Mzee aliona mkewe anachelewa kurudi, akamtafuta kwa simu, hakupatikana, hakupenda mkewe aende huko kabla hajagundua ukweli, hakupenda kumuambia mkewe ukweli, kwani alijua akimuambia,...mke hatamsamehe, lakini hadi sasa hajaamini, ..
Na kwa jinsi mkewe alivyochelewa ndivyo alivyozidi kuingiwa na mashaka, huenda kuna jambo jingine limetokea kwa mkewe;
***********
Usiku ukaingia na Mzee hakuweza kuvumilia tena, huwezi kulala
huku hujui mke kaenda wapi, au amekutwa na masahibu gani… kwa haraka akaingia
ndani ya chumba chake maalumu, huko alikuwa kaweka silaha yake maalumu na
vitatu maalumu.
Hakupenda kabisa
kuigusa hiyo silaha, tangia wahamie hapo, alitengeneza chumba chake maalumu cha
kuhifadhia kumbukumbu zake za kazi, ikiwemo silaha hiyo na viatu hivyo. Vyote
hivyo alipewa akiwa jeshini, silaha hiyo alipewa kama zawadi, alipokuwa kazini,
wakati huo serikali ilikuwa na ushirikiano na Cuba, kutokana na umahiri wake wa
kazi, na kuibuka kuwa mlenga shabaha mahiri kwa kipindi hicho.
Viatu alipewa wakati wa mashindano ya upelelezi
maalumu akiwa msyari wa mbele, kuwachunguza maadui, siri ya viatu hivyo
ukiviona ni viatu kamili vya kijeshi, lakini chini vimetengenezwa maalumu,…hata
urukue juu kiasi gani ukitua chini havitoi sauti…na vinaweza kukuwezesha
kutembea kwenye ukuta kama paka.
Alipoviona viatu hivyo, mara akaili yake ikamkumbusha
ndoto, au tukio ambalo yeye aliliona kama ndoto, mpaka sasa hajajua kuwa ni
kweli au ni ndoto,maana kama ni kweli basi, …ana kesi ya kujibu, na pia huenda
kafanya kosa ambalo hataweza kulisahau maishani..
Binadamu kichwa chake ni cha ajbu sana, muda wa
sekunde kadhaa unaweza kukumbuka tukio la siku nzima,..hapo akiwa ndio
anakishika hicho kiatu akakumbuka ilivyotokea…
Tuendelee na kisa chetu….
***********
Alipovigusa vile viatu…, ndio akakumbuka kitu, kwanza
akashindwa kuelewa, ilikuwa ni ndoto au ni kweli, anachokumbuka, ni kuwa,
alipokuwa ndani…, alihisi mwili ukimlegea,…akili ikawa kama sio yake, na mara
ikaja nguvu fulani inayomvuta kuwa aende mahali fulani, na bila hata kuwa na
utashi wa kujizuia, akafanya hivyo, kuelekea huko anakovutika kwenda, …
‘Fanya hivyo haraka , ukamuokoe binti yako, usipofanya hivyo bint yako atauwawa..’akaambiwa
kinamna ambayo haelewi kuwa anaambiwa au anahisi hivyo.
Na ili
athibitishe hilo,…kuwa binti yake yupo matatani, basi kwanza aende kwenye nyumba
yake ya zamani-makaburini! Ile nguvu ikamvuta, na kufanya hivyo akachukua
bajaji na kwa haraka akafika huko…na cha ajabu kweli alimuona bint yake
akiingia kwenye hilo jengo.
‘Kweli yule ni binti yangu, lakini mbona anatembea
vile, ana nini binti yangu…’akawa anajiuliza kwani alimuona binti yake akitembea
kiaina yake, sio utembeaji wa binadamu wa kawaida..kama roboti, kama kunyata
lakini kwa haraka.
Akataka
kumuendea ili aone kama binti yake yupo sawa, lakini kuna hali ikamzuia,
akiambiwa hana muda wa kufany ahivyo, anatakiwa kufanya jambo jingine ili
kumuokoa binti yake.
'Ukitaka umuokoe bint yako kwa haraka, kwani yupo
matatani, wewe unatakiwa uende kwenye lile gorofa kubwa linalojengwa na upande
hadi juu kabisa…huko utaweza kumuona kule alipo, na utapata maelekezo zaidi!’
akaambiwa.
Basi akafanya
hivyo,…akiwa na hamasa kubwa, kwa haraka, akaanza kupanda kuelekea juu, akiwa
na vile viatu alikuawa mwepesi sana, na aliweza kuruka ngazi tatu kwa wakati
mmoja, na alipofika juu, akaona silaha…
‘Silaha…’ akajikuta akitamka hivyo.
‘Ndio hiyo ni silaha ya kumuokoa binti yako…hiyo ina
darubini utamuona binti yako akiwa kule kwenye jango lako…’akaambiwa.
Bila kubisha akaisogelea ile silaha,uzuri wa silaha
hiyo, unaweza kumuona mtu akiwa mbali na hata kumuua mtu akiwa mbali sana…moyoni
akawa na hamasa, ya kumuona binti yake, na kumuhami na adui yoyote, akaiweka
ile silaha vizuri.
'Unaona silaha hiyo, itumie darubini hiyo uangalie
kule kwenye jengo lako, utamuona mtu aliyetumwa kumuua bint yako,…umuwahi kabla
hajafanya hivyo, nia yako ni kummaliza binti yako kabisa…’akaambiwa.
Mzee kusikia
hivyo hakuchelewa, akaichukua ile darubin na kuangalia kule, kwenye jengo lake,
na kwa muda huo dirisha la kile chumba ambacho bint yake alikuwa akikitumia wakati
ule walipokuwa wakiishi,…alishangaa hata dirisha lipo wazi! Na walipohama
nyumba hiyo, waliacha kila kitu, kitanda makabati…
Mara akamuona mtu akiingia kwenye chumba hicho cha
binti yake akiwa na bastola mkononi,…sasa anatembea akionekana kulenga ile
bastola muelekeo wa sehemu anayolala binti yake,..taswira ikamuonyesha binti
yake kama anapiga yowe la kuogopa,..kapanua mdomo kama anataka kupiga yowe
lakini sauti haitoki,…mzee akahamaki.
‘Wewe..kwanini unataka kumuua binti yangu…’akasema na
mara ila hali ikamwambia;
'Umemuona adui
ya bint yako huyo…, ukichelewa tu bint yako anauwawa, sasa wewe cha kufanya
umuwahi huyo binti kabla hajamuwahi binti yako…, silaha hiyo, sizani kama
umesahau jinsi ya kuitumia..na shabaha unayo, kazi kwako…’akaambiwa.
Mzee,
akaichukua ile silaha ikiwa na darubini, akawa anaangalia kule ndani, nyumbani
kwake. Darubin ile ilikuwa na nguvu sana, ni zaid ya nguvu za kawaida, kwani
aliweza kuona vyema kule chumbani kwa bint yake…na zaidi ni taswira kama vile
unaangalia video..ya kuonyesha chumba kizima...
Yule mtu akiwa
na bastola akawa sasa anajiweka sawa kulenga kule alipo bint yake, akiongea
maneno ambayo hakuweza kuyaelewa na binti yake akawa kama anaomba msamaha…, na
mara binti yake akachomoa bastola…
Mzee akasita..binti yake kapatia wapi hiyo bastola….
'Mzee
ukichelewa bint yako anauwawa..lakini macho yake sasa yakavutwa kuangalia
kiwambo cha kufyatua bastola cha yule mtu ili aone jinsi gani anavyofyatua…
Akaona kidole
kikianza kuvuta, na yeye, akashika cha kwake, akijua sasa kachelewa,
mara...yule kule akafyatua na yeye akawa keshatangulia kufyatua, aliona risasi
kule ikitoka kuelekea kwa bint yake na wakati huo huo risasi ya silaha yake ikielekea
kwa huyo binti…
Ilikuwa kama movie…unaona risasi inavyokwenda kwa bini
yake,..anatamani kuizuia…, risasi inampiga binti na muda huo risasi kutoka
kwenye bunduki yake ikimtoboa huyo mtu kichwa, lakini keshachelewa,…Yule mtu
alirushwa na kulala sakafuni, kule kitandani binti yake ananyonga na
kutulia..kuashiria na yeye…oh, alishindwa hata kuvumilia, akapiga ukelele wa
nguvu.
'Unaona huo ni uzembe wako, nimekuambia umuwahi huyo
mtu,…ukajifanya kuonyesha huruma, umesahau vita, adui yako akikuwahi umekufa,,
dawa ni kumwahi yeye,…sasa jamaa kamuua bint yako , na wewe umemuua huyo mtu, lakini
yote hayo ni kwa uzembe wako…ndio maana mke wako hakuamini, huwezi kulinda
familia yako wewe…’akaambiwa.
Mzee akasukuma ile salaha mbali na yeye, sasa akitaka
kuteremka pale kuelekea chini hadi kule kwenye nyumba aone kama anaweza kumuoko
binti yake, labda risasi ile haijamuua..lakini akakumbuka alimuona binti yake
kabisa akiwa na dalili za kukata roho…
‘Oh, ni nini hiki, kwanini…’akawa analalamika
Sikiliza mzee
wewe umefika vitani, risasi haina mchezo,…lakini hata hivyo ujue bado upo
vitani, sasa kaa ukilia hapo askari waje kukukamata ushindwe hata kuja kulipiza
ka binti yako… ondoka hapo haraka, askari watakuja kukukamata,..’ile hali
ikamuambia, na hapo kweli akagundua hatari iliyopo …
Basi akiwa hata
hajielewi,..keshachanganyikiwa lakini hakuwa na mamlaka ya kujizuia amri
ikitolewa fanya hivi unatii tu… akaanza kukimbia kushuka chini, na wakati
anashuka kuelekea chini, mara akamuona
mtu, akiwa kasimama kwenye ngazi,…hakujali
akampita,hakuwa na muda tena…keshasikia king’ora cha polisi…na alipofika chini,
akageuza kichwa kutizama juu, …kumuangalia yule mtu aliyempita ni nani, je
anaelekea juu, au ni fundi tu…
Wakati anamitizama kumbe na yule mtu alikuwa
akimuangalia kwa mashaka, yule mtu alikuwa akimshangaa…wakakutanisha macho…oh!
‘Huyu sio yule
mwenye nyumba yangu ya zamani,..!’ akasema na muda huo hakuwa na muda wa
kuhakikisha, alishaambiwa polis wanakuja, na keshaua, na hajui hatima ya bint
yake…huyo mtu atampigia simu akifika nyumbani kutafuta njia za kumvunga, anajua
yataisha lakini ni lazima amtafute huyo aliyemuaa binti yake…
'Wewe fika
kwako, lala, pumzika, mengine utasikia baadae…’akaamrishwa
‘Haiwezekani…’akataka kupinga lakini hakuweza kuipinga
hiyo amri akajikuta anavutika kwenda kwake.
‘Huwezi kufanya lolote kwa sasa…’akaambiwa
**************
Na kweli alirudi kwake akaingia chumbani kwake na
kulala,…baadae alizinduka wakati mke wake anamuamusha..
‘Wewe vipi mbona unalala na viatu…na hivyo viatu, si
ulisema hutavivaa tena…’akaambiwa na hapo akasimama na kujikagua, hakuweza hata
kumuelezea mke wake,..na muda huo ile akili ya kuingizwa kwenye nguvu za giza
imeshaondoka, na hajui kama kilichotokea ni ndoto au ni kweli, lakini kama ni
ndoto, mbona kavaa hivyo..viatu...viatu vyake maalumu vya kivita ...
'Kwann umelala na hivyo viatu mume wangu, na unanuka
jasho, ulikuwa wapi, unachkua mazoezi, au…maana nikumbavyo, kwa kauli yako,
ulisema hutaki kuviona tena hivyo viatu…na mlango wa kile chumba upo wazi,…kulikoni,
mbona unavunja sheria zako mwenyewe…’mke wake akamuambia.
‘We acha tu mke, ….sijui, …hata sielewi..ngona
nivirudishe huko ndani,…maana hata siwezi kusema lolote nimechanganyikiwa…’akasema
na kukimbilia kwenye hiyo ofisi yake na kuvirudisha hivyo viatu,…na siku hiyo
akawa mpole, hataki hata kuongea na mtu…
*********
Ukumbuke hapo
ni wakati anavichukua hivyo viatu kutoka kwenye sanduku ambalo huhifadhi hivyo
vitu, na ukumbuke sasa yupo na akili zake timamu, sio kama ile awali alikuwa
kwenye hiyo hali isiyoelezeka,… sasa akaiendea dhamira yake, kwenda kupambana
na hao watu,…akavaa viatu vyake na sasa anaiendea silaha yake.
‘Lakini hata hivyo akajiuliza anakwenda kupambana na nani…!’
Akakumbuka siku…kwenye
hiyo ndoto, au tukio…siku kweli alimuona
mtu wakati anakimbia kuteremka chini ya
lile jengo…hajampigia simu,….na yule ana uhakika ni yule mwenye nyumba, ambapo
waliwahi kapanga awali akianza maisha, ni lazma huyo mtu atakuwa anajua lolote,
ni lazma atakuwa anajua kitu…ni lazima aende kwake leo hii hii…
Na wa pili…wa kumshuku
tu, ni huyo anayemiliki super market,
nduguye na marehemu, …sijui kwanini dhamira yake inamuweka huyo mtu kwenye
makundi hayo mabaya, hana uhakika au ushahidi, aliwahi kumuelezea mkuu wa
kituo, huyo ambaye kaenda likizo, lakini huyo mkuu, hakutilia manani,…na huyo
ni lazima atakuwa anahusika, na kwa vile na huyo mkuu, alimzarau, hakutilia
maanani alichokigundua yeye, japokuwa hakina ushahidi, absi hata huyo mkuu
anahusika.
‘Hawa watu wana kesi ya kujibu, na watajibu tu,….’akasema
akilini akidhamiria kutumia bastola ikibidi kuwatisha waseme…hatajali sasa nani
ni nani..hatajali kuwa huyo alikuwa mwenye nyumba yake, au huyo ni tajiri, au
huyo ni mkuu wa kituo cha polisi…
‘Hawa watu wataniambia…na wataniambia maana nitakuwa
na silaha,…’akasema kwa sauti…sasa akisogeza hilo sanduku la viatu na koti
lenye kuzia risasi, hakuwataka kulivaa hilo koti,…alitaka kwanza kuichukua
silaha yake maalumu.
'Sasa sioni umuhimu wa kuishi, na nikishamaliza hii
kazi na mimi nitajiua, ...nipotee mbai kwenye hii dunia ya mateso…’akasema
akipiga piga kifua…
Alipofikia hapo,
akafunua sanduku, pale anapoweka bastola yake,…cha ajabu kwanza sanduku
lilikuwa limefunguliwa, …halijafungwa na fungua…na alipolifungua kabisa ,
sanduku lilikuwa tupu…na bastola haipo..
Mzee akahisi nguvu…alibakia kukodoa macho yasiyoaamini…na
baadae akasema kwa sauti,
'Ni nani huyu kachukua bastola yangu..'akajikuta
akisema tena na tena…lakini hakuna wa kumpa jibu…,
Na kwa haraka,
na akili za haraka,.. akahisi ni mkewe,
Hakuna mtu anayeweza kufungua chumba hicho zaidi ya
mkewe, hakuna anayejua ufunguo wa chumba hicho zaidi ya mkewe, na jinsi ya
kuufungua mlango huo anayeujulia huo mlango zaidi yake ni mkewe!...Kwasababu
mlango huo unahitajia umakini wake, katika kukizungusha kitasa cha mlango, ni
kama una namba za siri, na mkewe peke yake ndio anajua.
'Sasa kwanini akachukua hii silaha,…kwanini jamani….
mke wangu, kwanini, unajitakia matatizo,na sasa hata sijui, imekuwaje, na kama
ni yeye , najua ni yeye, maana …hapana ni yeye, swali ni kwanini kaichukua na …oh..?!
'akajiuliza
‘Huyu mke wangu anajitakia matatizo...sijui kafanya
nini na hii silaha, maana hiyo silaha kwasasa haina, ...sijaisajili tena,
nilitaka...oh, …hili sasa ni balaa jingine..sasa labda kazidiwa nguvu na hao
watu wameshamuu..a....a…a..hhh!...’mzee akaishiwa nguvu kabisa.
‘Potelea mbali…..nitakwenda hivi hivi, na sime yangu,
kama ni kunimaliza, wanimalize tu…, nina maana gani kwenye hii dunia, watoto
wangu wote wamewaua, sasa mke...mimi nina faida gani kwenye hii dunia…siwezi
kulala hapa nyumbani kama kondoo..nitakufa kama chui….’akasema sasa akiendea
kabatio jingine ambalo kaweka sime maalumu….
Na muda huo tayari alishavaa hivyo viatu…bahati sime
ilikuwepo, akaichukua na kuitwika kiuononi, mara akasikia mlango, ukifunguliwa….
‘Oh, atakuwa
mke wangu, kweli mungu mkubwa…’
Kwa haraka akatoka
kwenye kile chumba huku akihakikisha kuwa amekifunga chumba hicho, kawaida hafanyi makosa, labda
hiyo siku ya tukio ambalo mpaka muda huo hajaamini..ila ushahidi unavyozidi
kutokea, anaanza kuhisi kuwa ile sio ndoto, ilikuwa ni kweli,….na kama ni kweli
binti ni marehemu, na saa mke naye hayupo…labda ndio huyo kaja, kama ndio yeye,
basi atamsimulia kila kitu…
Haraka haraka, akawa anakimbia kuelekea mlango wa
kutoka nje, na wakati anashika kitasa ,
mlango ukatangulia kufunguliwa, yaani yeye analegeza kitasa kwa ndani ili uweze
kuufungua kwa nje, huyo mtu wa nje akatangulia kufungua.
Tahamaki
wanapigana kikumbo na huyo mtu anayeingia kwa kasi ya ajabu kweli ni mwanamke
..na akili yake ishajirizisha kuwa ni mkewe….lakini ule uingiaji wa kasi na mna
ile kulikoni, na kile kikumbo kililimfaya
apepesuke akitaka kuanguka,:
'Aah vipi wewe mbona haraka hivyo....'akasema sasa
akijihami, akijua mkewe labda anafukuzwa na kitu cha hatari….akawa anachungulia
nje kwa tahadhari, mkono umeshikilia sehemu aliyofutika jamvia kiuoni…
Akachungulia
nje, hakuona kitu wala mtu, zaidi ya bajaji lililokuwa likiondoka kwa kasi…,
kuashiria kuwa mkewe kaletwa na hilo bajaji.
‘Oh, mke wangu naye,…’akasema sasa akigeuka kuangalia
huko mkewe alipo..
Sasa akageuka, akijua atamkuta mkewe kasimama karibu
yake…., akimsubiria, akijua yeye kakasirika, kwahiyo…lakini ..kitu cha kwanza
kumshtua ni nguo...
Alitangulia kuziona nguo kwasababu, huyo mtu, aliyejua
ni mkewe, sasa kampa mgongo, anaelekea eneo la vyumba..na anakumbuka kabisa mkewe
hakuwa amevaa hizo nguo wakati anaondoka…Na ni nguo za hospitalini…ina maana
mke labda aliumizwa akalazwa..sasa katoroka hospilaini….akawaza hivyo!
Mzee akainu amguu kumfuatilia …lakini kabla mguu
haujainuka,…yule mtu, ambaye sasa anahisi ni mkewe..akageuza kichwa,,...
Mzee alihisi mwili
ukiwashtuka….macho yakimtoka,..akili ..ikawa kama …kitu kikichoma kifuani,
akahisi mlio fulani kichwani,..nziiiiii, na hapo hapo giza likatanda usoni!
NB: Ni kazi kweli kuiweka sehemu hii kama hivyo, lakini tupo
pamoja,
WAZO LA LEO: Ukipenda kutendea wenzako ubaya, ukipenda kuwaumbua
wenzako na kuwafichulia aibu zao, ukapenda kuwatangaza wenzako ubaya hata bila
ya kujua ukweli halisi, …kwako waona raha tu..ujue na wewe ipo siku utafanyiwa
hivyo!
Swali,…je wewe ni kazi yako, kisheria, kufanya hivyo, hapana…ila
wafanya hivyo kutafuta sifa, biashara ya mtandao wako, sawa utapata watazamaji
wengi,…yawezekana kwa mtizamo wako unawakomoa hao watu,…au kama usemavyo,
unawafanyia hao watu hivyo ili wajirekebishe, ..lakini je ni kweli….na je ni
sahihi, kuweka aibu za wengine mitandaoni, picha za uchi, picha za kebehi,
kuzalilishana…kiukweli sio vyema,sio uungwana, sio hekima, sio busara, sio utu!
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment