Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, April 22, 2010

Tunajikaanga kwa mafuta yetu wenyewe

 Mvua zinanyesha na ni neema, lakini barabara zetu hasa tuishio maeneo yaliyosahauliwa inakuwa kero. Magari yanakuwa shida na yakipatikana yanajipandishia nauli wapendavyo, `kama hutaki chukua bodaboda'. Hii imenipata leo asubuhi, na nilishangaa abiria wenzangu walivyoamua kukiuka sheria baada ya mwenye daladala kuamua kuongeza nauli.
 Baadhi ya abiria wakakataa kutoa nauli aliyojipangia kondakta, lakini baadhi ya waliowengi wakasema haina haja watalipa. Wachache tuliokataa kulipa ikabidi tushuke na hapo tilishafika mbali kidoo na kituo tulichoanzia. Nilijaribu kuwaelimisha wenzangu kuwa tukiwa na umoja hawa watu wanaokiuka sheria tutawashinda, kinachotakiwa ni kulipa nauli halali na vinginevyo twende polisi
'Bwana sisi tuna haraka, hiyo shilingi hamsini aliyoongeza itamsaidia nini, kama hutaki shuka' mwanamama mmoja akasema kwa hasira.
 Hivi ndivyo tunavyoamua kujikaanga kwa mafuta yetu wenyewe, tunaona tunachofanya ni kitu kidogo kwa muda ule lakini madhara yake ni mengi. Huyo mwenye daladala anachotaka ni faida na akijaribu mara mbili ataona ni kawida na matokeo yake ni kuumia kwa abiria walio wengi. Wewe ambaye unayeona hiyo hamsini ni ndogo ungejaribu kuchukua taxi ukawaachia walalahoi wakapanda kwa nauli iliyohalali.
 Hili ni moja ya tukio ambalo sisi wananchi tunachangia kuharibu utawala bora wa sheria, na matokeo yake tutakuja kuwalaumu viongozi. Tunachotakiwa ni sisi walengwa , ambao ni wananchi kuwa mstari wa mbele kuzilinda sheria, na tukiona mtu anazivunja tuwasilishe mahala panahusika. Kama tutaona tuna haraka, au ni pesa ndogo iliyoongezwa tujue uharaka na udogo huo ni madhara ambayo hatimaye ni kuchipuka kwa mafisadi uchwara.
From miram3

No comments :