Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, November 24, 2016

TOBA YA KWELI-19



Mapenzi ni kitu cha ajabu sana, unaweza ukapenda kitu kwasababu ndogo tu., au ukachukia kitu kwasababu ndogo tu, na chuki inaweza pia kubadilika na kuwa upendo,  upendo huo ukawa wa dhati kupindukia.

Siku ya kwanza ikapita taratibu, ikaja siku ya pili, ya tatu,…sasa nikawa siwezi kuvumilia tena, nikachukua simu na kuanza kupiga, simu yam dada ikawa haipatikani,…kwanini simu yake haipatikani na mimi ninajua haina matatizo yoyote,nikawa kila mara najaribu lakini ilikuwa kimia…, nikawa najiuliza bila kupata jibu.

Kwanza nikawasiliana na docta, maana yeye ndio anawafahamu vyema huko kijini, mkewe anatokea huko..nilitaka wajaribu kufuatilia, ni nini kinachoendelea, na jirani yangu huyu…, docta akaniambia nitulie tu, nivute subira..

‘Wewe una wasiwasi gani, subiria kwanza…kuna mambo yatakuwa yanaendelea huko kijijini, shemeji yako anafuatilia kwa karibu, nitakujulisha mambo yakiwa tayari ’akasema docta, kumbe alishajua ni nini kinachoendelea.

Mimi nikamuuliza docta;

‘Je wakimlazimisha huyo binti kuolewa na hao watu wa huko kijini itakuwaje, wakumbuek kuwa wao ndio walimsikia mke wngu akitaka mimi nimuoe huyo binti, na wao wameshindwa kuwashawishi hao wazazi…na ilitakiwa wao waende huko wakamsaidie huyo binti maana nijuavyo mimi, huyo binti hawezi kuwakaidi wazazi wake...?’ Nikamuuliza docta na docta kwanza akacheka kwa mdhaha na kusema;

‘Sikiliza ndigu yangu kwanza hiyo sio kazi yetu, kazi yetu ilikuwa kusema ukweli, na ilitakiwa wewe ndio ufanya juhudi hizo toka awali..lakini hata hivyo, unawasi wasi gani, tusubirie matokea, huwezi kulazimisha hali halisi..mungu anajua zaidi…’akasema docta.

‘Kwani shemeji si yuko huko kijini anasemaje…?’ nikamuuliza

‘Anasema ….kuna vikao vya kila siku vya wazazi....na ni kawaida lakini, hasa kwa binti kama huyo ambaye wengi wamekuwa wakimtaka,…wazazi wanatamani vijana wao wamuoe binti kama huyo, kutokana na tabia yake…’ akasema docta.

‘Sasa kweli mimi watanikubalia…maana wananifahamu, ..lakini hawanifahami nilivyobadilika,..docta mimi nimebadilika kabisa, na siwezi kurejea tabia yangu ya zamani kamwe..hilo naapa…’nikasema

‘Mimi ninajua, lakini je wale wazee wanakufahamu hivyo…?’ akaniuliza

‘Sasa wewe nisaidie kwa hilo …’nikasema

‘Mimi wakinihitajia …nitajaribu kukutetea..., lakini siwezi kukuahidi moja kwa moja, unajua tena hicho ni kikao cha wazazi, wao kama wazazi wanajaribu kuona ni nani muhimu kwa binti yao...ila mimi nitajitahidi, hata semeji yako yuko huko anajaribu kadri ya uwezo wake, lakini mara nyingi, ....mtu baki hasikilizwi sana...muhimu kwasasa ni wewe umtegemee mungu wako tu, wewe ushaiva kiimani kwanini unalegeza imani yako…’akasema docta.

‘Oh…lakini ni lazima hapo nifanye juhudi ya kuwaaminisha kuwa kweli nina nia hiyo ya kumuoa binti yao, na mimi nimeshabadilika sio mimi yule wa zamani....ujue mimi sijapeleka mshenga wala kitu chohote zaidi ya kauli ya binti...'nikasema

'Ndio najua...'akasema docta

'Sasa wewe huoni hapo kuwa mimi na nyie kama ...wewe uwe mshenga wangu mnisaidie twende huko kijijini, nikajitambulishe kwanza, unaona eeeh….’nikasema

'Mhh...mimi naona bado...ngoja kwanza....'akasema docta

'Ningoje, wakati wenzangu wameshajitambulisha, naisikia na wengine walishaanza kutoa vitangulizi, unajua wazee wa kule..ukitoa zawadi zawadi wanakuthamini...sasa mimi sijafanya hivyo...'nikasema

'Wewe usijali bwana,...hata wakitoa, kama binti hataki je....mimi nina imani huyo binti sasa hivi anakutaka wewe....'akasema docta..hapo mimi niliona docta halichukulii kwa uzito wake, kama walivyokuwa wakinishawishi awali, nikahisi kuna jambo jingine limajificha, hawataki tu kuaniambia, na akili yangu ya haraka haraka ikahidi huenda ni hali yangu ya afya, huenda vipimo

‘Muda utasema jirani yangu, wewe vuta subira,….wala usijali…kama huyo binti kapangiwa kuwa ni wako ni wako tu…’akasema hivyo docta, niliona kama yeye hajali,hajui ni kiasi gani napata shida!

**********
‘Rafiki yangu, duwa ya…kumuomba mungu,ni silaha kubwa kwetu,wengi wetu hatulijui hilo, utasema mbona kila siku naomba, namuomba mungu…lakini je unamuombaje mola wako, maana kila mtu anaomba hata jambazi anaomba akienda kuiba au sio,…. Hebu kihalisia, tujaribu kujiuliza utakwendaje kuomba kazi kwa bosi fulani  ukiwa mchafu, unaweza kufanya hivyo kweli…huo ndio mfano wetu kwa mambo dhahiri ya hapa duniani,..

Ninajua  kwa mwenyezi mungu yeye haangalii miili yetu,usafi wa miili yetu na mavazi yetu…zaidi ni usafi wa mioyo yetu, uchamungu wetu…, ile ile nafsi inayotuamrisha tufanye hiki na kile ndiyo mola wetu anaiangalia zaidi, je imetii maagizo yake, tumeweza kuidhiti hiyo nafsi….,umeonaeeh…’akasema rafiki yangu akiendelea kunihadithia kisa chake…

‘ Na mimi mungu akanijalia nikawa nacheza na hiyo nafsi,…na kama ulivyoona nilianza kwa kutubia, kufunga kukesha na ilikuwa ni toba ya ukweli ya kutoka moyoni, na hiyo haikuwa kazi rahisi kama ninavyoongea hapa…unaweza ukasema hapa mdomoni tu, nimetubu, nimemuomba mungu wangu, nimeokoka, mimi ni msafi….lakini vitendoni ipo kazi,…ni kazi kubwa sana, na nafsi zetu ni kichaka na uhalisia, na hatuwezi kumdanganya mola wetu…’akatulia akitabasamu kidogo

‘Mhhh..sasa ilikuwaje huyo binti alikupigia kuwa imekuwaje, au ilikuwaje, .?’ Nikamuuliza, nilipoona haendi moja kwa moja kwenye tukio lenyewe.

*************
‘Hahaha.., anipiigie simu mimi…wakati alipofika simu ikachukuliwa, wazazi wengine wakorofi…kiukweli…haikuwa kazi rahisi kwa huyo binti, na ilifikia muda, akasalimu amri, na ikabidi ayafuate matakwa ya wazazi wake…’akasema

‘Kwahiyo ina maana hukuwahi kumuoa huyo binti…?’ nikamuuliza na hapo akakunja uso, kuashiria huzuni na huku akitabasamu pia, akasema;

‘Ilikuwa tukio la namna yake, na hapo ndio utafahamu toba ya kweli ilivyo..huyo binti alikubali kweli amri ya wazazi wake,…na ikapangwa ndoa, kabisa, akawa hana jinsi, akaridhia kuwa sasa anaolewa na chaguo la wazazi wake, na taarifa hiyo nikaipata,…na hata docta akaipata ndio akaja kwangu kunipa moyo, maana alijua nitakasirika sana, ninaweza kufanya mambo ya ajabu.

Ni kweli, taarifa hiyo ilinivunja nguvu kabisa, kwanza nilijilaumu kwanini nilimruhusu huyo binti aondoke, ni kwanini….ikawa nanilaumu kwa kila kitu…na hata kuwalaumu docta kwa vile hawakutaka tulichukulie kwa uzito wake, lakini docta akaniambia

‘Kiukweli hali ilipofika, hatuna jinsi….inabidi tu tukubaliane na hali halisi, …’akasema docta

‘Hapana mimi siwezi..ni lazima nifanya jambo, …yawezekana ni kwa vile mimi sijaenda huko…ni kwa vile sijatoa chochote….’nikasema

‘Wewe usijali, kama sio halali yako huwezi kuilazimisha, na wazazi wana mashaka na hali yako ya kiafya ,..hatuwezi kuwaumu kwa hilo,..ila bado hawajafikia uamuzi, ngoja tusubirie kwanza,..’akasema

‘Kwa vipi, …?’ nikamuuliza

‘Ninajua wao wanaweza kunipigia simu,…wanaiulize kuhusu wewe mimi siwezi kuwaaambia lolote zaidi, si unajua tena… naweza kukubali kuwa wewe umepona laini je nina uhakika gani kuwa umepona kweli,…maana vipimo vyako bado havijakubaliana na kauli hiyo, ndio maana hata mimi navuta subira, tuone mbeleni itakuwaje...bado kuna walakini..mimi naona tusubirie tu…’alasema docta.

‘Kwahiyo unataka kusema nini, kuwa wao wamepitisha hayo kuwa mimi ni mgonjwa, siwezi kuzaa au sio…je wao, wana uhakika gani, wanajua matakwa ya mungu, mimi siwezi kukubaliani na hilo ndio maana mimi ninataka kwenda kuonana na wao , ili niwathibitishie kuwa mimi nimepona…’nikasema

‘Una uhakika gani kuwa umepona, maana vipimo bado havionyeshe hivyo, ila kuna dalili kuwa umepona, unanielewa hapo…?’ akaniuliza docta

‘Kwani vipimo vyangu vinasemaje, kuna dalili kuna dalili, mbona unaitia mashaka, mbona mwanzoni ulinipa matumaini kuwa nimepona…?’ nikamuuliza docta na docta hakuweza kunipatia jibu la moja kwa moja, lakini mimi nilishajiona nimepona, sikuwa na shaka na hilo, na sikuweza kusibiria kama alivyosema docta , mimi kesho yake, nikafunga safari kwenda huko kijijini kabla ili niweze kumshawishi huyo binti,, lakini sikuweza kuipata nafasi hiyo.

Ndugu yangu kuna mlolongo ulitokea, kuna mengi yalitokea, na naona kuna umuhimu wa kuyasimulia hayo kwa manufaa yetu, na vizazi vyetu. Tutasimulia kidogo tu ilivyotokea na na ndio itakuwa hitimisho la kisa chetu,....mungu akipenda.…’akasema msimuliaji

NB: Haya,..ndio hivyo,...tukae mkao wa kula ili tupate hitimisho la kisa hiki, sikuweza kukimalizia kisa hiki kwa leo,maana jino linanisumbua,…tukutane kwenye hitimisho mungu akipenda

WAZO LA LEO: Wakati mwingine inabidi tukubaliane na hali halisi, ..wakati mwingine hali halisi inatokea nia ni kutupima jinsi gani tulivyo, na huenda ikawa ni kwa manufaa yetu , au ni mtihani tu, tukitulia na kufanya subira tunaweza kupata kile tunachotaka kwa muda muafaka


Kwahiyo likitokea jambo, likawa linakwenda kinyume na matakwa yetu, tusikimbilie kulaani, kulalamika, kulia, na hata kukufuru, na wengine hujenga chuki kabisa, na kumchukia kila mtu..muhimu …tuache hali halisi ifanye kazi yake na mwenyezimungu anajua zaidi. 
Ni mimi: emu-three

No comments :