Na mara mlangoni
akaingia mdada mmoja, na wote wakageukia kuangalia huko mlango , na huyo mdada
alipona hiyo hali, watu wote wanamuangalia yeye, akasita kuingia, baadae akawa
anaingia kwe mwendo wa taratibu….
Wa kwanza kuongea
alikuwa ni dereva, ambaye alionekana mwenye mshangao mkubwa mdomoni, na kusema;
‘Mke angu umekuja, mbona
hukunipa taarifa…?’ akauliza dereva.
‘Nimeamua kuja tu, ….na
nilipokuwa hapo mlangoni nimesikia mama akiongea neno, Mama, mbona unasema
hivyo, mwanao hana matatizo yoyote ya uzazi, mimi hapa nina mimba,...nina mimba
ya dereva, mimba ya mume wangu dereva…’akasema.
'Haiwezekani...'akasema dereva kwa mshangao.
‘Kwanini haiwezekani,
huo ndio ukweli..nimeshapima na nimethibitisha hilo…’akasema
'Haya, kama ulijifanya huzai, ukatembea na binti wa watu, sasa huna cha
kujitetea tena, sasa una watoto wawili…wa kwanza ndio huyo unamkataa na wa pili
bado kuzaliwa…’akasema akimuangalia yule mdada aliyejifunika usoni, na huyo
mdada alionekana kama kuchanganyikwia fulani, akawa kama anataka kuongea jambo.
Mke wa Dereva akasita
aliposikia kauli ile kutoka kwa Soldier akauliza kwa mshangao
‘Watoto wawili…?’
akauliza mke wa dereva.
‘Ndio muulize atakuambia
vyema….’akasema Soldier
‘Muongo huyu,
usimsikilize kabisa, bro kwanini unafanya hivyo…’akasema Dereva akimuangalia
Soldier…
‘Nataka ukweli ujulikane…’akasema
Soldier
Tuendelee na kisa chetu…
**********************
‘Unasema ‘Muongo huyu’…ni nani muongo..?’ akauliza mke wa
Dereva akiwa kashika kiuno huku akimuangalia mumewe. Na dereva akasema kwa
harakaharaka.
‘Huyu anayedai eti mimi nina watoto wawili,…huyo mwingine
katoka wapi, mimi najua huyo aliyepo tumboni mwako,…. hawa watu wanataka
kuniharibia ndoa yangu, kama ni mtoto wangu ningelimuambia mke wangu, kwanini
nimkatae…’akasema akimuonyeshea kidole dereva.
‘Unasema kama mtoto ni wako ungelimkubali, kumbe ndio tabia
yako, kumbe una vimada nje,..sasa nimekuelewa, uliniona mimi sizai au sio,
yaani kuhangaika kote huko kumbe mwenzangu unaniendea kinyume, haya sema ukweli
kama ni mtoto wako au sio, ..na nikija kugundua kuwa ni mtoto wako, itakuwa
mwisho wangu mimi na wewe, na ’Lisemwalo lipo…’akasema mkewe
‘Mke wanu hayo yametoka wapi..haya ni maongezi tu,
wanajaribu kutafuta baba wa mtoto aliyeokotwa huko kambi ya wakimbizi nchi
jirani…na mimi nilikuwa kiongozi kwenye kundi la kuwasaidia wakimbizi,
wakaniletea huyo mtoto..sasa kuangaika kwangu kote kumtafuta mzazi wa huyo
mtoto, ndio imekuwa kosa…’akasema.
‘Najua..unafikiri sikujui, nawafahamu sana nyie wanaume,
haya hii hapa ni mimba yako, kama una mtoto mwingine ni shauri lako,
nimeshakuambia hivyo….nimewaacha wanaume wengi wa maana kwa ajili yako,
…’akasema akigeuka kutaka kuondoka.
‘Mke wangu hebu subiri, kwanza nimefurahi sana kusikia una
mimba, siamini, unajua, nilishakata tamaa,…sasa sina wasiwasi tena, kuwa huenda
hatuwezi kupata mtoto tena, mama alishaanza kusema ooh, urithi, oor baba yako,
hapana mama hiyo ni bahati mbaya tu….’akasema na kumgeukia baba yake pale
kitandani, akasema;
‘Baba mungu akipenda utapata mjukuu wako, …ni furaha
iliyoje, mjukuu wako wa kwanza, umeona eeh …’akasema akionyesha furaha, na hapo
hapo Soldier akasema;
‘Sasa kwanini unasema mjukuu wako wa kwanza, huyu aliyewahi
kuzaliwa je, mbona humtaji, au umeshamkataa kabisa, utapata dhambi wewe, kazi
kupora visivyo vyako, haya mungu kakujalia mtoto unamkataa, kisa una ajenda
yako ya siri, au unaogopa kuwa shemeji atakuacha,....’Soldier akasema
akimuangalia shemeji yake, ukumbuke huyo mdada ndiye awali kabisa alitakiwa
kuolewa na Soldier, lakini akaja huyo ndugu yake akamzidi kete.
‘Bro, usiniharibie furaha yangu, huyo mtoto ni wa kwako, na
kwa vile hamjajaliwa mtoto atawafaa sana, na hajatambulikana kama mjukuu wa
baba, maana …’ akasita kidogo, na halafu akaendelea kusema;
‘Mke wangu naona tuondoke hapa, naona hakuna cha maana cha
kuongea, wewe mdada huyo mtoto ni wa kwako, kama umeshindwa kuthibitisha kuwa
baba yake ni nani, basi nenda kaishi naye na ukiwa na shida yoyote usisite
kutuambia, kwani nahisi ana damu ya mzee …’akasema akimgeukia mkewe na mama
yake alikuwa bado kaduwaa, akimkagua mkwewe, kama haamini alichokisikia.
‘Haondoki mtu kwanza hapa, unasikia dereva nilikuambiaje,
sasa usitake niongee tena nikazidi kukuharibia, subiri tuyamalize haya, na
tukitoka hapa sote tunakwenda huko nilipowaambia.., sasa ukitoka huko ndio mtakwenda
kujipongeza….na shemeji…’akasema Soldier.
Mara yule mdada aliyekuwa kajifunika uso, ambaye kwa muda
huo walisogea pembeni kidogo wakiteta, na shemeji mtu akasogea karibu na pale
walipokuwepo wengine, naona bado walikuwa hawajaelewana na shemeji wa Soldier, kwani
huyo shemeji alikuwa kama anamzuia, lakini ikawa haiwezekani tena, huyo mdada
akasogea kwenye kundi, na kusema;
‘Jamani pamoja na hayo, nimeona niondoke na mtoto wangu, ila
nahisi nina deni kwenu, ni lazima niuseme ukweli, japokuwa jamaa yangu mfadhili
wangu ananionya kuwa nikisema huo ukweli huenda ikawa ni matatizo ya
kiafamilia, na…huenda na mimi nikaingia matatizoni, lakini mimi sioni tatizo
hilo ….’akageuka kumuangalia shemeji mtu.
‘Nimeshakuambia ukisema huo ukweli na mimi nitajitahidi
ukafungwe, maana ulitoroka huko kwenu, na bado mumetoroka kambini, wewe na
ndugu yako,..nyie ni wakimbizi..’akasema shemeji mtu kwa hasira, na huyo mdada akawa
kainama chini, halafu akainua kichwa na kusema;
‘Kwani nikiusema ukweli wewe utakuathiri nini…sitaongelea
mambo yako, naongea kisa changu na mtoto,…na hicho kisa kinastahiki kijulikane
na hawa watu ili kuondoa dhana mbaya, na ili mwisho wa siku wasije kunilaumu
,..maana ni lazima niondoke na mtoto wangu…’akasema
‘Kama ni lazima kuondoka na mtoto ina haja gani ya kuwasimulia
hayo yote…unataka hawa watu wakuhurumie, hawa watu hawana huruma kamwe…hasa huyu,
..huyu ni tapeli wanamfahamu sana huko mjini, na huyu anayejiingiza kwenye kazi
zisizo muhusu, nenda ukapigane vita huko …’akasema akimuelekezea kidole dereva
huku akimuangalia Soldier
‘Shemeji, usinikashifu, sina utani na wewe….’dereva akasema
kwa hasira.
‘Huo sio utani, Dereva huo ni ukweli, na sitaogopa kusema
ukweli kwako na kwa huyu ndugu yenu…na hata kwa baba yenu, ndio maana
nimemshauri huyo dada, kama nilivyomshauri dada ndugu yangu, kuwa hii familia
haifai, asiache mtoto wake hapa…hanielewi, ok, fanya upendavyo…’akasema
********
Yule mdada akawa katulia kidogo, halafu akasema;
akimuonyeshea shemeji kwa mkono,
‘Huyu jamaa namshukuru sana, kwani kama asingelikuwa yeye,
huenda sasa hivi ningelikuwa maiti, yeye ndiye aliyeniokota nikiwa
sijiwezi,….nikiwa ufwekeni mwa mto, na huo mto una mamba, hata sijui ilikuwaje,
hao mamba wasinitafune…’akasema.
Basi kwa neema zake mungu akanichukua hadi kwenye hospitali
ya karibu na hapo nilitibiwa, ma hali yangu ilikuwa mbaya sana, sijitambui na
nilikaa hapo hospitalini mpaka wanataka kunifukuza, na muda huo mimba ikawa
anakua,.
‘Na baadae alikuja akanichukua hadi kwenye nyumba za
marafiki zake,na kipindi hicho bado afya yangu ilikuwa mbaya, na ilikaribia
muda wa kujifungua, hata hivyo nilionekama mdhaifu, sina damu…taabu moja kwa
moja, vidonda,…ooh, siwezi hata kuelezea..na niliposhikwa uchungu nikapelekwa
hospitalini, hizo za serikali, unajua kulivyo, na hali niliyokuwa nayo,.. lakini
nashukuru, walijitahidi sana…nakumbuka wakati napelekwa kufanyiwa upasuaji,
maana ilibidi nizae kwa njia hiyo, docta alisema; ‘hapa ni moja,mama au mtoto…’akatulia.
Nashukuru sana, madocta wakafanya juhudi na bahati nzuri,
mtoto akatoka salama, lakini mimi nilikuwa kwenye hali mbaya, sana, ikawa kama
mtu wa kusubiriwa tu, masaa yangu yafike, niage dunia..’akasema.
‘Lakini ya mungu mengi, mungu anajua viumbe vyake , siku ya
kwanza ya pili hali yangu ikaanza kurudia vizuri, lakini bado sikuwa mtu wa
kutumainiwa, nilikaa pale hospitalini kama wiki mbili hivi, baadae matumaini
yakaja, na afya yangu ikarejea, lakini nilikuwa kama sio mtu, nimekonda, makovu
..vidonda,…na hata mtoto alikuwa hapati maziwa, mtoto alianza kunyonya maziwa
ya chupa akiwa bado mchanga.
Namshukuru jamaa huyu, ndiye aliyekuwa msaada wangu mkubwa,
kunitafutia madawa, vyakula ..na sehemu ya kuishi,..na kweli baadae nilitoroka
sehemu niliyokuwa naishia, lakini nilifanya hivyo kwasababu ya msingi.
‘Sema ukweli uligundua kuwa huyo jamaa anafanya biashara
garamu…’akasema Soldier
‘Mimi sijui mambo yake, na sikuwa na muda wa kufuatilia
mambo yake,….’akasema
**********
‘Siku moja nikiwa hapo alikuja jamaa mmoja anayenifahamu, na
jamaa huyo anafahamika, mimi namfahamu kwasababu niliwahi kumuona huko, ni wale
watu wanaocheza na sura mbili, anachukua habari za serikali anawapelekea waasi,
…na kuniona mimi, ilikuwa ni hatari kwake, kwahiyo nilijua tu, atawasiliana na
waasi, ili niuwawe. Aliponiona alijifanya hajaniona, akawa ananifuatilia,
lakini nami nikamuwahi.. tukakutana uso kwa uso..
‘Wewe upo hai bado…?’ akaniuliza
‘Mungu mkubwa nipo hai, umetumwa kuja kuniua..?’ nikamuuliza
‘Nitatumwaje kuja kuua maiti, unajulikana wewe ni
maiti…’akasema
‘Kwahiyo umekuja kufanya nini huku?’ nikamuuliza
‘Hiyo sio kazi yako,…ila kwa vile nimekuona na unataka watu
wasikujue inabidi uwajibike,…’akasema
‘Unataka shilingi ngapi…?’ nikamuuliza na akataja pesa
nyingi sana, nikamwambia nitazitafuta, nilimwambia tu ilimradi niachane naye…
Basi nikaona dawa ni kutoroka sehemu hiyo na kwenda sehemu
nyingine, na huko nako kulikuwa na msako wa wageni haramu.., nikaona jambo jema
ni kwenda kambi ya wakimbizi, na huko kambini nikajibadili, nikawa navaa hivi
hadi leo.
‘Kwahiyo mfadhili wangu sikufanya hayo makusudi, na
naheshimu sana msaada wako, sina cha kukulipa lakini ipo siku nitazilipa
fadhila zako…’akasema akimuangalia shemeji mtu.
‘Sihitaji malipo yoyote, nimesaidia watu wengi sana…’akasema
huyo shemeji kama kujinadi hivi, na Soldier, akamuangalia kwa makini halafu
akamuuliza shemeji yake;
‘Wewe wakati unamsaidia ulikuwa wapi, au ulitokea wapi…?’
akauliza Soldier
‘Nilijua tu utauliza maswali hayo..jibu lake ni kuwa
hayakuhusu maisha yangu, kwani wewe ni polisi, au.’ Akasema shemeji yake.
‘Najua maeneo hayo ni ya mpakani, na maeneo hayo ni sehemu
wanapopitia wauza magendo, na madaa ya kulevya, na wewe ni moja ya kazi
yako…’akasema Soldier
‘Nilijua hilo ndilo unalonitafutia, lakini kumbuka, polisi
wameshanishuku hivyo mara nyingi, tukaongea nao, nikwaambia wanionyeshe
ushahidi hakuna, wakanichunguza wee hawakuona kitu..unajua niwaambie nyie watu,
msifanye kazi kwa wivu…hilo ndio kosa lenu, mimi nahangaika kivyangu, napiga
dili zangu , kutafuta maisha yangu, hayo yanawahusu nini…’akasema
‘Tatizo lako wewe hufuati sheria,…na biashara zako sio
halali, kama ni halali kwanini unapita njia za magendo, kwanini huna lesoni
iliyotambulikana kisheria…ina maana kuna biashara zako sio halali…’akasema
Soldier.
‘Unajua wewe unajifanya sio mbongo, haya maisha ukiamua
kufuata sheria, utafanikiwa kweli, kuipata leseni ni mlolongo mrefu, na hapo
nia yao ni kukukata kodi nyingi tu, utapata faida kweli..ni maisha yetu ya
kawaida, uhangaike kwanza ukijiweka vyema utakata hiyo leseni yao,..lakini pesa
hizi za kubangaiza, biashara yenyewe ya msimu, ..je ukiwa huna pesa utalipia
nini hiyo kodi..usijifanye hujui maisha yetu….’akasema.
‘Hayo unaweza ukaongea na wahusika wakakuelewa, sidani kama
hilo ni tatizo, nikuulize wewe unafanya biashara gani rasmi…?’ akauliza
‘Hayo maswali ya polisi, sitaki, na usitake kunichefua, mimi
naweza kuwaambia polisi tabia yako ilivyo…’akasema.
‘Sawa kama unataka ukayajibie polisi hakuna shida, ni lazima
utafika huko, …’akasema Soldier.
‘Na wewe mdada mlikutana wapi na huyo mtu…?’ akauliza
Soldier.
‘Aliniokotea mpakani…nikiwa sijijui, ni mpakani mwa nchi
hiyo yenye vita na ncho hiyo inayofadhili wakimbizi…’akasema
‘Sawa kabisa nilijua ni kwanini hataki wewe useme ukweli,
huko huko ndio nia ya wauza madawa ya kulevya na biashara haramu, huwezi
kulikwepa hilo…’akasema Soldier.
‘Hahaha, hamna shida, tutapambana, hujui ni kiasi gani
nakufahamu wewe,…nina mambo yako mengi, na nikifika huko nayataja yote, sijali
kuwa wewe uliwahi kumuoa mdogo wangu, kwanza ndoa yenye haipo…’akasema
akimuangalia dada yake.
Dada yake alionekana hana raha, yaonekana kuna kitu kilikuwa
kinamkera, na alipoona watu wanamuangalia, akasema;
‘Mimi naona tunapoteza muda kwa maswala mengine, sijui lengo
lenu ni nini, hapa tuna jambo la awali, kutaka kujua, baba wa huyo mtoto ni
nani, dada kwanini humtaji mara moja tukajua moja, hayo mengine hayatuhusu
sisi…’akasema mke wa Soldier.
‘Ndio nilikuwa naanza kuelekezea ilivyo kuwa, maana kiukweli
hadi nafika hapa bado nilikuwa sijaelewa, lakini nikielezea wapi nilipotoka,
basi mwenyewe atajielewa…sitaki kumshinikiza mtu, sitaki mtoto wangu abakai
huku, nitaondoka naye..’akasema.
‘Ok, elezea wewe umetokea wapi..ilikuwaje, mpaka ukapata
hayo makovu, na hayo makovu yanaonekana uliiungua uliungua na nini?’ akauliza
baba akiwa kitandani.
‘Haya makovu ni athari za mabomu…nilikanyaga bomu, wakati
natoroka kutoka kambo ya wakimbizi…’akasema
‘What!.....Ukanyage bomu upone, haiwezekani…’akasema
Soldier.
‘Ndivyo ilivyokuwa ndio maana wengi walijua mimi nimeshakufa,….hadi
wiki iliyopita ndio niliweza kuongea na wazazi wangu, huko walishamaliza
matanga yangu, kwasababu waliambiwa hivyo…’akasema
‘Oh, yaonekana una hadithi ya kuvutia ya maisha yako, au
mlipanga hiyo hadithi wewe na dereva, maana inaonekana na wewe u mjanja-mjanja,
hebu tuhadithia hiyo hadithi vizuri….. ilikuwaje, mpaka ukatoroka huko porini,
tena kwa waasi, ilikuwaje ukafika kwa waasi, na mnashirikiana nini na hawa
watu, nataka ukweli vinginevyo nitakukabidhi kwa poliai…?’akauliza Soldier, na
huyo mdada, akaduwaa…na kutikisa kichwa, na kusema;
‘Ina maana huamini hayo ninayokuambia, kwahiyo sasa
unahitajia ukweli, sawa mimi nitausema ukweli wote, ,…najua ni kwanini
huaniamini, sasa mimi sitaki kuficha kitu tena,..nitauelezea ukweli wote hata
kama utawaumiza watu…’akasema huku akimuangalia dereva halafu shemeji mtu.
‘Shauri lako…’akasema shemeji mtu
‘Asikutishe huyu…huyu kwanza yupo chini ya ulinzi…’akasema
Soldier
‘Hahaha…soldier soldier, ungelijua,…hahaha,eti nipo chini ya
ulinzi, usngelijua kuwa mimi kuna mambo nakuhifadhia tu,kwa vile umemuoa dada
yangu, pamoja na uadui wetu lakini bado najali, lakini ipo siku, dada
akinielewa tu utaliona vumbi langu …’akacheka huyo shemeji mtu, halafu akageuka
kumuangalia dada yake, na kusema;
‘Jiandae, tuondoke…ukweli anaotaka kuongea huyo mdada,
utakuumiza, …na nisingelipenda uusikie…’akasema na dada yake akawa kama anawaza
jambo, halafu akasema;
‘Mimi naomba kwanza tuongea mimi na huyu mdada pembeni, nina
wazo kwake, na ….sioni kwanini upoteze muda wako hapa, wewe sema neno moja huyu
mtoto ni wa dereva, au Soldier, mimi nimeshajua huyu mtoto ni wa nani, nina
ushahidi,…lakini kauli njema ni ya mzazi au sio..sasa sema ni nani baba wa
mtoto, basi inatosha…’akasema
‘Dada kiukweli, hata mimi nimechanganyikiwa, ….kwa hivi sasa
hata sielewi, lakini nina imani kuwa mwenye atajijua, nikianza kuelezea
ilivyokuwa…, lakini kwanini nisielezee nilivyopata hiyo mimba, ..sikupenda,
…sikutarajia, naona ilikuwa ni mapenzi ya mungu…’akatulia.
Wakati anaongea hivyo
Soldier akachukua simu yake na kupiga namba, akasogea pembeni kidogo halafu
aakarudi na kusema;
‘Haya elezea…tusipoteze muda, nimeshapiga simu polisi,
wakati wowote wanaweza kufika hapa…’akasema Soldier
‘Polisi wa nini, Soldier sasa unataka kuharibu…?’ akauliza
shemeji sasa akiangalia mlangoni
‘Waache waje….’akasema huyo mdada na kuanza kuelezea kisa
cha maisha yake ambacho ndio chanzo cha kupata mtoto ….
‘Mimi nimezaliwa hapa hapa Tanzania, ila mama ni mzaliwa wa nchi
hiyo yenye machafuko, wasi wanapiga na serikali… na baba ni Mtanzania….wazazi
wangu walihamia kwenye hiyo ncho katika kutafuta maisha, walihamia huko kabla
ya machafuko na sisi tukiwa wadogo sana….’ Mdada huyo akaanza kuelezea….
NB: Tuvute subira tusikie kisa cha huyu mdada, na ndani ya
kisa hiki ndio utapata ukweli halisi wa mtoto, alipatikanaje.
WAZO LA LEO:
Kujenga chuki, na kutafuta sababu ya chuko, badala ya kujenga urafiki na
kutafuta njia za kuwa marafiki, ni dalili kuwa sisi hatuna imani thabidi na
muumba wetu ambaye katuagiza tupendane tuhurumiane. Watu kila mara hutafuta
sababu za kuchukiana, utakuta umimi, sisi…nk ndiyo mazungumzo yetu
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment