Mimi nikiwa kwenye sehemu ambayo nimekuwa kama
nimegandishwa, niliweza kusiki akile kinachoongelewa kwenye sehemu nyingine ya
chumba na kwa muda huo niliweza kumsikia binti akipambana na hao watu kwa
maneno, akilalamika kuwa wamuachie…na mara huyo kiongozi wao akasema kwa sauti
kali;
'Muda umekwisha, ...mleteni huyo bint huku, tusipoteze
muda….na mara kukawa na vurumai baadae akaletwa …niliweza kusikia sauti lakini
sikuweza kuwaona na iliyonisaidia ni kuwa mlango ulikuwa umefunguka kidogo,
lakini kufunguka huko siwezi kuona huko walipo, na siwezi kusogea hapo nilipo…
Na mara
kukasikika sauti ya binti akilia, akiomba asifanyiwe huo ubaya, na wakati
analalamika ndio kukasikika sauti nyingine, ilikuwa ni sauti ya kike, lakini
yaonekana ni sauti ya mama hivi;
‘Subirini kwanza…’ilikuwa sauti ya kike lakini sio ile
ya binti…
‘Wewe….unataka nini huku…’sauti ya huyo kiongozi
ikauliza.
‘Achani, mnataka kufanya nini…?’ akauliza
‘Haya hayakuhusu wewe..rudi huko ulipokuwa…’akaambiwa.
Na mara huyo binti akawa analalamika, kuomba msaada
zaidi
Tuendelee na kisa chetu….
****************
'Sitaki jamani, nimechoka…, niacheni, mnaniumiza...najua
mnataka kuniua, kwanini lakini, ....sitaki...mama upo wapi,…mama jamani …baba
…oh, nimewakosea nini hawa watu, kwanini hivi jamani, niacheni jamani..’ilikuwa
sauti ya binti.
Huyo binti yawezekana ana miaka kama kumi nane hivi,
kwa makisio yangu kwa kukisia sauti hiyo lakini sina uhakika maana sikuwa
namuona sura yake, kiukweli alivyokuwa analia,…nilimuonea huruma sana, mpaka
nikatamani niende huko nikajaribu kumtetea, lakini nikuembie ukweli, pale
nilipo nilikuwa kama nimenatishwa.
‘Hivi ndio inatakiwa alie, ili shetani wetu,
afurahi…inaniuma hata mimi lakini tutafanyaje….’ilikuwa sauti ya huyo mwanaume.
Mara kukasikika kitu ama vurumai, baadae ikasikika sauti ya watu wanazozana,
sikuweza kujua ni nani..lakini kulikuwa na sauti nyingine ya kike.
'Mshikilie...unafanya nini sasa..mlete hapa, …kwanini,
…mnashindwa kumshika huyo binti,….hahaha, sitaki kumlegeza kwa madawa, shetani
wetu anataka asikie kilio,…manunng’uniko, hayo ndio yanampa raha….halafu damu
yake….hahaha…’ilikuwa suti ya huyo mtu.
Ikatokea tena sauti
ya kuzozana, …baadae sauti hiyo ikapaa hewani, na kusikika vyema, ikasema;
'Hawezi kuja hapo, nimechoka na haya machafu yako,
wewe si ndugu yangu tena, na sitaki kuwasikiliza na kufuata haya mauchafu yenu,
sitaki sitaki, nilishakuambia sitaki, kumbe ndio hii kazi unafanya,…hapana,wewe
ni shetani….’ilikuwa sauti ya mwanamke, anaonekana ni mtu mnzima.
'Unataka kufanya nini dada,….unapoteza muda, kwanza ni
nani kakuambia uje huku,…hii kazi ni ya wanaume, na …nakujua wewe hutaweza
kuvumilia,…na muda unakwisha dada,…unaona sasa imebakia dakika tano tu,
tusipofanikiwa hili, basi, mimi au wewe damu yetu itahitajika..upo tayari kufa
eeh, hebu niambie..’akasema huyo mwanaume.
'Mimi sijali
kufa,..kama mambo yenyewe ndio haya, ..hapana ni bora kufa tu, na nimegundua ni
wewe utakwua umemuua mwanangu…nimeshajua hilo,..na huyo binti yangu mwingine yupo
wapi…unataka na yeye umuue au sio…kwanini unakuwa mnayama , shetani…’sauti ya
kike
'Bint yako yupi..yule hatuna kazi naye,
nilishakuambia, hatuna kazi naye, kazi yake uliiharibu wewe..sasa hivi
tungelikuwa tumemaliza kazi…sasa unanipa wakati mgumu,.huyu binti wa watu
hakustahiki kuwa hapa….unaona …sio kwamba mimi napenda…’akasema huyo mwanauma
'Usinifanye mjinga, niambie binti yangu yupo
wapi…’akasema
‘Jamani binti yake yupo wapi,… niliwaambia huyo binti
hana kazi tena kwetu, arudi kwao,
sasa…mlifanya nini..?’ akauliza na kukawa na ukimiya baadae akasema;
‘Dada nasikia ni watu wenu…muulize huyo anayeitwa
docta,…huyo mtu mbaya sana, na ole wake, ngoja tumalizane na hili…huyo ni adui
yetu, mkimuona msisite kuvuta trigger…maliza, ua..mumesikia, mtu atakayelata
kichwa chake hapa nitampa dola elifu kumu, mumesikia…’akasema na kukawa na kama
vurumai halafu sauti ikasema…
'Dada kuhusu binti yako mkubwa, nilikuambia wazi
alijiua kwa sumu…hayo ni majanga uliyojitakia wewe mwenyewe, hukutaka kufuata
niliyokuambia,…sikuwa na jinsi ya kuweza kumsaidia, ..hata hivyo, siku zake
zilishafika au sio jamani…’akasema na kukawa na ukimia.
'Unafikiri mimi mjinga eeh…najua kabisa wewe uliamua
kumuua kwa mbinu za sumu, kisa unataka mazindiko yako yafanikiwe,…na shukuru
mungu huna watoto, ungekuwa nao ..ungelijua uchungu wa mtoto, usingelifanya
hivyo…’akasema mwanamke.
‘Sikiliza dada mimi nakuheshimu sana, ndio maana
nikakutaka uwe mwenza wa kazi hizi, ningelikuwa na roho mbaya nisingeku…lakini
wewe huna shukurani, mali zote hizo nimekuambia ni zako..nyumba hii ni
yako…mumeo, hana kitu tena…lile duka la..super market ni lako…..huyo ndugu yako
ni…usitake niseme mengi…’akatulia.
‘Kwanini mnapoteza muda..huyu mchukueni mrudisheni
huko chumbani, tukimaliza kazi atakuja, najua dawa yake ni nini..na kama
unaleta ubishi dada…, mtoto wako hutamuona tena, nakuambia sasa ukweli..unanijua
nilivyo…’akasema kwa ukali.
‘Nimeshakuambia uniue tu..hapa sitoki mpaka
nihakikishe umemleta binti yangu, pili..uape kuwa hutaingilia familia yangu
tena,…kwanini familia yangu,..nenda kazae wa kwako, ndio uwafanya ndondocha,
shetani mkubwa wewe…’akasema huyo mwanamke.
‘Hahaha..dada uniniita jina ambalo tayari
ninalo…shetani, mimi ndio dunia yangu, kwani kwenye dunia halisi naonekana mtu,
lakini mimi sio mtu..hahaha, siku nilipopewa huo moba, uliouktaa,a nilisema
nataka niwe kama mfalme…hahaha, sasa unaonaje, ..usiku napaa naenda
nitakapo….mchana mimi ni bosi…watu wananinyenyekea, …wewe si utaki,…hahaha,
…’ilikuwa sauti ya kejeli.
‘Nakumbia kila kitu kina mwisho wake,..mungu ni
mkubwa, najua..wewe ulimuua binti yangu, wewe umemuua, ndugu yako
mwenyewe….ulikuwa ukimtumia, kama mtumwa wako…lakini huna shukurani…unafikiri
utaishi milele…ipo siku…utakufa na kifo chako..sijui,…’akasema.
‘Kufa nitakufa najua kabisa lakini ni nani hata
kufa,..hata hivyo kabla ya kufa, najua nitakuwa nimefanya jambo, dunia hii
itanikumbuka….ni nani angelijua hapa nchini …ninatawala…hahaha, hawajui, lakini
siku watajua, ..watanikumbuka…mitandao yote hiyo, nina ….hahaha, watu kila siku
wanatukuza, hawajui tu….sasa hili,likipita najua kabisa, nitaogopwa…’akatulia
‘Halipiti na hutafanikiwa, labda nife…’ilikuwa sauti
ya kike
‘Usinilazimishe dada kufanya nisichotaka
kukifanya..kama unataka wewe ugeuke tambiko…, itakuwa vyema,..amua tumuache
huyo binti wewe uchukue nafasi yake… utafaa sana kuwa kafara la leo…’sauti
ikasema
‘Kwanini wewe usichukue nafasi yake..wewe hufai kuishi
kwenye hii dunia ya watu, wewe ni shetani, unafuga mashetani, unaishi na
mashetani… na sasa unataka kuharibu dunia hii iwe ya mashetani…, kwa kuwekeza
mashetani yako kwenye mitandao, ili watoto wetu wote wawe watumwa wako, si ndio
hivyo…’akasema.
'Dada, unajua
unachokitaka…unanilazimisha nisiwe na jinsi nyingine…mimi nakupenda sana ndio
maana nimekuwa nikitafuta mbadala wake…na kila nimekuap ahadi nyingi tu…unataka
nini wewe…ukumbuke haya mambo yanakwenda kwa muda.., huo sio muda wa
kulumbana...askari, hebu mshughulikieni huyu mama…’ akasema na mara kukasikika
vurumai, mara milio ya risasi...
'Aaaah....'kilio cha maumivu
‘Umetaka mwenyewe,…’sauti ya kiume na mara kukawa na
vurumai, mara…
‘Tumeingiliwa, askari
maliza wote...hakikisha unawamaliza….maliza…’
Kulisikika milio ya risasi, baadae kukawa kimia..
********************
Docta aliyekuwa akiangalia haya yote kwenye komputa yake, akaona
mkuu atashindwa kudhibiti hiyo hali kama hatamtahadharisha, ….kwani kwa nje
kulikuwa na mtu mwingine ambaye anaonekana ni mmoja wa hilo kundi,kaja na watu
wake, wanaonekana wamejidhatiti na silaha…na huyo mtu, alikuwa akitaka kuingia
ndani.
‘Huyu ni nani…’docta akawa anajiuliuza.
Mara yule mtu akawa kama kashtuka, anataka kurudi, lakini akatokea
mtu mwingine aliyekuwa pembeni, atakuwa ni askari wa mkuu, akamshika yule mtu,na
walinzi wake wakataka kuingilia kati lakini yule mtu akawazuia walinzi wake
wasifanye kitu, akawa anaongea na huyu
askari,…
Tendo hilo la huko nje, lilimfanya docta ashindwe kuangalia upande
wa huko ndani na kuona ni kitu gani kinachoendelea kwa muda huo, yule mtu akawekwa mikononi mwa askari
waliokuwa nje..na walinzi wake wakawa wananyng’anywa silaha..haikuleta vurumai…
‘Huyu mtu ni nani…’docta akawa anaingiza picha kwenye kumbukumbu
zake, na mara jina likatokea…
‘Haiwezekani…’akasema tu, na baadae akaachana na sehemu hiyo,
akarudi ukumbini na muda huo ndio vurumai zimeanza, risasi,…polisi wakaingia,
…kukawa na kutupiana risasi, na huyi kiongozi wao akaanza kukimbia, na sasa
alikuwa akielekea pale alipojificha msaidizi wake, ikabidi afanye namna ili
msaidizi wake ajifiche sehemu.
Na mara mtu huyu ambaye anaonekana kama ni kiongozi wa hilo
kundi akatokea pale alipokuwa msaidizi wake awali , akawa sasa anatafuta nafasi
ya kukimbilia,…na ghafla, msaidizi wake akatokea kwa nyuma na kumpiga huyo
kiongozi kitu kwenye kichwa na huyo kiongozi akadondoka chini…
Na muda huo watu wa huyo kiongozi wakawa wanakuja kutaka
kumsaidia mtu wao, na mara ..polisi
wakatokea…risasi zikarindima.
Haikupita muda, wote wakawa chini ya ulinzi, na yule
kiongozi bado alikuwa kalala chini..kapoteza
fahamu…
‘Huyu ni kiongozi wao, sawa, lakini ni nani..maana hii sura haipo
kabisa kwenye kumbukumbu zangu, huyu ni nani…’docta akawa anajiuliza bila
kupata majibu ya haraka, lakini wazo likamjia akagundua kitu.
Akaona ampigie simu
msaidizi wake,..hakutaka kumpigia mkuu mbaye kwa muda huo alikuwa na shughuli
nyingi sana.
‘Sikiliza fanya hivi…huyo kiongozi wao, anaweza akatupotea,…
japokuwa yupo mikononi mwa polisi,yaonekana hiyo sura yake, sio yeye, atakuwa
ni mtu mwingine kabisa, atakuwa kafanya
jambo…’akasema docta
‘Nifanyeje..?’ akauliza
‘Kwenye kichwa chake, hebu chunguza, atakuwa kavaa, sura ya
bandia…’akasema docta na msaidizi wake akamuendea huyo kiongozi askari walitaka
kumzuia, lakini mkuu akasema;
‘Wewe unataka kufanya nini..?’ akauliza huyo mkuu.
‘Huyu mtu kavaa sura ya bandia…’akasema msaidizi wake.
Na mkuu naye akavutika na hiyo taarifa, akamsogelea huyo mtu, na
kumshika usoni, akavuta kitu,…ooh, ni kweli, ilikuwa kama anabadua ngozi kwenye
uso wa huyo mtu, na sura ya nje
ikatoka..kweli alikuwa kava ngozi ya bandia, …na watu wote wakabakia midomo
wazi…haiwezekani….hata watu wake hawakuamini….
‘Ni wewe….’akasema msaidizi wa mkuu.
‘Haiwezekani, siamini….’na mara huyo mtu akaporomoka na
kudondoka chini,…akapoteza fahamu!
****************
Docta akajua kazi hapo imemalizika, iliyobakia ni kazi za
polisi, watajua wenyewe..ila akahisi lolote linaweza kutokea, lakini hakuwa na
la kufanya, yeye akarudisha mitambo yake sehemu ya pili, huko alipokuwa mpelelezi,
kwanza aliivuita sehemu hiyo hadi awali, ili kujua kilichoendelea, tangia
aachane na mpelelezi alipofika humo ndani.
Mpelelezi alikuwa kakamatwa, kawekwa kwenye kiti, kiti hicho ni
cha maalumu cha kuulia watu, ni cha umeme…na watu wale walisubiria amri kutoka
kwa bosi wao, lakini amri ilikuwa inachelewa, hawakujua kuwa mawasiliani
yamekatika,..na hapo ndio docta akatoa amri, kuwa mtu huyo aoandelewe hapo
apelekwe chumba kingine
Watu hao walijua kuwa ni amri ya bosi wao, maana hapo huwa
wanawasiliana kwa mitambo…tu, ni uchawi wa kidigitali…
Mpelelezi alipoachwa kwenye hicho chumba, docta akamzindua
kinamna na kuanza kumuelekeza cha kufanya, mpelelezi akatoka kwenye kile chumba
na kutembea kuelekea kwenye chumba kile alichotaka mpelelezi aende..
Akamuelekeza afungue mlango wa kwenda chini…na mpelelezi akafanya hivyo, na akawa sasa
anasuka ngazi za kwenda chini, ilikuwa ni rahis tu, maana docta aliwaarifu
walinzi waje juu, kuna kikao cha dharura, walinzi walijua ni bosi wao anaongea
kumbe walinzi hao walitegwa kwenye chumba ambacho hawataweza kutoka hadi askari
waje kuwakamata…
Mpelelezi akawa anatembea kuelekea jinsi pango hilo
lilivyotengezwa, na alipofika kwenye chumba fulani, …kipo ndani kwa ndani, hapo
docta akaingiwa na hamu, akamuelekeza mpelelezi akifungue hicho chumba…oh, ni
chumba kizuri tu, kina kitanda na meza,…ni chumba maridadi, na pale kitandani
kuna mtu kalala…ni mwanadada, lakini alivyolala ni kama..hajiwezi hata kuinuka.
‘Huyu ni nani tena..?’ docta akajiuliza , hakuwa na muda wa
kutafuta picha hiyo kwenye mtandao, akamuelekeza mpelelezi aifanye hiyo kazi..
Mpelelezi akasubiria amri…mpelelezi kwa muda huo alikuwa hana
nguvu zake za kawaida,…watu hao walikuwa wamezilegeza nguvu zake za kawaida..,
na kumwekea nguvu zao, anakuwa kama zezeta fulani tu, au mtumwa wao…., lakini
kwa vile ile mitambo sasa hivi inamilikuwa na docta, docta akawa ndiye
anamuongoza mpelelezi.
Mpelelezi, akaamrishwa aende kumkagua huyo mdada, akafanya hivyo…na
docta akatafuta kwenye mtandao, wapi huyo mdada kawekezewa, mpaka akapata hiyo
sehemu,lakini bado picha ilikuwa ngeni kwake,,…akaamrisha huyo mdada azindukane…
‘Wewe ni nani..?’ mpelelezi akauliza
‘Mimi , hahaha, mimi ndiye Mpenzi wa facebook…’akasema huyo
mdada, na docta hakuamini, akarudisha nyuma hilo swali, na alipojibiwa hivyo,
akaikuza ile picha…na taswira ikajaa kwenye uso wa komputa…
‘Ooh…ina maana ndio huyu, haiwezekani,….’ docta akashindwa kabisa
kuling’amua hilo, kwa jinsi gani lilitendeka, akalipa muda wa ziada, kwani kuna
mengi ya kufanya, hakutaka kuuchsha ubongo wake kufikiria kililivyofanyika,
akasema tu;
‘Oh…hatimaye…’akasema docta sasa akianza kutafuta kumbukumbu
zote za huyo mdada ili ikiwezekana, baada ya kuondoa nguvu za giza kwenye huo
mwili wa huo mdada, sasa awe tayari na kumbukumbu za huyo mdada,…na kama
hajamalizwa kabisa basi yawezekana, huyo mdada akaweza kurejea kwenye hali yake
ya kawaida, yote hii itategemea huyo ….aliyemfanya hivyo,..…, na mara simu ya
docta ikaita, akajua ni nani, msaidizi wake anampigia,anasubiria apewe amri
afanye nini…
‘Huyu sasa atakuwa ni mzigo..’docta akasema, akaona jambo jema
sasa ni kuanza kumuondoa huyo msaidizi wake kutoka kwenye minyororo ya hao watu
kwa kuanza kuondoa sumu aliyowekezewa,….docta alijua kabisa hayo yote yapo
kwenye huo mtandao wao wa ajabu…muda ukawa ni muhimu sana akaanza kazi kwa huyo
msaidizi wake huku akiendelea na maelekezo kwa mpelelezi..
‘Kwanza ni kuondoa nguvu za giza za hawa watu..mungu ni saidie
nimalize hii kazi kwa haraka, kabla ya hawa watu hawajaweza kurejesha mitambo
yao…’akasema docta.
Ukumbuke hayo yote sasa yanafanyika kwenye mitandao ya hao watu,
lakini sasa ipo mikononi mwa docta, na ni swala la muda, kama hao watu wataweza
kurejesha mitandao yao,mambo yanaweza kubadilika,…muda ni muhimu sana hapo.
NB: Tutaona itakuwaje, sehemu ijayo..uone jinsi watu walivyoweza
kuwekeza nguvu za giza kwenye mitandao..ni hatari, tuweni makini sana...
WAZO ZA
LEO: Vyo vyote tufanyavyo, tuwe ana akili ya ziada, utundu, ujuzi,
kipaji, elimu , madaraka, utajiri, tukumbuke kuwa kuna mungu, mola ndiye mpaji
wa yoye hayo…, na ili uhakiki hilo, hebu kumbuka wangapi waliokuwa matajiri,
wenye akili, warembo, wenye nguvu, wenye
kila sifa za kila aina, sasa hivi wapo wapi,…Mungu ni mkubwa , mrehemevu,
mwenye kusamehe , tumuabudu yeye na kumtegemea yeye, na kumshukuru yeye
kwa kila mara mara.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment