Mzee Adui aliinuka kwenye kiti chake cha enzi huku akiwaza
kuhusu hiyo taarifa aliyopewa, akamwangalia
yule askari aliyemletea hiyo taarifa kwa muda mrefu na macho yake makali, hadi
yule askari akaingiwa na waiwasi. Yule mzee akilini mwake alikuwa akimuwazia
huyu askari, ni kweli anamfahamu sana kama mmoja wa vijana wake anaowatumia kwa
upelelezi, na mara nyingi akimletea taarifa zake huwa ni za ukweli, lakini kwa
mtizamo wake wa harakaharaka, hilo jambo aliloambiwa haliwezekani,…akatabsamu
na kusema;
‘Una uhakika
kuwa kweli kuwa huyo kijana wao, kauwawa, …?’ akauliza tena swali hilo , hiyo
ilikuwa ni mara ya tatu, anauliza swali kama hilo hilo, na yule askari akawa
anatoa maelezo yale yale, aliyokwisha kumuelezea mwanzoni, kwa jinsi
alivyosikia na jinsi alivyofuatilia na hata kuweza kuongea na maaskari wahasimu
wao, ambao waliandamana kwenye huo msafara.
‘Mzee,mimi
nimeongea mwenyewe na mmoja wa maaskari wao, ambaye aliongozana na huyo kijana,
yeye ndiye alikuwa kiongozi, baada ya huyo kijana wao, wanayemuita jemedari
wao. Kwahiyo taarifa yake tunaipa uhakika kuwa ni ya kweli…’akatulia yula
askari kumpa nafasi mzee wake kuyaweka hayo maelezoakilini, halafu akaendelea
kutoa maelezo;
‘Kama
unavyomjua jamaa huyo, huwa hapendi kushindwa, na siku hiyo ya tukio walikuwa
katika moja ya mafunzo yao, maana siku nzote siku hizi wana mafunzo magumu,
wanatuiga. Walipofika pale kwenye mto, kwa maelezo ya huyo askari, wakidondosha
moja ya mzigo wao, uliokuwa na vifaa vyao muhimu, na ilihitajika lazima mzigo,
huo uokolewe.
Mwenzetu
huyo akaamua kujitosa,…kama unavyojua mzee, kwenye ule mto kuna sehemu ambazo
haziingiliki, hata kama ungelijua kuogole, kwasababu ya matope, unaweza ukaona
maji juu, kumbe chini ni matope. Wenzake waliogopa,….walijaribu kumshauri kuwa
ndani ya ule mto, huwezi kuingia kipindi kama hiki, kwani pia mamba wengi wana
njaa, hakusikia…’akasema
‘Aliingia
kufuata huo mzigo tu, au kulikuwa na kitu gani kingine, maana lazima kuwe na
jambo kubwa ,lililomsukuma kuingie humo ndani ya mto, huo mzigo ulikuwa na vitu
gani ambazo vilimfanya huyo kijana ahatarishe maisha yake kiasi hicho,
ikizingatia kuwa yeye ni jemedari wao, na walikuwepo majasiri wengine ambao
wangeliweza kuifanay hiyo kazi, au alikuwa akitaka kumuokoa nani?’ akauliza
yule mzee kwa mashaka.
‘Baada ya
kupata hiyo taarifa hata mimi niliwaza sna hilo jambo, kuwa inawezeka, huenda
alikuwa akitaka kumuokoa yule mwanamke aliyetakiwa kuuliwa kwasababu hakutakiwa
hapa kwenye ardhi yetu, lakini sehemu hiyo ni mbali na kule alipotupwa huyo
mwanamke, …au nikiwaza kuwa huenda alikuwa akitaka kuvuka kwa ujanja ili aje
sehemu hiyo lakini akashindwa…kwa maana likuwa akikaidi amri ya wakuu’akasema
huyo askari.
‘Kwahiyo
huyo askari wao anasema alihakikisha akiliwa na hawo mamba,..mbona hiyo haiji
akilini,?’ akauliza huyo mzee huku akitabasamu kwa dharau, na alisema hivyo
akidhihaki kwani kwa imani yao watu wanaostahili kuwa ndani ya eneo takatifu
hawawezi kuliwa na mamba, labda iwe kwa hukumu maalumu.
‘Wanasema
alipiga mbizi , akijua kuwa kuna maji mengi, akazama moja kwa moja,hakuonekana
akiibuka tena, …..kwani sehemu aliyoingia ilikuwa na matope, na wanahisi
alipofika chini, alishindwa kutoka , tope litakuwa lilimzidi nguvu,….na wenzake
walitafuta vifaaa vya kumuokoa, kwa kuingia na kamba, na wakajaribu kutafuta
sehemu hiyo aliyoingilia, hawakuona kitu na wakati huo huo, mamba walishafika
eneo hilo, hakuna angeliweza kufanya lolote…’akasema huyo aaskari.
‘Mamba hao
hawakuonekana wakimla huyo kijana?’ akauliza mzee
‘Wanasema
waliona mamba wakigombea kitu,….lakini hakuonekana moja kwa moja kuwa ni yeye,
ila vipande vipande vya nguo yake vilionekana baadaye vikielea kwenye maji, na
ndipo, wakawa na uhakika kuwa keshaliwa na mamba, na ikabidi watoe taarifa kwa
wakuu wao…’akasema
‘Kama hiyo
ni kweli, hilo ni jambo muhimu sana, na tutalitumia kuwaondoa hawa watu , na
pia kama keshakufa, ina maana yule malikia anahitajika kuondolewa kwenye hiyo
familia haraka, na anahitajika kuolewa na jemedari mwingine, ..’akasema kwa
sauti na kwa kimoyomoyo akasema;
`Na kijana wangu atakuwa na nafasi kubwa ya
kumuoa,….malikia hastahili kuishi tena kwenye hiyo familia..labda asiwe huyo
malikia tuliyebashiriwa.’akasema yule mzee, huku akiinuka kwenye kiti chake na kuichukua fimbo yake,
kuonyesha kuwa anataka kuondoka. Yule askari akawa anasubiri amri nyingine yoyote.
‘Ngoja
nikawaone wenzangu, kwani hili ni jambo kubwa sana, lakini …..mbona sijasikia
mlio wa msiba, sijasikia wapiga parapanda la msiba, hii inaashiria kuwa bado kuna utata, hebu
fuatilia kwa makini, nataka nipate taarifa zote toka ndani ya familia yao, ili
tujue kuna nini kinachoendelea….’akasema huku akitembea kuelekea makao yao
makuu. Na yule askari akaondoka, kutii hiyo amri.
Mzee
alipofika alikutana na washauri wake na baadaye wakakubaliana kuitisha kikao
cha dharura, na wazee mbali mbali walipofika, akaanza kuwaelezea nini
kilichotokea;
‘Wazee
wenzangu sijui kama mumeisikia hiyo taarifa kuwa kijana wa asimu wangu huenda
kaliwa na mamba…’akasema na wenzake
wakashituka kwa taarifa hiyo, na wengi hawakukubaliana na hiyo taarifa, kwani
kiimani zao, mtu analiwa na mamba kama ni mtu mbaya, au awe amehukumiwa. Wao
wanaamini kuwa mamba hawo hawawezi kumla mtu ambaye anastahili kuwa miongoni
mwa watu wa eneo takatifu.
‘Hii
inaashiria kuwa huyo kijana hakustahili kuwa miongoni mwa watu wa sehemu yetu
takatifu, toka lini mkasikia mtu wa nyumba hii takatifu akaliwa na mamba…hii
nilishawaambia kuwa hawa watu hawastahili kuishi kwenye nyumba hii….wanatakiwa
wafukuzwe haraka wasije wakatuletea mabalaa mengine…’akasema na wenzake wakawa
wametulia.
‘Mimi bado sijamini
…hiyo taarifa bado ina utata, kwani kama ingelikuwa ni kweli, tungesikia,
hatujasikia baragumu la msiba, hatujaona wenzetu wakikutana kwa ishara ya
msiba, na ikizingatiwa kuwa huyo jemedari, mbona vikosi havijawekwa kwenye
tahadhari, msiba haufichiki, tumefanya upelelezi wa kutosha kuthibitisha hilo?’
akasema mmoja wa wazee.
‘Wewe
unawajua hawa wenzetu, lengo lao ni kupoteza muda, ili wajipange vyema,
hawawezi kuiweka hiyo taarifa hadharani mapema hivyo, lazima kwanza wawe
wameshapanga mambo yao vyema, na huenda bado wanatapatapa kumtafuta, lakini mtu
ukishaingie pale na kukutana na hawo mamba, unafikiri nini kitafuata. Mamba
hana urafiki na binadamu, na ikizingatia kuwa kipindi hiki ni cha njaa sana kwa
mamba. Na pia huenda wanajipanga, ili wamchague kijana mwingine kushika nafasi
yake….’akasema huyo mzee.
‘Sasa
tufanyeje, maana kama ni kweli tunatakiwa kujiandaa kwa hatua nyingine,….pia
tujue kuwa malikia bado yupo kwenye miliki yao, kama tukio hilo limetokea,
malikia anatakiwa atolewe na kuwa huru, kwa maamuzi mengine ambayo , yatatokana
nay eye mwenyewe kumkubali mtu mwingine?’ Akauliza mzee mmoja.
‘Kwanza
tunahitajika kuwa na ujumbe maalumu, ujumbe huo utakwenda kutoa rambi rambi,
lakini tukiwa na lengo la kuchokonoa, ili hili swala lijulikana na kama
walitaka kulificha wasipate nafasi hiyo tena. Tukifika tunafika kama watu walio
na uhakika na taarifa hiyo, na kutoa rambi rambi zetu, na wito wa kumpata
mrithi wa kijana wao, na hapo hapo tutahitaji huyo malikia atolewe kwenye hiyo
familia haraka iwezekanavyo’akasema huyo mzee.
Baada ya
mjadala huo ujumbe ukaundwa, ukiongozwa na mzee mwenyewe, na waliondoka hapo
haraka kuelekea makao ya wahasimu wao, ili wakitoka hapo waelekee nyumbani kwa
mzee hasimu wao, kumpa pole.
*******
Huku kwa
mzee mwingine taarifa hizo zilikuwa zilikfanyiwa kazi, na moja ya makubaliano
ni kuhakikisha kuwa taarifa hizo hazifiki kwa mahasimu wao. Kwahiyo mambo
mengine yalikuwa yakiendelea kama kawaida, huku kikosi maalumu kikuwa
kinafutailia ukweli wa jambo hilo.
‘Mimi nina
uhakika kijana wetu bado yupo hai,ila kuna sehemu ka kwama. Najua vyema
inavyokuwa pale hawo mamba wanapokula mtu, nimefuatilia kwa amkini, sikuona
dalili yoyote’akasema mmoja wa wazee ambaye anaaminika sana, ni mtaalamu wa
mamba na dawa za kutibiwa watu walijeruhiwa na mamba.
‘Kwa mtizamo
wako, hata huyo mwanamke aliyetupwa siku ile, hakuwa ameliwa na hawo mamba?’
akaulizwa.
‘Ndilo jambo
la kushangaza, maana hawo mamba wakila mtu , wanajulikana, na hali ya hapo
mahali inakuwa na damu , kwa sababu mara nyingi wanakuwa wakigombea ile nyama
yake….hakuna dalili kama hizo, hii ni kuashiria kuwa kijana anaweza kanasa
mahali, au yupo mahali…’akasema huyo mzee.
Vijana alio
kuwa nao kwa kazi maalumu tuliyowatuma, wamerudi, na wanasema mwenzao, jemedari
wao, walimuona kabisa akizama,…hii inanipa amshaka kidogo,kwanini yeye aliamua
kujitosa sehemu ambayo wengi tunaifahamu kuwa haifai kuingia…?’ akauliza mzee
mmoja.
‘Ajali
ikipangwa haina kinga,mimi naona tufanye
uchunguzi wa kina, …maana tunavyojua, wahasimuwetu wakipata hii taarifa, basi
watakimbiliakuchukua hatua, na kama ujuavyo malikia, yupo mikononi mwetu, na
ikitokea taarifa kama hii, anahitajika kuwa huru,….anatakiwa tumtoe, aiswe
mikononi mwetu tena,…’akasema mmoja wa wazee wa sheria.
‘Lazima
tuhakikishe taarifa hii haifiki kwao,na kama ikifika kwao tujue jinsi gani ya
kujihami, ….tuhakikisha hakuna
makundi,hakuna vikao, shughuli zote ziendelee
kama kawaida…’akasema mzee mkuu wao, huku akiwa na huzuni moyoni.
Mzee huyo
alipoletewa taarifa hiyo kwa mara ya kwanza , hakuamini, lakini siku
zilivyozidi kwenda mbele, alihisi kuna jambo baya limetokea, na kama limetokea
kweli, alishajua kuwa huenda mwisho wake wa kuishi kwenye sehemu takatifu
umefika,lakini myoni alijipa moyo, akijua kuwa kijana wake ndiye stahili la eneo
hilo, bila yeye sehemu hiyo itaendelea kuwa na uhasama.
‘Lazima
lifanyike jambo…’akasema na akazamiria kusafiri hadi eneo lao walipotokea,
..mara nyingi huenda huko anapokwama,na kabla hajaondoka ikabidi aitishe hicho
kikao kupata ushauri wa wenzake, na kikao kilipoisha, wakawa wanatwanyika,
lakini kabla ahwajatawanyika waliona wajumbe wakiongozwa na mzee adui, wakija
maeneo ya kwao.
‘Hawa
wameshapata taarifa?’ mmoja wao akauliza na wazee wote wakaduwaa wakisubiri huo
ujumbe umekuja na taarifa gani.
NB Haya hayo
ni mambo ya wazee wetu, tunahitajika kuyakumbuka, huenda katika destruri na
mila zao tunaweza kujifunza kitu.
WAZO LA LEO: Tuwaenzi wazee wetu, kwani bila wao,
hali hii tuliyo nayo sasa isingelikuwepo , je kama nchi kuna utaratibu gani wa
kuwaenzi kwa vitendo hawa wazee, …hasa katika kupatiwa huduma muhimu, za
kiafya, makazi na haki zao. Ukiangalia maeneo mengi ya kijijini, wamebakia
wazee, hawana mbele wala nyuma, hatuoni kuwa tunajilaani wenyewe? Tuwaenzini
wazee wetu kwa vitendo,na sio kwa kauli za mdomoni tu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment