Japokuwa,
jamaa alionekana kuwa na hali mbaya, lakini akajitutumua, na lakini alionekana
kuongea kwa shida, na wale akina mama wakaangaliana na wakawa wanatoleana
ishara….Nilivyowaangalia mimi nikajua wanaonyeshana ishara kuwa jamaa anaigiza
tu ili kukwepa maswali.
‘Vipi
hali imekuwaje mtaalamu..mbona upo hivyo, au unataka kukimbia maswali yetu,
usihofu nia ni kutaka kukusaidia tu wewe…kama tulivyokuambia awali..’akaambiwa.
‘Hapana,
sio kwamba nataka kukwepa maswali yenu,..kiukweli kuna hali napamabana nayo,
hamuwezi kuiona,.. najisikia vibaya tu, lakini tuendee tu, nipo sawa sasa
nimeshinda….oh, kazi kweli kweli,..’akasema na kujinyosha halafu akasema;
‘Na
hayo masharti mengine yanasemaje…?’ akasema kuuliza, huku akishika kichwa.
Kama hakuna
matatizo, basi tuendelee maana docta alisema ukiwa hujisikii vyema tuachane na
wewe, hata hivyo muda umekwisha, lakini ni muhimu tukakubaliana ili tukija tena
tunakuja kuwekeana sahihi ya makubaliano, au sio, na kuendelea na mchakato
mwingine, ila muhimu kuanzia sasa uanze kuyaondoa hayo mazindiko yako
uliyoyaweka huko majumbani kwetu…tumekubaliana na hilo au sio..?’ akaulizwa
‘Mhh..sawa…huyu
mtu bila kumuondoa, atanitesa….’akasema.
‘Unasemaje..mtu
gani…?’ akaulizwa
‘Hapana,
ni mambo yangu napambana nayo kichwani, tuendelee tu….’akasema.
‘Kwahiyo
kwanza uifanye hiyo kazi, uyaondoe hayo mazindiko uliyosema yapo majumbani
kwetu , ukifanya hilo tutaweza kuendelea na mengine, kama
tutakavyokubaliana…’akaambiwa.
‘Nitayaondoaje
hayo mazindiko…?’ akauliza.
‘Wewe
si ndio umeyaweka, kwahiyo unajua jinsi gani ya kuyaondoa, au…?’ akaulizwa.
‘Mimi
nipo hapa hospitalini, na kwanini mnasema ni mimi nimeyaweka, sijasema hivyo, kuwa
mimi ndiyo nimeyaweka jamani,….’akasema.
‘Sasa
ni nani,… ‘ wakasema wale mama kwa
pamoja.
Jamaa
aliposikia hao akina mama wakisema kwa pamoja tena kwa hasira, akainu uso na
kuwaangalia mmoja mmoja, kama anawahesabu, halafu akatulia kimia, hakujibu
kitu, na mama muuliza maswali akasema
‘Tuambie
ni nani, kwasabbu tokea awali ulishakubali kuwa ni wewe, unahusika na mauchafu
hayo, tusipotezeane muda hapa, unajua hili ni kwa manufaa yako, ukumbuke
nilivyokuambia awali, usipokubaliana nasi, basi tutachukua hatua nyingine, wapo
mashahidi, na mmojawapo anakujua kuliko unavyofikiria, na kile kifaa pale
kilishachukua mazungumzo yetu yote…’akaulizwa hivyo, huku huyo mama
akimuonyesha kwa kidole kile chombo kilichopo.
‘Tatizo
nyie watu hamnielewi, hebu jiuliizeni tu,…kwanini kama ni mimi nimeyaweka hayo
mazindiko, kwanini tena niwe mimi wa kuja kuyatoa, yaani mimi niwe nacheza
mchezo wa kuigiza, mimi sina tabia hiyo, tatizo ni kuwa hamjafahamu
nilivyo,..ila nafahamu ni nani kayaweka,…, na kwanini kafanya hivyo, ndio maana
nikajitolea kuja kuwaambia, katika namna ya kupambana naye, ni adui yangu
mkubwa sana na ndiye …aah…’akashika kifuani kama kun akitu kimemchoma..
‘Vipi
tena….?’ Akaulizwa, akabakia kimia akiwa anatoa jasho, baadae akasema;
‘Haya
tuendelee, mimi nawasikiliza nyie.., nitafanya mtakavyo, ila munielewe
hivyo….’akasema
‘Hapo
sawa, sasa pamoja na masharti hayo, kwa vile nia yetu ni kukusaidia, ili
uondokane na mauchafu hayo, sisi tutahitajia uharibu uchawi wako wote… maana
ukishatubu, huhitajiki kuendelea na madhambi hayo tena, hilo ni ombi kwetu na
sharti la mwisho…, na kama ukiendelea kitakachokupata tena usije
kutulaumu…’akaambiwa
'Kwa
vipi mtalihakikisha hilo, maana nyie hamjui uchawi ni nini, hamjui watu
wameupataje, hamjui unavyofany akazi, je ni kikubali kuwa nimeharibu , hivi
hivi na bado nikawa naendelea nao, mtajuaje,…niwaambie kitu sio wote wanao-ununua
uganga, wengine ni urithi kwa mashinikizo makali sana, wakiuacha, waanishia
kubaya…’akasema
'Kwa
vipi,…eeh, unauliza kwa vipi,..unajua sisi tutakuamini, si kwa masilahi yako,
kwani wewe unaweza kushidnana na mungu, kiapo chako kitawekezwa kwenye nguvu za
mwenyezimungu, kama utaweza kushindana naye haya, hata hivyo, wapo watu wa
kutusaidia, ambao ni zaidi yako…’akaambiwa
‘Mhh,
nani hao, ambao ni zaidi yangu, nitafurahi kuwafahamu, ….’akasema
‘Unajua
mzee, wapo wenzako tena wa karibu yako mnaoshirikiana nao, wanakufahamu uwezo
wako wote, na wao wameshaamua kuachana na mambo hayo na wapo tayari
kushirikiana na sisi, wametubu na sasa
wapo kwenye michakao ya kuharibu uchawi wao wote…’akaambiwa.
‘Hahaha,
kweli nyie mnanichekesha, hivi mnafikiri hilo ni jambo rahisi kihivyo,…saa,
mimi sijui, labda mniambia ni akina nani,..mkinitajia nitaweza kuwashauri kama
kweli wamesema kweli au uwongo…?’ akauliza na kuto hayo maelezo.
‘Hao
hao waliokuwa walimu wako,….’akaambiwa na hapo akatoa jicho la kushtuka, na
kusema.
‘Walimu
wangu…mmh, ajabu kabisa, ni akina nani,
…mimi sina mwalimu, mwalimu wangu wa uganga, ni nani huyo, maana mimi nimepitia
sehemu mbali mbali hadi kufikia hapa,..na niwaambie ukweli, uganga wangu
nimeurithi kutoka kwa mababu zangu, mengine ni ziada tu…’akasema
‘Tatizo
lako bado hujaamua kusema ukweli..hujaamua kutubu, hujajua kuwa hapo ulipo
umefikia kubaya, hebu tukuulize unajua mguu wako una tatizo gani..?’ akaulizwa
na yeye akainama kuuangalia mguu wake, na kusema;
‘Najua,
nimeshaongea na docta, wameniambia tatizo ni nini… lakini mimi nafahamu jinsi
gani ya kujitibia, magonjwa kama haya nimekuwa nikiwatibia watu wengi, wamepona,
ulizeni huko ninapotokea,..lakini hili la kwangu limekuwa la aina yake, nahisi
ndio katika vita hivi na maadui zangu…’akatulia.
‘Kwahiyo
una imani kuwa matatizo yako hayo yanatokana na maadui zako..?’ akaulizwa.
‘Mhh…naweza
kusema hivyo, na mizimu nayo imenigeuka, lakini, sikuwa na jinsi,..hata hivyo,
bado sijakata tamaa, na wao watu wangu wanajaribu kunipima, hawawezi
kuniacha…’akasema hivyo.
‘Kwahiyo
mpaka unafikia hapo kutaka msaada kwetu si ina maana mumeshindwa…?’ akaulizwa
‘Kushindwa,
sio kwa maana sijui madawa yake, ila
kuna madawa mengi natakiwa kuyapata, yanatokea mbali, huko yana bei sana…hali
yangu imekuwa ikizidi siku baada ya siku …sasa nikaona nije huku hospitalini, labda
kuna njia rahisi, kumbe ndio nimejiweka kitanzi,..hakuna wanachokifanya hapa,
nimeona nimekuja bure tu.. vipimo, vipimo..lakini eeh, sawa ngoje nivute subira
tu…’akasema.
‘Je
ukiambiwa mguu huo ukatwe utasemaje…?’ akaulizwa
‘Kwanini
ukatwe, haaah, we mguu wangu ukatwe hapana, hilo sikubali, nilishawaambia, waliniambia
hivyo, awali nikagoma, …baadae wakaenda huko na vipimo vyao, wakaja na shauri
hilo kuwa , ili nipone natakiwa kwenda kutibiwa India,..hilo hata mizimu yangu
umekubali..lakini kwenda huko sasa, ooh, gharama, ndio nikaanza mchakato wa kutafuta pesa,..hata
hivyo, ..aah, sijui kwanini..’akasema akitikisa kichwa.
‘Wewe
unahisi kwa tiba zako utapona, sio umeshashindwa na je una uhakika gani kuwa
utapata msaada wa kwenda kutibiwa huko India…?’ akaulizwa.
‘Kama
nikipata hizo dawa zangu nitaweza kujitibia mwenyewe,..lakini sasa kwa hilo
inaniwia vigumu, maana kuna mtu ananipiga vita, kila nifanyalo yupo nyuma
yangu,…muda mfupi uliopita alinitembelea hapa, hamkumuona tu,…ndio mkaniona
kimia, nilikuwa napambana naye, kakimbia, nilichomfanya hatakisahau, alijua
nipi bure bure hapa..…’akasema.
‘Ni
nani huyo..?’ akaulizwa.
‘Siwezi
kuwatajia,…maana huenda ni mshirika wenu keshawahadaa, sasa anataka kunipata
kwa kutumia mgongo wenu, haniwezi,..’akasema na kabla hajatulia mara akatoa
jicho, kama kaona kitu mbele yake, akakunja uso, alionekana anahisi maumivu,
..jasho likawa linamtoka…akawa anaongea lugha ya aina yake huku anahangaika
pale alipokaa,…baadae akatulia, akawa anahema kweli kweli…
‘Kama
haupo sawa, basi tutakuja kesho…’akaambiwa.
‘Hapana
ya kesho hayo mengine, …hamjui mwenzenu nipo vitani, natamani niondoke
humu…nyie tuendelee tu maana nataka mkitoka hapa na mimi niwe na tumaini ..
nawategemea nyie, lakini pia mkumbuke kuwa na nyie ndio mnanitegemea mimi ili
niweze kuwasaidia, kwa hilo tatizo lenu….mna matatizo kwenye majumba yenu, hilo
tatizo mimi nalifahamu jinsi gani ya kuwasaidia, lakini linahitajia haraka,
mkinikosa mimi litawaumiza, na mtaishia kudanganywa tu…’akasema.
‘Mbona
wenzako wamesema ni tatizo dogo tu…wewe naona ni zako za kutaka kutupata
kirahisi,. Na hayo wamesema ni mazindiko ya watu wameyaweka, kututishia, na
kutesa wengine, na wewe upo nyuma ya hilo, hawajasema ni wewe, ila upo nyuma ya
hilo…’akaambiwa.
‘Umeona
kama ni mimi wasingelisita kunitaja kwa vile ni maadui zangu, wanafahamu kuwa
sio mimi, ila mimi ndiye naweza kuyaondoa kwa urahisi, wao, watakuwa
wanabahatisha tu…na mniombee niendelee kuishi,la sivyo,..sijui, mimi siwatishi,
lakini….’akatikisa kichwa.
‘Tukuambie
ukweli, wenzako walikuwa kama wewe, tumeongea nao, na sasa wamekubali kutoa
ushirikiano, wamekubali kuachana na mambo hayo, kwani wameona hayana faida
kwao….kama ni uganga, basi wataendelea nao kwa nia njema kabisa tu, imebakia ni
wewe, kwanini unakuwa mgumu hivyo,…’akaambiwa.
'Ni nani
hao, wanaowadanganya hivyo, mmh, nyie hamjui tu…?’ akauliza tena.
'Huna
haja ya kuwafahamu, ukikubalina nasi, basi utawafahamu, kwasababu mtakutana
katika hali ya kubadilshana mawazo na mnatakiwa muungane ili muweze kubuni njia
mbadala ya maisha mazuri, kuliko kutegemea maisha hayo ya kutesa wengine, ifike
sehemu mjirudi, hivi hamumuogopi mungu…..’akaambiwa.
'Mimi nina imani, nitapona, mimi nina imani
sina matatizo kama hao wengine, tatizo langu limtokea kwa vile nimeamua
kupambana nao, baada ya kutaka kunigeuka, na jingine kwa vile na mimi
nimekengeuka kugoma kufuatilia mambo ya mizimu, wakati mwingine najuta kwanini
nilikubali haya mambo, nakuwa sina uhuru wa maisha…’akasema.
'Sasa unasemaje maana muda umekwisha, anza
kazi, yako, haraka, kwa kuondoa hayo mazindiko yako, mengine tutaendelea hatua
kwa hatu,au sio wenzangu..?’ huyo mama akasema na kuwageukia wenzake.
‘Sawa
kabisa sisi tunamsikiliza yeye,….’wakasema hao akina mama wengine.
‘Kwa
hilo lenu siwezi kulifanya nikiwa humu hospitalini, siwezi kuwadanganya, mimi
sina tabia hiyo ya uwongo, hayo mambo yenu nitaweza kupambana nayo nikiwa
majumbani kwenu, ana kwa ana, na kama kuna mtu kawaambia ataweza haya nendeni
mkafanyiwe, lakini nina uhakika mtakuja kurudi hapa kwangu, na muombe mungu
niwe bado sijaondoka,..…’akasema na ghafla, akashika kifuani tena na kukunja
uso, kuashiria maumivu.
‘Kuondoka,
kwenda wapi…?’ wakauliza
‘Huko
kwenye mat-t-tibabu,..ooh, ole wako…’akasema kwa shida
‘Basi
sisi tukuache kwanza, naona hauko vyema, au…, … tutaongea na docta tuone
atakavyoweza kukusaidia, ili ikiwezekana utoke kwanza ukayaondoe hayo mazindiko
yako, na huku michakato yako ya kutibiwa ikiendelea …’akaambiwa
'Tatizo,
hamjui ubaya wa hayo mazindiko mliyowekewa, ,…nawaambia mkiondoka hapa, mnaweza
kuanza kupagawa, na hebu fikiria mkibadilika akili mkawa hamjijui ni nani
atawafuatilia, na labda mimi nitakuwa sipo, mtapata shida sana, nawaonea sana
huruma…’akasema.
‘Sasa
kwahiyo unasemaje ..?’ akaulizwa.
‘Kuna
mtu kasema anaweza kuyafanyia kazi, kama wewe utagoma,..’akaambiwa
‘Tatizo
la waganga wa kienyeji, wengi wao hawatki kusema ukweli, sawa watajaribu lakini
watafikia sehemu watashidnwa, na muda huo mumeshaliwa pesa zenu na kiendacho
kwa mganga hakirudi au sio….’akasema
‘Lakini
yeye ni mwalimu wako, kakufundisha wewe, sasa kwanini yeye ashindwe….’akaambiwa
'Nani
mwalimu wangu, yupo huyooo….?’ Akauliza akiwa kakunja uso, na akatikisa kichwa
huku na kule halafu akasema
‘Oooh,
ni huyo muhini, ....sasa nimewaelewa, nilikuwa najiuliza ni nani huyo
aliyewadanganya, kumbe ni huyu, wewe…unanitafutia nini, nitakuumiza,sitajali
kuwa wewe ni mwalimu wangu…’akasema sasa akiangalia mbele, ukumbuke sisi
tulikuwa tumesimama mbele yake, kwahiyo ni kama alikuwa akituangalia sisi .
Baadaye akatulia, akahema kama mtu aliyetua
mzigo, akasema
‘Kumbe
ni huyu muhuni, hahaha, hahaha hana kitu kwa sasa, sawa kiukweli alikuwa anajua
madawa, lakini mambo makubwa kama hayo, hana uwezo nayo kwasasa, anachojua
yeye, kwasasa kwa vile keshanyang’anywa
karibu kila kitu anachofanya ni kucheza mazingaumbwe…uwawekezea watu mazindiko,
na hapo hapo anakuja kuyatoa, ni mazingaumwe tu aliyobakia nayo…’akasema.
‘Kwahiyo
yeye, ni kweli alikuwa mwalimu wako…?’ akaulizwa.
‘Hilo
nalikubali, ni kweli siku nilipokabidhiwa mikoba na mababu zangu, walinipeleka
kwa mababu wa huyo mtu, na yeye alipewa mikoba kabla, na hao watu, nilipofikishwa
kwa hao mababu nikaambiwa huyi atakuwa ndiye mwalimu wangu, na kweli alikuwa
anajua sana…na hakujua kuwa na mimi nilikuwa mwepesi wa kujifunza haraka sana..hakuamini
hilo…’akatulia.
‘Kwahiyo
ukawa sawa na yeye..au ukamzidi..?’ akaulizwa.
‘Kuna mambo
hakutaka kunifundisha, kama angelifundisha wakati huo ningelikuwa zaidi yake
kwa kipindi hicho na iisngelikuwa na maana ya kukaa kuendelea kuwa mwanafunzi
wake tena…lakini tatizo lake kubwa alikuwa mchoyo, na si mchoyo tu akawa
anatutumia sisi kufanikisha malengo yake mabaya…’akasema.
‘Kwa
vipi…?’ akaulizwa.
'Uganga,
na hasa uchawi, umegubikwa na matambiko, na makafara, na tofauti kubwa ya
mchawi na mganga unaweza kuuona kwenye hayo mambo mawili, matambiko, na makafara,
ila waganga wengi wasiojihusisha na mambo hayo wanakuwa na utaalamu wa madawa
tu, ukiona mganga kakuingizo kwenye hayo mambo mawili uwe makini sana, ….’akasema.
'Wachawi wao wapo tayari kutoa makafara ya
damu za watu, kuua kwao ni kitu rahisi tu…nia ni ili wafanikiwe zaidi, na wanafanya hivyo kwa
kuwatumia mashetani wenye nguvu, ambao wanahitajia damu za watu. Mashetani ndio
watumishi wao, kwa ujira wa damu za watu..na maagano yao ni makali zaidi,
wakokosea na wao wanadhurika,…sasa yeye katika kutufundisha hayo, akawa
anatuelekeza hayo kwa kutupima…, tufanye hayo kwa vitendo, anatutuma kutafuta
damu za watu…’akasema.
'Kwahiyo
mkawa mnaua, ili mpate damu au…?’ akaulizwa
‘Unajua
sisi tulikuwa wanafunzi, na wanafunzi, kama walivyo wanakuwa na uchu wa kujua,
na wakati mwingine huwezi kuwa makini na unachokifanya, kwasabau hukijui, na
kama unajua ni hivyo, bado, unamtegemea mwalimu wako kuwa ataweza kuzuia kwa
namna nyingine, kama ni majaribio tu ya kawaidia..sijui mnanielewa, maana mwalimu yeye ndio anafahamu matokea
yake, sisi tulikuwa tunafanya kile tunachoagizwa, tukijua ni sehemu ya
mafunzo…’akatulia.
'Sawa
kwahiyo mkiagizwa kuua, mnaua si ndio hivyo,…, kwa maelekezo ya huyo mwalimu
wenu, si ndio hivyo,….?’ Akaulizwa.
‘Lakini
sisi hatukujua madhara yake, kwa upande huo, na tuliambiwa tusipofanya hivyo,
sisi au familia zenu ndio zinatakiwa kukamilisha makafara hayo…’akajitetea.
‘Kuua
si kuua, madhara ya kuua, ni nini hapo, kwa kifupi mlikuwa mnaua lakini
kutokana na maelekzo ya mwalimu wenu au sio.?’ Akaulizwa.
‘Nina
maana hivi, kwasababu sio unakwenda unamuua mtu hivi moja kwa moja, unaambia
fanyeni hivi na vile, halafu mtaona kitakachotokea, eeh, sisi tunafanya,
tunasubiria, mara haipiti muda, huyo mtu
anakutwa na mabalaa, ajali, au chochote, au wakati mwingine huyo mtu anapoteza
maisha, baadae tunaambiwa twende kwake, tukafanye jambo…’akasema
‘Jambo
kama lipi..?’ akaulizwa na hapo akasita kidogo , baadae akasema;
‘Kama
ni ajali, tunawahi damu yake, kama…ni viungo vyake vinahitajika, tunaviwahi
kabla hajafa…maana vinahitajika vikiwa na moto, na vitu kama hivyo…’akasema.
‘Oh…ina
maana ajali nyingine sio ajali za kawaida…mnatengeneza nyie…?’ akaulizwa.
‘Sisi
tulikuwa hatujui, unielewe hapo, mpaka tulipofikia hatua ya kujua, ndio
tukagundua kumbe tulikuwa tunatumiwa, na wale walioamua kuachana naye, na kuwa
watu safi wakafanya hivyo, ila wale waliozidiwa na mambo hayo wakaona ni mambo
ya kawaida tu wameshagibikwa na ibilisi.., wakabobea huko kwenye
uchawi….’akasema.
‘Wewe
ulifanyaje, si uliendelea naye, usitudanganye hapo..?’ akaulizwa.
‘Kwa
vile mimi nilikabidhiwa kwa huyo mtu, haikuwa kazi rahisi kwangu kuachana naye,
nikaendelea kuwa naye lakini huku nikitafuta mwanya wa kumzidi nguvu, kwa
kuyafahamu hayo anayoyajua ambayo ndio yanamfanya awe zaidi ya sisi, na nikawa
nagoma kuyafanya yale ambayo najua yanamadhara kwa watu ndio hapo tukaanza
kusigishana…’akasema.
‘Kwahiyo
ukafanikiwa..au ilikuwaje?’ akaulizwa.
‘Haikuwa
kazi rahisi, nilianza kukosana naye zaidi na hata kutengana naye, pale
aliponiambia, nahitajika kuua mtoto wangu, ili niweze kukabidhiwa mikoba yangu…’akasema
‘Mikoba
yako, kwa vipi, kwani ni yeye alitakiwa kukupa au …wewe si ulisema uganga wako
ni kutokana na mababu zako,…?’ akaulizwa.
‘Mikoba
yangu alipewa yeye, ili nikiiva, na kuwa tayari ndio anikabidhi, na nisipo
kabidhiwa kuna madhara nitayapata mimi na familia yangu,…na hatua niliyofikia
sikutakiwa kuikosa, hata niliposema, niachane naye, ikawa siwezi, kuachana
naye, ningeharibikiwa kabisa, na mabaya yangeniandama…’akasema.
‘Kwahiyo
ukafanya hivyo..?’ akaulizwa
‘Awali
hakuniambia moja kwa moja nahitajika kumuua mtoto wangu, aliniambia, nahitajia,
kupata nguvu, ili niweze kuyabeba hayo majukumu, na nguvu hizo zipo kwenye viumbe
vizivyo na dhambi, ..’akasema.
‘Viumbe
gani hivyo…?’ akaulizwa
‘Mfano
watoto wadogo….’akasema.
'Mungu
wangu, kumbe ni kweli...'akasema mdada akimuangalia huyo jamaa kwa macho
yaliyojaa chuki.
'Kweli
nini…kuwa mimi nilimuaa mtoto wangu mwenyewe , hapana wewe hujui tu, kwanini
mnakimbilia kunishutumu kabla amjasikia ilivyokuwa,…’akauliza alipomuona mdada
anamuangalia hivyo.
‘Si
ndivyo ulivyofanya, uliua mtoto wako ili upate huo mkoba, ni kweli, usibishe,
uliwahi kuniambia,….’akasema huyo mdada
‘Hebu
subiri kwanza , …’akasema huyo mama akimzuia huyo mdada asiongee zaidi.
‘Kwahiyo
huyo mwalimu wako, alikuambia kuwa ili akukabidhi hicho kijiti, au mkoba, ili
ufuzu mafunzo yako, inahitajika damu ya viumbe visivyo na dhambi, ambavyo uliambiwa
ni watoto wadogo, si ndio hivyo…?’ akaulizwa
‘Ndio
hivyo….’akasema
‘Kwahiyo
ukatakiwa utafute damu ya mtoto mdogo, ..?’ akaulizwa
‘Ndio,
lakini hakusema hivyo kuwa damu kwa maana ya kuua, hapana alisema, tunahitajika
damu ya viumbe hivyo, vipatikane
vifanyiwe kafara, na vitakuwa kama kinga yetu,…’akasema
‘Kwa
vipi..kafara ni nini hapo, si ina maana kuua, ili damu itoke, au tueleweshe
hapo zaidi..?’ akaulizwa
‘Ina
maana ukitaka kupambana na adui, mtoto huyo anakuwa ngao yako, sio lazima kila
siku, ndivyo alivyotuambia hivyo,…’akasema
‘Hapo
naona unakwepa kutuambia ukweli….nikuulize hivi hilo kafara ni nini hasa…?’
akaulizwa
‘Kafara
mara nyingi linafanyika kwa kutumia damu….’akasema.
‘Damu
ya watu au wanyama..?’ akaulizwa.
‘Kwa
mambo ya kichawi, mara nyingi ni damu za watu, mara chache ni damu za
wanyama,..lakini kwa huyo mwalimu wetu yeye mara nyingi alikuwa akihitajia damu
za watu….’akasema.
‘Kwahiyo
nyie kila mara kwenye makafara yenu mkawa mnatafuta damu za watu, si ndio hivyo…?’
akaulizwa
‘Kwa mara
chache tulikuwa tunafanya hivyo, hasa..kwa matambiko makubwa sana,…’akasema
‘Sawa hata kama ni machache, ila mliyafanya kwa kutumia damu za watu…?’ akaulizwa.
‘Ndio…lakini hatukuwa
tunajua hayo awali, kama nilivyosema tulikuwa ni wanafunzi tu….’akajitetea.
‘Na
sasa ukaambiwa damu ya mtoto mdogo, si ndio hivyo..wakati huo unajua, sio mwanafunzi tena si ndio hivyo…?’
akaulizwa
‘Elewa
nilivyokuambia awali, hapa huyu mtu alinitega, akisema anahitajia mtoto kama kinga,
yaani ili nipate huo mkoba wangu, ni lazima nimpate mtoto kama kinga yangu…’akasema.
‘Umpate
kwa vipi, si kwa kafara au sijui mnaita matambiko au sio…?’ akaulizwa.
‘Hakunifafanulia
hivyo awali,..angelisema hivyo ningelijua na ningelichukua tahadhari, nisingelikubali kumchukua mtoto wangu…’akasema.
'Ungelimchukua mtoto wa nani...?' akaulizwa
'Ningelijua , ningejua jinsi gani ya kulikwepa hilo , mbona kuna mengi aliniambia nikakataa, kwanini hilo nisingelikataa,...mimi sio mjinga kiasi hicho....'akasema
‘Kwanini
sasa, kwanini mtoto mdogo asiye na dhambi, …hapo tueleweshe kidogo…’akaulizwa.
‘Mhh…hapo
alivyonieleza yeye, akinivunga..sijui kwanini nilifunikwa akili nisielewe...aliniambia sasa nimeiva, lakini sio kwamba nimeshafikia hatua ambayo
ninaweza kujilinda mwenyewe, lakini kwa hatua niliyofikia, hatua kwa hatua, na kwa jinsi nitakavyopambana na
majanga, mitihani nk, kwenye kutibia watu na kwenye kujilinda, ni lazima nitakutana na mitihani mbali mbali, kwahiyo kwa vile
bado najifunza kwa vitendo, nahitajia kuwa na ngao…’akasema.
‘Ngao hiyo inatokana na kafara la damu ya mtoto au sio…?’ akaulizwa.
‘Subiri,... unielewe hapo…’akasema
‘Ehee
elezea inakuwaje…?’ akaulizwa
‘Katika
kuendelea na kazi hizo, nitakutana na mitihani, kutakuwepo na maadui, wengine
wanaweza wakawa wametuzidi huwezi kujua, sasa ili uweze kupambana nao,
unahitajika kuwa na, ngao ambayo nguvu yake hupatikana kwa watoto wadogo tu, ...…akatuambia hivyo maana tulikuwa watatu, wengine walishaondoka....'akasema.
‘Mkauliza
ngao hiyo ni nini, mkaambiwa ni watoto au damu ya watoto wadogo au sio…?’
akaulizwa.
‘Hakufafanua
hivyo…yeye alichoendelea kusema ni kuwa kila mmoja atatahiniwa kivyake,..’akasema
‘Uliambiwaje
mpaka ukamchukua mtoto wako,..?’ akaulizwa
‘Ili
nifanyiwe hilo nimchukue mtoto ambaye, ninaweza kuwa naye mara kwa mara na nitaonyeshwa hatua kwa hatua, jinsi
gani inafanya kazi…’akasema
‘Kwahiyo
wewe ukamchukua mtoto wako, kwa vile yeye mpo naye mara kwa mara au sio..?' akaulizwa
'Awali, nilimuuliza mtoto yoyote..akasema je unaweza kumchukua mtoto wa atu ukakaa naye muda wote...basi nikasubiria siku moja akasema mlete huyo mtoto…ili tufanye hicho kitendo...'akasema
'Alisema mlete huyo mtoto mfanye nini...?' akaulizwa
'Kafara la kumaliza na kuwa na ngao kwa ajili ya kupewa huo mkoba
'Hapo alitamka kafara si ndio...?' akaulizwa
'Kihivyo, lakini alishafafanua, ni vipi, kwahiyo mimi nilijua sio kafara kama lile....akili hapo ilinituma hivyo...'akasema
'Lakini awali ulisema kafara hufanywaje...'akaulizwa
'Hapo akili ilikuwa imefunikwa kiukweli,...nakumbuka kauli yake ya mwisho alitamka hivyo, kuwa mlete huyo mtoto tumalizie hicho kitendo, cha kafara la mwisho...'akasema
'Ok ikawaje..maana usitudanganye hapo maana kiulimu ulikuwa hatua ya juu, ulishaiva, na ulijua ni nini maana ya kafara, ulijua ni nini kitatendeka kama ni kafara, au sio?’
akaulizwa.
‘Mhh,
unajua ni hivi, alisema anahitaji mtoto ambaye utakuwa naye karibu siku zote,
na huwezi kumchukua mtoto wa mtu mwingine…hapo elewa, nitakuwa naye siku zote, hiyo ni kauli yake ya awali, …ina
maana gani hapo, ni mtoto wako na , kwa vile hata hizo nguvu zitamsaidia na huyo
mtoto wako....hayo aliyatamka hivyo..., kwahiyo ina maana nifanye nini...'akauliza
'Jibu wewe ambaye ulifanya....'akaambiwa
'Ni moja kwa moja alimtaka mtoto wangu...'akasema
'Lakini hakuwahi kusema mtoto wako, sema ukweli wako...?' akaulizwa
'Maelezo yake yalilimaanisha hivyo, asijitete bwana...'akasema
'Kwahiyo wewe kwa maelezo yako, na kwa vile ulikuwa na uchu wa kuupata huo mkoba, akili ikafunga, ukawa huna uchungu wa mtoto tena, ukamchukua mtoto kwenye mambo yenu ya kishirikina, sema ukweli na ukiri kosa, hapoo huwezi kuchomoa...'akaambiwa
'Usilazimishe maana haikuwa hivyo unavyofikiria wewe...sikuwa na uchu na huo mkoba,kama huyo mwalimu atasema ukweli ataweza kukuelezea jinsi gani nilivyokuwa nataka kuachana na mambo hayo na yeye ananiwekea mitihani migumu mpaka nakubali kurudi tena, muulizeni kama ataweza kusema ukweli...'akasema
'Kwahiyo wewe ukamchukua mtoto wako, ili mpate faidi wote
wawili ndio kauli yake iliyokufanya uvutike kumchukua mtoto wako au sio…’akasema.
'Ndio hivyo,lakini nikijua nitakuwa naye, kama ngao, katika kazi zangu za kila siku...'akasema
‘Kwahiyo
ukamchukua mtoto wako…mkafanya nini hapo..?’ akaulizwa na hapo jamaa akainamisha
kichwa chini na alipoinua akawa kajawa na machozi
‘Kiukweli
mimi sikujua, ningelijua nisingelifanya hilo..alinihadaa…kwanini nimuue mtoto
wangu, …’akalalamika.
‘Tuambie
sasa mlifanyaje..mlifany atambiko la kumwaga damu au sio damu ya mtoto mdogo, asiye na dhambi, ili iweje,..uweze kuupata huo mkoba, na mkoba si umeshaupata, si ndio hivyo?’ akaulizwa.
‘Unajua ukiongea hivyo unalazimisha,...yeye hakusema moja kwa moja ni tambiko la kumwaga damu, hakusema hivyo, mwishoni wakati imeshafikia hatua ya mwisho ndio akatamka neno kafara la mwisho...muulizeni vizuri, kauli hiyo aliitamka mwishoni kabisa, na mimi sikuwa na ....utashi, maana nilishajenga hisia kuwa , atakuwa kinga yangu....'akajitetea
'Tuendelee, hapo, sijui.....tuendelee, inauma kwa kweli, ..mimi ni mama na kauli hiyo, inaanza kunifany anitake kulia, kwanini muwe na tamaa kiasi hicho...'akasema
'Najua hadi hapo hamtanielewa, ..lakini hamjui ni mateso gani nilipitia, maana hadi namchukua mtoto nilipitia mateso, niligoma awali, nikaanza kuteswa, silali, muulizeni hata mke wangu, kipindi hicho..'akasema
'Kwanini sasa..?' akaulizwa
'Kwa vile sikutaka familia yangu hata mmoja ije kujihusisha na mambo hayo, siyapendi kabisa...'akasema
'Kwanini..?' akaulizwa
'Ni mabaya...'akasema
'Kwa vipi..?' akaulizwa
'Oh, naona unataka kunitega...'akasema
'Kwasababu ni kazi ya uchawi, sema ukweli, na uchawi kama ulivyosema umegubikwa na makafara ya kuua watu, ili mpate damu zao, na wewe hukupenda mtoto wako apitie huko, kweli si kweli...?' akaulizwa na kukaa kimia
'Haya tuambie ikawaje, maana hapo hata mimi sitaki kusikia, lakini ni lazima useme ili ujikoshe au ujiweke sehemuu ambau sis tutakusamehe...'akaambiwa
'Ndio
akaanza kuonyesha jinsi gani ya kujikinga, nikipambana na hao, walionizidi
nguvu, akanitupia kombora, akasema, fanya hivi na vile nikafanya, …ooh…’hapo
akatulia kimia.
‘Ikawaje,….?’
Akaulizwa jamaa akwa kimia…jamaa alikuwa kaduwaa, macho yamemtoka, hasemi kitu, katulia
kama mfu…
Akina
mama pale wakashtuka, mmoja akasema;
‘Tumuite
docta, mwingine akasogea kutaka kumgusa jamaa,…na mara mlango ukagongwa kwa nguvu, na mama mmoja,
akaenda kuufungu akijua ni docta kaja kwa dharura,…alipotaka kuufungua, huyu
mgonjwa akasema kwa sauti kubwa.
‘Usifungue…’
lakini huyo mama alikuwa keshafungua, mlango
..
NB:
Mhh..hapo sasa
WAZO LA LEO: Usikusudie kutenda dhambi huku
unajua, ukiitakidia kuwa utatubu, au hutarudia tena baada ya tendo hilo la
dhambi, au unatenda ili upate, ukipata hicho unachotaka kukipata, japo ni kwa
njia ya dhambi, utaacha, na kutubu dhambi hizo..SWALI. Je una uhakika gani
baada ya kitendo hicho utaweza kutubia, au utafanikiwa kukipata hicho kitu, au baada ya kufanikiwa utakuwa na utashi wa
kutubia, au una uhakika gani, kuwa utaweza kuiona hiyo kesho yake…Dhambi ya
kukusudia, ina dhamira ndani yake, ni kufuru..ni heri utende ukiwa hujui na
ukijua utatubu, lakini sio kwa kukusudia, ili baadae utubu, tumuogope mola wetu.
Tumuombe mola wetu atusaidie, tuweze kuyatenda yaliyo haki, na mabaya tuweze
kuyaepuka Aamin.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment