Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, May 19, 2017

MPENZI WA FACEBOOK-31



Baadae wakawa wanafanya mambo yao,...kila mmoja na kazi yake, na  walipomaliza huyo mkubwa wao akasema;...


 ‘Sasa hapo tusipoteza muda, kwanza tukiendelea kukaa hapa ni hatari, hasa kwangu, mnaelewa nina maana gani, nyie ni mimi. muhimu kwasasa ni kutawanyika kila mtu kwenye mambo yake...

Na kutawanyika hapa ni hivi,...wewe pitia mlango wa kule, wewe ule wa mbele, wewe upande ule, na wewe huku..mumenielewa,..wakainamisha vichwa kukubali

'Hata…tutawanyike, tutarudi hapa kama muda wa saa kumi…naona kwa muda huo itafaa, najua hapo kila kitu kitakuwa  tayari, kila mtu sasa na muelekeo wake…mimi narudi nje ya nchi…’akasema na wakaanza kutoka taratibu, kila mmoja akawa anatokea mlango wake.
'Saa kumi...' muda wa kukutana 

Tuendelee na kisa chetu

************

Docta, alimalizia kazi yake, ilikuwa kazi maalumu akitumia ujuzi wake wa mambo ya mitandao, udakitari na elimu ya mambo ya kienyeji, kwa kadri ya uwezo wake, alijua kuwa huo ndio mtihani wake wa mwisho, kufaulu kwake, ndio anaweza kukamlisha, ‘project’ yake. ..na ndipo atajiona kweli sasa kaiva kama dakitari wa kisasa!

Ilibidi awasiliane na rafiki yake wa nchi za nje, ili aweze kupata maelekezo zaidi,…kama ujuavypo, itafute elimu hata uchina, kwake elimu ilikuwa ni muhimu kuliko, na elimu nzuri ni ile inayowekezeka..usome na uweze kuifanyia kazi, ndivyo alivyotaka yeye, sasa ana ujuzi huo, kwanini asiufanyie kazi,…

Docta kwa kupitia mitandao, na kwa kupitia mawasiliano na marafiki zake, akaweza kuongeza ujuzi wake wa mawasiliano kwa njia ya mitandao ya kisasa.., jinsi gani ya kuunganisha herufi zikazalisha kitu..jinsi gani ya kuunganisha mawasiliano kwa kutumia herufi, au waya…na mambo ya upelelezi kwa kutumia mitandao.

Docta alitaka utaalamu wake uende na wakati, na...sasa ilipozuka hii elimu ya mitandao, akajua huku nako kunahitajia kujifunza, ili kuweza kuona dunia nyingine ipoje, au watu ambao wanataka kucheza na akili za watu kwa nia mbaya wanafanyaje kwa kutumia mitandao, ambayo sio wengi wanaifahamu, kwake yeye, alijua ni muhimu kujifunza ili kwenda na wakati…,

'Ina maana hata udakitari...?' aliwahi kuulizwa na jamaa mmoja, na yeye akasema

'Ndio unahitajika zaidi, kutibu watu na mitandao yenyewe, na ujue ndani ya mitand hiyo kuna magonjwa, kuna virusi, kuna watu wanatumia mitandao kuwaumiza watu wengine, sisi kama madocta tunahitajika kufahamu hayo...'akasema.

Kwa namna hiyo, akaona kuna ulazima wa kusomea maswala ya mitandao, zaidi ya upeo wake...lakini akitumia taaluma yake ya kidakitari zaidi…haikuchukua muda kwake yeye kuifahamu taaluma hiyo,…kichwa chake ni chepesi sana.

 Sasa wakati anahangaika kuunganisha mawasiliani yake na viunganishi mbali mbali ambavyo vingi vipo kwenye miili ya watu, akafika sehemu akakwama, hapo akaona kuna umuhimu wa kuwasiliana na rafiki yake huyo wa nchi za nje.

Alifanya haraka kwuasiliana naye kabla mpelelezi hajafika huko anapokwenda,…na akamuuliza alichotaka kukifanya, akiwa anamuamini,hakumuelezea kiundani yeye alitaka namna ya kuwasiliana, kuonana, na kuzuia mtu kukuona wakati wewe unamuona,..sio uchawi, ni elimu ya mitandao…hapo akapata maelekezo mazuri tu….

 'Hilo unalotaka kulifanya , muda ni kitu muhimu sana,… ‘timing…’ …..’ akambiwa.

‘So ..do like this…kama umeshaweka point ya mawasiliano, kama ni mtu ndiye ponti yako,…na huyo mtu anacho hicho kifaa kama point yako ya mawasiliano..yeye akiingia tu eneo hilo, ujue kama wao wana chombo cha kuhisi, watajua kuwa kuna ‘mwizi’au inasema 'intruder…kwahiyo wewe, unatakiwa, uwe mwepesi, kumlina huyo kwa kumuwekea kinga.

'Cha zaidi ni kuwa pale utakapounganisha mawasiliano yako na kwa huyo mtu akiwa ndani ya hilo jengo au eneo, ujue, na wao watakuona...'akasema huyo mtaalamu.

 'Sasa nifanyeje wasinione huko…ndio hapo nimekwama…’akasema.

'Ukishajiunganisha na huyo mtu, uliyemwekea hiyo waya, ‘whatever’…wewe sasa weka vizuizi hivi....'akamtajia herufi za kuunganisha ili kujificha na kulizuia ili mtu mwingine asiwezi kukuona..

 Baada ya hapo, tuma ujumbe huu,…huu ni ujumbe wenye virusi, vya kuharibu mitambo yao…hairuhisiwi kitaalamu, lakini kwa vile unahitajia kwa manufaa ya jamii, inabidi ufanye hivyo…, na mitambo yao itakuwa haifanyi kazi tena…mpaka waje kuunganisha upya,…kila kitu kwenye mitando yao…na itachukua muda…’akasema.

'Je ujumbe wa virusi hivyo, wataufunguaje wao..?’ akamuuliza.

'Kwasababu, ukiwazuia wao kukusoma huko ulipo, watapata ujumbe kuwa kuna ugeni, ..’intruder..’..yaani kitu kimeingia kigeni, na wao watajua kuna tatizo..na mara nyingi hutokea kama kuna mtu kaweka chombo cha mawasiliano cha nje ya mitandao yao…na wanajua ni vipi kukizuia kama kina madhara..

 ‘Kawaida ikitokea hivyo, mitambo yenyewe hutuma ujumbe wa kujisafisha, kwahiyo, wao wakipokea ujumbe uliotuma wewe, kwa haraka watajua ni huo ujumbe wa kujisafisha,… wataufungua, …na wakiunfungua tu…haraka unaanza kufanya kazi,..wao kwa muda huo watajua kuwa ni huo utaratibu wa kujisafisha… kumbe ndio mitambo yao inaliwa na hao wadudu, na ikianza kuharibu huwezi kuizuia, ‘too late’...watagundua mwishoni, 

‘Ahsante sana..’akasema docta, hakupenda kufanya hivyo , ila hiyo ni vita, na dawa ya hao watu ndio hiyo, wao wanatumia mitandao na nguvu ya giza kuumiza jamii, lakini yeye anatumia kwa manufaa ya uma, hana kosa.

***************

Docta alisubiria, hadi ishara kuwa mpelelezi keshaingia eneo analotakiwa kwenda, ishara ya kuashiria kuwa unywele ule au waya maalumu iliyotengenezwa kwa kazi hiyo, umeshahisi mitambo inayoendana nayo, docta, kwa haraka akaanza kazi…nguvu za giza hazikuwa na nafasi hapo, alishazizima kwa kumuomba mola wake, alijua ni nini akifanye kwa wakati gani…

 Sasa anacheza na mitambo halisi, inayohitajia elimu ya mitandao…’muda hapo ni kitu muhimu…’akakumbuka hilo,…akawekeza zile herufi bila kukosea, na alipohakikisha zipo safi, akazibofya kuwa zianze kazi mara moja…kazi ikaanza..

Ni wakati anamalizia kuhimiza mtando ufanye kazi,  ndio hapo akapokea simu, kuwa mtu wake, yaani msaidizi keshafika sehemu inayohitajika…huyo naye alikuwa akimfuatili hatua kwa hatua, ni sehemu nyingine muhimu ambapo amewekeza ponti ya mawasiliano…akaona ili ampe mataumaini, sasa anaweza kumpigia..baada ya kujiwekea kinga ya kutokuoenakana…

Alipiga simu , huku akiendelea kuangalia maendeleo ya kila anachokifanya,..haitakiwa kufanyika kosa, kosa dogo ataharibu kila kitu na huyo alitewekezewa mitambo hiyo anaweza kuwa kwenye hatari y akugundulikana na matokea yake atauliwa… hatimae akafanikiwa, na alipohakikisha kuwa kila kitu kipo sawa,  akampigia simu mkuu.

 'Mambo sasa tayari kama nilivyokuambia…sio uchawi, ni mitandao.., hawataweza kutuona tena…, ila sisi kuanzia sasa tunaweza kuwaona na kuona kila wanachokifanya.

'Sawa kabisa, nimeona huku kwangu...'akasema mkuu, na kumfanya docta ajiulize kumbe mkuu ana mambo yake , ... mkuu naye wamo..lakini akijiwa na neno jingine la kumuuliza, mkuu akasema;

 'Unasemaje kuhusu mke wa mzee…mliwasiliana naye au sio..umechukua hatua gani…?’ akauliza

'Huyo kwa sasa tuachane naye kwanza, maana tukimalizana na hawa watu, hayo mambo mengine yatajileta yenyewe, huyo mama atakuwa huru, kama katekwa, ...na sijui kama ndio yeye, nilimuona mahali…nina imani ..atakuwa salama…’akasema mkuu

‘Sawa nimekuelewa…ngoja tuendelee na kazi…’akasema docta, sasa akijua kila anachokifany ahata mkuu wake anakiona, 

'Natakiwa niwe makini na huyu mtu, sijamuamini bado...'akasema kiakili, na sasa akipanga jinsi gani y akuweza kujilinda kama lolote litatokea kutoka kwa huyo mtu.

'Hii kazi huwezi kumuamini hata mkeo...'akakumbuka maneno hayo kutoka kwa jamaa yake mmoja.

************

 Docta alipoona kakamilisha kila kitu, sasa akaanza kazi nyingine, maana ukitaka kumshinda adui yako, mfahamu alivyo kabla hajakufahamu wewe, yeye alichofany ani kuazna kutengeneza mtandao wa kuisoma ramani ya jengo...hilo jengo lenyewe lilikuw anaramani kwenye mitandao yao, ambayo kwa ujumla alishaiiba ...na kuweka kwake, ni kama yeye ndio anafany akazi ndani ya jengo lao.

Alijua huko kwa hivi sasa wanafanya kazi ya kutafuta namna ya kurejesha mitandoa yao, lakini kwa jinsi akuavyo, itachukua muda karibu siku nzima, na hata wakifanikiwa bado yeye anao mtando wao wakuwasoma, na hawataweza kumzuia ...

Kwa kujiamini kabisa akaendelea na kazi yake sasa aliweza kutembelea hilo eneo ambalo ndilo makao ya huyo mkuu wao, bila shaka….utafikiri yupo humo ndani,..ni mambo ya mitandao, wala sio uchawi…akaangalia taswira ya eneo, na kila hatua aligunda mambo mengi kwenye hilo jengo,.

'Kumbe hapa ndipo wanapofanyia mambo yao...sasa wamekwisha...'akasema docta.

Kwani jengo hilo linaloenekena la kawaida, lakini kwa ndani, kuna mambo mengi ya siri , ambayo bila mitandao hiyo usingeliweza kuona,…na kama alivyoambiwa kwenye njozi, mpelelezi ndiye atakuwa njia yake,…na kweli mpelelezi kamfikisha kule alipokuwa akipatafuta kwa siku nyingi.

 Jengo hilo lilikuwa na nyumba za chini ya ardhi ambazo hazijulikani na kwa jinsi ilivyo, kuna vitu kama mahandaki, yanayotoka hapo kwenye jengo na kuelekea sehemu nyingine…alipogundua hilo, akatikisa kichwa, akawa anajiuliza kama mkuu keshaliona hilo, hakuwa na muda wa kumuuliza.

Kwa haraka akafuatilia pango moja, laonekana ni refu sana, kama bomba kubwa sana..akawa anajaribu kulifuata na ramani yake,.. akagundua kuna linakwenda hadi kutokea…oh, maeneo ya makaburini…ni rafu sana, hawa watu ni wajabu sana, wanapita chini ya ardhi watu juu hawana habari.

'Duuh...kumbe....'akasema na mara simu yake ikalia…

 Alipoangalia saa akagundua muda umefika, saa kumi, na haikupita muda mkuu naye akaingia.

‘Umeona eeh…?’ akauliza docta.

‘Nimeona nini..ok, sawa nimeona, ..japokuwa sina uhakika, na unachokiuliza, ila hapa nimekuja kwa ombo moja…’akasema mkuu,

‘Sawa ombi gani…?’ akauliza

 'Sasa docta, kazi iliyobakia ni yetu sisi watu wa usalama,…kila kitu kipo wazi, ..muhimu ni kwenda kuwakamata hao watu, tukiwa na ushahidi kamili.., mimi nakuomba ubakie hapa kwenye mitambo,tutawasiliana…au sio…?’..'akasema mkuu, na docta hakuwa na kipingamizi, japokuwa alihis bado huyo mtu hajamuamini.

 'Sawa, kwangu haina shaka, mkinihitajia msaada wangu nipo tayari…Muhimu ni kumuwahi binti wa Inspecta kabla hawajampiga hizo sindano za kumlegeza viungo vyake..wakifanikiwa kufanya hivyo, itatuwia shida sana kumrejesha, katika hali ya kawaida, unaona jinsi binti wa mzee anavyopata taabu, ...'akasema docta.

 'Sawa, hilo lipo makini..kila kitu kina watu wake..sizani kama vijana wetu watatuangusha kwa sasa…’akasema mkuu.

‘Sawa mimi nawatakia mafanikio mema…’akasema docta, na kupeana mikono na mkuu huyu.

Mkuu na kikosi chake kamili wakaelekea eneo la mapambano, wakiwa na zana za kila namna mavazi ya kubadilisha kila hatua…

 ***************

Mimi nilianza kuwa na wasiwasi pale niliposhindwa kupata nafasi ya kuingia ndani ya hilo jengo, ningeingiaje wakati  jengo lote lilizingirwa na watu, ambao nilijua ni watu wa hao watu…nilihisi hivyo!

 Baadae sana, niliona watu, wakiwa wamebeba majeneza, mawili…nilijua wanataka kuzika, sasa kwanini hawaendi makaburini wanakuja kwenye hiyo nyumba..walipofika kwenye geti, wakawa wanaongea na mlinzi, na mmojawapo akawa anazozana na mlinzi, na mimi nikawa na hamu ya kusikia wanachoongea,nikasogea karibu.

'Sisi tulimuomba mzee kuleta hizi maiti hapa kabla ya kuanza mazishi....'akasema mmojawapo.

'Haiwezekani, kwanza huyo mzee hana mamlaka na hii nyumba tena…, mke wake ndiye anaisimamia kila kitu, je mliongea na mama mwenye nyumba..?’ akauliza.

'Sisi tuliongea na mzee kwasababu tunajua yeye ndiye baba mwenye nyumba, kama unabisha mpigie simu..’wakasema hao watu.

Basi kukawa na mzozano, na mara kukasikika mlio kama wa bomu, ndani ya jengo..na jengo zima likatikisika,  watu waliokuwa pembeni wakawa wanasogea karibu kuona kuna kitu gani..na hapo kukawa na msukumano, watu wakitafuta upenyo wa kuona kinachoendelea hapo..

‘Kuna nini kimetokea…’watu wakauliza

‘Bwanaeeh, hilo jengo lina viroja, sijui ni mashetani yanapigana humo ndani…’mmoja wao akasema.

‘Kwani kuna mashetani humo ndan…?’ akauliza mtu mwingine.

‘Unauliza jibu, jengo hilo limeguzwa chaka la wanga, wanaoingia humo, wengi ni wachawi..angali hata mavazi yao..wanatoka huko walipotoka, wakifika hapo wanabadilisha nguo zaao..’akasema mtu.

‘Wewe shauri lako ropoka tu, kama utauona usiku…’akasema mtu mwingine na kukawa kimia.

Mara nikiwa naangalia huku na kule,nikaona watu kwa nyuma ya jengo wakiruka ukuta kwa kasi sana,…walikuwa wepesi, .. sikujua ni watu gani, baadae kukatulia.

 Mimi nikahisi sasa kama kuna kitu kinavuta, hisia ya kutaka niingie ndani, na nikafanya hivyo, nikapita pale pale mlangoni, ….kilichotokea ni kuwa yule mlinzi aliinama kama anaokota kitu, au kuna kitu kimeingia kwenye kiatu chake kinamsumbua,..akawa anahangaika hadi kuvua kiatu…na mimi nikachukua nafasi hiyo niliona kama bahati tu…, nikajikuta nimeshaingia eneo la jengo.

 Nikawa nahisi kuelekea nyuma ya nyumba,…nikatembea nikiwa samba mba na ukuta, ili watu wa ndani wasije kuniona… na hapo nikafika mlango wa nyuma, ulikuwa wazi,…alitoka mtu, na kutembea upande wa pili hakugeuka nyuma na mimi kwa haraka nikaingia ndani.., nilihisi kuna watu wamejificha juu ya paa, cha ajabu, sikuona wakinizuia..Nahisi ni kama wameniona..

 Nikafika sehemu, nikawa kama nimeambiwa nisubirie hapo…na mara nikasikia sauti ya hasira ikisema;

'Haiwezekani...mitambo imekuwaje,..'sauti kali ikasema, nikaikumbuka hiyo sauti, nilishaisikia mahali, kule kwenye jengo nililotoroka, ni yule yule mtu aliyefika uwanja wa ndege….nikataka kwenda kumuona lakini cha ajabu miguuu ikawa mizito, hataki kutembea, ni kama nimeshikiliwa.

 Nilikabakia hapo hapo kwa muda, mara nikasikia sauti ile ikisema tena kwa hasira.

************
 Hapo nilipo niliweza kusikia sauti hiyo kupitia kwenye mlango uliokuwa nusu wazi, kumbe ni chumba ambacho ukitoka humo unaingia hapo hao watu walipo...

'Muda umekwisha, ...mleteni huyo bint huku, tusipoteze muda….

 Na mara kukasikika sauti ya binti akilia….

‘Msiniue msiniue….’

'Usiwe.na wasiwasi bint, tunataka kukuondolea hilo tatizo lako, baada ya hapa, utasahau kila kitu…hii dunia ya mateso, utaiacha,..na huko utaenda kuungana na baba yako...'sauti ikasema.

‘Baba yangu, ina maana mumeshamuua…?’ sauti ya kike, nahisi ni huyo binti ikauliza

‘Hahahaha….usiulize kitu kama hicho, elewa kuwa na yeye imebidi, kwasababu…anahitajika kupumzika,…unanielewa binti mrembo…’sauti ikasema.

‘Wewe ni shetani, muuaji, kama nitapata nafasi ya mwishi, nitahakikisha na wewe umekufa kifo kibaya…shetani mkubwa wewe…’sauti ya kike ikasema.

‘Hahaha..usijali…haya yote utayasahau…sasa hivi, ngoja tusubirie taarifa ya kutoka huko alipo baba yako…tunataka yeye atangulie kabla yako..ndivyo inatakiwa..unasikia, na tulia ..mwekeni sawa…’akasema huyo muongeaji.

‘Subirini kwanza…’ilikuwa sauti ya kike lakini sio ile ya binti…

NB: Ni Nani huyo


WAZO LA LEO: Watenda mabaya, hufikia mahali wakaona kuwa wao hii dunia ni yao,..wana haki hata ya kuua, wanasahau kuwa kila nafsi itauonja umauti kwa wakati wake…na wao muda wao utafika, na wao watarejea kwa hakimu wa mahakimu,ewe mwanadamu tubia kabla muda haujafika, ubaya hauna heri hapa duniani. Tumuombeni mola wetu atujalie tuishi vyema, atulinde na vitimbwi vya shetani, na atujalie tuwe na mwisho mwema. Aaamin..
Ni mimi: emu-three

No comments :