Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, July 22, 2017

DUWA LA KUKU.....17


Tulifika mlangoni na muda huo ndio geti likawa linafunguliwa, ina maana walipogonga geti hawakusibiria kuja kufunguliwa mama mwenye nyumba mwenyewe, alishuka kwenye gari lake, na kuingia ndani kwa kupitia mlango mdogo ambao, ulikuwa haujafungwa,  akafungua geti mwenyewe, na kuwakaribnisha wageni wake..

Wakati huo mimi na mdada tupo ndani hatuna habari, na kugongwa huko mdada alikusikia, lakini alijua ni watu wa nje wasumbufu tu, hakutoka kwa haraka, ila ilipolia honi ya gari, akajua ni wenye nyumba, anaangalia getini anaona magari yanaingia yaliongozana magari matatu…
Ndio akaja kule nilipo,

‘Fanya uondoke….’akasema


‘Kwani vipi, kuna nini kwani...…?’ nikauliza


‘Madamu kaja na wageni wake, na hao wageni usingelipenda wakuone….’


Tuendelee na kisa chetu…


************

‘Mungu wangu sasa ni nani hao, wageni gani, itakuwaje sasa..?’ nikauliza nikianza kutembea kuelekea nje.


‘Fanya haraka ni mwenye nyumba, kaja na wageni wake, hakuniambia watawahi kufika, sasa katafute sehemu ukajifiche…, nikipata nafasi nitakuita, au nikipata mwanya nitatoka nje tuongee vizuri, lakini sasa kama wameshaingia getinni, utapitia wapi, ....'akasema sasa akinishika mkono kabisa kuhakikisha natoka nje.


Tunafila mlangoni, ile tunafungua mlango , ndio muda huo geti limeshafunguliwa magari matatu yanaingizana…la madamu likiwa la mwisho…yalikuwa ni magari matatu, yaliyoingia, likiwemo hio la madamu…hapo mdada akawa anahaha, na kusema;


‘Madamu na wageni wake….sijui itakuwaje leo, umeniharibia kazi yangu, nilijua tu hili litatokea na wewe ndiye utaniharibia maisha yangu, …mungu wangu eeh…, najua wameshakuona, sijui tufanyeje…’akasema sasa akijaribu kujituliza.


Mimi nilikuwa kwa ndani, nilijirudisha haraka pale nilipoona magari hayo yanaingia,…


‘Sikiliza, mimi nitatoka kwa haraka wakati wanapaki magari yao, hawakuwa na muda wa kuniangalia, au unasemaje, hao wengine hawanifahamu mimi ni nani…’nikasema


‘Hivi unaelewa hayo magari mngine ni ya akina nani, umeshayasahau..?’ akaniuliza na mimi ndio nikatokeza kichwa na kuyaangalia, ndio nikayagundua ni magari ya akina nani, japokuwa magari yanafanana, lakini kwa fikira za haraka nikawazia hao ni akina nani…


‘Mungu wangu wamefuata nini huku…?’ nikauliza huku nikirudi ndani na kuangalia huku na kule..


‘Unataka kufanya nini sasa, kujificha humu ndani, ..haiwezekani wewe toka nje, ujifanye hivyo hivyo, kama ulivyosema ulikuja kuomba maji, inamisha kichwa chako chini  wasikuone…’akasema na nikataka kufanya hivyo, lakini haikusaidia


‘Wewe ni nani na unataka kwenda wapi…?’ ilikuwa sauti ya mama mwenye nyumba kumbe yeye alishatoka tayari kwenye gari lake, na wenzake ndio walikuwa wanatoka taratibu.


‘Hahaha et anajifanya kuinama chini kuwa hatutamtambua..’ilikuwa sauti ya mama mwingine ambaye naye tayari alishatoka kwenye gari, wakawa wote wananiangalia mimi. Nilimuona mdada kwa ndani, akiwa kashikilia kichwa, …keshachanganyikiwa.


‘Mnafiki mkubwa huyu, hakujua kuwa tunajua huku leo hii, kumbe huko ndipo alipokimbilia, hahaha,…hahaha, haya tuambie ulikuwa unakimbilia wapi sasa si ulikuja kujificha huku au…’.ilikuwa sauti ya mama mwingine, nikasimama nikiwa nimeduwaa.


‘Kwani ni nani huyu unamfahamu…?’ akauliza madamu…


**************
Wakina mama wale wakakaribishana ndani, na mimi nikabakia pale nje nimesimama tu, na mwenzangu akawa anafanya kazi ya kuwaandalia hao wageni, na mara sauti ikasema;

‘Mwambie huyo mwenzako akusaidia, au bado anaumwa…’ilikuwa sauti ya mmojawapo wa wale wamama wengine wawili.

‘Anasema anajisikia vibaya,…’akanitetea, lakini sikujali kunitetea kwake, nikaungana naye na kuanza kusaidia kazi za kuwaandalia, mpaka zilipokwisha na wakawa wanakula wakijadili mambo yao ya kibiashara, na mimi nikawa na mdada, alikuwa hataki hata kuongea maana nimeshamuharibia kazi yake,..na baadae tukaitwa;

‘Haya nyie marafiki wawili njooni hapa…’ilikuwa ni sauti ya mwenye hiyo nyumba, na kwa aibu tukafika mbele yao na kusimama, nikijaribu kujificha nyuma ya mwenzangu.

‘Hebu kaeni msije kutuangukia hapa, na wewe unajificha nini, hahaha, unaogopa madhambi yako, hapa umeshafika, na hukumu yako ni mara moja tu,hatuhitajii kuwaita polisi, maana umekuja umeingia kweney nyumba za watu bila kukaribishwa, wewe ni sawa na mwizi tu..’akasema mwenye nyumba, na tukakaa , unakaa kwenye sofa upande upande, kwa kuogopa.

‘Haya tuambieni lengo lenu ni nini, maana mlipata muda wa kuongea, tuanze na wewe mwenyeji, tuambie mwenzako ulimuita au alikuja mwenyewe, au…?’ akauliza mama mwenye nyumba, na tukabakia kimia

‘Nilipotoka hapa, niligundua kuna mtu kajificha pembeni mwa nyumba yangu, niliingiwa na mashaka sana, nikampigia simu mume wangu, akaniambia amekuona umeshaingia ndani na unaongea na mfanyakazi wangu wa ndani, na umetoka nje… lakini sikuamini…nikajua huenda ni nyumba ndogo za mume wangu, …’akasema akiwaangalia wenzake.

‘Nyumba ndogo…waume zetu hawa…’akasema mwingine.

‘Basi nikamtuma mtu wangu mmoja kuja kuchunguza…aliingia hadi huku ndani, hamukumuona muone jinsi gani unavyojisahau,na siku nikiibiwa humu ndani najua ni wewe, ni kwa vile huna muda humu tena…’akasema na kauli hii ilimfanya mwanzangu awe kama anatetemeka.

‘Nilishakuvumilia sana, na nilikuwa natafuta mwanya wa kukufukuza humu ndani, sasa nimeupata, lakini kabla hujaondoka, nataka kusikie ukweli,…’akasema mama mwenye nyumba, na wote tukabakia kimia.

‘Haya na wewe tuambie,…umetokea wapi na kwanini umekuja hapa nyumbani kwangu,…?’ akaniuliza akiniangalia kwa dharau. Na mimi nikakaa kimia

‘Huyu namfahamu, alikuwa kule kwangu…na hutaamini,  alinitoroka hospitalini, nikawa najiuliza amekwenda wapi, na ulipokuja kuniambia kuna mtu kajificha pembeni mwa nyumba yako, na ulivyoelezea jinsi alivyovaa, nikajua ni yeye, lakini hakuwa ameva hivi, kabadilisha nguo…’akasema

‘Ni kweli, nilivyomuona awali hakuwa amevaa hivi…’akasema mwenye hiyo nyumba.

‘Sasa wapendwa, mtuambie mumepanga kufanya nini, au mlikutana kupanga mikakati ya kutumalizia ndoa zetu..?’ akauliza yule mwingine ambaye muda mwingi alikuwa kimia, akiandika kitu kwenye simu yake.

‘Ngoja mimi niwasaidie kidogo, maana wote wawili wamefanyia kazi nyumbani kwangu, na huyu wa kwanza, ndiye kasababisha yote haya, ..sio mbaya, siwezi kusema yeye ni mbaya kihivyo, kutokana na uchunguzi wangu, ila tunataka kuwaambia kuwa sasa muda wenu wa kuishi kwenye jiji hili umekwisha, kwa usalama wenu, itabidi mrudi makwenu, au sio wenzangu…’akasema huyo mama mwingine, na wenzake wakakubali.

‘Jamani kwanini mumeamua hivyo, wakati mnafahamu kuwa haya yote yanayotokea sio kwa makusdio yetu..’akasema mdada na mimi nikabakia kimia.

‘Tatizo wewe unajifanya ni mjanja sana,…na ujanja wako unawafundisha na wengine, unajua kutunga maneno na kuwhdaa watu wengine, lakini sio hapa kwangu, unasikia,..nilikukanya sana, …’akasema mama mwenye nyumba.

‘Lakini mimi sijawahi kufanya kitu chochote kibaya humu ndani, …’akajitetea

‘Nilikuambia nini kila siku, nikiondoka usilete wageni humu ndani, maana sio wageni wote wana nia nzuri, huyu ni nani…?’ akauliza mama mwenye hiyo nyumba.

‘Huyu kaja ghafla, wala sikujua kuwa atafika humu, na nilikuwa namfukuza aondoke, unajua ilivyo mtu kaja kwako, na sikutakiwa ni mfukuze kama mwizi..’akajitetea.

‘Usijifanye mjanja, haya unayoyafanya hujayaanza leo, umekuwa ukirudia kila mara na mimi nakusamehe.., na wasiwasi wangu huyu kwa mambo yake haya, na hao wanafunzi wake, wakiendelea kubakia hapa jijini mtawatia waume wetu wazimu, maana kila siku mazungumzo ni hayo hayo, kwanini tumefanya hivi kwanini , kwanini..kwani nyie ni nani …eeh, tuambieni, wema wetu ndio imekuwa adhabu kwetu, hapana inabidi muondoke tu…’akasema.

‘Lakini kabla hamjaondoka, ili msije kuona sisi ni wabaya kihivyo, sisi sio wabaya kama mnavyofikiria nyie, sisi tunawajali sana, tunawaonea huruma sana kwa maisha mliyopitia ndio maana tuliwakubali,  lakini kama kuna mdudu ambaye ataambukiza maradhi mabaya ndani ya mwili, dawa yake ni nini, eti dawa yake ni nini, tukitumia dawa ya kumuua kuna makosa, lakini sisi hatutaki kuwaaua, tunataka mrudi makwenu…’akasema.

Hapo nikaona ni bora na mimi niongee, nikanyosha kidole kama darasani kuomba ruhusa, na mwenye nyumba akasema;

‘Haya sasa ongea naona umeguswa sasa….’akasema

‘Mimi naombeni jambo moja, sawa kama mnataka turudi makwetu….ni sawa tu, kwasababu hatuna haki kwenu, ..hamuwezi mkahisi maisha yetu kwasababu hamukuwahi kuyaishi kabla…lakini tungelipenda tupate muda, kwasababu kurudi huko nyumbani ni kama mnatupeleka kuuwawa, kama huko kwetu watu wanauwawa ovyo, sasa tunawaombeni sana mtupe muda…’nikasema

‘Unajua kwanini anasema hivyo…’akasema mama mmojawapo, yule aliyenipeleka hospitalini.
‘Kwanini anasema hivyo..?’ akauliza mama mwenye nyumba.

‘Ana mimba…sasa huenda anataka njia ya kwenda kwa huyo bwana wake…’akasema huyo mama.

‘What!…..! unasema ukweli..?’ akauliza yule mama aliyekuwa mfadhili wangu wa kwanza..

‘Nilimgundua kutokana na dalili alizokuwa nazo, mimi na mume wangu tukaamua kumpeleka hospitalini, akapimwa, na docta akagundua hilo tatizo, docta naye akajifanya kumtetea, nikamwambia wewe si una huruma, sasa tunaenda kumchukua akakae kwako….unajua alisema nini…?’ akawauliza wenzako
‘Tuambie….’wakasema

‘Siwezi kumchukua maana sio  mimi niliyemtoa huko kijijini, na huyo aliyempa huo uja uzito anatakiwa akapatikane ili akawajibike, nikamwambia, haya mtafute huyo mtu, sisi hatumjui…, ukimpata mlete, …na umemuuliza huyo binti ni nani alimbaka, ni nani alitembea naye…ni nani aliyempa hiyo mimba, kakuambia nini…’akatulia.

‘Alisema ni nani kafanya hivyo..?’ akaulizwa na wenzake.

‘Kasema huyo binti anadai yeye aliota tu, …hahaha’ akacheka na wote wakacheka kwa pamoja.

‘Hapo sasa…wewe si docta, kama yeye anadai kuwa aliota tu, na hakuna mtu aliyewahi kutembea naye, basi docta utusaidie kumtafuta huyo mtu, hapo docta akagwaya, akasema tumuite huyo binti ili tusaidiane, yeye anaweza kutusaidia tukampata huyo mtu..tukasema haya, ..mimi natoka nje kumuita ..hakuna mtu, keshakimbia…’akasema.

Docta kwanza hakuamini, akatoka yeye mwenye nje kumtafuta, baadae anarudi anasema,…

‘Kweli huyo binti ni tatizo….’

Hapo ndio docta akajua huyo binti ni muongo na tapeli, kama angelikuwa mkweli angelisubiria tumalize mazungumzo, tuone muafaka wake utafikia wapi, kwanini akakimbia, basi docta akanyosha mikono.

Sisi tukamsihi docta, kuwa yeye si anataka haki itendeke, basi aende mahakamani, yeye si anajifanya mtetezi wa wanyonge, mtetezi wa wanawae wanaonyanyaswa, basi afanye hiyo kazi na sisi tutaitwa, kujieleza, huyo binti amtaje aliyemfanyia hivyo, ni nani…’akasema.

‘Hahaha, atamuona wapi na yeye aliota tu…’akasema huyo mama mwingine na wakaangua kicheko tena.

‘Sasa ndugu zanguni, wadada warembo, wanaowachengua waume zetu, sisi hatuna lengo baya na nyie, lakini tunachotaka ni kuzilinda ndoa zetu,..tunakwepa sana mambo hayo ya kishirikina, tunakwepa sana kuingiza mambo mabaya kwenye familia zetu, …mfano sasa wewe una mimba, hatujui umaipatia wapi, ni nini kitatoka baada ya hapo, .humjui aliyekupa hiyo miba au sio…, ina maana gani hapo, familia zetu zitaingia matatani kwa mambo yenu mliokuja nayo…’akatulia.

‘Unajua niwaambie kitu, sisi tulishakubaliana huyu mdada atafutiwe chumba, na biashara, ajiwekeze, maana akikaa kwenye nyumba za watu mambo kama haya yatajitokeza kwa wengine, basi awe na kwake, ajihangaikie, tulipanga kumtafutia mtaji..kuna mambo bado hatujakubaliana na mume wangu, lakini tulishafika hatua ya mwisho, sasa kama kuna hili la mimba tena,..mmh, sijui itakuwaje…’akasema mama mmojawapo.

‘Kwahiyo mume wako ataambiwa ni yeye au ni kijana wako, ..si ndio hivyo, kuwa wao ndio walimpa mimba au itakuwaje hapo, ndio maana watu kama hawa watakiwa warejeshwe huko walipotoka…’akauliza mama wa hiyo nyumba

‘Kama sasa ana mimba tunachohitajia ni yeye atoe ushahidi, kama kweli kapachikwa na mtu wa familia yangu, lakini yeye, tangia awali nilimuuliza kama kweli aliwahi kuwa na mahusiano na mume wangu , akasema hana na hajawahi kumuona mume wangu akiingia chumbani kwake…

‘Mhh…kwahiyo kumbe hakuna lolote la kuwashinikiza familia yako kaa itafika mahakamani, maana wanaweza kwenda kushawishiwa na watu fanyeni hivi, nendeni mahakamani, sasa waende, waone watavyoumbuka,…’akasema mama mwenye myuma.

‘Mimi nilihsjitolea kumsaidia huyu binti, kama kweli angelikuwa mkweli, ningelimsaidia kwa namna niliyoona ni bora kwake, lakini akawa muongo, akanificha ukweli,…sasa atajijua mwenyewe, …’akasema.

‘Je kama kweli ni mimba ya mwanafamilia yako itakuwaje…?’ akauliza mama mwenye myumba.

‘Muhimu ni ushahidi, ..kama aliota ni nani atamshika, ..kama anaficha ukweli ni nani atamsaidia, naona dunia ikamfundishe, hakuna jinsi hapa,…asije akaja kutuletea watoto balaa kwenye familia zetu…’akasema

‘Mimi naona tuliongelee hili sisi wenyewe kwanza maana linaleta picha mbaya, tukifikia muafaka tutachukua hatua, haina haja ya kuwashirikisha waume zetu..sasa nyie mabint nendeni huko ndani au huko nje, mkaongee, mtafute njia gani, sisi tunaweza kuwasaidia, mje na wazo lenye maana, na sisi mtuache tuongee, lakini mkae mkijiandaa na safari ya kurudi huko kijijini kwenu, sawa…’tukaambiwa,

‘Lakini mimi nina kosa gani..?’ akauliza yule mdada

‘Na wewe ndio chanzo cha yote hayo, unauliza una kosa gani, tukuulize bila ya wewe haya yote yangelitokeaje, wewe ndiye chanzo, na kwahiyo wewe ndiye mkosaji mkuu, unastahili adhabu kubwa sana, na adhabu yako ni kurejeshwa huko makwenu,…’akajibiwa na yule mama, mfadhili wangu wa kwanza.

‘Lakini nilishawaambia kisa na sababu …nilijitolea kuja kuusema ukweli, ili mjua kinachoendelea hivyo mimi nilifanya kosa,…’akajitetea.

‘Ndio maana tunataka nyie make waili muongee, mtafuta njia nzuri ya kulimaliza hili, kama mtahitajia msaada wetu, sawa, na sisi tutaliongelea kivyetu, tuna mambo yetu mengi tunayaongea hii leo, na hili limekuja tu, litatupotezea malengo yetu ya maendeleo,..kwahiyo nendeni mkaongee huko…’akasema yule mama mfadhili wa kwanza.

‘Na mimi nawapa ofa, kwa leo, na kesho na kesho kuwa mtakaa  humu ndani kwangu , mtakaa humu, mtakula, lakini mtanisaidia kazi, huku nikitafuta mfanyakazi mwingine, huku mkijifungasha virago vyenu tayari kwa kuondoka, na kama kuna lolote la ziadi, tutaangalia, mimi ndiye kiongozi wa kundi letu na maamuzi yangu ni mwisho, nendeni…’akasema mama mwenye nyumba.

‘Au mimi niulize tu, maana nyie mnawajulia zaidi hawa mabinti wawili zaidi yangu, huyu bint, ailetwa kwangu, na mume wangu na sikutakiwa kuuliza, kwa vile ni mgeni, ..nilikubali nilijua njia ya mnafiki ni fupi…niliambiwa kaja kwa muda, mara naona mwezi huo, mara kumbe mgeni kaja na mzigo tumboni, sasa nauliza, huyu anasema sio kusudio lake, kuna mtu kasababisha hivyo, wao si wanamfahamu, sasa watuelekeze sisi tutawasaidia kupambana na huyo mtu, kama ni kisheria, au vyovyote inavyowezekana,..’akasema yule mama aliyenipeleka hospitalini.

‘Wanadai ni mchawi mmoja kutoka huko kijijini kwao…’akasema mama fadhili wa kwanza

‘Mchawi tena ni yale yale niliyoyapiga marufuku hapa nyumbani kwangu, huyu binti alikuja na hadithi ndefu, kuwa kuna mchawi anaweza kuingia usiku akafanya hivi na vile, nikamwambia wee, ishia hapo hapo, hapa nyumbani kwangu kuna ulinzi , mchai hawezi kuingiza mguu wake humu….’akasema

‘Je hakuwahi kupiga kelele za kuota usiku…?’ akaulizwa mama mwenye nyumba.

‘Thibutu, angepiga ningemuonyesha kazi, hakuna cha uchawi au shetani anaingia humu ndani kwangu ninajua nikwanini….nilimpiga marufu, na nilimuambia kama ataleta mtu wa namna hiyo, yeye, na huyo mtu wake, watakwenda jela..’akasema mama mwenye nyumba.
‘Kumbe wachawi wanaogopa jela…’akasema yule mama mlezi wa kwanza..

‘Hebu tuambie, ni nani huyo mchawi aliyewafanyia hivyo, je ndiye aliyemfanyia mwenzako hivyo, na huenda ndiye alimpa mimba, ili wasingiziwe wanafamilia…’akasema yule mama aliyenipeleka hopsitalini.

‘Atuambie huyo mdada wa kwanza…’akasema yule mama mfadhili wa kwanza.

‘Ndi-ndi- ndio yeye, aliyesababisha yote hayo, lakini sina uhakika na hiyo mimba ya huyu…’akasema

‘Na awali ulikuwa na dalili ya mimba ulipofika hapa kwangu, ilikwenda wapi hiyo mimba…?’ akaulizwa

‘Mimi sijui, ilipoteaje..’akasema na akina mama hao wakaangaliana huku wakionyesha uso wa kushangaa.

‘Mimba imepotea, hahaha, kwa vile nilimuambia kama ana mimba basi afungashe, kwani kidogo alianza kunisumbua, anaumwa, ..nikahangaika,..baada ya kutoa hivyo vitisho, aah, akajirudi, lakini kwa hili sasa simtaki tena…’akasema
‘Sasa huyo mtu wenu, unayemuita mchawi, yupo wapi..?’ akaulizwa

‘Alikuja hapa dar, akasema anakwenda kutibiwa…’akasema

‘Mlionana naye wapi…?’ akaulizwa

‘Ali-ali-kuja hapa nyumbani…akasema huyo mdada kwa mashaka.

‘Ni yupi huyo,..lini, ooh,.. ni yule jamaa alikuja akasema wewe ni ndugu yake, kumbe familia yenu ni wachawi eeh,…’akasema mama mwenye nyumba.

‘Hapana sio ndugu yangu yule, alisema hivyo tu, ili aweze kuongea na mimi….’akasema

‘Unaoan jinsi ulivyo muongo, siku ili ulituambia nini mimi na mume wangu kuwa huyo mtu ni nani wako…’akasema mama mwenye nyumba

‘Niliogopa kusema ukweli maana hata mimi sikutaka aendelee kunisumbua, ndio nikamfukuza, …’akasema

‘Je tutampataje huyo mtu, kwa kuwasaidia, ili wajibike, kama mimba ni yake ahakikishe anamtunza mwenzako tutampataje..?’ wakauliza

‘Alisema kaja kutibiwa, sasa sijui kama kaondoka au la…’akasema mdada

‘Anaumwa nini, huna namba yake ya simu..?’ akaulizwa

‘Anasema anaumwa mguu umevimba, kaja kutibiwa, namba yake nilikuwa nayo nikaifuta, sikutaka kuwa na mawasiliano naye …’akasema mdada.

‘Ni kweli nakumbuka huyo jamaa alipofika hapa, alikuwa anachechemea, na ilionyesha wazi mguu mmoja umevimba, kama ana tege, la mguu mmoja, na ulikuwa unatoa harufu , au..ilikua ni harufu ya nini sijui, sikukumbuka kulifuatilia hilo,…’akasema

‘Mimi sijui kama ulikuwa ukitoa harufu, ila alisema anahitajika kutibiwa na kama nina pesa nimkopeshe…’mdada akasema

‘Hahaha, ndio huyo aliyetaka kukuoa, na sasa anataka kukukopa mmh, una pesa nyingi wewe, utuambie umezipatia wapi…?’ akaulizwa

‘Simtaki kabisa,..nilimkataa,na kumkataa ndio chanzo cha yote hayo. Na sikuwahi kumpa pesa nilimfukuza…’akasema.

‘Sawa, sasa nyie kayaongeeni yote hayo..ila msimamo wetu ndio huo huo, …lazima muhame huu mji, maana mkindelea kubakia hapa,  mtawatia wazimu waume zetu, wanaojifanya kuwajali sana…mnasikia, kaongeeni muone sisi tutawasaidiaje na mkitaka tunaweza kukutana na huyo mtu mnayesema ni mchawi, sisi tutapambana naye, hatuogopi uchawi…’wakasema wakigongeana mikono.

Mara simu ya mama mwenye nyumba ikalia, na akaipokea, na kuuliza

‘Wewe ni nani..?’ akauliza na kusikiliza

‘Unataka nini..?’ akauliza

‘Unamtaka aje hospitalini, wapi,…?’ akauliza

‘Ocean road, kwani wewe ni nani kwake..?’ akauliza na kusikiliza

‘Aaah, ndio wewe eeh, ulikuja hapa siku ile, aheri umepiga simu, tunakutafuta sana, sasa sikiliza tutakuja huko hospitalini, tuna maongezii na wewe, wewe si mchawi, au sio…’akauliza na kusiliza.

‘Hahaha, ulikuwa mchawi na sasa umeacha, kwanini umeacha, uchawi wa kurithi utauachaje,…?’ akaulizwa

‘Nini…usamehewe, mbona wewe hukuwasamehe uliokuwa ukiwatendea hayo maovu yako..?’ akaulizwa

‘Kwahiyo wewe unataka nini sasa…, msaada wa kutibiwa, mchawi anaumwaga.. ..huyu mdada atapatia wapi pesa, anikopeshe mimi, haaa, mimi ni benki wa kukopesha watu… na atazirudishaje,..hahaha, wewe kweli umepagawa kwa mshahara gani alio nao yeye,  na kwanini yeye akugharamie hivyo, wakati wewe ….nini, unataka kuwaondolea nini,…mazindiko ndio nini…mmh, haya ..subiri nitakupigia…’akakata simu

‘Mumesikia jamani, nilikuwa naongea na mchawi mwenyewe…hahaha’akasema na wale wengine wakatulia.
‘Anasemaje..?’ akaulizwa.

‘Anasema anahitajia msaada wa kipesa, anahitajia pesa kwa ajili ya matibabu, anatakiwa pesa nyingi tu, milioni kadhaa, sasa anataka huyu mdada akope kwangu,..watu wa ajabu sana hawa…’akasema

‘Akope kwako kwa vipi…?’ akauliza

‘Anasema yeye anajua kwa vipi maana asipofanya hivyo hatakubali kuyaondoa, ..mazindiko, kitu kaam hicho….’akasema

‘Oooh, kumbe, sasa kayawekaje ..?’ wakaulizana.

‘Labda tumuulize mpenzi wake…’akasema mama mwenye nyumba.

‘Huyo sio mpenzi wangu jamani, huyo ni adui yangu…’akasema.

‘Ndio ananitishia mimi kuwa eti nisipokubali kutoa huo mkopo, hataweza kuyaondoa hayo mazindiko, kwa wote aliowawekea, na hapa kwangu ameshakamlisha kazi hiyo tutaanza kupata shida…’akasema.

‘Hahaha…hawa watu wanachekesha, halafu anatishia, kwa kujiamini kabisa, mtu anaumwa, badala ya kuongea vizuri anatishia, hivi..eeh yupoje huyo mtu..?’ akauliza yule mama aliyenipeleka hospitalini.
‘Sio mtu mzima sana, nashangaa kwanini kajiingiza kwenye mambo kama hayo…’akasema mama mwenye hiyo nyumba.

‘Mimi naona,…tukakutane na huyo mchawi, maana kwanza kama kwli ni yeye aliingia kwenye nyumba yangu akafany ahayo aliyoyafanya , nahitajia kuonana naye , na atanitambua, ..kuna ushahudi ninao, .. waonyesha kweli aliingia, …sikutaka kuliingilia sana hili, maana nitakuwa naamini mambo ya kishirikina, lakini kwa vile keshaanza kututushia amani, basi kesho twendeni huko, hata leo ikiwezekana…’akasema yule mama mfadhili wa kwanza

‘Na wewe kama hiyo mimba ni kwake, basi tukifika pale sisi tunakubidhisha kwake, mtajuana wewe nay eye, unasikia, sasa hili limefika kubaya, mtu anayetishia amani mwenzake, anakuwa katenda kosa, sasa atapambana na polisi…’akasema yule mfadhili wa kwanza

‘Ngojeni kwanza niwasiliane na mume wangu, hajui kuwa mume wangu ni polisi, eeh, ngoja, hapa sasa inabidi tuwashikirishe waume zetu, atanyea jela…’akasema mke wa hiyo nyumba.

WAZO LA LEO:  Kuna watu wengine wanaona ufahari kushindana kwenye kesi, ugomvi, malumabano hata kama kuna njia nyingine mbadala, kila jambo wao wanalijenga ligi ya ushindani,  hata kama ni jambo la kusameheana tu,..ugomvi, shutuma, visasi na uhasama imekuwa ni hulka zao. Kusameheana ni jambo lenye kuleta heri, na maridhiano ya kujenga mshikamano ndio njia ya salama ya kuleta amani. Tusikimbilie kuonyeshana ubabe, ubabe hauabna heri kamwe, bali tuwe na tabia njema ya kusameheana, kusaidiana na kuhurumiana, na mola ataleta heri zake.

Ni mimi: emu-three

No comments :