Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, May 13, 2015

NANI KAMA MAMA-76


‘Rafiki yangu kabla hatuajendelea huko sisi tuna hamu sana ya kusikia jinsi gani uliyochukuliwa na mama yako, na ile familia iliyokulea ilikuwaje, ..nesi yupo wapi, hukuwahi kuonana naye tena…na yule mume mwenye nyumba na mama yako mlezi, hamkuwarudia kuomba msaada…?’ nikamuuliza

`Ukumbuke kuwa mama ndiye aliyekuwa akinisimulia hiki kisa, na mama alikuwa akinisimulia huku akiwa kalala kwenye kochi, kwani mwanzoni nilikuwa nimekaa naye na kichwa chake kilikuwa kwenye mapaja yangu, lakini baadaye nilipokwenda kumchukulia maji na dawa ya kutuliza maumivu, akawa kalala kwenye kochi…

 Mnakumbuka sehemu hiyo mama aliposema;

‘Mwanangu nitafutie nauli niondoke…sitaki niwakosanishe wewe na mke wako, lakni kabla sijaondoka, nataka nikuhadithia maisha yangu yaliyopita, ambayo hujawahi kuyasikia,….’ Akasema na mimi nilimuambiaje;

‘Mama nilishakuambia huwezi kuondoka hapa nyumbani, ..huwezi kuniacha..’nikasema na mama akasema hivi

‘Hapa ilivyo mke wako keshatoa tamko, ama mimi ama yeye…je unahisi hapo utafanya nini, …huwezi kumuacha mkeo kwasababu yangu mimi, hilo silikubali, mke wako ni muhimu sana,….’akasema mama

‘Mnakumbuka sehemu hiyo…?’ akatuuliza

‘Ndio…kwani ilikuwaje kwa mama mpaka ashindwe kuendelea kuongea..?’ nikamuuliza

‘Sikujua kuwa japokuwa mama alikuwa kiongea kumbe kichwa kilikuwa bado kinmuuma, ila alitaka kuhakikisha nafahamu wapi nilipotokea, kwahiyo akawa anajikaza tu..huku anaumia ndani kwa ndani..na jinsi muda ulivyokwenda hali yake ilikuwa inajionyesha sasa, hali yake ilikuwa sio nzuri…, ‘akasema

‘Oh ina maana mama yako,…alikuja kufa…?’ jamaa mmoja akauliza

‘Mama hali yake kwa muda ule ilikuwa mbaya,…mimi nikawa nimekaa pembeni yakenikimsikiliza, akili ikiwa imetekwa na hayo matukio ya nyuma…nikawa nikimsikiliza tu anavyohadithia hayo yote niliyowaelezea... Lakini baadaye nikaja kugundua…, kuwa kila muda ulivyokuwa ukienda sauti ya mama ilikuwa ikibadilika, ilikuwa inakuwa ndogo,  yaani sauti ilikuwa kama inafifia…’akasema

‘Nikawa mara kwa mara najaribu kumchungulia, nikajua ni kiu, kwa vile kaongea sana, basi nikainuka na kumpa maji, akanywa kidogo tu na kuendelea kusimulia kisa hicho kama nilivyowahadithia huko nyuma…’akatulia

‘Lakini jinsi muda ulivyokwenda , na ndivyo sauti ya mama ilivyozidi kufifia ikawa nasikia kwa shida…nikaingiwa na wasiwasi nikijua kuwa mama hali yake sio nzuri. Na lipofika ile sehemu ambayo nesi alikuwa akifurahia kumuona dada yake ni mja mzito, wakiwa kule kijijini, hapo nikajua mama sasa sio tatizo la sauti, …kwani ghafla mama  akanyamaza kimya.

‘Mama vipi mbona unaonekana hupo sawa sawa…?’ nikamuuliza

Mama akatikisa kichwa, akainua mkono na kushika kichwa, alikuwa kama kapitiwa nausingizi wa ghafla,  akasema kama vile yupo usingizini,

 ‘Mwanangu…mwanangu..nashindwa kuongea zaidi…nguvu inanishia, ila mwanangu usikate tamaa ya maisha..utafanikiwa tu, nimeridhika kuwa wewe huna kosa, japokuwa ulaghai wa wake unaweza kumteka mume asijue thamani ya mama yake, siwezi kukulaumu kwa hilo, kwani huyo mke ni dhamana yako, umekabidhiwa na wazazi wako,…lakini mama ni mama tu…’akasema

‘Mama mimi nakupenda, …’nikasema

‘Mwanangu nafahamu kuwa kweli unanipenda sana mama yako na kweli huna kinyongo na mimi kama mkeo anavyodai kuwa eti mimi nimewaloga…mimi niloge damu yangu anajua wapi ulipotokea, kwanini nisingelikuua huko…kwanini nikahangaika nilivyohangika ukiwa huna mbele wala nyuma hujui dunia ni nini..kwanini nije kufanya hivyo sasa hivi….kwa lipi nitpata….’sauti ikawa inatoka kwa shida

‘Mama ngoja nikupeleke hospitali…naona kama hali sio nzuri….’nikamwambia

‘Mwanangu nisikilize kwanza, maisha bila mama hakuna,…. ni nani aliyezaliwa hewani, ndio baba yupo, aliweka mbegu kwa mama…, sasa yupo wapi,..hebu niambie sasa hivi baba yako yupo wapi..najua akikuona sasa hivi umekuwa dume …atakukimbilia, atakutaka ….lakini anajua wapi ulipotokea…’akawa kama anauliza

‘Mama achana na huyo baba, wala simjui na sina haja ya kumjua..’nikasema

‘Hapana..ili maisha yako yakamlike, ili upate radhi za mungu , jitahidi umtafute baba yako,..yule ni mzazi wako na mzizi wa mzazi haukatiki hadi hapo atakapoingia kaburini..bado una dhamana naye..’akasema mama

‘Mama kwa hayo uliyonihadithia, hata siku moja sitaweza kupoteza muda wangu kumtafuta, maana nikikutana naye, sijui kama nitaweza kuvumilia…tutakosana kabisa na huenda akaniachia laana..’akasema

‘Hapana,….nikuambie kitu, baba ni baba..hata kama ananuka, …hata kama hana kitu, kama ni baba yako umpe thamani yake kama baba…jitahidi sana umtafute, kama yupo hai, basi jitambulishe kwake, na umpe salamu zangu..’akasema

‘Mama ina maana katika akili yako bado unamuwaza baba , mtu aliyekufanyia hivyo…’nikasema

‘Namuwaza kwa hayo yaliyotokea..lakini nikikuangalia wewe namuona baba yako, kwanini nisimuwaze, bila yeye labda ningekuwa na sura nyingine, kuwepo kwako ni fahari kwangu, kama wewe umetokana na yeye, ni lazima nimuwaze, nimshukuru mungu kuwa wewe umepatikana kupitia yeye…’akasema

‘Mama…..achana na baba…’nikasema nikionyesha kukereka na huyo baba

‘Mwanangu hilo sio ombi, ni amri, …mtafute baba yako ili baraka za mungu zishuke kwako, utaona mabadiliko yake, ..utakuja kunikumbuka kama utafanya hivyo…’akasema  na sauti ikawa kama inakata.

‘Mama ngoja nikatita usafiri, hali yako sio nzuri…’nikasema

‘Pili hakikisha unaishi na mkeo vyema, mpe mawaidaha mema , mwambie kuwa hata siku moja mama hawezi kumloga mwanae, tena mtoto wa tumbo lake …hizo ni dhana potofu za kishirikina tu, kwanini mama amloge mtoto wake, ina maana analoga tumbo lako….’akasema

‘Mama hayo yamepita niachie mwenyewe …nitajua la kufanya..’nikasema

‘Mwanangu mimi nilikutafuta nikiwa sijiwezi, sijijui, sina kumbukumbu, kumbukumbu iliyokuwa imebakia ilikuwa ni ya kwako, ya kuku-kumbuka wewe,hebu jiulize kwanini mungu hakuiondoa hiyo kumbukumbu, sababu kubwa ni uchungu wa uzazi…’akatulia

‘Uchungu huo anayeufahamu ni mama peke yake…unafikia kwenye kuzaa, mtoto hutoki, unapasuliwa sehemu zako ili wewe mtoto uweze kutoka, wakati mwingine bila ganzi, unashonwa nyuzi bila ganzi..lakini hayo maumivu ya kushonwa, huyasikii, unachosikia ni ule uchungu wa uzazi, hebu fikiria huo utamu wake, kama ni utamu kweli….’akasema mama

‘Mwanangu sijui kwanini mkeo ananishutumu kwa uchawi….nimewaza saan hilonakosa majibu, kama asingelikuwa amezaa ningelisema hajui uchungu wa uzazi,lakini amezaa, labda alizaa bila shida…hata hivyo kama mke, angelijua thamani ya mama kwa mtoto wake…

‘Hapana..mkeo anahitajia ushauri, na mawaidha makubwa, aachane na hizo dhana potofu za kishirikina, ukiwa na dhana hizo, kamwe hutaendelea , kamwe hutakuwa na amani,..na kamwe hautakuwa na maisha mema…kiukweli…imeniuma sana kunidhania mambo kama hayo…lakini nimemsamehe, najua hajui alitendalo….’akatulia

‘Mama basi subiri nikachukue usafiri..naona hali yako sio nzuri….’nikasema nikiwa najiuliza nitapatia wapi usafiri , maana hapo sina kitu mfukoni....lakini mama hakuniachia mkono wangu akasema

‘Ngoja niongee hayo nitakayoweza kuyaongea,…sijui kama nitaweza kuyaongea tena, mungu mwenyewe ndiye anajua…oh, mwanangu, kweli nguvu zimekwisha, naona muda umefika…sasa nashindwa kukusimulia mengi yaliyonikuta..nguvu sina tena mwanangu, jitahidi, jitahidi…..’akawa anahema kwa nguvu

‘Mama usiniache mama..mama, mamaaaa..’nikajikuta nimemuinamia mama, akainua mkono wake mwingine kwa shida akanishika kichwa

‘Mwanangu ujikaze kwa lolote litakalotokea, mimi nimeshaishi sana inatosha, wewe bado unahitaji , maisha bado yapo mbele yako,  …pambana na maisha…ukumbuke kuwa maisha ni magumu..maisha sasa yametapeliwa na wachache, lakini usikate tamaa, fanya kila ufanyalo ukimuweka mungu wako mbele,….mimi  niliyoyafanya kwa ajili yako yanatosha…’akatulia ma mkono uliokuwa kichwani ukadondoka.

‘Mama…’nikaita na kuushika ule mkono, ulikuwa umelegea lakini sauti bado ilikuwa inatoka kwa shida.

‘Mwanangu sasa hivi umekuwa mkubwa, na unaweza kusimama kwa miguu yako mwenyewe, huumwi tena.., kama mkono wangu umeweza kukishika kichwa chako kwa wakati huu wa mwisho wa maisha yangu, basi ujue utapona, na utaneemeka,…najua sasa hata nikiondoka leo sitajutia…ila kumbuka kitu,  hakuna kama mama, hakuna kama mama ……mwa-na-ngu…’ akanyamza kimya.

‘Mama…’nikaita,…mama akawa kimia,hatikisiki kabisa, nikajaribu kumwangalia mapigo ya moyo, nikaona kama yamesimama…mungu wangu ina maana mama oh haiwezekani,…hapana haiwezekani, itakuwa kazimia tu…’nikasema

‘Ukumbuke muda huo mimi mwili umekwisha mabega yamepanda juu,..naonekana kama mtoto kimwili, ila uso umekomaa, na kukunjamana kama mzee ... na wengi walijua naumwa ugonjwa huo wa ukimwi..sina nguvu kabisa…sasa na hali kama hiyo mama, hajiwezi, mimi mwenyewe, hata kutembea siwezi, lakini nifanyeje..

‘Nilikurupuka pale nikatoka nje, nia nimwangalie mke wangu ili tusaidiane tumpeleke mama hospitalini,  nilikuwa napepesuka, ..miguu inagongana nilikuwa nimekonda rafiki yangu siunakumbuka ulivyoniona pale Lugalo…hapo nina mawazo nina njaa, lakina havina maana kwa muda huo…kwahiyoo kwa hali niliyokuwa nayo hata kumuinua mama peke yangu nisingeweza.

Nilipotoka nje nikashangaa kupo kimyaa…, hakuna cha mke wangu wala mtoto. Nikaingia chumbani nikakutana na mshangao, …chumba kina mlango wa nyuma, mlango huop ulikuwa wazi, mara nyingi tulikuwa hatuutumii…chumba kilikua kama hema, hakuna kitu hata kimoja…

‘Hebu jaribu kufikiria chumba kilikuwa kina vitu vingi, kitanda, redio yangu ambayo niliipenda sana, kabati la vyombo, kwani ilibidi tuhamishie vitu karibu vyote kwenye chumba hicho, ili kuwepo an nafasi ya kulala mama, …vyote vilikuwa vimebebwa.

Sikuamini kuwa tukio hilo limefanyika hapa kwangu, kwani na umasikini wangu wote bado watu wanachukua hata kile kidogo nilicho kuwa nacho, ..sikufikiria kuwa aliyefanya hivyo ni mke wangu…akili hapo ilikuwa haijakaa sawa,…na hata hivyo hao watu waliwezaje kuingia humo chumbani kama sio mke wangu,…hapo sasa nikahisi, nikajua aliyefanya hivyo bas atakuwa kashirikiana na mke wangu, sasa mke wangu yupo wapi…sikuwa na muda huo tena..

Mimi nikawa nahangaika kutafuta mtu wa kunisaidia, kunisaidia mama afike hospitalini, hayo mengine ni mamb ya kupita tu…hata hivyo nikawa najiuliza hao watu a gari walifika saa ngapi, na gari lililochukua hivyo vifaa vyangu lilikuja saa ngapi, mbona sikulisikia hata mngurumo!. Nikatoka haraka hadi nyumba ya jirani kuulizia kama nitapata msaada, jirani yangu huyo ana baiskeli...

‘Jamani mumesikia gari likiingia hapo kwangu ..nimeibiwa..’nikasema huku nikishika kichwa

‘Sisi tulijua kuwa mnahama, maana kuna gari lilikuja na kusimama mbali kidogo na hapo kwenu, na watu wakawa wanachukua vifaa hapo kwako wanavihamshia kwenye hilo gari, huku mke wako akiwa anawasimamia …’ akaniambia jirani yangu.

‘Oh, huyu mke wangu kama kafanya hivyo basi sio mtu ni..shetani, lakini sasa jirani yangu, nina shida kubwa sana, naomba msaada, maana mama hali yake sio nzuri, je mume wako yupo aniazime baiskeli?’ nikamuuliza huku nikijizuia machozi kunitoka.

‘Mume wangu aliondoka kitambo na baiskeli yake, lakini alisema hatakawia kurudi…ina maana mama kazidiwa sana…?’ akasema akishika simu yake akitaka kumpigia mume wake simu na kabla hajafanya hivyo tukasikia kengele ya baiskeli, …

‘Huyo amekuja…’ akasema yule jirani yangu mwanamama, na hapo nikamuona mume wake akija na baiskeli, nikashukuru sana.

Alipokuja yule rafiki yangu sikupoteza muda nikamwambia hali ya mama ni mbaya sana anisaidie baiskeli ili tumpeleke mama hospitali…Yeye bila ubishi akaingia ndani kwake halafu akatoka na kunifuata nyumbani kwangu, na mle ndani tulimkuta mama kalala vilevile, ina maana kazimia…sijui, au ndio keshakufa sijui mungu wangu…!

Kwa hali kama ile, nikawa nimechanganyikiwa nahaha huku na kule…mfukoni sina kitu, hata kama tutamfikisha hospitalini , tutaambiwa kuchangia pesa nitapatia wapi pesa, na tutakula nini maana hata kama kulikuwa na akiba ya chochote huyo mwanamke kasomba kila kitu….. Isingekuwa huyo rafiki yangu, sijui ingekuwaje.

Yeye alimbeba mama na kumtoa nje, na akachukua simu yake na kumpigia jamaa mmoja mwenye bajaji, na huyu jamaa akaja haraka wakasaidiana kumbeba mama hadi kwenye hiyo bajaji, na sisi tukaingia na kuelekea hospitalini.

Hebu tuishia hapa kwa leo…maaana inasikitisha

WAZO LA LEO: Wazazi ni muhimu sana kwetu mama na baba, tusiwatelekeze mama kama mama hana mfano wake, muheshimu na mtimizie mahitaji yake yote kwa kadri ulivyojaliwa na hata siku moja usimlinganishe mama yako na mkeo, kwani hivyo ni vyeo viwili tofauti…kwanza mama kama mumejaliwa,… mkeo mtajitajitahidi mtajua la kufanya kwani bado mna nguvu. Lakini pia usimsahau baba yako, ..kwani ili upatikane baba alikuwa mshirika. Mtafute na mtambue kama baba yako.

Usijali historia za wazazi wako, hata kama ilikuwa ni historia mbaya ya wawili hao wewe kama mtoto timiza wajibu wako kwao , muheshimu baba yako na mpe stahiki yake.

Ni mimi: emu-three

No comments :