Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, October 28, 2013

Mkuki ni kwa Nguruwe-17


  
Siku hiyo nilikuwa nimekaa nyumbani, sebuleni, na mume wangu alikuwa amelala chumbani baada ya kupata dawa. Dawa hizo huwa akishazitumia, zinampa usingizi mnzito. Na nilipohakikisha amelala, niaona nitoke kidogo nje, na ikibidi nifike madukani, lakini wakati najiandaa kufanya hivyo,  nikasikia hodi, mlangoni.

Kwanza ilibidi nigeuke huku na kule kumwangalia mfanyakazi wangu wa ndani, kwani msaidizi wangu alikuwa katoka kidogo,, nilihisi anaweza kuwa ni mgeni wao, maana mimi muda kama huo wengi wanafahamu kuwa nipo kazini...kabla sijafungua mlango, nikachungulia kupitia dirishani, nikagundua kuwa kumbe ni mdogo wa mume wangu.

Kwanza nikataka nimzuie asiingie ndani, kwani sikutaka mtu yoyote kumsumbua mume wangu, japokuwa nafahamu kuwa mdogo wake, atakuwa analifahamu hilo, lakini moyoni nilikuwa na hamu sana ya kuongea na huyu mtu, na nikaona huenda ndiyo nafasi pekee ya kujua lolote kuhusu kwa shemeji yangu huyu..hata hivyo sikutaka kufanya jambo ambalo ninaweza kujijutia baadaye nikikumbuka onyo kutoka kwa rafiki ya mume wangu.

Hata hivyo, japokuwa nilijua kuwa mume wangu kalala fofo kutokana na hizo dawa, lakini sikuwa na uhakika hizo dawa zinaweza kuchukua muda gani kabla mue wangu hazijazindukana,na mara nyingi akiwa hana usingizi, hapendi kukaa ndani, anapenda kuzungushwa nje na kigari chake cha kukokotwa. Nikaona nitumie muda kidogo kuongea na huyu mtu, lakini kwa tahadhari.

Baada ya kuwaza hivyo,nikafungua mlango, na kutoka nje, nilihakikisha nimeusindika mlango nyuma yangu, na nikawa naangaliana uso kwa uso na shemeji yangu huyu, ambaye inaonekana hakutarajia kuniona hapo nyumbani, akabakia mdomo wazi akishindwa hata kuongea, nikatabasamu ili kumuondoa wasiwasi, na yeye kwa aibu akatizama chini..

‘Habari yako shemeji, mbona unaonekana kama umeona kitu cha kukuogofya, hukutarajia kuniona mimi nini, au una wasiwasi gani?’ nikamuuliza

‘Ni kweli, sikutarajia muda kama huu hapa nyumbani, nafahamu muda kama huu upo kazini....’akasema.

‘Hapa ni nyumbani kwangu bwana, naweza kuja wakati wowote, kwahiyo,...unaogopa kuniona nipo hapa nyumbani, au kwanini unaonekana kuwa na wasiwasi, kuna nini kinaendelea kati yako na mfanyakazi wangu?’ nikamuuliza.

‘Hakuna kitu shemeji, na mfanyakazi wako hakuna kitu kabisa ...mimi hufika hapa kwa ajili ya kumwangalia kaka, na kama kuna lolote la kusaidia, nasaidia, ...na kwanini useme hivyo, wakati hapa ndipo nilipotafutia maisha, ...nafika mara kwa mara....’akasema,

Ni kweli shemeji yangu huyu, alimchukua mume wangu kutoka huko kijijini, tukawa tunaishi naye hapa kwangu, nia na lengi ni kumsaidia kujiendeleza, haa katika kumsomesha na kumjenga kimaisha, na kwa vile kwa muda huo alikuwa amemaliza kidato cha sita,mimi nilimshauri mume wangu tumuendeleze ndugu yake huyo ili asome chuo kikuu.

Alipofika hapo tumamweleze nia na makusdio yetu, yeye kwa muda huo,, hakutaka kusoma tena,alidai hata kusoma huko hadi kidato cha sita, alisoma kwa shida sana, na kuna muda alitaka kuacha kabisa kusoma, ....maisha yalikuwa magumu, na japokuwa kaka yake alijitahidi kumsaidia lakini yeye alitaka kuanza maisha ya kujitegemea haraka, ili apate pesa, na kuliko kutegemea pesa za kuomba omba...alisema yeye alishakata tamaa ya kusoma zaidi, lakini tukapa moyo, na kumuelezea umuhimu wa elimu katika maisha yake. Mimi mwenyewe nilijitahidi sana kumpa moyo hadi akabadilika, na akatulia na kuanza kusoma.

Nilimwangalia alivyokuwa akipata taabu ya kutaka kujieleza , na baadaye akasema;

‘Shemeji hapa kwangu ni nyumbani , bila ya nyie watu wawili sijui maisha yangu yangelikuwaje, ndio maana japokuwa nimeshapata makazi yangu, lakini bado siachi kufika hapa, na ikizingatiwa kwa sasa kaka ni mgonjwa, inanibidi nifike kumuona....’akasema.

‘Mhh, ni ya kweli hayo...?’ nikauliza nikimwangalia.

‘Ni kweli shemeji, mimi nyie ni watu muhimu sana, maana nilishakata tamaa ya maisha, niliona kama maisha yangu yameshaharibika, hasa nilipokuwa nikiwaona wenzangu wa umri wangu wakiwa na maisha mazuri....’akasema.

‘Ni kweli, ..hata hivyo mimi sijazungumzia hilo, nafahamu kabisa hapa ni nyumbani kwako, unaweza kufika muda na wakati wowote upendavyo, lakini wasiwasi wangu ni kuwa unaweza ukawa unafika hapa kwa nia nyingine kabisa, ambayo sitaifurahia, ....’nikasema.

‘Niamini shemeji, huyu mfanyakazi wa hapa nyumbani namchukulia kama mdogo wangu, na sitafanya lolote baya dhidi yake, namjali sana, na kumharibia maisha yake ni kosa kubwa sana kwangu....’akasema na mimi nilimwamini hivyo, na sikuwa na nia ya kumshutumu kwa lolote kuhusu huyo mfanyakazi, nilikuwa natafuta njia ya kumweka sawa kabla sijaongea naye lile nililitoka kumuuliza,

‘Nakuamini sana shemeji yangu, wewe ni sawa na mdogo wangu, ....nakuona sawa kama anavyokuona kaka yako, ndio maana wakati wote nimekuwa nikihakikisha kuwa maisha yako yanakuwa bora, ili uweze kusimama kwa miguu yako mwenyewe, na natumai hayo yameshakamilika...na hapa ni nyumbani kwako, wakati wowote unaruhusiwa kufika, nilishangaa tu, kukuona unakuwa kama unaogopa uliponiona mimi...’nikasema.

‘Mimi niliingiwa na wasiwasi kuwa huenda kaka kazidiwa,...maana muda kama huu, mara nyingi unakuwa ofisini..’akasema.

‘Hakuna tatizo kwa kaka yako , hajambo yupo ndani, kalala, ....na nisingelipenda akazindukana, akute tunaongea hayo ninayotaka kuongea na wewe, ni kati yangu mimi na wewe tu, ....’nikasema na hapo akaniangalia kwa macho yaliyojaa wasiwasi.

‘Unataka kuongea na mimi kuhusu jambo gani..?’ akaniuliza kwa mashaka ikionyesha kuwa kuna mambo huenda alishaonywa, au kwa mtizamo wake, hakutaka kuongea na mimi.

‘Usiwe na wasiwasi, sio jambo kubwa sana,....unaweza kuja  tukaongea huku nyumba kwenye bustani, sijtachukua muda wako mwingi’nikasema huku nikitangulia kwenda kwenye eneo la bustani ambapo ulikuwa na shemeu maalumu tuliitengeneza kwa ajili ya kupumizikia, kulikuwa na viti maalumu, nilifika na kukaa, na mfanyakazi wangu akafika akiniuliza kama anaweza kulete chochote.

‘Tuletee vinywaji, na hakikisha kuwa mume wangu akiamuka unaniita mara moja....’nikasema.

‘Nitafanya hivyo dada.....’akasema.

Na mara akafika shemeji yangu bado akiwa na wasiwasi, nikamwambia akae, na yule mfanyakazi wangu akawa anamminia kinywaji, na alipomaliza akauliza kuna kitu gani tunahitaji, nikamwambia kwasasa hakuna, baada ya kumuuliza shemeji yangu akama anahitaji kitafunio chochote, na kusema kinywaji kinatosha, nilisubiri hadi huyo mfanyakazi wangu alipoondoka, ndipo nikaanza mazungumzo.

*********

‘Mume wako anaendelea vyema, lakini nilikuwa nakushauri, nafahamu kazi kwako ni muhimu sana, lakini pia mume wako ni muhimu, ikizingatia kuwa hata ukiwa kazini bado mawazo yako yatakuwa nyumbani ukiwa huna uhakika kuwa hudumu muhumu zinatolewa kwa mume wako.....’akasema docta

‘Ulikuwa unataka kusema nini docta?’ nikamuuliza.

‘Nilikuwa nataka kusema hivi, kama inawezekana, ningelishauri uchukue likizo, angalau ya mwezi mmoja, ili uweze kuwa karibu na mume wako, hii inaweza kumsaidia mume wako kupona haraka, na kwa faraja,.....’akasema na mimi nikawa sina jinsi, japokuwa ni kipindi ambacho kulikuwa na kazi nyingi ambazo nilihitajika kuzisimamia, lakini ikabidi niwaachie wafanyakazi wangu na kuwaambia kama watashindwa kabisa wanipigie simu.

Mimi nikaamua kuchukua likizo ya mwezi mnzima, kwa ajili ya mume wangu,...kuna kazi nyingine za kiofisi nilikuwa nazifanyia nyumbani, na kama ni lazima nilikuwa nafika ofisini mara moja moja kusaini hundi, ...na, labda kama kuna dharaura, niliwaambia wanipigie simu, na nitaweza kujipanga na kufika ofisini kuzimaliza.

Baada ya wiki nikaona kumbe inawezekana, kumbe nilikuwa nabeba mzigo mkubwa mwenyewe, kumbe ningeliweza kuzigawa kwa watu wangu na wakazifanya itakiwavyo, japokuwa kulikuwa na makosa ya hapa na pale , lakini mengi yalikuwa ni ya kibinadamu.

‘Kama kutakuwa na mabadiliko yoyote, au mkiona kuna hali inamtokea isiyo ya kawaida, naomba unifahamishe haraka iwezekanavyo, na mna bahati kwani mnaishi karibu na dakitari, huyo anaweza kuwasaidia sana...’akaniambia akiwa na maana ya huyo dakitari rafiki wa mume wangu.

‘Ndio yeye ni rafiki mkubwa wa mume wangu, anatusaidia sana, kama kuna lolote tunaweza kumuita yeye pia, lakini huyu ni mgonjwa wako, tutakuwa tukikusumbua wewe .....’nikasema.

‘Sio kunisumbua hilo ni jukumu langu, na ni bora mnisimbue kuliko kukaa kimiya au kumuita dakitari mwingine ambaye hafahamu historia ya huyu mgonjwa....jitahidini sana kufuata masharti, mimi nina imani haitachukua wiki nyingine tatu, kabla hajaweza kusimama tena...’akasema

 ‘Nitafanya hivyo docta..’

*********

Sasa ni mwezi umepita, nipo namuhudumia mume wangu, kila siku nahakikisha namfanyia yale yote muhimu yanayohitajika, tukisaidia na dada mmoja niliyemchukua kama msaidizi wangu kwa ajili ya mume wangu tu, ili yule mfanyakazi wa nyumbani asije kushindwa kazi zake nyingine, kwa kisingizia cha kumshughulikia mume wangu.

Ilikuwa sio kazi rahisi, ikizingatia kuwa mume wangu wakati mwingine alikuwa akitaka kuongea yale yaliyopita, yale yaliyosababisha awe hivyo, na mimi nilishaonywa kabisa kuyakwepa kuyaongea hayo, hadi wakati muafaka utakapofika. Na nikajitahisi sana kufanya hivyo.

Hatua kwa hatua hali ya mume wangu ikaanza kuimarika, japokuwa ilikuwa kama hatua zile za mtoto mchanga,  akaanza kuinua mguu kidogo, lakini alikuwa hajaweza kusimama,lakini kuweza kuinua mguu akiwa amekaa ilikuwa ni hatua kubwa sana, ila wakati wote kigari cha kukukotwa, kilikuwa ndio miguu yake...

‘Kila siku mfanyishe mazoezi, na kuna dakitari maalumu wa mambo hayo, atakuwa anakuja nyumbani kwako mara moja moja, kwa ajili ya mazoezi,....lakini wakati huo unahitajika uwepo karibu ili kumuonyesha unamjali...’akaniambia rafiki wa mume wangu ambaye alijitolea kumuhudumia mume wangu, na ilibidi tufanye hivyo, ili kupunguza gharama, na muda wa kwenda hospitali.

‘Nafahamu huyu ni rafiki yako, na mimi naona uchukue jukumu la kumuhudumia wewe, ..na utanipa gharama zake kila mwezi...’nikamwambia na yeye akakubali huku akitaka shughuli zote hizo azifanya kwa kujitolea, lakini mimi sikukubali, nikamwambia nitalipa.

‘Hii haina shida, nitafanya hivyo, kwa ajili ya urafiki wetu, na kwa ajili ya mapenzi yangu kwako,....’akaniambia.

‘Sijakuambia ufanye hivyo bure, nataka uwe unanipa gharama zote, bila kuficha, sitaki iwe kisingizio cha kukufanya ushindwe kuingiza kipato chako kwa ajili yangu, nafahamu kabisa wewe upo kazini, usije na ajenda nyingine za siri...’nikamwambia.

‘Hamna shida, nitafanya hivyo mpendwa, na itakuwa vizuri, kwani nitaweza kukudhibiti wewe usije ukafanya jambo ambalo utakuja kujijutia...’akasema.

‘Siwezi kufanya hivyo, namjali sana mume wangu...’nikasema.

‘Nashukuru kusikia hivyo...’akasema

Mimi moyoni, nilikuwa na yangu, pamoja na kukubali hilo, lakini nilikuwa natafuta nafasi ya kupata taarifa muhimu, kujua yote yaliyotokea hadi kufikia hatua, hiyo, nilikuwa nimeshajipanga, lakini sikutaka kabisa mume wangu afahamu lolote, kwahiyo nikiwa nyumbani, najitahidi kila niwezavyo, kutokumuonyesha chochote kibaya, na nikawa najitahidi kutokuongea na mtu mwingine,jambo lolote linalomuhusu mume wangu. Na ndio siku hiyo akafika huyo mdogo wa mume wangu, nikaona kuwa moja ya malengo yangu yanaweza kutimia.

Na tulipokuwa peke yangu tukaanza mazungumzo na shemeji yangu ambaye alionekana kutokuwa na amani, ....nikamwambia;

‘Shemeji, nataka tuyafupishe  mazungumzo yetu iwezekanavyo, kwani kaka yako akiamuka natakiwa niwe naye karibu, kwahiyo nakuomba nikikuuliza swali ujitahidi kunijibu kwa ufasaha, bila ya kuogopa....’nikamwambia.

‘Uliza tu shemeji.’akasema.

‘Ninachotaka kukuuliza ni mambo ya kawaida tu usiwe na shaka...’nikasema.

‘Sawa nakusikiliza,...lakini kama ni kuhusu kaka, mimi sijui lolote...’akaanza kwa kujitetea.

‘Usijali,....wewe utaongea tu kile unachokifahamu, sio swala la kesi au swala la kukulazimisha kuongea kitu ambacho hukijui ,ila haya yote nayafanya kwa manufaa ya kaka yako,sizani kama unafurahia hii hali, sizani kama unafurahia kumuona kaka yako akiwa hivyo, na ikaja ikatokea hivyo au zaidi, huwezi jua, ni muhimu tujue tatizo ni nini, ili tuweze kumsaidia....’nikasema.

‘Kwakweli shemeji mimi sifurahi kabisa hii hiyo, kaka amekuwa ni kama mzazi kwangu, wazazi wetu kama unavyowafahamu, hawana mbele wala nyuma, wewe ndiye umeisaidia familia yetu kupitia kwa kaka,sasa naogopa sana kaka sije akaondoka..sijui itakuwaje, japokuwa nimeanza maisha lakini bia yeye nitapata taabu sana,...’akasema.

‘Basi kama unafahamu hivyo ni vyema, tukamsaidia kaka yako, kwani japokuwa kiafya anaendelea vyema, lakini mpaka sasa sijajua ni nini kilichomfanya hadi afikie hatua hii, je ni jambo la dharura tu, au kuna jambo jingine ambalo huenda bado lipo, na huenda akipona atakumbana nalo tena, je kuna mtu alimuhadaa,kama yupo mtu kama huyo, atakuwa akimsubiria, akipona atazidi kumuandama,kwa hivi sasa hawezi kujitokeza kwa vile kaka yako hana chochote cha kufanya..’nikasema.

‘Unaposema hivyo unaonyesha kama unahisi kuwa kuna mtu yupo nyuma ya hata yote, mimi nilijua kuwa ni ajali ya kawaida tu, ambayo anaweza kupatwa mtu yoyote’ akasema.

‘Ndio najaribu kuwaza hivyo, lakini hali kama hiyo, inahitajia mawazo ya watu wengi, hasa nyie ambao mnakuwa naye kipindi cha mchana, kama ujuavyo, mara nyingi tumekuwa kwenye kuhangaika, na kukutana kwetu ni usiku, je huko anapokuwa mchana kutwa, anakuwa na nani, anafanya nini, ndio hilo nataka tusaidiane,kama kweli unamjali kaka yako..’nikasema.

‘Shemeji mimi sio kwamba mchana kutwa nakuwa naye, unafahamu hilo, kwani hata mimi ninakuwa kwenye mishe mishe zangu,....baada ya kumaliza kusoma, na mimi najaribu kutafuta jinsi ya kusimama mwenyewe...japokuwa mumenisaidia sana, nisingelipenda kuwa tegemezi hadi muda huu,....kwahiyo skai sana ofisi kwa kaka,..sipndi nifanye kazi kwenye ofisi yake, kama tulivyowahi kuongea..’akasema.

‘Ni kweli wanandugu mkiwa kwenye ofisi moja mnaweza mkalemaa, mkaleta udugu badala ya uwajibikaji, hata mimi nililiunga mkono wazo lako, na nashukuru kuwa umejitahidi hadi umepata ajira, ila ninachokusisitizia, usilemae sana kwenye ajira za watu, jaribu kuhangaika uwe na ajira yako, ujiajiri,na kuwa na kampuni yako, utaona manufaa yake....’nikasema.

‘Ni kweli shemeji, ndio maana napenda sana kuwa karibu nawe, japokuwa kiujuma nakuogopa, kama vile mwanafuzni anavyomuogopa mwalimu...’akasema

Ni kweli shemeji yangu huyu, amekuwa akiniogopa, ..ni kwa vile nilikuwa mkali sana kwake, sikutaak mchezo, nilimfanya kama mdogo wangu, ili kuhakikisha anabadilika, na kuondokana na tabia ya kudeka,...alikuwa kaishi na wazazi wake, akawa hajielewi, kila kitu anategemea wazazi, nilifanya juhudi ya ziada kuhakikisha hali hiyo inamuondoka, na sasa keshaanza kujifunza kuishi maisha ya kujitegemea.

‘Usiniogope shemeji, nia yangu ilikuwa njema kwako, ..unafahamu, hata kaka yako, angekuwa na msimamo, kama alivyokuwa awali aisingeliweza kuingia kwenye mtgeo kama huo ...nahisi kakutana na  mtu akamlemaza, ...unatakiwa ujue ni nini unakianya, ambacho unafahamu faidia na hasara yake baadaye, bila ya tegemezi..ndio maana nimekuwa hivyo kwa kaka yako, ..huenda hakunielewa, akaona labda nakataa kutimiza wajibu wangu, sivyo hivyo..nataka ajiamini, nataka asiwe lelemama..hakunielewa.’nikasema.

‘Mhh, shemei hapo hata mimi sijakuelewa, kwasababu vyovyote iwavyo, ndoa nayo ina mahitajio yake, huwezi ukaifanya ndoa kama unavyofanya kazi nyingine, siwezi nikakulaumu, ila nahisi kama anahisi humtendei yale wanawake wanavyowatendea waume zao...’akasema , hapo nilitak kupndisha lakini nikaona niende naye taratibu huenda nikagundua jambo.

‘Unahisi nimekosea nini, ...?’ nikamuuliza.

‘Mimi siwezi kukufundisha, maana sijawahi kuoa, ila nahisi kama kuna jambo ambalo linamkwanza kaka, na nahisi nikutokana na wewe, nikutokana na nda yenu, ...kaka huwa hapendi kuniambia mengi, na hapendi sana kuiongelea ndoa yake, ..maana anakupenda sana, ...’akasema.

‘Unavyosema hivyo, ni kama vile aliwahi kulalamika, ukasikia....hajawahi kulalamika mbele yako, kuwa kuna tatizo analipata dhidi yangu?’ nikamuuliza.

‘Shemeji hapana, lakini mimi nimeishi na nyie, kwahiyo mengine nayafahamu, wakati mwingine nilikuwa natamani kukuambia, lakini naogopa, ...’akasema

‘Sasa usiogope, naomba uniambia waziwazi, nitafurahi sana kuyasikia hayo uliyokuwa ukiogopa kuniambia, niambie ukweli shemeji, kwa mfano unaweza kuniambia na mambo gani nilikuwa nayafanya ambayo yanamkwaza kaka yako?’ nikamuuliza.

‘Ukaribu wa mke na mume..mimi naona kama mlijali sana kazi kuliko, ndoa yenu,..nafahamu kazi ni muhimu sana, lakini kazi na dawa,....mimi nimesoma dini, kuwa ndoa ni sehemu kubwa ya starehe kati ya wanandoa, mkishachoka kwenye kazi, mnakutana kama mke na mume, mnasahau madhila yote ya dunia,...inatosha kuwa burudisho kuliko kwenda kulewa,...sasa nahisi kaka alikosa hilo, ndio maana akaona pombe ndiyo starehe yake...’akasema.

‘Hebu niambia ukweli maana umeishi name hapa, ina maana kweli tulikuwa hivyo, ..hatuthamini ndoa, tukawa tunathamini kazi kuliko ndoa,...inawezekana , sikatai, lakini huoni yote hayo yalikuwa kwa amsihali yetu, kwa masilahi yenu pia, kama tusingelifanya hivyo, ...tusingelikuwa hapa,..wewe hulioni hilo?’ nikamuuliza.

‘Ni kweli shemeji, lakini nakumbuka ulinifundisha kuwa ili ufanikiwa , inabidi uwe na mipango, uwe an ratiba ya kila siku, ukiwa na mipango, ukawa na ratiba ya kila siku, hata ukwia na shughuli nyingi kiasi gani utazimaliza kwa wakati..ndoa ni moja ndani ya ratiba ya wandoa, sasa kwanini isitendewe haki yake, mimi ndivyo nionavyo, sio kwamba nalaumu, sio kwamba nasema mumekosea, ila najaribu na mimi kushauri tu...’akasema.

‘Kwahiyo wewe unahisi tatizo la kaka yako limeanzia ndani ya ndoa, sio nje...?’ nikamuuliza.

‘Inawezekana kuna tatizo nje, mimi na wewe hatulijui, lakini kwa uoni wangu mdogo, kama wanandoa watajitahidi kuondoa matatizo yao ndani ya ndoa wakawa na amani na upendo, basi hali hiyo ingewawezesha kutenda mambo mengine ya nje, kwa amani, kwasababu, kwanza huyo mtu, atakuwa katuliza kichwa chake, hana msononeko...'akasema

'Pili, kuna baraka za mungu, na tatu, mnakuwa kitu kimoja, na umoja ni nguvu, ...sizani kama kaka angelidanganyika kirahisi hivyo, kama wewe nay eye mngelikuwa kitu kimoja..., kama kweli kuna mtu kama huyo nje kama ulivyodai.....mimi ndivyo nionavyo shemeji’akasema.

‘Shemeji nimekuelewa sana, na nashukuru kwa kuwa mkweli kwangu, sasa mimi nimekubali kuwa huenda nilikuwa nafanya makosa,na kwahiyo nitajitahidi sana kujirekebisha, nitahakikisha natimiza wajibu wangu,...japokuwa mimi nilifanya hivyo kwa nia njema kabisa, lakini huenda nilivyotaka mimi watu hawakunielewa, na itakuwa ngumu kueleweka...kwa minajili hiyo basi, naona kwa masilahi ya wengi, nijirudishe nyuma, nifanye mnavyotaka, nifanye wanavyotaka wengi, kwangu haina shida...’nikasema.

‘Lakini shemeji sijasema ubadilike na kuacha juhudi zako ya kazi,kazi ni msingi wa maendeleo  ....mimi nimetoa kama ushauri, kwa jinsi nionavyo mimi,  kuwa msijichoshe sana kwenye kazi, jaribu kujiliwaza kama mke na mume, tokeni pamoja, tembeeni siku moja moja pamoja, kazi zipo na hazitaisha,...kwanini mjichoshe saana,...huenda mimi nimekosea, lakini nimetoa yale ninayoona moyoni...’akasema.

‘Ni kweli, ni mekuelewa, na ulivyosema ni muhimu sana, hata mimi nimeliona hilo ....sasa sikiliza, pamoja na hayo, kuna mambo nataka kukuliza, baadhi nitakuuliza hapa, lakini mengina nahitaji muda maalumu wa kuongea na wewe, sio hapa...’nikasema

‘Kuhusu kaka?’ akaniuliza akionyesha wasiwasi, na nilimuona akiangalia , kama vile kaona kitu nyuma yangu, mimi sikujali, maana namfahamu sana shemeji yangu huyu, niliendelea kumkazia macho. Nikasema;

‘Ni mambo ya kawaida, kuhusu kaka yako, kuhusu mimi, kuhusu huyo ambaye hajulikani,....nahisi kuna mtu mwingine kati yetu, sijawahi kuwaza hivi kabla, ila nimelazimika kutokana na haya yaliyotokea, ..sijawahi kumshuku kaka yako vibaya, hata siku moja, na hata sasa hivi sijaamini kuwa kuna mtu katikati yetu....lakini kwa vile watu wanasema, kwa vile hali kama hii imetokea, inabidi na mimi nianze kuwa na mashaka ..’nikatulia kidogo.

‘Ingawaje mimi sipendi kufuata fuata sana watu, huwa nina tabia ya kuamini, wale ninaoona ni marafiki zangu. ...Mume wangu namwamini sana, halikadahalika wewe na rafiki zangu..lakini naona kuna kitu kinachoendelea kwa siri, na kinanitia mashaka. Kuna sintofahamu inayoendelea, na hiyo sintofahamu inanitia mashaka, ...mimi sipendi kukaa na mashaka, sio kawaida yangu, ndio maana nawaamini watu, ila ikitokea hali kama hii, inabidi nifanye jambo.....’nikasema

‘Unataka ufanye nini shemeji..mbona ni ya kawaida tu, hayo yaliyotokea kwa kaka ni ajali tu, kama kuna mengine, ni ya kawaida tu, yataisha, sioni kwanini mkosane na kaka , shemeji kaka yangu anakupenda sana..’akasema kwa unyonge huku akitamani kunipigia magoti.

‘Sijasema kaka yako hanipendi, na wala sina mawazi hayo, na sijawahi kufikiria hivyo, ila ninachotaka ni ukweli...na nisipoambwa ukweli, kutoka kwako, kutoka kwa rafiki ya kaka yako, kutoka kwa rafiki yangu, ni nani mwingine ataniambia ukweli. Na kama mnafahamu ukweli mkanificha, nitajua kuwa ninaishi na watu wanaojifanya ni marafiki kwangu kumbe sio, kumbe ni wanafiki.....na kama ni hivyo, ina haja gani ya kuishi na watu kama hao, ambao nawasaidia, lakini hawataki kunisaidia mimi...’nikasema na hapo nikamfanyashemeji yako aniangalie kwa macho yaliyojaa uwoga.

‘Sasa sikiliza, mimi ninakupa wewe muda wa kuyatafakari haya kwa makini,  nitaongea na wewe tena kesho, lakini sio hapa nyumbani, nataka tuyaongelee haya na mengine ofisi kwangu,....’nikasema.

‘Kuhusu nini tena shemeji..mimi naona kama tumemaliza, sina jingine ninalolifahamu’akalalamika.

‘Nimefurahia sana maongezi yako ya leo, hatujawahi kukaa na kuongea hivi, ukaniambia ukweli kutoka moyoni mwako,,..nimefurahi sana, na wakati wote ninakuona kuwa ni mtu mwema, unayejali, wale wanaokujali, nimefurahi sana...’nikasema.

‘Nashukuru sana shemeji, kama umenielewa, na mimi ninakujali sana shemeji zaidi ya unavyofikiria wewe, sitaki wewe na kaka mkosane,ningelifurahi ninawaone mnaishi kwa raha wakati wote....’akasema.

‘Kama ni hivyo basi, kama kweli hayo yanatoka moyoni mwako,naomba tusaidiane kwa hili.....unisaidie ili nimsaidia kaka yako, ili nifanya yale yanayostahiki kwa kaka yako, kwanza nimekubali ushauri wako, naahidi kuwa nitabadilika na kuwa mke mwema, au sio....?’nikasema na nikawa kama namuuliza.

‘Lakini shemeji wewe ni mke mwema, kila mtu anafahamu hilo, hata wazazi wangu wanakusifia sana..’akasema na mimi sikujali maelezo yake, nikaendelea kusema;

‘Pili, nataka kuisafisha nyumba yangu, nataka ndoa yetu iwe ndoa safi, siyo na kashifa,hili ni urithi kutoka katika fanilia yangu...kashifa mbaya, haitakiwi kwenye familia yetu,..na kama kumejitokeza kitu kama hicho, nataka tukiwahi kabla hakijafika mbali,...na nilitarajia rafiki yangu angenisaidia hili, lakini hayupo, lakini hakijaharibika kitu, ...’nikatulia kidogo.

‘Ila nahisi, kuwa wale niliowapenda kama marafiki, wale nilijitahidi kadri ya uwezi wangu ....wawe ni marafiki zangu huenda....sina uhakika, ...huenda wananigeuka. Hilo sitalikubali..sasa nataka nianze kuwatambua marafiki zangu wa ukweli ni akina nani.’nikasema.

‘Hapana shemeji, hakuna aliyekugeuka huenda hujatuelewa tu, wengi tunaishi kutokana na ushauri wako, hasa mimi najitahidi sana kuishi kama ulivyonishauri na kweli nimefanikiwa sana, huenda hata wenzangu wanafanya hivyo, kwa nia njema kabisa.....’akasema.

‘Kwanini nisiwaelewe, kama mtaniambia ukweli...unafahamu shemeji, huoni leo umeniambia ukweli, kwani nimekasirika?’ nikamuuliza

‘Hujakasiriak shemeji...’akasema.

‘Sasa kwanini watu hawanielewi, kwanini wasiniambie ukweli, kabla hawajaamua kufanya makosa, ...haya tuseme wameteleza, kwanini hawatubu madhambi yao kiukweli, na nijuavyo mimi  kutubu makosa yako kiukweli ni kusema ukweli, na kwenda kwa yule uliyemkosea ukatubu mbele yake, si ndio hivyo, shemeji yangu maana wewe ni muumini mzuri wa dini,....’nikasema nikimwangalia moja kwa moja.

‘Kwahiyo mimi ninavyoona kwasasa, na nitambue hivyo, ni kuwa kuna kosa limeshafanyika, ...basi kama ni hivyo,nimabiwe ukweli, ..mbona wote mnakuwa mabubu ninapowauliza hivyo, hii inaonyesha nini, kama sio unafiki,...kwa hali kama hiyo mnatarajia mimi nifanye nini,....msione ajabu tukitengana, nasema ukweli kama hamtaniambia ukweli sasa tutatengana....’nikasema na mara shemeji yangu akasimama na ghafla akapiga magoti.

‘Shemeji usiseme hivyo, mtatengana na nani shemeji una maana unataka kutengana na kaka, hapana shemeji usifanye hivyo, mimi nipo chini ya miguu yako shemeji, nipo tayari kufanya lolote unalotaka, ilimradi tu usimuache kaka yangu, niambie nifanye nini shemeji...’akasema huku akinipigia magoti, sikutarajia tendo hili kutoka kwa huyu mdogo wa shemeji yangu,..na mara simu yake ikalia; Mimi nikasema kwa ukali.

‘Sipendi mtu kunyongea mbele yangu, mimi sio mtu wa kupigiwa magoti, usifanye hivyo hata siku moja mbele yangu, nilikufundisha nini, ....nilikufundisha kuwa uwe mjasiri, huo sio ujasiri, huo ni unyonge, huo ni utumwa, usikubali kuwa mnyonge, usikubali kuwa mtumwa wa mwenzako, mtu wa kupigiwa magoti na kuombwa ni mungu peke yake..unajidai kuwa umuumini wakati matendo yako yanakusaliti.....inuka haraka....’nikasema, na yeye akasimama kwa haraka na kufuta futa majani yaliyoganda kwenye suruwali yake.

‘Pokea simu yako,..’nikasema huku nikiwa nimekunja uso, kama vile nipo ofisini, na hapo nikakumbuka, ..nikakunjua uso wangu na kutabasamu, tabasamu la kubandika.

‘Ni docta, rafiki yake kaka, nilimwambia nitapitia kwake, naona kaona nimechelewa ndio maana kaamua kunipigia simu,..’akasema huku simu ikiendela kunilia, na akawa haipokei

‘Ongea naye tu sasa, mwambia unakuja,....’nikasema na yeye akasogea pembeni kidogo, na waliongea kwa muda mfupi, baadaye shemeji akanisogelea na kusema;

‘Haya shemeji ngona mimi niende,,nakwenda kwa huyo docta, na sizani kama nikitoka huko nitafika hapa nyumbani, ...., sijui naye ananihitajia kwa jambo gani maana kaniambia nisikose kwenda kwake...’akasema akionyesha kutukupendezewa na hali iliyotokea

‘Ukiongea naye, usimwambia kuwa tulikuwa na maongezi mimi na wewe, na pia kuwa nimekuambia tukutane na wewe kesho,unasikia, usimwambia lolote kuhusu maongezi yetu haya, kama kweli unamjali kaka yako, ..vinginevyo, utakuja kujuta, maana hujui ni nani adui wa kaka yako,hujui adui wa familia yetu hii,....mimi nasema hivyo kama mke wa kaka yako, ambaye namjali sana kaka yako kuliko hawo watu wengine wa nje wanaojifanya wanamjali kaka yako....’nikasema.

‘Ni kweli shemeji, lakini huyo docta, ni rafiki mkubwa na wa karibu wa kaka, na sio mtu mwingine wa  nje na nijuavyo mimi, yeye amekuwa akimsaidia sana kaka, wakati wote, ....na yeye ndiye amemfanya kaka, asitaabike zaidi, .....’akasema.
‘Kutaabika zaidi kwa vipi, kwani kaka yako alikuwa akitaabika !?’ nikamuuliza kwa mshangao.

‘Kama nilivyokuambia shemeji, kwa mtizamo wangu , kaka alibadilika na kuwa mlevi, ili kuondoa mawazo, akawa mtu wa kunywa kunywa pombe, na kila siku akawa anazidisha ...labda akiona kakwazika kwa hili na lile....mimi sijui zaidi...’akasita kidogo, halafu akasema.

‘Kuna siku niliamua kumuuliza akaniambia ni maswala yake binafsi, na siku moja nikiwa na rafiki yake huyo akaulizwa na kubanwa sana na maswali, akasema ni mambo yake ya ndoa hayamuhusu mtu mwingine..na kumbuka pia aliwahi kuniambia ni subiri nioe, nikioa, nitakuja kujua kwanini anafanya hivyo...nafikri shemeji wewe unafahamu zaidi kuliko mimi, ngoja niondoke,.....docta ananisubiria.....’akasema na kuniancha nikiwa nimeshikwa na bumbuazi.

‘Sawa lakini kumbuka hatujamalizana na wewe, nataka uje kesho ofisini kwangu, muda wa saa nne, tukutane huko, nataka uje ukiwa umekamilika, tayari kwa kuniambia ukweli wote unaoufahamu kuhusu kaka yako, ....nataka ukweli ili nisije nikachukua uamuzi ambao wewe na wengineo hawataupendezewa nao....’nikasema huku nikisimama kuondoka.

‘Kama hamtaniambia nikachukua jukumu la kuutafuta mwenyewe, ...sizani kama mtanielewa, ni bora mniambie ukweli ili mimi nipate muda wa kutafakari nah ii itanisaidia kutokukimbilia kuchukua maamuzi ya haraka, na huenda nikasamehe, kutegemeana na kosa lenyewe,..lakini kama mtanificha, nikaja kugundua mwenyewe..sitamsameeh mtu, hilo naahidi...nitachukua uamuzi wangu, ninaoujua mimi,....ambao huenda utaumiza wengi...mnanifahamu nilivyo...haya unaweza kwenda...usijali shemeji, wewe ni mtu mwema, basi endelea kuwa mwema....’nikasema

Shemeji yangu aliondoka huku akiwa kanyong’onyea,..mpaka nilimuonea huruma, lakini niliona bora iwe hivyo, hiyo ndio njia pekee ya kupata ukweli, nikaingia sebuleni,na kukaa kwenye sofa huku nikiegeemza kichwa kama mtu anayetaka kusinzia, sikuwa na mawazo ya kuingia chumbani kuangalia kama mume wangu bado kalala, nilichokuwa nacho kichwani ni hayo maneno ya huyo shemejii yangu:

‘Ni kweli, lakini huyo ni rafiki yake wa karibu, na sio mtu mwingine wa  nje na nijuavyo mimi, yeye amekuwa akimsaidia sana kaka, wakati wote, ....na yeye ndiye amemfanya kaka, asitaabike zaidi...’

‘Asitaabike zaidi, ina maana yote niliyofanya kwa mwenzangu ni kazi bure...’nikajiuliza.

‘Na kwanini asiniambia....’nikazidi kujiuliza

Wakati maneno mengine yakiendelea kujirudia akilini na kuzidi kunipandisha hasira, mara nikasikia sauti za watu wakiongea nje, .nikainuka na kuangalia nje....

Nikashituka kutoka kwenye lindi la mawazo, kwanza nilitaka kukimbilia chumbani kuhakikisha kuwa mume wangu bado kalala, ..., lakini haikuwa na haja kwani nilipochungulia nje kwa kupitia dirishani nilimuona yule msaidizi wangu akiwa anasukuma kile kigari cha mume wangu, na mume wangu akiwa kakaa na alikuwa kama kasinzia, lakini hiyo ilikuwa ni dalili, kuwa alikuwa na mawazo.

Kumbe msaidizi wangu alikuwa amerudi, na kuingia ndani akamkuta mume wangu keshaamuaka, na wakatoka naye nje,inaonekana walikuwa wanazunguka huku na kule na kigari....ndivyo anavyopenda mume wangu, hataki kukaa sehemu moja kwa muda mrefu.

Kwanza nikaingiwa na wasiwasi, nikijiuliza huyu mtu alitoka muda gani, isije ikawa,walifika hadi kule bustanini, wakasikia maongezi yetu na shemeji yangu,kitu ambacho muda wote nilikuwa nikikikwepa, nikaona nithibitishe hilo, nikafungua mlango na kutoka nje,....

Mume wangu aliponiona, kwanza aliniangalia kwa macho yaliyojaa huruma, nikatabasamu, lakini yeye hakutabasamu kama ilivyokuwa kawaida yake, ...nikamuona akikunja uso kama vile mtu anayehisi maumivu, na kabla sijasema neno akauliza;

‘Mdogo wangu kakukosea, nini.....’ nikagwaya, na simu ilikuwa tayari mkononi tayari kumuita dakitari.

NB: Kwa leo inatosha ....eeh, two-in-one, zawadi maalumu hii.


WAZO LA LEO:Katika maisha yetu ya ndoa, na katika maisha yetu ya kila siku, tujifunze kuwa wakweli, kila mmoja amwamini mwenzake ....kwani, ukweli wakati wote, ni kinga ya uhasama,...japokuwa kuna wakati mwingine inatulazima kukwepa kusema ukweli kwa wakati fulani, ili kukwepa madhara...ikiwa ni kwa nia njema, lakini kwa vyovyote iwavyo, tujifunze kuwa wakweli kwa wenza wetu, ili kujenga uaminifu, 
Ni mimi: emu-three

No comments :