‘Wewe umesema uliwahi kusikia mambo kuhusu mkataba wa familia
kupitia kwa rafiki yako, na ina maana kuwa wewe ulikuwa unafahamu vipengele
vyake, na ulifahamu kuwa ukifanya lolot baya, inakuwa ni tatizo kwa mume wa
familia, huoni hapo unatudanganya,..kuwa wewe ulijua hatari yake na bado
ukatumia mbinu ili umpate mume wa familia, ukijua kuwa utapata masilahi fulani baadae…?’ akauliza
wakili
'Masilahi gani...' akauliza mdada
'Mali, na hata kama ndoa hiyo ikivunjika wewe utaolewa na mume wa familia
'Kwanza umesema mali, kama ndoa itavunjika, huyo mume atapataia wapi mali, wakati hana kitu, atarudia kwenye umasikini wake, maana atanyang'anywa kila kitu si ndivyo mkataba unasema wao halali unasemaje...?' akauliza mdada.
'Kwahiyo kumbe wewe ulikuwa unafahamu kila kitu, kwanini sasa hukufanya juhudi za kuhakikisha hilo tendo halifanyiki...?' akaulizwa
'Tendo gani...?' akaulizwa
'Lililokufanya upate huo ujauzito..kama kweli hukudhamiria hilo litendeke kwa kuangalia masilahi fulani kwako...'akaambiwa.
Tuendelee na kisa chetu
*************.
'Kuhusu undani wa huo mkataba
nilishasema nilikuwa nasikia rafiki yangu akiongea baadhi ya vipengele vyake, na moja ya vitu
alivyoviongea kuhuus vipengele hivyo, ni kuhusu miiko ya ndoa, alinielezea kuwa mume wake asingeliweza
kusaliti ndoa yake, kwani anafahamu ugumu wa mkataba wao ulivyo…’akasema
‘Kwahiyo kwa vile ulilifahamu hilo ukataka umshawishi mume wa
familia ili umpate wewe, kwa yeye kuvunja hiyo miiko, ili ndoa yao, ivunjike, na wewe uchukue nafasi ya mke wa familia au sio…’akaulizwa
Mdada huyo kwanza akamuangalia huyo wakili kwa makini, halafu akatabasamu na kusema
‘Kama ni kufanya hivyo ningelifanya hivyo zamani sana, lakini hiyo sio
tabia yangu, ulizia, utaambiwa, usitake maneno ndio yawe ushahidi, wakati matendo yalikuwepo, mume wa familia alikuwa akijifanya mpole kwa watu lakini mkibakia naye wawili huwezi amini kuwa ndio yeye, …’akasema
Mume wa familia akatikisa kichwa kama kulipinga hilo.
‘Kiukweli hata walivyoniambia kuwa mkataba wao unawapa mamlaka ya
kufanya kila kitu sikuamini, maana mkataba ulikuwa umesajiliwa iweje leo
mkataba uwe tofauti,…nikajua kuna jambo limefanyika, nyie mawakili tunaowaamini mnageuza batili kuwa haki, au sio...baadhi yenu nyie, mnathamini sana pesa, na kuacha taaluma zenu pembeni…’akasema na hapo wakili akanywea, na kuangalia pembeni
‘Niambie muheshimiwa wakili, kwanini mligushi huo mkataba, maana hilo
sasa lipo wazi,..wewe ndiye wakili wa kutetea mkataba wa kugushiwa, kwanini ulikubali kuusimamia mkataba uliogishiwa,...?’ akauliza mdada
‘Wewe hutakiwi kuniuliza maswali mimi, wewe kama shahidi, unatakiwa ujibu maswali yangu, na sio wewe kuniuliza maswali…’akasema wakili
‘Haya uliza hayo maswali yako, lakin ukae ukitambua kuwa wewe
unatetea mktaba batili,.. na ukizungumzia mkataba ujue unazungumzia
mkataba upi, mliogushi nyie , au huo wa kitapeli, au..wa halali, ubainishe
maswali yako, maana wewe ndiyewakili wao, na unawatetea matepeli…’akasema mdada na mume wa
familia akataka kuongea lakini wakili wake akamzuia
‘Endelea na maelezo yako…’akasema mwenyekiti.
‘Kwahiyo kiukweli ndugu
mwenyekiti, mimi nilikuja kuutambua ukweli kuwa mkatba umegushiwa, baada ya kurudi masomoni. Na nikagundua
ubabaishaji wao wote…na ushahidi ninao, mkitaka kila kitu naweza kukiweka
hadharani..’akasema
‘Endelea na maelezo, ushahidi baadae…’akasema mwenyekiti
‘ Huyu mume wa familia kwa kujiamini aliniambia kuwa akitoka huku
kwenye kikao atakuwa kamaliza kazi, kila kitu kitakuwa kwenye miliki yake,
kwahiyo kinachofuatia ni kuhakikisha kila kitu sasa kinakuwa wazi, mambo ya
urithi, na umiliki za mali, nay eye kuchukua hatamu kama mume wa familia…’akasema.
‘Kiukweli kimoyo moyo nilicheka sana, maana ukweli
nimeshauafahamu, nikajua huyu mtu keshaharibiwa
akili, nilitumia lugha ya kumuonya kuwa hilo haliwezekani, yeye aliniona mimi
ndiye mjinga nisiyeelewa, na akaniambia, kama ikishindikina yeye ana plan B,
sasa muulizeni plan B, ni ipi hiyo, ndugu wakili mtetezi…’akasema mdada,
akimuangalia wakili.
Wakali akawa kimia,
akimuangalia tu
' Mimi nilimwambia cha muhimu kitakachomsaidia, ni yeye kupigania
ndoa yake tu, vinginevyo, atakosa kila kitu, ndoa, na mali, nilimuambia kuwa
kilichomuharibia ni tabia yake hiyo mbaya, tamaa, na umalaya, ..na nilipotamka
neno hilo akanijia juu, kuwa nimemtukana, nahisi ndio maana alipokuja hapa,
akawa na jaziba hizo hizo za kauli hiyo, lakini matendo…yanajionyesha….’akasema
'Je sio haki kwa baba kudai haki za mtoto, je sio haki kwa mume
mliyezaa naye kudai haki za mtoto wake,…?’ akauliza wakili
‘Anaweza kufanya hivyo, lakini sio kwa kugushi, sio kwa utapeli,
na mimi nilishamuambia ukweli, kuwa huyu mtoto ni wangu, haina haja ya yeye
kuhangaiia, nitaweza kumuhudumia mwenyewe, ….’akasema.
‘Lakini ni lazima mtoto awe na baba yake, na mtoto kama mtoto ana
haki ya kuja kumfahamu baba yake, kwanini utake kuuficha huo ukweli, huoni hapo
unatuficha mambo kwa kujikosha, ili uonekane wewe ni bora…?’ akaulizwa
‘Ni kweli kuwa mtoto ni lazima awe na baba yake, lakini kwa
mazingira niliyompatia huyu mtoto sikutaka kuwe na mtu anayeitwa baba, ukumbuke
kuwa hii mimba nimeipata kutoka kwa mume wa mtu, na katika maisha yangu niliipa
kuwa sitatembea na mume wa mtu..
'Kuna uwongo ulipangwa kuwa mimi nilikuwa na mahusiano na huyu
mwanaume kabla sio kweli...yaliyoyokuwa yakiendelea kati yangu na huyu mwanaume
yalikuwa maswala mengine kabisa ya kazi nyingine...sio lazima kuyataja,
hayahusiani na hii familia, mimi nina mambo yangu mengi ya kimaisha...lakini
pia nilitumia muda huo kumlinda huyu mwanaume, hamjui tu alivyo...kuna mengi
nimemuokoa nayo..
'Na pia hili lazima niliseme tu,...hadi mimi kufikia kutembea na
mume wa mtu, sio kazi rahis kama inavyoonekana kwa wengi, mimi sipo hivyo
jamani.., ilitokea baada ya hawa watu kunifanyia huo ubaya,...na baada ya tendo
hilo, sikuwa nimejihakikishia kuwa kweli nina mimba, au mimba ni ya nani hasa,..mtasema
kwanini sikuchukua hatua...nisingeliweza maana hata mimi nitaonekana tu
nilipenda iwe hivyo,..
'Baada ya kugundua kuwa nina mimba,nikawa nimechanganyikiwa,nilianza
kujiuliza ni ya nani, ni ya …unajua usiku ule sikuwa na ufahamu kabisa,..hata
hivyo, niliomba mungu na kuvuta subira…
‘Unaona unaanza kujionyesha mwenyewe, unasema, hukujua ni nani
aliyekupachka hiyo mimba, kwasababu gani, ulikuwa na wanaume wengi au sio…?’
akaulizwa
‘Hapana sio kuwa na maana hiyo, mimi sikuwahi kukutana na mwanaume
mwingine kabla, na mimi sina tabia hiyo ya kihuni, ukiniona na wanaume ujue
naongea tu nao tu, au nipo kazini..
‘Tutaaminije hilo, una ushahidi gani wa kulithibitisha hilo..?’
akaulizwa
‘Ushahidi upo…mimi huyu mtoto sikumpata tu kama unavyofikiria
wewe,…’akasema
‘Utoe sasa huo ushahid wako, ulimpataje huyo mtoto, kama sio
umalaya wako…’aliyesema sasa ni mume wa familia
‘Endelea na maelezo…’akasema mwenyekiti
**********
' Ndugu mwenyekiti, kuna jingine ambalo nataka kulisema hii leo, japokuwa
wengi watanishangaa,...inabidi na lenyewe nilisema tu, kuwa ushauri wakati
mwingine unaweza kukutumbukiza kubaya, sio kweli kuwa mimi nachukua ushauri tu
bila kufikiria, hapana, lakini ushauri mwingine unategemea kama una
manufaa,...'akasema
Alipoanza kusema hivyo nikajua sasa anataka kunilaumu mimi, lakin
sikujali hilo, nikasubiria tu aongee apendavyo...
'Mimi nilikuja kupata ushauri kwa watu, ni kipindi ambacho, hata
mimi nilikuwa kwenye wakati mgumu, unatamani na wewe uwe na mume, uwe na
watoto, lakini hajapatikana, ufanyeje…unatamani upate mtu wa kukushauri ufanye
nini ili ufanikiwe hilo…kiukweli umri umri wangu ulishakwenda…’akatulia
‘Naombeni mnielewe hapo, simlaumu mtu kwa hilo,..ila naongea
ukweli, wa nafsi yangu, nilivyovutika hadi kuhamasika, na hata ilipotokea ,
sikupenda kujilaumu sana, na siwezi kusema nilivutika kufanya hivyo, kwa vile
mimi sikufanya kiutashi wangu pia,…sasa ukiwa kwenye hiyo hali, na ghafla unakutana
na ushauri, tena sio wa hivi hivi, wakitaalamu, kutoka kwa mtaalamu mwenyewe,
utafanyaje, ..na zaidi unakuja kuupata ushaudri huo huo, kwa watu wako wa
karibu unaowathamini, kuwa ukichelewa
hutaweza kuzaa tena, au ukizaa unaweza kuwa matatani..hivi kweli tuangalai kote
kote, hali niliyokuwa nayo, ilinishinikiza kujiingiza kwenye …’hapo akatulia
‘Mimi ni binadamu, na siwezi kukwepa ukweli kuwa mimi ni mwanamke
pia, sisi tulivyo tuna hulka zetu aaah, ndio, naweza kusema hivyo,… ‘akashika
kichwa kama anawaza jambo
‘Ni hivi.., nataka muone jinsi hali hiyo ilivyojijenga akilini
mwangu hadi kufikia huko, hata kujichanganya na wale ambao nilikuwa nakutana
nao, lakini sikuweza kuwapatia ukaribu ule,…ni kweli, nilijikurubish kihivyo,
hata hivyo dhamira yangu ilikuwa bado haijakubaliana na kutenda tendo hilo…sikupenda
hivyo, sikutaka hivyo, nahasa kwa ..mmh nataka niliongee hili ili munielewe...'akasema
huku anakatisha kumalizia..
‘Ndio sikudhamairia hilo…huyo mume wa familia, moyoni analifahamu
hilo, hata mbele ya mungu atakuwa ni shahidi..hapa duniani anajidanganya tu..huyo
ni kigoo jamani msimuone anatembea kichwa chini…’akasema
Wakili akacheka, na mume mtu akatikisa kichwa kusikitika…n watu
wakacheka kidogo.
Kabla ya kuja kulielezea hilo, kuna jambo jingine nataka liwe wazi
kwenu, kama mna vichwa vya kuomba mbali, mnaweza kuafikiana name, maana naona
muda umekwenda, kuna mambo ambayo hatuyaoni kwa jinsi yalivyo,..kwa ukaribu wa
akili zetu, lakini yapo, kwa wenye kuona mbali, sikuwa makini na hili, ila
baadae nimakuja kuliona hilo..
‘Yawezekana ikawa ni bahati mbaya, au wanzetu wanasema ‘coincidence’
haya kutokea, au kuna mipango ya
kitaalamu ilitengenezwa, hapa sisemi kuhusu kupata mtoto, nasema yawezekana kashfa zilipangwa iwe hivyo, siwezi kuwalazimsiha
kuliamini hivyo, maana ushahidi wake ni mgumu kupatikana, ila kwangu mimi
nimeamini kuwa kuna namna hiyo ilipangwa, chochote chawezekana kwenye uwanja wa
kisiada..’akatulia
‘Unajitetea, au unatoa ushahidi..?’ akauliza wakili
‘Nimeshakuambia, mwenyekiti akiruhusu ‘ushahidi’ hilo litafanyika,
usitake kunipotezea muda, hapa…’akasema mdada
‘Endelea na maelezo yako..’akasema mwenyekiti
' Nasema hili hata baba, mwenyekiti wetu hapa ni shahidi, hili
tukio zima limekuja kutumiwa kisiasa baadae, je lilijulikana kuwa litatokea, au
ni hiyo ‘bahati’ kuwa limetokea sasa tutumie hiyo, kashfa kisiasa, hapo ndio
pale tunamuhitajia, mume wa familia afunguke, auseme ukweli, atatusaidia sana
kwa hilo…’akasema
Mume wa familia kusikia hivyo, kwanza alionyesha ishara ya ‘huyu
anasema nini’ halafu akacheka
‘Kama nilivyosema wengine hatutaweza kuliona hili kwa uoni wetu wa
kawaida,..haya kama yalipangwa au la, ila baadae haya sasa yamegeuzwa kisiasa
kama kashfa, kwa jaili ya kuibomoa familia ya mzee, na sisis wahanga tunakuwa
kwenye wakati mgumu hasa mimi ambaye nilikuwa mmoja wa watekelezaji na walinzi
wa hizi familia, inaniuma sana,..’akasema
‘Hayo unayoyaelezea kuwa ni mbinu za kisiasa, ni kujitetea au umeyatoa
wapi…?’ akaulizwa
‘Haya nimekuja kuyagundua, baada ya mimi kuingizwa huko, ili nitoe
ushahidi kuwa haya yapo, nitaje kuwa nimezaa na nani, na kuahidiwa pesa nyingi,
ikiwemo vitega uchumi, na hata kupewa hisa kwenye makampuni mbali mbali, …’akasema
‘Na akina nani…?’ akaulizwa
‘Na akina nani siwezi kuwataja,…lakini mimi sio kama walivyonifikiria
wao, kuwa nipo hivyo..hawakupata kitu kutoka kwangu, na hawatapata kitu kutoka
kwangu,..nimekana na kukataa mipango yao yote, hilo mniamini, na vitisho vyao
kwangui haviwezi kufua dafu,..nimezoea vitisho…’akasema
'Sasa muone ajabu kwa huyo mnayemuita mume wa familia,…hata yeye
aliitwa huko, je anaweza kulikiri hili, kuwa hata yeye aliitwa huko, na je
aliweza kuitetea familia,je hakuweza kuukubali ukweli, maana haya yote
yamejulikanaje huko, ..kiukweli mimi nililificha sana hili,lakini hutaamini huko
wanafahamu mengi ya haya,..’akasema
‘Ni nani aliyetoa siri za upande huu na kuzipeleka huko,..yeye
asema ukweli, kama hakutumiwa, na huenda alipoahidiwa manono akakubali
kushirikiana nayo,…’akasema.
‘Uwongo, acha fitina, toa ushahidi wa jinsi ulivyobeba hiyo mimba,
kumbe ulikuwa na mabwana wengi, eeh…ndio maana ulikuwa unaficha ukweli, sasa
nimeshagundua.’akasema mume wa familia.
‘Kiukweli huyu mume wa familia alishatekwa huko…na asiposema
ukweli, tunaweza kumuona ni msaliti wa hii familia, ndio maana nikasema hapa
hapa tutaweza kulibaini hilo, ni nani msaliti wa hii familia,..na huenda hajijui
hivyo, na huenda hajataka ila wanamtumia bila ya yeye kufahamu, atuambie basi,
akiri ukweli, kama mimi hapa…’akasema
‘Mwongo wewe, kwanini unajenga fitina zisizo za ukweli, unataka
nini , ili ndoa yangu ivunjike, ili wewe upate nini…’akasema mume wa familia
‘Kama hujakubaliana nao, na unafahamu fika ni maadui wa mkwe wako,
uliwahi kuwaelezea lolote wakwe zako, au mkeo kuwa kuna maadui wa mzee wanataka kukutumia wewe kwa masilahi yao..sema
ukweli wako..je uliwahi hata mara moja kuwaonya wanafamilia wenzako, maana hili
sio jambo dogoa..?’ akamuuliza mume wangu.
‘Nisingeliweza kukimbilia kuwaelezea hayo, mimi mwenyewe nilijua
namna ya kupamabana nao, mimi ni mume wa familia nilijua ni namna gani ya
kuilinda familia yangu, maana kama ningelichukulia pupa, je wangekuja kuifanyia
ubaya familia yangu, ingelikuwaje,…wewe kwa vile ..huna familia, ok, ndo sasa
umepaata mtoto jiulize mtu akitishia familia yako utafanya nini,…’akasema
‘Kwahiyo kumbe ulitishiwa ndio maana ukajiunga na hao watu, kisiri
au sio..?’ akauliza mdada
‘Mimi sijasema nimejiunga na hao watu, kwanza hao watu akina nani,
sikuelewei kabisa, mimi sio mwanasiasa,..na kuna watu ndio waliniuliza hayo
kuwa eti nimzaa na wewe, na vitu kama hivyo, lakini sikuwa na majibu ya
kuwaambia, na nilichofanya ni kwa masilahi ya familia yangu, siwezi kuyaonga
hapa maana nafahamu athari zak kwenye familia yangu…’akasema mume wa familia,
na wakili akawa anamzuia asiendelee kuongea.
‘Mimi nina ushahid mkubwa zaidi ya unavyofikiria wewe, natumai
unanifahamu ninafanya kazi gani, kwahiyo siongei haya kwa nia ya kukufitinisha wewe
na wakwe zako, hapa na ongea ukweli ulivyo, ukitaka ushahidi upo….’akasema
halafu akawageukia wajumbe na kusema
‘Huyu mtu, nilishamuambia akitaka kupambana na mimi ajipange vyema,
yeye kwangu kwa mambo hayo sio saizi yangu kabisa, hapa nina kila kitu, ushahidi
na sheria bado inanilinda, maana mimi sivunji sheria, mimi sigushi, natafuta
hakika na kweli, kama vielelezo viambata, huyu mtu atakuwa alitekwa na kuanza
kutoa siri za familia hii, apinga kama nasema uwongo…’akasema
Mume wa familia akasimama na kusema;
'Wewe ni mwongo, mfitini mkubwa wewe..na kuambia, shauri lako,
unafikiri kwa kusema hivyo, ndio watakuona ni mnzuri kwao, kuwa uniharibie mimi
ili wewe wakuone ni mnzuri,.., kama umeharibu umeshaharibu tu..na ole wako, hao
watu wakija kusikia unavyoongea hapa, unafikiri marehemu kafariki vipi, hao
watu hawana simile wakiona kuwa wewe umewasaliti, hawasiti kukumaliza, au mtoto..'akasema
'Hahaha, unaogopa eeh, mimi ndio uwanja wangu huo, kifo kwangu
kimeshaandikwa, mimi nipo vitani, ndio maisha yangu yalivyo, vitisho, ndio
sehemu ya maisha yangu..lakini pamoja na hayo, niliapa kuwa sitakwenda kinyume
na mkuu wangu wa kazi, hiyo ni ahadi hata kama hataniamini, yeye ndiye
alinijenga hivyo, na yeye ndiye alinionyesha njia, haya yaliyotokea ni bahati
mbaya tu...'akasema
‘Hahaha ‘bahati mbaya tu’…, wadanganye hao hao, lakini sio mimi, namimi nina ushahid
kuwa wewe una wapenzi wengi na mimi hatukuanza mapenzi..nini, acha niseme…’hapo
akatulia, wakili akimzuia kuendelea kuongea
‘Ongea mbona unasita, sema, mimi na wewe tulianza lini, nilipokuwa
naishi kwenu au sio……hahaha, ulikuwa unanitongoza, nikawa sikutaki, sema ukweli
ili wakusikie huo ni ushahidi mwingine wa kauli yako hiyo, hiyo kauli yako
japokuwa wakili wako kakuwahi ni ushahidi mwingine…’akasema
‘Wewe ni mnafiki tu wewe… mbona hutoi maelezo ya ushahidi kuwa
huyo mtoto hukumpata kwasababu ya umalaya wako, eeh, jitetee sasa, unanitumia
mimi kama ngazi ya kuficha maovu yako au sio…’akasema mume wa familia
'Tutakuja kuliona hilo kuwa mimi na wewe ni nani Malaya au mnafiki,
eeh,…’akasema rafiki yangu.
‘Endelea na maelezo yako, tusipoteze muda, mnajichelewesha
wenyewe..’akasema mwenyekiti naona hata sauti yake, iliashiria hayupo sawa,
nahisi kuna kitu kimegusa nafsini mwake.
********
‘Ndugu mwenyekiti, kwanini huyu mtu hataka kusema ukweli wa hiyo mimba
ilitungwaje , sio kwa tabia zake
zisizisahihi, na akaja kumrubuni mteja wangu..?’ akauliza wakili, na mwenyekiti
akamgeukia mzungumzaji..,
‘Nimeshasema kuwa huyu mtoto hadi kuzaliwa kulikuwa na michakato yake,
kabla hata sijafikiria hivyo, kuwa natakiwa kuwa na mtoto, kuna watu walinishauri,
kuwa nipate mtoto kwa kila hali..,hata ikibidi nitembee na mume wa mtu,..mimi
sikuwa na tabia hiyo kabla, wengi wananifahamu hivyo.., lakini kauli hiyo
ilikuwa moja ya sababu iliyonijenga kisaikolojia kuwa kumbe yawezekana
eeh..’akasema
'Ni kweli, kiubinadamu labda nisingelitakiwa nifanye hivyo, maana
huyo nitakaye tembea naye kama ni mume wa mtu, ana mkewe, je huyo mkewe atajisikiaje,
je kama ningelikuwa mimi nimefanyiwa hivyo ningekubali,,..’akatulia kidogo
‘Kiukweli mimi sikupenda hilo litokee hivyo, nilitamani nipate
mtoto kwa mtu asiyekuwa mume wa mtu, na ingelikuwa bora zaidi awe ni mume
wangu, lakini kwa bahati mbaya sikujaliwa kumpata mume wa kunioa…
‘Sio kwamba sikuwahi kutakwa, au mtu kunitaka kunioa, wapo sana na mmoja
wapo ni huyo mume wa familia,lakini kuolewa na mtu asiyekuwa moyoni mwako ni
jambo ambalo sikupenda kulikaribisha kwangu, huyu mume wa mtu, ni mume wa mtu
nilijua fika hizo ni hadaa zake za kutaka kunitaka, nikamkataa, wapo wengi,
siwezi kuwataja, niliwakataa kwasaabu hizo hizo.....'akasema
'Pamoja na ushauri huo kuwa nijitahidi kupata mtoto hata kwa mume
wa mtu, lakini mimi sikuwa na dhamira ya kweli ya kutembea na mume wa mtu
hususani mume wa rafiki yangu hilo halikuwepo kabisa akilini mwangu..huyu
kwangu ni shemeji..’akasema
‘Shemeji eeh…’aliyesema hivyo ni mama, na watu wakacheka
‘Ni kweli mama,..nitawaelezea yote ili muweze kunielewa,..hili
jambo lilitokea kwa mbinu za huyo mwanaume kama ni mkweli atalikubali hilo, sio
mimi nilifanya juhudi hizo, ni yeye, sijui kama alishirikishwa kulifanikisha hilo, au ni mbinu zake za kufanikisha malengo yake, …ila hilo sio
muhimu, ila yeye ndiye anabeba lawama hizo, ...'akasema
'Na sio kweli kuwa mimi nilimtaka yeye, kuwa eti mimi nilimuendea
na kumwambia hivyo, kuwa nataka mtoto, na nimeshauriwa hivyo, hapana hiyo sio
kweli kabisa, asema kutoka moyoni kuwa nilifika kabla na kumuambia hivyo, hayo
ni maneno ya uzushi, tukio zima liligubikwa na mbinu zao, walizozipanga, yeye
na ndugu zake, na huenda kama nilivyosema awali, alilifanikisha hilo kukidhi
matakwa ya upande wa pili, kw kujua au kwa kutokuelewa, akatumiwa na ikaja
kutokea hivyo…’akasema
'Kiukweli mimba yangu ilitokea katika mazingira ambayo sikutegemea
kabisa,na mabaya zaidi ikaja kutokea kwa mume wa mtu, na mbaya zaidi kwa sehemu
ambayo, najuta kiukweli,…imekuwa ni mtihani kwangu…baada ya kuipata hiyo mimba
kiukweli nilikuwa na wakati mgumu sana…hata kujipa matumaini ilikuwa tu, ili
nisije kupatwa na ugonjwa wa shinikizo la damu.
‘Kipindi hicho nilijaribu kujificha sana, na hata ilipokaribia
siku nikatoweka kinamna lakini kwenye kujifungua ikabidi nije kujifungulia hapa
Dar…na ndio ikaliweka hilo wazi kwa jamii… nahisi ni mwenyezimungu alitaka hili
tukio libainike, kw avile halikufuata utaratibu ulio sahihi….’akatulia na
kuhema
‘Hata hivyo mimi nilijipa matumaini kuwa, kwa vile haya yalitokea
ni pamoja na ushauri wa watu, tena sio watu wa hivi hivi, ni watu ninaowaamini,
washauri wangu, na wao walisema kwa kauli thabiti kuwa haijalishi, ..muhimu nipate
mtoto, basi nimeshampata mtoto, wao kama ni wa kweli kwa ushauri wao
wataendelea kunilinda na kunitetea kwa hilo.
'Sio rahisi, kama nilivyofikiria, ilifikia hatua nikajuta,…basi ndio
imetokea hivyo sasa nitafanyaje, labda hli ndilo litathibitisha urafiki wetu kwa
hao watu kuwa kweli walikuwa wakinijali mimi, au wakijali, yale ninayowafanyia,
na walifanya hivyo kuniweka kwenye hali ya kuwaona kuwa wao ni marafiki zangu,
naliongelea hili sio kwa kujitetea, maana hata hivyo mimi sikupenda litokee
hivyo, huo ndio ukweli wa hilo, sikupenda kabia, mungu wangu ndiye shahidi
nafahamu hapa hakuna atakayenielewa kwa hilo..'akasema
Baada ya tukio hilo niliwapoteza marafiki zangu, nikawa sasa
naonekana mimi ni mbaya,..kwanini, kwanini, kwanza kwanini simtaji baba wa huyo mtoto,..kwanini
namficha huyo mtoto, kwanini…basi ikawa ni taabu kwangu,.. urafiki sasa ukaja
kugeuka kuwa ni uadui,…maana lisemwalo lipo halijajificha,..
‘Lakini jamani si nyie mlinishauri, kuwa nikishapata mtoto hiyo
iwe siri yangu…na ikibidi, hata huyo baba yake asifahamu, hayo yote
yakashindikana,..ni nani alifanya yasshindikane, ni mimi au ni nani, na hadi
hapo alaumiwe nani, ..’akatulia
‘Najiuliza ni kwanini sasa nigeukwe, nahata kukamatishwa watoto w
a kihuni, ili waje kunizalilisha, hili kiukweli limeniuma sana, lakini hata
hivyo hao watoto wakihuni hawakufanikiwa,je ni kwanini hawakufanikiwa,
jiulizeni kwa akili za kutafakari na kujifunza, ina maana kweli na mbinu zao,
kwanini wakashindwa, maana walishaniziba pumzii na madawa ya kupoteza faamu
iliyokuwa imebakia ni kutenda matendo yao maovu, lakini ..mungu akaniokoa,
nasema mungu akaniokoa, si vinginevyo,…jiulizeni ni kwanini…kuna jambo la
kujifunza hapo…’akasema.
‘Ila sasa najiuliza, kwanini, mumesahau urafiki wetu, mumesahau
kuwa nyie ndio mlikuwa washauri wangu wa kubwa, je mliponishauri,
hamkulifikiria hilo…sawa limekuwa ni kosa, lakini je hamtaki hata kunipa muda
wa kutubu, …’akatulia akiwa anatikisa kichwa kama kusikitika
‘Ni sawa nastahiki adhabu, je mlimfikiriaje yule aliyefanya hili
litokee, yeye mlianga adhabu gani kubwa kwake, ambayo nistahiki yake,… je
mwafahamu ukweli halisi wa tukio zima hadi mimi kushika mimba hiyo, ilitokeaje,
kiukweli, …hili lilitakiwa watu watulie kwanza, wajiulize kwanza, kabla ya
kuhukumu,..kuna mambo mengi hapo, hata hilo la kisiasa laweza kuwa ni sababu,
litizameni kwa macho mapana..’akatulia
'Kwa bahati mbaya, mungu wngu alitaka nisipate hiyo adhabu kabla
ukweli haujabanika, maana kama kweli wangelifanikiwa hao watu, sizani kama
ningelikuwa na ubavu wa kuja kusimama hapa hii leo..ila nina amini, hata wao
wasingeliweza kuishi…haaah,..hawanijui tu, ingeliwa jino kwa jino, kabla
sijafanya walichowahi kufanya wengine…’akasema
‘Siwezi kujiaminisha hivyo, maana kihabari ninayoifahamu kuhusu
hao watu wao wakafanikiwa kwako, huwezi kuishi, utatamani ujiue tu, ila mimi
nisingejiua kabla hawajauwawa wao kwanza, …akatulia
‘Ila mimi hapo najiuliza kama lengo hilo ni kunifundisha mimi adabu,
je ingelitokea kuwa mimi nimepata hii mimba na mume mwingine adhabu hiyo
ingelikuwepo pia, au ni mkuki kwa nguruwe tu…najiuliza tu hapo..’akasema
‘Ninachoshukuru ni kuwa wahuni hao hawakufanikiwa, walishindwa
kufanya hivyo, baada ya mbinu zao kugundulikana na polisi, vijana hawo sasa
wapo jela, na nitahakikisha wanaozea huko jela, na humo wanakipata cha moto,
humo nina watu wangu wanaifanya hiyo kazi, waonje uchungu wa kile walichokuwa
wakiwafanyia wengine,..na nina uhakika, wakitoka jela, sizani kama watatamani
kuishi hapa Dar tena, sasa mkuki umewageukia wao...'akasema
'Nyie mliowatuma mkawatoe kabla haja-ozea huko jela, maana kumbe
walikuwa wakitafutwa kwa ushahidi, sasa ushahidi umepatikana, nyie sasa...mnahitajika kuwadhamini, kiutu,..lakini
kwangu mimi, wataiona hii dunia ni chungu..wamechezea kusipochezewa..’akatulia
‘Sio vyema jamani, ni kweli inauma…ni kweli kilichofanyika ilikuwa
sio sahihi.., lakini hata mimi sikupenda hili litokee hivi jamani…hata hivyo,
hivi sasa mimi nimekuwa, nakushukuru sana rafiki yangu uliyejitolea kwa ajili
yangu hadi hatua hii, ni wewe uliyenijenga hivi, na sasa nipo zaidi ya vile
ulivyonijenga, ninaweza kuishi mwenyewe, bila huo utapeli wao…’akasema
‘Kiukweli mimi sihitajii kujiingiza kwenye utapeli huo ulitakiwa
kwangu mimi, lakhasha, nipo kivyangu na namuomba mungu niweze kuishi hivyo,
kwenye maisha yangu ya haki, na sio dhuluma,
nafahamu fika rafiki , nimekukosea sana, ila wewe ndani ya moyo wako,
unanifahamu nilivyo, haya yaliyotokea ni mtihani tu, ni mbinu, na mungu
mwenyewe ndiye anajua...’akasema.
‘Ni nani huyo aliyekushauri, maana naona unajitetea hivyo..kusingizia
uovu wako..kwa watu wengine?’ akaulizwa
‘Hahaha, mimi sisemi kwa kujitetea, nasema ukweli wa nafsi yangu,
kuwa wapo walionishauri hivyo,, kuwa nikazae kwa vile umri wangu umeshapita, hata
kama huyo nitakayetembea naye…ni..ni… ,sina haja ya kumtaja huyo mtu, ni utomvu
wa adabu, na mim sikulelewa hivyo,..’akasema
‘Kwanini humtaji, mbona mume wa familia, hujajali, umekuwa mwepesi
kumnyoshea kidole kwa kila kitu, mabaya yote umeyaelekeza kwake,.. yeye
hakuwahi kukutendea wema, wewe uliwahi kuishi kwenye nyumba yao, yeye ni mume
wa familia, alikulea, leo hii umesahau fadhila zake…’akaambiwa
‘Tatizo ni kuwa mume wa familia hakubali kosa, kama yeye
angelikubali kosa,haya mengine yasingelijulikana, mbona mimi nimekuali makosa
yangu nimeelezeakilakitu,..’akasema
‘Lakini pia yeye kama shemeji, mlezi wangu alitakiwa kunilea
katika maadili mema, lakini yeye alitumia mwanya huo kunirubuni, kunishawishi,
kutumia kila mbinu za kuniingiza kwenye ushawsihi huo mbaya, je huyu anastahiki
kuheshimiwa,..niambieni, ukweli, ….’akasema
‘Sasa hata baada ya hayo, kwanini hakubali kusema ukweli,.. je
yeye hajakosea, kwanini hakubali sasa..kwa vile yeye ni mume wa familia,
kijogoo, au sio,.., sasa hivi mimi nina ushahid hapa wa mazungumzo yake mimi na
yeye , kwenye maongei hayo kajieleza alivyo, nilimchota akaongea kila kitu
..naona..eeh, sasa ni wakati wake muafaka auseme ukweli, akiri makosa yake la
sivyo, ushahidi huo ufanye kazi yake…’akasema..
‘Hapana, hatuendi hivyo, …’akasema wakili
‘Kwanini, hatuendi hivyo… nyie si mnajiona hamjakosa..mpo sahihi,
ngoja wayasikie yale tuliyoyaongea ili kikao hiki kibaini je ni mimi
nilimshawishi hadi akanipa mimba au ni mipango yake, huenda hata hiyo mipango,
ilipangwa kisiasa na mume wangu akashawishiwa kuikamilisha, kama ni hivyo basi
alibainishe hilo, lakini kwa ushahidi sio kwa kujikosha,..’akasema
Mume wa familia akawa kimia…
‘Je mume wa famalia, upo radhi wayasikie au utakubali makosa yako
ili kuwasaidia hawa watu, kuwa wewe kweli ndivyo ulivyo, na nia yako mbaya
kwao, ili na wao wapate muda wa kukufikiria, au kama hutaki, basi, waniruhusu
wasikie japokuwa kidogo, kauli zako, dhidi yao, nafahamu wakisikia hayo,
watakufahamu ulivyo…’akatulia
‘Nasema na wewe… au unaogopa kwa vile wakisikia uliyoyaongea kamwe
hawatakusamehe..’akasema.
‘Mwongo wewe..hizo ni mbinu zako tu….’akasema
‘Mimi mwongo, eeh,..Je niweke hayo mazungumzo bayana, watu
wayasikie…?’ akageuka kumuangalia wakili wake, na wakati huo mume wa familia
alikuwa akitaka kuongea jambo lakini akaghairi, na baadae akainamisha kichwa
chini
‘Ndugu mwenyekiti, mimi nataka nimalize hii kazi, ili isiwe ni
kazi sana kwenu, msipoteze muda wenu bure, wakati ukweli upo bayana, na mimi
nashukuru mungu kwa ujuzi nilio nao, niliufanyia kazi, nilijiahidi kukusanya
yote…akashika mkoba wake.
Hapa nimekamilika, na sio hapa tu,maana wengine wanaweza kufany
ambinu za kuninyang’anya huu ushahidi , ushahidi huu upo sehemu nyeti, na muda
wote ukihitajika, unapatikana, …tunaenda kidigitali…
‘Sasa kama mimi nimetangulia kuyasema madhambi yangu, wengine nao
wafuate, aje mume wa familia akiri madhambi yake ili aokoe yale ambayo bado sijaanza kuyasema, ninao mengi, hasa sehemu ya pili, hapa ndio kwanza naanza…’akasema
Mwenyekiti akageuka kumuangalia mkewe, kuna kitu mkewe alitaka kumuelezea, wawili hao wakawa wanateta kidogo,
halafu mwenyekiti akainua kichwa kuniangalia mimi, kama anataka mimi nisema jambo.
Kiukweli mimi pale nilikuwa nimeshahama kimawazo, kuna muda nilianza kujilaumu, kuna muda nilikuwa na hasira za kutaka kufanya ubaya, kuna muda...niliona sina la kufanya,, lakini hasira chuki, vilikuwa vinikinisakama kooni...pale pale nikawatupia macho watoto wale wawili
Nilimuangalia mtoto wa yule binti, alikuwa anafanana kwa kila kitu na mtoto wa rafiki yangu,...nikajiuliza hao watoto wana hatia gani, kwanini haya yametokea kwenye familia yangu...
'Upo na sisi mke wa familia,...?' nilishituka nikiulizwa na mwenyekiti, sikuelewa niliulizwa swali gani awali, nikajikuta nikisema
'Nipo mwenyekiti, tupo pamoja,...'nikasema
Mara wakili wa mume wangu akanyosha mkono, na ikaonekana kama vile mume wa familia anamzuia,....
‘Mnataka kusema nini…?’ akauliza mwenyekiti akimuangalia wakili
huyo, na huku simu yake ikiingia ujumbe akawa anausoma huo ujumbe, na baadae akainu uso kumuangalia huyo wakili. Uso sasa ulikuwa umekunjamana, ina maana ujumbe huo , aliousoma mwenyekiti ulikuwa na jambo nzito...
WAZO LA LEO: Tunapopewa dhamana ya kuhukum, tuhukumu kwa uadilifu,
na tunapopewa dhamana ya utetezi, tutetee kwa wema ili haki ukweli uwe bayana,
na tunapotoa ushahidi tuwe na uhakika na ushahidi wetu, kwani hapo tunacheza na
maisha ya mtu, tunawakilisha sehemu ya haki na ukweli , ukipindisha ukweli na
haki ikaenda kusipostahiki, utabeba hiyo dhamana na mzigo huo utakufa nao.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment