Simini kuwa ni mwaka
mwingine unaingia,….namshukuru sana mwenyezimungu, nawashkuru sana marafiki na
wadau wenzangu…
Siku nilipoamua kuandika mambo ya diary yangu(shajara yangu)
kwenye mtandao ili kila mtu ayasome, nilihofia sana, maana sikuwa na uhakika na
mitandao…. Nakumbuka nilivyopenda kuweka kumbukumbu zangu kwenye
shajara(diary), kila tukio nalihifadhi katika mtindo wa kisa. Ndoto yangu
ilikuwa kutunga vitabu, kuwa mwandishi wa tamithilya, ..oh, sijui lini
itatimia.
Kiukweli mpaka sasa kuna mambo mengi mazuri yenye kufundisha kufurahisha lakini bado sijaweza kuyaandika yote...kawaida yangu nataka niandike kitu chenye uhalisia, sio kufikirika tu,..lakini pia kiwe na hekima, ili kizazi chochote kiweze kusoma. Nia yangu ni kuelimisha, kuonya na kusaidiana. Inaniuma sana nikiona, mayatima, wajane, masikini wakinyanyaswa...
Huu ni mwaka mwingine sijakata tamaa, ninachofurahi ni kuwa
wapo ambao wanaiona kazi yangu kuwa inasaidia jamii….nawashukuru sana. Ni kazi
ngumu kwa vile wakati mwingine unakuwa huna pesa ya kununulia vocha, lkn nimejitahidi
kadri ya uwezo wangu, kuwakilisha kile nilichoona kinafaa.
Siku ya leo ninachoweza kuwaambia ni kuwa wale wote ambao
hawajafika ndani ya diary yangu, (
http://miram3.blogspot.com/)
wajitahidi kufika humo kuna visa vingi sana…kuna matukio mengi ambay
yanasubiria kuandikwa kama story. Matukio hayo ni ya kweli, ila mimi ninachofanya
ni kuyaongezea ladha yawe story, tatizo ndio hilo..gharama na muda…
Ama katika kulifanya hili kuna wengine hawafurahishwi, labda
walitaka niandike vile na vile, wasisite kunishauri, maana diary yangu kwa
kiasi kikubwa mwandishi na mtunzi ni mimi mwenyewe, sijawashirikisha wtu wengine
bado, ila wapo walionihadithia habari za
maisha yao nikajaribu kuyaweka kinamna ya visa..nawashukuru sana, siwezi
kuwataja maana hawakutaka wajulikane!
Basi kwa wale ambao hawaja-LIKE diary yangu facebook,
nawaombeni mfanye hivyo, kama hujafanya hivyo, itanibidi nianze kuwafuta ili
niweze kuwaongeza wengine waliopo tayari kulike. Kulike kunasaidia wewe na mimi
tuwe pamoja, uone kila kitu ninachokiandika, pia inanipa moyo na mimi.
Ahsanteni na mungu awazidishie Baraka, wale wote tuliokuwa nao pamoja na wote waliojitokeza kunipa moyo, kukomment, kulike...sina cha kuwalipa ila mola ndiye atawalipa...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment