Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, April 6, 2010

Mtu akiumwa na nyoka...!

‘Jamani ajali muisikie tu, imenifanya hata kupanda gari nijiulize mara mbili tatu. Kilichotokea siku ile ilikuwa kama ndoto’ Huyu alikuwa dada yangu akielezea ajali iliyomkuta.


Siku ile tulikuwa tumeenda kwenye kikao nje ya ofisi, na tuliporudi usafiri ukawa shida kweli. Siunajua tena mabosi waliondoka na magari yao, sisi ikabidi tuanze kuhangaika na madaladala, nina imani kabisa kama mabosi wangeamua kutuchukua kwenye magari yao, kila mmoja akabeba wawili-wawili tungeondoka wote, lakini kila mmoja alidai kuna mahali anapitia, siunajua tena walitaka kwenda kuzimua!

Mvua ikawa imesababisha mengi, usafiri ukawa wa shida, gari likija ni wale wenye nguvu ndio wanaopata nafassi ya kuingia, wengine wakawa wanarukia madirishani, yaani ni mchafukoge. Sisi akina mama na nguo zetu ikawa mtihani, inabidi ujibarague, lakini ilifikia mahali kila mmoja akajisahau kuwa kavaaje, gari likija ni kusukumana tu. Lakini asilimia kubwa tukawa bado hatujapata gari. Na wakati tumekata tama likatokea basi moja, likasimama. Hapo nami nikabahatika kuingia na bahati nzuri nikapata kiti.

Gari lenyewe likawa lakusukuma, likaondoka huku nikiwa na mashaka, kwani hata huyo dereva wake inaonekana ni hao wanaowaita dereva wa siku au `day-worker’. Alikuwa akilikimbiza gari hata pasipo na sababu, wakati mwingine ilibidi akatishe njia na kuingia kusipo na barabara, kukatisha njia, vichochoroni …jamani!

Tulifika sehemu kuna foleni ndefu, hapo tulisimama karibu saa nzima, magari yakawa yanaondoka kidogokidogo, kwasababu foleni ni ndefu. Dereve wetu kama kawaida yake akaanza utundu, anatoka kwenye foleni na kuingia njia ya magari yanayokuja, upande wa pili anaendesha hadi akifika sehemu ambapo anaona gari linakuja mbele anaomba magari yaliyopo kwenye foleni anaingia kwenye foleni, tunasogea mblele. Alifanya hivi karibu mara tatu, ya nne ikawa mbaya. Alitoka kwenye njia yake akaendesha kwa kasi, akafika kwenye barabara inayokatisha kuingia, kumbe kulikuwa na gari linakatisha. Na lenyewe lilikuwa likija kwa kasi. Hamadi,…nilichosikia hapo ni mlio wa ajabu, na mara tukasikia tunapaishwa na …..

Nilijiona nipo kwenye ndoto, nilijaribu kufumbua macho kuchungulia lakini macho yakawa hayafumbuki, lakini nilihisi nipo kwene gari, na nilichungulia kwa juu nikaona madirisha ya viyoo yapo mbali ajabu, na mvua ya mawe, na mawe yenyewe kama kokoto yakawa yanatudondokea. Niliinua mkono ili nijifunike na begi nililokuwa nalo, lakini mkono haukusogea. Kitu cha ajabu nilichohisi ni watu kunitumia mimi kama ngazi wananikanyaga na kurukia juu kule ninapoona kwa mbali, nilihisi ni dirishhani, lakini dirisha hilo nililiona kwa mbali ajabu.

Mara akili ikaniruudia na nilishangaa kujiona nipo peke yangu. Moshi ulikuwa umetanda sehemu zote za gari, kiaso kwamba nilikuwa sioni nini kilichopo mbele yangu. Wazo la kwanza nilijaribu kujiinua ili kuona kuwa kweli nipo mzima, kwani kumbukumbu za kuwa tumepata ajali zilshanijia. Nilipoona hakuna sehemu iliyovunjika nikajitutumua kuinuka. Nikahisi kama nipo kwenye kidaraja Fulani, manake miguu ilikuwa imekanyaga sehemu ndogo tu, na nikikosea naweza kuzama chini, na huko chini sikujua kuna umbali gani, lakini nilihisi kuna maji. Je tupo kwenye mto, niliwaza bila jibu, Akili ikanijia kuwa nipige kelele. Na kweli kelele ikanisaidia, kwani mara niliona watu wakinyosha mikono kupitia dirishani wakaniambia nikamate ile mikono ili wanivute kwa nje.

Kwanza wazo la wezi likanijia kichwani, je hawo niwasamaria wema au ni wezi. Nafikiri walinielewa wakasema kuwa nisiwe na wasiwasi wao ni waokozi wema. Nikanyosha mikono na mara nikawa naelewa hewani huku nikivutwa kwa juu. Kumbe gari lilikuwa limelala upande kwenye mtaro wa maji machafu, na ile mvua ya mawe ilikuwa sio mvua ni viyoo vilivvyovunjika ndivyo vilikuwa vikiniangukia vilikuwa vimesagikasagika. Nilipotolewa nje wazo langu kubwa lilikuwa kukimbia, lakini watu walinishika barabara. Nikabakia kupiga kelele, sijui ni kwanini.

Jamani mpaka nafikishwa hospitali sikujua kuwa nimeumia, nilijiona mzima kabisa. Ila kila muda uliokuwa ukipita ndipo maumivu ya mwili yalivyoanza kunijia, Na mara mwili ukaanza kuhumuka, nilkuwa kama kinyago Fulani hivi. Nafikiri ni kwasababu ya kukannyagwa na wenzangu, lakini nashukuru mungu waliponipima hawakuona sehemu iliyoumia kwa ndani..’ Huyu ni dada yangu akihadithia ajali yake ilivyokuwa na wengi wetu tumeshakumbana na ajali kama hizi. Wapo ambao hawajiwezi, wapo waliopoteza viuongo vyao, na wapo waliopoteza maisha, lakini hatimaye tunasahau.

Hii ni hulka ya kibinadamu kusahau, hata kama ajali iliyokupata ni kubwa kiasi gani, tunaishia kusahau! Na kama tusingeweza kusahau huenda hata akina mama wasingelipenda kubeba mimba mara ya pili. Kwani kuna wengine wanaponea tundu la sindano. Lakini kila mtu hufa kwa wakati wake, au sio. Zipo ajali za kujitakia na hizo zikipita tunasahau, na huenda wakati zinatokea mtu huahidi kuwa mimi sitarudia tena, lakini siku kadhaaa mtu huyohuyo yupo palepale, na sie tulioshuhudia tunamuunga mkono, na kumpa sifa. Jamani si mtu akiumwa na nyoka huogopa hata unyasi! Ndio huogopa hata unyasi kwa siku kadhaa baadaye husau!



From miram3

1 comment :

Anonymous said...

Event zako unatakiwa usiwe mvivu wa kusoma, but very interested...i like your style