Yule
binti akaondoka kwa shingo upande, hakuweza kupingana na baba yake, aliondoka
akiwa mnyonge sana. Alitamani hata kulia,hata hivyo hakuwa na uwezo wa kufanya
lolote, akatembea taratibu kuelekea shambani, akimuacha baba yake akitengeneza
dawa zake.
Moyoni
alishaingiwa na kitu, licha ya huruma, lakini alihisi kuingiwa na kitu kipya
moyoni, hakutaka kuachana na huyo, alitamani awe karibu naye, sasa kusikia kuwa
anataka kuchukuliwa na watu, na watu wenyewe huenda wana nia mbaya, akajihiis
kuumua sana.
‘Sasa
nifenyeje, kumuokoa huyo mtu..?’akajiuliza, na mara akasikia gari likija,
akajificha kichakani,…na alipoona lile gari likikaribia nyumba yao akajua basi,
huyo mtu keshachukuliwa, ..
‘Hata
jina lake simjui…’akasema huku akiomba kwa mungu amsaidie huyo mu asichukuliwe.
Pale
alipojificha alimuona baba yake aiendelea kutengeneza dawa zake, na hakuonyesha
wasiwasi, akawaona watu wakitoka na silaha, na mtu mmoja akamsogelea baba yake
na kwa sauti ya mbali akasikia yule mtu akimuuliza baba yake maswali.
Alikaa
pale akiwa na wasiwasi, akijua watamzuru baba yake, Na mara akahisi kitu nyumba
yake alipogeuka akazibwa mdomo..akajua na yeye keshakamatwa na hao watu wabaya.
Tuendelee
na kisa chetu…
***********
‘Yupo
wapi huyu mtu….?’
‘Kwani
nyie ni nani?’ akauliza mzee.
‘Wewe
mzee unakumbuka tuliongea wote kwenye simu ukasema kuna mtu wetu hapa,
…’akasema.
‘Mliongea
kwenye simu na mimi?’ akauliza kwa mshangao.
‘Mzee
usitupotezee muda, sisi tumekuja kumchukua mtu wetu, na wewe tunakukabidhi
chako…ujue sisi ni askari hatuna muda wa kupoteza hapa…’akasema huyo mtu
akigeuka kutoa ishara kwa mtu aliyekuwa kabakia kwenye gari, na huyo mtu akaja
akiwa na bahasha kubwa iliyotuna.
‘Unaona
sisi hatutaki longo longo, humu kuna milioni kumi na tano, kama huyo mtu wetu
yupo hapa, hii hapa ni zawadi yako yote….’akasema.
‘Ingieni
ndani yupo kalala, lakini bado naendelea na matibabu yake hamuoni hapa ndio
namtengenezea dawa yake…’akasema huyo mzee akiuangalia ule mfuko kwa hamasa.
‘Usijali,
kama ni dawa zake tutazichukua atakwenda kuzitumia huko mbele kwa mbele, ni mu
wetu tulijua ameshakufa, siumeona kwenye gazeti walivyoandika, …kuna watu
wabaya walimteka nyara,..tunashukuru sana mzee umemponyesha,…’akasema lakini
kabla hajamaliza mtu mmoja aliyeingia ndani akatoka na kusema;
‘Mbona
hayupo, ….’akasema huyo mtu akiwa kashikilia silaha, na wenzake wakatoa na
kutoa maneno hayohayo.
‘Mimi
sielewi…maana asubuhi nilitoka kwenda kuzitafuta hizi dawa, nikamuacha akiwa
kalala, na dawa nilizompa zausingizi asingeliweza kuamuka, ..nahisi basi kuna
mtu kaja kamchukua, maana haiwezekani…’akasema huyo mzee akitaka kungia ndani.
‘Mzee
usitupotezee muda wetu, hebu tuambie huyu mtu yupo wapi?’ akauliza huyo jamaa
sasa akiwa kabadilika na akawa anamsogelea mzee kwa hasira.
‘Kwakweli
kama hayupo huko ndani, siwezi kujua wapi alipokwenda, na haiwezekani dawa
aliyotumia ina nguvu sana?’ akasema
‘Ulipoondoka
ulimuacha humo ndani na nani…?’ akauliza
‘Nilimuacha
peke yake, maaana nina uhakika kwa hizo dawa alizokunywa za usingizi
asingeliweza kuinuka, …hizo dawa zina nguvu sana…’akasema akiogopa kusema
alimuacha na binti yake.
‘Mzee
unazikosa hizi pesa hivi hivi, na pia unajiweka katika mazingira magumu ya
kuvunja uaminifu wako…’akasema huyo jamaa akiwa kashikilia ile bahasha
akiichezesha chezesha mkononi.
‘Mimi
nina uhakika yupo ndani, asingeliweza kuondoka, kwa hizo dawa..ngojeni
nihakikishe..’akasema na kuingia ndani,na haikuchukua muda akatoka, na kusema
‘Kweli
hayupo…sijui kaenda wapi, na sizani kama atakuwa katoka
mwenyewe…haiwezekani….’akasema
‘Tafuteni
kila mahali,…tusipomuona huyu mzee atawajibika, tutaondoka na kichwa
chake…’akasema yule mtu na yule mzee aliposikia hivyo akasema
‘Kichwa
changu kinahusu nini, mimi nimejitolea kuwaambia ukweli, ndio mnataka kulipa
fadhila, kama kweli alikuwa mtu wenu mngelinishukuru kuwa nimemsaidia akapona,
sasa mnataka kuniua,…’akasema
‘Kumdaidia
kwako hakutusaidii sisi, ungelikuwa na maana kama huyo mtu angelipatikana, sasa
ama kichwa chake ama kichwa chako ndio
maagizo tuliyopewa….’akasema
‘Kumbe
nyie watu ni watu wabaya eeh, mnataka kuniingilia kwenye himaya yangu
..manataka kuingilia himaya ya Ndumba eeh, haya tuone….’akasema na kusogea pale
kwenye dawa zake akatoa kichupa kidogo akatoa unga unga akarusha hewani na
kusema maneno yasiyotambulikana.
Yule
jamaa akawa anamuangalia tu kwa dharau mara kukatanda moshi mkubwa sana
uliokuwa ukikereketa na yule jamaa na askari ambao walikuwa wakihangaika huku
na kule, wakaanza kukohoa na kuanza kupepesuka..
‘Wewe
mzee ndio umefanya nini…unatujaribu na uchawi wako, ngoja tuone uchawi na
risasi ni kipi chenye nguvu, wewe ni lazima ufe…’yule jamaa akajaribu kuinua
silaha kutaka kumlenga huyo mzee lakini hakuweza akadondoka chini…na wala jamaa
wenzake waliokuwa wamerudi kutoa taarifa kuwa hawajamuona mtu wanayemtafuta
wakakutana na huo moshi, wote wakadondoka chini.
Yule
mzee kwa haraka akakusanya zile silaha zao na kuzipeleka nyuma ya nyumba na
alipomaliza kufanya hivyo , akachukua kamba akawafunga wale watu na alipomaliza
akaingia ndani na haikupita muda akatoka akiwa na mkoba wake begani…
Alipofika
hatua chache akakumbuka jambo, akarudi na kuchukua ile bahasha kutoka kwa yule
mtu akaangalia ndani kulikuwa na pesa nyingi tu ambazo hajawahi kuzishika maishani….
Akasogea
hadi kwenye gari la hao watu akaliangalia, akakumbuka ujuzi wake wa kuendesha,
lakini hakuwa na uhakika, hata hivyo hakujali akaingia na kuanza kuliwasha hilo
gari, lakini hakuweza, na kabla hajakata tamaa mara akasikia sauti ya watu
wakikohoa kwa mbalia
Alijua
na hao watu wengine, walikuwa hawajarudi, akatoka kwenye lile gari na kuanza
kukimbia, lakini sauti ya binti yake ikamfanya ageuke nyuma;
‘Baba…ni
sisi…’akageuka na akatoa kichupa cha dawa, akawasogelea, walikuwa binti yake
wakiwa na mgonjwa wao, akawapaka hiyo dawa puani, na kusema;
‘Unajua
juendesha …?’ akamuuliza mgonjwa wao.
‘Ndio
…’akasema Inspecta
‘Tuondokeni
hapa haraka maana hapa kuna hatari…’
‘Kwani
kumetokea nini?’ akauliza Inspecta ambaye bado alikuwa na mawenge mawenge
kichwani
‘Hao
watu walikuja kukuchukua wewe, na kauli yao ya mwisho ni ama kichwa chako au
kichwa changu…’akasema
‘Sasa
umewafanya nini?’ akaulizwa
‘Wanacheza
na mizimu ya kwetu nimewafunga msukule, hapo hawawezi kuamuka mpaka nipende
mimi mwenyewe,lakini nahisi kuna hatari hapa ni bora tuondoke haraka…’akasema
‘Twende
wapi, maana hawa watu wana pesa watatusa hata kwa kutumia ndege angani au mbwa wa polisi…’akasema
‘Kwahiyo
tufanyeje…?’ akauliza huyo mzee
‘Tatizo
ni wewe na familia yako je familia yako ipo karibu , je ukiondoka watakuwa salama?’
akaulizwa
‘Kuhusu
familia yangu usiwe na wasiwasi nao, nitaikusanya huko mbele muhimu tuondoke
hapa….’akasema
‘Ok
sawa…’akasema Inspecta akijitutumua kusimama, akili sasa ilishakaa vyema,kutokana
na dawa za huyo mzee aalizo mpaka tena puani, wakaingia kwenye gari na
kuondoka, kuelekea huko shambani kulipokuwepo watoto wa huyu mzee, na kwa mbali
kukawa na gari jingine likija kuelekea nyumbani kwa huyo mzee
****************
Wakati
hayo yakiendelea Inspecta Maneno alikuwa kwenye chumba cha Inspecta Moto alikuwa
akitafuta kitu, kitu ambacho ni muhimu sana kwake alikitafuta kila mahali hicho
kitu bila mafanikio, mwisho akakata tamaa, na kusema;
‘Labda
aliharibu ushahidi wote, kama alifanya hivyo, atakuwa kaniokoa,maana pale kuna
kila kitu, kama mambo ya kiharibika natumia kama ni uchnguzi niliouwafanya,
vinginevyo, …’akasema akitaka kutoka, na wakati huo simu yake ikawa inaita;
Akapokea
bila kuangalia mpigaji, na sauti yenye wasiwasi ikasema
‘Hatukumpata,
na tumewakuta watu wetu wamefungwa kamba, hawajiwezi, wameleweshwa madawa gani
sijui, wapo kama wamepagawa…’akasema
‘What, haiwezekani…ina maana nyie na
uaskari wenu wote mumeshindwa na mzee wa kijijini, lakini si mlisema kuwa mumeongea
na mzee mmoja ambaye amesema kuwa anaye huyo mtu, na akakubali kuwaonyesha kwa
malipo ya pesa ya zawadi tuliyotangaza…?’ ukauliza
‘Ndivyo
ilivyokuwa lakini naona imekuwa tofauti….’akasema kwa sauti ya kukatika katika
‘Ni
muhimu kulimaliza hilo zoezi sasa hivi…,maana kuna mambo yametokea, na kuna
taarifa kuwa kesho kesi ya mauaji ya mke wa Inspecta inasikilizwa kwa mara ya
mwisho, kama yeye hayupo,na walalamikaji hawapo itafutwa, lakini pia kesi
nyingine imeletwa na watu wasiojulikana …..’akasema
‘Kesi
gani hiyo kumshitaki nani?’ akaulizwa
‘Kuwa
kuna kundi linalotishia amani, na ndilo linalohusika na haya yote yanatokea,
kifo cha muheshimiwa, kifo cha mke wa Inspecta na mambo mengi tu …hii
inaashiria kuwa kuna mtu keshajiandaa kupambana na kundi …’akasema
‘Sasa
tutafanyaje?’ akaulizwa
‘Sisi
hatuhusiki kwa hilo kwa sasa, au sio, sisi ni askari, …msimamo wetu ndio huo,
lakini ili tufanikiwe, ni lazima kusiwe na ushahidi wowote wa kutukwaza sisi na
ndio hapo tunahitajika kuondoa kila aina ya watu wanaotujua kuwa tunahusika kwa
namna moja au nyingine, na mmojawapo ni huyo mtu, mtafuteni, na malizeni kazi…’akasema
‘Ndio…lakini
sasa haonekani….’akasema
‘Kama
haonekani ni bora mjimalize na nyie kabisa……mnasikia, kama hamtakuja na ushahidi
kuwa huyo mtu ni maiti, ni bora nyie mpotee, …bosi hataki kusikia makosa, keshatoa angalizo…’akasema
‘Sawa
afande tutalifanyia hilo kazi, ila tunahitaji mshiko wetu kabisa, mwambie huyo
bosi wako asiyeonekana kuwa hatujalipwa
mshiko wetu kwa kazi zilizopita,…..’akalalamika
‘Kazi
kwanza …’akasema na kukata simu, akawa anaangalia juu ya kabati, alihisi kuona
kitu…lakini…
Na
muda huo huo akasikia gari likisimama nje, akachungulia dirishani, alikuwa mmoja
wa wasaidizi wake wampya wa kitengo cha polisi, ambaye hawaivani kabisa, na
hakujua kafuata nini hapo,na alishatakiwa kumfanya asalimi amri ya kundi, na
harakati zilishaanza, lakini alikuwa bado hajawekwa sawa
‘Kwa
haraka akafunga mlango wa chumba cha Moto, na kutoka nje kukutana na huyo
askari mwenzake, akipanga ni kitu gani cha kumuambia.
‘Kumbe upo hapa mkuu, tumekutafuta na simu
hupatikani, …’akasema
‘Nilikuwa nahakikisha, unajua huyu alikuwa rafiki yangu mkubwa kwahiyo nataka niwe na uhakika wa kila kitu, namalizia
malizia uchunguzi wake kujirizisha, lakini nina uhakika huyu mtu kauwawa, sizani kama yupo hai…’akasema
‘Mkuu
unahitajika makao makuu haraka….’akasema huyo msaidizi wake
‘Kuna
nini tena…?’ akuliza kwa mashaka
‘Inspecta
Moto kapatikana….’akasema
‘Eti
nini….!’
WAZO LA LEO: Kauli ni kitu
muhimu sana cha kuchunga, kauli inaweza kuzua jambo, jambo dogo likawa kubwa
sana, au kauli hiyo hiyo ikamkwaza mwenzako, hata kumuumiza, na huenda hukuwa
na nia mbaya, lakini kwa jinsi ulivyoitoa hiyo kauli, ikatafsiriwa vingine.
Tunapoongea tujaribu kuangalia ni nani tunayeongea naye, na kwa wakati gani, na
kauli zijaribu kuangalia matokea yake, na ili ufanikiwe hilo hebu jaribu kwanza
kujiuliza je kama mimi ningeliambiwa hivyo ningelijisikiaje.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment