Profesa
aliposikia hivyo akakumbuka jinsi alivyosikia habari za huyu mpelelezi wa kujitegemea,ilikuwa siku ile wakijipongeza wakiwa na mtaalamu wa dili na mitandao.
‘Katika kazi
hizi zetu kuna watu wanasifika sana kupekenyua, I mean wapelelezi, idara
hiyo ina wapelelezi wa namna nyingi...siogopi sana, polisi....’akatulia
‘Polisi
nimeshawasoma,na najua jinsi gani ya kupambana nao, ili mradi tu, kusitokee
mauwaji...’akasema
‘Ila kuna
hawa, wapelelezi binafsi, hawa njaa mbaya,....hawa ni wabaya sana, hasa katika
upelelezi wa hizi dili zetu...kuna mtu mmoja mbaya sana,..., mtu huyu
wanamuamini sana,...kiukweli kazi hiyo anaiwezea sana kuwafichua watu wa
mlungula,....’akasema
Ni nani
huyo...?’ akauliza
‘Ni askari
mmoja njaa kali, anaitwa Njagu...’akasema Mtalaamu siku wakisherehekea fungu la
kwanza kutoka kwa mtu wao.
‘Njagu,
ndiye huyo...?’ akauliza kama vile hamfahamu
‘Ndiye huyo
huyo aliyepewa kazi hiyo na mama mtemi, mpaka akakupata ....unajua ni
kwanini..?’ akawa kama anauliza
‘Hapana
..hata mimi nilishangaa sana...maana mambo yangu yalikuwa ni siri kubwa sana,
sikumhusisha mtu....’akasema
‘Hukuhusisha
watu, hahaha, wewe hukuenda kuwauliza baadhi ya watu kuhusu maisha ya huyo mama,
ukapita huku na kule, unajua mimi huyo mama namfahamu, na kwa vile namfahamu
sitaki kabisa kumuingilia, tunajuana na hatuingiliani, unasikia sana, sasa
kwanini ulimfuata huyo mama.....?’ akauliza
‘Nilikuwa
sijui,...unajua kila ninapofanya kazi kwa mtu nikipata sababu ya kupata pesa,
huwa siangalii huyu ni nani...ndio hivyo tu,...kwahiyo nilipopata nafasi hiyo
ikabidi nidadisi kupata uhakika...’akasema
‘Basi kwa
kufanya hivyo, ulijichora, uliweka nyayo za miguu yako kila ulipopita..’akasema
‘Mhh...nilikuwa
makini sana, sikuuliza kinamna ya kujiweka wazi...’akasema
‘Kwa mtu
kama njagu, dalili ndogo tu, inamfanya ajue mengi...namuamini sana kaika
upelelezi,..unajua polisi walifanya makosa kumsimamisha mapema huyu mtu,
wangemfunda, na kumtumia katika kuwatafuta watu kama nyie...’akasema
‘Eti watu
kama sisi, wewe je....eeh,Ina maana aliachishwa kazi idara ya polisi...?’
akauliza
‘Alikuwa
askari mpelelezi wa ngazi za juu..., akafanya makosa mengi tu, wakamsimamisha
kwa mujibu wa sheria..lakini sio kwa kumfukuza, kilichotumika ni yeye
kujiuzulu...ilitumika hekima fulani aonekane hakufukuzwa....na ndio maana
wakampa kibali cha upelelezi wa kujitegemea...’akasema
‘Mhh, mtu
mkosaji lakini bado wampe leseni, ....hapo siamini....’akasema
‘Polisi ni
wajanja, wao wanataka kumtumia kama mpini kwenye shoka,...na ni kweli kwakupitia
yeye wameweza kuwakamata wahalifu wengi tu, kwa vile yeye alishahusishwa na
makundi ya wahalifu,na nia yao kwasasa ni kutaka kuja kumkamata hata yeye
lakini wanatafuta ushahidi wenye mshiko....’akasema
‘Kwanini
sasa wamuogope...?’ akauliza
‘Sio
kumuogopa...kama ulivyosikia, nyuma kulikuwa na kundi baya la wahalifu, na ni
kipindi hicho Njagu alikuwa kashika usukani, ...idara ya polisi , katika
kuchunguza wakagundua kuwa, alikuwa na mahusiano kwa namna moja au nyingine na
haya makundi....’akasema
‘Kwa
vipi...?’ akauliza
‘Huyu jamaa
ana tamaa, alikuwa akipata pesa kutoka kwa wakuu wa haya makundi, japokuwa
haikuonekana moja kwa moja....na mmoja wa wakuu wa hayo makundi anafahamika, ni
huyo mama mtemi,...ndio maana unaona wapo sambamba....huyo mama anafahamu
makundi yote ya mitaani, na huyo Njagu, halikadhalika....’akatulia
‘Mhh,
kumbe.....’akasema
‘Kwahiyo uwe
mbali na hawa watu wawili, huwezi kuwaficha kitu kuhusu ujambazi, kuhusu mlungula,
kuhusu......wanajua kila kitu...’akaambiwa
‘mhh kumbe, Ningelijua...’akasema
‘Hahaha..ungelijua,
kama uliingia anga zao, ujue unao..ujue unalo,..hasa huyo mama hatakubali mpaka
ahakikisha haupo,... unapotea, au unakwenda kuozea jela, na huko jela ana watu
wake, ukiingia huko wewe ni maiti mtarajiwa....’akasema
Alipoyakumbuka
hayo, ndio maana akauliza swali hilo kwa mashaka;
‘Oh,...ina maana kumbe keshamtafuta mpelelezi
tayari, na ni nani huyo
mpelelezi,ni...Njagu nini...?’ profesa
akauliza
*********
‘Ndio ni
huyo huyo,NJAGU...unakuambuka nilishakuonya kuhusu huyo mtu...’akasema
‘Nakumbuka
ndio maana naogopa sana....’akasema
‘Hata hivyo kwangu
mimi simuogopi sana huyo mpelelezi ...’akasema mtaalamu
‘Kwanini, na
wewe uliniamba kuwa huyo mpelelezi anayafahamu makundi yote ya wakorofi hapa mjini
na ni mtu makini sana, tofauti ni kuwa ana tamaa sana...’akasema
‘Ni kweli,
ila mimi ni mjanja zaidi yake,...mtalaamu wa mambo yote yanatokea , yeye
mwenyewe ananifahamu kwa hilo , ...ananifahamu
na namfahamu...., ‘akasema
‘Kwahiyo...?’
akauliza profesa
‘Ila ikibidi
nitaongea naye, ila kwa jinsi alivyo na tamaa, na njaa yake kali, atahitajia
pesa hapo ndipo nampatia.... huyo mtu yupo mkononi mwangu,hanitishi kabisa
lakini kuwe na pesa ya kutosha, unaona ilivyo, iabidi nitumie pesa nyingi sana
wakati mwingine, ila kwa huyu nafahamu sehemu gani ya kumpatia, hanitishi.....’akasema
mtaalamu
‘Unataka
kusema nini sasa...?’ akauliza Profesa
‘Huyo mtu
nimeshamsaidia sana,... vinginevyo angelishakamatwa kwa makosa ya uuaji, unajua
katika kuziba mapengo yake alijaribu sana kuwanyamazisha wale wote waliotaka
kutoa taarifa zake,...nina skendo zake nyingi tu, ana mauchafu yake mengi
nimeyahifadhi,....hata hivyo kwa sasa nataka nione nyendo zake...anataka
kufanya nini..., najua mwisho wa siku atanijia kutaka taarifa fulani fulani..’akasema
‘Mhh
kumbe....nimekuelewa,kumbe hata hao watu wanakuja kwako..’akasema kwa kuonyesha
mshangao
‘Huyu mtu ni
mjanja sana yeye anawashinda watu wa usalama kwa vile anauma huku na huku,
anachua vichochoroo vyote vya watu wakorofi, anakula nao,unasikia sana.....ile ukijifanya
kumuendea kwa kasi anaweza kukushushua ukajiona mjinga,..mimi sio mjinga, mimi
ni mjanja, na kwahiyo nahitaji njia za kumbana....’akasema
‘Kwahiyo
utanisaidia au sio maana hii sasa inahitajia utaalamu wako au sio....?’
akauliza
‘Nitakusaidia...hahaha
kwa vipi, mimi nazungumzia upande wangu, kama atapewa kazi na huyo mtu, najua
mwisho wa siku anaweza kunifikia mimi,....sasa...nitapambana naye...nina hamu
sana ya kupambana na huyu mtu maana kila
akipewa kazi anajaribu kunipima, anataka kupambana na mimi ili nionekane mimi
mjinga.....’akasema
‘Mhh, mimi
hata sikuelewi, ina maana unafanya mzaha...hii sio kazi ya kupimana ujanja,
...huyo ni mpelelezi, na hana tofauti na watu wa usalama,sema ni kwa vile
anaifaya kibinafsi, au sio, sasa hapo hapataki mzaha ....’akasema
‘Hahaha,ukiwa
kwenye anga zangu, wakati mwingine, unahitajia changamoto, unapopata
changamoto, unaongeza utaalamu zaidi, unajua kipi kimepungua ili ukitafutie
ujuzi zaidi, sijapata changamoto kwa muda sasa, akili yangu imelala, .....’akasema
‘Mhh,
...hapo sitakuelewa...’akasema
‘Sio kazi
yako kunielewa,...wewe fanya yako yanayokuhusu....mimi najua jinsi gani ya
kujilida,....hili eneo lipo kwenye anga zangu, nawaona wote mchana mkihangaika
na usiku mkitenda yasiyotakiwa,na mimi
hapo ndio nawashindia watu wangu, usiwaone watu wamevalia masuti mchana,
usiku ni watu wabaya sana...’akasema.
‘Mhh,
ungekuwa kwetu ungeitwa mchawi...’akasema profesa
‘Mhh,lakini
mchawi wa utaalamu wa kisasa......sasa eeh, unataka nini zaidi...?’ akasema
‘Najua kuwa hii
sio kazi yako, lakini kumbuka unachezea shilingi chooni, pesa hiyo tunaweza
kuikosa na ni pesa nyingi, ...tukiiachia, kwa kutaka kupimana na huyo mtu,
itakuwa ni hasara...’akasema
‘Kwangu mimi
sio hasara,...sifanyi kazi ya hasara....najua ni nini ninachokifanya...’akasema
‘Sasa huoni
kuwa kuna kukamatwa na watu wa usalama kwa makosa kama hayo...wewe unabuni dili
za kuwadhulumu watu haki zao kwa kutengeneza uchafu wao na kuwatishia nao, kwa
minajili ya kupata pesa...’akasema profesa
‘Mimi siwadhulumu
watu, mimi natumia ujuzi wangu kwa manufaa ya kuzalisha, ujuzi ninao, sasa
niupeleke wapi,....nitangaze dini, hahaha, nikuambie kitu, mimi siogopi
kukamatwa, hasa nai mtu kama njagu....huyo ndiye kabisa haniwezi kunikamata kwa
kosa lolote, ....mimi ni mtaalamu bwana....’akasema huku akicheka
‘Mhh,....’profesa
akaguna tu
‘Njagu,...anajua
hilo, ila anaweza kuwakamata watu kama nyie, watu ambao anafahamu hawawezi
kupambana na yeye..., hilo ndugu yangu siwezi kukuficha,huyo jamaa akiamua
atawatia hatiani...lakini sio mtu kama mimi
...’akasema
‘Kwanini na
wewe ndiye unayetupa hizo dili....?’ akauliza profesa
‘Unajua
sheria wewe, ...wewe ni mtoto mdogo, uambiwe ukaibe, ukaue,...hna unajua ni kitu
kibaya, ufanye halafu useme nilielekezwa na yule.....haiji ....’akatulia
‘Halafu mtu
mwenyewe yule pamoja na ujanja wake wote wakati mwingine ananitegemea mimi, hapo
ndipo mimi namshidia, mimi ni mjanja...hahaha’ akacheka kwa dharau
‘Hata
hivyo,.... ni lazima nifanye jambo,maana dili hii ina pesa nyingi, na huyu
jamaa akianza kazi ya kuchunguza, ni lazima atanusa , atajua kuwa dili hii ina
pesa, na akijua hilo, mhhh, atazing’ang’ania, unaona eeh,.... sasa mikono
itakuwa mingi na hapo sizani kutakuwa na kitu cha maana, pesa itapungua sana....’akasema
‘Umeonaeeh,
tutapata pesa ndogo kwa kugawana watu wengi au sio...sasa hakikisha unanisaidia,
...si unaliona hilo,....sasa tusaidiane,wewe wabane hao watu, hasa huyo
mpelelezi, ili niwewe kucheza na huyu mtu wetu au sio...’akasema
‘Kiukweli hii
pesa itakuwa ndogo sana,vinginevyo watu wapungue ....sasa ni nani
atoke.....’akawa kama anauliza
‘Nani
atoke.....?’ akauliza profesa
‘Kwanza
ukumbuke kwa mimi kulifanya hili inakubidi wewe uongeze kiwango changu cha
ushuru, hicho ni kitu baki kabisa....sasa kama unataka niendelee kukufuatilia mambo
yako, hayo ni makubaliano mengine ..kwani hiyo ilikuwa ni kazi yako, subiri
nipige mahesabu kidogo hapa eeh,....’akasema huku akiwa anafanya mahesabu yake.
‘Mtaalamu
wewe nakuaminia,kwa hivi sasa inabidi iwe hivyo,ila kwanza kumbuka ombi langu
ni muhimu sana, nipate pesa kwa ajili ya huyo mama...na...mtu kama Njagu,
siwezi kupambana naye sijui mengi sana kumuhusu yeye,...hilo nakuachia wewe au
sio...’akasema
‘Kwa mtaji
huo , itabidi Njagu aingie kwenye mgawo,....sasa tutakuwa watu wengi,...mhh,
kipato kitakuwa kidogo, aah, haitoshi lazima watu wapungue,....’mtalaamu akawa
anaendelea kupiga mahesabu yake.
‘Mimi hapo
unaposema kupungua ni nani wa kupungua maana sote ni washika usukani, utamtoa
nani, ....hebu nambie...sikuelewi hapo kabisa....’akasema profesa.
‘Huwezi
kunielewa...lakini mwisho utasema....’akasema profesa
‘Na ukumbuke
pia, huyu mtu wetu pia, kama ulivyoshauri, ....sijafika kwake kwa muda sasa,
ningekuwa nafika pale nyumbani kwao, ningelijua ni nini anachokifanya,unaona
hilo,kwahiyo hapo nakutegemea wewe pia kujua kinachoendelea ili nikiongea naye
asije kuniona tapeli...’akasema
‘Tapeli,
tapeli mara ngapi.....mmh, ukimweka njagu hapa....’ilionekana mtaalamu
alishazama kwenye mahesabu ya pesa.
‘Lakini
mtaalamu, wewe umezama kwenye mahesabu ya pesa, Je kweli huyo jamaa atazitoa
hizo pesa....usipige mahesabu ya pesa wakati hujajua kuwa zitapatikana kweli
wakati mkewe keshaziingilia, hilo kwanini hulioni...’akasema profesa
‘Poaaah,
sasa.....nimeona kitu, ila zitakutoka pesa nyingi sana, kwasababu Njagu
ni lazima aingizwe kwenye mgawo...na usikie kabisa mimi sina pesa kwa ajili ya huyo mama
mtemi, kwahiyo sitaki kabisa hilo wazo lako la kuwa mimi nikukopeshe pesa kwa
ajili ya huyo mama, hiyo pesa hapa kwenye mahesabu naiondoa haipo....’akasema
‘Lakini sasa
nitapatia wapi pesa za kumpooza huyo mama, namfahamu alivyo, nikimpa kitu
kidogo, atalainika...., na kiukweli bila kuwa na pesa huyo mama ataniweka
kubaya, atanifunga, na mimi siwezi kwenda jela, najua nikienda huko wataniua...’akasema profesa
‘My,
my.....ok, sasa.....mhh, pesa itakuwa ndogo sana, ...ngoja nione cha kufanya,....kwa
hali hiyo, ukitoa ushuru wangu, kitakachobakia ni nusu kwa nusu,nuusu kwa nusu eeh, nusu kwa yap...’akasema
'Nusu kwa nusu....!?' akauliza profesa hakuwa anaelewa mwenzake anafanya nini huko, hakujua kuwa mwenzake akili yake imezama kwenye mahesabu
‘Unaona hapo,
na nusu yako sasa, itabidi ugawane na Njagu,... na wala sio nusu kwa nusu,
maana hao kwanza, ....mmh hii ni kutoka kwenye nusu yako, au sio,..utakuwa na deni langu, halafu itakayobakia
unagawana na Njagu,...sasa hapo sawa....huku kwako, kunaisha,..., sijui kama wewe utakibakia na kitu,..sizani ngoja tuone...mmmh huyu Njagu atalalamika ...vinginevyo, wewe u-o-ndo-ke,....mmh, sijui...’akasema mtaalamu
‘Haiwezekani, unasema nini...
hapo utaniumiza nitawezaje kulipa madeni ya watu, unajua mimi nadaiwa sana,
mama mtemi, kuna madeni mengine, nilikuwa nakaa hotelini, kwani si unajua tena,
sina pa kuishi.....’akalalamika profesa
‘Haya kama unaona
utaweza kufanya kazi kazi mwenyewe,... basi,beba mzigo wako mwenyewe, ila...mmh hapana , utaharibu kabisa hii dili nikikuachia mwenyewe, unajua
unaniharibia mahesabu yangu,..halafu naona kwa jinsi ilivyo, wewe sasa
utaniletea kiwungu -cheusi,sijui niifanye hii kazi mwenyewe, na Njagu, wewe ni gharama
tu, hasara tupu ...’akawa anasema
‘Peke yako
kwa vile imeshafikia sehemu ya kuchuma ndio unataka kunisaliti au sio, ujue
pesa haijapatikana bado na mimi ndiye atakayefanya ipatikane...unaona hapo,
sasa mimi nakuwa gharama kwa vipi, wakati ndiye mtafutaji...wewe nisaidie hao
watu unasikia mtaalamu, usije kufanya ujanja ujanja wako....nakuelewa wewe
,umeshaanza tamaa zako....’profesa akawa analalamika
‘Unajua
umeiharibu sana hii dili, sikupenda, ulivyoendesha hii dili, unajua nilikuamini
sana, lakini umeharibu kabisa, umefanya mambo utakavyo wewe....unajua
ulichofanya...unajua ulichokifanya mpaka naingia gharama nyingi zaidi...unajua
au nikuambie?’ akauliza
‘Kwani
nimefanya nini kibaya zaidi, au unanitafutia visa ili niachane na hii dili...ni
huko kukuomba pesa ndio imekuwa ni tatizo...kuna kosa gai jingine nimefanya,
acha tamaa na roho mbaya ...?’ akauliza
‘Kwanini
ulimuhusisha huyu jamaa jambazi,kwenye hii dili,sikukuambia umuweke, na hilo ni
kosa kubwa sana, kwanini ulifanya hivyo....?’ akauliza
‘Jamaa gani huyo,
ni jambazi gani huyo, mbona ...zaidi ya yule binti ambaye alikuwa ni...ndiye
kitega uchumi chetu, hakuna mtu mwingine kwa upande wangu, wengine walikuwa
wakisaidia tu...na ni kazi yao,mtu kalewa, inabidi kubebwa,kuwekwa
sehemu...ndio hivyo tu...sasa ni nani mwingine...’akasema
‘Huyu
jambazi kaka wa huyo mdada, kwanini ukamuhusisha kwenye hii dili, unamfahamu
sana huyo mtu...umeongeza gharama....unaona hapo....’akasema
‘Kaka yupi
huyo, mbona unanichanganya,...mbona mimi sijafanya hivyo...kaka yupi una maana
kaka wa huyo msichana tuliyemtumia kwenye hii dili..hapana mimi wala sijawahi
kuongea naye..., kwanini unasema hivyo?’ profesa akahisi mwili ukimcheza kwa wasiwasi
‘Usijifanye huelewi,
usinifanye mimi ni mjinga...huyu mtu ni mbaya sana...katika watu nisiopenda
kufanya kazi nao, huyo ni wa mwisho kutoka juu,...yaani hafai, haaminiki,ni
tapeli, hatosheki, ni muuaji, jambazi,...ukifanya
naye kazi ni lazima akuzunguke, ....sasa hivi kwa taarifa yako huyo mtu anakufuatilia
kwa karibu sana, sijui utamkwepaje, maana ni kupe...’akasema mtaalamu
‘Yupo
wapi...?’ profesa akasema huku akigeuka nyuma, alijisahau kuwa yupo kwenye
kibanda cha simu
‘Mimi
nijuavyo, huyu mtu aliondoka na dada yake , kwani yeye ndiye mlinzi wa huyo mdada, na hawezi kumuacha huyo dada
peke yake, ndivyo alivyonielezea huyo
mdada...au unataka kusema nini, una uhakika umemuona huyo jamaa akinifuatilia...nambie
ukweli,....ananifuatilia kwa lipi...eeh?’ akauliza na kugeuka huku na kule,....
‘Na hata
hivyo mimi sikumshirikisha kabisa, hakuwepo kabisa kwenye hilo tukio....’akalalamika
profesa
‘Ok,ok...mimi
kwa hilo halinihusu,....hilo utalibeba wewe mwenyewe,...kama unahisi
nakudangaya, basi, after all, I have
finished with you,....’akasema
‘Una maana
gani kusema hivyo,....umemalizana na mimi kwa vipi....?’ akauliza
‘Kiukweli,
nimeshachoka na wewe, ...ila kwa kukupa tu angalizo, ukipata kiasi chako, kama kweli utapata, kama
kweli utabakiwa na kitu, ujue huyo jamaa unaye, huyo ni kupe keshakuganda...sijui
mtagawanaje...’akatulia
‘Sa-sa-sa
kwanini.....?’ akauliza
‘Usije
ukasema sikuku-tahadharisha, ....unanifahamu sana, mimi sisemi kwa kukisia, nakupa
tu kama angalizo,...huyo mtu unaye, na
ukumbuke huyu mtu ni muuaji, na hasiti kuua pale kunapokuwa na pesa.....na alivyo,
...ni tabia yake haiachi, ni lazima akuzunguke kwenye kazi yoyote, akijua una
mshiko, hata kama haimuhusu, he is a master in double crossing....utakuja
kuniambia....’akaambiwa
‘Mhh, lakini...anaingiliaje
,anahusikaje...maana kiukweli nilishamuhisi vibaya, nilipoongea na yule mdada,
nikamkanya kabisa kuwa huyo jamaa simtaki, na huyo mdada akasema huyo jamaa hatahusika,
yeye ni mlinzi wake tu........’akasema
‘Ok,...its
over, tumalizane kwa haya mazungunzo,nenda kawajibike, ....hakikisha unafanya
yale tu niliyokuelekeza, .....sijui kama umenielewa....ok’akasema
‘Nambie
ukweli, kuhusu huyo mtu je umemuona akinifuatilia,...?’ akauliza profesa
‘Mimi
sipendi kurudia rudia mambo, naona wewe huniamini, wewe ni mtu pekee
asiyeniamini.....na mtu kama wewe sitaweza kuendana naye kabisa.....sijui kama
nitafanya dili na wewe tena....’akasema
‘Sio kwamba
sikuamini, ila kiukweli, mimi nilimwambia huyo mdada sihitaji mtu mwingine, hususani
huyo kaka yake,....kwahiyo kama umeona anahusika, labda ni kwa vile umemuona
akiwa karibu na huyo mdada,kama mlinzi wake au sio....ulimuona lini
akinifuatilia...?’akasema na kuuliza
‘Sawa hamna
shida....’akasema profesa akisikika kwenye simu akiongea na watu wengine.
‘Mtaalamuu
hebu niambie ukweli kama umemuona huyo mtu hivi karibuni, au ni kiona mbali
chako tu kinhisi hivyo...na wewe kwa ramli bwana, ...’akalalamika
‘Ramli eeh,.mimi naiga ramli eeh, ....Ok, but
nakuambia ukweli, my brother wewe upo kubaya,huyo mtu unaye, utakuja kuniambia, ....anyway, its yu’baby,....na sina la
kufanya kwa hilo...huyo ni ndumila kuwili, double
crosser, jambazi, muuaji,....na .....sijui
utafanyaje,...sijui...na sitaki kujua, ...’akasema
‘Oh,...ina
maana ni kweli.....?’ akauliza profesa
‘Unajua
....nimekuchoka,..hivi wewe ni nani kwangu, na nitakubeba kiasi gani kiukweli my brother hubebeki, na sijui...i wish, niimalizie hii dili
mwenyewe...maana hata ikiisha naona wewe utakuwa ni mzigo kwangu....,kwa
mahesabu yangu, naona huna chako kabisa, hutabakia na kitu,....am’ sory to tell you that..’akaambiwa na
simu ikakatika.
Profesa
akahisi mwili ukimcheza kwa woga, hasira, ...akihisi kuzungukwa na maadui kila upande,
akajua sasa keshatapeliwa, hata hiyo kazi sasa hatapata kitu,lakini hana jinsi
anahitajika kuimaliza hiyo kazi ili kupata pesa... ..
‘Hahaha,
hawanijuau hawa watu eeh, mimi ni mtoto wa mjini, nimekulia manzese.....hahaha,
tutaona...wanataka kunidhulumu, tutaona....ila mhh...kupe, ...ina maana kweli
ananifuatilia,....’akasema huku akitoka kwenye kile kibanda cha simu.
Na ni kipindi
kile wakati profesa anatoka kwenye kibanda cha simu,.....
Akiwa na
mawazo mengi, akiwa hana uhakika wa kupata pesa, na akiwa keshatishiwa kuwa ana
kupe keshamganda. Mara ghafla wakati anatoka nje ya kibanda, akajikuta anagongana
na jamaa,....
Huyu jamaa
alikuwa akija kwenye hicho kibanda kwa kasi, kama vile anawahi nafasi au...na
wakajikuta wanagongana bega kwa bega, profesa akajikuta akipepesuka na huyo
jamaa akamuwahi kumdaka,...
Kama
isingelikuwa huyo jamaa kumdaka mkono profesa, basi profesa angelidondoka
vibata sana,...na ile hali ya kugongana bega kwa bega,profesa alihisi maumivu makali
kwenye bega, na maumivi hayo yakasambaa mwili mzima, yaonekana jamaa huyo ana
mwili mgumu kama chuma.
‘Mhh....’akajikuta
akigugumia kwa maumivu
Akainua uso
kumuangalia huyo jamaa, hajawahi kugongwa
hivyo na kuhisi maumivu makali hivyo, ni heri angeligongana na chuma chenyewe,...
akataka kuhakikisha kuwa huyo mtu ni mtu kweli au ni roboti la chuma,...akainua
kichwa kumuangalia huyo jamaa, wakati huo ameshikiwa mkono, ili aweze kusimama
vyema.
Mtu huyo
huyo alikuwa kavaa kofia pana,kama vile kuficha uso, na mawani meusi machoni...
‘Oh... am’ sory....nilikuwa nawahi kupiga simu
....’huyo jamaa akasema, akiyavua yale mawani yake, na kumtupia jicho profesa,
na macho yao yakakutana,....
Profesa akahisi moyo ukimlipuka kwa mshituko, badala
ya maumivu sasa mwili ulitawaliwa na woga, akahisi miguu ikimtetemeka kama
aliyeshikwa na ubaridi wa ghafla,....., hakutegemea kukutana na huyu mtu
kabisa...akabakia kaduwaa,mdomo wazi..
Huyu jamaa
akajifanya hajali, akimuachia profesa mkono huku akisema;
‘Its you again...hahaha....’akasema na
kuingia kwenye kibanda cha simu, kama vile hana habari na profesa.
NB: Ni nani
huyu
WAZO LA LEO: Mipango mizuri ya haki na ukweli, ya
mambo ya heri, hutokana na malengo yenye fanaka na matarajio yake ni matunda
yenye neema...., lakini kama mipango hiyo ni kuhusu dhuluma, hata mikakati yake
huwa na kasoro, na mwisho huishia kutapeliana,
na kunyang’anyana hicho kilichopatikana, maana pato la dhuluma kamwe halina
baraka.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment