‘Kiukweli
inabidi nielezee, ila nakuomba sana mke wangu uniongoze, najua wewe unaweza
kuniuliza maswali ya kuniongoza….’nikamwambia mke wangu, na yeye akabakia
kimia.
‘Wewe
ongea bwana, wewe si mwanaume,….’akasema mke wake kwa hasira.
‘Sawa,
nitaelezea tu, ila hamuwezi kuamini, inaniuma sana ikizingatiwa kuwa mimi
nilishawishika kijinga na kuyafanya hayo yote, lakini kama ungelinifunua moyo
wangu ukauona ulivyo ungeniamini haya ninayowaambia, hii ni familia yangu, na
nilitaka kufanya hivyo nikijua…’akawa anataka kuongea zaidi, lakini mke wake,
akamkatiza kwa kusema
‘Wewe
ongea hayo ya muhimu, hayo ya kujidai kuwa unaijali fanulia yako yataonekana
kwenye maelezo yako…’ akaambiwa
‘Inabidi
nijitetee kwa hili kuwa nilifanya hadi hapo, licha ya kuwa nilishaona kuna madhara,
ila kwa hatua niliofikia hadi hapo sikuweza kuacha, kwa masharti hayo, kuwa
nikiacha kuendelea kuyafanya kama yalivyotakiwa ili yawezekane, basi kafara
lake ni mmoja wa ninaowapenda afe…awawe kama kafara la hiyo mizimu.
‘Sawa
hapo tumekuelewa na imani zenu za kishirikina,…..endelea ….’akasema mke wake
naona alishakubalia kumuongoza kwa maswali.
‘Basi,
baada ya tendo lile la kuhamisha nguvu za uwezo wangu kama mume wa familia, …na
kuhamishiwa kwa kijana wangu,…,ikawa mimi kazi yangu ni kuwa msindikizaji tu,
ila kila anachofanya kijana nilitakiwa niwepo, na niwe nimemshika mkono,
inakuwa nguvu zetu zipo pamoja,….hayo yanafanyika mimi sijijui..na hata kijana wetu
hajijui..’akasema
‘Kwahiyo
kila mkienda kwenye hizo shughuli za usiku, ilikuwa ni lazima kijana wako,
apitie kwa mama yake afanye yale uliyotakiwa wewe uyafanye kwa mama yake..?’
akaulizwa sasa na mama Ntilie.
‘Nahisi
ndio hivyo, ili dawa hizo zifanye kazi, …’akasema
‘Kwahiyo
unahisi huna uhakika….hakuwahi kukuambia kuwa ndivyo ilivyokuwa inafanyika...?’
akaulizwa na mke wake.
‘Aliniambia,
ndio kawaida ….kila safari ikifanyika huniambia kilichofanyika, ila mimi
nilimuomba hayo ya kijana wangu asiwe ananiambia, lakini akasisitiza kuwa ni
lazima nijue kila kinachotendela kabla ya kutenda na baada ya kutenda ndivyo
masharti yalivyo hivyo, ….’akasema.
‘Kwahiyo
hiyo safari ya kijana wako kuchukua nafasi yako na kufany akila ulichokuwa
ukikifanya wewe kama mume wa familia, ni zaidi ya mara moja…’akaulizwa.
‘Ndio..mimi
siwezi kuwa na uhakika ilikuwa mara ngapi, lakini ni zaidi ya mara moja, na
baadae huyo mtu akasema tayari nguvu zimeshahamia kwa kijana na nyota
imeshaanza kuonyesha uhai, iliyobakia ni matendo mengine sasa ya kuihamisha
kutoka kwa kijana kuja kwangu, lakini hiyo si lazima kwa sasa, ilimradi nyota
sasa ipo ndani ya familia yetu….’akasema.
‘Kwahiyo
utajiri ulianza kuonekana ..au?’ akulizwa
‘Kijana
alianza kubadilika, ..ghafla akanunua gari la kifahari tu… nakumbuka
tuliulizana na mke wangu kijana kapatia wapi pesa kiasi hicho cha kuweza
kununua gari la gharama hivyo, mimi akilini najua ni kitu gani, mke wangu akawa
hajui, kwahiyo yeye akataka tumuulize kijana, na mimi nikamwambia ni juhudi za
kijana wetu tusipende kumuingilia maisha yake…’akatulia akisubiria kuulizwa
maswali.
‘Ehe,
endelea sio lazima nikuulize maswali wewe si unaendelea kuelezea tu…..’akasema
mke wake.
‘Kijana
akaanza kubadilika, akawa hata nyumbani haonekani mara kwa mara , kitu ambacho
sio kawaida yake, ukimpigia simu anakuambia, nipo kwenye mishe mishe zangu,
ninalala hotelini, na anaongezea kwa kusema, sasa atanunua nyumba yake ili
tusiwe tunamuulizia ulizia, kuwa yupo wapi…’
‘Kununua
nyumba au kupanga nyumba?’ akaulizwa
‘Yeye
alisema anataka kununua nyumba ..tukamuuliza pesa kapatia wapi, yeye alisema
kwenye dili zake za hapa na pale, ikabidi mama yake amuwekee watu wakufuatilia
nyendo zake, na akagundua kuwa pamoja na mengine kijana, alikuwa akicheza
kamari, na alikuwa akipata pesa nyingi sana, na ndio hizo anazichezea
hivyo…mimi nilijua ni hiyo nyota sasa inafanya kazi,…lakini sikuwa na raha na
hali iliyokuwa ikiendelea maana sio mimi naonekana mwenye utajiri, na mimi
nilitaka nionekane mimi ni tajiri kwa ajili ya kumuonyesha baba mkwe.
Mama
yake hakuwa na raha na mabadiliko hayo ya kijana wake, akashangaa kuniona mimi
namtetea, sitaki kumfuatilia, …na akataka tumuite huyo kijana kwenye kikao, na
kijana alipokuja akawa anatujibu kijeuri, kuwa kama ni pesa anazitafuta kwa
akili zake, kwahiyo tusimfuate fuate…ilikuwa kwa mara ya kwanza kijana wetu anatujibu hivyo, hakuwa na
tabia hiyo kabisa,…’akatulia.
‘Unaona
kijana wako alivyobadilika, wewe unakaa kimia tu…sasa mke wangu akaanza
kuniandama mimi, mimi sikupenda kubishana na mke wangu maana nilijua ni nini
kinachoendelea..
Na
mara nyingine namjibu, hivi;
‘Atatulia
tu, nina imani akioa, mambo yatakuwa safi…ndio maana nafurahi akiwaleta mabinti
ili niweze kuwachunguza ni nani anafaa…’nikamwambia mke wangu.
Katika
mambo yake aliyokuwa akifanya, zaidi ilikuwa ulevi, kubadilishana mabinti, na
siku nyingine anakuja na mabinti wa watu zaidi ya watano, kustarehe nao, kwangu
nilijua ni kwasababu gani, na ni mimi nilimshauri afanye hivyo awali, na nilimuambi ahakikishe
anachagua wazuri…hakujua usiku hao mabinti wanachukuliwa kufanyiwa mambo na hao
wachawi…
‘Basi
ikawa sasa ni kero hata mimi nikawa sina raha, maana mama yake alikuwa haachi
kunisemesha kuhusu mtoto, na hata ndugu zake achilia mbali wazazi wake,…nikaona
sasa ni bora nitafuta njia ya kulituliza hili, nikawasaliana na huyo mtaalamu,
ndio akaniambia japokuwa yupo kwenye matatizo na huyo mpinzani wake, lakini
yeye anatarajia kuja huku hivi karibuni, na akija huku atahakikisha analimaliza
hilo tatizo…
Kweli
haikupita muda, akafika huku Dar, tukaongea naye, akaniambia ni nini cha
kufanya…na hapo nikazidi kuingia matatani…lakini sikuwa na jinsi…’akasema
‘Uliambiwa
ufanye nini…?’ akaulizwa
‘Ili
tulimalize hilo, inabidi turejeshe hizo nguvu alizo nazo kijana kwangu mimi,
kwani hizi sasa inawezekana kufanya hivyo, awali ilikuwa haiwezekani, ilitakiwa
muda fulani upite…na muda huo ulishapita…’akasema.
‘Ina
maana ukizirejesha hizo nguvu kwangu, hali yangu itakuwa kama awali, na kijana
atakuwaje..?’ nikamuuliza
‘Ndio,
hali yako itakuwa bora, kama kijana wako… ila kijana wako yeye, anaweza akawa
kama wewe…’akaniambia hivyo..na kunifanya nishtuke.
‘Kwa
vipi…awe kama mimi?’ nikamuuliza.
‘Ujue
hizo nguvu utakazozipata sio zile za kwako za asili, hizo ni nguvu za
kupandikizwa, lakini zinafanya kazi kama kawaida,, ….’akaniambia
‘Ina
maana mimi sitaweza kuwa na nguvu zangu za asaili…?’ nikamuuliza
‘Hilo
hatujui, maana mizimu ndio inayokumiliki, na hatuwezi kuilazimisha,…kwahiyo kwa
hivi sasa tunatakiwa kufanya yale wanayotaka wao kwanza, …ila ukiona umechoka
na hizo nguvu, kwa kipindi fulani mtakwua mkibadilishana na kijana wako,
ukitaka lakini…’akasema.
‘Lakini
yeye bado kijana anazihitajia sana kuliko mimi…’nikamwambia
‘Sasa
ni wewe mwenyewe kuchagua, kama unataka kijana wako aendelee kuwa hivyo, na
hatari yake ni kama mnavyoona, yeye ni kjana hajui kujizuia, hana busara,
atawaletea keshi humu ndani, bora umnyamazishe kwa hivyo kwanza, na baadae
akirejeshewa atajirudi…’akanishauri hivyo.
Basi
nikaongea na mama yake nikamwambia kuna dawa natakiwa nimfanyia kijana ili
atulie, aachane na mambo hayo.
‘Dawa,
kwanini dawa, kwani huwezi kumshauri tu hivi hivi akatulia…?’ akaniuliza.
‘Tumemuita
mara ngapi, mke wangu….na tumemkanya mara ngapi…, umeona majibu yake, sasa
uamue mwenyewe , tumueche hivyo hivyo au tumtafutie hizo dawa, maana ni wewe
unanisumbua kuhusu yeye…’nikasema na mke wangu akasema;
‘Hizo
dawa unazitafutia wapi…?’ akaniuliza kwa mashaka.
‘Wewe
niruhusu tu, nitazipata, kuna mtu kaniambia zipo dawa za kumdhibiti mtu wa
namna hiyo, vinginevyo atazidi kuharibika na hata kuchanganyikiwa, wewe huoni
imekuwa ni tatizo sasa…uso wetu tutauweka wapi….au wewe unasemaje mke wangu…’nikamwambia
mke wangu nikiwa kama muungwa anayetaka kushirikiana mambo na mke wake, lakini
hakujua kuwa mimi ni ndumila kuwili…’akasema akitabasamu ile ya kuumia.
‘Basi
sawa ilimradi zisiwe za kishirikina..’mke wangu akasema hivyo
Mimi
nikawasiliana na huyo mtaalamu, na kuwa muda huo bado yupo hapa Dar, akiwa na
shughuli zake, akaniambia tujiandae usiku, atakuja na watu wake….
‘Na
ujue zoezi lilivyo, ni kama lile la siku ile,…sasa sijui mke wako kajiandaaje,
lakini tumeshamjulia madhaifu yake hawezi kutushinda,..ila kuna kazi ya ziada,
kuna mambo yatakiwa kufanyika kuzimuni…’akaniambia hivyo.
‘Kuzimu
ndio wapi..?’ nikamuuliza
‘Makaburini,
na huko wewe unatakiwa kuona, utachukuliwa hujijui, ila ukifika huko
utarejeshewa fahamu zako, na utaona
yatakayofanyika, ila kijana wako atanyamazishwa…kama ilivyo kawaida
yake….’nikaambiwa
‘Kwani
ni lazima niyaone hayo mambo yenu ya kichawi…?’ nikamuuliza
‘Ndio
kwasababu hayo ni dhidi yako na kijana wako, …inakuwa ni wewe unamfanyia kijana
wako..’nikaambiwa
‘Na
mama yake je…?’ nikauliza
‘Kawaida
njiayetu nikupitia kwa mama yake, atafanya yote kama kawaida, na tukishamaliza
mambo ya huko kuzumuni ukirudi wewe ndio utashika usukani, na ukitoka kwa mkeo,
ni lazima kuwe na mabinti kama kawaida, hao mabinti ni wa kuwafurahisha vijana
wangu,…unanielewa…’nikaambiwa.
‘Na itakuwaje kwa mtoto wangu baada ya hapo…?’
nikauliza
‘Itakuwaje
kwa vipi, si unataka mtoto wako atulie, atatulia kama awali…’akasema
‘Sawa…’mimi
nikakubalia, nikijua kwua kijana wangu atakuwa kama zamani, sikujua kuwa kuna
jambo linguine litamtokea….’akasema.
‘Basi
usiku hiyo ikafanyika hivyo, nakumbuka kijana sijui ilikuwaje, wakati tupo huko
makaburini, ghafla akazindukana na kuanza kukimbia, …na ikawa kazi ya
kumtafuta, …lakini alipatikana na kazi ikafanyika kama kawaida…’akasema…
‘Asubuhi yake ikawaje…?’ akaulizwa
‘Kijana
akawa mgonjwa hatoki kitandani, hatoki nje yeye na ndani tu, …sasa ikawa kuhangaika
mimi na mama yake, maana inabid nifanye hivyo, ili mama yake asijuei
kinachoendelea,…kijana akawa habadiliki, mpaka mama yake akaanza kukata tamaa..
‘Hivi
kijana wangu kawaje tena…?’ akaniuliza
‘Mimi
sijui labda ni hizo dawa ndio zimemfanya hivyo…’nikasema
‘Dawa
gani ulimpa mtoto wangu…?’ akaniuliza kwa ukali
‘Ni
dawa za kumzuia mtu mlevi, aache pombe, na huyo mganga alisema, hali hiyo
itatokea lakini itakwisha taratibu taratibu, kwahiyo tusubiria tu mke
wangu…’nikasema.
‘Na
kama umemfanyia mtoto wangu mambo ya kishirikina hatutaelewana, sizani kama
nitaweza kukusamehe kwa hilo, maana wewe mtu sasa sikuelewi elewi…’akaniambia
hivyo, na ninachoshukuru ni kuwa mke wangu alikuwa haamini mambo hayo zaidi ya
kuhimiza tumpeleke mtoto wetu hospitalini, lakini mimi nikawa nazuia kinamna.
‘Kwanini
hukutaka apelekwe hospitalini…?’ nikaulizwa
‘Haikutakiwa
kupelekwa hospitalini, vinginevyo angeliharibika kabisa….ndivyo nilivyoambiwa
na huyo mtaalamu…’akasema
‘Basi
sina hili na lile siku moja nilikuwa nimetoka maana kuna mambo mengine
ilibiaidi nisafiri kama alivyotaka huyo mtaalamu, nikawa nimesafiri kufuatilia
vifaa fulani, niliporudi, mke wangu akasema alimpeleka kijana hospitalini.
‘Eti
nini…kwanini umefanya hivyo, si nilikuambia dawa hizo alizopewa, hazitakiwi
kuchanganya na madawa ya hospitalini, sasa utakuwa umemuharibu mtoto..’nikasena
nikiwa nahaha sasa…
Na
kiukweli, hali ya kijana sasa ikazidi kuwa mbaya zaidi ya hapo, akawa kama
kachanganyikiwa kila mara anapiga makelele, wakati mwingine anakimbia na
kupotea, tunamtafuta anarudi, akawa sasa ni mtu wa kufunga kamba ndani…anatoa
ulimi nje kama mbwa anavyofanya, mtoto akawa sio mtoto bali ni kama dalili za
mnyama anavyokuwa…’hapo akatulia.
‘Je hamkuwasiliana
na huyo mtaalamu wako ili muone jinsi gani ya kumsaidia…?’ akaulizwa.
‘Tulifanya
hivyo yeye,alisema hiyo hali itakwenda na itakuja kutulia baadae, ila sisi
tumeharibu kwa kumpeleka mtoto huyo hospitalini,…
Basi
muda ukafika akatulia, na wakati huo yale matendo ya kuhamisha zile nguvu
kutoka kwake, zikawa zimafanyika na mimi nikawa na nguvu …nguvu za ajabu, ikawa
ni shida sasa, yale aliyokuwa akiyafanya kijana yakahamia kwangu, japokuwa mimi
nilikuwa nikiyafanya ki utu uzima zaidi.
‘Ukawa
unacheza kamari..?’ akaulizwa
‘Ndio,
unajua pesa za kishetani hupatikana kwenye njia za kishetani pia, kwenye kamari
ndio ilikuwa sehemu ya kukusanya mali, na kila ukicheza hukosi, na hiyo hali ya
kupata pesa inakuvutia kucheza zaidi na zaidi, na huko ulevi, umalaya ndio
sterehe yenyewe,…na kiukweli kwa mapesa hayo, ni lazima ufanye mambo ya
kujionyesha, ndio nikaanza kujenga
majumba, unakumbuka mke wangu alilalamika kuwa nina nyumba mahali,..ndio hizo
pesa, lakini utajiri wake haudumu, unajenga nyumba nzuri ikiisha unauza, au unahonga kwa wanawake…ni utajiri
wa shida tu, na muda huo hujitambui, akili inakuwa na kumuhe muhe cha kufanya
machafu, starehe, ‘akasema
‘Kwahiyo
hata wewe ulikuwa ukiwachukua mabinti wadogo…?’ akaulizwa
‘Ndio..maana
ndio makafara ya hao watu wa mtaalamu, ni lazima hayo yafanyike kila
akiwahitajia, na mimi usiku kama wamekuja ni lazima nishirikie, kuwepo,,
…’akasema.
‘Kwahiyo
kumbe ndio wewe ulimpa ujauzito huyo mdada aliyetoa mimba…?’ akaulizwa
‘Hapana,
sio mimi, pamoja na mengine pamoja na hata kumtamani huyo binti, kufanya hivyo,
sikuweza kwasababu ukumbuke huyo binti ni msichana aliyekuwa akitakiwa na huyo
mtaalamu, ni mtu wake, ila alitaka kumfundisha adabu, na akatumia watu wake
wengine kumzalilisha…’akasema.
‘Wakina
nani hao…?’ akaulizwa
‘Mimi
siwajui, ila anasema ana vijana wake, ana watu wake ambao hutembea naye usiku
na hao ndio wanatumiwa kushiriki na hao mabinti wakichukua makafara yao…’akasema.
‘Kwahiyo
tuseme kuwa kwa upande wako hao mabinti wa usiku ulikuwa huhusikani nao, hao ni
kwa ajili ya hao wachawi ….?’ Akaulizwa
‘Ndio….’akasema
‘Je si
hayo mambo ya kutuma mabinti na kuhamisha nyota yalishakamilika kwanini sasa
muendelee kuwazalilisha watoto wa watu usiku ..?’ akaulizwa.
‘Hayo
mambo ya muda wake kila mara kuna namna ya kuyaweka yawe yanafanya kazi, kwa
hiyo mara kwa mara wao walikuwa wakija, na kunichukua ili kuwezesha nguvu
ziendelee kuwemo, kwahiyo vitendo hivyo vilikuwepo lakini sio kama awali, ni
mara moja labda kwa mwezi, au mara mbili hivi…’akasema.
‘Wewe hayo
yakitokea ni lazima ujue..?’ akaulizwa
‘Wakitaka
kuja wananiarifu kuwa watakuja, ..kama wanakuja kwa kushitukizia ujue wamekuja
kwa mambo yao mengine..ambayo mimi sihusiki…’akasema
‘Kijana
wako ikawaje..?’ akaulizwa
‘Kijana
japokuwa alikuwa kapona kinamna…, lakini hakuwa na nguvu zake, …na hali hiyo
ikaanza kumtesa kimawazo, si unajua tena…ikabidi hata aniambia mimi kuwa na
hali fulani inamkera…akaniambia ukweli alivyo, na ikabidi sasa nimshauri twende
hospitalini.
‘Si
uliambiw usiende huko hospitalini…?’ akaulizwa
‘Hio
ilikuwa ni awali, kwasasa haikuwa na shida, mimi najua ni kwanini, ila kwa
kumuaminisha kijana ikabidi nimshauri hivyo,..twende akapimwe,..na kupimwa ndio
ikagundulikana ana magonjwa kama yangu, kisukari ..na shinikizo la damu..yaani
yale yale niliyokuwa naumwa mimi ndio sasa anaumwa mtoto wangu, nikajua ni hizo
nguvu ndio zimesababisha hayo…
‘Oh,
kwahiyo wewe ukawa radhi na hali hiyo ya kijana wako ateseke wewe, uwe kijogoo..au
sio…?’ akaulizwa
‘Kiukweli,
kwa muda huo sikujali kabisa, niliona ni sawa tu, atulie nyumbani, ilimradi
nafahamu ni kwanini, na utajiri ukipatikana itakuwa kwa manufaa ya familia, sio
kama ilivyokuwa yeye, utajiri ulikuwa kwa ajili yake tu, na hakutaka
kuulizwa…’akasema.
.
‘Kwahiyo
kumbe ni kweli, kuwa ukifanya hayo mambo unapata utajiri, japokuwa ni wa
kichawi..?’ akaulizwa
‘Ukweli
ndio huo kuwa unapata utajiri, lakin kwa kupitia njia za kishetani..unafanya
mambo mabaya sana..mengine siwezi hata kusimulia, na mbaya zaidi huwezi kufaidi
huo utajiri maana unaumiza wengine, unaumiza hata familia yako, na wakati wote
huna amani, kila muda una mawazo kuwa huenda nikajulikana huenda watu wananiona
huenda…halafu shughuli unazozofanya kwa jamii, ni za kukuzaraulisha tu japokuwa
mwenyewe unajifanya hujali…’akasema
‘ Sasa
ikawaje kwa kijana wako….?’ Akaulizwa.
.
‘Nilianza
kukaa naye kumshauri, na nilimuahidi kuwa kila anachotaka nitampa, lakini
hakuwa na raha kabisa,..unajua tena hali ya kibindamu ilivyo, ulikuwa hivi,
mwanume sasa unajiona tofauti, huna kazi, alizoea kubadili mabinti sasa
akiwaleta anaishia kuabika tu…, na taarifa zikawa zinazagaa kuwa kijana hana
nguvu tena..ikawa ni aibu na ikawa inamtesa sana kisaikolojia…’akasema
‘Mungu
wangu ikawaje sasa…?’ akaulizwa
‘Ndio hapo
akaanza kutumia pombe zaidi kupitiliza,…, na hakutosheka na hilo, akaanza kutumia
madawa ya kulevya
‘Mungu
wangu, kwanini, na wewe ulijua hilo…?’ akaulizwa
‘Mimi
nilijua, ila mama yake alikuwa hajui kuwa kijana wake kaanza kutumia madawa ya
kulevya, nikawa namtetea na kuificha hiyo hali, na nikawa najaribu kumshauri
kijana wangu aachane na madawa kwani ni mabaya zaidi…
‘Sasa
kwanini uifiche wakati unajua kijana anaharibika kwasababu yako…?’ akaulizwa
‘Mtaalamu
aliniambia nisimzuie kwa yale anayoyafanya , maana yatakuja kuisha kwa muda
muafaka,… ni mambo ya muda tu, lakini hayo hayakuwa kweli..nikaona kama huyu
mtu hamtakii mema kijana wangu…’akasema
‘Kwanini
sio kweli..?’ akaulizwa
‘Kwasababu
kipindi kile kijana wangu akiwa kijogoo, yule binti wa awali alishafika, huyu
mtaalamu kume aligundua kuwa kijana wangu kampenda huyo binti, na akagundua
kuwa wana mahusiano ya siri…’akasema
‘Kwa
vipi sasa kijana nguvu zake ulishazichukua..au ilikuwa bado…hapo unatuchanganya?’akaambiwa
‘ Huyo
binti alikuja muda, ..na muda aliofika niikuwa bado zitazichukua, hizo nguvu kutoka
kwa kijana,..na nilikuja kugundua baadae kuwa kumbe huyo mtaalamu alifanya
hivyo kumuadhibu kijana wangu, pamoja na mengine …’akasema.
‘Ikawaje
sasa,….je huyo mtaalamu hakutaka kumsamehe huyo kijana wako…?’ akaulizwa
Ghafla ndio huyo mtaalamu akaanza kuzidiwa zaidi,…tatizo
lake likazidi kuwa kubwa zaidi, awali sikujua ni tatizo gani, hadi alipofika
kuniambia kuwa kagundulika ana ugonjwa mbaya, ila anahisi kuwa mbaya wake ndiye
kamfanyia hivyo.
‘Lakini
wewe si ulikuwa na pesa kwanini sasa alikimbilia kuomba kwa akina mama, au
kipndi hicho alichokuja kuomba pesa ilikuwa bado,…?’ akaulizwa
‘Kipindi
hicho, ilikuwa bado, kipindi anakuja kuomba pesa, ni kipindi hali imebadilika
hata kwangu….’akasema
‘Ehee,
endelea…..’akaambiwa
‘Kukawa
kunakuja taarifa kuwa kwa wakwe zangu hali yao ni mbaya, kiuchumi,
‘Kwahiyo kumbe kweli nyota iliondoka kule kwao
na kuja huko kwenu au sio…?’ akaulizwa
‘Hapo
mimi sijui, ila kiukweli, wazazi wa mke wangu walikuwa na hali mbaya, na mimi
nikitaka kuwasaidia lakini wao walikataa kabisa, waliniambi wazi wazi kuwa wao hawataki
pesa za kishetani….
‘Oh,
ina maana wao walishajua kuwa pesa zako ni za kishetani…?’ akaulizwa
‘Wao
waliniambia hivyo, na sikuwa na muda wa kuwafuatilia kwa nini wanasema hivyo,
ila walikuja kumuita mke wangu wakamkanya kunihusu mimi, na kipindi hicho ndio
mke wangu akaanza kunifuatilia kwa karibu, …’akatulia.
‘Haya
sasa tuambie kuhusu yaliyotokea kwa hao mabinti wawili….maana naona umefikia
kipindi chao, ilikuwaje maana mama alisema kuna mambo mabaya mliwafanyia
wao..?’ Akaulizwa
‘Kama nilivyosema binti wa mwanzo
nisingeliweza kumgusa, japokuwa nilifanya juhudi hizo mara kwa mara, na wakati
mwingine naamua kwenda kwake usiku,lakini kila nilipojaribu nilijikuta
nikikutana na huyo mtaalamu.
‘Unakutana
naye kwa vipi, yeye si anakuja humuoni,…?’ akaulizwa
‘Simuoni
ila ananifanyia mambo yanayo-onyesha kuwa yupo….’akasema
‘Sasa
yeye anajuaje kuwa wewe unakuja kwa huyo binti…?’ akaulizwa
.
‘Sijui
anajuaje, sio kila siku, ila siku ambazo, navutika kwenda kwa huyo binti, ndio
siku nakutana naye, na yeye, ananiuliza nimefuta nini kwa mke wake…na hata
kesho yake lazima atanipigia simu kuniuliza na kunikanya, kuwa nisipoacha hiyo
tabia atanifanya kitu kibaya sana….’akasema.
‘Mke
wake!!!..kwanini anamuita mke wake…?’ akaulizwa
‘Yeye
anadai alishamuoa kimzimu, kwahiyo ni mke wake kihivyo…’akasema.
‘Kwahiyo
yawezekana mimba iliyotolewa ya huyo binti ni ya huyo mzee..au sio…?’ akaulizwa.
‘Hapo
mimi sijui….maana siku ilipotolewa, huyo mjamaa alikasirika sana kuwa huyo
binti kamfanyia kitu kibaya, na zaidi kajiunga na adui yake kummaliza yeye, na
kwahiyo anafanya kila njia kuhakikisha huyo binti anamrejea yeye.
‘Oh,
sasa ikawaje…?’ akaulizwa
‘Muda
huo ndio vita ikapamba moto, kati ya hao watu wawli....mimi muda huo sina hili
wala lile kumbe wajamaa wanapambana usiku na mchana, na ndio ikaja huyo binti
mpya…huyu hapa…’akasema
‘Je
hayo ya kumleta huyu binti mpya ilitokea kwa amri ya huyo mjamaa, kuwa huyo
binti aondoke hapo, mlete mwingine au ni wewe na mke wako mlipanga hivyo…?’
akaulizwa
‘Ni
amri ya huyo jamaa aliniambia hapo nyumbani kwangu mambo yanaanza kuwa mabaya,
tumeingiliwa, kwahiyo tutafuta makao mapya ya kufanyia shughuli zetu, na huyo
binti aliyepo humo aondolewe, tutafuta binti mwingine, na ndipo nikamshauri mke
wangu atafute binti mwingine, na alipokwenda huko kijijini ndio akaja na huyo
binti …’akasema.
‘Shughuli
gani hizo zilihitajika kufanyika kwingine..?’akaulizwa
‘Si
nimekuambia, hayo mambo yalihitajia kuyaongezea nguvu ili yaweze kufanyaa kazi,
yana-expire, kwahiyo yanahitajia kuwa activiwa…labda niseme hivyo kwa
kiingereza…’akasema.
‘Kwahiyo
mkafanyaje…?’ akaulizwa
‘Huyo
binti akaondoka pale, na kuhamia huko kwa rafiki wa mke wangu, na huko ndio hao
wachawi wakaweka makao mapya,..lakini haikuwa rahisi kihivyo, …’akasema
‘Kwanini…?’
akaulizwa.
‘Huyo
binti alishajiunga na huyo adui wa jamaa, akawa kapata namna ya kujilinda, na
huko kwenye hiyo nyumba alipokwenda wenyeji wake ni wacha mungu, hawaingiliki
ovyo…ndio akaja na hoja ile ya kuondoa makafara…nia yake ni kuweza kuweka mambo
yake…lakini kama mlivyoona haikuwa kazi rahisi, na yeye hali yake kiafya
ikazidi kuwa mbaya, akawa sasa analemewa na adui yake…’akasema
‘Kwahiyo
na wewe ikawaje…?’ akulizwa
‘Sasa
kwa vile hayo mambo hayafanyiki tena, madawa na zile nguvu za kishetani zikawa
zinaisha nguvu, mimi nikawa naanza kuishiwa nguvu, mambo yakaanza kuwa mabaya,
madeni,..kamari, ukicheza hushindi, unaishia kukopa, kulipa siwezi, nikaishia
kunyang’anywa nyumba, magari…hali ikaanza kuwa mbaya sasa …’akasema
Na
siku moja kijana wangu akanitaka tuongee, kipindi hicho naanza kuchanganyikiwa,
jamaa mtaalamu hapatikani na akipatikana analalamika hali mbaya anahitajia pesa
za matibabu, hana pesa, nimsaidie au nitaishia kubaya, na leo kijana wangu
ananiita, sikutaka kabisa kuongea naye…
‘Mliongea
naye, ..alikuambia nini…?’ akaulizwa
‘Baba
nimegundua kuwa matatizo haya niliyo nayo sababu kubwa ni wewe, umenifanyia
hivi ili nifirisike ili nisiwe tajiri, umenipa madawa ya kuniharibia nguvu
zangu za kiume,… ili nisiwe natembea na wasichana warembo umenionea wivu na kunifanya..hivi
sasa nakupa wiki moja tu, unirejeshee hali yangu la sivyo , nitamuambia mama
haya yanayoendelea humu ndani….’akaniambia hivyo na kuondoka.
‘Sasa
ilikuwaje….?’ Aakulizwa
‘Nikawasaliana
na mtaalamu, na mtaalamu akasema dawa ipo hapo hapo nyumbani, …huyo binti mpya
ndiye kafara, kwani ana sifa zote…nisiwe na wasiwsi atayamaliza hayo, ila mimi
hali yangu itawa vigumu kuirejeshwa kwani mambo yameharibika, na kijana ili
afanyiwe hivyo, kuna mambo makubwa yanatakiwa kufanyika, nitafute mbwa..…’akasema
mzee sasa akiona aibu kuniangalia mimi machoni.
‘Mbwa
wa nini…?’ akaulizwa
NB:
Mbwa wa nini….tutakuja kusikia sehemu ijayo..
WAZO LA LEO: Utajiri wa kishetani hata kama
utaupata lakini ukumbuke mwisho wake ni mbaya sana,..wengi waliofanya hivyo,
wameishia kubaya sana, na kama itatokea ukafariki kabla hujatubu , kifo cha mtu
kama huyo kinakuwa kibaya sana, wengine wanafikia kuoza wakiwa wazima, na mambo
mengi mabaya hutokea kwa watu hawa hata kabla ya kukata roho, jamani tumuogope
mola wetu, kwani hayo tunayoyataka ya utajiri ni vitu tu vya kupita, na mwisho
wake tutarejea kwa yule aliyetuumba, je unajuaje kuwa utaupata huo utajiri na
kuendelea kuutumia, hukumbuki kuwa siku ya kufa ni siri ya mola pekee…tutubie
na tuache…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment