Mume wangu nilimpenda sana,…utaniuliza kwanini natumia neno
‘nilimpenda,..kwanini sasa nashindwa ‘Ninampenda…’…sijasema simpendi, lakini
kama binadamu kuna matendo ambayo yakitokea ukayashuhudia hata kama ulikuwa na
moyo wa chuma, utabadilika tu…yanaumiza na kutesa sana, na baya zaidi ni pale
unapomuuliza mwenzako, akakataa, na hata kukufanya wewe umechanganyikiwa.
‘Sijasema hivyo, ni wewe tu mke wangu…’mume akasema lakini
mke hakutaka kubishana naye akaendelea kuongea.
‘Wazee wangu ,…sijui niseme nini, najua mungu anajua
kilichopo moyoni mwanagu na machungu ninayoyapitia, maana mwanzoni nilipoona
hayo kwa macho yangu, niliumia sana, ikafika
muda nikasema basi labda,..labda,..nisamehe tu, na nikajitahidi kufany ahivyo…,
japokuwa moyoni nilikuwa naumia, lakini ilipojirudia tena na tena, nikasema
sasa basi, kama mimi nina moyo wa chuma basi chuma hicho kimeshashika kutu….mimi
siwezi tena kuvumilia…’akasema.
‘Mume wangu nampenda sana haya yeye, analifahamu hilo…’
akatulia pale mume wake aliposema
‘Hata mimi nakupenda sana ni wewe….’akasema na kutilia.
‘Kumpenda kwangu huko kulinifanya nikosane na wazazi wangu,
hadi hii leo, ni wao kwa tatazo kama hili wangelifika hapa kunisaidia, lakini
wapo wapi, huko walipo wakisikia haya, watasema, ‘’tulikuambia,..’ lakini
ningefanyaje, na ili hali mtu nilishampenda. Namshukuru sana baba yangu huyu mkubwa,
alinielewa, na mpaka sasa ananilewa..yeye ndiye aliyesimamia ndoa yangu, baada
ya wazazi wangu kunisusia.
Pamoja na yote,
wazazi ni wazazi tu, wao walitupatia hii nyumba, na uone ajabu baba
aliindikisha kwa sote wawili, ndio maana mwenzangu nikimtishia kumfukuza,
ananijibu kwa jeuri kuwa nyumba hii ni yetu sote, lakini anasahau kuwa nyumba
hii ilitolewa na wazazi wangu, na wao wanaweza kumuondoa yeye, kama…haya watakuja
kuyafahamu, hilo halijui…sawa kisheria ipo hivyo, nyumba imeandikishwa kwa sote
wawili, lakini sheria nayo inaangalia sheria
za ndoa, huwezi ukavunja sheria za ndoa, na sheria ikakubeba tu….’akasema.
‘Lakini nani kavunja sheriza ndoa mke wangu…?’ akauliza na
mkuu wa dini akasema;
‘Usimuingilie muache aongee….’akasema.
‘Samahani wazee, haya ngoja tumsikilize…’akasema.
‘Najua baada ya haya
yote, anajua nitamfukuza humu ndani…, lakini hata hivyo, ni nani angeliweza
kuyavumilia hayo yote… natamani nisiyaongee maana kuyaongea zaidi ndio nazidi
kujiumiza, lakini kwanini niendelee kunyamza wakati mwenzangu ananiona mimi ni
ninaota tu, eti naota, sio kweli…hivi kweli mimi nimzushie uwongo mtu niliyempenda
ikafikia hadi nitengane na familia yangu, kwanini nifanye hivyo…’akasema na
kutulia kidogo.
Mwenzangu amesahau tulipotoka, amesahau, nilivyojitolea kwa
ajili yake, nilifikia hadi kuiba pesa kwa wazazi wangu au kudanganya, ili tu
nimpatie ada aendelee kusoma, na hata alipofika chuo kikuu, tukiwa pamoja naye,
alikuwa hana mbele wala nyuma, mimi
nilikuwa namfadhili, aseme ukweli wake kama sikutafanya hayo kwa ajili ya
upendo wetu, leo hii kafanikiwa, maana hana tatizo, tena, ana kazi nzuri,
kipato kizuri, na nasikia kaanza kujenga nyumba yake, haniambii, nasikia kwa
watu tu, mimi siwezi kumuingili huko.
‘Hilo nalo jipya….’akasema mume wake, na alipokumbuka kuwa
kaambiwa asiingilie akatulia kwa haraka.
‘Hayo sio muhimu sana kwa leo, maana anaweza kusema hayo
yliyokuwa ya kale, zilipendwa, sasa umezeeka, nataka damu mpya, kwasababu mume
hazeeki, sawa, ..ni kweli mimi nimezeeka, hayo ya mapenzi ya ujana mimi sina
tena, sina …nasema kweli sina..na sitaki tena kuendekeza mambo hayo.., ndio
maana nilimpa uhuru wa kufanya pendavyo, lakini sio ndani ya nyumba yangu…’akatulia
Hayo nilimuambia mapema tu, akasema mimi mzushi,
…nikamwambia ipo siku nitakuthibitishia hilo, na kweli nikaja kuyaona , sasa
ndani ya nyumba yangu mwenyewe, kaamua kunikomoa …hivi kweli mimi ni binadamu
gani wa kuvumilia haya, na bado namuuliza hataki kusema ukweli, nitamsaidiaje
mtu kama huyu…’akawa kama anauliza
‘Haya basi kama kaona mimi simtoshelezi, kama kaona
anahitajia damu changa, basi aniambie tu…mimi nitamsaidia hata kumtafutia mke mwenza
anayefaa, sio kutembea na wafanyakazi wa ndani,…’akatulia pale mume wake
alipotaka kuingilia . Mume akatulia hakusema neno.
‘Mimi naweza kukubali aoe tu…lakini iwe kwa utaratibu mnzuri
na makubaliano…, yeye akasema hayo najitungia tu mimi mwenyewe kwa vile
simtaki, kwa vile nataka yeye aondoke kwenye hii nyumba, kwanini kila kitu
anarefaa kwenye hii nyumba, hii nyumba ni nini jamani...’akasema akionyesha
nyumba.
‘Siyasemi haya kwa
kujionyesha kuwa sisi tupoje, labda nafanya makosa kutoa siri hizo, lakini sasa
nifanyeje, ni lazima niwaambie nyie wazazi wangu ili mfahamu hiki kinachoendelea
humu ndani, ili muone je hii ndoa kweli
ipo au ni geresha tu…’akawaangalia wazee wake.
‘Huyu mume wangu nilimpenda sana, nay eye alionyesha kuwa ananipenda
kwa vile, sasa naanza kufahamu ni kwa vile alihitajia kitu, na sasa kakipata, …sasa
sina thamani tena kwake, naomba mnisaidia sana, kwa hili, labda mimi nimkosaji,
kama nimekosea, basi mje mniambie, lakini hapa ilipofikia, siwezi kuvumilia
tena…’akatulia
‘Mke wangu jamani..usiseme hivyo….’mume mtu akasema kwa
sauti ya huruma.
‘Sisemi hivi kwa vile utasema mimi najivunia wazazi wenye
uwezo, hapana, mimi sasa hivi sitegemei wazazi wangu, nilishajitoa kwao, na
nilishajipanga kuishi maisha yangu bila kuwategemea wao, na ndio maana pale
tulipopewa hii nyumba nilikataa,….unakumbuka mimi nilikuambie tutafute chetu,
tuanzie nyumba ya kupanga, wewe ukanishauri nikubali tu, mpaka hapo
tutakapojenga nyumba yetu, sasa…kipowapi,….’akageuka kumuangalia mume wake.
‘Ongea tu, ongea kila kitu, ila mimi nataka ushahidi, maana
umeamua kunivua nguo mbele ya watu, haya endelea….’akasema mume wake kwa sauti
ya huzuni.
‘Ni mimi nakuvua nguo au ni wewe umejivua nguo mwenyewe kwa
tamaa zako za mwili, umejishushia hadi wewe mwenyewe japokuwa hutaki kuukubali
ukweli….’ akauliza
‘Samahani wazee wangu, ngoja nimuulize swali…?’ akasema na
wazee wakakaa kimia tu, nay eye akasema.
‘Mke wangu wewe unasema niimejitakia kwa vipi fafanua hapo
ili na mimi nielewe,…wewe unazunguka, unaelezea mengi ya zamani, nia yako ni
nini,kuwa mimi nilikuwa mtoto wa mitaani, ukanisaidia, na kufikia hapa, au sio,
sawa ni kweli, nakubali hilo, na nakushuruku sana, lakini hili la kuniambia
mimi nakusaliti, siwezi kulivumilia, niambie wapi , na nani nilifanya naye
hivyo…, hilo tu…tusizunguke saana…’akasema.
‘Huko nitafika, maana hata mimi nashangaa baada ya kuongea
na wewe na kukuelezea kuwa ninao ushahidi bado huamini, bado unaniona
nakusingizia, hapo natilia mashaka,…wewe una tatizo, haupo sawa, sio yule mume
niliyemfahamu kabla… ningekuwa mshirikina ningelisema wewe kuna kitu
wamekuwekea, lakini mimi sio mshikirina na siamini mambo hayo, huo ni
ulimbukeni wako tu…’akasema.
‘Sawa..sasa si useme,…unaogopa nini…unajua mke wangu kwanini
hujiulizi, kwanini mimi nijiamini kiasi hicho, ..utakuja kuumbuka mwenyewe, …nakuatahdharisha
mapema..’akasema.
‘Nitasema, leo nitasema kila kitu, na ..ushahidi ukitaka
nitauonyesha, kama upo tayari wazazi hawa wauone uchafu wako mimi nitauonyesha,
kwasababu mimi nilishauona, unatia kinyaaa…sasa sijui baada ya hilo utakwenda
wapi, utaficha wapi hayo macho yako yenye aibu, nakuonea huruma jinsi gani
utateseka…’akasema.
‘Hahaha, mimi au wewe…wewe ndio utaumbuka, kwa kuwapotezea
hawa wazee muda wao,..maana sijafanya kitu jamani, wewe unakisia tu,…kama kweli
huo mkanda wa video ulichukua hali halisi iliyokuwepo,…kuwa mimi nilikwenda mle
ndani kuhakiki…maan nina haki, kelele zilisikika na mimi nakaenda kuhakiki,
..hao ni watoto wangu, …haya onyesha, labda uwe umetengenezwa huko mitaani…’
akasema kwa kujiamini.
‘Mume wangu nakuomba tena utubu madhambi yako, tuone ni nini
cha kufanya, nakuuliza tena mbeel ya hawa wazee je hukufanya hayo madhambi…?’
akaulizwa.
‘Sijafanya ndio maana mpaka sasa naendelea kupinga, mimi sijafanya
hayo madhambi unayoyasema wewe, huo uwongo na uzushi…kama ni kweli toa huo
ushahidi wako..’akasema.
‘Kwanza, kabla sijaendelea na hilo, niwaulize nyie wazee, na
kiongozi wetu wa imani, je nikifanya hivyo nitakuwa nimekosea…?’ akauliza mama
mwenye nyumba.
‘Ukifanya vipi..?’ akauliza kiongozi wa dini.
‘Nikitoa huo ushahidi unaonyesha ukweli wa haya yote, maana
unaonyesha matendo yasiyofaa, kwa mume kama huyu , mzee kama huyu,..…maana sio
mnzuri kuangalia, na ..sikupenda iwe hivyo, kama angelikubaliana na mimi, basi
ningeona jinsi gani nyingine ya kufanya, ili ajifunze, na dunia ingemfunza tu…’akasema.
‘Kwanini unazunguka kwanini mpaka uwaulize hao wazee kuwa
utoe au la…wa kuulizwa ni mimi, kama ni aibu si zangu mimi au sio..,..nimeshakuambia
mimi nipo tayari, kuuona na kuwasikia hao mashahidi wako, waite mmoja mmoja
waseme ukweli hapa mbele ya wazee, kama kweli watasema ukweli, lakini kama ni
wao ni waongo, haya tutawasikia…’akasema.
‘Mhh…haya, kwanza nimuulize huyu binti ambaye yupo hapa,
asema ukweli wake, yaliyotokea humu ndani, je ni kweli hajawahi kufanyiwa mambo
yasiyo faa, maana nisiende mbali, wewe binti, unamuogopa mungu wako,niambie
ukweli kinachoendelea humu ndani..na ukumbuke, kama utaficha na ikatokea
tatizo, ujue mimi sitakuwa nawe tena,….’akasema akimuangalia huyo binti.
‘Je ulishawahi kufanyiwa matendo yasiyofaa..?’ nikaulizwa ,
nilitarajia hivyo, lakini hapo akawa kaniwahi , bila kujiandaa, hapo nikajikuta
natokwa na jasho jingi mwilini nikakaa kimia kwanza na yaliyokuja kichwani ni
yale maneno ya kijana ya kunitahdharisha nisije kuvunja ndoa ya watu.
‘Binti hebu ongea ukweli, usiogope..’akasema mzee
‘Mhh..hapana mimi sipo tayari kuongea lolote, nahitajia muda
hivyo..’nikasema.
‘Kwanini..unahitajia muda gani, wa kusema ukweli, sema
ukweli kilichokutokea, unaogopa kusema ukweli, au unamuogopa baba mwenye
nyumba..?’ nikaulizwa.
‘Kwasababu yote nayaona kama ndoto, sina uhakika…na naogopa
kuja kusema uwongo, kumbe ni ndoto tu, mimi sijui, ..’nikasema.
‘Kwani hiyo ndoto ilitokeaje..?’ nikaulizwa
‘Kiukweli tangu nifike hapa nyumbani nimekuwa nikitokewa na
vitu vya kutisha…’nikasema
‘Ukitokewa kwa vipi..?’ akaulizwa.
‘Huwa naota ndoto za kukabwa, na….’hapo nikasita kuendelea
kuongea kwa kuogopa kuelezea mambo kama hayo mbele ya watu wazima.
‘Mnasikia, anafanya nini..anaota, ndoto zinatokea wapi…jamani
tusaidianeni hili ndoto hutokea kichwani akilini, sio matendo…..’akasema baba
mwenye nyumba.
‘Tulia,….’akasema kiongozi wa dini
‘Ongea ukweli, sisi tunataka kusaidia hili jambo…tumekupa
nafasi hiyo, usiogope kutuvunjia wazee heshima kwa maneno yasiyofaa kuongelewa,…nia
hapa ni kuwasaidia hawa wana ndoa wawili na nyie pia…, hatutakubali ndoa hii ivunjike,
tunajua jinsi gani ya kuliweka hili jambo sawa sawa, nimegundua kitu hapa,
lakini siwezi kukisema mpaka nipate maelezo zaidi yenye uhakika….’akasema mkuu
wa dini.
‘Mimi kwakweli nashindwa kuongea maana naota tu, kuna vitu
vinanikaba, mwili unaisha nguvu kabisa siwezi hata kugeuka, siwezi kufanya
lolote ….ni majinamizi sijui….nahisi kama kuna mtu ananishika kwa nguvu, ananikaba,
nakosa pumzi, hata kupiga kelele siwezi, nalegea mwili mnzima, nahangaika wee,
na ..inafikia sehemu nahisi kama nazalilishwa,..nafanyiwa vitendo
vibaya…’nikasema
‘Unazalilishwa kwa vipi, usiogope kufafanua …?’ akaulizwa
‘Nafanyiwa vitendo vibaya,…’akasema
‘Na nani…?’ akaulizwa
‘Simjui , maana simuoni, nahisi tu, sioni kitu, nahisi
kwenye njozi tu….’akasema
‘Je kwa hali kama hiyo ya kuzalilishwa, ukiamuka unajiona
kweli umefanyiwa vitendo kama hivyo..?’ akaulizwa
‘Aaah…,mimi siwezi kujua, maana ni vitu nimekuja kuvionea
huku,…na sijui una maana gani kwenye hilo swali,…, na wala sijui nijibuje..…naona
kama ndoto tu ndicho ninachoweza kukisema, lakini nateseka, sijui
kwakweli…’akasema.
‘Imetokea hivyo mara ngapi..?’ nikaulizwa
‘Kwa kuzalilishwa, mmh, mara nyingi tu, sijaweza kupata
amani labda nikiwa kwenye siku zangu, mara nyingine naweza kukabwa tu, nikasumbuliwa
wee, aah, hata sielewi ni kitu gani na kinataka nini .…’akasema
‘Na ndio maana yule binti wa kwanza, ilimtokea hivyo mpaka akapata
mimba, huyu mume wangu mwenyewe akamsaidia kuitoa, anabisha na hilo…’akasema
mama mwenye nyumba.
‘Nani..mimi, wewe….hebu sema ukweli hapo…wewe mwenyewe
unajua ni kwanini tulifanya hivyo, na wewe ndiye ulinishauri tufanye hivyo….,
kama ningelikuwa na nia mbaya kwanini nikakushirikisha..?’ akauliza baba mwenye
nyumba kama anashtuka!
‘Ulinishirikisha kwa vile alishaamua kuja kuniambia ukweli,
ukaona ili ujikoshe, uje kuniambia kuwa mumesingiziwa wewe na mtoto wangu,
nikaona sasa hayo yatakuwa makubwa, na sifa ya familia yetu itaharibika, ndio
maana nilikukubalia ombi lako…’akasema mke wake
‘Mke wangu, mke wangu, ombi langu au ombi letu,..usikwepe
hapo kabisa, umeamua kulisema hilo , basi liseme vyema, wewe ndiye ulipendekeza
hilo la kutoa mimba, kweli si kweli, tutakubaliana tufanye hivyo, kweli si
ikweli, sasa unajifanya kuogopa kusema ukweli eeh, sema ukweli wako, unaogopa
nini sasa, muone jinsi mke wangu alivyo…’akasema.
‘Ninajua ni wewe uliyempa mimba binti wa watu, kwasababu
nilikupenda, nikaona tuhakikishe hilo jambo halisambai, na wewe ukaniahidi kuwa
utajitunza, ukasema kama ni kweli hutarudia tena…’akasema mke wake.
‘Wewe mwanamke sema ukweli wote, mimi nilikuambia kama ni
kweli,…nilitamka hivyo,…mimi nilikuambia sio mimi, na kama ni kijana wetu basi
amuoe, wewe ukasema kijana wetu hawezi kumuoa mtu kama huyo, kweli si kweli…na kijana wetu kuna kipindi
alikuwa hana raha, tulipomuhoji alionekana kuwa na mashaka, tukahisi ndio yeye
kafanya hivyo, ndio maana tukakubaliana na hilo..inatakiwa hapa useme ukweli
wote, muogope sana mungu kwa kuzua uwongo....’akasema mumewe.
‘Wewe ndio umuogope mungu wako, hutaki kuukubali ukweli
ukasaidiwa…wewe una tatizo, mume wangu wewe una tatizo, kwanini usikubali
ukasaidiwa,…mimi nahsi kuna kitu kimekutokea, sio bure…’akasema
‘Hahaha, huna jipya wewe…mimi ndio mwenye tatizo au ni wewe…wewe
una tatizo, unaingiwa na akili ya kuzua mambo, unahitajia kusaidiwa, ….na kauli
yako hiyo naona inaanza kukugeuza mtizamo wako, wa kuamini mambo kishirikina,…umempata
wapi mganga wa kukudanganya, ?’ akauliza
‘Mimi naona tunapoteza muda hapa…’akasema mkewe.
‘Wewe ndio unapoteza muda, na nakuambia sasa, mimi leo hatumalizi hiki kikao mpaka uutoe huo
ushahidi wako unaosema unao,…nimechoka kuzalilishwa na kauli zako zisizo na
ukweli, …’akasema.
‘Ushahidi si ndio huo kwanza kwa huyu binti anapatwa na kitu
gani, …na ni nani anamfanyia hivyo,na sisi tupo humu ndani wa ngapi…?’ akauliza.
‘Kwahiyo na hili pia, unataka kumsingizia hata mwanao au
sio,..?’ akauliza.
‘Sijamsingizia mtoto wangu, na kama na yeye anafanya hivyo,
ni wewe umemfundisha, maana alishaniambia…yanaoyoendelea humu, ila anakutetea,
sasa umemsikia huyu binti alivyosema, kuna mtu anamkaba usiku, na kitendo hicho
kinafanyika lakini anashindwa kujigeuza,…au kuona kuwa ni nani, sasa ni nani
angeliingia humu ndani na kufanya hivyo, wakati tumefunga mlango, ni nani kama
sio wewe…?’ akaulizwa.
‘Na mwanangu sio..?’ akauliza
‘Sijamsema mtoto wangu maana hata ushahidi huu nilio nao,
unakuonyesha wewe peke yako, ukiwa na huyo binti…..’akatoa kanda ya video
kwenye mfuko.
‘Unakuonyesha wewe….ukiwa na yule binti aliyeondoka mkifanya
uchafu wenu,…si unataka tuuonyeshe huo uchafu wako mbele ya wazazi,..na
utaabika kweli ukionekana…’akasema na hapo mumewe akabakia kimia akikodoa macho
kuaangalia huo mkanda.
‘Wewe mwanamke umefikia hapo..umeupatia wapi huo mkanda?’
akauliza
‘Kufanya nini, si unataka ushahid wa video, wewe ulifikiria
natania, sasa mkanda ni huu hapa, nionyeshe wauone wazazi wako…?’ akaulizwa
‘Kwanini nilikuambia unionyeshe huo ushahidi awali, ukakataa,
..sasa unautoa mbele za watu…’akasema mme mtu sasa akionyesha mashaka.
‘Swali je ni kweli ulifanya..?’ akaulizwa
‘Sijafanya..sio kweli na huo mkanda kama ni kweli utakuwa umeutengeneza
huko na hao watu wako,…mimi nayafahamu hayo sana..siku hizi vitu kama hivyo
vinafanyika…ila mimi bado nasema sio kweli, …kama ulichukua matendo halisi,
basi hakuna cha maana kitakachoonyeshwa, mimi sijafanya madhambi hayo..’akasema,
lakini sasa sauti ilikuwa sio ya kujiamini kama awali.
‘Nakuuliza tena mume wangu ..nakupenda sana, kwani hayo yatakayotokea baadae hutaaamini, baada
ya hili, basi tena, …maana ni aibu kuonyesha mbele ya wazazi hawa, kitu kama
hicho…na mimi sitakuwa radhi kuendelea kuishi na wewe…’akasema.
‘Kwanini unanitisha maswala ya kuachana…, kwanini hutaki
kuutoa huo ushahidi, huyu binti hapa ulisema ni shahidi yako kakataa, kasema ni
ndoto tu, sasa hebu niambie ninaingiaje kwenye huo ubongo wake,…akilini mwake…
na kuyafanya hayo anayosema anayaota, au unanishuku mimi ni mchawi, niambie…’akasema
‘Huyu binti, hawezi kusema maana hana uhakika, yeye anahisi
kaota, lakini sio kweli, hayo yaliyomtokea ni kweli,..nilimdadidi akasema
aliona hiyo athari mwilini mwake..hawezi kuyasema hayo hapa.. ninachojiuliza
iweje,…ifanyike na yeye ashindwe kuzindukana, ina maana kuna kitu anafanyiwa,
mpaka anashindwa kuzindukana, sasa ni nani anamfanyia hivyo…’akasema
‘Kwahiyo mimi ndio namfanyia hivyo…?’ akauliza baba mwenye
nyumba kwa sauti ya kutahayari.
‘Hapo mimi sijui ni wewe au ni nani, ndio maana nikakuuliza
na kama hutaki kukubali ukweli, basi tutafute njia za wewe kukubali, na kama
hawa mabinti wengekubali kushirikiana, basi tungelishalimazlia hili,…’akasema
na mumewe akatikisa kichwa, na kugeuka kumuangalia huyo binti, akauliza
akimuangalia huyo binti;
‘Wewe binti uliwahi kuniona nikiingia chumbani kwako usiku
kama anavyodai huyo mama yako, sema ukweli wako wala usiogope, maana kikao hiki
ni cha kusaidiana, na ukisema ukweli, siwezi kukufany alolote, mbele ya wazee
hawa, sema uliwahi kuniona nikiingia chumbani kwako usiku na kukufanya hivyo,
inavyodaiwa, kuingia sikatai, niliwahi, lakini je niliwahi kukugusa, …?’
akauliza
‘Hapana….mimi sijawahi kumuona....hata kukuona ukiingia kama
unavyodai kuwa unaingia usiku, kiukweli tangia nifike hapa sijawahi kukuona
ukiingia chumbani kwangu usiku, nasema hilo kiukweli wangu,…, maana huwa
nimelala,..huwa ninakuwa na usingizi mnzito, isingelikuwa ni hayo majinamizi..
kwahiyo mimi …siwezi kulithibitisha hilo…’nikasema na wazee wakamgeukia mama
mwenye nyumba ili aendelee
Na baba mwenye nyumba akasema;
‘Umesikia…..jamani mumesikia wenyewe, ….shahidi wa kwanza
kakukana, haya tafuta ushahidi mwingine, au unataka kuonyesh hiyo kanda kwanza,
mimi ningelishauri, …tunampigie huyo binti mwingine au sio..mimi nataka
tulimalize hili kwa amani, ili tuone ni
nani mwenye matatizo, ni mimi au ni wewe….’akasema mume mtu huku akianza kupiga
simu kumuita huyo binti mwingine.
NB: Ushahidi utaendelea sehemu ijayo..je binti atakubali
kuja, au utaonyeshwa ushahidi wa video,
WAZO LA LEO: Kila
mtu ana udhaifu wake, na udhaifi mwingine unakuja kuwa ni ugonjwa mtu
asipokubali kusaidiwa, kuna watu wanaingia kwenye ulevi wa pombe au sigara, au
kwenye matatizo fulani, kumbe ni
kutokana na misongo ya mawazo!
Wengi wao, wangelikubali kusaidiwa huenda matatizo hayo
yasingelifikia huko. Kama wewe ni mke wa mtu, au mume wa mtu, jaribuni kukaa na
mwenzako, muongee matatizo yenu, kuliko kuyaweka kichwani, au kuanza kutafuta
njia zisizo halali , eti kuondoa mawazo…ikishikindikana watafuetni wazee wenye
busara, mpate mawazo ye hekima na busara!
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment