Kwanini nyie mumenifanyia hivi, lini mlisikia
mtoto anamnyanyulia mzazi mkono wake,
haijawahi kutokea, mimi na umri wangu huu, kama ikitokea kuzozana mzazi na
mwanae , mtoto akawa mkaidi, akamkosea mzazi wake, wazee wenzangu mnafahamu
nini kinafanyika,...eti wazee
wenzangu,....?’ akauliza na wazee wakakaa kimia
‘Huu
si mkosi jamani, ..... halafu eti mimi ndio nikae na huyo muhuni meza moja
tuongee. Eti mimi mzazi ndio,
nijishushe, haitatokea hilo kwangu kamwe....’akasema mshitkiwa akitikisa
kichwa
Wale
wazee nao wakawa wanatikisa kichwa na mmoja akataka kuongea lakini wakili
mtetezi akawamuwahi na kusema;
‘Kwa
hali ilivyo, na kesi ilivyo inabidi , kwani sisi ndio tunaomba....kama
nilivyosema awali, wenye kuomba inabidi wao wanyenyekee, na ni muhimu mzee ukajua kuwa hili
halitaingilia mila na desturi zenu, baada ya kukamilika hili, basi mtafaya
taratibu zenu, au sio wakili mtetezi, au sio Profesa..’akasema msaidizi wa
wakili na kumuangalia wakili mtetezi ambaye alikubali kwa kichwa, halafu
akamuangalia profesa na Profesa akageuka kumuangalia kaka yake...
Mshitakiwa
akiwa anatikisa kichwa kama kukataa akasema;
‘Na
mbaya zaidi, mdogo wangu mwenyewe ananiendea kinyume, anafanya mambo anavyotaka
yeye mwenyewe, ...kilichompata huko Ulaya keshasahau, hajui kuwa yote haya yalitokea
kwa vile alidharau mila na desturi zetu za malezi, na dini zinasisitiza sana
hayo, malezi bora kwa vijana wetu, na mtoto hata siku moja hawezi kuwa juu ya
mzazi....’akatulia
‘Ni
sawa kabisa....’akasema wakili
‘Mdogo
wangu kwa vile kaishi na wazugu, basi anajifanya kalisahau hilo, na kutokana na
kikiuka hayo, amejikuta kwenye mitihani na mateso mengi, hadi katimuliwa huko,
wakijua keshakufa....mimi nashangaa, kuwa bado tena anarudia makosa yale yale,...hivi
unataka yakupate yapi ndio ukiri kuwa umekosea....’akasema akimuangalia ndugu
yake
Wote
wakageuka kumuangalia Profesa ambaye
alionekana kutaka kumzuia kaka yake asiendelee kuongea lakini kaka yake
akaendelea kuongea kwa kusema;
‘Sasa
huyu....unataka na mimi yanipate .....hahaaah, sio mimi, kamwe mimi sitageuka
jiwe, acha niende jela, kama ikifanya hivyo ni makosa, na nasema tena mnisikie ,
acha nihukumiwe, lakini sitakwenda kinyume na mila na desturi zetu za jinsi ya
kulea na taratibu za kifamilia,...’akasema
‘Bro....’Profesa
akataka kumkatisha kaka yake,lakini kaka yake akamuashiria kuwa anyamaze
‘Acha
niongee,...nikuembie hili mlisikia wote, kama mimi kwa kufanya hivyo itatoklea ikahukumiwa kwenda jela, kwasababu ya
kutimiza wajibu wangu kama mzazi, na ikawa ni kutokana na huyo mtoto,.....nyie
mtakuwa mashahidi, yatakayomkuta huyo
mtoto, ....sipenndi na wala sio mimi,....’akawageukia wazee na kusema
‘Wazee
mnayafahamu hayo, lakini sijui, ...labda iwe kweli,yeye hakutokana na damu
yangu, labda kama anavyodai yeye sio kweli mtoto wa kutokana na mimi....’akasema
na kufanya kama ananawa mikono....
Tuendelee na kisa chetu
*****************
‘Lakini mzee mwenzetu hayo tutakuja kuyamaliza kinyumbani,tutahitajika
kuyasafisha na kijana aelekezwe la kufanya ...hapa kama unavyoona, ni sheria
inahitajika, na wao wamejaribu kuliona hilo, na wakajua kama hali itakwenda
kisheria zaidi wewe utakwenda jela, je itasaidia..’akasema mzee
‘Kwahiyo, hebu kwanza, tuyasikilize hayo ya kisheria
yanavyotaka kwanza, na tukirudi nyumbani, tutaendelea na taratibu zetu kabla
hatujachelewa,,....muhimu huyo kijana apate mtu amuelekeze, lakini kwa hivi
sasa tukubaliane na hili,..’akasema huyo mzee mwingine.
‘Hahaha wazee wenzangu, kwanini mnifanyie hivyo,
mnasema tutayaongea....kweli mnasema hivyo, tuache mimi nivuliwe nguo,halafu
....ndio tuje tukae tuyaongee, wakati mimi
nimesha-aibika, nimeshakiuka miiko yetu,...hamjui wanachotaka mimi nifanye,...hebu
niambieni wazee wenzangu tunamzihaki nani hapo...?’ akawa kama anauliza
Wazee wakawa kimia, na yeye akaendelea kuongea
‘Huu wazee wenzangu ni utoto, ....natamka hivi kwani
mnafahamu hivyo, huo ni utoto, eti tufanye hivi,tukimalize tujifaye yale
tuliyofanya sio, tulikosea wakati huo tunafahamu tulikosea haya tunayotaka
kuyafanya, hivi kweli inakuja akilini,..?’ akawaangalia wazee wenzake, ambao
walikuwa kimia wameagalia chini.
‘Najua hili ni langu, najua .....huu ni mkosi,
umeingia kwenye familia yangu, na chanzo ni huyu mdogo wangu, kwa kujifanya
yeye ni msomi, kaishi na wazungu..kaiga mambo yao, na nakuambia, ....wewe, toka
awali nililiona hili, sasa sio mimi. Ni wewe ...utabeba huo mzigo
mwenyewe....’akasema akimuangalia mdogo huku akimnyoshea kidole.
Mdogo mtu akawa kainamisha kichwa chini, akionekana
mwingi wa mawazo, kabla hajajitetea, wakili mtetezi akasema;
‘Mzee, mimi nakuelewa sana, sio kwamba siyaelewi
hayo,....mimi ni mzaliwa wa huko na pamoja na kusomea sheria, lakini pia
nimejitahidi kujifunza mila na desturi zetu, na mila za ulezi ni kila mahali
hata huko ulaya zipo, sema wenzetu wana yao ...sipendi kuyaongelea zaidi,...na
hata hakimu anaelewa hayoo ndio maana akatumia hekima badala ya kusimamia
kwenye sheria tu...akaona hekima itumike......’akasema wakili mtetezi
‘Kama ni hivyo, huoni.....’akataka kusema mshitakiwa
na wakili mtetezi akamkatisha kwa kusema;
‘Huenda utasema nisingeliongea hilo mahakamani, sasa
angalia kwa upande mwingine kama nisigelifanya hivyo, ingetokea nini,...’
‘Ungelifungwa,....’akadakia msaidizi wake, na wakili
mtetezi akatikisa kichwa kukubali
‘Ni kweli hukumu ingeweza kuwa mbaya kihivyo, na
baadaye ungelifahamu kuwa aliyekufunga ni mwanao, wakati huo hali imeshafikia
huko, haingeliwezekana kabisa kuwa na suluhu, haya niliyawazia na mwisho wake
nikaona ni heri nifanye hicho nilichofanya,...’akasema wakili akimuangalia
mshitakiwa
‘Hapana, hamkunitendea yanayostahiki,.....’akasema
mashitakiwa na Profesa akadakia kwa kusema
‘Bro, mimi naona kwanza tumsikilize wakili, ....na mimi
sioni kwamba vibaya, hajafaya vibaya kabisa ni wewe tu hutaki kuelewa, kafaya
jambo ambalo limezuia ubaya zaidi ...sasa tusipoze muda, kwa maswala hayo ya
kimila na desturi, hayo yanaweza kusubiria, lakini kuna hili swala la sheria,
wakili kapewa kazi na hakimu, tusipoteze muda,...’akasema Profesa
‘We bwana mdaogo unazarau tu...nakuelewa
sana....’akasema kaka mtu
‘Ama hilo la kunilaumu mimi, nafahamu sana kosa
langu,najua kama ingelitokea vinginevyo kijana akarudi vingine akawakubali, na
hali nzuri, msingelisema haya, lakini hayo tuyaache hayo ..’akasema Profesa
‘Usijitetee makosa, huwezi kufuga nyoka wa sumu
useme angesaidia baadaye, wakati keshaanza kuumiza watu..nyoka uliyemfuga huko
sasa anatugeuka....ukaona ukae kimia, wengine nao wakione cha moto.....’akasema
kaka mtu
‘Bro,...nina maana kubwa kwa mimi kukaa kimia
kukuambia hili, nitakuja kukuambia ni
kwanini nilifanya hivyo, kwa hapa siwezi kukuambia, sipendi kulizungumza hili hapa,
litaharibu kila kitu....’akasema Profesa
‘Unajua wewe bwana mdogo nakufahamu sana toka
utotoni, wewe ni mbinafasi, inapofikia kwenye jambo la kuamua kwanza unaangalia
ubinafsi wako, hujali wengine, hili ndilo limetufikisha hapa, na tabia yako
umemuambukiza na huyo mtoto,hupendi kuambiwa ukweli, hupendi kuelekezwa, wataka
kujiamulia utakavyo....’akasema
‘Bro....’akataka kujitetea
‘Sasa huyo nyoka,...natumia neno hilo, mnielewe,
huyo mtoto, ni wako, na mimi kama ni kwenda kufungwa sawa, si na mimi natakiwa
nikione cha moto,...lakini .....’akasema
‘Nani kakuambia utafungwa...’akasema wakili mtetezi
‘Unafahamu nyie hamnifahamu mimi vyema, ....haya
yote mimi nilishayaona kwenye njozi, na kuna makubwa yanakuja,....kosa
lilianzia mbali, sitaki kusema hapa, nikaoa, yakatokea haya, ya kutokea baadaye
nikawa sina jinsi, sasa cha moto nakiona.....’akasema akiwa anatikisa kichwa,
na wakili akawa anamuangalia huyo mzee kwa macho ya kutafakari.....
‘Lakini hayo yalishapita, nilishaosha mkono na
kutubu dhambi zangu,...kumbe ..kumbe...kumbe...mambo bado, maana naishi na watu
wasielewa, hawa watu hawa ndio wnaharibu jamii....’akasema akimnyoshea kidole
profesa
‘Lakini hata hivyo mimi sitakubali, ..yanayokuja
mimi sitakuwepo, wewe bwana mdogo utapambana nayo, ...si ndivyo ,mnavyotaka,
utajiri au sio, haya utaupata, lakini hutapata raha....hilo
nakuambia,.....’akatulia
‘Bro ....’akataka kukatisha lakini wakili
akamtuliza, na mshitakiwa naye akanyamaza kimia
Kukapita ukimia kidogo kama vile kila mmoja
aliyekuwepo hapo alikuwa akiliwazia hilo jambo na wakili mtetezi akaanza
kuongea;
*************
‘Naona tusipoteze muda, ni muhimu nikawaelezea tukakamilisha
hayo ninayotakiwa kuwaambia, utekelezaji wake, kama alivyopendekeza muheshimiwa
hakimu , tukiyafanya hayo,tunaweza kumshawishi muheshimiwa hakimu...’akaanza
kusema
‘Nafahamu sana mila na desturi zetu za malezi ndani
ya jamii zetu, nafahamu sana mitihani ya ulezi hasa kizazi hiki cha sasa
ambacho kunakumbana na mitihani mingi inayotakana na utanndawazi, ...’
‘Tunaweza kuwalaumu sana vijana wetu, lakini wakati
ndio umetufikisha hapa, sio wao tu,...ni mabadiliko ya maisha duniani nzima
kizuri kina changamoto zake,..utandawazi ni mnzuri, lakini changamoto zake ni
nyingi...., na inapofikia kwenye ulezi, kwenye watoto wetu kila mwenye hekima
litamgusa hili,....’akatulia
‘Usione mwenzako limetokea hili ukahisi wewe upo
salama, labda wewe uwe una kijiji chako, una dunia yako, ambayo watoto wako
wanaishi peke yao, na usiwe na aina yoyote ya mawasiliano, kitu ambacho
hakiwezekani....hili ni letu sote kwani mwenzako
akinyolewa, na wewe tia maji, hili...
‘Mzee, hilo sio swala lako tu, wengi kila mmoja wetu
hapa linamgusa kama sio kihivyo, ni kivile,....na kwingine ni kubaya zaidi
kuliko hata hili lako, ni kwa vile tu halijawekwa hadharani....’akasema na kila
mtu akawa anatikisa kichwa kukubali
‘Sasa ndugu zanguni, hili sasa limetokea tulione
kama swala latu sisi wazazi..,ilitakiwa iwe hivyo, wazazi wote tungetakiwa tuwe
kitu kimoja, likitokea jambo sio la kawaida, wazazi tukutane tuone
tutalirekebisha vipi, kabla halijasambaa, lakini sasa hivi ulezi ni kila mtu na watoto
wake,....’akasema wakili
‘Siku hizi mtoto wa mwenzako akikosea, ukajaribu
kumuadhibu, acha kumuadhibu, ile kumkemea tu, utazua ugomvi,...na ukiwa ndio
mzee itazua balaa, mzee mwanga mzee mchawi, na maneno ya kukatisha tamaa na hata kuvunja
undugu au ujirani, utasikia wewe ulinisaidia kuzaa, ulinisaidia kulea
wewe....hayo na mengine mengi, na matokea yake ndio haya....’akasema wakili
‘Sasa tusikimbilie kulaumu kama wapo wenye uoni wa
mbali, basi tujaribu kulitatua lile linalowezekana, na hili letu liwe kama
mfano, tusiadianeni, kabla hijafika mbali....’akasema wakili
‘Wazee wenzangu, nimeamua tusaidiane hili, na
nimefaya hili kwa kujitolea, ni kwelii mimi kama ningetaka pesa ,
nisingelifuatilia hili jambo,hadi hatua hii, ..lakini aliposimulia huyu rafiki yangu
Profesa, nilihisi mwili mnzima ukinicheza, nikiwazia watoto wangu, nikiwazia
watoto wa watoto wangu, huko tunapokweda ni kubaya,....’akasema wakili
akiwaangalia wazee wale waliokuwepo
‘Huu ni mtihani, na ....hata kama sheria zitawekwa,
adhabu zikatolewa, haitasaidia kitu, kwani chanzo kipo pale pale.....na
kinazidi kuota mapembe, kiajitanua siku hadi siku, huko mbeleni yatazuka mabaya
zaidi.....’akasema wakili
‘Sasa wazee , tulifikiria hili kama njia ya
kuonyesha njia ili wegine wafuate, najua sio kazi rahisi, lakini sisi tutakuwa
tumetimiza wajibu wetu, mimi nimeamua kutokuagalia masilahi, nimeamua
kujitolea, ni kwanini, najua kujitolea siku hizi ni gharama, lakini najua ni
faida mbele ya mungu....’akasema
‘Baada ya kusema haya, tusipoteze muda, najua
mnahitajika kurudi kijijini, lakini nimeona ni bora tulifanye hili , tuanze
utekelezaji mapema, ili mkirudi tena hapa mahakamani tukakuja kulimaliza hili
kabisa,...’akasema
‘Sasa kuna mambo ya kufanya, naomba haya myasikilize
kwa makini ili mimi niweze kulifanikisha hili, msiposhirikiana nami, itafika
sehemu nitashindwa...’akasema
‘Hii ni kesi ya aina yake mtoto kumshitakia baba
yake, na wakati huo wawili hawa hawafahamiani, ....’akasema
‘Haya sasa wamefahamiana iweje, na wamefahamiana
wakati kesi inaendelea,...ila
tuelewe tatizo sio kwa vile ni kesi ya baba na
mtoto, hilo laweza kutokea, mtoto akamshitakia baba yake, na baba akamshitaki
mtoto, na sheria ikafuata mkondo....’akasema wakili
‘Mimi nilimuelezea muheshimiwa hakimu hali halisi, kwa
kadri alivyonielezea Profesa, na hakimu alishangaa sana kwanini hali hiyo ikawepo,
Profesa ilitakiwa uwepo kujibu maswali
mengi , ya kwanini ilitokea hivyo,....mimi
nikatumia uzoefu wangu kumfahamishana hakimu, na ni kwanini tunaomba hii
kesi iwe hivyo, ndipo hakimu akataka muda kulitafakari ombi letu...’akasema
‘Alitumia maneno hayo, apewe muda kulitafakari ombi
letu, lakini akitia maagizo ya mambo yanayotakiwa sisi tufanye .....’akasema
‘Kwahiyo kuahirishwa huko ni kwa manufaa yetu, lakini
kama tutafanya hayo aliyoagiza hakimu, ili yaweze kumshawishi hakimu, kuwa hili
lilitokea kwa bahati mbaya , ....’akasema wakili
‘Tafadhali hapo kidogo.....’alikuwa mshitakiwa
aliyetaka kuongea lakini Profesa akamzuia
‘Bro mengine tutaongea nyumbani najua unataka
kuongea kitu gani.........’akasema na wakili akamuangalia mshitakiwa halafu
Profesa, na baadaye akaendelea kuongea:
‘Sasa ni hivi, japokuwa hakimu kaahirisha hii kesi,
lakini kesi yetu bado ni ngumu, kutokana na utata wake,...ni kesi ya jinai, na
lengo letu ilikuwa kuirejesha hii kesi kuwa kesi ya madai, na.....zaidi
tuliomba ikiwezekana ikaongelewe nje ya mahakama,....inakuwa ngumu sana kwa
hakimu kuamua hivyo, lakini pamoja na sheria hekima nayo ni muhimu sana, nimefurahishwa
sana na huyu hakimu...’akasema
‘Sasa kuna mambo muhimu sana tunahitajika kuyafanya
...’akasema na wote sasa wakatulia kumsikiliza wakili
‘Ili ombi letu liwe na uzito, inabidi sisi wenyewe kukaa
kikao na waliotendewa hilo kosa tuwe na kitu cha maridhiano, na pande zote
zikubaliane na hilo, hii ina maana waliotendewa hilo kosa, wakiri kuwa wameshasamehe
na wapo tayari, kama wanahitaji fidia au itategemea na wao watakuja na hoja
gani....’akasema wakili sasa akijaribu kumuangalia kila mtu kwa muda wake kuona
kama hilo limeeleweka...na alipofika kwa mshitakiwa, ...
‘Tafadhali ngoja kwanza, ,,,..’akasema mshitakiwa
‘Bro tutaongea hayo yako tukifika nyumbanii, subiria wakili aeleze kilichoongelewa na
hakimu ili tukifika huko nyumbani tujue tunaanzia wapi, hii ni kwa manufaa ya
hii kesi...’akaambiwa.
‘Mimi nataka niliweka hili wazi mbele yenu, mkisema niache akaongea tu,
wakati mimi sijakubaliana, itasaidia nini, ....mimi sijakubaliana na hilo ombi,
kwasababu kwa mila na desturi zetu hicho hakipo....’akasema
‘Lakini hapa hatupo kimila, tupo kisheria...’akasema
msaidizi wa wakili mtetezi
‘Sasa kama mpo kisheria, nasema hivi, mimi mzee
Makunjazi, kamwe sitaweza kukaa na huyo muhuni, eti mimi mzazi nimuombe mtoto
msamaha, na pia eti nimbembelezi kuwa mimi ni baba yake, nimuombe afute kesi,....yeye
kama nani,...?’ akatulia
‘Eti wazee
wenzangu mbona hamnisaidii kwa hili, mnafahamu mila zilivyo, au kwa vile sio
mtoto wenu, hahahaa basi sio mimi....kamwe....’akasema mshitakiwa
‘Bro, sikiliza kwanza, anachoongea wakili...tumsikilize
wewe unang’ang’ania, hapa hatuongei maswala ya mila,tunaangalia sheria
itatusaidiaje ili hii kesi iishe kwa amani, hapa hujashitakiwa na
mila,...uelewe hilo,....’akasema Profesa
‘Haina haja ya kusikiliza zaidi basi, mimi
nimeshaelewa, nia na lengo lenu ni kumvimbisha kichwa huyo mhuni, vijana wa
namna hiyo ukiwapa nafasi wanazidi kuharibika, na kuona alichokifanya ni sahihi
...., ‘akasema kwa hasira
‘Kwa hivi sasa tutajifanya hivyo, ...’akasema
msaidizi wa wakili
‘Kweli dunia imekwisha, mtoto anizalilishe mimi hivi,
mtoto anipige, mtoto anivunje mbavu, kisa ni nini, halafu bado sisi
tumbembeleze, hapana mimi sikubaliani nanyi kabisa...’akasema mshitakiwa
‘Lakini hayo ya kukufanyia hivyo, sio kosa lake, alikuwa
hajui kuwa wewe ni baba yake, mzee
mwenzetu....’alikuwa mzee mmojawapo aliyesema
‘Kwahiyo kama mtu mzima sio baba yake afanye hivyo,
ampige kama mwizi, bila kujua ni nini kilitokea kisa kafika nyumbani kwake
akakosa kuelewana na mlinzi..hakutaka kujua kisa ni nini, mlinzi kaumia na
kujigonga alipodondoka.....aaah, hata haina haja ya kuwaelezea zaidi...’akasema
akitikisa kichwa
‘Hayo sasa tutayaongea nyumbani tusubirie, tunaomba wakili uendelee kutoa maelezo yako...’akasema
Profesa na kaka mtu akatulia akiwa kakaangalia pembeni kama vile hataki
kusikiliza, na wakili akaendelea kuongea;
‘Sasa ndugu zanguni, hili nii ombi , tumeomba sisi,
kwa muheshimiwa hakimu, na ombi letu lipo mikononi mwake, hakimu anataka
kutumia busara zake,na kuacha vipengele vya kisheria, fujo imefanyika, na ukikwaji wa sheria upo
wazi, lakini kwa mustakabali wa kifamilia, muheshimiwa anaweza kufumba macho...’akasema
wakili akiongea kwa sauti ya chini kama vile hataki watu wengine wasikie.
‘Japokuwa katika utetezi wangu, hakimu aliona kuwa
kuna namna ya shahidi kuwa muongo, kutokana na jinsi nilivyombana, lakini bado
haikuwa na tija,....mtu kaumizwa, na matendo hayo yametokea kwenye makazi ya
mtu...hilo ni kosa....’akasema wakili kwa sauti ya chini
‘Hilo ni jambo moja lakini kuna hili jambo jingine
kuwa tunahitajika tuwe na vielelezo vya kuthibitsha kuwa kweli huyo mtoto ni
mtoto wako kweli, mshitakiwa...’akasema
‘Vielelezo gani...?’ akauliza mshitakiwa
‘Vipimo vya kitaalamu kuwa kweli huyo ni mtoto
wako..’akasema wakili
‘Mimi sina haja ya kuthibitisha hilo kama yeye
kakana na kusema mbele ya mahakama kuwa mimi si baba yake, basi, kuna haja gani
ya hilo, vipimo vya nini, nataka kuthibitisha nini, kumbembeleza kuwa mimi ni
baba yake, hapana hili tuachane nalo.....’akasema
‘Sio kwamba ni hiari,....mimi nimeshalitamka hilo
mahakamani na hakimu anahitaji ushahidi wa kitaalamu, ili kuweka uzito wa madai yetu, ni taratibu na ni muhimu
zifuatwe, na sisi ndio wenye shida, ..’akasema na kuwaangalia mshitakiwa na
mdogo wake, na hakutaka kuwapa nafasi ya kuongea akasema;
‘Ujue sisi ndio tuliofanya kosa, na kosa ni kosa na
mtendaji wa kosa hata akiwa nani kamtendea
nani sheria ipo pale pale, ukifanya kosa utahukumiwa tu,haijalishi kuwa wewe ni
baba yake, hilo tulielewe kwanza ....lakini kutoka na hali ilivyo, hakimu kwa busara
zake kaliona hilo,kaamua kutumia busara
zake ......’akasema
‘Kwahiyo ili tuwe na mshiko wa maombi yetu, inabidi
wewe mshitakiwa na mtoto mkae kikao kilichoratibiwa, mbele ya wanasheria
yawezekana ikawa mimi au yoyote mtakayemchagua, kulithibitisha hilo....’akasema
wakili na kumuangalia mzee
‘Hahahaha, unajua wewe unaongea kirahisi sana, ...mimi
ni mzazi, ndio natakiwa nimnyenyekee mtoto, si ndio maana yake, yaani, nikae na
huyo mtoto muhuni asiye na adabu, nianze
kumbembeleza.... hivi nyinyi mnalionaje hili, au kwa vile haliwahusu saana, .....?’
akauliza mshitakiwa akimuangalia wakili na baadaye akawaangalia wazee wenzake.
‘Kukaa kikao ndivyo inatakiwa, lakini hilo la
kumbembeleza,....hapana, yeye ataongea na muendesha mashitaka ataelekezwa la
kufanya, akikubalia, sizani kama kuna maswala ya kubembelezana mzee, sizani
kama atakuwa na ujeuri huo mbele ya mzazi wake....’akasema wakili
‘Pamoja na hilo kunahitajika vielelezo vya
kulithibitisha hilo kitaalamu kuwa wewe kweli ni baba yake, ni utaratibu tu, kwa
ajili ya kumbukumbu, na muhimu vielelezo hivyo viwepo ....’akasema
‘Una maana gani kuthibitisha....?’ akauliza
‘Ni hivi, wewe ni baba yake, kihalisia, lakini
kimaandishi tutathibitisha vipi, ...kimaandishi tunahitajika kuwa na vielelezo,
tunahitajika tupate vipimo vya kitaalamu, na siku hizi kuna vipimo ambavyo
havina mashaka, ambavyo ukipimwa kweli inathibitisha kuwa wewe kweli ni baba
yake halisi, vipimo hivyo vinaitwa DNA, ...’akasema
‘Hapo mzee kama ulibambikiwa
itathibitika.....’akasema msaidizi wa wakili mtetezi akionyesha utani, ...
‘Kwa minajili hiyo mshitakiwa na mtoto tutahitajika twende
hospitali za serikali, mtoe damu zenu, zipimwe, na majibu yake yataambatishwa kwenye
maombi yetu...’akasema wakili
‘Lakini itakuwa na haja gani, hata kama vipimo hivyo
vitathibtisha hivyo, lakini moyoni mwa huyo kijana haipo hivyo, hakubali, mtoto
keshakana, na kasema hata kama itakuwaje, yeye hayupo tayari kunikubali mimi
kuwa ni mzazi wake, mlisikia wenyewe akisema...’akasema mzee
‘Hayo aliongea tu, kwa hasira, lakini atakaa chini
na atajirudi, haya hutokea kwa vijana kama yeye, lakini akipata muongoza
hujirudi....’akasema msaidiazi wa wakili
‘Na jingine kwa hali ilivyo, Mzee tukubali kuwa sisi
ndio tuatakiwa tuwe wampole, kwani yote hayo yanafanyika ili kukusaidia ombi
letu likubaliwe, na ukiangalia zaidi mtoto au kijana yeye ni shahidi tu,
japokuwa ni shahidi mkuu ambaye anaweza kukufunga, kwa hayo yaliyotokea,
.....’akasema jamaa aliyekuwepo
‘Kwahiyo nyie mnataka mimi nifanyeje nini....ehee,
siamini hayo?’ akaulizwa mzee akimuangalia wakili mtetezi
‘La kufanya ni kushirikiana na kile anachohitajia wakili,...yeye
kajitolea kwa ajli yako, kwa mfano kuna hilo la kupata ushahidi wa kitaalamu unatakiwa
kwenda hospitalini kutoa damu ili ikapimwe...., hilo sizani kama utakuwa na
pingamizi nalo, nina uhakika mtoto huyo ni wako, ....’akaambiwa
‘Labda yeye anamfahamu baba yake mwingine,
....’akasema mshitakiwa
‘Ni kiburi tu, si unajua tena vijana wa siku hizi,
lakini hilo tutalifankisha kwa njia zozote, hata kama kijana atalipingahilo,
kuna njia nyingi tu za kulifanikisha hilo, lakini kuna hilo jingine
umeambiwa,...’akasema jamaa ambaye anamsaidia wakili mtetezi
‘Lipi ...?’ akauliza mshitakiwa
‘Hilo la wewe kukaa meza moja na kijana wako ili
mridhiane, wewe ukubali ni baba yake na yeye akubali kuwa wewe ni mzazi wake, mumekoseana,
kwa bahati mbaya,...yapite yaliyopita tugange yajayo, sisi sote ni binadamu na
mwanadamu ni mwingi wa kiburi,kujisahau, kukosea na hata kutakabari...hasa pale
anapojiona unacho...’akasema
‘Na wewe ni mtu mzima, kwa busara zako tunajua
utaliona hilo kihekima zaidi, unajua yote haya tunayafanya tukiangalia kuwa yanahitajika
maandishi kuwa kweli mumekubalina na hilo, kuwa mtoto wako amekubali na yupo
tayari kulifuta shitaka hilo, na ....anaweza kufidiwa kwa hasara uliyompatia.....au
sio wakili....’akasema huyo jamaa
‘Ndio hivyo.....’akasema wakili
‘Fidia ....ya nini, nimempa hasara gani, mimi
kaniumiza, ni nani atanifidia, hili hamulioni..?’ akauliza mshitakiwa akiwa
kakunja uso.....na kabla wakili hajajibu au kuelekezea, Profesa akasema;
‘Lakini je kijana yupo tayari kwa hilo....huo ndio
wasiwasi wangu mkubwa maana mhh.....?’
akauliza Profesa na kukatisha maneno yake.
‘Wewe ndiye unayetakiwa utusaidie kwa hilo, maana
wewe ndiye uliyeishi naye au sio.....?’ akasema huyo msaidizi wa wakili mtetezi
na wakili mtetezi akasema;
‘Ni kweli, wewe ndiye unayetakiwa ufanye juhudi hiyo
kuhakikisha wawili hawa wanaelewana, na tukuulize wewe uliyewahi kuishi naye,
je ikiwa vielelezo vyote vitathibitisha hilo, kuwa huyu mzee ni baba yake bado anaweza
kuendelea kukataa ?’ akaulizwa Profesa
‘Tangu awali alishajenga hiyo hisia kuwa hana
wazazi, japokuwa wakati naishi naye nilijaribu kumuelezea kilichotokea hadi
yeye ikafikia kuwa hivyo, lakini.....sijui kwanini, yeye hakutaka kukubali, ,
kama ujuavyo, wenzetu huko juu, watoto wana haki zao, hawatakiwi kulazimishwa,kwahiyo
sikuwa na la kufanya.....’akasema Profesa
‘Unaona ulivyomuharibu huyo mtoto, na madhara yetu
yanaturudia sisi wenyewe...’akasema mshitakiwa
‘Sasa Profesa huu ni mpira wako, hatutaki kusikia
kuwa wewe hutaki kuongea na huyo mtu hivi sasa, hili ni kwa manufaa ya familia
yenu, ni kwa ajili ya kusaidia hii kesi imalizike na nyie kama familia mkae
pamoja muelewane.....huyo ni kijana wenu’akasema wakili
‘Tatizo sio mimi, ....kama akikubali, tutakaa
naye,,,,lakini sio rahisi kama mnavyofikiria nyie, huyo kijana, aliwahi kutoa
ushahidi wa kunifunga mimi, kuonyesha jinsi gani asivyoikubali hii familia,...hebu
fikiria, hakujali kuwa mimi ndiye niliyemfanikisha akafika hapo
alipo....akawasikiliza wakwe zake , .....sasa ukiniambia mimi nikakae naye eti
sijui nimshawishi..sijui ....kama ikibidi kufanya hivyo nitafanya, japo, apende
asipende atakuja kukaa na mimi meza moja, hili likiisha,....’akasema Profesa
‘Unasema aliwahi kutoa ushahidi kama huo,.....mkiwa
wapi, huko nje,...mmmh kumbe ndio tabia
yake...oh, dio hivyo, vijana wengine hubadilika kutegemeana na mazigira
waliyokulia, lakini bado, msikate tamaa, mtu hujirudi, ....’akasema msaidizi wa
wakili kwa mshangao.
‘Ila mimi ninachotaka ni kaka alielewe hili akubali,
kwani mpaka sasa sijui kama yupo pamoja na sisi, ...’Profesa akasema
akimuangalia kaka yake.
‘Ni wewe utafanya yote hayo, sio mimi....’akasema
kaka yake
‘Unasikia bro, wewe usiwe ni kikwazo kwa hili, jaribu
kulichukulia hili kama namna ya kumsaidia kijana ili ajirudi, najua mimi
nitalaumiwa sana, lakinii nia yangu kwa kipindi hicho ilikuwa njema kumsaidia
kijana ili apate nafasi hiyoo ya kusoma
nje, nafasi hiyo ilitolewa kwa watoto wenye mazingira magumu, nikaona nitumie
huo mwanya ....sasa siwezi kuyasema hayo yote mahakamani, nielewe hivyo.....’akasema
Profesa akimwangalia kaka yake aliyekuwa kainamisha kichwa chini huku akiwa kakishikilia
akionekana kuwa na mawazo.
‘Kwani mimi nimesema nini, kwa vile wewe uamfahamu,
mliishi naye basi endeleeni hivyo hivyo,mtakaa naye, mkubaliane, kama kuna
maswala ya hati, wewe uwe ni kila kitu,....lakini sio mimi....’akasema kaka mtu
‘Bro huyo ni mwanao..mtoto wako,...usiharibu tena,
tumeshakubaliana hilo....’akasema Profesa akizidi kumwangalia kaka yake
‘Lakini yote
hayo ni kutokana na malezi, nyie wazazi mnayo
sehemu yenu ya lawama, japokuwa hilo kwa hivi sasa hatuna nafasi nalo, tukianza
kulaumiana hapa tutapoteza muda...’akasema msaidizi wa wakili
‘Wakulaumiwa ni huyu, aliyemlea,....’akasema kaka
mtu akimnyooshea ,kidole Profesa
‘Mwambieni yeye, kwanii yeye ndiye aliyemchukua na
kumharibu huyo mtoto ...., ndio maana mimi sitaki kukaa meza moja na huyo
muhuni, atakaa na huyu baba yake mlezi, wayamalize , yeye na mtoto wake, ,,,.’akasema
kaka mtu akimuangalia profesa
‘Lakini mzee, kwenye maongezi ya maridhiano ni
lazima wewe uwepo, ndivyo inavyotakiwa, ili mkataba wa makubaliano hayo
ukamilike, ili hata hakimu aweze kushawishika na kuweza kutumia busara zake
kukubaliana na maombi yetu, mtambue hiii ni michakato ya kumshawishi hakimu, ni
kwa manfufaa ya hii kesi,.....’akasema wakili, na mshitakiwa akatikisa kichwa
kuashiria kukataa akisema;
‘Mimi, labda kama yupo mzazi wake mwingine atalifanya
hilo,...mimi sitaweza kukaa na huyo muhuni, huo ndio msimamo wangu, ....kama
nilivyosema ,.huyu ndiye baba yake, atakaa naye watakubaliana, kama mama yake
angelikuwepo hapa, basi angejumuika naye, lakini sio.....’kabla hajamaliza mara
nyuma yako sauti ikatokea ikisema
‘Mimi mama yake nipo nitakaa naye meza moja nitaongea
naye, ....’na wote wakageuka kuangalia sauti ilipotokea
NB: Kwa leo ndio hivyo, wewe wasemaje,.. Je ni
kwanini pamoja na elimu kubwa wanayopata vijana wetu mbona bado elimu hiyo, haiwasaidiii
kimaadili....?
WAZO
LA LEO: Katika swala la malezi kila mtu ana nafasi yake,
hata kama mtoto muhusika hujamzaa wewe, lakini pindi unapoona kuwa mtoto huyo kapotoka
una wajibu wa kumuelekeza kama mzazi, kama vile ungelifanya kwa mtoto wako wa
kumzaa,....tukumbuke, wito huu, ‘’Tenda kwa mtoto wa mwenzako ukijua na wewe ni
mzazi pia,’’
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment