Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, July 17, 2014

DUNIA YANGU-6


`Kushoto, kulia, angalia juu, ehe, namna hiyo…’ Alimsogelea yule binti mwanafunzi na kumpapasa kimahaba, kuanzia shingoni hadi sehemu zote za mwili. Tabia kama hii aliipenda na kumpa raha , na hali hii ilimfanya ajisahau kuwa yeye ni mwanamke , na pamoja na kujipenda, kujiremba, kiusichana, lakini moyoni mwake alipenda sana kuwa kama mwanaume

Mawazo haya ya kuwa kama mwanaume humjia mara kwa mara, hasa pale ananapowaona wasichana warembo, na alipoianza hii kazi, akawa anapata nafasi ya kukutana na hao warembo, na hapo akawa anajifurahisha kwa kujiigiza mwanaume...ila leo yupo kikazi zaidi, alikuwa akihitajia warembo kwa ajili ya monyesho makubwa, kwa ajili ya kazi maalumu na mtu asiyempenda kabisa katika maisha yake, lakini hakuwa na jinsi.

Alipokumbuka umuhimu wa maonyesho hayo, akayaondoa haraka yale mawazo mabaya kichwani mwake na kuwaza kazi iliyopo mbele yake. Alitakuwa kupata warembo maalumu kwa kazi maalumu,...kwa ajili ya kufanikisha mambo ambayo hakuwa akiyafahamu undani wake.

Hapo akawa anawaza mengi, na mojawapo ni kumsikitikia yule binti aliyekuwa akimshika shika, kwa kukubali kujiunga naye, kwani pamoja na maonyesho haya, lakini pia kulikuwa  na lengo baya ambalo lilipangwa dhidi yao, na yote kwa ajili manufaa ya mtu ambaye kwake alimuona kama shetani

‘Mhh binti kama huyu ataniingizia mabilioni ya mahela, kwanza mzuri , ana umbo la mvuto, kisomo si haba, kiingereza ndio mwenyewe...lakini ningelijaliwa awe kwa msilahi yangu tu, ...anyway, mimi sijali sana’ akawa anajisemea moyoni


`Umepita, nenda kaandikishe maelezo yako, kwenye chumba kile’ Alimweleza yule binti huku bado akiendelea kumshikashika.

`Mwingine’ aliita kwa sauti kubwa, sauti ya ujasiri, hutaamini ndiye yule aliyekuwa akimshikshika yule binti mrembo. Katika fani yake hii alijua nini na wakati gani afanye nini. Kitu muhimu ni kuwa muelekevu kutokana na wakati, hata sauti inatakiwa iendane na jambo lenyewe.

Mlango ulifunguliwa na aliyeingia hapo hakuamini macho yake. Ilibidi ayaachie yale mafaili aliyokuwa ameyashika na kudondoka chini...

‘Haiwezekani ni wewe...’akasema.

`Rose Mwelekevu... hatimaye umekuja mwenyewe...’akasema na yule binti akamuangalia huku akionyesha kutokuwa na raha, alikunja uso, halafu, akatabasamu.

‘Ndio nimekuja kufanya unachokitaka wewe....’akasema

  Alikumbuka jinsi binti huyu alivyomsumbua kumpata. Huyu ni binti wa jirani yake, baba yake ni mmoja wa matajiri pale mtaa wa Regent. Ni binti wa geti kali, kasomeshwa majuu, na kumuingia ilikuwa kazi, lakini somo alilompa huyu binti inaonekana lilimbadili, na inavyoonekana ameamua kuja mwenyewe,

‘Nilijua ipo siku utakuja mwenyewe.....’akasema na moyoni akiongezea kusema;

‘Na umekubali kuingia kwenye anga zake umekwisha wewe na familia yako, sasa nimeua ndege wawili kwa jiwe moja...baba yako na huyu shetani aliyenipa hii kazi nina usongo nao,...ipo siku, na nahisi siku imeshatimia...’akasema kimoyo moyo, akimkumbuka baba yake huyu mtoto ambaye alikuwa mwiba mkali kwake.

Baba yake huyu binti aliwahi kumchapa pale alipomkuta akiwa mitaani na wavulana, hataisahau siku hiyo, kwani alichapwa vibaya sana, na baadaye akapelekwa kwa wazazi wake, akachapwa tena, ni kipigo ambacho hataweza kukisahau katika maisha yake,kilimuuma sana, akawa anamchukia sana huyo baba, na hadi alipokuwa mkubwa, hakutaka hata kumsalimia.

‘Haya niambie nifanye nini?’ akauliza wakati huo mawazo yake yalikuwa mbali, yakiwaza
 siku alipokuwa akimsubiri huyu binti na hakutokea, na bahati mbaya akakutana na baba yake, na baba yake alimkaripia sana, akimuambia amesikia kuwa yeye ana kampuni ya kihuni yenye nia ya kuharibi watoto wa wenzao

‘Mzee sivyo kama unavyofikiria, nia na lengo langu ni kuwapa ajira wasichana wenzangu, wajishughulishe...’akasema

‘Sitaki kabisa kwa watoto wangu , ole wako nisikie umemrubuni binti yangu nitahakikisha nimeharibu kabisa biashara zako...’akasema

‘Usijali mzee, mimi nafanya kazi kwa kufuata sheria na taratibu za nchi...’akasema na huyo mzee akaondoka.

Akamuangalia yule binti na kusema;

‘Wewe umepita bila kupingwa, ingia pale ofisi ukaandikishe mkataba wako...’akasema akilini akikumbuka siku mbaya kuliko zote, siku ambayo inamfanya sasa hivi afanye hii kazi, ambayo japokuwa alikuwa akiifanya kwa masilahi yake, lakini leo anaifanya kwa masilahi ya shetani mmoja...

‘Huyu shetani ipo siku yake...’akajikuta akisema kwa sauti, na yule binti akasikia na kugeuka kumuangalia

‘Sio wewe binti, kuna mtu mmoja namuwaza sana, mtu huyo sitamsahau katika maisha yangu...’akasema

‘Ni nani huyo?’ akauliza huyo binti

‘Ni shetani mmoja hivi...’akasema na yule binti akatabasamu na kueleka kwenye hiyo ofisi aliyoelekezwa

Katika kumbukumbu zake, siku hiyo aliiweka kama siku mbaya kuliko zote, akawa anakimbuka siku hiyo alipokutana na shetani mnywa damu za watu...

*********.
‘Ni shetani mmoja hivi....’akayarudia yale maneno kimoyo moyo, akiikumbuka siku hiyo ya bahati mbaya...

Ilikuwa ni bahati mbaya na siku mbaya kwake. Hakutarajia kukutana na huyu shetani tena katika maisha yake, kwani aliporejea toka ng’ambo, ambapo moja ya misaada ya ya kufanikiwa kwenye kazi hiyo ya urembo ilitoka kwa huyo aliyemuita shetani. Shetani huyo ndiye aliyemdhamini kwenda kusoma Ulaya na Marekani ambapo huko alihitimu taaluma hiyo ya Urembo.

Tajiri huyu ambaye kwake ni shetani, alikutana naye akiwa mitaani, na muda huo alikuwa akitafuta pesa, na haikuwa kazi rahisi japokuwa alikuwa mrembo, hakupenda iwe hivyo, ila alijikuta akilazimika ili apate pesa za kujikimu akiwa chuoni, pesa zake alizokuwa kapewa,ziliibiwa zote pamoja na nguo zake, akabakia mweupe, sasa ataishije kwenye hicho chuo, akaona ajaribu kazi ambayo hakuwa akiitaka lakini ilibidi ili aweze kuishi na kuonekana mtu.

Basi katika kuhangaika hangaika siku moja akakutana na tajiri huyu, na akapata pesa ambazo hakutarajia, na ikawa ndio mwanzo wa kuwa buzi lake, akawa akilichuna kweli, na kwa jinsi alivyokuwa akipewa pesa, na kutunzwa hata maswala ya shule akayasahau,chuo kikawa ni kupoteza muda.

 Siku moja alimtapeli huyo buzi dola elifu kumi, akapotea jiji, na aliporudi kuchukua baadhi ya vitu vyake, ilivyokuwa kaviacha, alikakamatwa na kwa mara ya kwanza akaingizwa ndani ya jengo la kifahari la huyu tajiri, jengo hilo lilikuwa na vyumba vya chini kwa chini, na siku hiyo akapelekwa ndani ya chumba ambacho hatakisahau,

Chumba hicho ambacho kipo chini ya ardhi, kilinakishiwa kwa umaridadi wa hali ya juu, lakini pamoja na hayo kulikuwa na kila aina ya vifaa vya utesaji, na akalazwa juu ya meza akiwa kafungwa mikono na miguu kwenye meza, huku akavuliwa nguo na kubakia kama alivyozaliwa, akaachwa hapo juu ya meza kwa dakika kadhaa.

Haikupita muda akaingia jamaa, pande la mtu, jamaa huyo ni kama mnyama, mwili wote una manyoya, na kashupaa kama muinua vyuma, alikuwa na sura kama ya nyani, macho yake yalikuwa yakitisha, binti huyu hajawahi kuona mtu kama huyo kabla,...

‘Mungu wangu...’akasema akihisi mwili mzima ukizizima kwa woga

‘Usijali, sina nia ya kukuumiza, ila nataka kukuonyesha, jinsi gani ninavyoweza kukufanya pale mtu unapokiuka masharti yangu, unakumbuka nilipokuchukua mitaani ulisema nini?’ akaulizwa na sauti iliyokuwa ikitokea juu, lakini hakuweza kumuona aliyekuwa akiongea

‘Nisamehe bosi...’akasema huku akimuangalia yule mtu aliyekuwa kasimama mbele yake, akiwa kavaa chupi tu.

‘Sihitajii maombi yako ya msamaha, mimi nataka nikutengeneze, nimeona pamoja na mengine mengi unaweza kuwa mtu muhimu kwangu, nahitajia kipawa chako, nakuhitaji uje kufanya kazi na mimi...’akasema

‘Kazi , kazi gani?’ akauliza

‘Kwanza nataka ukasome, nataka ukasomee hayo mambo yako ya urembo, lakini ni zaidi ya huo urembo, nataka ukirudi uje kufungua chuo cha warembo, na hao warembo watakuwa na kazi maalumu, utakuja kuifahamu ukiwa huko masomoni...’akaambiwa

‘Niende kusoma nje..?’ akauliza akiwa haamini

‘Unashangaa, ....wengi niliwaambia hivyo wakashangaa kama wewe,nawasubiri warudi, wapo wanasoma na wewe utakwenda kusoma,ukirudi tutaanza kazi maalumu, nataka kutumia vipaji vya watu kwa nia ya maendeleo zaidi ...’akaambiwa

 Ni kweli ilikuwa kama ndoto, lakini ikawa kweli, binti huyu kweli alipelekwa ulaya kusoma..na alipofika huko hakupoteza muda wake, hakutaka kulirudia lile kosa alilowahi kulifanya, akaisimamia vyema hiyo elimu, kwani ni jambo alilokuwa akilipenda, alijifunza mambo mengi ya urembo, mavazi, na mambo mengi ya wanawake,

Pia alijifunza kuhusu miili ya wanadamu, hisia zao, akili zao,ujasiri, kujiamini, zaidi sana ni urembo, na kumjenga mwanamke kimaumbile, akili na muoenekano, mafunzo hayo  aliyofundishwa yalimjenga sana kiakili, na kuwa jasiri zaidi, na huko ndipo alianza kujijengea hulka ya kuwa mwanaume-mwanamke...

Alirejea kinyemela, akijua huyo bosi keshamsahau na atakuwa kapata watu wengine, maana masomo yake yalikuwa ya mwaka mmoja tu,

‘Mtu kama huyo anayependa wanawake, atakuwa ameshanisahau,..na hata akiniona atakuwa ameshanisahau, nimejibadili sana, kimaumbile , kitabia na kimwenendo,...cha muhimu sasa ni kuanzisha kampuni yangu binafsi...’akajisemea na kweli akaweza kufanya hivyo, akaanzisha kampuni yake ya mitindo na urembo.

Kutokana na ujuzi wake alioupata huko Ulaya, aliweza kuliteka soko hilo la mitindo na urembo, na humo aliweza kufanya mambo mengi aliyoyataka mwenyewe, na hata kuwarubuni mabinti kufanya biashara za kujiuza, na kampuni yake ikakua kwa haraka, kutokana na shughuli zake, na haikupita muda akaweka kasino la ndani kwa ndani.

Siku moja aliamua kutoka kwenye eneo lake na kwenda kustarehe kwenye hoteli moja , akitafuta kubadili mazingira, na kupata muda wa kuwaza mambo yake, alipofika kwenye hiyo hoteli,kwa vile ni mtu mashuhuri akakaribishwa kwenye chumba maalumu, hakupenda kukaa huko, akasema;

‘Hapana leo nataka kujichanganya, nitakaa pale...’akaonyesha meza moja iliyokuwa pembeni kabisa kwenye chumba hicho cha hoteli, ni sehemu ya vinywaji na vyakula maalumu

‘Karibu sana bosi wetu,....’akakaribishwa, na yeye akaenda kukaa kwenye hiyo meza, akaagiza alichopenda, na wakati anasubiria vinywaji vyake na vitafunio vyake ambavyo ni nyamaa maalumu, mara akaja muhudumu mwingine wa hiyo hoteli, akamwambia;

‘Kuna mgeni mmoja amefika anasema anataka kuja kuonana na wewe...’akasema

‘Ni mgeni gani huyo mbona sina miadi na mtu yoyote, na hata hivyo,leo sitaki kuongea na mtu nina mambo yangu ya kuwaza, nataka upweke...nileteeni vinywaji vyangu, mwambieni hana nafasi ya kuongea na mtu kwa sasa, kwanza ni nani huyo mtu?’ akauliza na kusema

‘Huyo mtu kasema ni muhimu sana, ...’ akasema

‘Hakuna mtu muhimu kwangu kwa sasa, naomba unielewe hivyo, nahitaji kuwa peke yangu...’akasema kwa hasira

‘Samahani bosi, mimi nafikisha ujumbe tu, yeye kasema ukimjua hutakasirika, kwani ni mtu muhimu sana kwako...’akazidi kusisitiza yule muhudumu.

‘Kwanza ni nani huyo mtu ...?’ akauliza na kabla swali lake halijajibiwa na huyo binti, mara kwa mbali akamuona mtu akija kuelekea pale alipokuwa amekaa

‘Huyu ni nani...?’ akawa anajiuliza maana mtu huyu alikuwa na suti kali ya bei mbaya, machoni kavaa mawani makubwa meusi ya baei mbaya, nahisi hakutaka kujulikana sura yake, akawa anakuja kwa madaha akionekana ni mtu tajiri sana, nyuma kulikuwa na watu , nahisi ni walinzi wake, akawaonyeshea ishara ya kusubiri, ...akawa anakuja peke yake

Kwa jinsi alivyoonekana, huyu mdada akawa na hamu ya kumuona sura yake, kwahiyo akamuashiria huyo muhudumu aondoke kwa mkono, na yule muhudumu akaondoka, na akawa sasa anamsuburi huyo jamaa afike kwenye meza yake.

Yule jamaa alipofika pale karibu kwenye meza, akasalimia kwa kusema;

‘Samahani mpendwa, natumai sijakuvurugia siku yako...’akasema na kugeuka kumuangalia muhudumu aliyekuwa anataka kuondoka, akasema;

‘Nakushukuru sana muhudumu, unaweza kuendelea na shughuli zako, hakutaharibika kitu...’akasema, na mdada akawa katulia akijaribu kuikumbuka sauti hiyo ni ya nani, lakini hakuweza kukumbuka, maana alishakutana na watu wengi wanaoongea hivyo, Kiswahili chenye lafudhi ya kizungu.

Yule mtu alipohakikisha yule muhudumu kaondoka,yule mtu kwa taratibu akatoa mawani yake, na akafanya jambo la ajabu, alipitisha kiganja cha mkono wake usoni, akatoa ngozi,....kumbe ni uso wa bandia, na ana kwa ana akawa anaangaliana...na na

‘Oh, Di-amu, my God, ...’akasema huyu binti akitaka kusimama ikiwezekana kukimbia, lakini hakuwa na jinsi, zaidi ya kunywea na kusikiliza atakachoambiwa, akamtupia jicho tajiri huyu na tajiri huyu akawa anamuangalia kwa tabasamu mdomoni

‘Ndio mimi, ..japokuwa spendi sana kuonekana onekana,...na hii hoteli ni moja ya hoteli zangu kwahiyo usiwe na wasiwasi...’akasema

Ni kweli tajiri huyu ni nadra sana kuonekana hadharani, wengi wanajua hayupo hapa nchini, huwezi hata kuona picha yake kwenye gazeti au vyombo vya habari, leo alishangaa kumuona tajiri huyu akimtokea mwenyewe. Mara nyingi akihitajia kitu au kufuatilia jambo huwa anamtuma mfanyakazi wake anayemuamini.

 Mdada huyu akamuangalia huyu mtu kwa macho ya kujiiba iba kuhakikisha kuwa ni kweli ndiye yule mtu, anayemfahamu. Ndio, ni yuleyule. Alikuwa yule yule jamaa, hazeeki, mtanashati, na mpenda raha, bwana Di-amu. Jina hili lilikuwa kama jinamizi kila alipolifikiria na mara nyingine alimuota na kumwita Damu, ikiwa na maana mtoa damu za watu, au shetani mtoa damu za watu.
 
‘Ni mimi ...huamini eeh,?’akasema huyo mtu akitabasamu na kumuangalia huyu mdada kwa kujiamini

‘Khaaa, siamini,....mbona nimesikia kuwa haupo hapa nchini,...haya niambie unataka nini kutoka kwangu, au unahitajia nikulipe gharama zako ulizotumia kwangu ....’akasema na huyo jamaa akacheka sana, na kusema;

‘Eti unataka kunilipa gharama zangu, hivi kweli unaweza kuzilipa, acha mzaha! Nikuulize ndivyo tulivyokubaliana wakati nakutuma kwenda kusoma huko Ulaya?’ akauliza

‘Ulinisaidia sawa, sikatai na ninakushukuru sana, lakini nimeona bora nianzishe kitu changu, ili niweze kusimama kwa miguu yangu, na nikipata gharama zako nije kukulipa fadhila zako...’akasema

‘Mpendwa, hilo sio jibu la swali langu, mimi nimekuuliza je hivyo ndivyo tulivyokubaliana wakati unakwenda kusoma huko nje..., mimi sihitajii kurudhishwa hizo gharama, kabisa sihitaji, nafahamu sana hizo ndizo shukurani zenu,....’akasema

‘Kwani nimefanya kitu gani kibaya, mimi nilipofika, nilisikia haupo, upo, nikaona nisikae bure, nijishughulishe, ...kuna ubaya gani hapo...?’ akauliza

‘Na kauli zenu ni kama mlipanga, maana wenzako wote niliwafanyia hivyo hivyo, na wote waliporudi wameanzisha makampuni yao, wakiwa na kauli hizo hizo, na wamefanya hivyo wakihisi sitaweza kuwaona, hivi kweli unaweza kujificha kwenye hili jiji, mnajidanganya....’akasema

‘Lakini mimi sijajificha, kila kitu changu kipo wazi....’akasema

‘Ulitakiwa kuja angalau kunisalimia, halafu uniambie malengo yako, nisingelikukatalia, lakini umeshaharibu, umeshanionyesha jinsi gani ulivyo, japokuwa nafahamu ni ni ungelifanya,...’akasema

‘Kama ulifahamu kuna haja gani ya kuniuliza, sioni ubaya wake, wewe nisubiri niweke mambo yangu sawa, nitakuja kwako tukae, tuone unanidai shilingi ngapi, na mimi nitaangalia mahesabu yangu,...nitakulipa tu...’akasema

‘Unajidanganya binti, wewe na wenzako mumefanya hivyo mkijifanya sitawaona, nyie, hasa wewe umesahau kuwa mimi kwenye jijini hili, na sehemu kubwa ya nchi, nina masikio na macho ardhini, unakumbuka ulivyoniibia zile pesa ulipatikanaje,...mimi naweza kusikia kila kitu na kuona kila kitu kinachoendelea kwenye hili jiji, kama kina masilahi na mimi..., kamwe huwezi kujificha, labda ukimbilie vijijini ambapo sijawahi kuwekeza...’akasema

‘Lakini boo-si nilifanya hivyo kwa nia njema kabisa...’akasema akitamka neno bosi kwa dharau, hakutaka kumuita mtu mwingine bosi wakati yeye mwenyewe ni bosi wa kampuni yake.

‘Najua kabisa, ...una nia njema ya kujiwekeza, ili usije kufanya kazi na mimi, nakufahamu sana, kwa ujanja-ujanja wako, tabia ya mtu haiwezi kujificha, lakini nikuambie ukweli mimi napenda sana hiyo tabia yako japokuwa ni tabia mbovu...’akasema

‘Mimi sio yule binti wa mitaani tena, najitambua na akili yangu imepevuka...amini hilo nakuambia...’akasema

‘Sawa, kama ingelikuwa hivyo, ungelionyesha busara, kwa kuja kwangu angalau kunisalimia,...tusipoteze muda, mimi  nataka kutumia huo ujanja ujanja wako, kwa lile swal nililowahi kukuambia kabla hujaenda kusoma,...nataka tutumie ujuzi wako, elimu yako, uzoefu wako, na kampuni yako, kufanya yale niliyoyakusudia...’akasema

Boo-si mimi kwakweli kwasasa sitaki kufanya kazi kwa mtu, sitaki kabisa kuwa mtumwa wa mtu,....’akasema

`Sijasema uje kufanya kazi kwangu,...hapana wewe utaendelea na kazi zako, na ndilo lengo langu, kila mtu ajishughulishe na kazi yake, ninachotaka kufanya ni kuwekeza hisa zangu kwenye kampuni zenu, na humo tutaendelea kufanya yale niliyoyapanga, ....’akasema

‘Natumai umenielewa, huwa sipendi kurudia rudia, mimi ni mtu na wadhifa wangu, nina watu wananiangalia kama bosi wao, iweje sasa niwe chini ya mtu mwingine, hapana hilo halitawezekana sitaki kabisa kuchangia na mtu yoyote...’akasema

‘Mrembo, unajifanya umesahau fadhila zangu sio, au ndio fadhila zenu za punda.Sikia binti najua mlivyo mkifanikiwa hamjali wafadhili wenu, mnajiona mumefika. Sasa mimi natoa amri, sio ombi tena, na nataka ulitekeleza, na kwa kuanzia, nataka unifanyie kazi moja kwa hivi sasa...’akasema

‘Kazi!, kazi gani wewe mtu, naomba unielewe, mimi ni bosi wa kampuni zangu huwezi kunutuma kazi yoyote, nimeshakuambia kama ni gharama zako nitakulipa, naomba unielewe hivyo, sitaki kusumbuana na watu, nina mambo yangu mengi ya kufikiria, ndio maana nilikuja hapa niwe peke yangu, sasa umeniharibia yale yote niliyokuwa nikipanga kichwani...’akasema huku akisimama kutaka kuondoka, lakini jamaa huyo akasimama, na kumuwahi wakawa wameangaliana wakitoleana macho

‘Nimekuelewa kuwa wewe sasa ni bosi, ila nataka hizi kadi za mualiko ziwafikie walengwa, na hakikisha wanafika kwenye hoteli yangu ya Paradiso bila kukosa, pia na wewe ni mmoja wa waalikwa...’akasema na kutoa bahasha kubwa na kuweka mezani

‘Kumbuka...ni muhimu sana, na hakikisha wote wamefika...na wewe mwenyewe ukiwemo, vinginevyo, utanisahau katika maisha yako, utapotea katika hii dunia, ....’ Sauti hiyo ilienda sambaba na mikono ambao ilishafika begani kwake, kama wapenzi waliokuwa wakiongea, mkono huo mmoja ukawa ukitembea kutoka begani ukashuka na kupanda na kumfanya binti huyu ahisi mwili ukimsisimuka, akawa anakumbuka enzi zao na huyu buzi

Binti huyu aliduwaa, akageuka kuiangalia ile bahasha kubwa mezani, ambayo huenda ndani yake kuna hizo kadi, hakutaka kabisa kuigusa, lakini alijua kuwa kukataa kungelimuharibia kazi yake, kwani huyu jamaa akisema neno ujue kweli atalifanya, na anaogopewa, hatanii...

Akukumbuka wasichana anaowajua waliopotea kimiujiza,na kuna fununu kuwa aliowafanya wapotee ni huyu tajiri, japokuwa polisi hawakuweza kulisibitisha hilo, kwani huyu mtu mwenyewe haonekani, na inajuliana yupo nchi za nje.

Lakini yeye kama bosi wa kampuni yake hawezi kufanya hiyo kazi,kwanini yeye ndio afanye hiyo kazi, kuna wahudumu, wanaweza kuifanya hiyo kazi,huku ni kuzalilishana. Lakini akilini akasema, au nifanya tu iwe namna nyingine ya kulipa fadhila...hata hivyo sipendi huyu mtu anione mnyonge, nataka anitambue kuwa mimi sio yule binti wa mitaani tena..’ Alijisema moyoni

Akainua mkono wake na kuondoa ule mkono wa huyo bosi, uliokuwa unaendelea kumshika shika, akasogea karibu na ile meza akainama kuichukua ile bahasha kubwa akiwa na dhamira ya kumrejeshea huyu jamaa na kumwambia;

‘Go to hell...’

Aliinama kuichukua ile bahasha pale mezani, na alipoishika, akainua kichwa kumwangalia huyo tajiri , lakini hapakuwepo wala dalili yake, na macho yake yalitua usoni mwa mtu ambaye alimfanya atake kutapika, na kujisikia kichefuchefu.

Mtu huyu alimuona mara moja kwenye jumba la kifahari la tajiri huyu, siku alipoweka mezani akiwa uchi, mtu huyu japokuwa alikuwa kavaa suti kali, na kwanza machoni alikuwa kavaa kofia na mawani, na baadaye akayatoa yale mawani, na kumuangalia huyo mdada...

Mdada alihisi mwili ukitikisika kwa woga,...akikumbuka kazi ya huyu mtu ambayo ni kutesa watu, na kutoa roho za wale wasiotii amri ya bwana wake. Mara nyingi akitumwa kwako ukiwa nje ya hilo jengo lao ujue kuna mawili, kukupa onyo, au kuitoa roho yako. Na ukiwa ndani ya jengo hilo hiutwa kwa ajili ya kukupa mateso au kuitoa roho yako. Huyu ndiye mkono wa Diamu...

Huyu mdada alipomuona huyu mtu, kasimama mbele yake, hakutaka hata kusubiri, woga ulimtanda, akataka kupiga ukelele, lakini akajipa moyo, alichofanya ni kuichukua  ile bahasha na kuanza kukimbia kutoka nje ya hiyo hoteli, akimpita muhudumu akiwa na vinywaji alivyokuwa akimletea, muhudumu alibakia kaduwaa...

NB Mambo ndio hayo,


WAZO LA LEO: Zipo tabia za kukera, na hazifai katika jamii, lakini wengine wanaona ni kawaida tu, sio vyema kabisa, tunatakiwa kujifunza jinsi gani ya kuishi na watu kwa ustaarabu. Kama wewe unapenda kelele, wengine hawapendi kabisa hizo kelele, wengine wana matatizo ya kiafya, kelele kwao ni adha, lakini utawakuta watu wanafungulia redio, au televisheni zao kwa sauti kubwa inakuwa kero,..unawaathiri wengine. Tujaribu kuwa waungwana kidogo.

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Yasinta Ngonyani said...

mmmhhh ..kujua kusoma ni raha na pia utamu sana...utamuuuu