Mnajua
kuna vitu vingine ukivisikia kwa watu utasema wanazusha, huwezi kuamini, kuwa
binadamu anawezaje kudanganyika na kufanya mambo mabaya bila kufikiria athari
zake baadae, bila kujali familia yake, bila kujali watu wengine, lakini zaidi
bila kujali damu yake mwenyewe ..mimi sikuamini hilo kabla…’akasema huyo mama
Yule
mzee pale akawa kainama huku kashika shavu, akiashiria kuhuzunika sana
Mimi
na mume wangu tulioana bila ridhaa ya wazazi wangu, labda hilo naweza kusema
linaweza kuwa ni sababu sikuwa na radhi ya wazazi wangu,labda,…imefikia kila
likitokea baya wanasema tulikuambia,sasa ubebe mzigo wako mwenyewe, wanadai
walishamchunguza mume wangu na kugundua kuwa hataweza kubadilika, na mimi sasa
nimeliamini hilo…
‘Sio
kweli….’akasema mume wake kwa sauti ya unyonge.
Kumbe
mume wangu baada ya kuona hilo kuwa wazazi wangu hawamtaki, yeye akaenda mbali
zaidi na kufikiria kuwa anafanyiwa hivyo kwa vile anatokea kwenye familia masikini,
kakulia kwenye mazingira ya kimasikini..ndio maana hathaminiki, kwahiyo
alichofanya yeye ni kutafuta njia ya kulipiza kisasi,..nakumbuka siku moja
tulipokwenda kusema sisi tutaoana mume wangu wakati anajibishana na wazee
aliwaambia
‘Wazee
wangu, mimi sikupenda niwe masikini au familia yangu iwe masikini, yote ni
maisha tu, na huwezi kujua, ipo siku naweza kuwa kama nyie, na mkawa
mnanitegemea mimi…’aliwaambia wazee wangu.
‘Sawa
lakini hatutaki wewe umuoe binti yetu, maana wapo wengi tu, unaweza kuwaoa,
mnaoendana nao, sisi tunajiuliza ni kwanini huyu, sisi tuna kujua wewe
vilivyo.., tumepeleleza nyendo za kizazi chako na hata wewe mwenyewe
ulivyokulia, hutaweza kutulia wewe, una tamaa, japokuwa hapo ulipo hauna kitu, ukipata
utabadilika,…sisi ni waze tunajua mengi….’wakasema.
‘Wazee
ipo siku mtanishangaa, ipo siku na mimi nitakuwa kama nyie na nyie mtakuwa
hamna kitu, hilo nawahakikishia,.mimi nawajali na nitawasaidia kama wazazi
wangu….’akasema
‘Utafanyaje
wewe…?’ akaulizwa na wazee wangu
‘Katika
dunia hii hakishindwi kitu ukiwa na nia, mimi nina nia ya kufikia hapo
mlipo, na ipo siku nitafanikiwa tu wazee
wangu, na huwezi jua, ipo siku na nyie mtahitajia uwepo wangu, tuombeeni tu
mungu, ipo siku mtajijutia, na siku ya leo iwepo kama kumbukumbu…’akasema.
‘Kwanini
unasema hivyo…hamna haja ya kubishana na wazazi wangu nimeshakuambia
nitasimamiwa ndoa na baba mkubwa, inatosha, sipendi hayo maongezi yako..?’ mimi
nikamwambi ili tuondoke hapo.
‘Wewe
huoni wanatufanyia hivi kwa vile wao wana utajiri, utajiri wao ni nini si mali
tu, mali si inatafutwa, na sisi tutaitafuta kwa njia yoyote ile,..na huenda
hata hiyo mali yao hawakuipata kwa halali, ngoja na mimi nitaitafuta wewe ngoja
tu…’akasema .
‘Kiukweli
kipindi hicho nilijua kwa vile anasoma , kwa vile ana juhudi ya kutafuta basi
atafanikiwa kwa wivu huo wa maendeleo kumbe mwenzangu alikuwa ana ajenda yake
kichwani, ana wivu wa kishetani, lengo lake ni kujitajirisha kwa haraka, kwa
njia za kishetani..
‘Sijui
alikutana na nani akamdanganya, pamoja na usomi wake wote huo, akakubali
kujiingiza kwenye mambo ya kishirikina, akaenda kwa waganga wa kienyeji, akadanganywa…sijui
elimu yake ilikuwa na maana gani sijui, labda ni kweli kama walivyosema wazazi
wangu….’akasema.
‘Sikutaka
kuyaongea haya tena….maana jinsi ninavyozidi kuyaongea ndivyo hasira zinazidi
kunijaa …nilishaamua basi bora nibakie mwenyewe na hayo yaliyopita yapite tu,….’akaashiria
mikono ya kukata tamaa.
Sasa
kilichofanyika kipindi hicho ni kuwa,Mume wangu akawa ananiaga kuwa anakwenda
safari za kikazi,mikoani, kumbe safari hizo zilikuwa sio za kikazi hasa,
niliulizia kazini kwao, wakasema hawajawahi kumtuma huko kwenye huo mkoa, haya
niliyafanya kabla sijafunuliwa huo ukweli, kumbe yeye alikuwa akienda kwa
mganga mmoja ambaye wanasema anaaminika kwa mambo hayo….’akatulia.
‘Sasa huko
ndio wakamdanganya, kuwa akifanya hiki na kile atafanikwia atakuwa tajiri, kama
wazazi wangu, na zaidi ya wazazi wangu muhimu ajitahidi aibe nyota ya wazazi
wangu,..sasa sijui nyota za mtu zinaibiwaje, …wenyewe wanajua walichokifanya, ila
alitakiwa afanye mambo kadha wa kaadha, kama alivyoelekezwa,..hakuwa peke yake
mwenye ndoto hizo za ajabu, alikuwa na wenzake na wote hao wameishia kubaya
kama alivyoishia huyu mwanaume hapa….’akasema
‘Huyo
mtu waliyemuendea alitaka kuwakomoa, yeye naye alikuwa na visasi vyake akaona
atumie mwanya huo kufanikisha mambo yake, sijui kwanini wanadamu tunachukiana,
wajinga hawa wakaingia kwenye anga za huyo mtu….’akatulia.
‘Aliporudi
nikamuona mwenzangu kabadilika, kipindi hicho sikuwa nafahamu lolote, maana
nishapenda tena, namuamini sana muda huo, haniambi mtu kuhusu yeye, kuna mambo alinifanyia mengi mabaya lakini kwa
muda huo nilikuwa siyaoni, akawa ananitumia kinamna nisiyojua kuiumiza familia
yangu…’akatikisa kichwa kwa kusikitika.
Ni
mambo mengi mabaya ,na sikupenda kuyaongelea,…na mengi aliyanifanyia aliyafanya
nikiwa usingizini, kama alivyoelekezwa, na huyo mtaalamu wao …mimi nikawa
napata shida sana, nikawa naumwa, nasumbuliwa na mambo ya ajabu ajabu, nikaenda
hospitalini, nikapimwa,…nikawa na magonjwa ambayo sikuyaratajia,…nikatibiwa
lakini yakawa yanajirudia rudia….mpaka madocta wakanitilia mashaka…ikafika
sehemu mimi mwenyewe nikawa sipendi kabisa wajibu wangu wa ndoa…’akatikisa
kichwa.
‘Yote
hayo nilifanyiwa ili nyota ya mali ya wazazi wangu ije ihamie kutoka kwenye familia
ya wazazi wangu iende kwa huyu mtu…mimi natumiwa kama chambo…huyu ni mtu kweli
au ni shetani…hivi angelifanyiwa kwa wazazi wake hivyo angelifurahi, na kwanini
ufanye hivyo..ina maana gani ya kwenda shule…’akasema
Jamaa akatikisa
kichwa kusikitika…
Kwa
kipindi hicho nisingeliweza kuyafahamu hayo,..maana huwezi kuamini kuwa mume
wako anaweza kukufanyia mambo kama hayo, baadae akasafiri tena aliporudi, sasa
ikawa kazi ya kuchukua wafanyakazi wa ndani,…alikuwepo mfanyakazi wa ndani hapa
mama mtu mnzima akamfukuza anasema yeye hafai, haendi na wakati kumbe
waligundua kuwa huyo mama akiendelea kuwepo hapo , wao hawataweza kufanya
madawa yao ya uzandiki….’akasema akitikisa kichwa.
‘Yeye
akaanza kuleta dogo dogo, na basi alete wasichana wakubwa, hapana analeta
watoto, vibinti vya watu hata kujielewa bado, …inasikitisha sana nikiwazia
hilo, ina maana hata wazazi wa hao mabinti walikuja kugundua hayo na kuiona
familia yangu ni kichawi..kuna mama mmoja alikuja kwangu akanisuta kweli,
niligombana naye karibu nimfunge jela,..kwa kuniita mimi mchawi, na mume wangu,
nilikuwa sijui hayo..kumbe naishi na shetani ndani ya nyumba…’akasema huyo
mama.
‘Ndugu
zanguni nayasema haya kutoka moyoni mwangu mkitaka kuoa au kuolewa chunguzeni
sana, huyo mtu anapotokea… mkiona mtu anamuelekeo wa mambo ya kishirikina
familia yao ipo hivyo achana naye, wapo wengi wazuri, ukumbuke familia yako
inajengwa kuanzia hapo..kwenye ndoa yako, ukikosea hapo umeharibu kizazi chako,
mshirikina sio mtu kabisa…’akasema.
‘Lakini
mke wangu mimi sio mshirikina ni ibilisi tu alinipitia, na hata wazazi wangu
sikumbuki kama walikuwa na tabia hiyo, hayo mengine walizuliwa tu, sio kweli….’akajitetea.
‘Si
umesema nieleze kila kitu, sasa kwanini walalamika, au niache kuelezea….?’
Akaulizwa
‘Hapana
endelea tatizo unahitimisha kuwa mimi sifai,..mshirikina na tabia hiyo ipo
kwenye damu, hapana hiyo tabia ilikuwa ya kughilibiwa tu, mimi naweza
kubadilika na nakuhakikishia nitabadilika hilo nakuahidi na ikitokea tena
niua,..tuachane kabisa,…’akasema.
‘Mimi
sio muuaji, mimi sina roho mbaya kihivyo, yaliyotokea hadi kuja kuwafukuza hawa
mabinti ni kutokana na wewe…mimi sipo hivyo kabisa, nawapenda wote bila kujali
huyu ni nani, ila sipatani na matendo mabaya hasa ya kishetani, …’akasema huyo
mama.
‘Sawa
endelea mpendwa, samahani kwa kukukatili…..’akasema
‘Kumbe
kuwaleta hao mabinti wadogo ni moja ya masharti waliyopewa na huyo mganga wa
kienyeji, mabinti wadogo ambao hawajaguswa na mwanaume, eti ndio wanaofaa
kwenye hizo dawa zao za kishirikina ambazo eti ndio hizo zitakazowaletea utajiri, ni ujinga,
elimu ndogo ya kufikiri,, na nashukuru sikuwahi kuzaa mabinti maana wangelikuwepo
kwa jinsi nilivyosikia,ungewatumia hao hao…’akamuangalia mume wake kwa hasira..
‘Kwani
walikuwa wakifanyiwa nini …?’ akaulizwa na huyo mama Ntilia.
‘Mambo
mabaya, wanazalilishwa, eti ile damu yao ichukuliwe na hao wachawi,
wakachanganye na makafara yao, ni watu wa ajabu kabisa, ….sasa hebu niambie
huyu sio mwanga mchawi, mimi niishi na mwanaume mchawi, jamani hamnitakii mema
nyie, leo kanifanyia hivyo kesho itakuwaje,….’akatikisa kichwa kukataa.
‘Mke
wangu usiseme hivyo…’akasema mume wake.
‘Wanadai
dawa hizo zilikua zikifanyika kwa awamu ,eti awamu ya kwanza ni kuhamisha nyota
ya wazazi wangu ije kwenye familia yetu, lakini kwanza ipitie kwangu, kama
mrithi,…halafu sasa itoke kwangu iingie kwa huyu mwanaume..mimi hapo ndio
natumika, usiku nafanyiwa mambo mabaya..ni mabaya kweli..sitaki hata kuyasemna.
Sasa
baya zaidi, kwa laana , mwenyezimungu ni mwingi wa rehama akampiga kiboko huyu
mume akashikwa na ugonjwa wa kisukari, si unajua tena kisukari, alikuwa hana
tatizo hilo ghafala akaanza kuhisi hali fulani mwilini, jogoo hawiki, na kazi
anayotakiwa inatakiwa jogoo awike, …kuona hivyo akaingiwa na mashaka, hapo
akaniambia
‘Mkee
wangu, nahisi nina tatizo…’akaniambia
‘Tatizo
gani…?’ nikamuuliza hapo na mimi nilishahangaika na hali yangu mengine nilikuwa
hata simuambii, sikutaka kuyaongea, nimeyaongea baada ya kupata uhakika huo, na
alipotka hapo nje na kumuuliza baadhi ya maswali ambayo bado nilikuwa sia
uhakika nayo, akakiri kuwa ni kweli, basi…nikajua huyu mtuu sio mtu…’akasema.
‘Watu hawa
walifikia kula nyama za wafu..hawa si wanga hawa…, wachawi wakubwa…, mnakula
nyama za watu waliokufa..hahaha, hapana sio mimi, nasema sio mimi..siwezi
kuishi na mchawi ndani ya nyumba yangu…’akasema.
‘Lakini
mke wangu nilidanganywa tu, ndio maana nilikuambia yote hayo,…kama ningelikuwa
mchawi eeh, ningewezaje kukubali hayo, nilidanganywa tu,…ni shetani alinipitia,
nikijua nitakuwa tajiri kama wazazi wako….’akasema .
‘Sasa
tatizo likaanza mwilini mwake, alipoenda kupimwa akaonekana ana kisukari ndio
sababu, jogoo hawezi kuwika hapo jasho likaanza kumtoka maana ili dawa hizo
zifanye kazi anahitajika kuwazalilisha mabinti wa watu wadogo,..na alipewa muda
fulani , baada ya hapo ataanza kuupata utajiri,…sasa tatizo limetokea kabla
hajamaliza hiyo kazi, masharti yakaanza kumshinda…, shetani ana mbinu, lakini
hawajui kuwa mungu yupo, mungu humlinda mja wake, kwa namna ambayo huwezi
kutegemea.
.
‘Kuna
kipindi mama aliniita, akaniambia je kweli nyumbani kwangu kuna
usalama,…nilishangaa mama alijuaje kuwa nipo kwenye matatizo,…mimi kwa
kujivunga nikasema, hakuna kitu kinanisumbua, sikumuelewa kipindi hicho,
nikajua ni zile chuki zao, kumbe wao walishaona,..unajua tena wazee wana njozi
zao, mama akaniambia, huyo mume wako hakufai, uwe makini,..mimi sitaki muachane
naye, ila bidisha ibada na umuombe sana mungu wako akulinde..bila hivyo
mtaangamia, …
‘Kwangu
mimi nikafuata kama alivyoniagiza mama,
na mambo yangu yakaisha na ndio mume akaanza kulalamika kuwa ana matatizo,
..yeye aliporudi kwa huyo mtaalamu wao, akaambiwa kwa hivi sasa hawezi
kumsaidia, ila itakuja kuisha hiyo hali akapewa, dawa, lakini akaambiwa dozi
haitakiwi kukatizwa, kwahiyo inatakiwa kutafutwa njia nyingine mbadala ya
haraka,…’akasema.
‘Njia
gani maana hali yangu ndio hivyo, yaani sina raha…’akasema mume wangu.
‘Kuna njia mbili ya kwanza, ambayo ndio naiona
ni nzuri kwako maana hatutawaruhudu mashetani watusaidie..ni wewe kumtumia mtoto wako badala yako..’akaambiwa
‘Mtoto
wangu, hapana mtaalamu usiingize mtoto wangu kwenye mambo haya…’akalalamika.
‘Ndio
nja rahisi nyingine itakuwa ngumu sana kwako, makafara yake ni mabaya zaidi, na
ukumbuke umeshaanza huwei kuacha, huoni umeshaanza kuneemeka, hali imebadilika
au nadanganya…’akaambiwa
‘Ni
kweli mtaalamu…’akasema
‘Na
kwa mtoto wako ndio itauwa bora zaidi, ..kwasababu ni mtoto wako na mambo kama
tunavyoyafanya kwako, kwani tukifika kwako unatuona, hutuoni, ila tunakuchukua
wewe tunafanya yetu tunaondoka, au sio,…na tutafanya hivyo hivyo kwa mtoto
wako, lakini ni lazima muwe naye sambamba, na ukubali kwa utashi wako,…wewe au
yeye hamuwezi kuona, wakati hayo yanafanyika… inafanyika usiku watu
wamelala,…hata nyie mnakuwa kama magoigoi tu, mnafanyizwa bila kujijua, asubuhi
utaona dalili tu…’akasema.
‘Kwa
vipi sasa…?’ akauliza maana ni kweli hali ya kimaisha ilishaanza kushamiri,
uone mungu anavyo mpima mwanadamu unataka utajiri kwa njia hiyo anakujaribu kwa
kukupa kidogo tu, kupima imani yako…wewe unazidi kusahau, …shetani
anashangilia,…’akatulia.
‘Kama
ilivyokuwa awali,…ina maana sasa mtoto wako ndiye atashika usukani wako, …ila
wewe na yeye mtakuwa pamoja, yeye anatekeleza majukumu wewe unamshikilia mkono
ili iwe kitu kimoja, iwe ni kama wewe unafanya ili kafara likamilike
…’akaambiwa
‘Sawa
kama ni hivyo hakuna shida…’akasema
‘Lakini
ili huo usukani yeye , mtoto wako aweze kuushika ni lazima awe kama wewe, ina
maana ile hali yako inahamia kwa mtoto wako, unanielewa hapo…’akaambiwa
‘Kwa
vipi…sasa hapo…?’ akauliza
‘Ina
mtoto anakuiwa ni wewe, si ndio hivyo..sasa takuwaje ni wewe, ina maana kuna
mambo anatakiwa kuyafanya ili awe ni wewe,…’akaambiwa ..hapa nilichoka, siku
nilipoambiwa hivyo, nilidondoka nikazimia, kwa hilo achilia mbali hayo
yaliyopita, kunizalilisha nikiwa nimelala, kula nyama za wafu, lakini hili,
haniambii mtu hapa, sitaki sitaki, ni bora niishe bila ndoa, sitaki….’akasema
na akawa kama anajisikia vibaya.
‘Vipi
…huwezi kuendelea?’ akaulizwa na mama Ntilie.
Huyo
mama alibakia vile vile ..huku anatikisika kwa hasira…, kumbe alikuwa analia,
alipoinua kichwa, usoni kulijaa machozi.
‘Niacheni
jamani, siwezi,…nimesema siwezi, kama ndoa ndio hivi sitaweza, wazee wamenishi
sana, lakini hapana,.. sitamki huyu mtu tena nyumbani kwangu….’akasimama
akitaka kuondoka
‘Lakini
ulishanisamehe….’akalalamika
‘Kukusamehe
sawa nimekusamehe, hilo halina shaka, lakini sio kwa wewe kuwa mume wangu tena, tutafanya
taratibu za kuachana, na nitakupa kila ukitakacho, ukitaka nyumba, nitakupa,
lakini wewe ….hapana….’akasema
‘Mama
mbona unaniacha njia panda, nimesikia yote hayo, najua ni makosa makubwa sana,
lakini yanaweza kusameheka,..’nikasema
‘Hujasikia
hilo kubwa lao,hujasikia walivyokuwa wakija kwako usiku, walivyokuwa wakikufanyia…..hapana…ndio
utaona kuwa huyu sio mtu wa kuishi naye…’akasema
‘Lakini
nakumbuka yule marehemu alisema…hawa walikuwa wanafanyiwa na wachawi, na sio
kwa dhamira yao…’nikasema.
‘Hivyo
ndivyo walipanga , huyo mtaalamu aliwaambia najua jinsi gani y akutuweka sawa,
ukumbuke zile nyumba tatu, yaani ya kwangu na marafiki zangu wawli zilifanywa
ndio makao ya watu hao kukutana, na walishahisi kuwa wamegundulikana, kwahiyo ili
wajilinde wakabuni uwongo huo, ….’akasema.
‘Mungu
wangu ni kweli baba…?’ nikamuuliza.
‘ Ni
kweli ndio maana nilitaka yeye aongee ili ….muone kuwa nimekosa na nimetubu
madhambi hayo yote , sitarudia tena…’akasema.
‘Sasa
wakati tunahangaika kumbe ulikuwa ukitusanifu baba, kwanini ulifanya
hivyo….’nikasema.
‘Ni
shetani tu,..nilitaka niwe tajiri kama wazazi wake mke wangu ili
nisisanifike…na sijui kwanini akili yangu ilikuwa haiwezi kutafakari, kumbe
yote yalikuwa ni viini macho huyo mjaa alikuwa akitutumia kwa masilahi
yake…’akasema .
‘ Ni
nani huyo…?’ nikauliza
‘Ni
marehemu…’akasema
‘Ina
maana kumbe ni yule yule aliyekuja kutuambia kuwa yeye atatusaidia, ….oh, sasa
yule rafiki yangu alihusikinaje , mbona alimtumia yeye…?’ nikauliza
‘Yule
ni binti wa adui yake mkubwa,…na binti huyo aliamua kutoroka kwao baada ya
kugundua kuwa baba yake huyo ana tabia hizo chafu, na hapo hapo, alitakiwa
kuolewa na huyu marehemu ambaye ndiye alikuwa mganga wa huyu mwanaume hapa,
umenielewa hapo,..…lakini hakutakiwa kumuambia mtu yoyote yule…, akisema tu,
atadhurika, kwa imani zao, ndio maana hata siku moja hataweza kukubali
hilo…’akaambiwa
‘Ina
maana anayajua yote hayo, kuwa…..’nikauliza
‘Hajui..haya
ya kuwa mume wangu anahusika, hajui kabisa, haya tumekuja kuyafahamu kipindi
hiki mume wangu alivyoanza kuchanganyikiwa, mume wangu alianza kutuelezea yote
huku akiomba msamaha akijua sasa anakufa, kwa jinsi alivyokuwa akiteseka…, na
tulijua anatania, labda ni kwa vile kachanganyikiwa, lakini nilipofika hapa leo
, akiwa na akili yake vyema, kumuuliza
akasema yote aliyotuambia na kuniambia mimi mwenyewe yalikuwa ni yya
kweli…kwakweli nilichoka, ndio maana nilibakia nje nikilia, …’akasema.
‘Sasa
mama ina maana huwezi kumsamehe kwa hayo,..je ukifanya hivyo mimi nifanyeje…najua
kakosea hata hivyo ili ajirudi na kujisikia kasamehewa, kiukweli, ni wewe
kumkubali na mrejeee kwenye maisha yenu ya kawaida, na najua hatarudia tena,
mimi nipo tayari kumsamehe, na nimeshamsamehe , na sina kinyongo naye japokuwa
inauma sana na sasa kuna uhakika labda hii mimba haina uhusiani na yeye au
shetani….’nikasema.
‘Hapana,
kumsamehe sawa,… sio shida, maana yaliyofanyika yamefanyika, mimi
nimeshamsamehe, lakini kutokana na hayo aliyokuja kumfanyia mtoto wangu,
..siwezi kumrejea, nitasemaje kwa mtoto wangu, nitamuangaliaje mtoto
wangu…mtoto wangu sasa hivi anaozea jela, mimi nikae na mtoto niamuambie
nilimsamehe baba yako kwa hayo aliyosababisha hadi upo hivyo….nitakuwa na akili
kweli…’akasema.
‘Lakini
mtoto si hajui hayo..?’ nikamuuliza.
‘Nitakuelezea
sehemu nyingine ndio utagundua ukweli wa chuki yangu, na nikimaliza
tutaagana,..maana inaumiza sana…’akasema.
‘Tumalizie
basi mama….lakini umsamehe tu …au sio mama.’nikasema nikiwa na hamasa ya
kusikia zaidi, lakini pale nilipo moyo wangu ulishaanza kudunda, sikuamini hayo,
ina maana basi huyu mtoto anaweza kuwa ni mtoto wa huyo mtoto wake,…niligeuka
na kumuangalia yule mbaba, alikuwa kainama, kama analia,..lakini kuna kitu
kilianza kunijaa, kama hasira, kwanini huyu mtu akafanya hivyo, kwanini…nilijaribu
kujizuia, lakini ...
‘Mke
wangu kama hutanisamehe, …kama ulikuwa unanidanganya, kama..basi mimi sina
maana ni bora nirejee kwenye huo ukichaa, au nikajinyonge tu…wewe unajua
sikufanya makusudi , wewe unajua yote nilikuwa nataka niwe kama wazazi wako ili
wasitunyanyase, niliyafanya kwa ajili yetu,…ndio nilikosea, na…yule marehemu
alinitega mpaka nikaweza kumweka mtoto wetu, iliniuma hata mimi….nakuomba nipo
chini ya miguu yako…’akasma sasa akimuendea mkewe,
Mkewe
akamkwepa na akawa kama anamsukuma ili asimsogelee..jamaa akazidi
kumuendea..niliona huyu mama akishika kichwa nahis alikuwa ana maumivu ya
kichwa, au…
Mara
yule mama akawa anayumba …mimi nilikuwa karibu yake nikamdaka, kabla
hajadondoka chini, na wakati huo mimi
nikawa sijihisi vizuri, sijui ni kwanini, nikahisi ghafla giza likitanda usoni,
mimi na huyo mama sote tukaserereka na kudondoka sakafuni…na jamaa alipoona
hivyo haraka akasimama na kumsogelea mke wake.
Na
muda huo huo simu ya huyo mama ikawa inaita, nani ataipokea wakati mama
hajiwezi, na mama Ntilia akaichukua na kusikiliza
‘Halloh
nani mwenzangu, eeh,…. polisi… ……mimi sio mwenye simu…..’
NB:
Ngoja niishie hapa kwa muda, tutaendelea baadae, maana inauma,..binadamu sio
wazuri, kwanini..
WAZO
LA LEO: Jinsi utandawazi unavyozidi na kuwa huru zaidi, ndivyo mwanadamu anavyozidi kutakabari, sasa ivi Mwanadamu kafikia hatua mbaya sana, anafanya mambo ambayo hata shetani atakuja
kutushangaa, yanayotendeka kwa hivi sasa ni ya aibu na yamezidi hata hayo
tuliyowahi kusimuliwa kwenye vitabu vitakatifu, watu wanafanya mambo zaidi ya
mnyama, jamani, jamani tunatafuta nini, wakati dunia hii ni ya kupita tu, wangapi
wangapi walikuwepo sasa hawapo, ina maana wao hawakutaj kuishi…tujirudi jamani,
tuache, tutubu, turejee kwenye njia sahihi.
Tumuombe mola wetu atulindie vizazi vyetu na atuwezeshe
kuyashinda majaribu haya yanayotuzunguka kwa sasa, vijana wetu wanakulia kwenye
mitihani mikubwa bila ya msaada wa mola wetu hawataweza. Ewe mola wetu tusaidie
na utuongoze kwenye njia sahihi…..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment