Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, May 7, 2010

barabara za uchaguzi

`Jamani hizi barabara za uchaguzi zitaumbua wengi’ akasema jamaa tukiwa ndani ya daladala ambalo lilikuwa likiyumba huku na huko kutafuta maeneo ya kupita, hutaamini kuwa vichochoro tulivyopita vilikuwa havipiti gari, lakini leo imekuwa ndio ahueni yetu, vinginevyo tungechelewa makazini, na sidhani kuwa mabosi wangetuelewa, na wataelewaje na wao wana vimotomoto!


‘Kweli hizi barabara za kampeni, zilitakiwa ziwe changamoto kwetu wapiga kura, hawa jamaa ikifika mwezi wa nane, na tisa watajifanya kuja kujaza kifusi huku wakinadi kuwa wakichaguliwa watamalizia kuweka lami, nasi kwa ujima wetu tunasema sawa bwana mkubwa, kura hiyo’ akasema mmoja wa abiria.

‘Hebu jamani tuamuke tutadanganywa mpaka lini, mimi simjui hata mbunge wetu kwa sura, namsikia tu kuwa kawa, sijui naibu mu-waziri, lakini jimboni kwake kunatia aibu. Tuamukeni jamani, huyu mtu akija kwenye kampeni tumuulize ni nini kakifanya katika miaka yake mitano’ akasema mama mmoja

‘Na nyie akina mama ndio wakwanza kudanganywa na vikanga’ akasema mzee mmoja

‘Na nyie je, mashati mnayopewa hamuayaoni, swala ni kupokea lakini akili kichwani mwako’ akasema Yule mama wa awali

‘Hata mseme nini, hawo msiowataka watakuwepo hadi waseme hatutaki, kwani nyie wenyewe hamtaki wasiwepo, niwaulize ni wangapi wanaopiga kura’ akasema jamaa mwingine.

Ni kweli zipo barabara za uchaguzi, hizi hufukiwa na vifusi siku za uchaguzi zikikaribia, na vifusi venyewe ni danganya toto, mvua ikinyesha hubadilika na kuwa matope yasiyokanyagika hebu tembelea barabara ya mji wa Kenya hadi Moshi Bar, na nyingine kama hizo utajionea mwenyewe, utafikiri sio Dar.

Tunaomba jamani mwaka huu hizi barabara ziendane na mji, na sio kwa maneno na ahadi, Umeme shida, barabara shida, maji ndio usiombe, ni mwendo wa visima ndoo...oh, subirini mkinipa ubunge nitawafanyie yote..hii ndiokauli yetu!

From miram3

No comments :