Baada ya
taarifa ya wazee kurejeshwa kijijini, wanafamilia walikutana kabla profesa kwenda kuonana na wakili
‘Bro hali
ndio hiyo, sasa tufanyeje, kwani hata wazee wenzako naona wamekasirika kabisa......?’
aliuliza Profesa
‘Kama
wamekataa tufanyeje sasa, iliyobakia sisi tutakutana huko mahakamani,......’akasema
kaka mtu
‘Kaka
umekiuka sheria, na mahakamani sio sehemu ya kuonyeshana ubabe, ni sehemu
inahitajia sheria , kiujumla umekosea, hata iweje, kinachotakiwa ni kutafuta
njia mbadala....’akasema
‘Njia gani mbadala,
kama wameamua kutumia pesa yao, waache wafenye hivyo,...au ulitaka mimi niseme
nini...?’ akauliza
‘Kuna swala
waligusia wazee, kuwa wewe kama unaweza uende ukaongee nao, uwaombe
msamaha,.....huenda hilo litasaidia...’akasema
‘Unasema
nini, mimi niende kuwaomba msamaha hao watu, kwa kosa gani, wewe hukuwepo
wakati huyo mlinzi anatoa maneno ya kashfa,. Ungelisikia huyo jamaa tena ni
kijana mdogo tu, sidhani kama ni ...anatamka maneno ya kashfa mbele yangu,
halafu niende kumuomba msamaha, mimi....’akatikisa kichwa
‘Ndio njia
inayoweza kusaida bro.....’akasema
‘Halafu
mlinzi na huyo bosi wao wananichangia kunipiga,....ole wao ...sikuwa na cha
kujitetea, ...na sasa wao wanaonekana hawana hatia mimi ndio mwenye hatia,
nilitakiwa nikae kimia wakinitukana , wakini dhalilisha....’akasema
‘Bro wewe
ulikuwa kiongozi wa kijiji, je watu wakija hapa wamepigana, ulikuwa
unawaamuliaje?’ akauliza Profesa na kaka mtu kwanza alitaka kutokujibu hilo
swali lakini baadaye akasema;
‘Inategemea
maelezo ya kila mmoja wao, nawauliza kila mmoja kwa wakati wake na tunatafuta
ni nani mwenye hatia,....maelezo yao yanasaidia kujua chanzo cha
tatizo,....ndio maana mimi sina wasiwasi hakimu atasikiliza chanzo cha tatizo,
atajua kwanini mimi ilifikia hadi kuchukua hatua hiyo. Mimi sio mwendawazimu, .....’akasema
‘Bro....chanzo
cha tatizo hakiwezi kukubalika kama wewe ulichukua sheria mkononi mwako, kupiga
na kuumiza,....hilo halitakubalika mbele ya sheria....’akaambiwa
‘Najua,
...nafahamu kuwa pale hasira zilinizidi, najua kwa namna fulani nina makosa
lakini nisingeliweza kukaa kimia,....’akasema
‘Kosa jingine
ulikubali hivyo mahakamani...kuwa ulifanya makosa hayo....’akasema
‘Kibinadamu
hata ingelikuwa wewe ungelichukua hatua niliyochukua, watu wengine wana majibu
yanye karaha hasa wanapokuwa kwenye kazi zao, maofisini mwao....na nlisema
ukweli mahakamani, ....’akasema
‘Hapo sasa
bro ndio uliharibu, maana kama ulikubali kuwa kuna kosa, ulimpa nafasi hakimu
kutafuta adhabu gani akupe, na adhabu ya makosa kama hayo ni kifungo na
faini....’akasema
‘Nisingelidanganya,....ulitaka
nisemeje kuwa sikufanya,.....’akasema
‘Ok, bro,
sasa.... unasemaje kuhusu hilo swala la wewe kwenda huko mjini, ukaongee nao,
uwaombe msamaha, ili haya maswala kama yawezekana yaisihie
kienyeji....’akaambiwa
‘Mdogo wangu
hilo mimi siwezi kulifanya, siwezi kuomba msamaha kwasababu sina kosa, acheni
nifungwe,...halafu nilikuuliza yule mwenye nyumba sura yake ni kama naifahamu, ni
nani yule, ni kijana mdogo,...sijui nilimuona wapi...’akasema
‘Hilo la
kumfahamu halitasaidia kitu kwa hivi sasa....na kama unamfahamu basi itakuwa ni
wakati mnzuri, mkaongea mkafahamiana na kuombana msamaha....’akasema Profesa
akimuangalia kaka yake kwa makini
‘Hahaha,
unajua ni kuambie kitu, ...kuonana nao sio tatizo, tatizo najua itakuwa majibu
na lugha yao, hatutaelewana,...nimekuambia wao wawili walinichangia kunipiga,
ungelikuwa walivyokuwa wakifanya, walikuwa kama wanaua nyoka,..wanaiga bila
huruma,....’akasema
‘Huyo sijui
ndio mwenye nyumba, akapiga mateke mbavuni niliodondoka, na yeye ndiye
kasababisha mbavu zangu kuachana...anaonekana ni kijana mdogo japo anaonekana
na mwili , unajua siku hizi vijana wanahumuka tu,...halafu akatamka maneno ya
kashfa ambayo sitaweza kumsamehe hata awe nani.....ndio maana sitaki kuonana
naye tena....’akasema
‘Maneno
ganii?’ akauliza
‘Alisema
mijitu hii yenye sura mbaya , inafanana kama michwawi ya kwenye sinema, inakuja
kuleta uchuro kwenye nyumba yangu, sitaki kuiona tena, ....’akasema
‘Oh,
angelijua,...lakini bro, ujue na yeye alitamka hivyo kwa hasira , hata kama
ingelikuwa wewe umeingiliwa kwenye nyumba yako ungeliweza kutamka
chochote...’akaambiwa
‘Kwahiyo wewe
unakubaliana na kauli yake hiyo kuwa mimi ni mchawi , ndio nina sura mbaya kwa
vile mimi ni mzee, lakini uzee sio jambo la kuomba, na imekuwa hivi kwa sababu
ya maisha magumu, je huyo mtu yeye hana wazazi....?’ akauliza
‘Alitamka tu
kwa hasira....sijui, atakuwa nao, na ...hajui tu kuwa wewe waweza pia kuwa
mzazi wake....’akaambiwa
‘Na je kauli
kama hiyo haiwezi kumpandisha mtu hasira...hahaha, siwezi kuwa na mtoto kama
huyo asiye na adabu, ...huyo, hapana, nakuuliza hivi kauli kama hiyo kweli
haiwezi kupandisha mtu hasira?’ akauliza
‘Inaweza ndio
lakini....’akataka kusema neno na kaka akamkatisha
‘Kama yeye
alidiriki kutamka maneno hayo bila kusikiliza upande wangu bila kufahamu kuwa
mlinzi wake aliumia kwa jiwe alipodondoka,...ulitaka mimi nikae kimia’akasema
‘Yeye
alipofika tu akaanza kujiunga na mlinzi wake bila kusikiliza upande wangu, yeye
alisikiliza kauli ya mlinzi wake na wote kwa pamoja wakaanza kunichangia
kunipiga, ulitegemea mimi nikae kimia wanipige tu....’akasema
‘Bro yule ni
mlinzi alikuwa kazini, ....’akasema na kaka yake akamkatisha
‘Sikiliza
mimi sitaki kuongea tena, utazidi kunipandisha hasira, tusubirie mahakama
itamua, mimi nitaelezea ilivyokuwa, na hakimu naye ataelewa, na kama ataamua
kunifunga hewala.....basi ...’akasema kwa hasira
‘Basi ngoja
mimi niende kuonana na wakili nitamuelezea ilivyokuwa na yeye ataona jinsi gani
ya kufanya.....’akasema
‘Wewe fanya
utakavyo, lakini mimi siwezi kwenda kuonana na hao watu, eti kuwaomba masamaha,
wameshanishitakia, wamesababisha hadi hali yangu imekuwa hivi, mimi katika maisha yangu unanifahamu nilivyo....’akatulia
‘Kawaida mimi
sipendi kabisa kuzalilishwa, hata kama ni umasikini, hata kama ni uzee, hata
kama ni nini, hayo ni maisha yangu, wanafikia kusema eti familia yetu ina
matatizo, magonjwa ..sijui....yanawahusu nini wao...hilo sitalivumilia, kwahiyo
kama ni kwenda, nenda wewe mimi siwezi kwenda kwa hao watu,...’akasema kaka mtu
‘Bro, wewe subiria
nikirudi nitakuwa na jibu muafaka, kama itabidi kwenda kuonana na hao watu,
itabidi tufanye hivyo,...ila kiukweli kwa mimi kuwaona hao watu, kwangu mimi
siwezi inatakiwa kaka ni wewe ujitahidi uende, sio mimi, ikibidi utakwenda...., lakini nina imani haya
maswala tutayamaliza tu, hata ikiwa ni huko huko mahakamani...’akasema
‘Sawa...maana
yote hayo ni kwasababu yako, na kwahiyo, ....inabidi nikuachie wewe, siamini
kuwa katika umri huu ningeingia jela, nilikucheka siku ile ulipokuwa
unanihadithia kisa cha maisha yako, nilikuona wewe ni mjinga...sasa leo yamenikuta
mimi...nawekwa ndani kwasababu, hata...’akasema kwa uchngu
‘Bro ndio
ujue dunia ilivyo,..usije hata siku moja ukamcheka aliye chini yako, kwa vile
wewe upo juu, ...hujafa hujaumbika...’akasema
‘Mimi
sikukucheka kwa hilo, nilikucheka kwa hayo uliyoyafanya..’akaambiwa
‘Amabayo na
wewe umekuja kuyafanya pia....’akasema
‘Mimi
nimefanya yaliyo sahihi, wewe ulitenda makosa, ...mimi nimetenda makosa
gani....? akauliza
‘Si ndio hayo
hayo, makosa ni makosa sio lazima yawe madogo au makubwa, sio lazima yawe
niliyotenda mimi na uliyotenda wewe, kama kisheria yatathibistishwa ni makosa,
ujue ni makosa tu.....’akasema
‘Wao
hawajatenda makosa, wao hawajachukua sheria mikononi mwao, ....walishirikiana
kunipiga, watu wa usalama wakanipiga ni virungu miguuni hadi nikaathirika
mifupa, mimi na uzee huu nagongwa kwenye vifundo vya miguu, wanatarajia nini,
si kunimaliza...docta kathibitisha kuwa mifupa ya miguuni imeathirika, kwa
virungu vya hao watu, ubavuni kwangu, mbavu zimeachana kutokana na kipigo cha
hao watu mlinzi na bosi wake...sasa hakimu aniambie kama wao wanaruhusiwa
kuchukua sheria mikononi mwao.....’akasema
‘Kama mimi
nina makosa na wao wanayo, kama mimi hakimu atanihuku, ahakikishe na hao watu
kawahukumu....’akasema
‘Lakini wao
walikuwa wakitimiza wajibu wao....’akasema
‘Ni kweli hilo
halitaonekana kuwa mimi nilizalilishwa , bila kujali uzee wangu, kwa vile wao
wanauwezo, kwa vile hayo nyalifanyika kwenye sehemu yake ya kazi, najua yeye
atasilizwa zaidi, japo alitoa matamshi ya kunizarau....najua inapofikia hapo
watu wanasahau kuwa kuna kauli nyingine huumiza zaidi ya matendo,...’ akasema
‘Lakini bro
yategemea hayo yamefanyikia wapi, wewe ulikwenda kwenye makazi ya watu, na yule
alikuwa kazini hapo ndipo utashindiwa, ...’akaambiwa
‘Najua
....walifaya hivyo wakifahamu hivyo, kuwa wapo kwao, wanitukane wanizalilishe, wameniiga wakaniumiza hilo halionekani tena.....lakini
...’akatulia
‘Ndio hivyo
bro, walikutega kihivyo, wakijua kuwa wao hawatakuwa na hatia usikimama
kisheria,....wana elimu wana pesa,...’akasema
‘Wapo juu
eeh.wana elimu eeh,....wanahisi kuwa kukaa juu ni milele, kuwa na madaraka ni
kuongoza milele, huyo mlinzi kapata kazi basi anajiona kafika,kweli masikini
akipata.....anatusahau hata sisi walala hoi wenzake, hajui yale madaraka ni ya miuda tu ipo siku
watashuka chini ,...hata kama ni ile siku yao ya mwisho....’akasema kaka mtu
‘Bro , yote
hayo ni sawa, lakini kwa hivi sasa tuangalie sheria itatusaidiaje...mengine
hayatasiadia kitu, tutabakia kulalamika tu, na ili kuyafahamu hayo, mambo ya
sheria, itatusaidiaje inabidi tuhangaike, tutafute wajuzi wa washeria,
waliosomea sheria,..tatizo bro,i tunahitajika pia tuwe na pesa,.....kwahiyo
ngoja nikaonane na mwanasheria....’akasema Profesa
‘Haya wewe nenda
kwa huyo wakili wako, kama una pesa za kumlipa..mimi sina kitu, hali yenyewe
ndio hiyo unaiona, .....wamenimaliza kabisa....mimi hapa nilikuwa kiongozi
niliweza kuhukumu, kusuluhisha watu wakaishi kwa amani na sheria za asili,
sikwenda shule ya sheria, leo hii inafikia kwangu unatafuta watu wa sheria eti
waliosomea sheria,...haya nitafanya nini ...’akasema kwa uchungu
‘Ndio hivyo
bro.....’akasema
‘Nilikuwa na
nguvu zangu, nilikuwa na uwezo wangu wa kujitafutia riziki yangu kwa mikono
yangu mwenyewe sasa ninageuka kuwa omba omba,...wamenifanya niwe hivyo, hilo
halitaonekana tena kwa vile mimi ni mnyonge....’akazidi kusema kwa uchungu
‘Lakini bro
wewe ndio uliowaanza, wewe hulioni hilo....’akaambiwa
‘Mimi ndio
niliowaanza, wakati nilikuwa nakutafuta wewe, kwanini hawakukubali ombi langu
angalau wakanisikiliza , kwanini wakimbilie kunikashifu,....oh, hata kuinuka
sasa shida, wamenivunja miguu yangu....wamevivunja mbavu zangu, ....wangeniua
kabisa basi....’akazidi kusema
‘Bro,
...’akataka kuongea lakini kaka yake akamkatisha na kusema
‘Sasa
sikiliza, ukifika huko, umwambie kabisa huyo wakili wako msomi, mimi sipendi
nije kurejeshwa jela,..na kama itatokea hivyo tena...ikitokea kuwa nimehukumiwa
eti kwenda jela,.., eti wanihukumu kifungo,aah, sijui... sizani kama
watanifikisha huko jela nikiwa mzima....watafikisha maiti yangu....hisia
zinanituma hivyo.....aah sijui...’akasema kaka mtu na Profesa akamuangalia
ndugu yake akimuonea huruma.
‘Usijali bro,
haya tutayamaliza tu, niachie mimi.....’akasema Profesa na kuondoka, huku
akilini akijiuliza hata kama atampata huyo wakili atamlipa nini, maana wakili
anahitajia pesa, na pesa hana, hata kama anamfahamu vipi, ndio alikuwa rafiki
yake, lakini uwakili ni kazi yake haweze kuifanya kazi hiyo bure!....
‘Ngoja nifike
huko kwa huyo wakili,....ikishindikana, bro, oh, sijui ‘akasema na akilini
akawa anawaza jinsi gani anaweza kuificha hiyo siri,....akajikuta akisema
‘Nitakuwa
sina jinsi inabidi niiweke siri hii hadharani....’akasema
‘Siri gani na
wewe, hebu ondoka mimi nilale, najisikia vibaya, hapa moyo unanienda mbio kwa
hasira.....’akasema kaka mtu
*******
Basi Profesa
akafunga safari kwenda mjini, huko akakutana na huyo wakili rafiki yake wakati
wa wakiwa shule ya msingi,,..., akamuelezea jinsi tukio lilivyokuwa, na
alipofika mwishonii wakili huyo akasema
‘Hiyo kwa macho
ni unaweza ukasema ni kesi ndogo tu,...hiyo sio kesi ndogo,hasa inaofika
mahakamani...’akasema
‘Najua hilo....si
unajua tena hali zetu ndio maana nikaja kwako....’akasema
‘Huyo ndugu
yako kavamia makazi ya watu, jaokuwa alikwenda kwa nia njema, akampiga mlinzi,
akamjerehi, hapo nia njema yake yote inaonekana kuwa ilikuwa kwa nia njema, wao
watajenga hoja kuwa alidhamiria...baya zaidi akapigana na mwenye nyumba,...hiyo
ni kesi kubwa..sio kesi rahisi,...’akaambiwa
‘Ni hasira za
kaka, na inategemea jinsi gani mlinzi alivyomjibu, kuna majibu mengine yanakera
hasa unapogusia hali mtu aliyonayo, ukamnyanyaaa, hata hali hiyo ni ya weli
lakini kauli nyingine zinakera, zinaumiza sasa yategemea uhimili wa mtu...’akasema
Profesa
‘Hata kama
alizalilishwa,....akatukanwa....hakutakiwa kuleta fujo,...na hakutakiwa kumgusa
huyo mlinzi kabisa maana yule alikuwa kwenye kituo chake cha kazi, akitimiza
matakwa ya bosi wake..kwahiyo hiyo ni kesi kubwa , inahitajia umakini katika
utetezi, na hata tufanyeje, hapo gharama haziepukiki,...unahitajika uwe na pesa
nyingi, ili niweze kufuatilia kila kitu..’akaambiwa
‘Pesa nyingi
ya nini...unajua nimekuja kwako wewe kama rafiki yangu, umbuka tulipotoka,
unakumbuka nilivyoweza kukufanyia yale mambo yako nilipokuwa ulaya,....’ akasema
‘Hizo ni
gharama za kawaida, kufungua jalada lake, kuna gharama natakiwa kuzilipia, ili
kukata rufaa, kwani sikudanganyi, kwa vile alishakubali kosa, kinachofuata ni
hukumu, na hukumu hapo ni kifungo na faini,...alikubali kiharaka, ndio tatizo
la kutokuwatumia mawakili....’akaambiwa
‘Rafiki yangu
sisi ni masikini hatuna kitu....’akasema
‘Ujue, kesi
ilivyo, kaka yako ana makosa, alikubali kuwa kweli alifanya hayo makosa
mahakamani, si ndio... kwasababu zake, kuwa alichanganyikiwa, nk, lakini huwezi
kuchukua hukumu mikononi mwako, hilo ni kosa...kaka
yako.atafungwa!...’akaambiwa
‘Ina maana hakuna njia ya kuimaliza hiyo kesi nje
ya mahakama...?’ akauliza
‘Unielewe
vyema hiyo ni kesi ya jinai, ..hii sio kesi ya madai, na imeshafikishwa
mahakamani, kwahiyo kuimaliza kwake ni mahakamani,...na ili ifikie hadi hakimu
akubali maombi hayo, ni hao waliofanyiwa hivyo, wafike mahakamani, ....’akasema
‘Kwani...’profesa
akataka kuongea lakini wakili huyo akasema
‘Kesi ikiwa ni
jinai ina maana ni serikali inayoiendesha, ,...sio hao wahusika,,..hata kama
hao waliotendewa hivyo watasema kuwa wamesamehe, hayo ni yenu tu, lakini
maamuzi makubwa yanategemea jinsi gani mtakavyo mshawishi hakimu....’akasema
‘Kwahiyo
haiwezekani kulimalizia hili tatizo nje ya mahakama.....?’ akauliza
‘Sijasema
haiwezekani,....lakini je ni jinsi gani ya kumshawsihi hakimu, mna maelezo
gani, ya kuweza kumshawishi hakimu, labda nikuulize wewe na hao waliotendewa
hilo kosa mumeshaongea na kuelewana...?’ akaulizwa
‘Mhhh tumeongea
nao, wazee walitumwa, wakaongea na hao watu,...lakini hakuna ushirikiano,
hawataki, ... wao wanadai hiyo kesi haipo mikononi mwao, kwahiyo hawawezi
kusaidia lolote, ndio maana nikaona nije niongee na wewe, ili nipata ushauri
wako....’akasema
‘Inavyoonyesha
mpaka sasa hampo kwenye maelewano na hao watu, au sio....?’ akauliza
‘Sasa
tufanyeje....?’ Profesa akauliza kabla hajajibu swali la wakil
‘Kwa kuweza
kujenga hoja za kumshawishi hakimu, ni muhimu mkaongee na hao wahusika,waliofanyiwa fujo,
ili hata tukipeleka hayo maombi,ya kuomba kesi hiyo ya madai .na tutafute
maelezo ya ziada ya kujitosheleza,...kitu ambacho bado kina ugumu, lakini
kwanza hakikisheni mumelewana na hao watu....’akatulia kidogo.
‘Je wewe
mwenyewe umeshaongea na hao waliofanyiwa na umeona kuwa wanaweza kuwa tayari
kutoa ushirikiano,...?’ akauliza
‘Bado...kwanza
nimekuja nije kwako kupata ushauri....’akasema
‘Ni vyema ukaongea
na hao watu, wakubali, na wawe tayari kutoa ushirikiano, bila wao huwezi
kufanya lolote...kwani wao wataitwa kama mashahidi, waliotendewa....’akasema
‘ Mhh hapo
sasa ndio inakuwa shida,....sijui kwa hilo utanisaidiaje, wewe huwezi kwenda kuongea
na hao watu...?’akauliza Profesa akimuangalia huyo wakili na wakili bila kusita
akasema;
‘Wewe ndiwe unatakiwa
ufanye hivyo, uende ukaongea, nao .... muelewane...., huo ndio ushauri wangu,...’ akasema wakili
akiangalia saa yake.
‘’Mimi
niongee nao...mmmh hapana, siwezi....kuna sababu za msingi zinanizuia kuongea
nao kwa sasa....’akasema na wakili akasimama kuashiria kuwa keshamaliza,
‘Sababu gani
za msingi,.....’akasema wakili akimuangalia Profesa, na Profesa akasimama, sasa
akitaka kuondoka.
WAZO LA LEO:
Ufumbuzi wa jambo lolote, lenye utata, hauwezi
kutatuliwa, na kufikia muafaka wa kudumu, iwapo WASULUHISHI, au WASIMAMIZI watakuwa na masilahi na hilo jambo.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment