Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, May 8, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-24


Docta akaingia kwenye boda boda, moja kwa moja hadi kwa Mzee.

Alipofika kwa mzee,
 akauliza

‘Msaidizi wangu yupo wapi..?’ 

'Hatujui…’wakasema mke na mume wake

‘Hamjui… kwa vipi,! Kwani ilikuwaje, akaondoka,.. aliondokaje , ina maana aliondoka bila ya kuaga, au ilikuwaje,…?’ 

Tuendelee na kisa chetu...

******************

Docta aliwauliza wana ndoa hao wakionekana kutokuivaana, nahisi ni kutokana na kuchukuliwa kwa binti yao.

Docta hakujali hali ya wanandoa hao, wazee hao, yeye akakimbilia kumuulizia msaidizi wake,.. na aliuliza maswali mengi ya mfululizo,  na wakati huo mama mwenye nyumba yeye alishakimbilia chumbani kwake..

Baba mwenye nyumba akawa anaonyesha uso wa mshango, akiwa haelewi kitu kuhusiana na msaidizi wa docta huyo, na hakuwa na mawazo kabisa ya kuwa huenda kuna tatizo kwa huyo mtu..yeye ndio akasema;

‘Sisi tulikuwa tumetoka na mke wangu kama ulivyo niagiza kwenye simu, baadae nikarudi ndani, nikamkuta msaidizi wako kashika mfuko, mifuko hii iliyoandikwa Rambo, na ndani nahisi  kulikuwa na  kitu kizito, kwa jinsi alivyokuwa ameushika, maana ni mfuko mkubwa, lakini kwa muda ule sikuwa na mawazo ya kumdadisi…’akasema

‘Oh….’docta akasema

‘Yeye alisema anatoka kidogo, atarudi muda si mfupi, …mimi muda huo nimeshazozana na mke wangu hatulewani, kichwa hakipo sawa, lakini mimi nikajua anataka kutoka nje ili awasiliana na wewe labda…,na hataki kuongea humu eeh,… kama ulivyosema, ina maana hamkuwasiliana naye?…’akasema na kuuliza huyo mzee.

‘Mhh..hapana..sijaongea naye, maana nimekuwa nikimpigia nikawa simpati, nikahisi kuwa kuna tatizo,…hisia zilikuwa zinaniashiria kuwa kuna tatizo, unajua mzee  sijui ..ndio hivyo, wanasema nina hulka au kipaji cha hivyo,..’akasema.

‘Kwahiyo unahisi ..huenda kuna tatizo..?’ akauliza mzee akiwa sasa na yeye na wasiwasi, akasimama, huku akiangalia nje.

‘Huyu mtu atakuwa kaingia kwenye mitego ya hawa watu,…’akasema docta

‘Kwa vipi docta, maana ..alitoka hakuwa na wasiwasi, alionyesha tu yupo safi..sizani, ni hisia zako tu docta, …’akasema mzee

‘Hao watu wana kila aina ya mbinu…kwa vile hawajui binti yenu yupo wapi, na huenda binti ….anyway, …muhimu tumpate huyo mtu…’akasema

‘Ina maana binti yangu atakuwa ana…jambo na hao watu….?’ Akauliza mzee.

‘Hapana…sizani, ngoja kwanza tumpate huyu mtu, muhimu ..tujue ni kitu gani wametega,…’akasema docta.

‘Oh, sasa naanza kuingiwa na wasiwasi…binti yangu ….nataka niongee naye, nijua kama ana jambo na hao watu…’akasema mzee.

‘Mzee huko usifike..nilikuambia nini kwenye simu,..kuwa makini,…’akasema docta

‘Sasa tukamtafute wapi huyo msaidizi wako…?’ akauliza
‘Hilo niachie mimi, wewe kaaa na mke wako, hakikisha anatulia…’akasema docta
‘Ok…basi unifahamishe kinachoendelea hata kwa ujumbe..simu yangu inazima zima, si unajua  tena..aaah, hali zenyewe ngumu hata simu nashindwa kununua, tumekuwa kwenye matatizo, matatizo…’akasema mzee.

‘Sasa mzee,nashindwa hata nianzie wapi, ..hivi  ni nani hapo nje ambaye anaweza kuona watu wakitoka humu ndani kwako wa kuaminika, nijaribu kumuuliza..?’ akauliza kwa sauti ya chini

Mzee akasogea mlango, wakawa wanatoka nje na docta, huku akimuambia hivi;

‘Hapo nje kuna fundi mmoja wa viatu kama hajaondoka, huyo na mwamini sana, muda kama huu, ..nahisi bado atakuwepo,…unaweza kumuuliza yeye..lakini kwani unahisi kapatwa na jambo baya ..?’ akauliza mzee

‘Muhumu kuonana naye kwanza….’akasema docta.

‘Haya nenda nisikucheleweshe,…utanifahamisha kinachoendelea…’akasema huyo mzee,  na docta kwa haraka  akatembea kutoka nje ya geti,  na kukutana na huyo fundi wa viatu, alikuwa anafunga funga kuondoka.

‘Eti fundi kuna jamaa yangu tunakuja naye hapa kwa mzee mara kwa mara, kwa leo ulimuona akitoka hapo mlangoni kwenye geti, na ni  muda gani ulimuona akitoka..?’ akamuuliza huyo fundi maswali kwa mfulululizo.

‘Aaah,.. yule jamaa mnayeongozana naye..nilimuona akitoka na mfuko wa Rambo, hii mikubwa, ni muda kidogo,…alitoka kwa haraka akaelekea upande huo… nahisi alikuwa na kitu labda..anataka kukitupa, maana huko alipoelekea mara nyingi watu wamepafanya kama ni dampo…’akasema na docta akaangalia upande ule akaona kuna miti miti tu…na mataka taka

Docta hakuhitaji kuuliza zaidi, kwa haraka akaelekea upande huo aliolekezwa, hakugeuka nyuma, na sasa alikuwa akifuatilia hisiza zake, hisia zake humsaidia sana,…kwa kipindi kama hiki, au kipindi cha hatari…

 Akatembea huku akiomba mungu , alijua kwa vyovyote vile msaidizi wake atakuwa kaingia kwenye mtego fulani, asingeliweza kuondoka hivyo kimia kimia, halafu ni kwanini aelekee maeneo hayo, na alibeba nini, akawa anawaza huku anatembea kwa haraka haraka, huku hisia zake zikinusa kama mbwa...

‘Kama angelikuwa na nia ya kuondoka asingelikuja upande huu, huku alifuata nini…’docta akawa anajiongelesha mwenyewe, pamoja na hisia hizo lakini pia laikuwa akitafuta dhamira, iliyomfanya mtu wake afanye hivyo.

‘Kutakuwa na jambo, hebu niwaze zaidi,..alipigiwa simu, kuwa achukue mzigo huku, na nani lakini au aliambiwa apelike huo mzigo, kwa mtu fulani, au ….’akasema akiwa sasa kafika kwenye gogo la kukalia, hapo akasita, akahisi kuna jambo hapo.

Akasimama na kugeuza kichwa huku na kule,…upande mwingine kulikuwa na taka taka zimelundikana, kuna harufu mbaya ya matakataka yaliooza, na alipotizama chini ya lile gogo , akaona karatasi, akaikumbuka  kuiona hiyo karatasi, lakini yaweza ikawa ni nyingine maana ilikuwa ni kipeperushi cha matangazo, akaiokota.

‘Kama ni yenyewe, nitaona ile sehemu alioandika namba ya simu, kwani siku ile alipokichuku ahicho kipeperushi, alikutana na jamaa yake mmoja, katika kuongea wakapeana namba ya simu, na akakiangalia hiyo namba kwenye hicho kipeperushi, maana jamaa yake huyo alikuwa na haraka,..’  ni kweli kilikuwa ndicho hicho akaiona hiyo namba,…

‘Ok,… kwahiyo atakuwa alifika eneo hili, ….sasa, ilikuwaje,..kwanini hii karatasi ilidondoka hapa, je kimakosa au …ni alama,…’akasema.

Akawa anaendelea kukagua huku na kule, na mara tena akaona waya…akavutika na huo waya, akaufuta, …kwanza alitaka kuuokota, lakini akasita, baadae alipojirizisha kuwa ni waya tu, akainama na kuuokota, ulikuwa umezama ndani ya majani.., akauvuta kwa tahadhari,…

‘Huu waya ni wa laptop, tena bado mpya, haiwezekani kuwa ulitupwa,  mhh…ngoja…’akaingiwa na wazo, kwa haraka akachukua simu yake na kumpigia  mzee.

‘Eti mzee, ulisema kuwa msaidizi wangu wakati anatoka alikuwa kabeba mfuko wa Rambo, na huwezi kukisia kuwa alibeba kitu gani, sio kwamba alibeba laptop..?’ akauliza, na mzee akasema hana uhakika

‘Binti yako ana laptop…?’ akauliza docta mzee akasema ndio

‘Basi hebu ingia chumbani kwake ukague kama hiyo laptop ipo …’akasema docta, huku aikisubiria,..hakukata simu, akawa bado anaendelea kuchunguza kwa macho, huku na kule, baadae mzee akawa hewani akasema hiyo laptop haipo ndani.

‘Ina tumia waya wa namna gani…?’ akauliza na mzee akasema hiyo laptop, waya wake wa betrii uliharibika na yeye alikwenda kumnunulia binti yake waya mwingine mpya na una karatasi imeandikwa,..jina la hiyo laptop, lakini pia  yeye aliandika kwa peni jina la huyo binti kwa herufi tatu za jina la binti yake...

‘Ndio yenyewe..’akasema docta, na mzee akamuuliza ndio yenyewe nini kaiona hiyo laptop au kaona nini, au kamuona msaidizi wake, akiwa …lakini docta hakumpa nafasi ya kuuliza zaidi, yeye akasema;

‘Ngoja nitakuambia nikihakiki, sijamuona huyo msaidizi wangu , lakini nahisi alifika maeneo haya, nitakupigia,…’akasema docta na kukata simu, sasa akiwa kavutika na jambo jingine jipya, hilo likampa jakamoyo na kuhusi mwili ukimsisimuka zaidi,iliashiria hatari

Docta alihisi sasa mwili ukimsisimuka, hii ni dalili nyingine hasa anapokaribia hatari..akawa sasa anakagua hicho alichoona, kwa macho, na huku akiinua mguu kwa tahadhari, huku anaendelea kuangalia ....

**********

Macho yake yaliona alama za mburuzo wa kitu kizito, mburuzo huo uliacha alama,  na yeye akaufuatilia kwa macho…na huku anatembea kwa tahadhari, maana inaweza ni chatu kapita,..au kitu kama gunia nzito lilikuwa linaburuzwa. …au mtu ..’hakutaa wazo hilo liingie akilini.

Sasa akawa anatembea kufuatilia alama hizo, akazifuatilia hadi akafika kwenye mtaro wa maji machafu, alama hizo zikaishia hapo, akajaribu kuona kama kuna gunia limetelekezwa au kitu cha namna hiyo, alichunguza aneo lote hakuona,…

‘Isije ikawa ni chatu…’akasema sasa akiangalia huu ya miti, kwa uwoga, lakini hisia za uwoga hazikuwepo zaidi ya hisia kuwa kuna kitu kingine zaidi ya hicho.

‘Lazima kama ni gunia, au …ningeona  hicho kitu, na kwanini huo mburuto ukaishia hapa, au umezamishwa kwenye huu mtaro…’akasema sasa akichungulia kwenye huo mtaro…

Ulikuwa ni mtaro mrefu kidogo wa kupitisha maji,…, na uzuri wake haukuwa na maji, ila una mataka taka..ya kuoza..

 Akagundua kuwa kwenye sehemu ya mbele kuna majaniyamelazwa, na mengine yamekauka, kuonyesha kuwa kuna kitu kimezamishwa hapo, hapo akajua huenda ndio hicho kitu kimetupwa hapo, lakini kwa jinsi majani yalivyowekwa ni kama kimefichwa..

Akasogelea pale na kuinama na kuanza kupachunguza, kwa tahadhari, kwanza akaanza kuyaondoa yale majani ya juu,akayasogeza pembeni, inavoonekana huyo mtu aliuweka huo mzigo kama kuuficha ili jae kuchukua baadae, sasa ni mzigo gani..

Docta akavutika kuugundua, japokuwa ilikuwa kupoteza muda, ..aliondoa yale majani mpaka kukatikana uwazi wa kuangalia ndani. Akahakikisha kuwa kuna usalama sio chatu au kitu cha hatari,…akaona ili agundue vyema hicho kitu ni bora aingie ndani ya huo mtaro… akatumbukia ndani ya mtaro..kulikuwa kuchafu..lakini ikabidi tu.

Alipofika ndani ya huo mtaro, akagundua, kitu ni kama furushi, lililofunikwa na shuka jeupe…kwanini lifunikwe na shuka jeupe, akasogea na kwa tahadhari akawa anavuta ile shuke…oh,…, ni mtu…

‘Ni mwili wa mtu…’ docta akahisi mwili ukimuisha nguvu, akavuta ile shuka jeupe kama sanda na kuhakikisha huo mwili umebakiwa wazi,…shati lilikuwa limelowa damu,….

‘Hizi…huyu..sio…ooh…’aligundua nguo alizokuwa amevaa msaidizi wake,…lakini kwa jinsi mwili ulivyosokomezwa hata kichwa kilikunjwa kama mtu anasujudu..hukioni vyema

Sasa akaanza kazi ya kuusukuma ule mwili mpaka ukafikia sehemu ya kuunyooka kwa kulala, ..haikuwa kazi rahisi alihitajia msaada, lakini kwa usalama zaidi akaona ahangaike pele yake.

 ‘Oh,..mungu  wangu…msaidizi wangu, ..ooh wamekuua..haiwezekani…’akasema sasa hata mwili ukimuishia nguvu..maana kwa hali aliyoiona sio ya kuona mtu, kwanza damu nyingi zimevuja kutoka kichwani.

‘Oh, mungu wangu, saidia mja wako…ni msaidizi wangu, alikuwa  katika kuwasaidia waja wako, sio kwa uwezo wetu,  yote haya ni kwa uwezo wako na rehema zako..,..’akasema

Alijua hataki kupoteza muda, akaanza  kazi ya kumtoa huyo msaidizi wake  kwenye hilo eneo, ilichukua muda mpaka kumtoa, halafu akaanza kumfanyia huduma ya kwanza, lakini ilionekana jamaa yake huyo hana uhai..

 ‘Hapana haiwezekani…mungu wangu saidia mja wako..’akasema sasa akikata tamaa, na hapo akaona haja jinsi, akachukua simu yake na kumpigia jamaa mmoja wa bajaji anayemfahamu,..na uzuri wake jamaa huyo akasema hayupo mbali,a nakuja hapomuda sio mfupi.

Wakati anamsubiria mwenye bajaji akawa sasa anajaribu kutafuta chochote cha kumsaidia kama ushahidi, na alipokuwa kifanya hivyo akaona peni, sio peni za bei rahisi, ni peni maalumu mtu anatengenezewa, inakuwa na nembo ya kampuni au..jina lako…ilikuwa ndani ya huo mtaro, kashuka tena na akaichunguza ile nembo, lakini hakuweza kugundua kuwa ni kampuni gani…akaifadhi tu

Na mara mwenye bajaji akafika, na wakasaidiana kumweka kwenye bajaji.

‘Mzee hii ni maiti, tunaipeleka wapi…’akasema mwenye bajaji

‘Nani kakuambia ni maiti..’akasema docta

‘Hapa huwezi kuuliza huyo keshakufa,..usije kuniingiza kwenye kesi, maisha yenyewe haya nianze kukimbizana mahakamani, au polisi, hapana mzee..’mwenye bajaji akaanza kuogopa

‘Sikiliza mimi ni docta, huyu ni mgonjwa wangu wewe tufike hospitali na usihie zako, ni nani atakuuliza…’akasema docta na baadae jamaa akakubali na wakaelekea hosiptalini.

Walifika kwa docta, na docta , japokuwa ni rafiki yake lakini akaanza kuweka pingamizi ;

‘Unajua huyu mtu kapigwa, kaumizwa, na ..na kafariki huyu…’akamkagua na kumpima, docta,…huyu hayupo hai…’akasema mwenzake kwa mashaka

‘Una uhakika kafariki…? Akauliza docta sasa na yeye akiwa  na mashaka, maana japokuwa yeye ni docta lakini kwa rafiki yake, ilikuwa hawezi hata kuhitimisha kuwa msaidizi wake kafa au la…Docta mwenzake sasa akaamua kutumia vipimo vya ziada kabla hajatoa jibu.

NB: Haya ilikuwaje..

WAZO LA LEO: Majanga, misiba, mitihani ya maisha inapotokea kwenye jamii, wengi wanaweza kukimbilia kwenye shiriki na kusema hapa sio bure kuna mkono wa mtu, tunasahau kuwa kuna mungu..Mola muweza wa yoye ambaye anaweza kutenda atakavyo, na mitihani ya maisha inatukia ili iwe kama onyo, au kama kumbusho kwetu.., kuwa sisi hatupo hapa duniani moja kwa moja, naya kuwa pamoja na kuhangaika kwetu katika kutafuta maisha bora, tunahitajika pi kumkumbuka kutenda mema na kukatazana mabaya. Na ikitufikia misiba tukumbuke kusema kwake tumetoka na kwake ndio marejeo yetu


Tuzidini kumuomba mola wetu atusaidie kutuongoza kwenye njia iliyonyooka, na kwa msiba uliotukuta, kwa kuwapoteza watoto wetu, na mingine iliyotokea baadae.,. tu poleni sana wazazi, kwani sisi sote ni wazazi wa watoto hao, na ndugu wa marehemu waliotangulia mbele ya haki, hii ni misiba yetu sote, na tunamuomba, mola awahifadhi watoto wetu hao, na ndugu zetu hao walifariki kwenye ajali hizoo na kuwahifadhi  mahali pema peponi…Amin
Ni mimi: emu-three

No comments :