‘Unasema wewe ni mpenzi wake wa facebook, kwanini hujampigia yeye
mwenyewe kwenye simu yake,..?’ akauliza docta
‘Hayupo hewani, lakini simu…’akasema akiniangalia mimi, ni kweli
simu yangu ilikuwa imezimika.
‘Umeipataje namba ya simu yangu..?’ akauliza
‘Oh,…kwahiyo wewe upo wapi..nyumbani kwako wapi…ok, kwahiyo wewe
unataka nini sasa,..aje au tuje, wapi sasa..nyumbani kwenu wapi..?’
‘Makaburini..?’ akauliza docta kwa mshangao
‘Unajua usituchezee akili, sema wewe ni nani..?’ akauliza docta kwa
sauti kali, halafu akawa anasikiliza.
‘Ok tunakuja, …na nasema sitaki kusumbuana, kama wewe ni mpenzi
wake kweli, basi ujitokeze, na tusiwe tunafika hapo, halafu hakuna mtu, mimi sio mtu wa kuchezewa,
unasikia,…sawa, tunakuja..’akasema na kukata simu
Docta akaniangalia kwa makini , halafu akasema;
‘Unajua kuna kitu kipo nyuma ya haya yote…, na inabidi twende huko
makaburini anapodai huyo mpenzi wako wa facebook yupo na tutakutana naye huko..,
lakini ..hebu fungua mtandao wako wa facebook..’akasema docta na mimi
nikafungua mtandao wangu na kwenye page yangu, sasa nikamuona huyo menzi wangu
wa facebook, sasa akiwa hewani.
‘Hebu chat naye…’akasema na mimi nikaanza kuchat naye, na huyo
mpenzi wa facebook, akaandika ujumbe kuwa mimi nimemsahau sitaki hata
kuwasiliana naye..yaonekana simpendi tena…
‘Lakini wewe ulikuwa umefunga akaunti yako ya facebook, ningewezaje
kuwasiliana naye…’nikamwandikia hivyo.
‘Samahani line yangu ilipotea, na sasa nimeirudisha tena, ila siku
kadhaa nilipojiunga tena, sikukuona ukiwa hewani ndio nikajua hunitaki tena..’akaandika
hivyo.
‘Sasa kwanini umempigia simu docta, …unataka sasa hata yeye
akufahamu kwanza umemfahamuje, na namba yake..?’ nikamuuliza
‘Ndio najua huyo ndie mshirika wako wa karibu…yeye anajulikana
sana, hata namba zake kazitoa, zipo hewani kwasababu ya utaalamu wake,…sasa
nilikuambia awali sitaki nijulikane na watu, sitaki urafiki wetu ujulikane na
watu, kabla wazazi wangu hawajafahamu, mbona umeshamjulisha huyo docta
wako...’akauliza
‘Lakini yeye ni dakitari wangu , na hajui kuwa mimi na wewe ni marafiki
ndio maana nashangaa wewe kumpigia simu yeye…’nikasema
‘Kwahiyo sasa umeshaanza kunidanganya, hivi kweli unania ya kunioa
mimi, ..wakati unanidanganya,…wakati mpo na huyo docta, kila kitu anakifahamu,…’akasema
‘Sasa unataka tufanyeje ili uweze kuniamini, ..nilishakuambia
nataka kuja kwako kujitambulisha, ukanielekeza vibaya, sasa unataka mimi
nifanye nini..’nikaandika
‘Kama umeshajiandaa haya wewe njoo, itakuwa vyema zaidi, …nataka
uje eeh, ok, njoo tu…’akaandika hivyo.
‘Nije wapi sasa..’nikauliza
‘Kule kule nilipokuelekeza kipindi kile…, utanikuta nakusubiria, ..’akasema
‘Unauhakika maana safari zote nikija unakuwa haupo, kiukweli nina
hamu sana ya kukutana na wewe..’nikasema
‘Usijali utanikuta…ukitaka unaweza kuja na huyo docta wako…baadae
kuna kazi nafanya..’akasema na kutoweka hewani.
Docta akasema twende…na tukaondoka naye hadi huko maeneo ya
makaburini, na tulipofika hatukukuta mtu, kama alivyodai yeye, tukazunguka wee,
mpaka tukachoka, tukapiga simu ikawa haipatikani.
‘Umeona eeh, huyu mtu kuna kitu anakitaka kwako…’akasema docta
‘Kitu gani docta…una maana huyu mpenzi wa facebook,?’ nikauliza ,
lakini docta hakunijibu alikuwa kama anachunguza jambo, akawa anaangalia huku
na kule kwa makini, hlafu akasema;
‘Hebu twende kwenye hilo kaburi, alilozikiwa huyo mpenzi
uliyemuasi,..akajiua..’akasema
‘Mimi silijui, …sijawahi kufika eneo hili nikaingia ndani kwenye
maeneo ya makaburi,, safari ile ya kwanza niliishia hapa…’nikasema
‘Litakuwa lile pale,..walisema limejengewa vizuri, lile pale,…huoni
hata jina lake..’akasema na kuanza kutembea kuelekea huko, sikupenda kwenda
huko lakini ikabidi, nikawa namfuatilia nyumna docta hadi tukafika.
Lilikuwa limejengewa vizuri tu,..ila kuna sehemu inaonekana kama
ilibomoka, au kubomolewa kwa pembeni, na kukarudishwa tofali kama kuegeshewa tu,…docta
akapachunguza, baadae akasema;
‘Hapa nahisi kama kuna mtu kabomoa,kwa makusudi, …hebu
kwanza,akajaribu kuinua lile tofauti kuliondoka, lakini likawa limekaza
halitoki..baadae akaghari na kucha kama lilivyo.
‘Kuna mtu anatuchezea akili..’akasema docta akiangalia huku na kule
‘Kwa vipi..?’ nikauliza
‘Wewe huoni hapa,…ni kama kuna mtu alipabomoa hapa kwa makusudi
halafu akaja kulirejesha hili tofali , kwa kulichimbi, hapa hapajajengwa
zamani, ni karibuni, unaona hii sementi sio y asiku nyingi…, angalia hapo, kuna
mguu uliokanyaga hapo, na kuacha nyayo za cement..’akaonyesha,..
‘Ina maana kuna maiti ..inatoka kaburini..na kuja duniania..?’ nikmuuliza
‘Maiti haiwezi kutoka kaburni…huyu ni mtu anafanya usanii, lakini
ngoja tuone kwanza, unajua kuna kitu tunatakiwa tukifanye kisayansi ili kuondoa
sintofahamu kwenye vichwa vya watu…kama ingeliwezekana , wenyewe wakaturuhusu
tungelilibomoa hili kaburi tuone huko ndani kupoje, inaonekana kabisa kuna
uwazi ndani, …’akasema
‘Oh, haiwezekani, maana kaburi linashushiwa udongo mwingi sana, na
kujazwa, iweje kuwe na uwazi..?’ nikauliza
‘Ndio maana hata mimi ninashangaa…’akasema , akawa
anachunguza,kulizunguka hilo kaburi, mpaka akaona kuna sehemu kuna uwazi, akachukua
kijiti na kukizamisha kwenye huo uwazi, kijiti kikazama chote..
‘Unaona…kuna uwazi kwa ndani, sijui kuna nini humo ndani, lakini
hatuwezi kufanya lolote kwa sasa, …’akasema
‘Sasa..?’ nikauliza nikichunguza ule uwazi, na kuhakikisha kuwa
kweli kuna uwazi fulani kwa ndani.
‘Inabidi , ikibidi tuongee na wahusika, ili tuje kubomoa,lakini
hata hivyo..kwanini kwenye hili kaburi, kuna kitu hapa,...’akasema docta
‘Labda tuwaambie kuna uchunguzi unafanya wa kidakitari, lakini
havyo docta, ili iweje, tunataka kuhakiki nini,…’nikasema
‘Ok,..tuachane na hilo,.. ukumbuke tuna safari ya kwenda nyumbani kwa Mashauri, nataka wewe ukaongee na
huyo binti yake, uone kama anakukumbuka, au ana nini anachokitaka kwako,je yupo
tayari umuoe, maana kiukweli ni lazima umuoe,..hiyo ni sehemu muhimu kwako, na
kwa hiyo familia..’akasema
‘Lakini docta, yawezekana huyo binti ndiye anatuchezea,… huenda
ndio yeye kajiingiza kwenye facebook akatafuta picha ya kihivyo..inayofanana
fanana na yeye au sio, na dio huyu ana…kaja huku kutuchezea akili, hulioni hilo..?’
nikauliza
‘Sizani, maana yeye anaumwa kweli, hawezi kutembea,ndio anaweza
kuchuku bajaji akaja akafanya hivyo, lakini jiulize ili iweje, anataka nini…haiji
akilini,…labda awe anashikirikiana na mtu mwingine, swali bado ili iweje,…nahisi
kuna mtu mwingine, yupo nyuma ya hili jambo, ana utaalamu wa mitandao, na…ni
mtaalamu wa nguvu za giza, yawezekana huyo huyo ana mawakala, au yeye huyo huyo
anajianya mpenzi wako wa
facebook…’akasema
‘Lakini awali ulisema huyo mtu ni shetani..’nikasema
‘Yawezekana ni shetani kweli…lakini uelewe shetan pia anaweza akawa
binadamu kutokana na matendo yake kuna watu mashetani, wanakula nyama za wafu,
..wanakunywa damu za watu, tunaishi nao….dunia hii ina mambo..’akasema
‘Docta..unaamini hayo mambo kuwa yapo kweli, mtu ale nyama za wafu,
ni mtu kweli huyo, hapana docta..’nikasema
‘Tutaona huko mbele, mimi sio mganga wa kienyeji, natumia sayansi
kuhakiki mambo, ila hisia zangu zinaona kuwa kuna mtu yupo nyuma ya hili jambo
sijui dhamira yake ni nini,…na pia yawezekana ni shetani, au ana tabia za
kishetani, kama nilivyokuambia kuna watu kwa sura na maumbile lakini kitabia
sio wenzetu...’akasema
‘Ohh, docta naona unanichanganya ok, uonavyo,,..sasa..’nikasema
‘Subiri…unaona ile karatasi pale, yaonekana imepeperushwa, ilikuwa
pale juu ya kaburi…,unaona alama ya kubanduka,…hebu, usiguze kwanza…’akasema na
kuchukua kijiti, akaigeuza ile karatasi,…na ndipo tukaona maandishi, kulikuwa
na maandishi yaliyoandikwa kwa rangi nyekundu, ni kama damu iliyotumika
kuandika; maneno haya;
‘Karibu
mpenzi wangu wa facebook, hapa ndio nyumbani kwangu, najua siku si chache
tutaungana pamoja..mimi nikupendaye ..mpenze wa facebook.
Docta akawa anatumia kijiti kukwangua kwangua yale maandishi…, ni
kama bado yalikuwa hayajakauka, kwani kila kikwangua na kile kijiti,
inajichora..…akaacha kile alichokuwa akikifanya akawa anaangalia huku na kule
‘Kuna mtu kaweka, huu ujumbe na hayupo mbali, mhh, huyu mtu ni
hatari….’akasema akichunguza huku na kule, lakini hakukuwepo na mtu karibu, ila
yeye ni kama naona kitu ambacho mimi sikuoni..
‘Hata maandishi hayajakauka vyema..’akasema, na kuchukua kifaa
chake kwenye vitu vyake, ni kidarubini kidogo, akawa anachunguza yale
maandishi,..na kusema
‘Hii damu kabisa..ya mnyama au mtu..’akasema na akachukua kichupa
na kuanza kukwangua ili kupata sample akaweka kwenye chombo, na kusema;
‘Nitaenda kupima kwenye maabara…’akaweka kwenye nailoni, halafu
akaichukua ile karatasi na kuiweka kwenye nailoni alikuwa kavaa kinga kwenye
mikono yake, na alipomaliza kuziweka hizo kumbukumbu, akasema;
‘Unajua hili jambo sasa linaanza kuleta sura nyingine tofauti na
nilivyodhania,..kuna hatari kubwa, nahisi kuna dalili za mauji….’akasema
‘Kwanini..?’ nikauliza sasa nikimuangalia docta kwa mashaka.
‘Inabidi tumtafute huyo mpenzi wako wa facebook au huyo
anayejiigiza kuwa ndio yeye, nahisi kuna mtu anakuchora,..anayekujua wewe na
mahusiano yenu ya nyuma, kuna mtu…sizani kama ni mtu kweli…’akasema
‘Oh, kwanini unafikiria hivyo, unahisi labda ni shetani..?’
nikauliza
‘Wewe huoni, kwanza jinsi gani alivyoweza kukulaghai, hadi ukaingia
kwenye mtego wake,… halafu akakuvuta hadi ukaja kukutana na hiyo familia, na
sasa kuna jambo anataka kulifanya,…usiogope, ila nahisi anataka kukutendea
jambo baya, lakini anataka kujenga hoja ya visingizio,..hoja ambayo hata
familia yako haitaweza kuigundua…’akasema
‘Una maana gani docta, kuwa ataniloga, au , doctaaa…, usijifanye
unaamini mambo hayo, hakuna mtu wa kuniloga mimi, kwanza siamini mambo hayo..’
nikasema kwa kujiamini.
‘Unajua mimi nina uzoefu sana na haya mambo ya watu na tabia zako, …kuna
watu wanaweza kutumia mshetani, au viini macho wakiwa na malengo yao binafsi,
kuna wengine wanayatumia mambo hayo kutaka utajiri, japokuwa hao wa hivyo na
utajiri wao,..hakuna hata mmoja anyeweza kuishi kwa raha, ni utajiri machoni
mwa watu ila kwao wao,… hawana amani, na kifo chao huwa kibaya sana…’akasema
docta
‘Mimi sijui..’nikasema.
‘Lakini wapo hao wenzangu na mimi…ushirikina, na uchawi, hawana
mbele wala nyuma, kazi yao kubwa, ni kughilibu vichwa vya watu, kuwasumbua watu
wamelala, na kuwachezea, hawana lolote, ujinga na wao,..na nikuambie kitu,..sio
wote wanaosema wana mashetani, kuwa wana mashetani, wengine ni ghiliba tu, ili
kutamiza malengo yao..sasa uwe makini sana…’akasema docta
‘Kwahiyo docta ndio kusema hayo mambo yapo, na wewe unayaamini , na
kama unayaamini, unataka tufanyeje sasa, mtu kama mimi ambaye siyaamini kabisa..,
kwanini tusiwaambie polisi,kama una imani kuwa kuna maafa dhidi ya watu kwa
kupitia njia hiyo, si tuna ushahidi, na wewe unayafahamu hayo mambo, au..’nikasema
‘Polisi hawawezi kuingilia mambo kama haya yasiyo na ushahidi
unaoshikika, kwa hili, kwa sasa hivi, sijui huko mbeleni, itakuwaje..ila kuanzia
sasa, kutokana na hili, sisi ni polisi , wapelelezi, … muhimu kwa hili, unisikilize,
na unifuate nitakachokuambia, narudia tena, ukiwasiliana na huyo mtu, usinifiche
jambo, kwa angalizo, sio nakutisha, wewe upo hatarini..’akasema
‘Nipo hatarini kwa vipi docta,…usinitishe….na unasema nichati na
huyo mdada, maana nimemumisi kweli.?’ nikauliza
‘Sawa…nakuona bado unalichukulia jambo hili ki mzahamzaha.., huu
sio mzaha, unawafahamu watu wanaoitwa freemasoni..?’ akaniuliza
‘Nawasikia tu…wapo kwenye mitandao, wana mpaka mtandao wao..unajua
mimi siamini mambo hayo ya kutaka utajiri, sijui …siamini, sasa wengi wanajiingiza
huko eti wakitaka utajiri, mimi sina tabia yangu…’nikasema
‘Sasa haya mambo yana fanana fanana hivyo, uwe makini sana, ..hii
mitandao kuna wengine wanaitumia kwa namna yao, wameshajua huku kuna watu
wanaingia lakini hawajui kabisa wakitendacho, kazi yao ni bendera fuata upepo,
wanaweka mapicha yao, wanaweka kumbukumbu zao za simu, ni hatari,..kuna watu
watalizwa humu, na..na hebu ngoja kwanza, kwenye ndoto yako uliota upo maeneo
gani ..?’akaniuliza
‘Hata sikumbuki…ila kweli…nilikuwa maeneo kama makaburini,
au..unajua unaota kama umelala, lakini upo mahali fulani hivi, ndio nakumbuka
nilikuwa sehemu tulivu, kuna miti miti…baadae tukajikuta tupo na hiyo familia,
kama vile tupo mahakamani, mimi nimesimamishwa kuhukumiwa,…mengine ni kama
nilivyokuambia...’nikasema
‘Kwanza nataka twende kwenye hilo jengo walipokuwa wanaishi hiyo
familia, na tukitoka huko tunaweza kwenda kuonana na wagonjwa wetu..’akasema
‘Ina maana huyo aliyekupigia simu alikuwa nani, mimi nilijua ni
huyo mgonjwa wetu, binti..?’ nikauliza
‘Sio yeye, ..nilidhania hivyo awali , lakini wakati tunakuja huku
niliwapigia simu, nikaongea na mama yake, anasema mgonjwa bado hajaweza
kutembea vizuri, na siku nzima ya leo alikuwa naye…sasa angeliwezaje kuja
huku…’akasema docta.
‘Kwahiyo ina maana uliyeongea naye,huuenda ni…ni huyo mpenzi wa
facebook..docta hapo mimi sijakuelewa, nahisi kama unachanganya mambo..?’
nikauliza
‘Wewe unasemaje…, je huyo mpenzi wa facebook, yawezekana akawa
nani, unahisi labda ni huyo dada mgonjwa au, hebu rudidha kumbukumbu zako…maana
mlikuwa mnatumiana picha,unasema picha zote alizifuta, lakini unamkumbuka
vyema, au sio…na sasa umeshamuona huyo binti mgonjwa, je wanafana ..?’ akauliza docta
‘Unajua nikimuangalia huyo binti, inakuja taswira machoni mwangu,
kama zile picha za huyo mpenzi wa facebook, lakini nikimuangalia sana, sura ile
inaondoka…na nikimchunguza sana huyu binti, ndio kuna kufanana fulani hivi…,
lakini sio yeye, maana, huyo mgonjwa, macho
yake yamezidi ukubwa na uzuri zaidi…na kwa upande wa huku usoni yule wa facebook
ni mnzuri zaidi, unaona, ,…kuna utofauti fulani, lakini mmh, utafikiri ndio
yeye…’nikasema
‘Hapo sasa,.huoni kuwa kuna jambo limejificha,..ndio maana nataka
twende huko kwenye hilo jengo lao walilolitelekeza, kuna kitu kinanivuta twende
huko,..nataka kuliona na kuingia ndani, …na sijui huyo mwenyeji wao kama yupo
au keshaondoka…’akasema
‘Aondoke kwenda wapi wakati yeye ndio mlinzi au..?’ nikauliza.
‘Sio mlinzi yule, ..alikuwa mpangaji wao..na walipohama wenye
nyumba, yeye akaendelea kubakia humo..’akasema
‘Kwanini sasa,…?’ nikauliza
‘Ndio swali langu hata mimi, hebu twende huko…nataka kuliona hilo
jengo, ila subiria kwanza tuombe ulinzi maana huko tunakwenda kwenye miliki za
watu..na kama hayupo itakuwa vyema,..nahisi hayupo,…’akasema
‘Unajuaje…?’ nikauliza, lakini docta hakunijibu yaonekana alikuwa
kwenye maombi, au anawaza jambo, huku tunatembea…
Tukatembea, ilikuwa sio mbali sana na hapo makaburini, tulipofika,
docta akaniambia niwe namfuata nyuma …nisitembea mbali na yeye, sikumulewa,
alikuwa kama anaona jambo, lakini hataki kuniambia.
‘Yaonekana hakuna mtu, ndani ya nyumba, ila kuna dalili za harufu
na moshi, huuoni …’akasema
‘Mhh, mimi siuoni, hata harufu bado….…’nikasema.
‘Hebu subiria,…’akachukua gloves za mikono, akavaa, akashika kitasa
cha mlango, akazungiusha kitasa, mlango ukafunguka,..akaniashiria tuingie
ndani,..nilihisi mwili ukinisisimuka…nikasita kuingia lakini kwa hali kama hiyo
nikaona nisicheze mbali na huyu mtu.
‘Sasa na mimi.., puani kulipenye harufu kali ya manukato ya
kufukiza, ..nilihisi hata kichwa kinaanza kuniuma, docta akawa anatembea
taratibu huku mimi namfuata nyuma, ni kama tunanyata…alikuwa na tahadhari
kweli, ni kama anaona kitu ambacho mimi sikioni,, …tukafika sehemu ya
mapokezi..kati kati ya sehemu hiyo ya mapokezi,..kulikuwa na chungu, kinafuka
moshi, na juu kimening’inizwa kitu kama vibuyu, kina shanga za rangi mbali
mbali…
Docta akawa anavichunguza vitu hivyo kwa macho, chini sakafuni, nikaona
karatasi,..kama ile ya kule kaburini, na maandishi yale yale… na pemben kuna
kuna picha, ..picha ya msichana,..niliitizama kwa makini…mmh, sio picha ya …marehemu…ndio
ni picha yake!…oh..na kabla sijasema kitu kwa docta mara nikaona picha yangu.
‘Picha yangu docta na ya marehemu...!’ nikasema.
‘Docta akaniashiria kwa kidole kuwa nisiongee, akasogea hadi kwenye
ile picha, akazisogeza mbali na kile chungu, hakuziokota kwanza…, akachukua
kijiti na kuchokonoa chokonoa kwenye kile chungu, ..yalikuwa makaa ya moto, na
yalikuwa na moto… na mafukizofukizo….
Docta akaangalia kushoto na kulia, …akawa kama anatafuta kitu,
akaona alichokitaka..maji,..kumba alikuwa akitafuta maji, akayaendeea, akayachukua
yale maji, kwenye chombo, akawa anayasomea kitu, halafu akafika kwenye kile
chetezo,..chungu akaanza kumwagia maji mle kwenye chetezo huku akiweweseka
maneno mdomoni,, na moshi ukawa unatoka, ,,kama vile ukizima makaa ya moto
inavyokuwa, lakini cha ajabu, ule moshi ulikuwa kama unakwenda juu na kuzama
kwenye kile kibuyu kilichokuwa kimening’inizwa.
Baadae akahakikisha kuwa ule mkaa umezimika wote, taratibu
akisogeza mkono na kukichukua kile kibuyu chenye uchanga, akakivuta, kwa vile
kilifungwa na kamba kutoka juu kikawa kimening’inia,..kwahiyo akakivuta hadi
ile kamba ikakatika akakichukua kile kibuyu, akawa anakikagua, halafu akatikisa
kichwa kama kukubali jambo.
Sikumuelewa,..ila alionyesha uso kama kutabasamu hivi …
‘Sasa basi kaisha..’akasema akawa anahakikisha kifuniko cha kile
kibuyu kimefunikwa vyema…
‘Nani…kaisha?’ nikauliza.
‘Atakuja mwenyewe, twende zetu…’akasema na mimi bila kusema neno
nikamfuata nyuma, nilikuwa sijisikii nyema humo ndani, maana pumzi likuwa
ndogo,..na kabla hatujatoka, docta alihakikisha amechukua zile picha na
kuhakikisha kuwa hakuna moto tena…
Tukatoka nje ya lile jengo, docta akatoa kitu kama mafuta akawa
anasoma soma soma huku anayarushia mafuta hiyo nyumba,..halafu akasema;
‘Kwa uwezo wa mungu,..mabaya yote, mashetani yote, na viini macho
vyote viteketee, na nyumbahii iwe salama na amani, kwa uwezo wako ewe muumba,
mungu mwenyezi, weka ulinzi kwenye nyumba hii na mabaya yote yaangamia, na
kupotea…’akarusha
hayo mafuta, na kukawa kama kitu kama upepo ukavuma halafu kukawa kimia.
‘Ok, sasa tumemaliza, twende…’akasema na mimi nikamfuata nyuma,
sikuwa na neno, nilihisi kabisa sehemu hiyo sio salama, harufu, mwili
unasisimuka, pumzi inakuwa ndogo..
‘Unajua ..kuna watu wabaya sana kwenye hii dunia, ..’akasema.
‘Nani hao..?’ nikamuuliza.
‘Bado sijajua,… mimi sio mganga wa kienyeji wa ramli, mimi nafanya
mambo kwa kumuomba mungu,..ndio napata njozi, napata maelekezo, lakini huwa
sifanyi jambo mpaka niwe na uhakika nalo..nilihis kuna jambo,..sasa naanza kugundua,kweli
lipo jambo,…lakini sina uhakika huyo mtu ni nani na ana mantiki gani, na lengo
lake hasa ni nini,..lakini atakuja mwenyewe..’akasema.
‘Docta sijakuelewa..’nikasema.
‘Ulikuwa unasema kuwa unahisi kuwa kuna mtu anakufuatilia mara kwa
mara ila humuoni…na kila unapokwenda, anakuw akaribu yako, …na ulipofika
hospitalini, ukaenda kwa mama mmoja,..unakumbuka..’akasema.
‘Ndio…nakumbuka docta nilikuambia hivyo…’nikasema.
‘Hawa watu wajanja sana,…wanataka kutawala kila mahali,..sasa
wameingilia hata mitandao,..na wana mawakala wao, wengine wameingia kwenye
majumba ya ibada wanajifanya watu wa dini, wanatoa mapepo, wanafanya miujiza
mbali mbali,..kuweni makini sana, sio wote wanaofanya hivyo, wana maana hiyo,
wengine ni mawakala wa shetani, wanamtumia shetani huyo huyo shetani kwa ajili
ya kutoa shetani…nia yao hao watu ni masilahi…’akasema.
‘Utajuaje sasa…maana kama ni hivyo wapo wanafanya mambo ya ukweli,
wanatoa mapepo, wanasaidia watu nk..nimewahi kuwaona ila mimi siwaamini…’nikasema
‘Muhimu kama wewe unamjua mungu wako, unaijua dini yako, fuata
maagizo ya dini yako ukiona mtu anafanya mambo kinyume na dini yako jiulize ni
kwanini,…hebu jiulize mungu katuambiaje, shetani ni adui yake, tumlaani na
tuachane naye, kwanini huyo mtu awe anatumia mashetani,
kwanini..jiulize..kwanini awe na ajenda za kishetani,..kuna tatizo hapo, kuweni
makini sana..’akasema
‘Oh, lakini docta ngoja nikuulize kitu, wewe umejuaje haya…kuwa
huku kwenye jengo kuna tatizo…?’ nikamuuliza
‘Ndoto yako..imenisaidia sana..’akasema
‘Kwa vipi…?’ nikauliza
‘Huyo sheteni, huyo mbaya wenu, anataka kukugombanisha wewe na
mimi,..ndio maana akakuvika viini macho uone kuwa mimi nataka
kukuangamiza,..nikajua kuna mtu yupo nyuma yako na keshagundua kuwa
nitamgundua..sasa ujanja wake nimeunasa..’akasema
‘Oh,…docta unataka kunifanya nianza kuogopa..’nikasema
‘Mambo bado, utagundua mambo ambayo huwezi kuamini, ila usiamini,
endelea na imani yako hiyo ya kutokuamini haya mambo, hiyo ndio
inakusaidia,..vinginevyo, ..picha hizo mbili zina maana ya kafara,..kulikuwa na
kitu kinatakiwa kufanywe dhidi yako…ulikuwa unaitwa taratibu uingie kwenye
mitego yao,…mungu anakulinda, imani yako, ushujaa wako wa kutokuogoa
vimekusaidia sana…, na ni mungu tu…wa kumshukuru, na siku zako hazijafika,..’akasema
Mara simu ya docta ikaita…docta akaitizama hakupokea, akakata
simu..
‘Mbona hupokei simu..?’ nikamuuliza.
‘Bado wakati muafaka…’akasema, na tukachukua usafiri hadi nyumbani
kwa familia ya Mzee majaliwa, tulipofika tulimkuta mzee Majaliwa yupo na mtu
mwingine wanaongea, yule mtu alipotuona tu, akasimama, akaoenakana hana raha,
akawa ananiangalia sana mimi kama haamini jambo,..
‘Karibuni..’akasema mzee Majaliwa
‘Asante…’tukakaa kwenye viti, na mara yule mtu akawa anaanza
kuondoka
‘Mbona unaondoka bila kuaga,..ndugu yangu subiri
nikutambulishe..kwa madocteri wangu,..’akasema Mzee majaliwa.
‘Hapana sikai, nahisi ..sijafunga mlango, ..’akasema huyo mtu sasa
akiondoka kwa haraka hadi mzee Majaliwa akabakia anamshangaa.
‘Hujafunga mlango wapi…kule makaoni kwako,… , kwani kuna nini cha
kuibiwa kule, na kwanini uondoke bila kufunga milango, unahatari wewe..?’
akauliza mzee majaliwa.
‘Hapana, sikutegemea kuwa nitafika huku,..…baadae …, nitakupigia
simu, kwaherini, sikai, …’akawa sasa kama anakimbia.
'Huyu mtu vipi...?' akauliza mzee Majaliwa akimuangalia huyo jamaa akiwa kama anakimbia, na kutuangalia sisi kwa macho ya mshangao, kama anataka tumpatie jibu
‘Atarudi tu…’akasema docta, akimuangalia kwa macho ya aina yake,
mimi nikabakia kuduwaa tu,siku hiyo ilikuwa ni ya maajabu, na kumbe bado
maajabu zaidi yanakuja!
NB: Ni nini hiki, hebu ..hata mimi naanza kuchanganyikiwa.
WAZO LA
LEO:Katika
hii dunia, kuna watu wanajifanya wajanja, kila kitu akifanya ukimuuliza
utasikia,’… unanijua mimi nani, au..nitakuonyesha cha mtema kuni, au…’ wanakuwa
na kiburi, cha kujiona wao ni zaidi, ni watalawa, ni matajiri, wana
nguvu..utawaambia nini…
Jamani jamani, katika dunia hii hatutakiwi tuwe na kiburi ,
hatutakiwi tutembee kwa kujigamba, maana hii dunia sii yetu, sisi ni wapiti njia
tu,..yupo mwenye kiburi, mwenye mamlaka ya hii dunia, akisema kiwe kinakuwa,
akisema wewe siku yako imefika hakuna majadala, huyo ndiye anastahiki kuwa na
kiburi,… sisi wanadamu hatuna kitu, si lolote si chochote,..Tumuombe mola tuwe
wenye kumtii yeye, na kufuata maagizo yake, na kuyaacha yale yote aliyotukataza
..Aamin
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment