MISSION TO HELL( MIKAKATI YA KUFA AU KUPONA)
UTANGULIZI:
Ni kisa cha mstaafu mmoja wa jeshi, aliyestaafu akiwa na
cheo cha ukapteni, na wakawa wanamuita Kapteni, na ni kweli alikuwa captain wa
ukweli, kiutendaji na umahiri wa kipaji lichojaliwa nacho hasa cha shabaha na
upangaji wa mikakati. Aliwahi kupewa nishani maalumu ya ‘shabaha na mikakati’
ni nishani ya aina yake.
Tatizo la mstafu huyu
jeshi lilikuwa kwenye damu, kila kitu
chake kilikuwa ni jeshi kutembea, kuongea…, hakujua kabisa maisha mengine ya
uraiani, kula kulala jeshini,.., aliwahi kusema damu na hata nyama yake imegeuka
kuwa jeshi. Na kwa bahati nzuri kutokana na cheo chake enzi hizo aliwahi hata kupewa
nyumba ya jeshini, nje kidogo ya eneo la jeshi lakini nyumba hiyo ilikuwa ni mali ya jeshi…baadae alinyang’anywa!
Tatizo umri,..na ile hali ya kujiona yeye ni mwanajeshi ,
ilimfanya asiwe na wazo la kuwa ipo siku atarejea uraiani, atakuja kustaafu,
atakuwa mzee…hili ni tatizo la wengi wetu, hasa tukiwa makazini….na kwa vile
alijengwa hivyo mtu wa kupokea amri na kutekeleza, hakuwahi kufikiria namna
nyingine ya maisha.
Muda umeisha, taratibu zimebadilika, utawala umebadilika,
sheria inafuatwa hakuna nafasi tena ya kuwaacha wazee wakati vijana
wapo..ikabidi mzee mzima apewe barua yake ya kustaafu, …hakuamini siku hiyo…,
alijua ataongezewa angalau hata muda kidogo ili ajipange, kutokana na ustadi wake, alijua atabakia
kambini awe angalau mwalimu,
Lakini hata akiongezewa muda, hata miaka miwili, atafanya
nini tena keshaonekana mzee kwenye makaratasi,..ukumbuke, anachojua yeye ni
kuitumia silaha, na fani za kijeshi, na zaidi ni kupanga mikakati ya kivita,…kupewa
amri na kutekeleza, akilini hakujua kitu kingine cha maisha ya uraiani...
‘Kwa mujibu wa sheria,
unahitajika kukabidhi kila kitu ikiwemo nyumba ya jeshi, na unapewa muda wa
mwenzi mmoja, uwe umekamilisha taratibu zote zikiwemo hizo za makabidhiano, na
taratibu nyingine za malipo yako ya kustaafu, yatakwenda kwa mujibu wa sheria
za nchi…’ yalikuwa maelezo ambayo aliwahi kuyaona wakiandikiwa wenzake,
hakujua kuwa ipo siku na yeye yatamkuta.
Siku alipopewa hiyo
barua,….alitoka ofisini muda wa kazi akaenda kunywa, hajawahi kufanya hivyo
kabla, akavunja sheria kwa mara ya kwanza,....hakuwa na tabia ya kunywa sana,
kwani alijua kunywa sana kunakupotezea focus,
malengo na msimamo..siku hiyo aliivunja hiyo ahadi,…
Alikunywa mpaka akachelewa kurudi nyumbani, na alipofika
nyumbani akaanza kugombana na mkewe aliyempenda sana, hajawahi kufanya hivyo
kabla.., na akawa tena kavunja ahadi yake ya kuwa mtawala bora, ya kuwa mtawala
bora huanzia kwenye familia yake…na kesho yake akachelewa kuamuka, akavunja
sheria nyingine ya kuwa ili uwe askari bora ujali muda…alifika ofisini kichwa
kinauma, na hakuweza hata kufuatilia majukumu yake,…akavunja nyingine na
nyingine..!
Siku kabla
hajakabidhi nyumba, akaja rafiki yake mmoja wa zamani..rafiki yake huyu kwenye hiki kisa ndiye
aliyemshawishi kutoroka nyumbani kwao na kuja kuishi dar kama chokoraa….kuna matukio
mengi alikutana nayo hapa kutoka kuteswa, hadi kwenda uchokoraa,…na wakiwa mitaani ndio wakaja kuunda kikundi cha
sarakasi,…..wakiwa kwenye kikundi hicho ndio kiongozi mmoja wa jeshi akawaona, na
kuwatafutia nafasi jeshini kwenye kikundi cha utamaduni .
Historia ya mstaafu
huyu akiwa mdogo, alikuwa na vipaji vingi vya kuzaliwa navyo, japo hakusoma… kwa
vile alikuwa yatima, hana baba wala mama, hakuweza kufuatilia vyema maswala ya
shule, matokea ya mtihani yakaja akiwa amefeli na kwa elimu yetu ya msingi isiyojali
vipaji akawa hana namna,…akawa mitaani, akaishi na baba mdogo, akaanza kuteswa
na mama wa kambo….ndio akakimbia nyumbani.
Sasa walipokuwa huku mjini, ndio vipaji vyake viikaanza
kuonekana kumbe huyu mtoto alikuwa na kipaji cha , sarakasi, na mwili wake ulikuwa mwepesi wa kupenya sehemu
isiyopenyeka,…kusoma kifaa na kukifungua akakirudishia kama kilivyo....pia
alikuwa na akili ya kushika mambo kwa haraka,…hata darasani waliliona hilo, ila
matokea ya mtihani akaonekana kafeli,..
Na alipofika jeshini akagundulikana kuwa pia ana kipaji cha
kulenga shabaha…kwa ustadi huo ikawa wepesi kwake, kuajiriwa na kuwa askari wa
jeshi.
Alipanda vyeo kwa shida,… private , koplo….maana hakuwa na
elimu , zaidi ya kuishia darasa la saba, kwahiyo kilichomsaidia ni ule ustadi
wake wa kukariri vitu kwa haraka,..aliifahamu silah kama kiganja chake cha
mkono…aliweza kuifungua na kurejesha akiwa kafunga macho…. Na zaidi baadaye aliwahi kwenda vitani, huko akaja kupanda cheo
hadi akafikia ‘Uluteni’,..na aliporudi nchini, akapata mafunzo ya uongozi , na
kuja kufikia cheo cha ‘ukapteni’..ndicho alichobakia nacho hadi kustaafu.
**********
‘Rafiki yangu ,utaona labda huu sasa ndio mwisho wa maisha yako,..lakini kwa
vile bado upo hai, unapumua, lazima akili ifanye kazi…., tatizo lakekwasasa ni kuwa maisha ya kutegemea kukinga kutoka
serikalini hilo halipo tena, ule umri wa kusubiria mwisho wa mwezi huo haupo tena, ule umri wa kupewa kila kitu,
hadi nguo za jeshi sasa huo haupo tena…sasa
ni umri wa wewe kutumia akili yako, uishi au ufe…ukilala imekula kwako,..hebu
niambie ...sasa utafanyaje,…’rafiki akamueleza.
‘Hata sijui nifanyeje,..nasubiria amri ya mungu…’akasema
mstaaafu.
‘Hilo ndilo tatizo lako, kila kitu amri..mungu hapa
anasubiria pia juhudi yako….mkono utoao ndio upewao.. jibidishe utapata, riziki
ipo, lakini itafute kwanza au sio…Mimi
ningekuhitajia, kama unataka,..’akaambiwa na jamaa , rafiki yake, mwenzake
alishawekeza, ana gari ana nyumba, miradi kadhaa..
‘Unakaribishwa uraioani,..ukumbuke haya ni maisha mengine
tofauti, kiukweli nilikuwa na jambo moja, unajua mimi nina mbinu
zangu za maisha kuna zakuonekana na nyingine hakuna anyezifahamu,..wananita
kinyonga…..najua hutanielewa kutokana na jinsi ulivyolelewa huko jeshini…, wewe
umekuwa mtu wa kufuata sheria za nchi..lakini sheria hizo zimekusaidia nini
hadi hii leo, hebu niambie…sheria hizo ndio zinakutupa mitaani, huna mbele wa
nyumba…’akaambiwa.
‘Sasa ulitaka mimi nifanye nini..muda umefika, lazima sheria ichukue mkondo wake,
siwezi kuwalaumu kwa hilo..najilaumu mwenyewe tu, kujisahau,..’akasema jamaa kwa shingo upande.
‘Hebu rafiki yangu niambie, nani na nani, si unawafahamu,…hao
umewaona walivyowekeza, mlikuwa nao hapa jeshini,…wakaondoka mapema tu, kabla
hata ya muda wa kustaafu, jiulize ni kwanini, chukua hatua kabla
hujakongoloka..,..acha hao, hawa wengine,..ambao walikuwa wakitumia mgongo
wako, kukupa amri, sasa hivi wana mehakalu, miradi..hawana shida, wengine
wamekuwa wakuu wa mikoa, nani sijui….wewe umepata nini…na leo wanakutupa nje,
bila hata kujali maisha yako ya baadae…’ akaambiwa
‘ Ni kweli inaniuma sana…’akasema kwa masikitiko.
‘Mimi sitaki kukuharibu, maana nyie ni waadilifu wa
nchi..hongereni sana.., ni sawa, sote twatakiwa tuwe hivyo, lakini je uadilifu
unajenga,..unaweza kuwa kama akina nanihii kweli…kweli, hebu chunguza
hili,..mimi nilifuatilia nyendo za kila mmojawapo, nimegundua mengi
sana..asikudanganye mtu,…ili ufikie kule, inabidi wakati mwingine uruke ngazi,
uruke ukuta…na ufanye hata yale yasiyofaa….sasa akili kichwani mwako, kama
wahitajia msaada wangu, nifuate, kama hutaki subiria ufe na kihoro… kama akina
nanihii…’akaambiwa.
‘Lakini wewe ndiye rafiki yangu, nisaidie kwa hili…’akasema.
‘Mimi nina misheni..najua wa kuifanikisha ni wewe…inaitwa
misheni ya mafanikio, lakini ni mawili kupata au kukosa,,….najua nikiwa na wewe
tutafanikiwa tu, hatuwezi kukosa, ila ukikosa, ndio to hell, hamna jinsi, lazima ukutane na Izraili hilo sikufichi…..maana
ukibakia duniani itakuwa ni tatizo,..ila nina uhakika misheni hiyo itafanikiwa,..sijawahi
kufeli kabla..labda nianzie kwako….siwezi kukuambia kila kitu kwa sasa…’akaambiwa.
‘Mhh, sijakuelewa, una maana gani , unataka nifanye nini…?’
hapo akashituka.
`It’s a mission to hell…’unanisikia, mimi nilibahatika
kusoma nilipoacha jeshi, lakini wewe kama mtaalamu wa mipango ya kivita nk….
utanielewa nina maana gani. Ina maana
kubwa ya kucheza karata yako ya mwisho ya maisha, ukifanikiwa, umeula…utayasahau haya yote, lakini ukifeli,…it’s a hell, man…you ar going to die,…sizani kama
utapenda kwenda jela,…na hata huko sizani kama utaishi, huko wapo watu wangu huko..,
vichaa….’ Akaambiwa.
‘Unajua rafiki yangu mimi sijakuelewa, mimi ninachotaka ni
shughuli ya kuniingizia kipato, halali..sijali ni kazi gani, lakini unavyoongea
yaonekana unataka niwe jambazi..au sio..mimi siwezi hivyo…’akasema.
‘Ipo siku utakuja kunielewa….huna namna
wewe..ushakwisha,..tumia kipaji chako ulichojaliwa na mungu wako kwa mara ya mwisho, cheza na karata yako
uliyobakia nayo, utakufa utafaidi wapi hilo…'akaambiwa.
'Kipaji gani, na uzee huu....?' akauliza
'Wewe unajua kupanga mikakati, hicho hakizeeki, na sasa unaweza kupanga vyema kihekima,,..lakini sasa ni mkakati ya vipi, sio ya
kivita tena, sasa upo uraiani utaipanga wapi hiyo mikakati.., hebu niambie….'akaambiwa
'Sasa uniambie wewe....'akasema
'Sikiza ndugu yangu, kila kitu kina shemu mbili nyuma na mbele...sasa hivi upo uwanja mwingine wa
maisha ya duniani,..uraiani,…mimi nayajua yote hayo....siwezi kukuambia kila kitu, kwa hivi sasa..muda utafika,.., njoo kwangu utajirike, kama hutaki, sikulazimishi…wewe
ni mpiganaji kufa sio tatizo au sio..but kifo cha uraiani ni tofauti na jeshini, ...ni kigumu, utateseka kitandani weee, mpaka watu wakuchoke,….'akaambiwa.
‘Mmhh…siamini…’akasema
‘Utakuja kuamini siku yake ikifika, ...., bado hujasota , ipo siku utanitafuta…’akaambiwa,
na rafiki yake huyo akaondoka
*************
Mazungumzo hayo
alikuja kuyakumbuka baada ya kusota sana..muda huo hana mbele wala nyumba,
kaibiwa kila kitu, kaumwa sana,. Kutokana na kuumizwa na hao majambazi,
walikuja kumuibia mafao yake,...wakamkata mkono..akaponea chupu chupu kuwa kilema, muda huo anayawaza hayo, yupo
ndani kwenye kibanda chake cha mbavu za mbwa…anaumwa…hana hata senti moja,
mstaafu wa jeshi, kapteni…!
‘Hiki ni kisa cha aina yake, kinaingia ndani ya Nyanja za
watu,….sipendi, lakini utafanya nini, wote ni hawa ni abira wetu,…hiki kisa kinamtoa mstaafu
mmoja ambaye sasa yupo kitandani anahesabu masiku, tunampa moyo kuwa ipo siku,
asikate tamaa ilimradi anapumua,...
Swali ni , je lifikaje hapo alipo....
Ni kisa cha ujasiri, masikitiko, kukata tamaaa,
ujambazi na kila aina ya ushenzi wa hii dunia..….
‘It’s a mission to hell,…’.hebu emuthree, ufanye vitu vyako
kidogo, watu wamechoka kusubiria, ni
kama kile cha ‘dunia yangu’ lakini kivingine kihalisia zaidi..,..
Tuweni pamoja, tuone namna nyingine ya maisha, ya wajasiri ,
wastaafu, mashujaa wetu wazee wetu wastaafu, lakini wamesahaulika masikini…ni kwanini
lakini, …na madhara yake ni yapi…mwenye kovu usione kapoa..tuweni makini na
hawa watu, tuwasaidie, tusiwatupe…
Ni mikakati mingine ya ‘mission to hell..’..
WAZO LA LEO: Katika kustaafu kuna kitu kinaitwa kiunua
mgongo, bima za maisha na kadhalika, ..bima hizi zinawekezwa kwenye miradi
mbali mbali, kutokana na michango ya watu. Nasikia eti kuna fadia inakuja
kurejeshwa kwenye michango hiyo, na nyingine hawarejeshewi, eti kutokana na
jinsi ulivyoijaza hiyo fomu ya makubaliano, japokuwa michango hiyo inatumika
kuzalishia, ni jasho la mtu hilo..
Sasa tuchukulie huyu mtu anachanga elifu kumi kwa mwezi,
kuanzia kaajiriwa, enzi anachanga hiyo hela, inaweza kununua kitu, ..na wakati
anafikia kustafu miaka labda thelathini
mbeleni, pesa hiyo haiwezi kununua hata shati….thamani yetu ya pesa hubadilika
haraka sana…, lakini kwa wakati huo imeweza kuwekezwa kwenye miradi yenye
maendeleo, ni jasho la mtu hilo..
Pesa hizo hizo zinakopwa na wakubwa, uaambiwa ukifa
zitasaidia maziko yako, hivi ulikopa ili uje uzikwe nazo…sielewi hapo..…
Hivi
hakuna namna nyingine ya kuwafikiria hawa wastaafu. Basi hizoo pesa zao
zihesabike kama share..mtaji,..ili wakistaafu waweze kuwa wawekezaji ndani ya hivyo
vitega uchumi..vinginevyo, mimi naona kama tunawadhulumu watu kwa michango
yao,..ni mawazo tu, ijui wengine mnasemaje… !
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment