‘Ndugu muheshimiwa
hakimu, katika orodha ya mashahidi huyu mtu hakuwepo, jina lake halipo kabisa,…iweje
aletwe sasa hivi, na kwaharaka apewe hiyo nafasi, kiukweli sisi tunashindwa, na
tunapojaribu kushinikiza ili utaratibu ufuatwe, tunashindwa muheshimiwa hakimu…’akasema
mtu wakili wa benki.
‘Kwahiyo unanilaumu
mimi, au…?’ akauliza hakimu akimuangalia huyo wakili.
‘Hapana muheshimiwa
hakimu….’akasema huyo wakili kwa adabu.
‘Mahakama inafanya
kile inachoona ni sahihi, je hayo yaliyoongewa na mashahidi ungeyafahamu vipi
kama tusingelifanya hivyo, ..?’ akauliza hakimu na wakili huyo akabakia kimia.
‘Kazi ya mahakama ni
kuhakikisha haki inatendeka, wakati mwingine inabidi tufanye hivyo , ili sauti
za wengine ambazo zinahitajika kusikika zisikike,…shahidi aliyefika sasa hivi kasema
ana ushahidi, na mahakama hii imekuwa ikisubiria huo ushahidi, ..ili haki iweze
kutendeka, wewe una wasiwasi gani mpaka hapo…?’ akauliza hakimu
‘Hakuna wasiwasi
muheshimiwa hakimu, maana sisi tunao
ushahidi wa kutosha, ushahidi ambao mahakama iliutambua awali, hatuna shaka na
hilo…’akasema wakili huyo.
‘Kama ni hivyo, basi,ngoja
wenzako na wao waweze kuonyeshe ushahidi wao, kama ni wa halali, tutaliona
hilo, ..ili tuhukumu kwa haki,…usilalamika kuwa utaratibu haupo, utaratibu upo, kwa namna
hiyo,…’akasema hakimu.
‘Sawa muheshimiwa
hakimu…’akasema wakili yule akigeuka kumuangalia huyo shahidi aliyefika…
Wakili wa upande wa wale
wanaodai kuwa madeni sio ya halali, akasogea mbele,…
‘Sio kweli kuwa huyu
shahidi hakuwepo kwenye orodha yetu,
shahidi huyu alikuwa muhimu sana kwetu, kwani yeye ndiye aliyekuwa
akishirikiana na watu wa usalama, kulifuatilia hili jambo, lakini akaja
kuumizwa, na kalazwa hospitalini…’akasema wakili huyo.
‘Na sasa ameweza kugundua
ushahidi muhimu kwenye hii kesi, na muheshimiwa
hakimu muda wote amekuwa akisisitizia hilo la ushahidi, maana walengwa,
wanaodaiwa kuwa wana madeni, hawakubaliana nayo,…sasa ushahidi umepatikana, muhimu tuona huo
ushahidi ulivyo,…’akasema wakili.
‘Sawa…tuonyesheni,
lakini usiwe wa maneno matupu, kiutaratibu wa kibenki, tunahitajia, maandishi,
..…’akasema wakili wa benki, kwa kujiamini
‘Wewe subiria tu, kila kitu kipo ,..mtu wa kuutoa huo ushahidi ndio
huyo,… hapo …’hata kabla hajamaliza hakimu akasema;
‘Wewe shahidii una
uhakika unao ushahdii wa kutosha maana muda umekwisha, tusije kupotezeana muda
tena hapa,… kama haujakamilika ni bora tuisitishe hii kesi, itakuja kuendelea
tarehe nyingine..?’ akauliza hakimu.
‘Ninao huo ushahidi muheshimiwa hakimu, …’nikasema na kabla hakimu
hajasema neno, nikaongea;
‘Na pamoja na huo
ushahidi, nina ombi moja muheshimiwa
hakimu …’akasema shahidi huyo mpya
‘Ombi gani tena…?’
akauliza hakimu huku akiangalia saa, na kukunja uso kidogo, kuashiria muda
unakwisha
‘Ningelipenda shahidi
aliyotoa maelezo mengi awepo hapa mbele, ili athibitishe ushahid huo, na
ahojiwe kuhusiana an ushahidi huo, maana yeye ndiye anayeufahamu zaidi, na
maelezo yake yatarahisisha kulimaliza hili tatizo, ..’akasema shahidi aliyefika
**********
Yule shahidi aliyekuwepo awali, akaitwa tena,
..alipoingia na kumuona huyo shahidi mpya aliyefika, akamuangalia, halafu
akacheka,…
‘Umepona…?’ akasema
hivyo tu, na mimi sikumjibu, nikampisha yeye akae sehemu huyo ya shahidi, na
mimi nikawa nimesimama kama wakili…japokuwa
maswali yangu sio ya kama wakili, bado wakili alitakiwa kuniongoza.
‘Umesema umeleta
ushahidi, sasa tunataka wewe uutoe huo ushahidi wako, na uendelee kumuhoji huyo
mtu uliyetaka kumuhoji kutokana na huo ushahidi…’akasema wakili.
‘Labda kwanza,
ningeliomba tuliweke hili wazi, ushahidi wangu pamoja na nyaraka, bado
unahitajia maelezo ya huyu shahidi, niliyemtaka aje hapa, nia ni kuthibitisha
hizo nyaraka na kupata maelezo yake,…’nikasema
‘Lakini nyaraka hizo,
au ushahidi huo unaonyesha dhahiri hilo deni lilitokea wapi, au. Hilo deni ni
la nani…?’ akauliza wakili
‘Bila shaka, ushahidi
huu unaonyesha deni lilivyotengenezwa, na nani ni muhusika wa hilo deni,
…muhimu ni shahid huyu kuwa mkweli,..’nikasema
‘Haya nakuachie
undelee na mtu wako,..ningeliwaomba upande wa pili, wasiingilie kwanza, ili
tuweze kuupata ukweli, kwasababu nia yetu ni kupata uhakika wa hilo au hayo
madeni,…’akasema wakili mtetezi wa madeni.
Wakili wa benki
akatikisa kichwa kama kukubali kwa shingo upande, akasema
‘Sisi hatuna shaka,
maana ushahidi halali tunao…’akasema
‘Sawa ngoja
tuone….’akasema wakili mtetezi wa madeni, akiniashiria mimi niendelee…
*************
Yule shahid aliendelea
kuniangalia mimi huku akitabasamu, akijifanya hana wasiwasi kabisa. Ni kweli
kwa muonekano wake pale, iliashiria hivyo.
‘Ndugu jina lako
halisi ni nani……?’ nikamuuliza, na wakili wa benki akataka kuingilia kati, na
…huyo jamaa akawahi kujibu, bila kumjali huyo wakili.
‘Jina langu kama
nilivyojitaja awali, naitwa..’akataja jina lake kwa kifupi vile vile.
‘Una uhakika hilo ndio
jina lako kamili,…maana naona kama ni kifupi cha majina yako, au wewe una
majina mangapi ya kisheria..?’ nikamuuliza.
‘Majina ni majina tu,
..naweza kuyataja kwa kifupi kwa kirefu, ilimradi kunakohusika nimeshaandika au kutaja majina yangu yote, au kuna tatizo kwenye hayo majina yangu…’akasema
na kama kuuliza.
‘Majina yako kwa
kirefu ni nani, nataka uyataje mahakama iyasikie..?’ nikamuuliza, hapo akasita,
na wakili wa benki akaingilia kati , akisema mimi napoteza muda, badala ya
kuonyesha huo ushahidi nauliza mambo yaliyokwisha kuulizwa.
‘Nina maana yangu
kubwa kumuuliza maswali hayo maswali, kwani yanaendana na huo ushahidi nilio
nao,…, shahidi huyu ana majina mengi, na katika nyaraka zake za kumbukumbu
kaandika majina tofauti tofauti, hii ina maana gani,…?’ nikauliza.
‘Hayo ni majina yangu,
nayamiliki mimi, naweza kuandika nipendavyo,..kwani kuna tatizo gani kwenye
hayo majina yangu…’akasema
‘Kwanini unatumia ni
muhimu sana tukalifahamu hilo…, maana hapa tunautafuta ukweli wa jambo, ukweli
wa kumbukumbu zako, ambazo zinaendana na hayo madeni, je unaweza kutuambia ni
kwanini unatumia majina tofauti tofauti…?’ nikauliza na hapo akageuka
kumuangalia hikimu, alipoona hakimu anamuangalia yeye, akasema;
‘Natumia majina hayo
kwa masilahi yangu binafsi, je kuna sheria inayomkataza mtu kutumia majina yake
apendavyo…, ilimradi haikizani na sheria au mahitaji ya serikali, niambie…?’
akauliza huyo shahidi.
‘Ninachotaka kufahamu
ni kwanini sehemu nyingine unatumia majina mengine na sehemu nyingine majina
mengine, wakati sehemu hizo ulitakiwa uandika majina yako kwa kirefu, …?’
nikamuuliza
‘Jibu rahisi ni kwa
kupenda mimi mwenyewe,…. na jibu unalotaka wewe, najua ndivyo unavyotaka wewe,
nimekuwa nikitumia majina hayo, nikiwa na maana yangu maalumu kibiashara,…’akasema
‘Tufafanulie
tafadhali, au biashara zako ni za siri, kampuni zako ulizoanziasha hutaki watu
wakufahamu au, ni sababu gani ya msingi,…?’ nikamuuliza
‘Ni kweli mimi ni
mfanyabiashara, nina vitega uchumi vyangu hapa na pale, na sio haramu,…na katika
biashara kuna mitihani yake, ushindani wa biashara nk..…mimi nafanya hivyo, kwa
nia ya kujihami, kwa namna moja au nyingine,..sihitajii kueleza hili kwa undani
zaidi, maana hapa wapo watu wengi, unanielewa hapo..’akasema
‘Jina lako la mwanzo halisi
ni lipi…?’ nikamuuliza, akaonekana kukerwa na hilo swali, lakini akasema kwa
shingo upande.
‘Majaliwa…’akasema
‘Sio majalala ?…., je
hilo la Majaliwa,Ulilitaja hapa mahakamani…?’ nikamuuliza
‘Niliandika
hivyo..lakini sikulitaja hivyo, kwa masilahi yangu yangu binafsi, na sikuulizwa
nilitaje, kama ulivyotaka wewe, na hali ya kidunia sasa hivi inajulikana, mtu
anajijua mwenyewe anachokifanya,.. mwenye kuelewa hilo kama mfanyabiashara, hana haja ya kudadidi sana kuhusu hilo…’akasema
‘Nakumbuka kwenye
maelezo yako, ulisema nesi, au docta sijui aliyeandika jina lako, aliandika kwa
dharau..kwa vile mama yako hakuweza kulitaja vyema…kitu kama hicho, wewe
uliliongelea hilo jina…hapa nakuuliza unasema jina sio muhimu, huoni kama
unatuficha kitu hapo…?’ nikamuuliza.
‘Nikufiche nini bro…,
sijaficha kitu kwenye jina langu, kama kuna kitu nimeficha, tuambie, hapa ni
sehemu wazi, mahakamani…’akasema
‘Nikuambie…?’ nikawa
kama nauliza
‘Ndio niambie, mimi
sina shaka na hilo, hayo ni majina yangu na sikufanya hivyo kwa ajili mbaya…’akasema
‘Jina lako unaitwa
Majaliwa,…na hayo majina mengine umekuwa ukiyatumia pale unapokuwa na shughuli
zako maalumu, au..ni kwa vile hukutaka itambulikane wewe ni nani , kwenye
baadhi ya shughuli zako,..’nikasema
‘Unaweza ukawa sahihi,
…sijui una maana gani, ukisema maalumu, au shughuli zako…’akasema
‘Sawa, wewe kwa mara
ya mwisho ulikuwa mfanyakazi wa kampuni gani..?’ nikamuuliza
Shahidi kwanza
akatabasamu, baadae akasema;
‘Ndio ushahid wako huo,…
nilijua unapekenyua kwenda wapi,…maana mimi ni mfanyabiashara, nimeshaeleza
hilo…’ akasema.
‘Kabla ya kuhamia kuwa
mfanyabiashara na muwekezaji, ulikuwa ukifanya kazi gani..?’ nikamuuliza,
halafu akatabasamu
‘Hahaha, wewe unazungukaaa,
kwanini husemi moja kwa moja…hahaha…, najua ulikuwa unataka kufika huko, ..mimi
nilikuwa nafanya kazi benki, sawa, ehee…’akasema akitikisa kicha na kubenua
mdomo kama kebehi fulani hivi.
‘Na wakati upo benki
ulikuwa ukitumia jina gani…?’ nikamuuliza na hapo akaangalia mbele akitabasamu,
ile ya kuonyesha anafurahia hiyo hali.
‘Kumbukumbu zangu zipo
wazi, jina hilo hilo , Majaliwa,…’akasema
‘Kwenye baadhi ya kumbukumbu zako za barua,..hata mawasiliano
ndani ya ofisi, ulikuwa ukitumia kifupi,… ulikuwa hupendo kutumia jina lako
hilo, wakati wewe ulikuwa sehemu nyeti kama hiyo, ni kwanini labda…’nikamuuliza.
‘Sikumbuki hilo…kuwa
nilikuwa natumia jina kifupi,..lakini hata hivyo, kama muajiri wangu angelikuwa
na tatizo na hilo, angelisema, au sio…au waliokuwa waajiri wangu kipindi hicho,
wamesema lolote kuhusu hilo…’akasema
‘Umeanza kusema
hukumbuki…lakini wewe umedai kuwa una akili sana, sizani kama maswala ya
kumbukumbu za ofisini , hasa za jina, na ulichokuwa ukifanya, unaweza
kusahau,…au ?’ nikamtega hivyo.
‘Hahaha ndugu yangu,
usione kwanini nakujibu hivyo, najua unataka nini, kiukweli kama ningelikuwa
mtu wa kawaida ningelishasahau yote ya benki, lakini akili yangu ina kumbukumbu
kubwa, kama nitasahau baadhi,…ujue ni bahati mbaya tu…’akasema
‘Vizuri, kama ni hivyo
utanisaidia sana…’nikasema sasa nikiogea kidogo mbele.
‘Hahaha…najua
unaelekea wapi ndugu yangu, tusipoteze muda, mimi nitakuambia hicho
unachokitafuta wewe kutoka kwangu…’akasema
‘Kama unakijua
ninachokitafuta basi niambie..ili tusipoteze muda…’nikasema
‘Maelezo yangu mengi
ya awali, yalilifafanua hilo, wewe hukuwepo,…mimi nililiweka hilo bayanai, kuwa
pamoja na mengine mengi,… mimi nilikuwa natafuta namna..ya kuwezesha, haki ya
wahanga, haki ya mama yangu mzazi,.., haki ya mama yangu mlezi, haki yangu mimi
mwenyewe viweze kufika sehemu kama hii, na haki iweze kutekelezwa,,’akatulia
nikajua kamaliza,
Na pale nilipotaka
kuuliza swali, akaendelea kuongea;
‘Kwa vyovote vile,…niliyoyafanya,
yaliyotokea kwa kupitia kwangu, sikuwa na maana nyingine japokuwa, kuna hili na
lile,…kama nilivyosema awali, kuna muda tamaa ya pesa iliniingia, hata hivyo,
kama hao walidhulumu walitumia pesa kama silaha yao, ulitaka mimi nifanye nini,
eeh….’akawa kama anauliza
‘Kwahiyo nilipokuwa
hapo kazini,..ambao wewe umepalenga… ndio nikaona ..nipo kwenye nafasi nzuri,
ya kuitumia hiyo silaha ya pesa,..kulifanikisha lengo langu..’akatulia
‘Najua nikisema hivyo,
wengi wanafikiria kuwa nilitengeza hilo au hayo madeni hivyo..mimi lango na nia
yangu, ni kuwatumia wababe hao walionidhulumu mimi na familia yangu, ili mwisho
wa siku wafike hapa..
‘Nia na madhumuni
yangu, ni ili kuisukuma haki ije kutendeka, na nilikuwa natamani sana nije hapa
niyaelezee hayo niliyoyaelezea, je ningelikaa kimia, ingefika hapa, sasa kama
kuna watu wameumia, nawaomba wanisamehe sana, ila wakumbuke mama yangu
aliumizwa, tena sana…’akasema.
‘Umemaliza…?’
nikamuuliza
‘Mhh, labda kama
unataka maelez o zaidi ya hayo…’akasema
‘Lakini hayo
uliyoyaelezea hapa, hayo…’nikaonyeshea ishara ya vidole ya kuaongea…,
‘Ni maneno tu ya
kujihami, hayajaweka bayana kuhusu madeni hayo ya watu, na hao watu sio wao
waliokufanyia huo ubaya, hilo lipo wazi …mbona umewalenga hao watu, kama mama
mjane na watoto wake, …mama mjane na yatima, na sio hao tu wapo wengine,…kwanini
unawadhulumu watu haki zao, huna huruma wewe…?’ nikauliza
‘Nikuulize swali moja,
je mimi nilikuwepo wakati baba anamtesa mama,..kwanini mimi naumia, nateseka
kwasababu ya hilo….damu ..ina nguvu, na…kama nisipofanya hivyo, haki yangu
nitaipataje maana ukisema hivyo, ina maana kwa vile sikuwepo, basi nisahau,
nisahau pia na kudai haki yangu, si ndio hivyo,…hapana…’akasema
‘Kesi hii msingi wake
mkubwa ni kuhus deni, au madeni ya watu
wanayodaiwa, wewe umeshasema kuwa hayo madeni ni halali kwao, wao hawakubaliani
na hilo…’akaambiwa na hapo akatikisa kichwa, halafu akasema;
‘Sasa mimi
nahusikanaje na hilo, mimi sio banki, …na mimi sasa hivi sio mfanyakazi wa
benki siwezi kuliongelea hilo, …nikiongea hayo ya ofisi za watu,..eeh..,
ninakiuka masharti ya uajiri…natumai hilo lipo wazi.au..sijaeleweka hapo...’akasema
‘Kisheria, hii sasa ni
kesi,..na ni kesi ya madai, ina maana kila jambo la madai, hata kama ni la
kiofisi halina usiri tena hapa, mahakama inaweza kuitisha kumbukumbu zote ili
kuhakiki hilo,…, kinachotakiwa hapa kwa hii kesi, … kwasasa ni wewe kuelezea
uliyowahi kuyafanya ukiwa mfanyakazi wa benki…’akaambiwa
‘Kama yapi…?’ akauliza,
hapo nikageuka kumuangalia wakili wangu ambaye alikuwa akitabasamu.
‘Ndio nilianza hivyo,
mimi nilijua utaelezea yote hayo, ili uwe mkweli kwa mama yako na kwa jamii,……sasa
nakuuliza swali hili, maana umesema wewe sasa hivi haupo benki, je huko benki
ulifukuzwa kazi au uliacha kazi.
‘Niliachishwa kazi…sio
rahisi mtu kuacha kazi, au sio, labda awe na masilahi mengine…’akasema
‘Kwa kosa gani…?’
nikamuuliza
‘Kwa kosa gani,
sijasema nilifukuzwa kazi,…eeh,…mimi sikuwahi kufukuzwa kazi, mimi nilipunguzwa
katika zoezi la upunguzwaji wafanyakazi, japokuwa walikuwa bado wananihitajia,
kilichochangia sana, ni kutokana na hali yangu ya kiafya, na mimi nikakubaliana
na hilo, kiukweli nilikuwa napata shida sana…’akasema.
‘Ni kwa vile
ulishawekeza vya kutosha au sio, maana huwezi kuacha kazi kama huna masilahi , kwa
mujibu wa kauli yako, au sio…’nikasema.
‘Hahaha, acha wivu ndugu
yangu wewe, najua ushapekenyua pekenyua
kila mahali, ukanijua nilivyo na miradi yangu,…hahaha, hiyo ni jasho langu, na …ilibid
nifanye hivyo, …haina shaka,…na kila kitu kipo kihalali, hilo na kuhakikishia…’akasema
kwa kujiamini kabisa
‘Wakati unafanya kazi
benki wewe ulikuwa kitengo gani..?’ akaulizwa
‘Kwanza cha mtandao
baadae nikahamishiwa kitengo cha madeni, twende, maana kuna lengo lako sio …’akasema
akitabasamu lakini akionyesha uso wa kutafakari, …
‘Kwanini ulihamia
kitengo cha madeni…cha mikopo, wakati wewe umesomea na uliajiriwa hapo benki
kama mtaalamu wa mitandao…?’ akaulizwa
‘Waajiri wangu waliona
ninafaa huko, mimi kama nilivyosema awali, akili yangu iliweza kujua mambo
mengi kwa haraka sana,…pamoja na kwamba mimi niliomba kazi benki kwa kupitia taaluma hiyo ya mitandao.., lakini
pia mimi nimesomea mambo ya mahesabu, ..uhasibu, pia masoko eeh, banking..…namshukuru
mungu kwa hilo…na kwa muda huo kitengo hicho kilihitajia mtu wa haraka kutokana
na mikopo kuwa mingi…’akasema.
‘Kuna taarifa kuwa
wewe ulifanya njama mtu aliyekuwepo hapo akafukuzwa, nia ni wewe uweze
kushikilia sehemu hiyo, kweli si kweli…?
‘Sio kweli…’akasema akionyesha kushangaa.
‘Nikimuita huyo mtu
akalithibitisha hilo, utasemaje…?’ akaulizwa
‘Muite,eeh, muite,…nia
si kuthibitisha hilo tu, aje tupambane naye hapa,..’akasema kwa kujiamini, mimi
nikamuangalia hakimu nikaona anatizama saa yake.
‘Kwa vile muda ni
mchache, hili tunaliweka kama bakia, tutakuja kulithibitisha hilo, kama ni
muhimu,..kuwa wewe ulifanya njama fulani fulani hadi jamaa akaonekana hafai, na
mengine zaidi ya hayo…ila kwa hivi sasa swali langu la muhimu..ni hili…’nikamuangalia
moja kwa moja usoni.
‘Wakati upo kitengo
hicho cha mikopo, kuna barua nyingi za watu kulalamika kuhusu mikopo yao, na
wengine walilalamika kuwa ndugu zao waliofariki wamepewa mikopo ambayo sio
sahihi,na zaidi kuna watu walilalamika pesa zinachukuliwa kwenye akaunti zao,
wakati wao hawajafanya hivyo…kweli si kweli…?’ nikamuuliza.
‘Mhh….mimi sijui,…ndio
eeh, yawezekana, ndio, …na hayo ni mambo ya kawaida tu kwenye sehemu za kazi..,
ila mimi nilipokuwa pale, eeh,mmh..…niliwajibu, wathibitishe, kitengo
kiliwajibu, na kumbukumbu zilikuwepo, je baada ya kuwajibu wao walifanya nini,
je kuna ambao walifika mahakamani..?’ akauliza
‘Ndio hawa hapa, baadhi
yao, ndio hawa wamefika mahakamani kudai haki yao…sasa rejea kwenye kumbukumbu
za ofisini kwako, wewe uliwahi kuitwa, kutokana na malalamiko hayo,…na pia
kutokana na madeni ya watu yliyokaa muda bila kulipwa, wewe kama mkuu wa
kitengo ulipendekeza kuwa hayo madeni mengine ya zamani, ya watu waliofariki, yafutwe kwa vile, hayana namna ya kulipika ,
kweli si kweli..?’ akaulizwa.
‘Hahaha, kweli
umefanya kazi….hilo ni kweli…lakini sio yote yaliyokubalika, mengine utawala
ulikataa, na yakaendelea kuwepo, ni mambo ya kawaida au sio…’akasema
‘Je deni hili la
…marehemu, mume wa mama mjane, ambaye ni mmoja wa wanaolalamika, ni miongoni
mwa hayo yaliyokataliwa,…?’ akaulizwa
‘Mhh…hapana,….’akasema
‘Kwanini….?’ Nikauliza
‘Halikuwa la muda
mrefu….’akasema
‘Je wewe kuwepo kwa
deni hilo, kuombwa hadi kutolewa, ulilisimamia wewe huo mchakato…?’ akaulizwa,
hapo akajifanya kama anafikiria, halafu akasema;
‘Kitengo ndicho
kililisimamia…’akasema
‘Wewe si ndio ulikuwa
bosi wa hicho kitengo kwa muda huo, au sio…?’ akaulizwa
‘Ndio nilikuwa, lakini
niliondoka na mambo yaliendelea au sio…’akasema
‘Kwahiyo unakumbuka
hilo deni, kuwa ni wewe ulilipitisha…?’ akaulizwa
‘Naweza nikakumbuka
hivyo, sawa, japokuwa nilisimamia madeni mengi tu,.., mhh, unasema lilikuwa la nani,
eeh, …sina uhakika, …utanisamehe kwa hilo..’akasema
‘Hahaha,…usijifanye hukumbuki
bwana madogo, nafsi inakusuta ,…adui yako mkubwa ambaye ndiye aliyekufanya
uhamie hicho kitendo, umusahau,…nakukumbusha, tu…je umelikumbuka hilo deni,
..?’ nikamuuliza.
‘Unajua usiwe
unazunguka ungelisema mapema tu, ningekujibu..maana huko unapokwenda, napajua
sana, na nilijua lengo lako ni hilo…ni sawa, hilo deni lilitolewa nikiwepo,…na
mimi nilipitisha kwa sahihi yangu, nakubalia hilo na ni…baada ya kuhakiki kuwa
lina vogezo vyote vinavyohitajika…’akasema.
Pale nikasogea
nakuchukua makaratasi,..nikasogea mbele yake…na kumuonyesha.
‘Unazikumbuka hizo
nyaraka…’nikamuonyesha, na hapo akatoa macho kama kuigiza kushangaa,..halafu
akacheka,..
‘Umezipata sio…hahaha,
wewe kweli kiboko, hahaha…’akacheka.
‘Hizi ni stakabadhi halisi
zinayoonyesha deni hilo lilivyotolewa,..je stakabadahi hizi, au payment vocha
hizi unazikumbuka vyema…?’ nikamuuliza
‘Zipo nyingi sana za
namna hiyo….sasa ukiniambia hiyo naikumbuka siwezi kukudanganya, kuwa
naikumbuka na ni kweli, au sio, yawezekana isiwe yenyewe, ila zinafanana…’akasema.
‘Hii ni ushahidi uliotoka
benki, inasadikiwa hivi vyote niliteketea kwa moto,…’nikasema
‘Sio kweli…’akasema
‘Cha ajabu hizi
nyaraka bado zipo hadi leo, ina maana alitokea malaika,akaja kuziokoa, …au
niseme nini, mtu akaja kuziokoa, akazihifadhi…’nikasema.
‘Hahaha…utasema
upendavyo,…wewe ndio utasema ulizipata wapi, …je nikisema si zitambui
utasemaje…?’ akauliza.
‘Najua hutasema hivyo,
wewe sio muongo kiasi hicho..na kwanini useme hivyo, wakati kila kitu kipo
wazi,…au unataka tuhakiki hilo…?’ nikauliza
‘Haina haja uliza
swali lako…’akasema
‘Hizi ni kumbukumbu za
benki, zenyewe hazikuwahi kuungua, na mkakati wa ‘moto’ au sio..unaujua sana
huo mkakati, ulitaka baadae hizi zote
ziteketee, lakini kwa uweze wa mungu, zikabakia hadi hii leo…’nikasema
‘Sawa…’akasema hivyo
tu.
‘Sasa katika kupitia
pitia hizi kumbukumbu,....unaiona hii, ni vocha, ya benki kwenda kwa
mlengwa,..na hapa kuna sahihi yako, wewe uliyethibitisha kuwa mkopo huo
umakamilika, hauna shaka, utolewe…,…’nikasema na akawa anaangalia kama
kuhakiki.
‘Najua unajiuliza hivi
vitu vimepatikanaje, na yule uliyemtuma akamalizie hiyo kazi , kwanini
hakuimalizia, ..mmh, ulichelewa,.kufuatilia hili, au sio….sasa swali langu ni
hili, ,…nauliza, je aliyeomba huu mkopo ni nani…?’ nikauliza
‘Kwani jina
halionekani hapo eeh,…’akasema
‘Nataka uhakika
wako..kauli yako…’nikasema
‘Itakuwa hivyo, ndio
yeye, huyi aliyeandikwa jina lake hapo juu, …’akasema
‘Ndio yeye, aliyekuja kwako , akaomba huo mkopo,
ukapitisha, na yeye akaja kuweka sahihi yake hapa, kuwa kaupokea huo mkopo,
sawa si sawa…?’ nikamuuliza
‘Sikiliza…’akasema
‘Tumeshakusikiliza
sana, sasa tunahitajia ukweli wako…kama kweli nia yako ni kutubu, na kulimaliza
hili jambo, jibu kwa ukweli wako..hii hapa ni kumbukumbu halali ya banki ambayo
ilikuwa inatumika, kipindi hicho, kweli si kweli…?’ akaulizwa
‘Ni kweli…’akasema
‘Sasa hivi kumbukumbu
kama hizo hazitumiki tena, ukiangalia, nembo, ukiangalia maelezo, ya kipindi
kile sio sawa na kipindi hiki..kweli si kweli…?’ akaulizwa hapo akasita kidogo
‘Mhh…sijakuelewa
hapo…’akasema
‘Wewe una akili sana,
hilo sio jambo la kufafanuliwa,…kiri kuwa hapo mlilofanya kosa, mlilisahau hilo…’nikasema na hapo akachukua ile karatasi
na kuiangalia kwa makini
‘Mimi siwezi kujua
hayo, na naweza kuikana hii kumbukumbu pia, naweza, umeitoa wapi,…sijui kuhusu
hilo…’akasema na hakimu akawa anamuangalia kwa uso wa kujiuliza.
‘Wewe si una akili
sana, kwanini usilitambue hilo…mmmh, na pia i wewe ulikuwa mtu wa mitandao,
ulishindwaje kuibadili hii nembo, si wewe awali ulikuwa unaifanya hiyo kazi,
eeh,…ukashindwa kitu kidogo kama hiki, ooh, umeniangusha rafiki yangu..’nikamwambia
, halafu kwa sauti ndogo, nikamwambia.
‘Umeliona kosa lako
eeh..huchomoki hapo…’nikamwambia na kucheka, na akakunja uso,..lakini baadae
akatabasamu, lakini hakusema neno.
‘Wewe ulichukua
karatasi mpya, ukajaza tarehe za nyuma, ukasahau kuwa tarehe za nyuma walikuwa
wakitumia nembo nyingine si ndio hivyo…, na nembo hizo ni za kificho hata kama
ungebadili kwa hapa juu, bado nembo ya kificho ipo, itaonekana, au sio,…kumbuka
mchakato w kubadili nembo…na wewe ulikuwepo kwa masilahi ya benki…’nikamwambia
na jamaa akatabasamu tu.
‘Ndugu yangu, ..kubali
tu kosaaah, hata kama wewe una akili sana lakini ndege mjanja hunaswa kwenye
nini…hahaha..’nikacheka jamaa kimia
‘Kabla hujakiri, na
..kama muungwana, ukajisalimisha, kuna jambo jingine, la kukusaidia ili uone
kuwa sasa, mchezo wako kwishinie, unatakiwa ukiri kosa, na utubu dhambi zako,
na mama yako huko alipo afurahi…’nikamwambia, halafu nikageuka kumuangalia
hakimu.
‘Ndugu muheshimiwa
hakimu, hili ilikuwa shida kulitambua
hili, ikizingatiwa hapa tunazungumzia benki ambao wana taratibu nyeti, kuna
maswala ya sahihi , kuna dole gumba vyote hivyo vinamgusa mlengwa,..utawezaje
kufanya jambo kubwa kama hilo kwa mtu mwingine eeh…’nikasema
‘Ni kweli….kila mjanja
ana mbinu zake, lakini tunasahau kuwa yupo mwenye uwezo kuliko sisi, ambaye
ndiye muumba wetu, yeye, hachoki kuwasaidia waja wake,..kwa uwezo wake tukaja
kugundua ujanja huo, lakini sio sisi, ni
kwa uwezi wa mwenyezimungu…’nikasema. Na kumgeukia huo shahidi.
‘Shahidi…umeziona hizi
kumbukumbu hapa, mtu akichukua pesa anaweka sahihi yake hapa, si ndio hivyo, na
sahihi ni kitu nyeti sana, kweli si kweli ,..awali,..labda mimi sijui, dole gumba mlilitumia kwa mtu ambaye hawezi
kuweka sahihi yake, au sio…?’ nikamuuliza, hapo akacheka kwa dharau kidogo,
halafu akasema;
‘Sio kweli…kwa mkopo
mkubwa ni lazima aweke sahihi, na mtu yoyote akichukua mkopo, au kufungua
akaunti, dole gumba ni muhimu, sasa sijui hiyo hoja wewe umeitoa benki gani…’akasema
‘Sawa sawa kabisa…sasa
angalia..hii kumbukumbu hapa, inaonyesha sahihi, si ndio hivyo, na hapa ni
sehemu ya dole gumba , sawa…kwanza nikuulize..hii sahihi ni ya nani…?’
nikamuuliza, akaiangalia, halafu akasema ;
‘Ni ya
marehemu…’akasema na baadae akashtuka
‘Hebu…’akasema na mimi
nikamuangalia wakili ambaye alicheka kwa nguvu.
‘Umeshachelewa mdogo
wangu, ujanja mwingi unafanya nini…hahaha…’nikasema
‘Nimechelewa nini
hapo…’akasema
‘Umesema hii sahihi ni
ya nani…?’ nikamuuliza
‘Nahisi ni ya
marehemu…’akasema
‘Sasa UNAHISI, awali,
ulisemaje tena kwa kujiamini,… kwa hivi sasa kwa vile umegundua kosa lako,
unasema unahisi… ulishachelewa bwana mdogo, tulichotaka tumekipata kwa hoja
hii, au unasemaje…?’ nikamuuliza
‘Kwani hizi kumbukumbu
hapa juu zimeandikwa jina la nani,…kwa vile hizo kumbukumbu, ni za mwenye jina
hapa juu, kwahiyo moja kwa moja, sahihi itakuwa ni yake,..ndio maana nikajibu
kwa haraka hivyo..’akasema
‘Sio kwa vile sahihi
hii uliikariri, na uliweza kuirudia bila kukosea angalia hapa pembeni, hii
sahihi ni kama mtu alikuwa akiijaribu hapa… tatizo ulijaribia hapa hapa kwenye hii
karatasi…ungejaribia kwenye karatasi nyingine bwana…’nikasema na hapo akashtuka
na kusema
‘Sio kweli, hata kama
naifahamu hiyo sahihi…, naweza kuiweka kama hivyo, na naweza kuangalia sahihi
yako, kama haina ugumu, nikaiweka kama ilivyo,…lakini sio mimi niliyeweka
sahihi hiyo,..na sina mtindo huo, wa kuweka sahihi za watu… hizo ni shutuma
zako na sikubaliani na hiyo shutuma…’akasema
‘Nilikuuliza swali
awali..je ni kweli aliyeomba huo mkopo, nikiwa na maana marehemu, ndiye
aliyekuja kujaza hii fomu, na akaja kuweka sahihi yake yeye mwenyewe, kuwa anachukua
hilo deni, ulisita kujibu hilo swali, je sasa waweza kulijibu hilo swali…’nikaona
kama anataka kuongea lakini akaghairi
‘Maana haya yote kujaza
fomu ya mikopo, kuja kuweka sahihi kuwa mkopo umekubaliwa na pesa hiyo inawekwa
kwenye akaunti ya huyo mteja, yote yalikuwa yakifanyika ndani ya kitengo chako, mbele ya
usimamizi wako, unalikumbuka hilo..na kulikuwa na kamera juu…usisahau hilo
kamera huwezi kuzitia moto….’nikamwambia hapo akashtuka
‘Hahaah, kulikuwa
hakuna kamera kipindi hicho hpo kitengoni…’akasema
‘Una uhakika gani…kwa
vile wewe ndio ulikuwa IT au sio, ulihakikisha hilo halipo au… au….hahaha,
ilikuwepo lakini wewe ulikuwa hujui hilo…’nikasema na hapo akaonyesha uso wa
kushangaa, halafu akasema
‘Sio kweli….’akasema
hivyo
‘Na kipindi kile mlihakikisha
anayechukua mkopo anaingia kabisa kwenye ofisi yenu na kuweka sahihi, ili
umuone kuwa ni nani……je ni kweli marehemu alifika mbele yako, akaweka sahihi
yake…?’ nikamuuliza
Jamaa akabakia kimia
‘Ndugu yangu, kubali tu
yaishe…’nikasema
Jamaa
akatabasamu,…halafu akaanza kucheka…ghafla akanyamaza, …halafui akaniangalia akiwa
kanitolea macho….macho..ya kutisha, huku anahema, .. akasema;
‘Naona unahisi
umeshinda, si ndio hivyo....lakini bado hujashinda,…..’akahema kwa nguvu,
halafu akawageukia watu, akasema
‘Mimi sijafanya kosa…..,
nitasema hivyo hadi kesho, hata kama mahakama hii ikiamua vinginevyo….’halafu
akanigeukia, na kuanza kuongea…
‘Ukweli…si unataka
ukweli….’akasema
NB: Sehemu hii
inaendelea
WAZO LA LEO: Ukweli haujifichi, ukweli haupingiki, hata kama wanafiki
wataugeuzageuza, lakini ukweli kama ulivyo mwanga, utaonekana hata kama kuna
giza nene..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment