KILA KITU
SASA MPAKA TUMUULIZE NANI VILE.... ‘.AI’
Kuna sehemu
zenye majina ya asili, nimekuwa nikijitahid sana kupita pita maeneo hayo nione
jinsi gani kulivyo kwa hivi sasa, nikajiwa na mawazo..
1: Mnazi
mmoja ni jina maarufu, bila hata kuuliza hapo awali kulikuwa na mnazi mmoja
mrefu sana...sijui kama ulikuwa peke yake...kwangu mimi ningelipendekeza, kwa
historia ya vizazi vijavyo, basi kuwe na mnazi...ama wa kupanda, au utengenezwa
mnazi mmoja, ...japo naona kuna alama ya mwenge wa uhuru....au jina libadilike
liitwe, mwenye wa uhuru....
Ni mawazo
tu...
Huku mjini
kuna sehemu kama clock tower, kuna mnara wa simu, kwanini usiboreshwe, ukawa
mrefu na simu kubwa yenye kuonekana kwa mbali.
Kama
sikosei, maana niliwahi kufika Ujerumani kipindi fulani, nikaona jinsi gani
wanavyoboresha mandhari yao ya zamani, iwe kama kipindi hicho...
Kipindi
nafika walikuwa wakiboresha majengo ya zamani, yaonekane kama ilivyokuwa,
sijajua lile kanisa lilibomolewa kwa mabomu kama wameshaliboresha,....
Na zaidi ya
hayo kwenye treni zao, kuna watangazaji wanaelezea maeneo na historia zake,
Nilivutika
sana na wenzetu..
Mbona hata
sisi tunaweza
Mwendo kasi
huoo...ni ubunifu mnzuri.., unafanya kazi zake,...tunahitaji na treni pia za
kutoka mjini hadi nje ya jiji...na humoo....eeh, kuwe na watangazaji wa kelezea
maeneo,
‘Hapa
ni...eneo fulani, kwa maarufu kunaitwa kadhaa....asili ya jina hilo limetokana
na kadhaa..eeh....watu wanavutika, hasa watalii....’
Jamani sio
kila kitu tukione kwa wenzetu ndio tujifunze, watu wa kumbukumbu mpo wapi,
wanahistoria, wajenzi, wakufunzi mpo wapi jamani...au ndio tunasubiria tuwe
tunamuuliza AI....
Kwangu
mimi, elimu kichwani mwa watu inashuka,...usomaji wa vitabu unashuka...hii ina
maana gani...
Tutafakari
tusije tukaingia kwenye mtego wa kutawaliwa ‘KIFIKIRA’...tukawa watu wa ...kufikirishwa,
Kila jambo,
Tugoogle, tumtafute AI...ni maendeleo ndio , lakini akili za wengi zitalala....watu hawatahangaika kusoma, ....sijui mnanielewa!
Ni hayo tu
kwa leo kwenye diary yangu....

No comments :
Post a Comment