Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, March 25, 2010

Tumekanyaga mdudu

`Wewe njoo kwangu Mabibo nitakupa mchongo wa maisha, usikose ni muhimu sana. Sasa ufanye hivi, wewe, ukifika makutano, nyosha moja kwa moja hadi kwenye transfoma, pinda kulia, hesabu nyumba tatu, mtaa unaofuta kuna nyumba nyekundu, ulizia bob Dulla,…

Mimi hapo najulikana sana kama mpiga dili, au wakala,…wengine wanaijua kama Ubwabwa...kwenye shughuli hapo' nilisikiliza maelekezo kwenye simu kutoka kwa huyo jamaa, mchekeshaji wa kutupwa . Na kwa vile nimewahi kuishi maeneo hayo ya Mabibo, nilishajua wapi anapaongelea, kwahiyo nikamhakikishia kuwa nitafika tu bila matatizo.

 Niliwahi sana siku ya pili yake asubuhi, manake nilikuwa nahitaji sana kupata shughuli za kuingiza kipato, na jamaa mwenyewe sio haba anajua sana kufuatilia mambo kama hayo,…na hapo aliniambia kuwa kesho anakwenda safari, mikoani kidogo.

Nilipofika kituo cha Sokoni, kama kinavyoitwa nikashuka, nikaanza kutenmbea shoto kulia na TZ 11 yangu, hadi eneo linaloitwa Makutano. Nilipofika pale nikaona nichepuke kimtaa cha mkato, sinilishawahi kuishi maeneo hayo, kwahiyo vimitaa vilikuwa bado kichwani.

Nilipofika mbele nikakuta kile kimtaa kimefungwa na ukuta umepita kuizunguka nyumba. Ohoo, jiji hili kila siku mabadiliko. Ikanibidi niingie mtaa mwingine, nikatembea wee, sifiki!. 

Nilishangaa mbona sitokei barabarani, nikaona ngoja nirudi nyuma nianze upya. Wee nilichoka, nilitembea nikajikuta natokea eneo tofauti kabisa, nikasema ngoja nipinde kushoto niongoze ile barabara, labda nitatokea barabara kuu, nilijikuta natokea eneo kama la Kigogo vile, basi nikasema ngoja nirudi nyuma, kama ni Kigogo nitakuwa nimeenda mbali. Nilicheza kushoto kulia, nenda rudi hadi masaa matatu yakanikatikia...

 Kilichonisaidia niliamua kuangalia simu kuwa ni saa ngapi. Niliogopa hata kumpigia mwenyeji wangu simu kwani angenishangaa. Nitachekwa, nitaonekana wakuja, siunajua tena, ukikutana na mtu kama Bob, Dulla, anaweza kukuanika juani, bila kujali umri wako.Kuangalia kumbe simu nayo ilishazima, haina chaji. Nikaiwasha ili angalau niangalie muda na mara simu ikaita.

'Wewe mtu, vipi mbona huonekani..' jamaa akaniita

'Hutaamini, naitafuta nyumba yako siioni, sijui nimepotea..' nikasema
'Wewe, umekanyaga mdudu…’akasema kwa mzaha

‘Nimekanyaga mdugu..?’ nikamuuliza kwa mshangao.

‘Ndio…sikiliza wewe fanya hivi, geuza shati lako hilo, kwangu sio mahala pa kupotea, na wewe siulishawahi kuishi maeneo ya huku bwana, acha ushamba...’akasema

‘Sawa nitafika tu…’nikasema

‘Sikiliza, …wewe umekanyaga mdudu, geuza shati hilo,…unajua ni saa ngapi saa hizi, kama uusipofanya hivyo  utakesha ukiitafuta nyumba, shauri lako...' akasema huku anacheka.

 Nikafikiri wee, nikaangalia kushoto, kulia, nikaona watu wanapita, nikachepuka kwenye uchochoro, nikavua shati haraka nikageuza, kwasababu ilikuwa fulana, isingeweza kugundulika. Nilipomaliza, nikatokeza barabarani...oooh, barabara ya kwenda Ruhanga, kumbe nilipitiliza. Nikarudi nyuma kwa kuelekea Mabibo makutano, na mara nyumba ile, inaonekana wazi kabisa.

Swali likanitinga kichwani, je ni kweli nilikanyaga mdudu, au ni imani tu?

Na je nilifanikiwa kwasababu nimegeuza shati…huu sasa ushirikina, …!’

Unajua sikuamini hadi nilipofika kwa rafiki yangu na ikawa stori, na kwasababu kulikwa na jamaa zake kila mmoja anasema ilishawahi kumtokea, na dawa ikawa hiyo kugeuza shati, nikajipa imani kidogo ya kuamini, ili nisije kuonekana mshamba wa mji...sijui labda wewe au yule ilishawahi kumkuta hiyo.

Jamani maisha sasa kila mmoja anasema ni magumu,..kila mtu anaongea lake, wengine ni mageuzo, wengine ni siasa, wengine …ooh, kila mtu na lake, na hakuna nayejaribu kukumbuka dhamira yetu ya awali,…kupambana na mafisadi na wala rushwa


 Na ni karibu tu, uchaguzi utakuja, na ni vyema tukaangalia njia zetu, kwani nahisi tumepotea. Tusipoangalia tutapuyanga wee, hadi miaka nenda, rudi, na mika mingine mitano itapita, bila kujua wapi tunapokwenda. Ni heri yangu nilipigiwa simu na mwenyeji wangu, lakini sie tutapigiwa simu na nani? Haya, labda kama tutapigiwa simu, dawa yake ni kugeuza shati? mbona shati lenyewe halina ndani na nje, limeshachujuka hiloo! Labda dawa ni kule kuligeuza kulikokuwa ndani kuwe nje, kwasababu hivi sasa hali ilivyo haina cha ndani wala nje kote ni sawa. Wenye macho watizame na wenye akili watafakari kwani nahisi tumekanyaga mdudu.

From miram3

1 comment :

Anonymous said...



Also visіt mу web-ѕite :: more info about tantric massage
Also visit my web-site :: erotic massage