‘Mimi sipendagi kusimulia maisha yangu maana kila nikianza kusimulia
ninaishia kulia tu, najikumbusha machungu mengi yaliyonisibu, maisha yangu
yamekuwa ni kidonda kisichopona ambacho kila siku kinatoneshwa na watu…..’akasema
huyu bint
Kisa kilianzia pale nilipomkuta binti mmoja akiuza mihogo, na mgongoni kabeba mtoto mdogo, na mtoto huyo akawa analia sana,..hali ya yule mtoto akiwa kabebwa mgongoni ilisikitisha, nguo alizovyaa, ...na hali ilikuwa nayo, na hali ya hewaa ilikuwa ni ya ubaridi..nikashikwa na huruma , nikamsogelea huyo binti, kujua zaidi, nia hasa ilikuwa kumshauri amuonee huruma huyo mtoto..lakini majibu niliyokutana nayo, yalinifanya niingiwe na hamasa zaidi ya kumfahamu huyo binti..
Wakati nikiwa kwenye hamasa hiyo mara linazuka jingine kubwa.....
Hiki ni kisa cha binti yatima, hebu tuenddee nacho...
*************** 2***********
‘Sasa utasaidiwaje, maana shida ni kila mtu anazo, na hakuna
anayewez
a kusema mimi nimejitosheleza, nahitaji mtu wa kumsaidia, kila mtu hata
tajiri anaona maisha kwa ke ni magumu, hajatosheka…sasa ili watu waweze
kuvitika na matatizo yako ni wewe mwenye shida ujieleze…’nikasama na yeye akawa
kainamisha kichwa chini akilia.
‘Haya…, ndio maisha yetu yalivyo, …, huruma haipo karibu
kwenye nafsi zetu, ni mpaka ifukuliwe…unaonaeeh,. Na mwenye kukuhurumia zaidi
ni yule aliyewahi kupatwa na shida, na shida zipo kwetu sisi watu wa chini,….sasa,…
ukiongea watu wakakusikia wakaona shida zako wenye huruma za karibu wanaweza
kukusaidia…au sio, masikini tunasaidia wenyewe kwa wenyewe…’nikasema.
‘Hakuna mwenye huruma dunia hii…nimeteseka sana, watu
wananiona hivi hivi,….wanajua kabisa mimi sina baba wala mama, mimi ni yatima, au
yatima anatakiwa aweje,….mimi ni yatima aliyepitiliza, sina baba wala mama,
wala mjomba aau shaangazi, dunia imenitekeleza….’akasema
‘Katika maisha kama hayo ukiwa mdogo wa mwaka, ..utakuwaje,…ufe,
au…..sasa aliyejitolea kunisaidia ndio huyo amefariki,….wangapi waliniona na zaidi
ya msaada wao ulikuwa ni masimango na kunyanyapaliwa na hata kuzaliliswa…Namshukuru
sana bibi yangu, bila yeye, labda ningelishakufa zamani… oh, na ndio huyo ameshafariki,
na hata bila ya watu kumuelewa…binadamu, jamani binadam..’akasema
‘Mhh…pole sana…’
‘Na sasa ndio huyo amefariki bibi yangu masikini, nitakuwa
mgeni wa nani…sina ndugu sina jamaa…na na.., kinachoniuma ni kuwa amefariki
hata sijapata muda wa kulipa fadhila zake, alinilea nikiwa mdogo kwa shida….,
akanitibu nikiumwa,..akiwa hana mbele wala nyuma,.. akataabika kwa ajili yangu,
na…za zaidi nikamuongezea ugumu wa
maisha kwasababu ya tamaa zangu za kimwili….mungu wangu kwanini,
kwanini…..’akawa analia.
‘Pole sana, yote maisha….’nikisema
‘Yote maisha ehe..mnasema tu….’akainua uso uliojaa chuki.
‘Maisha…hahaha, maisha…, mengine yanauma….yanauma ukizingatiwa kuwa
mengi ya madhila hayo waliosababisha ni wanadamu wenzetu…na ni ndugu kabisa,
unajua ndugu...damu moja kabisa, tena wanaume, ….’akaninyoshea kidole, huku
akisema
‘Wanaume kama wewe…., eti wanajita wanaume, hahaha, kama ni
wanaume kweli ni kwanini wasihangaike kivyao, kwanini kama ni wanaume mbona
wanadhulumu,..nawachukia sana wanaume... unajua kuchukia,…masikini bibi yangu…’akawa
analia.
‘Kwani bibi yako kafariki lini…?’ nikamuuliza baada ya
kupita kitambo kidogo.
‘Ndio nimepewa taarifa leo nikiwa nahangaika kuuza
mihogo…lakini sijui kama kazikwa au la..maana hakuna mawasiliano huko kijijini,na
huenda wamemtelekeza kwenye kibanda chake, baada ya kumfukuza kwenye nyumba
yake ya urithi……na ndugu niliotegemea waniambie nini kinachoendelea ndio hao
hao aaah, bibi yangu masikini….’akawa
analia.
‘Pole sana….’nikasema
‘Oh…bibi yangu masikini, hivi mzee kama yule kawakosea nini
jamani, nyie walimwengu mna nini jamani, bibi, kizee, hakina nguvu kabisa,
masikini , hohe hahe…wana..wana…ole wao, nasema ole wao..…nilijua tu... nilijua
mwisho wa siku watamuua tu…’akasema
‘Ina maana wamemuua…?’ nikauliza
‘Kifo chake kitakuwa kimesababishwa na vipigo na mfadhaiko
alioupata…sijui kwanini watu hawana huruma, hivi kama wana miguvu kwanini
wasiende kupigana wakapata pesa, eti…yaani wanakwenda kumpiga kizee wa watu,…ni
kwanini lakini…’akasema.
‘Kipigo…!, mfadhaiko..!…hebu anza hatua kwa hatua, kwanini
bibi yako alipata kipigo..?’ nikamuuliza.
‘Eti wanasema bibi ni mchawi..’akasema na watu waliokuwa
wasikiliza wakaguna,
‘Ndio wanavyosema na hilo lilimuumiza sana bibi…hakujua hata
ajitetee vipi,akawa analia tu, akimuomba mungu amsaidia, hakuwa na jamaa
wakumsaidia, ikabakia kila siku akilia, akimuomba mungu siku ifike aondoke hapa
duniani, kuliko kupata adha hiyo…lakini aliomba kwanza anilee nifikie hatia
fulani…..’akatulia
***********
‘Mchawi,…..?’ watu wakaguna na kuuliza
‘Lakini wazee wengine vigagula….,. Yawezekana bibi yako
kweli alikuwa mchawi kweli….’watu wakazidi kuongea..
‘Ndio zenu hizo,…..mna uhakika gani na hilo…kama na nyie sio
wachawi…wanafiki wakubwa nyie…hakuna aliyemfahamu bibi, hakuna..zaidi ya uzushi
huo….’akasema akiwaangalia watu kwa hasira na hapo kukazuka zogo, kila mtu
akiongea lake
Kulizuka mabishano ya watu kila mmoja akisema lake, wengine
walifikia kusema huenda kweli huyo bibi alikuwa ni mchawi, lakini huyo binti hakujua
tu, au hata huyo bintu anajua lakini anamtetea tu bibi yake…..wengine wakasema
ni imani haba tu….yaani kila mtu akawa anasema lake, …nilitaka hayo mabishano
yaishe ili niweze kumsikiliza huyo binti…kwani atakeyeweza kuelezea ukweli wote
ni huyo binti!
‘Hebu nikuulize kwanini walisema bibi yako ni mchawi ,
alikuwaje mpaka wakamuhisi hivyo, maana wewe ulikuwa unaishi naye au sio,
kwahiyo unamfahamu alivyokuwa, unajua lolote kuhusu bibi yako…?’ nikauliza.
‘Hata sijui hayo ya bibi mchawi yalianzaje,…’akasema.
‘Ukituelezea maisha ya bibi yako, itakuwa rahisi kwetu
kuyafahamu hayo….’nikasema
‘Mimi bibi yangu ndiye aliyenilea, baada ya wazazi wangu
kufariki,..hata siwajui wazazi wangu wanafananaje,…maana hata picha hakuna,…wazazi
wangu walifariki nikiwa mdogo sana, bibi anasema nilikuwa na mwaka mmoja tu,
unaona…sasa kama angelikuwa ni mchawi angenichukua mimi, angenilea mimi,…’akaanza
kuelezea.
‘Si ili urithi uchawi wake…’akaropoka mtu mmoja.
‘Hujui unachokisema, kwasababu humfahamu bibi yangu…’akasema
‘Wazazi wako walikufa wote wawili kwa pamoja?’ nikauliza,
nikitaka kudodosa ili kujua ukweli halisi wa binti huyo, kuliko kuchukulia juu,
juu tu..
‘Alianza kufariki baba…..nilivyoambiwa na bibi, ..baba aliumwa
sana, lakini chanzo cha ugonjwa wake ni kuwa alikuwa hajatulia, mlevi,
mnzizi….ndio maana nasema siwapendi wanaume…kwasababu kutokana na tabia yake
hiyo ya ulevi na umalaya, ndio alimuambukiza mama yangu, mama alikuwa mpole
sana mcha mungu, lakini kutokana na baba, aah, nyie wanaume….’akasema akitikisa
kichwa.
‘Oh…unasema baba yako ndiye alimuambukiza mama yako, una
uhakika gani na hilo…?’akauliza jamaa mmoja.
‘Ndio nina uhakika..japokuwa sikuwepo, sikuwahi kuyaona
maisha ya baba kwa macho yangu, lakini mengi niliyasikia kuhusu maisha yake, na
sio mtu mmoja tu, wengi,….na hata waliowahi kutembea naye wamathibitisha hayo…wengi
ni marehemu, waliopo hai walielezea kwenye…haya mambo ya ukimwi na matumaini…’akasema
‘Kwahiyo maisha ya baba yako unayafahamu kwa kupitia
mazungumzo ya watu au sio…., je unaweza kutusimulia kidogo jinsi ulivyosikia
kwa watu…, kwa faida ya watu wengine ili wajifunze, ..kama hutojali lakini…’nikasema
‘Siogopi kuyasimulia, …maana maisha yake yamekuwa ni funzo
pale kijijini, kila mmoja amekuwa akitolea mfano kwake, hasa mzazi anapomuona
mtoto wake anapotea, anakuwa mlevi, Malaya..ana uchu wa madaraka, hamtunzi
mkewe….watu wamekuwa wakitoa mifano kwa kupitia maisha ya baba..kwahiyo hata nisipoongea
mimi leo…, yameshaongelewa sana…mungu amsamehe tu baba yangu…’akasema
‘Kwani baba yako alikuwaje, maisha yake yalikuwaje
ulivyosikia kwa watu...?’ nikamuuliza
NB: Haya haya…huyu baba mtu alikuwaje, kwani alikuwa
kiongozi, mzazi…na mwenye uwezo kifedha, je hayo yalikuwaje mtihani kwake, na
kwa jamii…, ni sehemu muhimu yenye mafunzo itafuata baadaye
WAZO LA LEO:
Wazazi tunatakiwa tuwe kiyoo cha familia zetu, matendo yetu, tabia zetu huwa
zinaaksi maisha ya watoto wetu, kwahiyo tuweni makini sana. Sisi wazazi ndio
chanzo cha misingi mema ya watoto wetu,..huwezi ukamfunza mtoto adabu wakati
wewe mwenyewe ni mtomvu wa nidhamu, unapigana na mkeo, mnazozana mbele ya
watoto…hutunzi vyema familia yako..haya na mengine mengi huathiri sana maisha
ya baadaye ya mtoto wetu. Na kama unatenda madhambi kwa watoto wa wenzako ujue
na wewe madhambi hayo yatahamia kwa watoto wako. Uone jinsi gani mzazi ulivyo
na dhamana kwa familia yako.
Tumuombe mungu tuwe wazazi wema, tutimize wajibu wetu, hata
kama maisha ni magumu lakini hivyo hivyo tu, kwa matendo yetu mema, tabia njema…
tunaweza kuwafanya watoto wetu wakawa nguzo imara ya vizazi vyetu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment