Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, December 5, 2016

MISSION TO HELL-tangulizi

                 

                         MISSION TO HELL( MIKAKATI YA KUFA AU KUPONA)


UTANGULIZI:

Ni kisa cha mstaafu mmoja wa jeshi, aliyestaafu akiwa na cheo cha ukapteni, na wakawa wanamuita Kapteni, na ni kweli alikuwa captain wa ukweli, kiutendaji na umahiri wa kipaji lichojaliwa nacho hasa cha shabaha na upangaji wa mikakati. Aliwahi kupewa nishani maalumu ya ‘shabaha na mikakati’ ni nishani ya aina yake.

 Tatizo la mstafu huyu jeshi lilikuwa kwenye damu,  kila kitu chake kilikuwa ni jeshi kutembea, kuongea…, hakujua kabisa maisha mengine ya uraiani, kula kulala jeshini,.., aliwahi kusema damu na hata nyama yake imegeuka kuwa jeshi. Na kwa bahati nzuri kutokana na cheo chake enzi hizo aliwahi hata kupewa nyumba ya jeshini, nje kidogo ya eneo la jeshi lakini nyumba hiyo  ilikuwa ni mali ya jeshi…baadae alinyang’anywa!

Tatizo umri,..na ile hali ya kujiona yeye ni mwanajeshi , ilimfanya asiwe na wazo la kuwa ipo siku atarejea uraiani, atakuja kustaafu, atakuwa mzee…hili ni tatizo la wengi wetu, hasa tukiwa makazini….na kwa vile alijengwa hivyo mtu wa kupokea amri na kutekeleza, hakuwahi kufikiria namna nyingine ya maisha.

Muda umeisha, taratibu zimebadilika, utawala umebadilika, sheria inafuatwa hakuna nafasi tena ya kuwaacha wazee wakati vijana wapo..ikabidi mzee mzima apewe barua yake ya kustaafu, …hakuamini siku hiyo…, alijua ataongezewa angalau hata muda kidogo ili ajipange,  kutokana na ustadi wake, alijua atabakia kambini  awe angalau mwalimu,

Lakini hata akiongezewa muda, hata miaka miwili, atafanya nini tena keshaonekana mzee kwenye makaratasi,..ukumbuke, anachojua yeye ni kuitumia silaha, na fani za kijeshi, na zaidi ni kupanga mikakati ya kivita,…kupewa amri na kutekeleza, akilini hakujua kitu kingine cha maisha ya uraiani...

‘Kwa mujibu wa sheria, unahitajika kukabidhi kila kitu ikiwemo nyumba ya jeshi, na unapewa muda wa mwenzi mmoja, uwe umekamilisha taratibu zote zikiwemo hizo za makabidhiano, na taratibu nyingine za malipo yako ya kustaafu, yatakwenda kwa mujibu wa sheria za nchi…’ yalikuwa maelezo ambayo aliwahi kuyaona wakiandikiwa wenzake, hakujua kuwa ipo siku na yeye yatamkuta.

Siku alipopewa hiyo barua,….alitoka ofisini muda wa kazi akaenda kunywa, hajawahi kufanya hivyo kabla, akavunja sheria kwa mara ya kwanza,....hakuwa na tabia ya kunywa sana, kwani alijua kunywa sana kunakupotezea focus, malengo na msimamo..siku hiyo aliivunja hiyo ahadi,…

Alikunywa mpaka akachelewa kurudi nyumbani, na alipofika nyumbani akaanza kugombana na mkewe aliyempenda sana, hajawahi kufanya hivyo kabla.., na akawa tena kavunja ahadi yake ya kuwa mtawala bora, ya kuwa mtawala bora huanzia kwenye familia yake…na kesho yake akachelewa kuamuka, akavunja sheria nyingine ya kuwa ili uwe askari bora ujali muda…alifika ofisini kichwa kinauma, na hakuweza hata kufuatilia majukumu yake,…akavunja nyingine na nyingine..!

Siku kabla hajakabidhi nyumba, akaja rafiki yake mmoja  wa zamani..rafiki  yake huyu kwenye hiki kisa ndiye aliyemshawishi kutoroka nyumbani kwao na kuja kuishi dar kama chokoraa….kuna matukio mengi alikutana nayo hapa kutoka kuteswa, hadi kwenda uchokoraa,…na  wakiwa mitaani ndio wakaja kuunda kikundi cha sarakasi,…..wakiwa kwenye kikundi hicho ndio kiongozi mmoja wa jeshi akawaona, na kuwatafutia nafasi jeshini kwenye kikundi cha utamaduni .

  Historia ya mstaafu huyu akiwa mdogo, alikuwa na vipaji  vingi vya kuzaliwa navyo, japo hakusoma… kwa vile alikuwa yatima, hana baba wala mama, hakuweza kufuatilia vyema maswala ya shule, matokea ya mtihani yakaja akiwa amefeli na kwa elimu yetu ya msingi isiyojali vipaji akawa hana namna,…akawa mitaani, akaishi na baba mdogo, akaanza kuteswa na mama wa kambo….ndio akakimbia nyumbani.

Sasa walipokuwa huku mjini, ndio vipaji vyake viikaanza kuonekana kumbe huyu mtoto alikuwa na kipaji cha , sarakasi, na  mwili wake ulikuwa mwepesi wa kupenya sehemu isiyopenyeka,…kusoma kifaa na kukifungua akakirudishia kama kilivyo....pia alikuwa na akili ya kushika mambo kwa haraka,…hata darasani waliliona hilo, ila matokea ya mtihani akaonekana kafeli,..

Na alipofika jeshini akagundulikana kuwa pia ana kipaji cha kulenga shabaha…kwa ustadi huo ikawa wepesi kwake, kuajiriwa na kuwa askari wa jeshi.

Alipanda vyeo kwa shida,… private , koplo….maana hakuwa na elimu , zaidi ya kuishia darasa la saba, kwahiyo kilichomsaidia ni ule ustadi wake wa kukariri vitu kwa haraka,..aliifahamu silah kama kiganja chake cha mkono…aliweza kuifungua na kurejesha akiwa kafunga macho…. Na zaidi baadaye  aliwahi kwenda vitani, huko akaja kupanda cheo hadi akafikia ‘Uluteni’,..na aliporudi nchini, akapata mafunzo ya uongozi , na kuja kufikia cheo cha ‘ukapteni’..ndicho alichobakia nacho hadi kustaafu.

**********

‘Rafiki yangu ,utaona labda  huu sasa ndio mwisho wa maisha yako,..lakini kwa vile bado upo hai, unapumua, lazima akili ifanye kazi…., tatizo lakekwasasa  ni kuwa maisha ya kutegemea kukinga kutoka serikalini hilo halipo tena, ule umri wa kusubiria mwisho  wa mwezi  huo haupo tena, ule umri wa kupewa kila kitu, hadi nguo za jeshi  sasa huo haupo tena…sasa ni umri wa wewe kutumia akili yako, uishi au ufe…ukilala imekula kwako,..hebu niambie ...sasa utafanyaje,…’rafiki akamueleza.

‘Hata sijui nifanyeje,..nasubiria amri ya mungu…’akasema mstaaafu.

‘Hilo ndilo tatizo lako, kila kitu amri..mungu hapa anasubiria pia juhudi yako….mkono utoao ndio upewao.. jibidishe utapata, riziki ipo, lakini itafute kwanza  au sio…Mimi ningekuhitajia, kama unataka,..’akaambiwa na jamaa , rafiki yake, mwenzake alishawekeza, ana gari ana nyumba, miradi kadhaa..

‘Unakaribishwa uraioani,..ukumbuke haya ni maisha mengine tofauti,  kiukweli  nilikuwa na jambo moja, unajua mimi nina mbinu zangu za maisha kuna zakuonekana na nyingine hakuna anyezifahamu,..wananita kinyonga…..najua hutanielewa kutokana na jinsi ulivyolelewa huko jeshini…, wewe umekuwa mtu wa kufuata sheria za nchi..lakini sheria hizo zimekusaidia nini hadi hii leo, hebu niambie…sheria hizo ndio zinakutupa mitaani, huna mbele wa nyumba…’akaambiwa.

‘Sasa ulitaka mimi nifanye nini..muda  umefika, lazima sheria ichukue mkondo wake, siwezi kuwalaumu kwa hilo..najilaumu mwenyewe tu, kujisahau,..’akasema jamaa kwa shingo upande.

‘Hebu rafiki yangu niambie, nani na nani, si unawafahamu,…hao umewaona walivyowekeza, mlikuwa nao hapa jeshini,…wakaondoka mapema tu, kabla hata ya muda wa kustaafu, jiulize ni kwanini, chukua hatua kabla hujakongoloka..,..acha hao, hawa wengine,..ambao walikuwa wakitumia mgongo wako, kukupa amri, sasa hivi wana mehakalu, miradi..hawana shida, wengine wamekuwa wakuu wa mikoa, nani sijui….wewe umepata nini…na leo wanakutupa nje, bila hata kujali maisha yako ya baadae…’ akaambiwa

‘ Ni kweli inaniuma sana…’akasema kwa masikitiko.

‘Mimi sitaki kukuharibu, maana nyie ni waadilifu wa nchi..hongereni sana.., ni sawa, sote twatakiwa tuwe hivyo, lakini je uadilifu unajenga,..unaweza kuwa kama akina nanihii kweli…kweli, hebu chunguza hili,..mimi nilifuatilia nyendo za kila mmojawapo, nimegundua mengi sana..asikudanganye mtu,…ili ufikie kule, inabidi wakati mwingine uruke ngazi, uruke ukuta…na ufanye hata yale yasiyofaa….sasa akili kichwani mwako, kama wahitajia msaada wangu, nifuate, kama hutaki subiria ufe na kihoro… kama akina nanihii…’akaambiwa.

‘Lakini wewe ndiye rafiki yangu, nisaidie kwa hili…’akasema.

‘Mimi nina misheni..najua wa kuifanikisha ni wewe…inaitwa misheni ya mafanikio, lakini ni mawili kupata au kukosa,,….najua nikiwa na wewe tutafanikiwa tu, hatuwezi kukosa, ila ukikosa, ndio to hell, hamna jinsi, lazima ukutane na Izraili hilo sikufichi…..maana ukibakia duniani itakuwa ni tatizo,..ila nina uhakika misheni hiyo itafanikiwa,..sijawahi kufeli kabla..labda nianzie kwako….siwezi kukuambia kila kitu kwa sasa…’akaambiwa.

‘Mhh, sijakuelewa, una maana gani , unataka nifanye nini…?’ hapo akashituka.

`It’s a mission to hell…’unanisikia, mimi nilibahatika kusoma nilipoacha jeshi, lakini wewe kama mtaalamu wa mipango ya kivita nk…. utanielewa nina maana gani.  Ina maana kubwa ya kucheza karata yako ya mwisho ya maisha, ukifanikiwa, umeula…utayasahau haya yote, lakini ukifeli,…it’s a hell, man…you ar going to die,…sizani kama utapenda kwenda jela,…na hata huko sizani kama utaishi, huko wapo watu wangu huko.., vichaa….’  Akaambiwa.

‘Unajua rafiki yangu mimi sijakuelewa, mimi ninachotaka ni shughuli ya kuniingizia kipato, halali..sijali ni kazi gani, lakini unavyoongea yaonekana unataka niwe jambazi..au sio..mimi siwezi hivyo…’akasema.

‘Ipo siku utakuja kunielewa….huna namna wewe..ushakwisha,..tumia kipaji chako ulichojaliwa na mungu wako kwa mara ya mwisho, cheza na karata yako uliyobakia nayo, utakufa  utafaidi wapi hilo…'akaambiwa.

'Kipaji gani, na uzee huu....?' akauliza

'Wewe unajua kupanga mikakati, hicho hakizeeki, na sasa unaweza kupanga vyema kihekima,,..lakini sasa ni mkakati ya vipi, sio  ya kivita tena, sasa upo uraiani utaipanga wapi hiyo mikakati.., hebu niambie….'akaambiwa

'Sasa uniambie wewe....'akasema

'Sikiza ndugu yangu, kila kitu kina shemu mbili nyuma na mbele...sasa hivi upo uwanja mwingine wa maisha ya duniani,..uraiani,…mimi nayajua yote hayo....siwezi kukuambia kila kitu, kwa hivi sasa..muda utafika,.., njoo kwangu utajirike, kama hutaki, sikulazimishi…wewe ni mpiganaji kufa sio tatizo au sio..but kifo cha uraiani ni tofauti na jeshini, ...ni kigumu, utateseka kitandani weee, mpaka watu wakuchoke,….'akaambiwa.

‘Mmhh…siamini…’akasema

‘Utakuja kuamini siku yake ikifika, ...., bado hujasota , ipo siku utanitafuta…’akaambiwa, na rafiki yake huyo akaondoka

*************

 Mazungumzo hayo alikuja kuyakumbuka baada ya kusota sana..muda huo hana mbele wala nyumba, kaibiwa kila kitu, kaumwa sana,. Kutokana na kuumizwa na hao majambazi, walikuja kumuibia mafao yake,...wakamkata mkono..akaponea chupu chupu kuwa kilema, muda huo anayawaza hayo, yupo ndani kwenye kibanda chake cha mbavu za mbwa…anaumwa…hana hata senti moja, mstaafu wa jeshi, kapteni…!

‘Hiki ni kisa cha aina yake, kinaingia ndani ya Nyanja za watu,….sipendi, lakini utafanya nini, wote ni hawa ni abira wetu,…hiki kisa kinamtoa mstaafu mmoja ambaye sasa yupo kitandani anahesabu masiku, tunampa moyo kuwa ipo siku, asikate tamaa ilimradi anapumua,...

Swali ni , je lifikaje hapo alipo....

Ni kisa cha ujasiri, masikitiko, kukata tamaaa, ujambazi  na kila aina ya ushenzi wa hii dunia..….

‘It’s a mission to hell,…’.hebu emuthree, ufanye vitu vyako kidogo,  watu wamechoka kusubiria, ni kama kile cha ‘dunia yangu’ lakini kivingine kihalisia zaidi..,..

Tuweni pamoja, tuone namna nyingine ya maisha, ya wajasiri , wastaafu, mashujaa wetu wazee wetu wastaafu, lakini wamesahaulika masikini…ni kwanini lakini, …na madhara yake ni yapi…mwenye kovu usione kapoa..tuweni makini na hawa watu, tuwasaidie, tusiwatupe…

Ni mikakati mingine ya  ‘mission to hell..’..

WAZO LA LEO: Katika kustaafu kuna kitu kinaitwa kiunua mgongo, bima za maisha na kadhalika, ..bima hizi zinawekezwa kwenye miradi mbali mbali, kutokana na michango ya watu. Nasikia eti kuna fadia inakuja kurejeshwa kwenye michango hiyo, na nyingine hawarejeshewi, eti kutokana na jinsi ulivyoijaza hiyo fomu ya makubaliano, japokuwa michango hiyo inatumika kuzalishia, ni jasho la mtu hilo..

Sasa tuchukulie huyu mtu anachanga elifu kumi kwa mwezi, kuanzia kaajiriwa, enzi anachanga hiyo hela, inaweza kununua kitu, ..na wakati anafikia kustafu  miaka labda thelathini mbeleni, pesa hiyo haiwezi kununua hata shati….thamani yetu ya pesa hubadilika haraka sana…, lakini kwa wakati huo imeweza kuwekezwa kwenye miradi yenye maendeleo, ni jasho la mtu hilo..
Pesa hizo hizo zinakopwa na wakubwa, uaambiwa ukifa zitasaidia maziko yako, hivi ulikopa ili uje uzikwe nazo…sielewi hapo..…

Hivi hakuna namna nyingine ya kuwafikiria hawa wastaafu. Basi hizoo pesa zao zihesabike kama share..mtaji,..ili wakistaafu waweze kuwa wawekezaji ndani ya hivyo vitega uchumi..vinginevyo, mimi naona kama tunawadhulumu watu kwa michango yao,..ni mawazo tu, ijui wengine mnasemaje… !
Ni mimi: emu-three

No comments :