Tulifika
mlangoni na muda huo ndio geti likawa linafunguliwa, ina maana walipogonga geti
hawakusibiria kuja kufunguliwa mama mwenye nyumba mwenyewe, alishuka kwenye
gari lake, na kuingia ndani kwa kupitia mlango mdogo ambao, ulikuwa
haujafungwa, akafungua geti mwenyewe, na
kuwakaribnisha wageni wake..
Wakati
huo mimi na mdada tupo ndani hatuna habari, na kugongwa huko mdada alikusikia,
lakini alijua ni watu wa nje wasumbufu tu, hakutoka kwa haraka, ila ilipolia
honi ya gari, akajua ni wenye nyumba, anaangalia getini anaona magari yanaingia
yaliongozana magari matatu…
Ndio
akaja kule nilipo,
‘Fanya
uondoke….’akasema
‘Kwani
vipi, kuna nini kwani...…?’ nikauliza
‘Madamu
kaja na wageni wake, na hao wageni usingelipenda wakuone….’
Tuendelee
na kisa chetu…
************
‘Mungu
wangu sasa ni nani hao, wageni gani, itakuwaje sasa..?’ nikauliza nikianza
kutembea kuelekea nje.
‘Fanya
haraka ni mwenye nyumba, kaja na wageni wake, hakuniambia watawahi kufika, sasa
katafute sehemu ukajifiche…, nikipata nafasi nitakuita, au nikipata mwanya
nitatoka nje tuongee vizuri, lakini sasa kama wameshaingia getinni, utapitia
wapi, ....'akasema sasa akinishika mkono kabisa kuhakikisha natoka nje.
Tunafila
mlangoni, ile tunafungua mlango , ndio muda huo geti limeshafunguliwa magari
matatu yanaingizana…la madamu likiwa la mwisho…yalikuwa ni magari matatu,
yaliyoingia, likiwemo hio la madamu…hapo mdada akawa anahaha, na kusema;
‘Madamu
na wageni wake….sijui itakuwaje leo, umeniharibia kazi yangu, nilijua tu hili
litatokea na wewe ndiye utaniharibia maisha yangu, …mungu wangu eeh…, najua
wameshakuona, sijui tufanyeje…’akasema sasa akijaribu kujituliza.
Mimi
nilikuwa kwa ndani, nilijirudisha haraka pale nilipoona magari hayo yanaingia,…
‘Sikiliza,
mimi nitatoka kwa haraka wakati wanapaki magari yao, hawakuwa na muda wa
kuniangalia, au unasemaje, hao wengine hawanifahamu mimi ni nani…’nikasema
‘Hivi
unaelewa hayo magari mngine ni ya akina nani, umeshayasahau..?’ akaniuliza na
mimi ndio nikatokeza kichwa na kuyaangalia, ndio nikayagundua ni magari ya
akina nani, japokuwa magari yanafanana, lakini kwa fikira za haraka nikawazia
hao ni akina nani…
‘Mungu
wangu wamefuata nini huku…?’ nikauliza huku nikirudi ndani na kuangalia huku na
kule..
‘Unataka
kufanya nini sasa, kujificha humu ndani, ..haiwezekani wewe toka nje, ujifanye
hivyo hivyo, kama ulivyosema ulikuja kuomba maji, inamisha kichwa chako chini wasikuone…’akasema na nikataka kufanya hivyo,
lakini haikusaidia
‘Wewe ni
nani na unataka kwenda wapi…?’ ilikuwa sauti ya mama mwenye nyumba kumbe yeye
alishatoka tayari kwenye gari lake, na wenzake ndio walikuwa wanatoka taratibu.
‘Hahaha
et anajifanya kuinama chini kuwa hatutamtambua..’ilikuwa sauti ya mama mwingine
ambaye naye tayari alishatoka kwenye gari, wakawa wote wananiangalia mimi.
Nilimuona mdada kwa ndani, akiwa kashikilia kichwa, …keshachanganyikiwa.
‘Mnafiki
mkubwa huyu, hakujua kuwa tunajua huku leo hii, kumbe huko ndipo alipokimbilia,
hahaha,…hahaha, haya tuambie ulikuwa unakimbilia wapi sasa si ulikuja kujificha
huku au…’.ilikuwa sauti ya mama mwingine, nikasimama nikiwa nimeduwaa.
‘Kwani
ni nani huyu unamfahamu…?’ akauliza madamu…
**************
Wakina
mama wale wakakaribishana ndani, na mimi nikabakia pale nje nimesimama tu, na
mwenzangu akawa anafanya kazi ya kuwaandalia hao wageni, na mara sauti ikasema;
‘Mwambie
huyo mwenzako akusaidia, au bado anaumwa…’ilikuwa sauti ya mmojawapo wa wale
wamama wengine wawili.
‘Anasema
anajisikia vibaya,…’akanitetea, lakini sikujali kunitetea kwake, nikaungana
naye na kuanza kusaidia kazi za kuwaandalia, mpaka zilipokwisha na wakawa
wanakula wakijadili mambo yao ya kibiashara, na mimi nikawa na mdada, alikuwa
hataki hata kuongea maana nimeshamuharibia kazi yake,..na baadae tukaitwa;
‘Haya
nyie marafiki wawili njooni hapa…’ilikuwa ni sauti ya mwenye hiyo nyumba, na
kwa aibu tukafika mbele yao na kusimama, nikijaribu kujificha nyuma ya
mwenzangu.
‘Hebu
kaeni msije kutuangukia hapa, na wewe unajificha nini, hahaha, unaogopa
madhambi yako, hapa umeshafika, na hukumu yako ni mara moja tu,hatuhitajii
kuwaita polisi, maana umekuja umeingia kweney nyumba za watu bila kukaribishwa,
wewe ni sawa na mwizi tu..’akasema mwenye nyumba, na tukakaa , unakaa kwenye
sofa upande upande, kwa kuogopa.
‘Haya
tuambieni lengo lenu ni nini, maana mlipata muda wa kuongea, tuanze na wewe mwenyeji,
tuambie mwenzako ulimuita au alikuja mwenyewe, au…?’ akauliza mama mwenye
nyumba, na tukabakia kimia
‘Nilipotoka
hapa, niligundua kuna mtu kajificha pembeni mwa nyumba yangu, niliingiwa na
mashaka sana, nikampigia simu mume wangu, akaniambia amekuona umeshaingia ndani
na unaongea na mfanyakazi wangu wa ndani, na umetoka nje… lakini sikuamini…nikajua
huenda ni nyumba ndogo za mume wangu, …’akasema akiwaangalia wenzake.
‘Nyumba
ndogo…waume zetu hawa…’akasema mwingine.
‘Basi
nikamtuma mtu wangu mmoja kuja kuchunguza…aliingia hadi huku ndani, hamukumuona
muone jinsi gani unavyojisahau,na siku nikiibiwa humu ndani najua ni wewe, ni
kwa vile huna muda humu tena…’akasema na kauli hii ilimfanya mwanzangu awe kama
anatetemeka.
‘Nilishakuvumilia
sana, na nilikuwa natafuta mwanya wa kukufukuza humu ndani, sasa nimeupata,
lakini kabla hujaondoka, nataka kusikie ukweli,…’akasema mama mwenye nyumba, na
wote tukabakia kimia.
‘Haya
na wewe tuambie,…umetokea wapi na kwanini umekuja hapa nyumbani kwangu,…?’
akaniuliza akiniangalia kwa dharau. Na mimi nikakaa kimia
‘Huyu
namfahamu, alikuwa kule kwangu…na hutaamini, alinitoroka hospitalini, nikawa najiuliza
amekwenda wapi, na ulipokuja kuniambia kuna mtu kajificha pembeni mwa nyumba
yako, na ulivyoelezea jinsi alivyovaa, nikajua ni yeye, lakini hakuwa ameva
hivi, kabadilisha nguo…’akasema
‘Ni
kweli, nilivyomuona awali hakuwa amevaa hivi…’akasema mwenye hiyo nyumba.
‘Sasa
wapendwa, mtuambie mumepanga kufanya nini, au mlikutana kupanga mikakati ya
kutumalizia ndoa zetu..?’ akauliza yule mwingine ambaye muda mwingi alikuwa
kimia, akiandika kitu kwenye simu yake.
‘Ngoja
mimi niwasaidie kidogo, maana wote wawili wamefanyia kazi nyumbani kwangu, na
huyu wa kwanza, ndiye kasababisha yote haya, ..sio mbaya, siwezi kusema yeye ni
mbaya kihivyo, kutokana na uchunguzi wangu, ila tunataka kuwaambia kuwa sasa
muda wenu wa kuishi kwenye jiji hili umekwisha, kwa usalama wenu, itabidi mrudi
makwenu, au sio wenzangu…’akasema huyo mama mwingine, na wenzake wakakubali.
‘Jamani
kwanini mumeamua hivyo, wakati mnafahamu kuwa haya yote yanayotokea sio kwa
makusdio yetu..’akasema mdada na mimi nikabakia kimia.
‘Tatizo
wewe unajifanya ni mjanja sana,…na ujanja wako unawafundisha na wengine, unajua
kutunga maneno na kuwhdaa watu wengine, lakini sio hapa kwangu,
unasikia,..nilikukanya sana, …’akasema mama mwenye nyumba.
‘Lakini
mimi sijawahi kufanya kitu chochote kibaya humu ndani, …’akajitetea
‘Nilikuambia
nini kila siku, nikiondoka usilete wageni humu ndani, maana sio wageni wote
wana nia nzuri, huyu ni nani…?’ akauliza mama mwenye hiyo nyumba.
‘Huyu
kaja ghafla, wala sikujua kuwa atafika humu, na nilikuwa namfukuza aondoke,
unajua ilivyo mtu kaja kwako, na sikutakiwa ni mfukuze kama mwizi..’akajitetea.
‘Usijifanye
mjanja, haya unayoyafanya hujayaanza leo, umekuwa ukirudia kila mara na mimi
nakusamehe.., na wasiwasi wangu huyu kwa mambo yake haya, na hao wanafunzi
wake, wakiendelea kubakia hapa jijini mtawatia waume wetu wazimu, maana kila
siku mazungumzo ni hayo hayo, kwanini tumefanya hivi kwanini , kwanini..kwani
nyie ni nani …eeh, tuambieni, wema wetu ndio imekuwa adhabu kwetu, hapana
inabidi muondoke tu…’akasema.
‘Lakini
kabla hamjaondoka, ili msije kuona sisi ni wabaya kihivyo, sisi sio wabaya kama
mnavyofikiria nyie, sisi tunawajali sana, tunawaonea huruma sana kwa maisha
mliyopitia ndio maana tuliwakubali, lakini kama kuna mdudu ambaye ataambukiza
maradhi mabaya ndani ya mwili, dawa yake ni nini, eti dawa yake ni nini,
tukitumia dawa ya kumuua kuna makosa, lakini sisi hatutaki kuwaaua, tunataka
mrudi makwenu…’akasema.
Hapo
nikaona ni bora na mimi niongee, nikanyosha kidole kama darasani kuomba ruhusa,
na mwenye nyumba akasema;
‘Haya
sasa ongea naona umeguswa sasa….’akasema
‘Mimi
naombeni jambo moja, sawa kama mnataka turudi makwetu….ni sawa tu, kwasababu
hatuna haki kwenu, ..hamuwezi mkahisi maisha yetu kwasababu hamukuwahi kuyaishi
kabla…lakini tungelipenda tupate muda, kwasababu kurudi huko nyumbani ni kama
mnatupeleka kuuwawa, kama huko kwetu watu wanauwawa ovyo, sasa tunawaombeni
sana mtupe muda…’nikasema
‘Unajua
kwanini anasema hivyo…’akasema mama mmojawapo, yule aliyenipeleka hospitalini.
‘Kwanini
anasema hivyo..?’ akauliza mama mwenye nyumba.
‘Ana
mimba…sasa huenda anataka njia ya kwenda kwa huyo bwana wake…’akasema huyo mama.
‘What!…..!
unasema ukweli..?’ akauliza yule mama aliyekuwa mfadhili wangu wa kwanza..
‘Nilimgundua
kutokana na dalili alizokuwa nazo, mimi na mume wangu tukaamua kumpeleka
hospitalini, akapimwa, na docta akagundua hilo tatizo, docta naye akajifanya
kumtetea, nikamwambia wewe si una huruma, sasa tunaenda kumchukua akakae
kwako….unajua alisema nini…?’ akawauliza wenzako
‘Tuambie….’wakasema
‘Siwezi
kumchukua maana sio mimi niliyemtoa huko
kijijini, na huyo aliyempa huo uja uzito anatakiwa akapatikane ili akawajibike,
nikamwambia, haya mtafute huyo mtu, sisi hatumjui…, ukimpata mlete, …na umemuuliza
huyo binti ni nani alimbaka, ni nani alitembea naye…ni nani aliyempa hiyo mimba,
kakuambia nini…’akatulia.
‘Alisema
ni nani kafanya hivyo..?’ akaulizwa na wenzake.
‘Kasema
huyo binti anadai yeye aliota tu, …hahaha’ akacheka na wote wakacheka kwa
pamoja.
‘Hapo
sasa…wewe si docta, kama yeye anadai kuwa aliota tu, na hakuna mtu aliyewahi
kutembea naye, basi docta utusaidie kumtafuta huyo mtu, hapo docta akagwaya,
akasema tumuite huyo binti ili tusaidiane, yeye anaweza kutusaidia tukampata
huyo mtu..tukasema haya, ..mimi natoka nje kumuita ..hakuna mtu, keshakimbia…’akasema.
Docta
kwanza hakuamini, akatoka yeye mwenye nje kumtafuta, baadae anarudi anasema,…
‘Kweli
huyo binti ni tatizo….’
Hapo
ndio docta akajua huyo binti ni muongo na tapeli, kama angelikuwa mkweli
angelisubiria tumalize mazungumzo, tuone muafaka wake utafikia wapi, kwanini
akakimbia, basi docta akanyosha mikono.
Sisi
tukamsihi docta, kuwa yeye si anataka haki itendeke, basi aende mahakamani,
yeye si anajifanya mtetezi wa wanyonge, mtetezi wa wanawae wanaonyanyaswa, basi
afanye hiyo kazi na sisi tutaitwa, kujieleza, huyo binti amtaje aliyemfanyia hivyo,
ni nani…’akasema.
‘Hahaha,
atamuona wapi na yeye aliota tu…’akasema huyo mama mwingine na wakaangua
kicheko tena.
‘Sasa
ndugu zanguni, wadada warembo, wanaowachengua waume zetu, sisi hatuna lengo
baya na nyie, lakini tunachotaka ni kuzilinda ndoa zetu,..tunakwepa sana mambo
hayo ya kishirikina, tunakwepa sana kuingiza mambo mabaya kwenye familia zetu,
…mfano sasa wewe una mimba, hatujui umaipatia wapi, ni nini kitatoka baada ya
hapo, .humjui aliyekupa hiyo miba au sio…, ina maana gani hapo, familia zetu
zitaingia matatani kwa mambo yenu mliokuja nayo…’akatulia.
‘Unajua
niwaambie kitu, sisi tulishakubaliana huyu mdada atafutiwe chumba, na biashara,
ajiwekeze, maana akikaa kwenye nyumba za watu mambo kama haya yatajitokeza kwa
wengine, basi awe na kwake, ajihangaikie, tulipanga kumtafutia mtaji..kuna
mambo bado hatujakubaliana na mume wangu, lakini tulishafika hatua ya mwisho,
sasa kama kuna hili la mimba tena,..mmh, sijui itakuwaje…’akasema mama
mmojawapo.
‘Kwahiyo
mume wako ataambiwa ni yeye au ni kijana wako, ..si ndio hivyo, kuwa wao ndio
walimpa mimba au itakuwaje hapo, ndio maana watu kama hawa watakiwa warejeshwe
huko walipotoka…’akauliza mama wa hiyo nyumba
‘Kama
sasa ana mimba tunachohitajia ni yeye atoe ushahidi, kama kweli kapachikwa na
mtu wa familia yangu, lakini yeye, tangia awali nilimuuliza kama kweli aliwahi
kuwa na mahusiano na mume wangu , akasema hana na hajawahi kumuona mume wangu
akiingia chumbani kwake…
‘Mhh…kwahiyo
kumbe hakuna lolote la kuwashinikiza familia yako kaa itafika mahakamani, maana
wanaweza kwenda kushawishiwa na watu fanyeni hivi, nendeni mahakamani, sasa
waende, waone watavyoumbuka,…’akasema mama mwenye myuma.
‘Mimi
nilihsjitolea kumsaidia huyu binti, kama kweli angelikuwa mkweli,
ningelimsaidia kwa namna niliyoona ni bora kwake, lakini akawa muongo,
akanificha ukweli,…sasa atajijua mwenyewe, …’akasema.
‘Je
kama kweli ni mimba ya mwanafamilia yako itakuwaje…?’ akauliza mama mwenye
myumba.
‘Muhimu
ni ushahidi, ..kama aliota ni nani atamshika, ..kama anaficha ukweli ni nani
atamsaidia, naona dunia ikamfundishe, hakuna jinsi hapa,…asije akaja kutuletea
watoto balaa kwenye familia zetu…’akasema
‘Mimi
naona tuliongelee hili sisi wenyewe kwanza maana linaleta picha mbaya,
tukifikia muafaka tutachukua hatua, haina haja ya kuwashirikisha waume
zetu..sasa nyie mabint nendeni huko ndani au huko nje, mkaongee, mtafute njia
gani, sisi tunaweza kuwasaidia, mje na wazo lenye maana, na sisi mtuache
tuongee, lakini mkae mkijiandaa na safari ya kurudi huko kijijini kwenu,
sawa…’tukaambiwa,
‘Lakini
mimi nina kosa gani..?’ akauliza yule mdada
‘Na
wewe ndio chanzo cha yote hayo, unauliza una kosa gani, tukuulize bila ya wewe
haya yote yangelitokeaje, wewe ndiye chanzo, na kwahiyo wewe ndiye mkosaji
mkuu, unastahili adhabu kubwa sana, na adhabu yako ni kurejeshwa huko makwenu,…’akajibiwa
na yule mama, mfadhili wangu wa kwanza.
‘Lakini
nilishawaambia kisa na sababu …nilijitolea kuja kuusema ukweli, ili mjua
kinachoendelea hivyo mimi nilifanya kosa,…’akajitetea.
‘Ndio
maana tunataka nyie make waili muongee, mtafuta njia nzuri ya kulimaliza hili,
kama mtahitajia msaada wetu, sawa, na sisi tutaliongelea kivyetu, tuna mambo
yetu mengi tunayaongea hii leo, na hili limekuja tu, litatupotezea malengo yetu
ya maendeleo,..kwahiyo nendeni mkaongee huko…’akasema yule mama mfadhili wa
kwanza.
‘Na
mimi nawapa ofa, kwa leo, na kesho na kesho kuwa mtakaa humu ndani kwangu , mtakaa humu, mtakula,
lakini mtanisaidia kazi, huku nikitafuta mfanyakazi mwingine, huku mkijifungasha
virago vyenu tayari kwa kuondoka, na kama kuna lolote la ziadi, tutaangalia,
mimi ndiye kiongozi wa kundi letu na maamuzi yangu ni mwisho, nendeni…’akasema
mama mwenye nyumba.
‘Au
mimi niulize tu, maana nyie mnawajulia zaidi hawa mabinti wawili zaidi yangu,
huyu bint, ailetwa kwangu, na mume wangu na sikutakiwa kuuliza, kwa vile ni
mgeni, ..nilikubali nilijua njia ya mnafiki ni fupi…niliambiwa kaja kwa muda,
mara naona mwezi huo, mara kumbe mgeni kaja na mzigo tumboni, sasa nauliza,
huyu anasema sio kusudio lake, kuna mtu kasababisha hivyo, wao si wanamfahamu,
sasa watuelekeze sisi tutawasaidia kupambana na huyo mtu, kama ni kisheria, au
vyovyote inavyowezekana,..’akasema yule mama aliyenipeleka hospitalini.
‘Wanadai
ni mchawi mmoja kutoka huko kijijini kwao…’akasema mama fadhili wa kwanza
‘Mchawi
tena ni yale yale niliyoyapiga marufuku hapa nyumbani kwangu, huyu binti
alikuja na hadithi ndefu, kuwa kuna mchawi anaweza kuingia usiku akafanya hivi
na vile, nikamwambia wee, ishia hapo hapo, hapa nyumbani kwangu kuna ulinzi ,
mchai hawezi kuingiza mguu wake humu….’akasema
‘Je
hakuwahi kupiga kelele za kuota usiku…?’ akaulizwa mama mwenye nyumba.
‘Thibutu,
angepiga ningemuonyesha kazi, hakuna cha uchawi au shetani anaingia humu ndani
kwangu ninajua nikwanini….nilimpiga marufu, na nilimuambia kama ataleta mtu wa
namna hiyo, yeye, na huyo mtu wake, watakwenda jela..’akasema mama mwenye
nyumba.
‘Kumbe
wachawi wanaogopa jela…’akasema yule mama mlezi wa kwanza..
‘Hebu
tuambie, ni nani huyo mchawi aliyewafanyia hivyo, je ndiye aliyemfanyia
mwenzako hivyo, na huenda ndiye alimpa mimba, ili wasingiziwe wanafamilia…’akasema
yule mama aliyenipeleka hopsitalini.
‘Atuambie
huyo mdada wa kwanza…’akasema yule mama mfadhili wa kwanza.
‘Ndi-ndi-
ndio yeye, aliyesababisha yote hayo, lakini sina uhakika na hiyo mimba ya huyu…’akasema
‘Na
awali ulikuwa na dalili ya mimba ulipofika hapa kwangu, ilikwenda wapi hiyo
mimba…?’ akaulizwa
‘Mimi
sijui, ilipoteaje..’akasema na akina mama hao wakaangaliana huku wakionyesha
uso wa kushangaa.
‘Mimba
imepotea, hahaha, kwa vile nilimuambia kama ana mimba basi afungashe, kwani
kidogo alianza kunisumbua, anaumwa, ..nikahangaika,..baada ya kutoa hivyo
vitisho, aah, akajirudi, lakini kwa hili sasa simtaki tena…’akasema
‘Sasa
huyo mtu wenu, unayemuita mchawi, yupo wapi..?’ akaulizwa
‘Alikuja
hapa dar, akasema anakwenda kutibiwa…’akasema
‘Mlionana
naye wapi…?’ akaulizwa
‘Ali-ali-kuja
hapa nyumbani…akasema huyo mdada kwa mashaka.
‘Ni
yupi huyo,..lini, ooh,.. ni yule jamaa alikuja akasema wewe ni ndugu yake, kumbe familia yenu
ni wachawi eeh,…’akasema mama mwenye nyumba.
‘Hapana
sio ndugu yangu yule, alisema hivyo tu, ili aweze kuongea na mimi….’akasema
‘Unaoan
jinsi ulivyo muongo, siku ili ulituambia nini mimi na mume wangu kuwa huyo mtu
ni nani wako…’akasema mama mwenye nyumba
‘Niliogopa
kusema ukweli maana hata mimi sikutaka aendelee kunisumbua, ndio nikamfukuza,
…’akasema
‘Je
tutampataje huyo mtu, kwa kuwasaidia, ili wajibike, kama mimba ni yake
ahakikishe anamtunza mwenzako tutampataje..?’ wakauliza
‘Alisema
kaja kutibiwa, sasa sijui kama kaondoka au la…’akasema mdada
‘Anaumwa
nini, huna namba yake ya simu..?’ akaulizwa
‘Anasema
anaumwa mguu umevimba, kaja kutibiwa, namba yake nilikuwa nayo nikaifuta,
sikutaka kuwa na mawasiliano naye …’akasema mdada.
‘Ni
kweli nakumbuka huyo jamaa alipofika hapa, alikuwa anachechemea, na ilionyesha
wazi mguu mmoja umevimba, kama ana tege, la mguu mmoja, na ulikuwa unatoa
harufu , au..ilikua ni harufu ya nini sijui, sikukumbuka kulifuatilia hilo,…’akasema
‘Mimi
sijui kama ulikuwa ukitoa harufu, ila alisema anahitajika kutibiwa na kama nina
pesa nimkopeshe…’mdada akasema
‘Hahaha,
ndio huyo aliyetaka kukuoa, na sasa anataka kukukopa mmh, una pesa nyingi wewe,
utuambie umezipatia wapi…?’ akaulizwa
‘Simtaki
kabisa,..nilimkataa,na kumkataa ndio chanzo cha yote hayo. Na sikuwahi kumpa
pesa nilimfukuza…’akasema.
‘Sawa,
sasa nyie kayaongeeni yote hayo..ila msimamo wetu ndio huo huo, …lazima muhame
huu mji, maana mkindelea kubakia hapa, mtawatia wazimu waume zetu, wanaojifanya
kuwajali sana…mnasikia, kaongeeni muone sisi tutawasaidiaje na mkitaka tunaweza
kukutana na huyo mtu mnayesema ni mchawi, sisi tutapambana naye, hatuogopi
uchawi…’wakasema wakigongeana mikono.
Mara
simu ya mama mwenye nyumba ikalia, na akaipokea, na kuuliza
‘Wewe
ni nani..?’ akauliza na kusikiliza
‘Unataka
nini..?’ akauliza
‘Unamtaka
aje hospitalini, wapi,…?’ akauliza
‘Ocean
road, kwani wewe ni nani kwake..?’ akauliza na kusikiliza
‘Aaah,
ndio wewe eeh, ulikuja hapa siku ile, aheri umepiga simu, tunakutafuta sana,
sasa sikiliza tutakuja huko hospitalini, tuna maongezii na wewe, wewe si mchawi,
au sio…’akauliza na kusiliza.
‘Hahaha,
ulikuwa mchawi na sasa umeacha, kwanini umeacha, uchawi wa kurithi utauachaje,…?’
akaulizwa
‘Nini…usamehewe,
mbona wewe hukuwasamehe uliokuwa ukiwatendea hayo maovu yako..?’ akaulizwa
‘Kwahiyo
wewe unataka nini sasa…, msaada wa kutibiwa, mchawi anaumwaga.. ..huyu mdada
atapatia wapi pesa, anikopeshe mimi, haaa, mimi ni benki wa kukopesha watu… na
atazirudishaje,..hahaha, wewe kweli umepagawa kwa mshahara gani alio nao yeye, na kwanini yeye akugharamie hivyo, wakati wewe
….nini, unataka kuwaondolea nini,…mazindiko ndio nini…mmh, haya ..subiri
nitakupigia…’akakata simu
‘Mumesikia
jamani, nilikuwa naongea na mchawi mwenyewe…hahaha’akasema na wale wengine
wakatulia.
‘Anasemaje..?’
akaulizwa.
‘Anasema
anahitajia msaada wa kipesa, anahitajia pesa kwa ajili ya matibabu, anatakiwa pesa
nyingi tu, milioni kadhaa, sasa anataka huyu mdada akope kwangu,..watu wa ajabu
sana hawa…’akasema
‘Akope
kwako kwa vipi…?’ akauliza
‘Anasema
yeye anajua kwa vipi maana asipofanya hivyo hatakubali kuyaondoa, ..mazindiko,
kitu kaam hicho….’akasema
‘Oooh,
kumbe, sasa kayawekaje ..?’ wakaulizana.
‘Labda
tumuulize mpenzi wake…’akasema mama mwenye nyumba.
‘Huyo
sio mpenzi wangu jamani, huyo ni adui yangu…’akasema.
‘Ndio
ananitishia mimi kuwa eti nisipokubali kutoa huo mkopo, hataweza kuyaondoa hayo
mazindiko, kwa wote aliowawekea, na hapa kwangu ameshakamlisha kazi hiyo
tutaanza kupata shida…’akasema.
‘Hahaha…hawa
watu wanachekesha, halafu anatishia, kwa kujiamini kabisa, mtu anaumwa, badala
ya kuongea vizuri anatishia, hivi..eeh yupoje huyo mtu..?’ akauliza yule mama
aliyenipeleka hospitalini.
‘Sio
mtu mzima sana, nashangaa kwanini kajiingiza kwenye mambo kama hayo…’akasema
mama mwenye hiyo nyumba.
‘Mimi
naona,…tukakutane na huyo mchawi, maana kwanza kama kwli ni yeye aliingia
kwenye nyumba yangu akafany ahayo aliyoyafanya , nahitajia kuonana naye , na
atanitambua, ..kuna ushahudi ninao, .. waonyesha kweli aliingia, …sikutaka
kuliingilia sana hili, maana nitakuwa naamini mambo ya kishirikina, lakini kwa
vile keshaanza kututushia amani, basi kesho twendeni huko, hata leo ikiwezekana…’akasema
yule mama mfadhili wa kwanza
‘Na
wewe kama hiyo mimba ni kwake, basi tukifika pale sisi tunakubidhisha kwake,
mtajuana wewe nay eye, unasikia, sasa hili limefika kubaya, mtu anayetishia
amani mwenzake, anakuwa katenda kosa, sasa atapambana na polisi…’akasema yule
mfadhili wa kwanza
‘Ngojeni
kwanza niwasiliane na mume wangu, hajui kuwa mume wangu ni polisi, eeh, ngoja,
hapa sasa inabidi tuwashikirishe waume zetu, atanyea jela…’akasema mke wa hiyo
nyumba.
WAZO LA LEO: Kuna watu wengine wanaona ufahari kushindana
kwenye kesi, ugomvi, malumabano hata kama kuna njia nyingine mbadala, kila
jambo wao wanalijenga ligi ya ushindani, hata kama ni jambo la kusameheana tu,..ugomvi,
shutuma, visasi na uhasama imekuwa ni hulka zao. Kusameheana ni jambo lenye
kuleta heri, na maridhiano ya kujenga mshikamano ndio njia ya salama ya kuleta
amani. Tusikimbilie kuonyeshana ubabe, ubabe hauabna heri kamwe, bali tuwe na
tabia njema ya kusameheana, kusaidiana na kuhurumiana, na mola ataleta heri
zake.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment