‘Karibu nesi…utuambie uliyoyapata
huko kijijini, …tunasubiria kwa hamu , maana hali ya mgonjwa kwasasa inahitajia
zaidi kujua historia yake, ili tujue chimbuko la tatizo lake limetokana na
nini, …unajua kuna kitu kinatushangaza, ..iweje huyo mama akunyoshee kidole
wewe…’akasema docta
‘Ananinyoshea kidole mimi, kwa vipi?’
akauliza nesi akiwaangalia mabosi wake kwa sura ya kushangaa, na kukunja uso
kidogo.
‘Hebu kwanza kaa kwenye kiti tusikie uliyoyapata huko….maana huyo mama
anaongea mengi…ni kuonyesha kuwa huyo mama alipatwa na jambo, hilo tatizo
likaziba ufahamu wake wa nyuma…kwa hivi anaonyesha dalili za kuanza
kukumbuka..kwahiyo atasema mengi, na kawaida hayo anayoyaema ni yale
yaliyotokea kabla hajapatwa na hilo tatizo, kwahiyo ni ya ukweli…’akasema docta
bingwa.
‘Ina maana….’akataka kusema nesi
lakini akashindwa aongee nini, na docta msaidizi akasema;
‘Anadai wewe umechukua mtoto
wake..’akasema docta msaidizi..na wakati huo nesi alikuwa hajakaa kwenye kiti
na aliposikia hivyo, sasa akakaa kwenye kiti huku akili ikianza kuchemka.
Tuendelee na kisa chetu.
**********
‘Hebu tuambie ulichokipata huko kijijini..’akasema docta mkuu, na
mwenzake naye akawa kashika kidevu huku wote wakimkazia macho nesi, nesi
akainua uso na kuwatizama, akasema;
‘Unafikiri, hakuna la muhimu nimelipata,….hakuna cha zaidi kinachoweza
kusaidia,..ni yale yale tu…imani zao…na….kumshutumu huyo mama, kwa mambo
yasiyoelezeka…’akaanza kusema
‘Hayo hayo uliyoyasikia , ..tunataka na sisi tuyasikie..’akasema docta
msaidizi.
Nesi aliwaelezea wale mdocta yote aliyoyakuta huko kijijini na
jinsi gani anavyofahamu , na mwisho akasema
‘Na hiyo kauli ya huyu mama kuwa eti mimi nina mtoto wake, sio
kwangu tu, hiyo ni kauli yake hata kabla mimi sijamfahamu…sijaonana naye.., yeye
nasikia lipoika hapo kijijini kutoka huko alipotoka, kila aliyekutana naye
anamwambia hivyo, na … kwa kila mtu..na hasa akikuona una mtoto basi atakuganda…’akasema
nesi.
‘Unajua tangia nianze hii kazi, watu kama hawa wakianza kuongea ,
huwa wanaongea yale ya kweli, yale yaliyowahi kutokea kwenye maisha yao huko
nyuma kabla hawajapoteza kumbukumbu zao…, lakini wanayazungumza pasipo na
mpangilio..ni vitu kama njozi vinakuja akilini mwao…na hatimaye atakuja
kukumbuka yote….’akasema docta.
‘Kwahiyo labda mnahisi kuwa
ni kweli kuwa mimi nimemchukua mtoto wake..kwanini nifanya hivyo…?’ akauliza
nesi
‘Hapana sio hivyo hatumaanishi hivyo…kama ulivyosema kuwa huyu
mama anashutumu yoyote yule…sisi tunajaribu kuona kama kuna ukweli kidogo..’akasema
docta ka kabla nesi hajasema kitu yeye docta akaongezea swali;
‘Hebu tukuulize, wewe ..maana unasema na hasa akikuona una mtoto, hebu
kumbuka vyema siku hiyo ulipokutana naye ulikuwa na mtoto au kabla..katika
kufika kwako huko, huenda uliwahi kuwa …au kupakata mtoto wa mtu mwingine
akakuona..’akasema docta
‘Mtoto..!?’nesi akauliza kwa mshangao, akawa anawaza, akijaribu
kukumbuka.
‘Unajua huyu mama alifikia kuniambia, kama shitaka kuwa wewe ndiye
umemchukua mtoto wake, nikamuuliza kwa vipi, akasema alikuona ukimchukua,..na
akakuona ukiwa naye huko…anasema tu hukooo, ukimuuliza wapi, anaendelea kusema
tu hukoo, na hapo anakuwa kama anajaribu kukummbuka ..’akasema docta.
‘Mimi sioni ajabu kwa kauli yake hiyo, kwani kama angeninyoshea
kidole mimi tu, labda ningelisema kuna hoja…lakini sio mimi tu, hata ndugu
zangu, majirani na yoyote pale kijijini anamwambia hivyo hivyo, na hata akawa
anaimba wimbo wake akisema ‘anataka mtoto wake’..’akasema nesi.
‘Hebu turudi nyuma kidogo..siku ulipokutana naye, ulikwenda
kijijini kufanya nini, ..najua ilikuwa ni mapumziko au kulikuwa na ni kitu maalumu…
, labda tukumbushane hivyo..?’ akauliza docta msaidizi.
‘Mhh, ni siku nyingi..na mara kwa mara huwa na kwenda huko
kijijini kusalimia tu..maana nimelelewa huko..lakini kwa vile nimeshakuwa na
mahali pangu pa kuishi,..huku mjini, siwezi kwenda huko kukaa saana.., ila
ninachokumbuka ni kuwa …mimi nilikutana na huyo mama wakati naelekea kituoni,
kutafuta usafiri wa kurudi huku kazini.’akasema
‘Ulikuwa na mtoto?’ akauliza docta.
‘Hapana, mtoto wa nini …maana narudi kazini , na sikuwa na mtu
yoyote ambaye labda nilimsaidia mtoto…nikamuona nikajaribu kumuongelesha, na
kama anavyowafanyia watu wengine..basi na mimi akanifanyia hivyo hivyo,
akawaanadai kuwa eti mimi nina mtoto wake..shutuma zake dhidi yangu zikaanzia
hapo…’akasema nesi.
‘Hebu kumbuka,….kipindi hicho, maana wewe ndiye nesi peke yake uliyebakia
hapa wa muda mrefu, na hata madocta wote sisi hapa ni wageni..kipindi hicho
ulichoenda huko kijijini,….ukakutana na huyo mama, ulikwenda vipi, kulikuwa na
tukio, au ilikuwa likizo yako tu…. hakuna tukio ….lolote hivi….linaloweza
kuwiana-wiana, yaani hakuna jambo lililokufanya kwenda huko kijijini, au hapa
hospitalini hakukutokea jamb lolote la mama kama huyu….?’ akauliza docta.
‘Tukio kama lipi….mmh, sikumbuki, mimi nahisi ilikuwa ni siku ya
mapumziko nikaamua kwenda kusalimia tu..unajua ni muda sikumbuki vyema …aaah
ndio ilikuwa ni ..mapumziko kama haya….ama kwa hapa hospitalini mmmh, tukio
..kama lipi..?’ akawa anaonga na kujaribu kutafakari
‘Unajua najaribu kuoanisha, hili analodai huyu mama kuhusu huyo
mtoto wake,…na tatizo lake..la udhaifu katika kumbukumbu, na kuchanganyikiwa...huyu
mama , nimemchunguza kwenye tumbo lake kuna dalili za kuwa alifanyiwa
upasuaji..’akasema docta.
‘Mhh..upasuaji…?’ akauliza nesi kwa mshangao.
‘Lakini haina, nahisi hivyo huenda haina, mahusiano,… hilo kwangu
sio tija, nataka tu kujua, wewe kipindi hicho ulipowkenda huko kijijini
hukuwahi kumbeba mtoto…huenda alikuona ukiwa na mtoto kitu kama hicho na je hao
ndugu zako hawana mtoto, hawakuwa na mtoto mchanga?’ akaulizwa
‘Kubeba mtoto wa mtu mwingine..mmmhe..hapana docta…..mhhh, ..sijui
maana mimi kwa mara ya kwanza kukutana naye ni hapo,..na ilikuwa ni barabarani,
sio nyumbani hapo kwa ndugu zangu…na ilikuwa ni wakati naondoka..mmh, ok, labda…lakini
haiwezekani, maana mimi sikuwahi kutoka nje na huyo mtoto wadada yangu..?’
akasema nesi.
‘Kwahiyo kumbe uliwahi kubeba mtoto, yaani..sio wa huyo mama, ila
uliwahi kubeba, huenda akakuona lakini wewe hukuweza kumuona kwa wakati yeye
anakuona,..je uliwahi kumbeba mtoto hata kama ni wa jirani, …?’ akaulizwa
‘Lakini kama ni huyo, mimi sikuwahi kutoka naye nje..?’ akasema.
‘Huyo mtoto ni wa nani hebu tuanzie hapo?’ akauliza docta.
‘Doctor, lakini huyo mtoto hana mahusiano na huyo mama..nina
uhakika kabisa..’akasema
‘Mhhh..hatujasema hivyo…kuwa ni mtoto wa huyu mama, wewe is
umesema kuwa huyu mama kila mwenye mtoto anamshuku au sio..lakini imetokea
kushuku kwake kwako kuwe na uzito zaidi…’akasema docta
‘Kwa vipi iwe hivyo?’ akauliza nesi.
‘Mimi nakuambia hili kwasababu wamekuja watu wakiwa na watoto wao,
na mimi mwenyewe nikajribu kmpima huyo mama kuona kama hiyo hali ya kudai kila mtu
mwenye mtoto ni wake…nikajaribisha kwa hao waliokuja na watoto wao…’akasema
docta.
‘Hakudai kuwa hao watoto au huyo ni mtoto ni wa kwake?’ akauliza
nesi.
‘Kwa muda ambao kaanza kupata kumbukumbu, hakudai hivyo…nilipomuuliza
hakusema ni mtoto wake, …ila anapenda watoto..’akasema docta
‘Ina maana hakudai kabisa kwua ni mtoto wake..?’ akauiliza tena
nesi.
‘Nilimjaribisha hivyo, nikamuliza ni mtoto wake, akasema hapana
mtoto wake kachukuliwa na nesi, nikamuuliza nesi yupi,… akasema ..huyo
mnayemuita nesi mkuu..’docta akasema
‘Alisema hivyo..?’ akauliza nesi kwa mshangao na kutahayari.
‘Ndio..ndio maana najaribu kutafuta ukweli…kama unavyoona, ilivvyo.
Ina maana sasa huyu mama kumbukumbu zimeshaanza kujijenga mpaka anakumbuka nesi
yupi , kasema huyo mnayemuita nesi mkuu,…na nikajaribu kumleta nesi mwingine
akasema sio huyo…labda kama unabisha tutakwenda sote nikamuulize mbele
yake..uone..lakini hilo sio muhimu kwa sasa..muhimu ni kutaka kujua..huedna
kuna kitu kilitokea….’akasema docta mkuu.
‘Mimi sielewi kabisa…mimi nitamchukuaje mtoto wake kwa lipi…sijui
mnanielewa…mtu mwenyewe mnaomuona alivyo, hivi kweli aliwahi kuwa na mtoto..?’
akauliza nesi kwa mshangao.
‘Aliwahi…aliwahi kuwa na mtoto…’akasema docta na nesi akamtupia
jicho la mshangao.
‘Ulimchunguza?’ akauliza nesi..
‘Hiyo operesheni aliyowahi kufanyiwa inaonyesha kuwa aliwahi kuzaa
kwa upasuaji…aliwahi kupata mtoto, sasa sijui kama mtoto alikuwaje, hai..au
vipi, lakini huo upasuaji ni wa uzazi…’akasema docta na wote wakawa kimia kwa
muda.
‘Nesi hebu kumbuka kipindi hicho hakuwahi kufika mama kama huyu,
mwenye matatizo, mtindio wa ubongo… , kuchanganyikiwa..akajifungua mkafanya
taratibu za kumchukua mtoto wake?’ akauliza docta msaidizi.
‘Kama huyu..mmmh, hapana…maana kuna taratibu kama akitokea mama
kama huyo , nikimaanisha mwenye matatizo ya akili,si zipo taratibu jamani… ikitokea
hivyo mtoto anakabidhia kwa ndugu zake,..hizo taratibu zilikuwepo hata kabla
hamjafika nyie…ni kweli imetokea hivyo mara kwa mara na taratibu zikafuatwa,
kweli si kweli…sasa mimi sikumbuki vyema…na mama kama huyu mwenye kuchanganyikiwa
kihivyo sikumbuki kumuona kabla…sikumbuki, ..’akasema nesi.
‘Katika kipindi hicho cha nyuma,..hakukuwahi kuzaliwa mtoto,
…akawa hana mzazi…labda mama yake akapatwa na jambo, akafariki..kitu kama
hicho…?’ akauliza docta.
‘Sasa kama mama yake alifariki huyu atakujaje kudai mtoto ni wake
, au na nyie mnaamini mambo hayo ya kijijini wanaodai kuwa mama huyo alikufa na
sasa kafufuka kuja kulipiza kisasi..’akasema nesi.
‘Hapana…unajua tunajaribu kuangalia kumbukumbu za nyuma….maana
kama mama huyu ni wa maeneo ya vijiji vinavyozunguka maeneo haya ya hii hospitali
na nijuavyo mimi hakuna hospitalini nyingine kubwa kwa maeneo haya ya wilaya inayotambulikana
kwa upasuaji kama huo ni hapa tu…hivi kuna hospitali nyingine..eeh, hakuna..eeh,
sasa kwa vyovyote basi huyu mama alifanyiwa upasuaji hapa…’akasema docta.
‘Hata mimi naona hivyo…labda nesi ukumbuke vyema..’akasema docta
msaidizi
‘Kwahiyo ina maana huyu mama kama aliwahi kujifungua kwa upasuaji
atakuwa alijifungulia hapa..au sio…sasa mtoto wake yupo wali..labda ni
kachukuliwa na ndug zake..labda…lakini je alijifungulia hapa?’ akauliza docta
akimgeukia docta mwenzake.
‘Au aliwahi kujifungulia sehemu nyingine na kuhamia vijiji vya
eneo hili..’akaongezea docta msaidizi….
‘Mhh,unajua docta nimekumbuka jambo, uliposema kama kuna tukio mama alijifungua
akafariki…au..mmh, nimekumbuka…lakini sio huyu mama,…kuna tukio liliwahi
kutokea hapa hospitalini, lakini halihusiani na huyu mama…nina uhakika kabisa
sio huyu mama,….maana huyo mama tulikuja kusikia kaokotwa akiwa amefariki,
akazikwa, na mmoja wa nesi wa hapa alihudhuria mazishi yake…’akasema nesi
‘Huyo yeye ilikuwaje?’ akaulizwa.
Nesi akashika kichwa akijaribu kukumuka tukio hilo analoikiria
yeye, maana yapo matukio mengi, ila hilo moja analikumbuka kwani lina mambo
mengi kichwani mwake..lakini kama ni hilo tukio hakupenda kuliongelea.
Sasa akawa anajuta kwanini kalikumbuka hilo tukio, maana lile
tukio halikutakiwa kuhadithiwa kabisa, kwani ilikuwa ni siri yao, yeye na
madkitari na ndugu zake..na aliwahi kukanywa kuwa ikitokea akavujisha siri
anaweza kupoteza ajira au hata kufungwa kwani walichokuwa wamekifanya wao ni
kumsaidia yeye kwa uzembe wake,..uzembe uliosababisha kifo…maana taarifa zilikuja
baadaye kuwa huyo mama kaokotwa, na amekiwsha kufa.
Na siki taaarifa ilipofika, wakati wameshachukua maamuzi, kuwa
nesi huyo abebe jukumu la kumlea mtoto…., ilibidi wakae tena kikao cha siri…,
na kuambizana kuwa tukio hilo sasa liwe siri kubwa sana.
‘Mhh, lakini docta, hilo tukio halihusiani kabisa na huyu
mama…’akajitetea nesi
‘Sawa liwe halihusiani, au linahusiana , mimi nikilisikia ninaweza
kupata japo fununu..mimi ninahisi huyu mama aliwahi kufika hapa…’akasema
‘Umejuaje hilo…?’ akauliza docta mwenzake.
‘Kuna muda nilimuuliza huyo mtoto wake anayedai kachukuliwa alichukuliwa
wapi…basi akasema atanionyesha, nikamwambia anionyeshe,…akasimama na kutembea
hadi chumba cha upasuaji cha wazazi akasimama hapo mlangoni akasema
alichukuliwa humo..’ akasema docta na baadaye akaongezea kusema;
‘Mimi nikamuuliza ni nani alimchukua, akasema alichukuliwa na
docta na nesi…unaona, sasa hapo akasema na docta na nesi….docta yupi,
nikamuuliza kama aliwahi kumuona..akasema huyo docta hajawahi kumuona hapo tena…’akatulia
docta akimuangalia nesi
‘Kama kasema hivyo, kuwa alichukuliwa na docta…maelezo yake
yanaonyesha uhalisia fulani…., maana madocta ndio wenye kezi hiyo, na nesi,
ndiye eliyemchukua mtoto kwenda kumuhifadhi…hebu angalia ilivyo, …haionyeshi ni
kauli ya mtu mwenye kuchanganyikiwa, ..huyu mama kaanza kukumbuka yaliyotokea,
ndio maana nahisi..anayozungumza yana ukweli…’akasema docta.
‘Lakini kama ni hilo tukio,…docta huyo mama likufa, sio huyo…hata
maumbile yake huyu hayafanani kabisa na yule…mimi siwaelewi, mnataka kusema
huyo mma kafufuka, na ndiye huyu anakuja kudai mtoto wake..’akasema nesi.
‘Eheee..sasa unaona kulikuwa na tukio…si ndio, ..na tukio hilo
linamuhusu mama na mtoto….sasa sisi tunahitajia kulifahamu hilo tukio, hata
kama sio lenyewe, lakini huenda likaleta picha..’akasema docta.
‘Mabosi zangu tutakuwa tunapoteza muda tu…maana nina uhakika huyu
mama sio yeye, kwa vile yule tulipata habari kuwa keshafariki..alipotoka hapa,
alizidiwa njiani akadondoka,…akaja kuokotwa na watu akiwa ameshafariki,…maiti
yake ilikuwa katika hali mbaya, wakamzika haraka…’akasema nesi.
‘Unajua nesi nikuambie kitu….hapa hatupotezi muda, maana hiyo
nimoja ya kazi yangu…na tukio hili linanifanya niendelee uchunguzi wangu,
kuhusu hizi imani..mtu kufa na baadaye kuonekana…au mtu kuonekana kafa, na
baadaye anazindukana..kuna maeelzo ya kiimani, na kisayansi, nataka kuyaonaisha
kiuchunguzi zaidi…’akasemda docta.
‘Kwahiyo unaamini kuwa mfu anaweza kufufuka kwa lengo la kulipiza
kisasi…au una maana gani kwenye uchunguzi wako…..?’ akaulizwa na docta
mwenzake.
‘Mfu hawezi kufufuka…mtu akishakufa amekufa, mfu ni mfu tu…sasa iweje watu waamini kuwa
kuna wafu wanaweza kufufuka…hiyo ndio
hoja…kisayansi, tunaona hilo halipo, ..sasa hawa watu wanaoamini hivyo
wanakigezo gani…nalichukulia hili tukio, maana naona kama linaweza kuleta hoja
fulani, nataka kuliangalia kihivyo kwanza..japokuwa mimi naamini mu hawezi
kufufuka, na ndivyo sayansi inavyosema…’akasema docta.
‘Sasa docta huoni kuwa tunafanya kitu ambacho kitatuchanganya tu…hebu
niambie huyu mama ana nini zaidi mwilini mwake..?’ akauliza nesi, na docta kwanza
akacheka , halafu, akatulia akiliwazia hilo, akasema;
‘Aaah, sio kwamba ana kitu cha ajabu mwilini…, zaidi ni hiyo alama
ya upasuaji mengine ni kawaida tu,..majeraha usoni ya kukatwa, katwa na mapanga…vinginevyo
ni mwanadamu kamili aliyekamilika, kama
ulikuwa na wasiwasi kuwa huenda huyo sio mwanadamu, labda ni mzuka,…. hapana
huyo ni mwanadamu kamili…..’aksema docta.
‘Lakini docta ..kama ni mwanadamu kamili, basi….sio yeye,…maana nilikuwepo, na narudia tena..yule mama alikufa…mimi
nilikuwepo nilimfahamu vyema huyo mama, maana mimi nilimuhudumia,..akazaa kwa
upasuaji, na ilikuwa yeye au mtoto kupona, na bahati wakapona wote…kwahiyo
nilimuona alivyokuwa…na huyu mama wa sasa ni mwingine na tofauti kabisa..’akasema
nesi
‘Yawezeka hivyo…lakini, hebu tuone tukio hilo lilikuwaje kwanza…’akasema
docta.
‘Docta nawaambia ukweli, huyu mama… hajawahi kufika hapa, labda
kama alifika mimi nikiwa sipo…nina kumbukumbu zangu kabisa..huyu mama ni mgeni
kabisa katika hospitali hii..labda kama alifika kwa matatizo ya kawaida, lakini
kama yalikuwa mazito kiasi kikubwa na jinsi anavyoonyesha kuwa kachanganyikiwa….hajawahi
kufika hapa…’akasema nesi
‘Usijali..hebu tuambie hilo tukio lilikuwaje….wewe lisimulie hatua
kwa hatua, kama alikufa basi huenda ni mzimu wa huyo mama umekuja kwa namna
nyingine..’akasema docta msaidizi akitabasamu huku akimuangalai docta mwenzake.
‘Yah…mimi nina hamu sana ya kusikia hilo tukio…tafadhali lielezee,
na usiogope, sisi hapa ni watendaji wenzako…hatuwezi kufanya lolote , tupo kitu
kimoja…na zaidi ya hayo tunachotaka ni nini, ni kumsaidia huyu mama, na wewe
utakuwa karibu na huyo mama kuanzia sasa, …maana kama kapona hataweza kukataa
kujifunua…pili hawezi kuleta matatizo, ningelitaka wewe tu ndiwe uwe karibu
yake..’akasema docta.
‘Mimi nimeshaanza kumuogopa..’akasema nesi
‘Kwanini..?’ akauliza docta msaidizi.
‘Maana nyie ambao nawategemea kiutalaamu, mumeshaanza kujenga hoja
kuwa huenda tukio hilo linahusiana na huyu mama,…ambaye nijuavyo mimi, huyo
mama alishafariki, sasa iweje awe ni huyu mama…hamuoni ni kama kuamini mambo
yasiyoelezeka, na mambo kama hayo mara ningi yanajenga hofu kichwani…’akasema
nesi.
‘Ili ysijenge hofu, hebu jaribu kukumbuka hilo tukio, utusimulie,
ili tuweze kusaidiana na kuliweka sawa, huenda huyu mama akaja kupata msaada
tu, kutokana na hilo tukio hata kama sio yeye…unasikia,…muhimu ni kupata
chochote kile kitakachoweza kusiadia….ila, narudi atena kwa uzoefu wangu… mimi
naamini hayo anayoyasema huyo mama yana ukweli..’akasema docta.
‘Hapa ndio sikuelewi docta…ni nini unataka kuthibitsha…’akaulza
docta mwenzake.
‘Ubongo wa mwanadamu uchukulie ni kama kumputa..unavyoweza kupokea
taarifa na zile taarifa zikahifadhiwa mahali, na ukizitaka zile taarifa
unazipata kwa kuitisha jina la ile taarifa ulivyoiweka,…sasa inakuja kuwa
taarifa fulani ni kuba kuliko ile asili yake..komputa inashindwa kubeba…maana
uzito wa kitu nao ni muhimu sana…sijui mnanielewa.
‘Watu hawa wanaochanganyikiwa, wanaweza kubeba kitu ambacho wakiwa
na akili zao hawawezi kukibeba..umeshaona hiyo kitu..sasa ni uwiano gani wa
akili, ..ambao uliwezesha mwili kuwa na nguvu zaidi…hapo ndipo imani za ghaibu
zinakuja..uwezo kuzidi uwezo halisia…ni kitu gani kinafanya iwe hivyo…tuliache
hilo..’akatulia
‘Mtu anaonekana kafa kabisa….kabisa..hata vyombo vya kitaalamu
vinathibitisha hilo,..baadaye anazindukana,..hebu rejea mtoririko wa damu,..na
msihipa ya fahamu, damu ikisimama ukaona hakuna mapigo, mwili unakuwa hauna
uhai..ina maana basi pale mnapoona mtu kafa, kuna mshipa fulani kwenye ubongo
utakuwa bado unafanya kazi, damunakila kitu ..lakini unakuwa hauna mawasiliano
kabisa na mwili…..’akatuliza
‘Docta hapo unatuchanganya…hatukuelewi..’akasema nesi
‘Najua hamtanielewa,..na mimi ndio nafanyia uchunguzi..ndio maana
nina hamu kabisa ya kusikia hilo tukio….na ili tusipoteze muda, …mimi nakupa
nafasi ya kulifikiri ..ukiwa tayari tuambie..au tutaongea wawili..mwenzangu
anaweza kwenda kuendelea na kazi zake, au mnaonaje..?’ akauliza docta.
‘Hata mimi nina hamu saan ya kulisikai hilo tukio..lina nipa
hamasa, ilikuwaje…?’ akasema docta msaidizi.
Na hapo nesi akatuliza kichwa, akatafakari,…akaona kabla
hajalisimulia, ni bora mwenyewe apate muda wa kuliwaizia, kwa makini, kabla
hajasema lolote, na ikibidi kuwasiliana na wale madocta walikuwepo, akiwemo
yule docta kijana ambaye ndiye alichukua jukumu la kumtetea…ndipo akili yake
ikaanza kulikumbuka tukio hilo hatua kwa hatua…akaanza kukumbuka ilivyokuwa….
NB: Sehemu ijayo itafunua kile kilichotokea nyuma siku ile nesi
alipokutwa na tatizo , tatizo lililochukuliwa kama uzembe, na likafikai yey
kumpata mtoto, mtoto ambaye yupo mikononi mwa ndugu zake,…..je siku ile
kulitokea nini…tuzidi kuwepo
WAZO LA LEO: Unapopata taarifa zisizo na uhakika, ambazo huenda ni
mzigo kwako, au zinakutia mashaka, jaribu kwanza kuwa na subira,..chunguza
ukweli wake… usikimbilie kuzikuza, ukaanza kupatwa na wasiwasi, uwoga…huzuni, ,,au
kukimbilia kushutumu kwanza...
Ukifanya hivyo utapunguza nguvu za mwili za
kuhimili, utajipandikizia magonjwa ya moyo..shinikizo la damu,…kabla ya ukweli
wa hiyo taarifa, hata taarifa hiyo ikija
huenda ikawa ni kweli au sio kweli..na kwa hali hiyo, utakuwa huna gunvu sahihi
tena ya kuzipokea hizo taarifa…ndipo unakut mtu anaptwa na kiharusi, au
kupoteza fahamu, au kushikwa na ugonjwa wa moyo. Ndio maana tunasema, Tusijitwike
mzigo kabla haujatua kichwani
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment