliinuka pale kitandani na kukimbilia chooni,….baadaye akarudi!

‘Shangazi, siku zote namuota Mhuja, lakini leo nimeota ndoto nyingine ya ajabu kabisa…’Maua akasema na kuinama kujikagua tena na kufunua lile shuka ple kitandani kukagua kuwa hakuna kitu…, na hakuamini macho yake kuwa kile alichokiona ilikuwa ni ndoto, na alisimama tena na kujaribu kuinama na kuinuka, halafu akaangalia tena miguuni, halafu iakasema kwa sauti `kumbe ilikuwa ni ndoto.

‘Umeota ndoto gani mbaya mwanangu’akauliza shangazi ambaye alikuwa kaduwaa, alipoona hivyo vitendo vya binti yake.

‘Hata siamini, maana nilijiona nimesimama kweney dimbwi la damu…na hayo maumivu hayaelezeki…!’akasema Maua.

‘Dimbwi la damu, damu hiyo ilikuwa ikitokea wapi..?’ akauliza shangazi.

‘Huku. Chini…na sijui ilianza kutoka lini, ila nilisikia maumivu ya tumbo yaliyoaanza kama kichomi, na nilipoinama chini nikakuata hivyo, mwanzoni nilikuwa nikifukuzwa na jitu nisililolifahamu limejifunika majani, na karibu linikamate,lakini sijui lilipoteaje..’akasema Maua.

‘Nimeshakuambia ukilala hakikisha umemuomba mungu akulinde na mabaya ya usiku, ujue maadui na watu wabaya wapo wengii na wote wanataka kujionyesha kuwa wao wana uwezo zaidi ya mungu, lakini hawataweza kama utamtegeema mungu peke yake…sikiliza mwaangu usigope kabisa, na ukiota ndoto kama hizo usiwe na wasiwasi moyoni, jipe moyo na ikiwezekana liambie hilo jitu au kitu chochote cha kutisha kuwa halikuwezi, na omba kwa mungu atakusaidia..’akasema shangazi.

‘Na huyu mtu nitamwendea leo na tutapambana naye, nilihisi hivyo, na sikulala , ilibidi usiku niamuke na kukesha kwenye ibada, na hataweza, lakini lazima nikamuone ajue kuwa najua nini anachokifanya, yeye anajifanya anajua mambo ya kishirikiana sio, basi mimi simuogopi..’akasema Shangazi kwa hasira.

‘Kwani ni nani mbona inaoneka kuwa kuna mtu unamjau ambaye unahisi kama anataka kunizuru,..au sivyo shsngazi, usiniambie kuwa unaamini mambo hayo,shangazi unaamini mambo hayo ya uchawi…?’ akauliza Maua kwa wasiwasi.

‘Hayo yaache, usiwe na wasiwasi, hakuna kitu kitakachokuzuru, ilimradi umtegemee mungu wako, ngoja nitoke kidogo, lakini sasa unajisikaaje..?akauliza shangazi mtu.
‘Sasa najisikia mwepesi, sio akam ilivyoikuwa ndani ya ndoto, nilikuwa mzito wa ajabu , hata kukimbia ilikuwa nakimbia kama roboti.

‘Basi tulia kwani wapambaji watafika muda sio mrefu, mimi natoka kidogo, wakija muendelee,…’akasema shangazi akiwa kajawa na hasira moyoni, na nia yake ilikuwa kwenda kwa huyo mtu anayemuhisi moyoni kuwa anataka kuleta mambo ya kishirikina akatika familia yake…hakujali na huwa hajali mtu . Akaondoka akiwa na hasira zake, na hili aliliona Maua , na kujiuliza moyoni shangazi anakwenda wapi.

‘Lazima nimfuate maana huko anakokwenda kunaweza kukazuka balaa,sipendi shangazi aijingize kweney matatizo kwa ajili yangu..’Maua akasema huku akijiandaa kumfuata shangazi yake, na kabla hajaondoa mguu akasikia kama mtu anagonga mlango, akainuka kweda kufungua mlano, alipofungua, alishikwa na mshituko mkubwa sana, karibu adondoke chini,….

NB, hii sehemu kama kawaida imeandikwa katika uharaka usio wakawaida, tusameheane kwa makosa ya hapa na pale. Na swali kubwa hapa ni uchawi na nguvu za giza, unaziaminije, je iliwahi kutokea kwako, na je ndoa yako iliwahi kukumbwa na mambo kama haya, mvutano, nk, naombe tuchangiane mawazao

Ni mimi: emu-three

Monday, November 21, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-52




‘Kaka nimekujia tena, …nina jambo moja la kujadili na wewe, najua kwa ubishi wako, hili jambo hutaliona la muhimu sana kwako, lakini kwetu kama wanafamilia ni la muhimu sana…’akaongea dada mtu, aliyefika akionyesha kuwa kaja lakini ana haraka ya kuondoka. Na wakati anaongea aakawa anachnuza mle ndani , kama vile ndio mara ya kwanza kuingia, …aligeuka kumwangalia kaka yake ambaye alibakia kaduwaa, …kwani hakutarajia ujuio huo na alishapangilia safari zake,lakini kwa kumuheshimu dada yake ikabidi asitishe hiyo safari yake, akijua labda ni mazunguzmo mafupi tu.

‘Jambo gani tena hilo daa, usiniambie umekuja kwa ajili ya rusha roho zenu na ya kuwa pesa hazitoshi, najua mambo yenu yanakwenda bila nidhamu ya bajeti, haya niambie dada kuna nini zaidi..maana umenijia bila kujua kuwa utafika, nilisharatibu mipangilio yangu…lakini kwa vile wewe ni mtu muhimu sana kwangu itabidi nikatishe hii safari, haya kuna nini cha muhimu…?’akauliza Maneno akiwa kaangalia nje kwa kupitia dirishani.

‘Kaka kwa kujifanya mzungu, ..hilo la rusha roho ni mojawapo ya mambo ambayo nataka tuyajadili leo, najua huhitajiki sana kulijadili hili nililokuja nalo leo, sisi kama wanandugu tulikuwa na jukumu la kujadili na kuamua na mwisho wa siku tunakupa taarifa tu,…huo ndio utaratibu …..,lakini hili linahitaji uwepo wako. Kwanza ni kuhusu tarehe ya siku ya harusi, hiyo tarehe hatuiafiki, kwa sababau za msingi, sio tu tumeamua hivyo, tunazo sababau za msingi…’akasema dada huku akikaa vyema.

‘Tarehe hamuaifiki kwa vipi tena…’akauliza Maneno kwa mshangao.

‘Kama sikosei tarehe hiyo iliyokuwa imepangwa awali, ilipangwa na waolewaji, au sio…?’ dada mtu akauliza na kabla Maneno hajajibu kitu dada huyo akaendelea kuongea kuonyesha kuwa hakuhitai jibu la Maneno kwani alishajua jibu lake ni nini. `Katika maandalizi yetu tumejikuta shughuli zinagongana, na ujue kuwa shughuli ni watu, na kuna watu muhimu sana wanahitajik akuwepo, ….na ni lazima wawemo, kuna vikorombwezo kama rusha roho na mambo mengine lazima yawepo, kuna mambo mengi sana yanahitaji muda kidogo, kama wiki mbili mbele ya tareje tuliyopanga, hata kama ikiwezekana mwezi mmoja, lakini tunajali kuwa wewe ni mfanyakazi, kwahiyo angalau wiki mbili mbele….’ Dada mtu akawa anaongea kama cherehani, maana familia hii ilijalwia kwa kuongea.
‘Hapo siwaelewi, nasubiri hizo sabaabu za msingi maana sijasikia sababu hizo ni zipi, …..Nakusikiliza dada yangu mpendwa, maana umeshaharibu kila kitu kichwani mwangu,, …we ongea tu,…’akasema Maneno na kuja kukaa kwenye sofa, lakini macho yake yalikuwa yakikwepa kumwangalia dada yake kwani alijua kuwa hoja aliyokuja nayo hatakubaliana nayo kabisa.

‘Unajua mwanzoni tulipanga juu kwa juu, tukawatuma watu wetu huku na kule, na kwa ujumla shughuli hii mumeifanya ya haraka sana, kama vile mlitaka harusi iwe yenu pekee, kitu ambacho familia imekipinga sana. Sasa tulipotuima watu kwa kiherehere chao wakatupa uhakika kuwa tarehe hiyo haina tatizo, …nasikia kaka.’Dada akatulia kidogo kutaka kaka mtu amuelewe, halafu akakohoa kama vile kumshitu Akaka yake ambaye alishashikwa na butwaa.

‘Tatizo sehemu nyingine tukawa tumechelewa kulipia pesa, na hawa wafanya biashara wetu wanajali sana pesa, wakapata mtu mwingine aliyewaahidi pesa nyingi zaidi na kulipwa hapo hapo, unaona jambo hilo, ina maana kutafuta sehemu nyingine na mtu mwingine, na kikundi kingine, itachukua muda tena, na wengi wameahidi baaada ya wiki moja au mbili, kwahiyo ikabidi tuweke nafasi hiyo ya wiki moja mbele, …na hata ikibidi wiki mbili mbele kwa ajili ya watu wetu wanaokuja toka kijijini., …hili ni mojawapo muhimu sana kuwa kuna watu wetu muhimu tarehe hiyo hawataweza kuwahi, na ni muhimu sana katika mambo ya kifamilia na kimila hayo wewe utajifanya sio muhimu kwako, lakini sisi kama wanafmilia ni muhimu sana....’akaongea dada mtu safari hii kwa taratibu.

‘Dada mambo ya kimila, hayo nilishawambia sihusiki, kama ni ngoma, sawa, chezeni, lakini hayo mnayosema matambiko, sijui mambo gani ya kimila, ….hapana, dunia hiii haiendi hivyo, kwanza hata imani zetu za kidini hazituruhusu hayo, na nataka ndoa yenye maadili ya kidini, sio kimila, vinginevyo ningesema tukaoe kimila…hilo halina hoja kwangu na naona sio muhimu sana….’akasema Maneno, na dada mtu alijua kuwa hapo wanaweza kubishana mpaka kesho. Anamjua ndugu yake huyu toka utotoni, kwani wamkuwa karibu karibu sana, huwa wakianza kubishana jambo watakesha mpaka aingilie mtu, hakuna mtu anayekubali kushindwa.

‘Ndugu yangu, hili sio la ubishi wa utotoni, sasa tumekuwa watu wazima naongea kama dada yako, nikiwa nimeiva kifamilia, sio wewe umeiva kisasa, kisasa kina mpaka wake, kama tutaamua kila kitu cha kimila tukiache kwasababu ya kujitia, au kutaka tuonekane wazungu au watu wa kisasa, tutaendelea kuwa watumwa wa watu wengine, …hebu jiulize nini maana ya uhuru, mojawapo ni kuwa na uhuru wa mambo yetu ya tangu enzi za mababu zetu, ina maana wao walikuwa hawana akili walipoanzisha hayo mambo …achana na uzungu, achana na usasa, achana na kutawaliwa kiakili, angali sana ambo yenu ya asili tusiwe watumwa….’akasema dada mtu kwa hasira.

‘Hayo sio mambo ya uzungu, hayo sio mambo ya usasa, ni mambo ya kiimani, ndoa hujengwa na mambo ya kiimani, mila hapo hazina nafasi, ila kwa kunogeza, sawa, kachezeni ngoma zenu , hilo siwakatazi, na kwa kusaidi hilo, hapa kuna vikundi vingi vinajua mila zote za Kitanzania, na sio Kitanzania tu , hata kiduania nzima, tutaawalika kama mnataka mila zetu zionekane, sio lazima kuwaita watu toka huko kijijini…lakini sitaki hayo mambo mengine sijui mnaita matambiko …ya nini hayo, eti mpaka watu waje toka kijijini kuyafanya hayo…, mnataka nieleweke vipi na watu wa familia ya kikeni, nimeshaambia kuwa ndoa yetu ni ya kidini, sasa mnataka kuleta nini hapa…hapana hilo liwekeni pembeni…’akasema Maneno .

‘Hilo sio lengo langu kubwa sana, lengo langu kubwa sana ni tarehe ya ndoa, tumepanga kuwa isogezwe mbele, wiki moja au mbili mbele, ili tupate muda wa kujipanga vyema, kwa ajili ya wanafamilia muhumi kuhudhuria, na wageni wengine na hivyo vikorombwezo vinginevyo, naongea kama muwakilishi wa familia, hili sio swala la dada yako peke yake, ni swala la wanafamilia, hutakiwi kulipinga na nimekuja kukupa taarifa tu kwa vile wewe na mimi tupo karibu sana, ilitakiwa kupewa taarifa tu yamekwisha lakini mimi nakujua kuliko watu wengine wote, ndio maana nikaja kukuelzea hili, unanaielewa kaka…’akasema dada kwa ujasiri.

‘Mwanzoni umekuja vyema, ukasema tujadiliane, sasa unataka uharibu, hapo tutakosana, na mtakuta nafunga ndoa peke yangu na washikaji zangu haafu tutasubiri hayo mambo yenu , lakini wakati huo nimeshafunga ndoa yangu.Dada hili halitawezekana tarehe ni ile ile piga ua,….’akasema Maneno huku akiwa kakunja ngumi na kuitikisa.

‘Tarehe itasogezwa mbel epiga ua, penda usispende,…mimi ndio dada yako na unanijua vyema, na sio kwamba nafanya kuonyesha kuwa mimi ni nani, ila nafanya kwa nia njema ya kifamilia, ukiwemo wewe, utakuja kunisifia baadaye kwa hilo, na ni lazima ujue kuwa ndoa itafungwa kwa mujibu wa familia, sio kwa kujitakia wewe upendavyo na hao watu wako, kama ungelitaka ungelifunga kimya kimiya, lakini kwa vile unajua kuwa ndoa inaigusa familia ndio maana ukatuarifu, sasa fuatana na wanafamilia, umenielewa hilo kaka…?’akasema dada mtu kwa jaziba huku akiwa kashika kiuona licha ya kuwa kakaa kwenye sofa.

‘Hapana hilo halitawezekana dada , maana nimeshaongea na waolewaji, na waliniuliza mara mbili, mara tatu ya jana nilipoongea na shangazi mtu, ambaye ndiye muhisika mkuu nimemkubalia kuwa taerhe ni hiyo hiyo. Unasikia dada, nilimuhakikishia kuwa tarehe ya kuoa ni siku hiyo hiyo iliyopangwa toka awali, ..hebu kaa katika upande wangu utalielewa hilo…hayo maswala mengine sioni kama yana umuhimu sana, kama mnataka mtayafanya hata baada ya ndoa…hiyo ndiyo kauli yangu mimi muoaji…basi’akasema Maneno.

‘Hivi wewe unaongea kama nani , kaka, kwanza kwanini ukaingilia mambo yasiyokuhusu sisi tulishakuambia kuwa maswali ya harusi hayakuhusu kwa sasa, wewe ni mgeni rasmi, waandaaji ni sisi, ilitakiwa ukae na sisi kwanza kabla ya kutoa tarehe hiyo, kazi ya kuongea nini kifanyike kati yetu na wao, inasimamiwa na mshenga wetu, je mlikaa na mshenga mkaliongelea hilo, au uliamua kuongea na wao peke yako…mbona unatuzarau kiasi hicho, sasa utajua mwenyewe jinsi ya kuwaambia, kwasababu nakuona kuwa wewe ndio mshenga, wewe ndio muoaji , wewe ndio familia, na utafanywa muolewaji pia badala ya kuwa muoaji…usibiruzwe kaka…,’akasema dada mtu.

‘Dada naona sasa umenichoka, unataka kuleta ubishi wa utotoni, …unajua dada sio kwamba najiamulia mwenyewe tu bila kuwa na sababu za kimsingi, naomba unielewe hivyo, sio kwamba naizarau familia yangu, hapana, ….mimi na familia ya mtarajaiwa wangu tumekuwa tukiishi nayo kwakaribu sana, tangu marehemu akiwemo, na aliniaminimapaka akniachia familia yake, na hili la kuoa ni moja ya kuonyesha upendo wangu kwako,kwa familia ya mke matarajiwa na upendo wangu wa dhati kwa maarhemu….’Hapo Maneno akatulia akimkumbuka marehemu, na dada amtu akamuelewa , aye akautulia kidogo.

‘Sasa dada mimi nilionekana kama mmoja wa wanafamilia hiyo husika, na tumekuwa tukikutana nao mara kwa mara..sio swala la kuburuzwa, mimi ni kama ndugu yao, na ilipofikia hili swala, tulishakaa nao na kuongea kwa mapana na kuangalia kipi kifanyike na kwa muda upi, kwa manufaa ya pande zote mbili, kwahiyo swala la lini sherehe ifanyike sikuona haja ya kukutana na familia yangu kwa muda huo, na nilipowaambia hamkupinga hoyo tarehe, mliikubali, …na kwa vile ilikuwa shughuli ya haraka kwasababu za afya ya mtarajiwa, muda huo ulitosha kabisa kwa sisi kujiandaa, na haikuwa na haja ya kufuata milolongo yote hiyo, sijui mshenga aende wakajaidli arudi, tukae tuongee …sijui muende mkaangalie tarehe hiyo ni…hapana dada hayo yamepitwa na wakati…naomba mnielewe, mengine sin haja ya kuyaongea…yana msingi …’akasema Maneno kwa kutulia.

‘Nimekuelewa sana kaka yangu, na kukuelewa huku sio kwamba nakubaliana na hayo maneno yako kama jina lako, hapana nimekuelewa kwasababu wenzetu wamkuwahi mapema,wameshakuweka hapa…’akanyosha kiganja cha mkono na kukigonga na kidole cha mkono mwingine. `Na hili tusipoliangalia mapema, tutakupoteza kaka yetu, tutakuwa hatuna usemi mbele ya wifi mtarajiwa, kaka utapotea , utakuwa mke badala ya mume, angalia sana hilo, sisi tunyajua haya yote hasa yanapoingiliwa na sisi wanawake, siumesema shangazi yenu alikuja hapa, mkaongea…nilijua tu, huo sio uamuzi wako,..’dada mtu akainuka haraka kutaka kuondoka.

‘Dada sasa unaondoak vipi, tumefikia wapi, nataka ukiondoka hapa ukanitetee, kumbuka dada tumekuwa pamoja, na tulikuwa tukisaidiana toka utotoni, hili unatakiwa unisaidie kwasababu lina umuhimu sana kwangu…dada mkikutana pigania tarehe hiyo hiyo kama kweli unanijali ndugu yako, na mkitaka kuibadili kinguvu, kwakweli mtakuwa mumeniweka mahala pagumu, na sijui kama nitaeleweka vipi,…naomba tafadhali uwaambie wanafamilia kuwa tarehe ni hiyo hiyo, vinginevyo tutagawana mapande, kitu ambacho sikitaki…’Maneno akawa anongea huku anamkumbuka shangazi mtu alipokuja hapo na kuongea naye, alikuja kama mbogo utafikiri kuna kosa limefanyika, alionyesha uso wa hasira.

‘Maneno nimekuja hapa kwa nia moja kuwa ndoa nataka ifungwe haraka iwezekanavyo, kwa ajili ya afya ya mwanangu, hili nalisisitiza tena, kwasababau wewe mwenyewe umelikoroga…na chanzo ni mimi kuwaruhusu mwende huko Arusha, umemweka mwenzako katika wasiwasi mkubwa, hajiamini,…’Akasema Shangazi mtu.

‘Kwanini hajiamini, kwani kuna ambolimetokea, anahis kuwa ana…’Maneno akasita kumalizia hayo maneno ayke akijua kuwa anaongea na mkwe wake.

‘Najau utawaza hilo, kwasababu wewe hukuon akuwa umefanya makosa, na najuta kwanini sikukuweka ndani kwanza ukawa ana adabu, kuwa familia yetu sio ya kuchezewa, …lakini nimekuja kuyazungumz ahaya nikiwa na maana kubwa sana, juzi alikuja mshenga wa yule jamaa ambaye toka siku nyingi anataka kumuoa Maua, akaweka mikwala kuwa yeye ndiye mwenye haki ya kumuoa Maua, sijui haki ghani hiyo…watu wengine bwana,anadai kuwa ana haki kwasababu ndiye aliwahi kuleta posa, …sasa kama hutumtaki …’akasema Shangazi huku akicheka, lakini kumbe moyoni kwa Maneno wivu ulishamjaa.

‘Eti anadai kuwa atafanya kila njia kuhakikisha ndoa hii haifanikiwi, kama atakataliwa yeye….kwangu mimi sikutishika, ila nyie vijana mkishauriwa mfanye nini cha muhimu hamfuatilii , matokeo yake mtaingia kwenye ndoa ka uanza kugombana na huyo jamaa kwani anajivunia pesa, ….sitalkipenda hilo …ndoa itakuwa inalega lega, lazima muanze kushirikiana kuanzia sasa, kuaminiana,…na dawa kubwa kwa sasa ni kuhakikisha mnaifunga ndoa hiyo haraja iwezekanavyo, msiwape hawo wabaya nafasi…hilo ni la kwanza ambalo nalilisisiza kwenu…tumekubaliana kuwa tarehe itakuw ile ile au sio…?’akauliza Shangazi.

‘Kwangu mimi hakuna mashaka, tarahe hiyo inajulikana labda itokee zarura, na mimi sio mungu, tunachoomba ni iwe hivyo, kwanini shangazi una mashaka na hilo, Maua ana lolote jipya..na umemuuliza kwanini ilikwenda kule hospitalini?’akauliza Maneno akiwa na mashaka.

‘Nimemuuliza, yeye alikuwa na mashaka ya afya yake, na nilimsuta sana kuwa ile hospitali ina jina baya, wengi wakeidna kule wanaonekana kuwa wamekwenda kutoa uja uzito, sasa yeye asijipeleka kule walimmwengu ni wabaya watazua mambo yao, na hata huyo docta ni muongo, anaweza akakubangika ugonjwa ambao huna ilimradi apate pesa…na ndilo nimekuja pia kukuonye akuwa yule jamaa sio wa kuamini sana, amewahi kumambikia msichana wa watu mimba kumbe hana, ilikuwa alimanusura angeingizwa kwenye kile chumba na mengine yangefuata, msiwe na hamasa za kumuona yule mtu atakuharibieni kila kitu…unanielewa mwanangu..? akasema shangazi.

‘Aaah, shsngazi kama unanihakikishia kuwa Maua hana tatizo alikwenda kule kwasababu ni ya kutibiwa tu, sina shaka, lakini nimekuwa nikiwaza sana, kwamba kwanini alitokea mlango wa nyuma, na…’akasema Manneno na shangazi aliposikia hivyo akashituka, kumbe Maneno alimuona akitokea mlango wa uani, …

‘Kumbe ulimuona, …Maua ananiogopa sana, na nilishampiga marufuku kutibiwa pale, kwahiyo aliposiki nakuja akaona anikimbie, …hakuna cha msingi cha kufanya hivyo zaidi ya kuniogopa. Sasa kunzia leo si wewe au yeye kukanyaga ile hospitali, nakushauri na kukuamuru kama mama, …vinginevyo mtakuja kuniambia, hakuna hata haja ya kukutana na huyo mtu kama ulikuwa na mpango huo, …yule namjua sana, ile nataka mliweke wazi, ni mmojawapo wa watu nisiowaamini…sawa, vinginevyo nitaisimamisha hii ndoa, akaolewe na mtu anayeniskiliza…’akasema Shangazi kwa msisitizo.

‘Shanagzi mbona umekwenda mbali kiasi hicho, na unaona hunitakii mema, unataka kuninya’nganya tonge mdomoni, Maua nampenda sana shangazi siwezi kumkosa, nakuhakikishia hilo, ilimradi umenihakikishia kuwa hakuna jambo lolote sina haja ya kuhangaika kwa hilo, ninakuamini wewe shangazi, lengo langu ni kumsaidia Maua kama kuna lolote, unajau yeye amekuwa akijifanyia mambo yake kwa lengo kuwa haihitajii msaada wa mtu yoyote, na matokea yake anaumia, ndio maana nilitaka kujua kama lipo hilo nimsaidie , sina nia nyingine mbaya nakuahidi kuwa sitakanyaga ile nyumba iitwayo hospitali maalumu, nimesikia sifa zake, na nitajitahidi kuhakikisha kuwa Maua hakanyagi hapo….’akasema Maneno kwa unyenyekevu na kumfanya Shangazi atulie roho yake akijua sasa ammbo yanakwenda vyema.

‘Na tumekubalaiana kuhusu tarehe, kwasababu kuna wageni wangu wanatoka nje, wamekata tiketi ya kwenda na kurudi, hawawezi kuja hapa waambiwe kuwa tarehe imebadilika, ….ni muhimu sana ujue hilo wewe ni msomi, mambo yanakwenda ki muda, usiyapeleke kienyeji maana najua wakikutana wanandugu wengi kila mmoja an lake, sisi tunajali sana muda, …tafadhali zingatia hilo ni kipindi cha kujua nini unachokifanya sio kuburuzwa huku na kule, sasa ni mueleeko mmoja wa wewe na mkeo hakuna cha wengine kukuingilia…nakuasa kwa hilo, kwaheri..’akasema shangazi na kuondoka.

Maneno alipokumbuka hayo Maneno ya shangazi na kauli za dada yake akajikuta njia panda, je afanaye nini cha kuhakikisha hii shughuli haitetereki, akachukua simu na kumpigia mshenga wake, ambaye alikuja baada ya muda mfupi na kuongea naye , alimweleza kuhusu mgongano wa siku ya harusi na anataka yeye asimamie uapnde wake, kuwa harusi tarehe ni ile ile, na anachotaka yeye afanye ni kwenda kwa waolewaji akachukue hizo sababu muhimu azifikishe kwa familia yao.

‘Afadhali nimeongea na wewe hili, maana hapa nilikuwa njiani kwenda huko huko kwa waolewaji, na bahati nikapokea simu yako, nimetumwa na familia yenu kwenda kuwaambia kuwa tarehe ya ndoa imebadilika, na hili nilijua mumeshakubaliana nalo, nashanga kusikia kuwa wewe upo kinyume na familia yenu, …naona ajabu, sasa niende kwa msimamo gani, wa tarehe ile ya awali au tarehe hii mpya?’ akauliza mshenga.

‘Nisikilize mimi muoaji, …tarehe haijabadilika,, wewe tafuta mbinu za kuja kuwaambia ndugu zangu ukitoka huko, kwani najua ukifika huko msimamo wao ni tarehe ya awali, na mimi nipo pamoja nao….’akasema Maneno.

‘Upo pamoja na famili yako au na famili ya waolewaji?’ akauliza Mshenga.

‘Si kwamba naipinga famili ayangu kwa tarehe hiyo, lakini henu animabie kama nilivyokuelezea awali, kama ingelikua wewe ungelifanyaje, maana waolewaji walishaniuliza swali hilo mata zaidi ya tatu nikawapa uhakika kuwa tarehe ni hiyo hiyo…’akasema Maneno.

‘Sasa mimi ni mshenga, hakujaharibika neno ngoja niende kuwaona, mabo yatajiweka sawa, ikishindikana inabidi familia zote mbili zikutane, zijadiliane, halafu tutaafikiana, sioni kuwa kuna tatizo, na kwa vile nmesikia kuwa wewe mhusika mkuu upo katika msimamao wa atrehe ile, ile sasa ninajua nini cha kufanya, hilo niachie mimi, ngoja nikaonane na waolewaji, hili muhimu sana kwangu….’akasema na kuondoka.

Kesho yake ilibidi kuwe na kikao cha familia mbili, kwani kila mmoja alikuwa kasimamia msimamo wake na kikao hicho kilikuwa kigumu sana, na hakuna aliyetaka kubadili msiamamo wake. Mwishowe shangazi akasimama na kusema;

‘Unajua tusiwe kama watoto kwa hili hatutaki kushindana kwa kitu kidgo kama hichi, ili twende sawa, kuna wageni wangu wametoka Ulaya, kama Maneno ana ubavu wa kuipia fidia ya tiketi ili kubadili siku zao za kukaa hapa sawa, pili gharama za makulaji , kwasababau wamefikia hotelini, tatu, gharama za usumbufu kwasababu siku hizi tunakwenda kitaalamu msizanie kuwa haya maswala ni ya kwangu mimi na Maua kuna wanafamilia wanaishi nje na wameamua kuja kushuhudia hi ndoa, ndio maana tukasisitiza sana hiyo tarehe, na tuliuliza mara nyingi sana…’akasema Shangazi.

‘Ulimuuliza nani, wewe ulimuuliza Maneno, Maneno hana mamlaka na familia, anayo lakini kwa ,makubaliaono, na hili linaonekana kuwa ulimshawishi Maneno kwa matakwa yenu, sisi ndio waoaji tunahitaji tarehe ile ambayo binti yenu akija kwetu kusiwe na shaka, kutokana na mipangilio yetu, kuna wazee wetu kwa haraka hivyo hawataweza kuhudhuria…tunakuomba utuelewe na sisi , …kwamba hata sisi tuna gharama kama hizo, …’akasema muongeaji wa waowaji.

‘Mimi naona tutashindana kwa swala dogo sana, hili tutalitatua kama muoaji atataoa kauli yake ya mwisho, naomba tumuite aseme mwenyewe anataka tarehe gani, kama atakubalaina na hilo la familia yao, basi tutaangalia jinsi gani ya kuchangia hizo gharama, kama atakuabaliana na tarehe ya awali inabidi wanafamilia mliangalie upya jinsi ya kuliweka sawa, tarehe isiwe kikwazoo cha jambo muhimu kama hili..’akaseme Mshenga.
‘Huyu muoaji hawezi kutuamulia , keshwekwa sawa, mkimuita hatatoa jibu lolote la muhimu..’akasema dada mtu.

‘Hpana yeye ni mtu muhimu sana, hasa ukiangalai kigharama , ukiangalia na muda wake wa kazi, na yeye ndiye anajua maisha yake ya baadaye, sisi ni wapiga debe tu, tunaomba hili mliangalie kwa makini…’akasema mshenga na wazee wengine wakakubaliana na hilo, na hapao akaitwa Maneno.
Maneno alipofika hapo kwenye kikao akakumbuka jana kuwa alipigiwa simu na baba yake mkubwa, baba yake huyu ni mtu maarufu katika familia yao, na alipenda aje kuhudhuria hiyo harusi , akaomba isigozwe mbele kidogo ili afike na kundi lake la wanafamilia wengine...

Maneno akabakia kuduwaa, na kujiuliza haya yote ni ya nini,na wakati anawaza haya huyu mzee alisisitiza kuwa kwa vile Maneno ni mwanaume peke katika familia ya ndugu yake, hakupenda kabisa kuikosa hiyo shughuli muhimu, …Maneno alishindwa kabisa kumshawishi kuhusu tarahe iliyopangwa awali, kwani alipomwambia kuwa tarehe ilishapangwa, baba huyu alimuuliza `ina maana hutaki mimi baba yako niliyekulea nihudhurie hiyo harusi…na tarehe hiyo sitaweza kufika kwasababu ya mipangilio ya hapa nyumbani, tafadhali naomba uisogeze mbele angalau wiki mbili mbele...!’ Basi Maneno akabakia kimiya,na hakujua afanye nini, sasa kaitwa kautoa kauli yake,…sasa afanyaje

NB JE INGELIKUWA WEWE Ungelichukua uamuazi gani,?

Ni mimi: emu-three

Friday, November 18, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-51



Maandalizi ya harusi yalipamba moto, vikao vya hapa na pale vikafanyika, na siku hiyo Maneno alitembelewa na mmoja wa dada zake, nia kubwa ni kutaka kujua mambo fulani fulani, kabla ya siku yenyewe, maana sherehe hasa ya harusi ni akina mama, huwezi kuwaambia, kitu.
‘Kaka hayo mambo yako ya kutaka sherehe fupi, sijui hutaki hiki, …nimesikia kuwa hutaki rusha roho, wewe, sitaki kusikia hilo, ukumbuke kwenye familia yetu wewe ndiwe kaka pakee, sasa nitapata wapi mwanya wa kujirusha kama sio kwako, nakuomba hayo mambo ya sherehe tuachie sisi dada zako, wewe jiangalie uvaaji wako na wapambe wako, lakini mambo ya shughuli, hayo hayakuhusu….’akasema dada mtu.

‘Tatizo nyie mnaongea tu, mwisho wa siku bajeti ikibana mnanitupia madeni, sipendi nikiwa ndani na mtu wangu kuambiwa hili halijalipwa , hili halikuwepo kwenye bajeti, nataka kila kitu kiende kimpangilio, najua mnataka mengi, kujirusha, sijui na nini, lakini mjue kuna maisha yanaendelea, sherehe ya siku mbili, isiharibu mpangilio wa maisha mengine…’akasema Maneno.

‘Hilo nalijua sana, kwani rusha roho, na mambo fulani, unafikiri yanahitaji mshiko mkubwa hakuna kitu kama hicho, huko tumeshajipanga, wala hatutagusa bajeti yako, kuna mambo ya kigodoro, hayo ni kwa jili yetu, wazazi na walezi wako , unajua tena, hayo ni mambo ya kijamiii huwezi kuyakwepa, …nafikiri tumeelewana…’akasema dada mtu akisimama kuondoka.

‘Sawa, kama ni hivyo sina neno, hapa nawasubiri wapambe wangu kuna kikao kidogo cha kuweka mambo sawa, na vikao vyenu vinaendeleaje?’ akauliza Maneno.

‘Hilo halikuhusu kaka, nimeshakuambia, ondoa shinikizo, usipungue uzito kabisa, hayo ni mambo yetu, wewe kaa pembeni, kazi yako ni kumchora wifi tu, jinsi gani mtakavyolicheza sebene siku ya fungate lenu…’akasema dada mtu , na Maneno akaishia kucheka, kwani wakikutana na dada zake hawa hutaamini kuwa ni kaka na dada, wanataniana kama mtu na binamu yake.


Dada mtu alianza kuondoka na kabla hajafika mlangoni akarudi ghafla na kumkaribia kaka yake na hapo aliongea kwa sauti ndogo;

‘Kaka lakini mumepima, …siunajua tena mambo fulani fulani, halafu unajua siku hizi mambo hayaeleweki,…mara HIV, mara `sikoseli,’ sijui vitu gani,…wewe wajua zaidi, lakini unaweza ukajisahau kwa hilo….?’akauliza huku kamuinamia kaka yake.

‘Dada hayo mambo geni tena, ..tatizo lako unafikiri mimi ni mtu wa kuja, hilo la kupima lilishafanyika siku nyingi, …,tulishapima, na kuonekana sote tupo safi, hata viasilia vya kujua mtoto akizaliwa asije akawa na athari za kurithi, hayo yote tumeyaangalia, hilo lisikutie shaka, tena tumepima mara mbili…’akasema Maneno.

‘Mhh, nakuaminia kaka, wewe ni msomi wa kweli, ….kwahiyo swala la miwaya hatuna wasiwasi nalo, lakini kuna mambo mengine …’akamsogelea kaka yake na kumshika begani , halafu akasita kuongea kile alichotka kukisema, ..baadaye akasema , `Huyo binti namfahamu vyema, mpole na mtaratibu, lakini huwezi jua, isije siku mbili tatu, tumbo hilo…utatuambia vyema, hiyo mimba imetunga saa ngapi kama sio kabla ya ndoa…..au uniambie ukwelia kama mumeshapiamana kinamna nyingine pia, kabla ya ndoa, maana mambo ya siku hizi ni kupimana kwanza, nataka kujua hilo mapema…mimi ni dada yako, aibu ikiibuka mimi ndiye mnyoshewa kidole, una uhakika yupo safi, hana kitu….’akashika tumboni, huku anacheka.

‘Hata kama ana kitu lazima kitakuwa changu, …kwani wewe inakuhusu nini, na kwanini umuhisi hivyo, …ushamuona mhuni sana au vipi…kwanza hebu fikiria, mumewe alitoweka lini, miaka sasa miwili, na hana mtu mwingine zaidi yangu, …sasa , kwanini nitie wasiwasi..’akasema Maneno akitabasamu.

‘Na wewe kaka kweli umo, yaani binti wa watu anaomboleza kwa kufiwa na mume wake, wewe hukujivunga,…hongera kaka, ila nilitaka niwe na uhakika nalo, maana sisi wanawake ni wasiri wa kubwa, unaweza ukawa na kitu, na huyo aliyekubebesha humtaki na umepata chombo chenye nafasi, unafikiri utafanya nini, unambambikia mwenye nafasi…mjini hapa! Kaka nakwambia hapa mjini,….unajua baada ya kujifungua ikionekaan sura sio sawa na mwanaume tunafanyaje tunadai mtoto kafanana na mjomba wa babu wa bibi mzaa baba mdogo..hahaha weya, shaurilo…’akapiga vigelele huku anaondoka.

‘Wanawake bwana, hayo yote ya nini…mimi nimeshafanikiwa kukichukua chombo, sasa wanaanza kuleta majunguyao, wao wanajua nini, wangelijua kuwa hicho chombo, nilikuwa nakiota, nakitamani kwa siku nyingi, ahsante sana Mungu, ahsante sana rafiki yangu kwa kunikabidhi huyu mwanadada, ….oooh, mungu anipe nini tena, hata kama …..lakini mmmh’akaguna na kuwaza, akikumbuak tukio lile la siku ile pale alipokwenda kwenye ile hospitali na shangazi yake , ambapo shsngazi alidai huwa wanakwenda mara kwa mara kuchunguza afya zao. Kwa ujumla waanmjua sana yule dakitari, ni mataalmu wa mambo ya akina mama, lakini kuna shutuma kuwa huyo dakiatari ana mambo mengine ya ziada.

‘Lakini kwa Maua haiwezekani , …’akakumbuka jambo, ambalo aliliona alifanyie kazi baada ya hicho kikao chake na washikaji zake, `Nitamtembeela yule docta, najua nikimpa chochote ataniambia kwanini Maua alifika hapo hospitlini, lazima kuna jambo limejificha hapo, ngoja, kikao kiishe. Ngoja, lazima namimi niwahakikishie kuwa naitwa Maneno, sio wa maneno tu bali na vitendo….’akasimama kwa hamasa.

‘Lakini kama nikigundua kuna jambo baya, …’ akaikuna kichwa, halafu akajiuliza mwenyewe `Jambo baya kama lipi,…’ akajishika kidevu akitafakari, `Kwanza ile hospitali ina sifa mbaya, yule docta ana mambo ya chini kwa chini, nasikia anatoa mimba, sasa kwa mfano, …nagundua kuwa Maua likwenda kutoa mimba..nasema kwa mfano, najua Maua hawezi kufanya jambo kama hilo, ila kwa mfano…’ akasimama na kuchungulia chini kwa muda.

‘Mungu wangu kama ikiwa ni hivyo, mungu wangu, nitaua mtu…..hapo wataniona kuwa sio Maneno yule wanayemjua,sitjali cha shangazi au nani….’akakaa kwenye sofa akitizama juu, akasimama tena huku akiwaza huku anaongea kama vile anaongea na mtu pembeni yake, `Lakini kwa mfano, …tuchukulie Maua ana mimba, …hiyo itakuwa ya kwangu, …ingawaje sizani kama anayo, ni kwa mfano tu …..sasa kama ni ya kwangu, kwanini aitoe,….aaah, hana mimba yule, kwanza aitoe wapi hiyo mimba….hapana, hana kabisa,..yule namuamini sana, …hata haivyo nilishawahi kumuliza siku ile alipojaribu kula chakula na kuanza kujisikia vibaya..akabisha kabisa….maana pale nilishamuhisi kuwa anayo….alibisha’Maneno akawa anaonge peke yake utafikiri kuna mtu mwingine humo ndani , na hapo akikumbuka tukio la siku ile, alipomshuku Maua ……

Aliikumbuka sana ile siku alipotoka kazini muda wa mchana, kwa nia ya kumpitia Maua wakapate chakuala cha mchana pamoja, alitoka kazini mapema, akampitia Maua kumuomba kuwa leo kaamua wakale pamoja hotelini, na Maua akakubali, walipofika kweney hoteli, chakula kikaletwa mezani, ile Maua kikionja tu, akasimama ghafla na kukimbilia chumba cha kunawia. Huko alikaa muda kidogo na aliporudi macho yalikuwa mekundu kama vile mtu aliyekwua akilia.

‘Vipi unajisikia vibaya nini…?’akauliza Maneno.

‘Hapana, sijui nimetafuna kitu gani, maana ile nasikia harufu kinywani, moyo ukatibuka, yaani nimesafisha kila kitu kilichukua ndani, sasa nitakula kwa raha…’akasema Maua.

‘Lakini Maua upo safi kweli ….maana huko kujisikia vibaya nimekusikia mara nyingi, mara moyo kutibuka, tuambiane ukweli…?’ Maneno akazumngumza kwa kufanya utani.

‘Wewe…, una maana gani kusema hivyo, maana mume wangu kaondoka karibu miaka miwili sasa, na simjui mtu mwingine, hiyo shutuma inatoka wapi…au unataka kusema nini…?’ Maua akazungumza kwa hasira.

‘Sina maana mbaya Maua, uwa waridi wa moyo wangu, …lakini kwani mimi siwezi kubadilisha hali yako, unakumbuka siku ile kule Arusha, …inawezekana ikawa ndio sababu, mmh lakini…, samahani sio kwamba nazungumza kukumbushia hilo kwa kulifurahia lile tukio hapana….ila..’Maneno aliogopa alipomuona Maua kabadilika ghafla na sura ilijaa chuki, kuonyesha kukerwa na hayo maneno.

‘Maneno naona umetibua kila kitu, na hata chakula chenyewe kimeniishia hamu, mambo gani unayaongea hayo, unafikiri mimi nilifurahia hilo tukio, kama kuna tukio lililo niumiza katika maisha yangu baada ya kuondoka mume wangu, mojawapo kubwa ni hilo, tukio hilo naliona kama chanzo cha kuharibikiwa na mpangilio wa kaili yangu. Tafadhali kama unapenda tule hiki chakula vyema, basi usiongelee kabisa tukio lile, silipendi kulisikia…’akasema Maua kwa hasira.

‘Maua siku hizi unapendeza kweli, maana hayo siju ndio mafuta au vipodozi unavyovipaka vinazidi kukuremebsha na kuwa mweupe, utafikiri mzungu, mmmh, Maua kama kuna kitu nilichojaliwa nacho na amabacho nitakifurahia, na nimeshakifurahia ni kukupata wewe, naomba siku hiyo ifike haraka tufunge ndoa,…namuomba mungu atupe subira njema, na baraka zake ifike hiyo siku tutangazwe kuwa sasa nyie ni mke na mume…’akasema Maneno kubadili hali ya hewa.

‘Mungu ni mwema, …hilo ndilo jambo la kuomba, ….

Maneno akasimama na kuangalia saa yake baada ya ile kumbukumbu kutoweka kichwani, aliona jamaa zake wakichelewa, kwani hawo ndio washikaji wake wakuu , anawategemea kufanikisha shusguli yake, na kabla hajasogeza mguu , mlango ukagongwa, na akainuka haraka akijua kuwa wageni wake aliowategemea wameshafika, …akafika mlangoni, na kufunguo mlango, moyo ukamlipuka kwa mshituko, akabakia mdomo wazi….
******
Shangazi alipofika kwa Maua alijaribu kukaa na kuongea naye vyema, alimdadisi kwa undani nini wamekigundua huko hospitalini, lakini Maua alisema hakuna, alikataa kata kata kuwa alikwenda kule kwa nia gani, …

‘Maua mimi nakujua sana kuliko unavyojijua wewe, nina uhakika ulikwenda pale kwa nia ya kutoa mimba…kwanini unataka kuniabisha , kwanini mwanangu, ….?’akauliza shsngzai mtu kwa hasira.

‘Wewe shangazi kwanini kama ulijua hukuniambia mpema, mimi nilijua ni hali yangu ile ile niliyokuwa nayo hata alipokuwepo mume wangu, kwahiyo sikuwa na wasiwasi na hilo, …lakini aliponiambia kuwa nina ….oooh sikuamini,…sijui kwanini imetokea hivi, kwanini mimi niingie kweney aibu hii kubwa…sasa shangazi nitafanyaje, nitamwambiaje huyu mwanaume…? Maua akaanza kulia.

‘Maua ndio maana sikutaka uliue hili, nilitaka ulijue hili baada ya kufunga ndoa, maana pupa zako zinaweza zikaharibu kila kitu, sasa sikiliza, hili swala sitaki uliseme kwa yoyote yule, sitaki kabisa kusikia kuwa umemwambia Maneno, swala hilo nitaliongea mwenyewe kwa Maneno, yule nimeshamuweka mkononi, kwanza nilishamtishia kuwa kakuharibu kinyume na maadili yetu ya familia...’akasema Shangazi na kumsogelea binti yake, akamlaza mapajani mwake.

‘Sikiliza Maua hayo niachie mimi, usiseme lolote, unanisikia vyema, na wala usiongeee sana na watu, kuanzia leo utakuwa hutoki ndani, mimi na wewe tu ndio tutakwua tunakutana, hadi siku hiyo ya ndoa, na nitahakikisha inafungwa haraka iwezekanavyo, ili mambo yasije yakajionyesha mapema, nashukuru kuwa mwili wako umeongezeka, na kwahiyo sio rahisi mtu kugundua lolote, kilichabakia ni wewe kujihami….na hilo litawezekana kama utajituliza ndani…unanielewa ?’ akasema Shangazi mtu.

‘Kwanini tufanye hivyo, kwaninitusimwambie Maneno tukaahirisha hii ndoa hadi nijifungue, ndivyo ilivyo kiimani,…huoni tutafanya mambo kinyume na maadili ya kiimani…’akasema Maua.

‘Wengi siku hizi wanaona wakiwa wameshaharibu, harusu nyingi ninazozishuhudia mabinti wengi wana mimba, hata nyingine zinaonekana wazi, sembuse yako, ambayo haijionyeshi kabisa , nakuomabi hilo niachie mimi, …kwanza huyo huyo ndiye aliyekuaribia, atasema nini….akisema nyoko, nitamweka ndani, unanichezea mimi,…kwanza leo nakwenda kwake , huko nitajua nini cha kumwambia, usijali, nakuomba ukae kwa amani, ila kama nilivyokuambia usitoke kabisa humu ndani, ngoja nikapambane na huyo kidume mtu, sikiea anasema nini…’akasema shangazi huku akiondoka.

Njiani alijawa na mawazo mengi, kwani hali ilivyo sasa imekuwa tete, kinyume na mipangilio yake, alikuwa na wasiwasi je kama harusu hiyo ikaahirishwa, na je kama Maneno ataamua kwenda kuonana na huyo dakitari aliyempima Maua na kupewa chochote ili aongee, atashindwa kweli kumwambia ukweli Maneno…akajikuta akibeba mzigo mkubwa wa mawazo, hasa akifikiri wazazi wa Maua ambao wanatarajia kufika karibuni.

‘Ili kuwaweka sawa hawa wazee wanzangu, nitahakikisha ninakaa nao kwangu, na sitawapa muda mwingi wa kukutana na Maua , huyu binti nitamfunda mwenyewe nyumbani kwake, hakuna mtu wa kumuona ona, na nitahakikisha kuwa wazazi wake hawalijui lolote kuhus hilo, …baada ya ndoa kupita, sitajali sana wakijua,….mimi ni shangazi wa kikweli,…’akajipiga kifua kwa kutamba, halafu akaangalia nje gari liliposimama na kusema `Kwanza ngoja nikahakikishe huyu anayejifanya ndiye kidume wa kuharibu watoto wa wenzao, anajau nini kuhusiana na hili na kama ana midadi ya kutaka kujua zaidi, nitacheza naye sahani moja,..huyu hanitii wasiwasi nitahakikisha kuwa namweka sawa….sizani kama atakuwa na moyo wa kwenda kupekenyuea huko hospitalini …’akajipa moyo huku akishuka kwenye gari kuelekea nyumbani kwa Maneno

NB. Nawatakia ijumaa njema

Ni mimi: emu-three

Wednesday, November 16, 2011

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-50



Shangazi wa Maua alikuwa hana raha kabisa , kwani alikuwa keshajiandaa kuondoka na Maua kama walivyopanga, walikuwa wameelewana kuwa wapiti dukani wakaangalia gauni la harusi. Maua alipoipokea ile simu sauti yake iliopnyesha dhahiri kuwa kuna tatizo, na hata kabla Shangazi mtu hajauliza vyema, Maua alisema kuwa ile safari waliyopanga waifanye kesho yake maana hajisikii vyema.

‘Una umwa sana, au ni uchomvu tu, au kutojisikia vyema huko ni kwa vipi?’ akauliza shangazi mtu.

‘Sio kuwa naumwa , hapana ila sijisikii vyema tu, na naona ni bora nijipumzishe kidogo, lakini kesho tutakwenda kwasababu sina shughuli ya kufanya..’akasema Maua.

Shangazi, alivyowaza zaidi alijikuta akiyakumbuka vyema hayo mawasiliano yake na Maua, na kila alivyojaribu kuyapuuzia alishindwa. Kwa uzoefu wake, pale moyo wake unaposita kuhusu jambo fulani, na kulitilia shaka, inabidi alitizae hilo jambo kwa mapana, maana mwisho wa siku hutokea jambo ambalo anakuja kujijutia baadaye. Alikumbuka jinsi moyo wake ulivyokuwa haupendi Maua asafiri na Maneno, lakini akapuuzia na matokea yake yakatokea yale ambayo hakuyataka.

‘Ohh, nahisi kuna jambo huko kwa Maua, …moyo wangu hautilii vyema….’akajikuta akiongea pake yake na kuharakisha kumalizia shughuli zake nyingine na baadaye akapiga simu tena kwa Maua.

‘Maua kama unaumwa niambie nije huko, …’akasema Shangazi mtu.

‘Shangazi nimeshakuambia siumwi, ni hali ya akwaida ambayo hunipata mara kwa mara, lakini baadaye hutulia, nikujisikia vibaya tu, na pia nahisi labda ni uchomvu wa kazi nilizozifanya leo…’akasema Maua.

Hapo shangazi, akaingiwa na faraja kidogo, yeye alijua ni kwanini mwane anajiskia hivyo, hizo ni hatua za mwanzo, na wengine husumbuka sana, na kwa vile Maua hajajua ni nini kinachomfanya hivyo, lazima atakuwa na wasiwasi. Shangazi alivyowaza hivyo, alijiuliza moyoni mwake je ina haja ya kumfahamisha Maua nini kinachomsumbua kwa sasa ili ajihami, au bado aendelee na msimamo wake huo, wa kukaa kimiya hadi ndoa ipite..

Baadaye Shangazi akaamua kuingia kwenye miradi yake, lakini kila aliloshika huki au kile nafsi yake ikawa haitulii, mawazo yake yote yakawa kwa mwanae, …kiujumla alimpenda sana Maua hata watoto wake walifikia hatua ya kulalamika na kumuonea wivu Maua jinsi alivyokuwa akipendwa na mama yao huyo, na kudai kuwa mama yao anampendelea sana Maua kuliko wao.

‘Sio kwamba nampendelea Maua, ila hata kama nyinyi mngelikwua katika nafasi yake ningeliwatendea hivyo hivyo,….’alisema Shangazi mtu bila kuwafafanulia wanae zaidi. Hata hivyo watoto wa mama huyo hawakumchukia Maua licha ya kumuonea wivu, waliendeela kumpenda kama ndugu yao …na mara nyingi walijitahidi kuiga tabia yake, ili na wao wapendwe zaidi kama anavyopendwa yeye, …shangazi mtu alijua kuwa sio kwamba Maua ana kitu kikubwa cha zaidi kuliko watoto wake, ila alifanya hivyo, akijua dhima ya kulea mtoto wa mwenzake.Licha ya kuwa Maua ni moja wa watoto katika familia yao, lakini bado ana wazazi wake, kwahiyo lolote utakalomfanyia kinyume na hisia zake, anaweza kudai ananyanyaswa, na hili hakulipenda kabisa mzazi huyo, lakini hata hivyo, hakuacha kabisa kutimiza wajibu wake wa malezi bora.

Kutokana na tabia hii Maua alijengeka katika maadili mema, hakudeka, na kubweteka, na hata aliposafiri kwenda kwao,wazazi wake walimsifia kuwa kajengeka kimaadili, kinyume na walivyokuwa wakifikiria kuwa mtoto akikulia mjini anakuwa na tabia isiyoendana na madili yao, …
‘Namjua dada yangu hana mchezo na watoto, …’siku moja alisema baba yake Maua.

‘Ni kweli, lakini Maua usije ukajivika ngozi ya kondoo, kujifanya una tabia nzuri, kumbe kisiri siri una yako…’akamuasa mama yake.

‘Na wewe mama sasa umeanza, nitakuwa na yangu yepi, ….mimi mnavyoniona ndivyo nilivyo, sina mambo ya kujificha ficha…’akajitetea Maua.

‘Usija ukamuabisha shangazi yako, maana sisi tumeshamuamini, …kumbuka kujiheshimu kama walivyojiheshimu wazazi wako, tumeoana tukiwa hatujui mapenzi ya na tukawapata nyie ndani ya ndoa, sasa usije ukafanya kinyume chake…’akasema baba yake.

‘Na ikitokea hivyo, nitamchamba wifi kianamna yake, nitamwambia ikowapi, ..ooh, mwanangu haya ni mazungumzo tu, mengine yote yanategemea uvumilivu wako, ukumbuke duni ahii imejaa vishawsihi vya kila namna , dunia hii ina mitihani ya kila namna, lakini yote kuishinda ni kuwa na subira, ni kuwa mvumilivu…mungu atakuasaidia mwanangu..’akasema mama yake.

Shangazi mtu alipoona akili yake haitulii vyema, inakuwa na mashakamashaka kuhusu Maua, akaona ili kuondoa sintofahamu hiyo kwenye akili yake ni bora aende nyumbani kwa Maua akutane naye ana kwa ana. Huku akili yake ikimshauri kuwa ni vyema apasue jipu, maana akiliacha hivyo hivyo linaweza likasabaabisha maumivu makali, lakini je ndio wakati muafaka huo, apana, nia yake alitaka baada ya ndoa tu, ndioo ataweka mamb hadharani,…lakini hata hivyo atakuwa kakiuka maadili ya kiimani. Akawaza hilo kwa makini, mwishowe akasema ngoja afike huko na akutane na Maua na mengine yatajileta yenyewe.

Akiwa njiani alikumbuka kauli ya kaka yake kuwa ahakikishe mtoto wao haingii kwenye maswala ya kuiabisha familia yao,

‘Dada hakikisha huyu mwanetu anakulia katika msingi mema, kama akimpata mume hakikisha wanaona haraka iwezekanavyo, hatutaki mimbakabla ya ndoa…’hii ilikuwa kauli aliyopewa kabla Maua hajampoteza mume wake, na baada ya mume wake kutoweka, na kuaminika kuwa keshakufa, wazazi hawa walikutana na shangazi akapewa jukumu la kuhakikisha kuwa huyo binti haingii kweney mitego mibaya, ..

‘Kama atapata mume utuambie haraka, hakikisha wanaoana, hatutaki mipango ya kubebeshana mimba kabla ya ndoa, …’shangazi alikumbuka kauli ya kaka yake, ambaye alimuheshmu sana, na hakupenda kabisa kumuabisha.

‘Kaka mimi mnanijua vyema , malezi yangu sio ya kubahatisha…nitahakikisha anapata mume mwingine na kabla hajaharibikiwa…’alitoa kauli hii kwa kujiamini,…sasa leo mambo yameharibika , je kaka yake akijua itakuwaje, na wifi yake ambaye anatafuta mwanya wa kumta makosa….hapana hili hawatalijua mpaka ndoa ipite…akasema kimoyomoyo.

‘Lazima nikaongee na Maua mapema, asije akaumwa na kukimbilia hospitalini, najua kwa vyovyote akienda huko docta atamgundua na siri itafichuka na taaarifa hizi zinaweza zikavuja..’akawa anawaza huku akiwa na wasiwasi mkubwa.

Alikumbuka siku alipomgundu akuwa ana mabadiliko yasiyo ya kawaida , na hisia zake zilimfanya amuulize Maua.

‘Maua hivi upo sawa,kweli hebu niambie una miezi mingapi kabla hajaziona siku zako…’alikumbuka siku alipomuulizia Maua baada ya kumuhisi kuwa hayupo sawa.

‘Shangazi nawe, kwani nina mabadiliko, gani, mbona kuumwa huk nimeanza tangu mume wangu alipopotea, na kuziona siku zangu sio tataizo huwa naweza hata kufika miezi mitatau na hata nikipmwa naonekana sina ,…ujauzito….kwanini niwe mjauzito, kwa mimba ya nani,,,,shangazi naona unanichuria….’akasema Maua.

‘Kama nikujichuria unajichuria mwenyewe, kwa matendo yako, na mabadiliko ya mwili …wewe hujioni, lakini sisi wenye uzoefu tuemshaliona hili,….itabidi twende ukapime…’ akasema shangazi mtu.

‘Shangazi mbona unaniwazia vibaya hivyo, nina mimba itoke wapi, ….shangazi ,kama sina ujauzito utanipa nini, tupinge shangazi,,,,’akasema Maua kwa utani.

‘Kama unao nitakupa mume haraka iwezekanavyo… kama huna nitakununulia zawadi nzuri sana…’akasema shangazi mtu, huku moyoni akiwa na mashaka na mabadiliko ya mtoto wao huyu.

‘Zawadi gani, ujue hiyo ni ahadi,,,,?’akauliza Maua kwa hamasa.

‘Nitakununulioa mkufu wa dhahabu utakaouvaa siku ya haruisi yako…lakini kama una ujauzito sijui nitauweka wapi uso wangu…’akasema shangazi, kipindi hicho Maneno alikuwa hajakubaliwa kumuoa Maua.

‘Haya shangazi we uandae kabisa huo mkufu wa dhahabu, sina wasiwasi…na usiwe na wasi wasi na mimi, umeniela mwenyewe, siwezi kabisa kukuangusha kama ni mimba nitaipatia ndani ya ndoa….’akasema Maua huku akiwa akikumbukia siku moja walibishana na mume wake kuhusiana na hilo na hata kuahidiana, mumewe alimwambia kama ataambiwa safari hii ana ujauzito atamnunulia gari…
‘Utaninunulia gari, unasema kweli mume wangu…?’akauliza Maua.

‘Nasema ukweli,…’akasema mume wake, na siku hiyo walipokwenda kupima na kuambiwa kuwa hakuna ujazuzito, Maua akakata tamaa kabisa ya kupata mimba.

‘Maua mbona mapema sana kulifikiria hilo, ilimradi docta kasema hakuna mwenye tatizo kati yetu, basi ni swala la muda , siku mungu akpenda tutatapata mtoto, bado mapema sana kukata tamaa, hilo wala lisikutie mashaka…’akasema mume wake.

‘Sawa mume wangu unafikiri kinachoumiza ni nini, mimi kama mimi naweza kusema ipo siku, navuta subira, lakini tatizo ni wapambe, watu baki, hawakupi muda huo, kila mkiongea, hivi wewe utapata mtoto lini, …hivi wewe vipi…’akasema Maua

‘Hawo usiwajali, mungu kawapa midomo ya kuongea, na huwezi kuwazuia, cha muhimu ni sisi wenyewe kuwa na moyo wa dhati, kuwa ipo siku tutampata mtoto,….unajau Maua nakupenda sana, sipendi kabisa nione unanyong’onyea kwa jambo hilo, …usijali mpenzi…’akasema mume wake.

‘Nashukuru sana mume wangu kwani umenipa faraja kubwa, nakupenda sana mume wangu na nitajitahidi sana kutowajali wapambe, …wewe ni faraja la moyo wangu, namuomba mungu asitutenganishe,…maana sijui nitaishije…’akasema Maua.

‘Mungu mkubwa, tupo pamoja mpenzi wangu…’akasema Meme wake, na maneno haya akiyakumbuka Maua yanamtonesha sana moyo wake, haamini kuwa ndio hivyo tena, mume aliyemepnda hayupo tena duniani. Na siku alipoongea an shsngazi yake kwa maneno yanayofanana yay ale aliyoahidiana na mume wake, kwa utani ule ule aliowahi kufanya na mume wake, moyo wake ulikumbuka mbali sana…na kwa minajili hiyo, ya kukata miezi mitatu bila kuona siku zake hakuwa na wasi wasi wowote kuwa ni mja mzito.

‘Na dalili kama hizi nilishaziona wakati nipo na mume wangu, ….sioni haja ya kwenda kupima….’Alimwambia shsngazi yake siku alimpomshauri kufanya hivyo.

Leo akaamuka vibaya, akawa hajisikiii vyema na hata safari aliyoipanga na shangazi yake ya kwenda kuangalia gauni la harusi akaiona haina maana, …akaamua kuahirisha kila kitu na bila kumwambia mtu akaondoka kueleka huko hospitaini,…lakini nian sio kuchunguza kuwa ana ujauzito, hilo hakuliwekea maanani, nia yake ilikuwa kujiangalia mwili wake kwa uumla, kwanini anajisikia vibaya kiasi hicho, huenda kuna tatizo jingine….hakuamini pale alipoambiwa kuwa ana ujauzito, na hapo taswira ya shangzi yake akiwa na hasira ilitanda usoni mwake, akajua sasa ana kesi ya kujibu, sasa …..

*******

Shangazi alipofika kwa Maua alikuta mlango umefungwa, akauliza majirani, wao waksema wamemuona akitoka, lakini hakusema anaeleeka wapi,….Shangazi akahamaki, akatoka mbio, na kuchukua taksi, alishajua kuwa Maua lazima atakuwa kaamua kwenda hospitlini, na taksi ilipemeleka moja kwa moja hadi hospitali yao wanayotibiwa mara kwa mara, huko akaambiwa hayupo. Akapiga simu yam AUA ilikuwa inaita tu haipokelewi.

‘Sasa atakuwa kaenda wapi Jumapili hii,leo hana akzi, …na mara nyingi huwa hatoki nyumbani..’akawa anajiuliza na wakati anatafakari hili akaumbuka jambo, na bila kusema kitu akaingia kwenye taxi nyingine, ilipofika njiani ikakutana nafoleni kubwa sana, …akawa analaani,na shinikizo la damu likawa linamapnda kwa wasiwasi.

Alichofanya ni kutoka kwenye ile taksi na kuchukua pikipiki, na kabla hajachukua hiyo pikipiki akapiga tena simu na safari hii alimpata Maua, …hakusikilizana naye vyema kwasababu ilikuwa barabarani, mingurumo ya magari, na makelele, lakini hata hivyo alimpa maneno amabayo kama atayafikiria haatweza kufanya hilo jambo alilozania kuwa huenda Maua anataka kulifanya, ilibidi amwambie ukweli, akamwambia mweney pikipiki atafute njia za mikato, na wakaingia vichochoro na baadaye wakatokea barabara kuu, walipokuwa waaningia barabara kuu, wakakutana na gari la Maneno, likasimama.

‘Shangazi unakwenda wapi haraharaka hivi, na pikipiki, nakumbuka uliniambia kuwa wewe hupatani na pikipiki, leo imekuwaje, au ndio hiyo foleni imekuponza…?’akauliza Maneno.

‘Ukiona hivyo ujue kuna jambo, kuna sehemu nawahi kidogo, sasa nilipofika hapo nyuma, nikakuta foleni kubwa, basi nikachukua pikipiki…lakini..’akasema Shangazi mtu akitafuta mwanya wa kumkwepa Maneno, lakini haikuwezekana.

‘Basi njoo nikuwahishe huko unakokwenda, …’akasema Maneno na kumuulizia yule mwenye pikipiki anadai kiasi gani, na hata kabla Shanagzi hajasema lolote, akawa keshamlipa mtu wa pikipiki na shangazi akawa hana jinsi ila kukubaliana na Mkwe wake mtarajiwa, na akaingia kwenye gari la Maneno.

‘Shangazi nina jambo nilitaka kukuulizia, maana nimefika kwa Maua sijamuona, na kama tulivyoahidiana leo ilikuwa siku ya kwenda kuangalia gauni la harusi, au mlishabadili siku ya kwenda huko, niliona nimpitie nimchukue halafu nije kwako …kwasabaabu gari lipo kwanini mhangaike na usafiri mwingine, sasa nimefika kwake hayupo, na sizani kuwa leo ana kazi yoyote,..’akasema Maneno akiwa na wasiwasi.

‘ Kwa ujumla , leo ilikuwa tufanye hivyo, lakini baadaye alinipa taarifa kuwa anajisikia uchomvu, akaona tuahirishe hiyo safari, sasa nahisi atakuwa kaenda kwenye hospitalini mojawapo ambayo tunapenda kwenda kuangalia afya zetu, sina uhakika sana, hebu tupitie tumuangalie, kabla sijaingi akwenye mishemishe zangu…’akasema Shangazi akijaribu kutafuta njia ya kumhadaa mkwe wake, kwani hapo hakuwa na ujanja wa kusema vinginevyo, ila alipanga wakifika hapo kwenye hiyo hospitali atamwambia amsubiri nje, na yeye ataingia ndani kuonana na Maua, kama kuna lolote limefanyika, atajua nini la kufanya.

NB. Naona tuingie kwenye sehemu ya hitimisho, kwani naona hata uchangiaji unaanza kuzorota, nan a lengo langu tukimaliza hiki kisa kinakuwa tayari kwa kutengeneza kitabu, sijajua kwa vipi, maana sina vyenzo na hata wapi pa kuanzia, naomba ambaye anaweza kunisaidi kwa hili anipe tafu.


Ni mimi: emu-three