Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, July 11, 2015

RADHI YA WAZAZI-18


‘Mume wangu leo nina mazungumzo na wewe..’ akasema mke wakati huo mumewe alikuwa kakaa kwenye kiti cha nje,  akiwa kakunja nne,kando yake ipo chupa ya kinywaji, utafikiri hana shida, kumbe kichwani alikuwa kama kachanganyikiwa, leo aliamua kununua kinywaji kuja kunywea nyumbani, bar hakuendeki tena.

‘Una mazungumzo gani tena mke wangu, tafadhali nakuomba nipumzike...sipo sa-sa-sawa...mwenyewe siunaona....’akaongea kwa sauti ya kilevi.

‘Haupo sawa kwa vipi unaumwa, na leo kwanini umeamua kuhamishia ulevi wako hapa nyumbani, si nilishakuambia mimi sipendi mambo ya pombe pombe hapa nyumani, kama unataka kunywa kanywee huko huko, na wanawake wako....’akasema kwa hasira

‘Mhhh,....sitaki tena kwenda bar, na hao wanawake sio wanawake wangu, wewe ndiye mke wangu, unasikia, hao, siwataki, na sitaki kwenda huko tena...nitakuwa nakunywa hapa hapa....’akasema

‘Sawa...sawa,  kweli naona leo haupo sawa,...tutaongea kesho,na hakikisha kuwa hiyo kesho hulewi, kwani hayo ninayotaka kuongea na wewe yanahitajika uwe na akili timamu..’,mke akasema na kugeuka kuondoka

‘Sasa unakwenda wapi....’akasema

‘Umesema haupo sawa, na jinsi ulivyo kweli haupo sawa, siwezi kuongea na wewe ukiwa hivyo tutakosana, na haya niliyokuwa nayo yatasubiria ukiwa mzima, ni muhimu sana.

‘Poa....unafikiri najali,...sijali, hata wakichukua zote, sijali....hata na wewe...kamaumenichoka, sijali...nikiona vipi, nakunywa weee,mpaka napitiliza, si mtazika tu.....’akawa anamumunya maneno

Mkewe akaondoka kuendelea na shughuli zake, hakusikiliza nini mumewe anaongea maana maneno yalikuwa kama ya kulalamika, basi siku hiyo ikapita na kesho yake sasa...

Tuendelee na kisa chetu

*****

Aliyeamuka mapema alikuwa ni mume, akatoka alifajiri sana,.. na kwa vile  ilikuwa siku ya mapumziko, yeye akatoka nje na kupitia pitia bustanini, nia ni kukwepa kuongea na mkewe, alihisii jana atakuwa kamkorofisha, ila anakumbuka kuwa mkewe alisema ana jambo la kuongea, akilini akawa anajiuliza ni kitu gani.

Akilini alikuwa katulia, lakini kuna kitu alitakiwa kukifuatilia, na alishaambiwa ili akipate, anahitajika kupeleka salio lililobakia.

‘Kwa vile pesa hii haitoshi, hatuwezi kukupa zile picha,....na kanda ya video, ujue hizo picha zimechukulia kwenye video,...’akaambiwa

‘Kilichfanyika mpaka sasa ni kuiondoa hilo tukio kwenye mitambo ya kwenye ile bar, hukohawawezi kulioa hilo tukio tena, sasa hilotukio lipo mikononi mwa watu, ambao wamejitolea kufuta huo uchafu wako....sasa utaka huo uchafu wote uwe mikononi mwako,kamilisha hiyo pesa iliyobakia....’akaambiwa

‘Lakini nimewaambia siwezi kutoa pesa banki....’akasema

‘Hizo nyaraka ni kitu kidogo sana, ukipeleka sasa hivi watakamilisha na wewe utaweza kuchukua pesa yako, sisi tunajua yote hayo, ukitoka hapa peleka hizo nyaraka,baada ya masaa 24, akaunti yako itakuwa huru..sasa ukizid kuchelewesha ndio unajiweka kubaya...’akaambiwa

‘Nina uhakika gani kuwa mtanipa hiyo video,je kama mumetoa kopi ili mje baadaye kunisumbua tena...’akasema

‘Sisi tuna uaminifu,...na sijui kwanini usituamini, kama tumeweza kufuta kila kitu kwenye mitambo ya ile hoteli na bar, kwanini tukufanyie hivyo tena.....’akaambiwa

‘Nakuapia, kama mtanifanyia ubaya, mkanisaliti,..hamjui nilivyo...nitawatafuta hata chini ya ardhi nitawapata..na nikiwapata  hamtaamii nitakachowafanya....’akasema

‘Hahaha,haina haja ya kutoa vitisho,tumeshakufahamu ulivyo...lakini huwa hata siku moja mtu hatishiwi nyau..wewe shukuru kuwa tumekusaidia, je kama tungeacha huo uchafu ukaonekana na utawala,...wakaufichua kwa wadaku, hizo ndio shukurani zako,kweli shukurani ya punda ni mateke....’akaambiwa

‘Niwashukuru kwa lipi, walamlungula nyie, blackmailer wabaya kabisa,najua kabisa hili mumelipanga, hizi ni njama,najua kabisa,... mimi sio mtoto mdogo,nyie ni shetani,mnaishi kuwa dhuluma,mfanye hivyo ili mpata pesa ya wizi....’akasema

‘Kwahiyo unasemaje, kama vipi ngoja tupeleke nakala moja ya picha kwa mkeo, aone huo uchafu wako  achilia mbali mkweo...’akasema

‘Mkwe wangu anawahusu nini...’akasema

‘Hahaha, ndugu, wewe umesema unafahamu sana,...hilo ni swali lakuuliza, ujue hawa unaopambana nao sio watu wa huko kwenu,ni wataalamu...sitaki nikuambie mengi, ....’akaambiwa

‘Siwaogopi kabisa, nitapambana na nyie, ngojeni,mumeniwahi,nakubali, lakini lipizo lake hamtaamini...’akasema

‘Kwahiyo unataka tupeleke nakala kwa mkweo.....unasemaje ili uone kuwa hawa watu hawaogopi...’akaambiwa, na hapo akahema tu.

‘Ndugu,ukumbuke mkweo alivyo, hakupendi, hawakutaka kabisa wewe uolewe na mkeo, nasema uolewe,maana hata mahari ya kulipa ulikuwa huna mkeo ndiye aliyekulipia mahari, kweli si kweli...’akaambiwa na akaa kimia akihema kwa hasira.

‘Kwahiyo mke wako anakupenda sana, hivi unataka upendwe vipi, ..nyie watu hamna shukurani,  ujue ni mkeo tu ndiye anayekupenda,...sasa na yeye akikuchukia utakuwa mgeni wa nani...utarudia umasikini wako,najua huko ulikuwa genge la vibaka, najua ulijiunga na kundi la kubaka, mkawa na mnaweka vifaa vya kuchukua video kwenye majumba ya watu mnawatishia na kuwadai pesa nyingi, hiyo ilikuwa kazi yako kabla hujakutana na huyu binti, ‘akaambiwa na aliposikia hivyo akajikuta mwili ukinywea

‘Mambo yako yote yaajulikana na mengi hayafahamu mke wako, wakitaka wanaweza kuyaweka wazi yote, lakini kwa vile upo tayari kutoa ushirikiano, basi, wameyasahau, ukilipa hiyo pesa,wanakukabidhi kila kitu, unakuwa huru, ila uache hiyo tabia....’akaambiwa

‘Mtaona....’akasema

‘Ndugu, hiyo tabia yako,  uliyokuwa nayo huko ni cha mtoto...ni sawa na mtoto  kuchezea kigari cha mwanasesere na kujiita dereva,...hapa kuna wajuuaji,wanajua ni nini wanachokifanya, mimi sitaki kukutisha saana, sasa kama wewe unabisha jaribu....’akaambiwa

‘Sawa nyie si mnahitajia pesa,...nyie si wajanja,pesa mtapata,mnasiki pesa mtapata, lakini mkumbuke hizo ni pesa chafu zitawaandama...’akasema

‘Kwetu sisi, kwao hao watu maana mimi ni mjumbe tu, kazi yangu ni kupeleka taarifa,....hatutofautishi pesa chafu na safi ilimradi inalipa...unasikia, fanya unavyoambiwa, vinginevyo,mimi nitawaambia umeshindwa, kutoa ushirikiano, ukiiona hii video,ndio utajua wewe hufai kabisa kuishi na huyo mwanamke...weweni mbakaji, mzinzi, mlevi.....hahaha....’akasema na kucheka

‘Nakuapia nitawapata tu....ni lazima mtalipa...’akasema

‘Hahaha, ..kumbe muda wote huo  ulikuwa unateseka,unatamani mabinti wa kwenye bar, au mkeo anakubania nini, hahaha, mzee mzima huna aibu...wewe, shukuru sana, maana video hii ikiingizwa sokoni,mbona inalipa sana, ina kichwa cha habari,   mzee kazidiwa na kugeuka kuwa mbakaji....hahaha...’akasema

You devil...nitahakikisha ninawapata mmoja baada ya mwingine,mtaona....hamunijui mimi...’akasema na kubamiza simu kwenye sofa....

‘Halloh ...unasikia....’akasikia jamaa akiita kwenye simu, akaitizama, baadaye akaiendea na kuchukua akaiweka sikioni kwa hasira akasema;

‘Kumbukeni hilo,...mimi siomjinga kama mnavyofikiria,...hayo maisha nilishawahi kuyapitia, hamjui ninapotokea,....mtaona...’akasema

‘Unachelewa mzee,...saa hivi ni saa ngapi....hujui ni nini mkeo  kakipanga,....shauri lako...’akaambiwa na alipotajiwa mkewe ndio akakurupuka haraka akaenda kuziwakilisha hizo nyaraka benki, akambiwa asubirie masaa 24

‘Oh,...’akasema akiwa hana ujanja

Kichwani alikuwa na hasira, lakini hata hivyo, aliogopa hayo mapicha yasije kufika kwa mkewe, lakini akawaanajiuliza je kama wanamchezea, atatoa pesa na itakuwa ndio mchezo wakumtoa pesa.

‘Mhh,hawa wanaonekana hawawezi kunitapeli...lakini lazima nipambane nao..’akajikuta akisema/

‘Halafu wamesema wanaweza kufikisha huo uchafu kwa mkwe wangu,hivi hawa watu wamenijuaje,na wamemjuaje mkwe wangu yaonekana ni watu wabaya sana,natakiwa kuwa makini nao..hata hivyo sikubali, nitapambana nao...’akasema

*******

Basi siku hiyo kazini alijifanya mgonjwa,akaruhusiwa kuondoka mapema, na alipotoka hapo kazini, akapitia bar , lakini sio ile ya kawaida,  akanunua vinywaji akaenda navyo nyumbani, akanywa huku anawaza jinsi gani ya kufanya

‘Ningelikuwa kwetu ningeliwatafuta wahuni wangu, ....nawafahamu wanajua kufuatilia haya mambo,..lakini huku simfahamu yoyote...ooh, nitamtafute nani sasa...?’ akawa anajiuliza baadaye akakumbuka jambo, akachukua simu akampigia rafiki yake mmoja

‘Ndugu yangu nipo Ulaya, na wameniingiza mjini, nataka unisaidie, ulisema huku kuna watu wako ehee...nataka unitafutie mpelelezi, binafsi...ehee, nataka anifanyia kazi yangu kuna watu wanajifanya wajanja...ehee, nitakurushia gharama zako, usijali, ...ndio nimekuelewa, ndio nimekunywa kidogo,...ndio nakuelewa, sijalewa sana nipo makini,..fanya hivyo...ni muhimu...’akasema na kurudi kwenye ulevi wake.

‘Lazima nipambane nao..na ole wao,nikimfahamu mmoja tu...atakuwa ni mfano,...’akasema na akakumbuka kitu, akasimama na kuingia ndani, alipofika akafungua kabati, sehemu ya chini, akavuta droo, na humo akakiona anachokitafuta,...

‘Mhh,..wewe hujatumika...miaka mingi hujatumika,....’akachukua kitambaa akakizungushia mkononi, halafu akatoa kitu, na kuanza kukiangalia, akaikagua...

‘Rafiki yangu upo eeh...’akasema, halafu akachukua boksi, , akatoa risasi, na kuzihesabu, halafu akazirudisha kwenye boksi,

‘Hizi zinatosha, mapambano yakianza, sijali....’akasema huku akichukua kitambaa kingine maalumu akafuta futa kile kitu na kuirudisha mahali pake...

‘Wewe ni rafiki yangu huwezi kuniangusha ...ukumbuke kunisaidia muda ukifika,umelala sana...najua,najua..upo ulaya hutaki shida, lakini, watu wananichezea, wananichokonoa,...’akawa anaongea utafikiri kuna mtu humo ndani...

‘Hivi ni kwanini, pesa zangu mwenyewe, wanazichukua,....kisa malaya....hahaha....hahaha’akawa anacheka kama kichaa, halafu akasikia sauti, akageuka kuangalia nyuma, alikuwa na uhakika ni sauti ya kitu, na ni lazima atakuwa ni mtu

Kwa haraka akafunga kabati, na kuhakikisha kila kitu kipo sawa, kama ilivyokuwa awali, halafu akatoka nje, ...

Alipofika sehemu ya maongezi, akahisi mlango upo wazi, lakini alikumbuka kuufunga, nywele zikamsisimuka, akaanza kunyemelea, ....kuelekea sehemu ya jikoni, huko alisikia kama sauti ya maji.

Alitembea hivyo kwa kunyemelea hadi akaingia jikoni,  akamuona mkewe akiwa kainama kwenye sehemu ya vyombo akiwa anapanga panga vitu, taratibu akageuka na kwa mwendo wa kunyata akarudi sehemu alipokuwepo awali na kuendelea kunywa, kunywa kwa hasira

‘Huyu mtu karudi saa ngapi, leo mbona kawahi hivyo....ni tatizo jingine hili , sina uhuru, sina...aah,...’akawa anaongea kwa sauti ndogo.

‘Nikwanini mke wangu mwenyewe, nikimuona mwili wote unazizima kwa woga, wasiwasi,....sijui nifanye nini.....ni kutokana na hao watu....’akasema huku akitupa jicho ya kujiiba kwa mkewe...

‘Aaah, aishie zake,leo,simtaki, nataka kinywaji tu...siwataki wote,hata yule malaya...aliyenifanyizia..’akasema akimimina kinywaji kwenye gilasi

‘Kama ningekuwa sehemu kazi hii angeifanya yule malaya...’akawa anaongea peke yaka.

‘Na yule malaya...siku nikikutana naye tena,...sijui,....nitajikumbushia ule uovu wangu wote wa zamani, ....hawanijui hawa watu...ngoja...’akawa anazidi kuongea peke yake

‘Hawa watu hawanijui, wananiona mimi lofaaa.., hawawezi kuniadhiri kiasi hichi,haijaahi kutokea, kiongozi wa genge haramu kuwekwa uchi...hawanijui hawa, hawanijui...’akasema na mara akahisi kama kuna mtu anamkaribia,akahisi mwili ukiingiwa na woga

Kwa hali ile alijua ni nani... ndio hapo akasikia...

‘Mume wangu leo nina mazungumzo na wewe..

‘Una mazungumzo gani tena mke wangu, tafadhali nakuomba nipumzike...sipo sa-sa-sawa...mwenyewe siunaona....

NB:Leo nakupa hiyo sehemu ndogo,  kufichua fichua kujua ilikuwaje,....tutaendelea na mazungumzo ya wawili hawa sehemu ijayo,mazungumzo yao  ni muhimu sana,..kwani kutokana na wao,tutaweza kuona jinsi gani mlungula ulivyo mbaya, unavyoweza kuharibu ndoa za watu,na hata kufikia watu kuuana...


WAZO LA LEO: Pombe ni kilevi kinachoathiri ubongo, japokuwa twaona ni kitu cha kustarehesha ubongo,lakini madhara yake ni makubwa, kiafya na pia ni kishawishi kibaya cha maasi. Ewe ndugu mpendwa, jiepushe na ulevi
Ni mimi: emu-three

No comments :