Ilichukua
muda, kabla huyo mama hajazindukana, mimi sikuwa nimepoteza fahamu kabisa
ilikuwa ni kizunguzungu tu, ndicho kilinifanya nidondoke na huyo mama, nikawa
nimekaa nikisubiria hali irejee vyema, na mama Ntilie akaniuliza naendeleaje
nikasema;
‘Mimi
nipo sawa, tuendelee…’nikasema hivyo.
‘Polisi
walikuwa wanataka kuongea na huyu mama, …wanamuhitajia kituoni leo
hii..nilishindwa kuwapa majibu ya haraka …sasa sijui huko kuna nini…’akasema.
‘Tusubirie
ikibidi nitaenda mimi mwenyewe…’akasema huyo mzee
‘Na
hiyo hali , ni nani atakuelewa huko…’akasema mama Ntilie
Na
muda huo ndio huyo mama akazindukana, na akawa anajaribu kuituliza ile hali, kwa
kujinyosha nyosha na kutikisa kichwa, na alipoulizwa hali na kama inawezekana
apelekwe hospitali akasema;
‘Hapana
mimi nipo ok…sijui ni kitu gani kimenipata….ila nataka kuondoka…’akasema
‘Polisi
walipiga simu, walikuwa wanataka kuongea na wewe…’akaambiwa
‘Oh,
basi mimi nakwenda huko huko najua labda ni kuhusu shauri la mwanangu,…’akasema
sasa akitaka kuondoka
‘Lakini
kwa hali hiyo utaweza kwenda huko…?’ akaulizwa
‘Ndio
nitaweza hakuna jinsi, japokuwa, mpaka
sasa sijajua la kufanya ili kwanza atoke,..lakini yeye anahitaji maelezo kujua
ni nini kilimtokea, anasema anahis mimi kama mama au baba tunafahamu tatizo
alilo nalo,…kwani huyo binti aliye naye kamwambia eti sisi wazazi wake
tunahusika,…sasa mimi nitamuambiaje….’akasema mama
‘Mimi
nitamuambia kila kitu….na ni bora nikafungwe mimi mwenyewe…’akasema yule mzee.
‘Usije
kuthibutu kumwambia kitu, mpaka nihakikishe nimeshindwa kumtibia, nina uhakika
tatizo hilo litakwisha, lakini sijajuia ni nani wa kulitatua hilo…’akasema huyo
mama
‘Mama
mimi nina imani litakwisha tu….na kwisha kwake inatokana na nyie
wawili…’nikajikuta nikisema hivyo, na sijui kwanini nilisema hivyo
‘Sawa
nitarudi tuyamalize haya mazungumzo, lakini sio leo tena…’akasema akijiandaa
kuondoka
‘Ngoja
tuongozane…’yule mzee akasema.
‘Na
nani, …hapana, wewe bakia hapa hapa,…’akaambiwa na huyo mama akaondoka
Tuendelee
na kisa chetu
************************
‘Natabakiaje
hapa kwani hapa ni nyumbani kwangu…’akasema yule mzee na kuanza kuondoka
kumfuata mkewe, na sisi tukabakiwa tukiwa na maswali mengi kichwani. Huku mama
Ntilie akisema;
‘Huyu
mzee bado akili haijakaa sawa, na shukuru kuwa hiyo mimba sio ya
kwake….’akasema
‘Hata
kama ingelikuwa ni ya kwake nisngelikubali anihudumie, sitaki kabisa…’nikasema
‘Kwahiyo
sasa hiyo mimba itakuwa ya nani…?’ akaniuliza mama ntilie
‘Kiukweli
mpaka sasa siwezi kujua ni ya nani…na sina haja ya kutaka kujua…’nikasema
‘Kwa
maelezo ya mwanzo ya huyo mama nilijua labda itakuwa ya huyo mzee, lakini sasa
anasema mumewe alianza kuumwa, akawa hana nguvu tena…je alianza kuumwa wakati
umeshafika au kabla…hapo mimi sijaelewa…?’ akauliza.
‘Mimi
sijui, maana ndio nimeanza kuyasikia hayo hapa kwa huyu mama, japokuwa kuna
maelezo yalitolewa awali kuwa huyu baba na kijana wake wanahusika,….lakini haya
ya sasa yanazidi kunichanganya,..ina maana kuna namna nyingine ilifanyika,
….hata sijui tuyaache tu…’nikasema.
‘Namna
nyingine kwa vipi, kuwa ulipandikiza mbegu ..kama ng’ombe hahaha..hapana kati
ya hao wawili kuna mmoja anahusika, sasa baba katoka, kabakia kijana, …haya
jiandae kama ni kijana ..inabidi akuoe, au sio…?’ akauliza
‘Sitaki
na simtaki kabisa…huyo wanaendana na yule binti, rafiki yangu, huoni mpaka
wamefungwa, kumbe walikuwa na jambo lao la pamoja…wanafaana hao…’nikasema
‘Mhhh….hapo
sasa, unalo, huyo mtoto ni wako, na huna jinsi utamzaa, bila ya kujua baba yake
ni nani, lakini mimi nashindwa kuelewa, ilikuwaje, watu waingie ndani usiku,
wakufanyia waliyokufanyia wewe umelala tu kama gogo,…ndio naamini kuwa ni
lazima kulikuwa na mtu wa ndani alikuwa anahusika….umeona eeh…’akasema.
‘Kama
ulivyosikia, wao wanakufanyia madawa unakuwa hujijui,…ndio hivyo ilivyofanyika…,
kiukweli mimi sijui..naona ni mtihani tu umenikuta…’nikasema.
‘Ingelikuwa
ni mimi, ningeliwaganda hao hao, maana sababu kubwa ni wao, lakini utamgandaje
mtu kama huyo, mtu kachanganyikiwa,…maana bado hapo naona hajakaa vyema, akili
bado haijatulia, hata hivyo, wao wanastahiki kubeba gharama zote…ngoja kama
tutaendelea kuwa pamoja nitakusaidia kupambana na hao watu hadi
kieleweke…’akasema.
‘Haina
haja, nilishaamua nitapambana mwenyewe na maisha yangu, nimegundua kuwa ili
nikae salama, basi nitafute njia ya kusimama kwa miguu yangu mwenyewe,…na muhimu
nimeshamkabidhi mwenyezi mungu yote yaliyotoea, mungu…’nikasema.
***********
Ilikuwa
siku nyingine huyo mama alikuja pale tunapofanyia biashara, mumewe hakuwepo,
kwani alipoondoka hapo kwenda polisi na mumewe alimfuata huko, sasa hatukuwa
tumejua ni nini kitokea huko, tukawa na hamasa ya kusikia kutoka kwa huyo mama.
‘Mumeo
yupo wapi…?’ tukamuuliza
‘Hata
sijui huko alipo, siku ile alinifuata huko polisi, hakuwaelewana, ikabidi polisi
wamfukuze, wakijua yeye bado kachanganyikiwa, na nilimuambia wazi atafute
sehemu nyingine ya kuishi hadi hapo matatizo haya yatakapomalizika.
‘Kwahiyo
mama uamuzi wako ni upi…?’ nikamuuliza
‘Nimeshaamua
sirudi nyuma,….hilo hakuna wakunishauri …..nasubiria watoto angu waje,
niwaelezee maamuzi yangu na wao watajua la kufanya, ila, sio wao au wazazi
wangu watakaoweza kulimaliza hili, ni mimi mwenyewe ndiye nitalimaliza…’akasema.
‘Na
vipi kuhusu mtoto…?’ tukamuuliza.
‘Kulikuwa
na makubaliano yafanyike kati ya walioibiwa na hao wezi, yaani yule binti na
mwanangu, tukaishia kulumbana tu…, wao wanataka walipwe kila kitu…, nikawaambia
kulipwa, itachukua muda, na kulipwa ina maana ni mimi sasa nibebe mzigo huo…mimi
nina kosa gani…sitaweza kulipa kwa hivi sasa, na aliyeiba ni huyo binti, mtoto
wangu anasema hakumshauri binti aibe, yeye alimpigia simu kuwa kafanya hivyo,
wakati ameshaiba na kutoroka
‘Aliniambia
mimi nina matatizo, ambayo yeye anajua jinsi gani ya kutibiwa…’akasema kijana
wangu.
‘Matatizo
gani…?’ akaulizwa.
‘Ya
kiafya, nisingelipenda kuyaongelea hapa maana yatanizalilisha….’akasema
‘Utayaongea
tu, maana hapa unatakiwa uongee kila kitu,…sasa kwahiyo wewe ukaenda huko ..kwa
huyo binti?’ akaulizwa.
‘Ndio
nikaenda kama alivyonielekeza….’akasema
‘Ndio
ulipofika akakuambiaje…?’ akaulizwa
‘Akaniambia
kafanya jambo baya sana, hakujua wakati analifanya, kuna kitu kilimsukuma
afanye hivyo, kuna kitu kila siku kilikuwa kikimshawishi afanye hivyo, na ikafikia
hatua kikamuambia haya muda ndio huu fanya, usipofanya sasa hutaweza tena, na
utaendelea kuwa masikini maisha yako yote…akafanya na , sasa kaanza kujuta na
hajui atafanyaje kujirudi na kuliongelea hilo kwa hao aliowafanyia…’akaniambia.
‘Kwahiyo
mpaka unafika kwake ulijkuwa bado hujajua kuwa kaiba…?’ akaulizwa.
‘Kiukweli
mimi nilikuwa bado sijajua hilo, nashangaa watu wanadai kuwa nimeshirikiana
naye, mimi nilikuwa sipo, niliafiri kidogo, niliporudi sijakaa vyema ndio
napata hiyo simu…’akasema.
‘Ulisafiri
kwenda wapi…?’ akaulizwa
‘Kuna
sehemu nilielekezwa kuwa kuna mtaalamu wa kusaidia matatizo yangu ya kiafya
ndio nilisafiri kwenda kwake…’akasema.
‘Ulisafiri
kwenda wapi, maana tunahitajia kuhakiki ukweli wako….?’ Akaulizwa
‘Tanga….’akasema
‘Sasa
ulijua muda gani kuwa huyo mdada kaiba..?’ akaulizwa.
‘Aliniambia
yeye mwenyewe nilipofika, aliniambia alitoroka pale alipokuwa akifanyia kazi, na
pesa nyingi, akiwa na maana atakwenda sehemu azifanyie biashara, akizalisha
atazirejesha kwa wenyewe…’akasema.
‘Nikamwambia
azirejeshe haraka kwa wenyewe….’akasema
‘Akasemaje…?’
akaulizwa na polisi
‘Kaibiwa
zote, walikuja majambazi na bunduki wakamvamia na kumpora kila kitu, nahapo
alipo hana hata pesa ya kula na anaogopa akitoka atakamatwa na polisi…kwahiyo ananiomba
msaada wa pesa, na mimi nikamwambia sina pesa, mwenyewe nahitaji pesa ,wazazi
wangu hawataki kunipa pesa tena…’akasema
‘Kwanini
sasa hukutoa taarifa polisi kwa haraka ulipoonana naye, mpaka tulipoonza
kukufuatilia, na kuwakamata…?’ akaulizwa na polisi.
‘Muda
huo nilikuwa sipo vyema, akili yangu ilishavurugika, nina matatizo yangu, nina
shida zangu, na nilijua anataka kunisaidia kumbe anataka mimi nimsadie…’akasema.
‘Kwasababu
ya madawa ya kulevya au sio…?’ akaulizwa
Hapo
akatulia kimia, na aliposhinikizwa ndio akakubali kuwa alihitajia madawa na
pesa hana, na alihitajia msaada wa huyo binti kwa vile kasema kuna namna ya
kumsaidia hilo tatizo liishe…’akasema.
Alipofikia
hapo ndio mama Ntilie akamuuliza huyo mama.
‘Ina
maana kumbe mtoto wako anatumia madawa ya kulevya…?’
‘Si
ndio nawaambia mume wangu kanifanya kitu kibaya kiasi kwamba nashindwa
kumsamehe,,,’akasema
‘Lakini
sio yeye aliyemfundisha mtoto, au sio…?’ akaulizwa
‘Sio
yeye, na hata yeye alikuwa hajui kuwa mtoto kajiingiza huko…’akasema
‘Sasa
kwanini unamshutumu kwa kuharibika kwa mtoto…?’ tukamuuliza
‘Ni
hivi…..’akatulia akiangalia simu yake kuna ujumbe was auto uliingia, na akajibu
, halafu akasema;
‘Huyo
mwanaume anakuja….’akasema
‘Anakuja
hapa…?’ nikauliza.
‘Ndio
maana alisema tuje kwako tuhakikishe tumeliweka hili jambo vyema, nilimuambia
yeye anshitajika kuhakikisha wewe upo katika hali nzuri, maana wewe kumsamehe
ni pamoja na kukulipa gharama zote, unakumbuka kuna kikao tulifanya nikamuambia
hivyo…’akasema
‘Lakini
mama mimi sihitaji msaada wake…nisingelipenda kumuingiza mtu kwenye haya
matatizo tena…nyie wawili mnatakiwa msameheane kwangu itakuwa ni faraja…’nikasema
‘Hilo
halina hiari….maana yote yalifanyika ndani ya nyumba yangu na waliofanya ni
familia yangu, japokuwa hatuna uhakika ni nani mwenye huo mzigo, lakini wawili
hao watawajibika,...na huyo mwanaume sio mtoto…mtoto aliingizwa bila hata
kujua,…’akasema
‘Kwahiyo
hata wewe hujajua ni nani ambaye tunaweza kusema ndio mwenye mtoto…?’ mama
Ntilia akauliza.
‘Yaani
sio rahisi….maana mume wangu alianza matatizo kabla hata huyu binti
hajafika,….’akasema
‘Kwahiyo
basi itakuwa ni kijana wako…’akaambiwa
‘Mhh…ni
kwa vile sijawahadithia ilivyokuwa baadae….’akasema na kukatisha baada ya
kusikia hodi, tulijua ni wateja, kumbe sio wateja.
Waliofika
walikuwa wale wanunuzi wa kiwanja wakasema ninatakiwa mimi nikafungue akaunti
benki kabla ya kuanza kazi ya malipo, na walisema kwa vile bado wapo kwenye
michakao ya kukusanya pesa, na haijakamilika kwanza, wao wamekuja na kiasi kidogo
tu cha kufungulia akaunti, na malipo kamili yatakuja baadae, mimi nikakualiana
na wao,
Niliondoka
na wao nikaenda kufungua akaunti benki, na wakati nataka kuachana nao , yule
kiongozi akaniuliza
‘Binti,
samahani kwa hili, wewe huna matatizo yoyote…?’ akaniuliza
‘Matatizo
gani…?’ nikamuuliza
‘Huyu
hapa ni mmoja wa wanafunzi wangu, kajaliwa kipaji cha ajabu, anaweza
kukuangalia hivi tu akajua wewe una matatizo, yeye kajua wewe una matatizo
…’akasema
‘Hapana
mimi sina matatizo…’nikasema
Yule
anayeambiwa ana kiaji hicho, akanisogelea na kuniangalia usoni kwa muda halafu
akawa ananitizama taratubu kushuka hadi tumboni halafu akasema;
‘Hiyo
mimba uliyo nayo sio ya kawaida…’akasema
‘Mhh,
kwanini unasema hivyo…?’ nikamuuliza
‘Mimi
sijui, ila nilivyokuona nikahisi kuna uchafu mwilini mwako,…na kwa vile tunajua
wapi ulipotokea maisha yako, na sasa tunagundua haya tukaona tukusaidie tu,
kupambana na hili tatizo, hatuhitaji malipo yoyote, usiwe na shaka na
hilo…’wakasema
‘Mhh..’nikaguna
tu
‘Siku
tukija kukulipa tutakuja tukiwa tumejiandaa, ni kisomo kidogo tu cha kumuomba
mwenyezimungu na mengine tutamuachia yeye, na hili linatakiwa , kabla
hujajifungua…’akasema
‘Lakini
nitajifundua salama…?’ nikauliza
‘Baada
ya maombi hayo, ya kumuomba mwenyezimungu kwa uwezo wake, utajifundua salama
maana hayo waliyokufanyia ni mambo ya kishetani, na shetani hatakiwi awe
mwilini mwa watu, akiwa mwilini atakusumbua sana, na mtoto atakuwa akisumbuliwa
sana,…sasa kabla hujajifungua tutalifukuza hilo shetani mwilini mwako,..’akasema
‘Mimi
hata sijui mnaongea nini…’nikasema
‘Tukija
utajua…’wakasema na kuondoka.
****************.
Siku nyingine wakaja yule mama , sasa akiwa na yule mzee,
nilifurahi kuwaona wakiwa wote sambamba…na mama akaanza moja kwa moja
kuhadithia mambo ya nyumbani kwake ambayo yanamfanya asiweze kumsamehe mume
wake…
‘Nimekuja
naye kaniomba tuje kuyaongea yale tuliyotaka kuyaongea, kwa msemo wake anataka
wewe, ambaye kukosea ujue alichokukosea, na pili, tuone jinsi gani ya
kukusaidia, yeye, kukusaidia…’akasema
‘Sisi
hamu yetu ni kutaka kujua, kama kuna yoyote kati ya hao wawili, yaani mume wako
na kijana ambaye anahusikana na huo ujauzito,..au sio binti…?’ akasema mama
Ntilie.
‘Ni
sawa..mimi sikuona haja ya kuyafanya haya mambo yawe makubwa, yaliyopita
yamepita, …ila nilitaka kujua zaidi kuhusu huyo kijana wako, imekuwaje hadi
kufikia hiyo hali,…?’ nikauliza.
‘Ni
vyema nikaelezea yote kutokea pale nilipoachia, ndio utajua jinsi gani hayo
yaliyotokea yalivyoiathiri familia yangu…na kwa vile yeye mwenyewe karuhus
hilo, basi ngoja niwaelezee tu, na tukitoka hapa kila mtu atajua hamsini
yake..’akasema huyo mama.
‘Tutasameheana
kiukweli…’mimi nikasema na nikijaribu kutabasamu lakini huyo mama hakutoa
tabasamu akasema;
‘Mnajua
mlipokuja nyiee mabinti wawili, yule wa kwanza,ambaye yupo jela kwa hivi sasa
na wewe ndio mliowezesha haya mambo kuanza kuonekana kwa uwazi, mabinti wengine
walifanyiwa mabaya lakini, labda nisema ni kwasababu ya utoto wao, sikuweza
kugundua kinachoendelea, au labda kutokana na mazindiko ya kichawi hata sielewi…’akaanza
kuelezea.
Yule
binti wa kwanza alifanyiwa na kushika mimba, akaja kuitoa hiyo mimba, na ..yaliyotokea
yanajulikana kwa huyu binti, sasa kwa huyu, ndio nikaamua kufanya uchunguzi wakwa
kuweka vifaa maalumu chumbani kwa huyu binti, na lengo langu ilikuwa kubaini
yale niyowahi kusikia , na kwa vile kuna mtu alishaniambia kweli wachawi
wanaweza kuingia usiku usiwaone, lakini yeye ana vifaa vya kuwezesha kuwapiga
picha,au kama picha imepigwa na karibu yake yupo mchawi au shetani anaweza
kuisafisha na kuona kilichojificha.
‘Ndio
nikawekeza hivyo vifaa….’akasema akimuangalia mume wake.
‘Yule
jamaa aliweza kufanya hayo na siku nataka kwenda kuonana naye, akaptawa na
dharura akasafiri, na kabla hajarudi ndio akaja huyo marehemu na maelezo yake
ambayo, tulikuja kuyaamini kuwa huenda ndio sahihi, na kwasababu hiyo
ikanifanya nisihangaike tena na huyo jamaa yangu, na mambo mengi yakawa
yametokea hapa kati kati..kwahiyo hilo likasahaulika.
‘Ina maana mume wako na huyo mtaalamu wako,
ndio waliweka hayo mazindiko aliyokuwa akiyasema yule marehemu…?’ akaulizwa.
‘Ndio,
na hayo ndiyo yalimfanya huyo jamaa yao, kuweza kutuona hata akiwa huko kwake, na
kuweza kuja usiku kwa mbinzu zao za kichawi na kufanya mamboyao bila
kujulikana..na walitafuta sehemu nyingine zaidi, ndio huko kwa wale marafiki
zangu, ..kote huko waliweka ili kila ninapokwenda ijulikane ninafanya nini…’akasema.
‘Mhh…mbona
hatari…’akasema mama Ntilie.
‘Kama nilivyosema awali, nilipogundua hayo, nilitaka
ndoa yetu ivunjwe mara moja, nikahangaika kisheria,lakini wazee wakagoma,
wakanishauri sana, na kunisihi sana, hasa bab yangu mkubwa, wazazi wangu kama
kawaida yao walishasema huo ni mzigi wangu wa kujitakia,..basi nikafuata
ushauri wa baba mkubwa kuwa siwezi kumuacha mume akiwa kwenye hiyo hali
anaumwa, nihangaike naye mpaka apone kwanza,…unajua inauma ikizingatiwa kuwa
alimuingiza hata kijana wangu kwenye
mambo yake ..iliniuma sana…’akasema.
‘Hapo
sasa tuambie kijana wako aliingizwaje…?’ akauliza Mama Ntilie
*************
Kama
nilivyosema awali, mume wangu alikuja kuathirika akawa hana nguvu tena kama
mwanaume na dawa zao za kishirikina zilihitajia hivyo, kufanya uchafu wao kwa
watoto wa watu wasio na hatia, wakihitajia damu..ni mambo ya ajabu kabisa,…basi
mume wangu alipoona hivyo ndio akamuendea huyo mtaalamu wao,huyo mtaalamu wao,
akamwambia;
‘Dozi
ya dawa haikatwishi,..kwahiyo ni lazima kutafutwa namna na namna ni kumtumia
mtoto wako, awe kama wewe, afanye majukumu yako..mume wangu hakukubaliana na
hilo awali, baadae akakubakubali akiwa hajui mtego uliwekwa hapo.
‘Kwahiyo
ili mwanao awe wewe ni lazima afanye kazi zako, kama wewe , kama mume…ashiriki
matendo yote tuliyokuwa tunayafanya, …’akaambiwa.
‘Nini,…hebu
hapo, una maana gani hapo…, matendo yapi maana mnapokuja usiku mimi sijiuu
nimelala..au sio…?’ akauliza.
‘Lakini
nilikuambia tunafanya nini, au sio,…tukifika kwanza ni lazima wewe ufanye mambo
kwa mkeo kupata baraka zake..huku tunashuhudia, ili zindiko lifanye kazi,
ukishamaliza kwa mkeo ndio tunakuchukua hadi kwa mwanawali, na huko tunakwenda
kutafuta damu ya mizimu, ambayo itawafurahisha na kuwezesha kuhamisha nyota ya
utajiri kutoka milki ya vizaz vile na kuhamia kuja hapo kwenu…’akasema.
‘Oh,
hapo..hata sielewi, maana sijawahi kuona ila nahisi kuna kitu kinafanyika..na
bora mfanya hivyo hivyo, nisijue kinachofanyika,…kwani naweza kuchanganyikiwa,
unajua sipendi, ila nafanya hayo kwa ajili ya kutaka huo utajiri, vinginevyo
nisingelifanya,..yule baba mkwe ananikera sana, moyoni mwangu…’akasema.
‘Hapana
ni lazima uelewe kinachofanyika ili ifanikiwe uwe wewe unafanya jambo ambalo
upo huru nalo, hatuna haja ya kukuweka wazi ulione ila kibali chako ndicho
tunakihitajia…’akaambiwa.
‘Ehe
niambie..mimi inakuwaje..maana ndio hivyo, na kama kijana wangu ndio anatakiwa
afanye, tafadhali, naomba asije kujua au kuwa na fununu hiyo….’yeye akaomba
hivyo.
‘Ni
hivyo, kwa vile wewe hufanyi kazi, kijana wako atachukua nafsi yako, atafanya
kazi zako, ina mama , yeye atashiriki na mkeo ili kuipata baraka kama
ulivyokuwa unafanya wewe kabla hatujawaendea hao wanawali….’akasema
‘What!!!..Una
maana gani hapo…ina maana, wewe hapana, huyo ni mtoto haiwezekani…..’mume
alisema kwa ukali
‘Kama
hutaki utajiri basi,..na hilo ni lazima lifanyike kwanza,..huwezi kupata baraka
za huyo mwenye nyota bila ya kuptia kwake, na unapitia kwake kwa njia hiyo, na
unakwenda kwa wanawali kuiongzea nguvu, mizumu inafurahi,…muhimu ni kuwa mkeo hajui,..yanayofanyika nyote hamuyaoni,
wewe na kijana wako mnakuwa kama magogo tu, kinachowasukuma ni mizimu inatembea
na nyie,…tusipoteze muda, maana hapo hakuna kurudi nyuma tena, ukitaka kukatiza
haya mambo kafara lake ni damu ya mtu, ina maana mmoja wenu anakufa..’akasema.
‘Oh,
hapana, sitaki hilo litokee, sitaki mtu afe…’akasema
‘Chagua
unaendelea au unakatiza…ukikatiza kijana wako au mkeo, au hata wewe kesho
unazikwa, na maisha yanaendelea…’akaambiwa,
‘Hapo
umeniweka njia panda…’akasema
‘Kesho
tutakuja kama kawaida na kijana wako atachukuliwa na yeye ataanza kazi zako,na
hakikisha binti mpya analetwa kama kawaida, mtumie huyo kijana wako awe
anawaleta mabinti, usiku watapitiwa na usingizi tutachagua mmojawapo, kazi
inaendelea mpaka tumalize hili zoezi, baada ya hapo nyota inahamia kweko, wewe
utaanza kujaa utajiri, …unaelewa…’akaambiwa.
Jamaa
alivyo mjinga,… hakuwa na jinsi ikabidi akubali hivyo hivyo..bila hata kufiria
athari zake.
‘Sasa
hao mabinti walipatikanaje..?’ akaulizwa na mama Ntilie.
‘Kama
nilivyosema awali mwanzoni alikuwa akichukua wafanyakazi wa ndani, wa muda, leo
huyu anakaa siku mbili tatu, anaondoka kesho mwingine, yeye akijifanya
anawasaidia mabinti wasiojiweza, alikuwa akienda hata vituo vya kulelea
mayatima kule anamchagua yoyote kuwa aje afanye kazi kwa muda…mmi sijui, kwangu
mimi niliona ni jambo la neema kuwasaidia waliopo kwenye mazingira magumu,
kumbe mwenzangu ana ajenda yake ya siri.
‘Sasa
akaja kuongea na kijana wake kuwa afanye paty, awaalike mabinti, ..yeye
alimsisitizia mabinti, na kijana akawa anajiuliza ni kwanini baba anataka jambo
kama hilo, kahisi labda ni kavile baba anataka yeye aoe, kwahiyo kati ya hao
mabinti atamchagulia anayemfaa, kwahiyo yeye akafanya juhudi ya kuwachukua
mabinti wazuri anaowafahamu , akawaalika na mabinti wengi wakakubali …
***************
Siku
hiyo ya kijana kukabidhiwa mikoba ya baba yake ikafika, usiku mabinti
walioalikuwa wakafika,…na hao wachawi wakawa safarini kuja huku,..wanajua
wenyewe walivyosafiri, na mimi nikapangiwa madawa ya kufanyiziwa ili niendelee
kulala kama siku nyingine..ili kijana wangu mwenyewe wa kumzaa aje afanye kazi ya
baba yake,..’ hapo huyo mama akanyamaza kwa muda, akiwa kainamisha kichwa
chini, baadae akainua kichwa huku machozi yanamtoka akasema;
‘Hebu
jamani niambieni hapo hata ingelikuwa wewe unasikia jambo kama hilo limekuja
kufanyika kwako, na anafanyiziwa mtoto wako, utajisikiaje, je utakuwa radhi
kumsamehe mtu kama huyu..?’ akaniuliza
Nilibakia
kimia, sikuweza kutoa jibu,…hapo hapo , akili ilikuwa imganda siamini kuwa ni
kweli…
‘Hebu
niambie kama ni wewe ungelikuwa umefanyiwa wewe hivyo na mumeo, ungelifanyaje,
ungemsamehe tu, yaishe, je una uhakika gani kama hatakuja kurudia tena, je una
uhakika gani kuwa hatafanya mengine makubwa zaidi ya hayo, je utamuelezaje
kijana wako….maana mpaka sasa mtoto wangu ana matatizo makubwa yaliyotokana na
vitendo hivyo..na kisa ni baba yao…
‘Huyu
hapa shetani mkubwa,…’akasema akimnyoshea kidole.
‘Kwahiyo
hebu kwanza hapo, huyo kijana wako kwa hivi sasa ana atatizo gani ni hayo ya
kutumia madawa kama ulivyosema au kuna mengine…?’ nikauliza.
‘Huko
kutumia madawa, imetokana na madhara ya hayo aliyofanyiwa, na alianza kutumia baadae,kwanza
alianza kuvuta sigara, akaja pombe na baadae madawa…nitakuelezea hatua kwa
hatua ili uelewe vyema…..na kukuelezea huko sio kwamba umchukia huyu mtu, …hapana,
ni ili uelewe pia kuwa kijana wangu hana hatia na mambo hayo, hata kama yeye
alikufanyia,..na …’kabla hajamaliza smu ya huyu mama ikaita, akaangalia ujumbe
wa maandishi,
‘Wazazi
wangu wananipigia simu natakiwa nikitoka hapa nikakutane nao, najua moja ya
maswala ya kuongelea ni hili, je nipo tayari kuwa nao, au kuwa na huyo mwanaume…’akasema.
‘Mke
wangu …’mumewe akataka kuongea jambo lakini yeye hakumruhusu akasema;
‘Ulitaka
niyahadithie yote subiria nimalize , nikimaliza hawa ndio watakuhukumu na
hukumu hiyo ni jinsi gani wewe uadhibiwe, na wakati huo huo, wewe ujue jinsi
gani ya kubeba huu mzigo wa huyu binti..na huwezi kujitetea kuwa hutaweza, kazi
bado unayo, hujaachishwa… ila kwangu, sahau….’akasema.
‘Mama…’mimi
nikasema
‘Unataka
niendelee au niache…?’ akaniuliza mimi
‘Endelea….’nikasema
Na huyo mama akaendelea kumalizia sehemu
iliyobakia…
NB:
Tutakuja kuiona sehemu iliyobakia ambayo, ndio iliyomfanya huyo mama akatae
kabisa kurudiana na mumewe.
WAZO LA LEO: Hutaamini kuna watu wamefikia hadi
kuwaumiza watoto wao wa kuzaa, kwa ajili ya kuutafuta utajiri, wanaenda kwa
waganga wanadanganywa wafanye hivi na vile, ..kuna wengine kweli wanaupata,
utajiri wa kishetani, , ikiwa ni mtihani kwao, lakini hebu wachunguze kama wana
raha maisha mwao, watakuwaje na raha wakati wanamuona mtoto wao akiwa hivyo,
zezeta, hajiwezi,, na wachunguzeni kwenye vifo vyao wanakuwaje, maana madhambi
kam hayo adhabu yake huanzia hapa hapa duniani,..…hivi jamani tumefikia hapo…INATISHA!
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment